Wednesday, May 4, 2011

Nyoka yupi wa CCM aliyejivua magamba?


    
FALSAFA ya Chama cha MapinduziI(CCM)kufanya matengenezo(reform) kwa mfano wa nyoka anayejivua magamba, imetupa Watanzania agenda na tafakuri tunduizi.
Nyoka, ametumiwa mahali pengi(hata katika Biblia) kama mifano ya Shetani, au mashetani na wafuasi wao. Nyoka hutumika kama alama ya kuwatambulisha Freemason.
Biblia hiyo hiyo, inamtumia nyoka kama aishara ya Ukombozi wa Waisraeli wa kale,kutoka Utumwani Misri walikokuwa kwa miaka 400,kwenda nchi ya Ahadi, Kaanani, ambayo leo ni Palestina.
Awali, katika kitabu cha Mwanzo 3:1-5 Biblia imesema nyoka alikuwa mnyama mwerevu(mjanja na laghai) kuliko wanyama wote aliowaumba Bwana Mungu.
 Nyoka huyu, wa kitabu cha Mwanzo, alishirikiana na Ibilisi au shetani kuwalaghai Adamu na Hawa kumwasi Bwana Mungu na kusababisha maangamizi,ufisadi na dhiki, majanga ya asili na mabaya yote yameletwa na uasi wa Adamu na Hawa na ulaghai wa Shetani.
Tena, katika kitabu cha KUTOKA 4:1-4 NA KADHALIKA Kutoka 7:9-12,Nyoka alitumiwa na Musa na Haruni kama ishara ya Mamlaka ya ukombozi kutoka kwa Mungu dhidi ya Mtawala wa Misri, Farao.
Nataka kusema kwamba, nyoka siyo tu ni alama ya kumtambulisha Shetani na malaika zake,majini na mizimu,na Freemasons.
Nyoka, ni sihara ya ukombozi kutoka utumwa kama huo wa Misri zama zile za Nabii Musa na Waisraeli wenzake huko Misri.
 Pia, nyoka ni alama ya ukombozi kutoka utumwa wa dhambi; ni alama ya tiba na ondoleo la maradhi ya kufisha kama sumu.
 Biblia, katika kitabu cha HESABU 21:5-9, hutufundisha falsafa ya NYOKA WA SHABA, aliyeinuliwa Jangwani, aliyewaokoa wana wa Israeli wasife kwa sumu kali ya nyoka wakali wenye sumu,pindi Waisraeli walipokuwa safarini kutoka Misri, wakadharau Ulinzi wa Mungu.
 Kila nyoka hujivua magamba.Konokono anapojivua magamba, hufa. Lakini,nyoka anapojivua magamba, huwa kijana zaidi mwenye kasi zaidi.
 Yohana, katika kitabu cha Injili ya Yohana Mtakatifu 3:14,15 hutufundisha kwamba,Yule NYOKA WA SHABA kule Jangwani,zama za ukombozi wa Nabii Musa, alimwakilisha Bwana Yesu Kristo.
 Nyoka,siyo ishara ya Shetani tu, pia ni ishara ya ondoleo la dhambi na mauti. Hata hivyo,kila nyoka hujivua magamba. Kuna nyoka wenye sumu na wasio na sumu;na wote hujivua magamba!
 Kwa sababu hiyo, tunapata fursa ya kujisaili: Nyoka wa CCM aliyejivua magamba, ni Yule aliyewadanganya Adamu na Hawa, sasa karejea kwa sura ya Chama cha Siasa,ili kuja kuwadanganya watu waangamie?
Au, huyu ni nyoka anayesemwa kujivua magamba ni Yule wa SHABAaliyeinuliwa Jangwani ili kuwakomboa watu wenye kukaribia kukata roho kwa sumu za maisha magumu,kukata tama na mauti yanayowakabili?
Labda,huyu nyoka wa CCM aliyejivua gamba ni Yule ambaye Bwana Mungu aliwaamuru Musa na Haruni wamtupe mbele ya kasri la Farao wa Misri?
 Basi, Farao naye akawaita wachawi wa Misri,wakatengeneza nyoka bandia lakini wadogo wadogo, wakamezwa na Yule nyoka wa Musa na Haruni!
Hakika, huyu nyoka wa Musa na Haruni,hakuwa nyoka halisi. Ilikuwa fimbo ambayo ni alama ya utawala,”Sceptre” ama alama ya Mamlaka ya ufalme wa Mungu, ambao hauna mipaka katika jambo lolote.
 Je, nyoka wa CCM,aliyejivua gamba,ndiye huyo ambaye ni fimbo yenye mamlaka ya ufalme, “a rod symbolizes Royal Power” ndiyo inayojigeuza sasa ama kujivua gamba ili kujiondoa katika hali yake ya uzee?
 Tujadili kidogo falsafa ya nyoka kujivua magamba.
Mungu wa dawa wa Kigiriki, AESCULSPIUS, ama kwa Kilatini, Asclepius, huwa anaonekana ameshika fimbo,halafu nyoka anaonekana akiwa amejizinga kwenye fimbo hiyo. Naam, hapa pia kuna Fimbo ya nyoka.
Bila shaka, msomaji umepata kuona alama ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa(WHO) kuna nyoka aliyejizinga kwenye fimbo, ama kijiti. Ni huyu, Asclepius-mungu wa dawa na uponyaji wa Kigiriki na Kirumi.
Alama hii,pia inaonekana kwenye noti ya shilingi 500/= hapa kwetu,na watu wengine husema hizi noti zina alama ya Freemasons!
Je, CCM wanapojivua magamba, ni nyoka Aesculapius ama Asclepius? Ni Freemasons? Ni nyoka wa Bustanini Edeni?
Hata hivyo, nyoka ni alama ya UPYA unaoleta UJANA. Kwa Sababu hiyo, nyoka ana uwezo wake wa kujivua magamba. Nyoka hutoa ngozi yake ya kale, analeta ngozi mpya.
 Wajitta wa Musoma vijijini,mkoani Mara wanaita, “Okwinyubhula”! Nyoka aliyejizinga katika kijiti,ni ishara ya uponyaji kutoka katika miungu ya dawa-aesculapius, aliyesadikiwa alikuwa na uwezo wa kuponya. Tazama kitabu kiitwacho, Compton’s A Britannica Publications Vol.1 ukurasa 87.
Hii miungu ya Kigiriki,ilisadikiwa kuishi katika kilele cha Mlima Olympus. Ilisemekana kwamba miungu hiyo 391 iliishi kama jamii moja kileleni mwa Mlima Olympus,pamoja na viumbe waliokufa(wanga na mizimu) na baadhi ya hiyo miungu ni Zeus, Titan, Poseidon(mungu wa maji), Hades au Pluto ambaye ni mungu wa wafu, Hestia, Hera,mungu wa vita-orodha ni ndefu.
Sina shaka,ulipata kusikia kwamba, Mwanafalsafa wa kale sana Ugiriki, Socrates au Sokrati, aliwafundisha wanafunzi wake, Aristotle, Plato na wenzake,kwamba kulikuwa na Mungu mmoja tu,naye aliishi mbinguni,wakampa sumu anywe ili afe.
Kwa sababu hiyo, Chama cha Mapinduzi hawakubahatisha kujifananisha na nyoka anayefanya, “Okwiyubula” yaani kujivua magamba.
 Tumeona Falsafa ya Kigiriki na Kirumi kwamba nyoka ni alama ya upya; ni ishara ya ujana. Kwa kuwa Katibu Mkuu Mpya wa CCM,Willson Mkama ni Mjitta awaeleze Watanzania, CCM imeji ‘nyubhula’ ili iwe mpya,ili kung’ata kwa sumu ya kuangamiza au kuponya?
CCM kujivua magamba mithili ya nyoka,ni kujifanya upya yaani CCM Mpya yenye ari zaidi,nguvu zaidi na kasi zaidi katika kuangamiza,au kuponya Watanzania sumu zilizomo miilini na akilini?
 Baadhi ya wasomaji wangu, wamenipigia simu kuniuliza: Je, CCM wanapojivua magamba mithili ya nyoka hutapika pia sumu?
 Na ndiyo kurejesha upya na ujana wao tayari kuleta madhara kwa kasi zaidi,ari zaidi na nguvu zaidi, au kuleta uponyaji na tiba na ondoleo la utumwa kwa ari,nguvu na kasi zaidi?
Niseme kwamba, falsafa ya CCM kujivua magamba ni kurejesha upya na ujana, sawa. Sijui kama CCM ni wale nyoka wa sumu kali waliowashambulia Waisraeli,Jangwani wakati wa safari yao ya kutoka Utumwani,Misri?
Labda, CCM ni Yule nyoka wa shaba ambaye alikuwa alama ya ukombozi kimwili na kiroho pia? CCM ni alama ya ukamilifu wa kimwili,kiroho na kiakili na hali bora kijamii?
 Sijafahamu,kama CCM ni nyoka waliojivua magamba kama ishara ya uponyaji mithili ya Aesculapius ama Asclepius, anayetumiwa na Freemnasons, WHO na mashirika ya madawa na uponyaji duniani.
Sijafahamu kama kikombe cha Babu wa Loliondo,kina alama gani ya uponyaji? Sitambui,kama nyoka wa CCM aliyejivua gamba ana sumu au hana.
Wapo nyoka wengi hawana sumu,chatu hana sumu lakini humeza watu!
Nikijuacho ni kwamba, nyoka akitumiwa vibaya ni alama ya laana na kifo. Nyoka aliyewadanganya Adamu na Hawa ni hatari.
 Alama ya nyoka ikitumiwa vizuri ni ishara ya ukombozi na tiba kwa matatizo sugu na kukata tama.
Labda, sasa CCM watwambie wenyewe, wao ni nyoka yupi aliyejivua gamba?
Nyoka mdanganyifu aliyeleta mauti na sumu kwa Watanzania, au nyoka wa Shaba, alama ya ukombozi wa kiroho na kimwili?
 0786-324 074

eti, hizi ndiyo haki za binadamu za Ulaya na Marekani?




 
UINGEREZA, ambayo ilifanikiwa kuzikusanya nchi nyingi zilizokuwa chini ya Utawala wa Rumi, na kuzifanya  makaoloni yake, imekuwa ikitawaliwa na wafalme tangu mwaka 829 A.D.
   Hawa wafalme, na dada zao na mabinti zao(malkia) wamewatawala Waingereza tangu karne ya tisa,
 Hadi leo, na hakuna raia aliyekwisha andamana kutaka utawala wa kifalme na kisultani uliodumu zaidi mya miaka 1,182 ung’olewe,ili kupisha demokrasia.
 Nchi hii, inayoongoza kuata kumpindua Kiongozi wa Libya, Kanali Muammar al-Gaddafi, kwamba amedumu uongozini tangu mwaka 1949(umri wa miaka 42) imetawaliwa na wafalme lukuki,tangu Egbert na zama za Saxons na Danes.
  Mwaka 1399,Uingereza ilikuwa chini ya House of Lancaster, wakitawaliwa na Wafalme  na Duke of Lancaster,hadi miaka ya 1900  wakawa chini ya Mfalme GeorgeV,Edward VIII, George VI baadaye akatawazwa Malkia Elizabeth II, ambaye ni BINTI mkubwa wa GeorgeVI.
 Huyu Malkia Elizabeth II alitawazwa kuwa Malkia wa Uingereza Feburuari 6,mwaka 1952 hadi leo anatawala Uingereza, na hakuna wa kuhoji mamlaka yake yaliyotamalaki hata hapa kwetu Tanzania.
   Serikali ya Uingereza inayoongozwa na Mawaziri wakuu,ilianzishwa ,mwaka 1721( karne tisa baada ya Mfalme wa kwanza, Egbert; wakati huo akaanza kutawala Waziri Mkuu,  Sir Robert Walpole.
 Sir, ni cheo anachopewa mtu anayeheshimiwa sana na Familia ya kifalme.Cheo hiki, “Knighthood” ametunukiwa hata Salman Rushdie. Sir Salman Rushdie alipigwa ‘Fatwa’ na utawala wa Ayatollah Khomeini,huko Iran,hivyo hutafutwa sana auawe kwa kuikashifu dini ya Kiislam. Niachane na hayo; hayanihusu.
  Kutoka Sir Robert Walpole, hadi sasa David Cameron, Uingereza yapata mawaziri wakuu takriban 80 vya vyama anuwai, ambavyo aslani haviwezi kuhoji bungeni mamlaka ya Malkia. Malkia Elizabeth II ANA UMRI WA MIAKA 84, alizaliwa Aprili 21 mwaka 1926.
 Akifa leo, ingawa ametawala Uingereza kwa jumla ya miaka 59, atatawala mwanaye,Prince Charles, ama wajukuu zake, Prince William na Harry.
Novemba 2008 Malkia na mumewe,Prince Phillip, walikuja Kampala,Uganda kuburuza mataifa lukuki hapa duniani, katika mkutano wa makoloni yao ya zamani, wao wanaita Jumuiya ya Madola, The Commonwealth.
 Hata Ufaransa imetawaliwa na akina Charlegne,au Charles Mkuu(742-614 AD) hadi wakati wa Jamhuri ya Tano zama za Rais Charles Andre J.M. de Gaulle(soma Chalz de Go)aliyeishi 1890-1070.                           Ni wakati wa akina Georges Pompidou,Valery Giscard d’ Estaing, Francois Mitterand,Jacqius Chirac hadi huyu “Mzee wa Vimwana” Nicolas Sarkozy.
 Nataka kusema kwamba, hizi dola kuu zilitoka mbali,kwenye tawala za kifalme,hadi leo kinachoitwa demokrasia halisi hakuna.
 Isipokuwa, wao wanataka wafalme wa Afrika(Gaddafi anaitwa , ‘King of Afrcan Kings’) watokomezwe.
Ili, akina Malkia na wajukuu zake Harry na Prince William wabaki wakitutawala huku,kwenye Commonwealth.
  Malkia huyu, bado anaburuza mataifa mengi tu kama Canada, Austria, New Zealand,Jamaica,Barbados, Bahamas kwa kuyataja machache.
 Tena, Marekani ndiko walikoiba kura katika uchaguzi wa mwaka 2000 pale Al Gore alikaribia kushinda, wakamwibia kura. Mashabiki wake na chama chake cha Democrat walikuwa wataarabu tu,ingekuwa kwetu huku,ingekuwa kama Cote d’ Ivoire.
 Dola iliyodumu kwa jumla ya miaka 235 wakahesabu kura kwa mashine kasha kwa mikono, wakamnyang’anya kura AlGore, wakampa Bush. Kesi ikaenda mahakamani, mahakama ikachakachua matokeo na kumpa Bush mhula wa kwanza wa utawala.
  Tunajua kura za Palm Beach na Miami-Dude zilileta shida, mwezi mzima ukapita bila kujulikana mshindi. Algore alipata kura za watu wote51,000,894wakati Bush alipata 50,495,211 akaongoza Florida na kujipatia kura za ushindi za electoral 271.
  Nataka kuwagutua wanaoshabikia Uingereza,Marekani,UfaransamUjerumani n.k kwamba kuna demokrasia pevu,kuna uhuru na haki za binadamu(zipi?) wanazofanya hapa duniani?
Mwaka 1936, Uwanja wa Olimpiki wa Berlin ulijengwa na Dikteta Adolf Hitler. Michezo ya Olimpiki ilifanywa hapo Berlun, na Hitler akawa mgeni wa heshima.
 Julai 9 mwaka 1936 Mwamerika Mweusi, Jesse Owens  akawatioa kamasi Wazungu wote kwenye mbio na riadha. Akajipatia nishani nne za dhahabu kwa muda wa dakika 45 tu. Hitler akakasirika kuona Mweusi akishinda kila mara, wakati Wazungu hawakumwona. Yeye alijua mtu mweusi ni mnyama, kwahiyo akasusia mashindano ya Olimpiki kwa sababu mnyama, Owen, salishinda!
Miaka 70 baadaye, mwaka 2006,uwanja huohuo wa Olimpiki wa Berlin,ndiko fainali za Kombe la Dunia zilikofanyika, Michael Materazzi wa Italia akamtukana Zenedine Zidane Zizou,matusi ya kibaguzi.
Chukua tabia hii ya akina Hitler na Materazzi halafu uchanganye na ubaguzi wa rangi huko Afrika ya Kusini zama za Makaburu.
  Angalia, ubaguzi wa rangi dhidi ya akina Samuel  Eto’o Fills wanaoitwa nyani, ama kawaulize akina Eric Abidal Claud Makelele,Zidane, Thiery Henry, William Gallas,Louis Saha,Patrick Vieira na wenzao waliposhindwa kuipa Ufaransa ubingwa, ilisemwa kwamba ni rangi yao Nyeusi ya mkosi!
 Hapa, msomaji, unaona haki gani za binadamu huko Ulaya?Agosti 2009 huko  Berlin,Ujerumani, Caster Semenya(19) wa Afrika Kusini akawatoa kamasi Wazungu katika mbio za mita 800, wakamnyima ushindi, kwa madai kuwa yeye ni ‘Dume-Jike,’ Wazungu bwana!
 Kwa Muingereza, eti neno uhuru ni mzaha linapofika kwa Mwafrika. Mwaka 1787 mji Mkuu wa Sierra Leone, Freetown(MJI ULIO HURU)ulijengwa na Muingereza huyu kama kituo huru cha watumwa! Watumwa walijengewa mji huru wa Freetown?! Ajabu.
Kifo cha Princess Diana mwaka 1997,na kuundwa kwa tume ya uchunguzi wa kifo chake, The Paget Probe, ni kielelezo kwamba Uingereza hakuna uhuru,hakuna demokrasia na haki za binadamu. Kuna ubaguzi wa rangi na ukaburu uliotamalaki.
Princess Diana(36) na Dodi al Fayed(42) walikufa Agosti 31 mwaka 1997 katika Ponto de I’Alma Park,mjini Paris, Ufaransa, mahali penye njia ya chini kwa chini.
 Ilikuficha tetesi kwamba ‘wivu’ wa Malkia na familia yake dhidi ya Diana aliyekuwa amevuka mipaka na kutaka kuolewa na Mwarabu, Dodi, na ikasemekana alikuwa na himila changa ya miezi miwili, ndicho kitu kilichomsababishia mauti ya tashtiti.
  Vyombo vya usalama mjini Paris, baada ya ajali yakupangwa, vikamsingizia dereva,Henri Paul kwamba aliendesha gari kwa kasi sana, ili kuwatoroka ma-Paparazzi.
Kwamba, Dodi na Diana waliutia mtindi kwa sana, hawakufunga mikanda wakati Mercedes Benz S-280 SEDAN, ilipogonga nguzo ya 13 hapo barabara ya chini na kusababisha vifo vya Diana na Dodi!
   Maneno yalipokuwa mengi, ikaundwa tume ya kuchunguza vifo hivi, Paget Probe iliyokuwa na wapelelezi 15 kutoka Scotland Yard, wakatumia Dola za Marekani 7,000,000 kuwahoji mashuhuda 300.
 Hata hivyo,Mkuu wa Paget Probe, zamani alikuwa Mkuu wa Scotland Yard, Lord John Stevens alishia kukaa ‘kama kamati’ na watoto wa Diana, Harry na William na kakaye,Lord Charles Spencer na dadaze wawili, wakasema haikuwa ajali ya kupangwa.ilikuwa ajali ya kibinadamu-tragic accident!
 Ripoti ya uchunguzi yenye jumla ya kurasa 832 haikuwa na jipya. Baba wa Dodi, Bilionea wa Kimisri, Mohammed al-Fayed akaipinga vikali tume hiyo, na kusema hadharani kwamba majasusi wa Uingereza waliwaua Dodi na Diana kwa sababu ya wivu,kuona Daiana angeolewa na Dodi.
  Diana na Prince Charles walishatengana  tangu Desenba 9 mwaka 1992 wakapeana talaka rasmi Agosti 28 mwaka 1996.
Prince Charles alishaoa kimwana mwingine, Camilla Parker Bowless, lakini Diana alifungwa kuolewa na mtu kwa sababu alikuwa wa familia ya ufalme!
 Mtu wa ‘Royal Family’ kama yeye hakuruhusiwa kuolewa na mtu,tena Muislam, sasa sijui kama kweli alikuwa na mimba, sasa kama Diana  angezaa Mwarabu, anaye angekuwa anakuja Makao Makuu ya Malkia-Buckingham Palace, kuwasalimia nduguze, Harry na Prince William?
Waingereza, walimuua Diana na Dodi,ili kutupilia mbali udhia na aibu ya warithi wa Ufalme kuwa na ndugu Mwarabu halafu Muislam.
 Si unajua dini ya Anglikana ndiyo dini yao na Malkia ndiye mkuu wa dini hii ya Uingereza? Sasa, hawakutaka Mwarabu azae na mke wa mwana wa Malkia, sasa tunajua Diana aliuawa kwa sababu ‘aliasi’ na kutaka kuolewa na Dodi na alikwisha kuwa na mimba changa ya miezi miwili,ikaleta taabu.
 Unaweza kumuuliza Mohammed al Fayed, Yule tajiri wa Kimisri, babaye Dodi,kama nasema uongo kwamba Diana aliuawa na majasusi wa Uingereza huko Paris.
 Ndiyo maana tunasema Uingereza hakuna demokrasia,uhuru wala Haki za Binadamu. Labda uhuru uko kwa mashoga kuvua nguo na kuandamana hadi bungeni wakiwa uchi, kuna uhuru wa wanaume kuoa na kuolewa kama Sir Elton John na David Furnish.
 Kuna uhuru wa maaskofu na wachungaji wa dini ya Malkia kuoana wanaume na wanawake, na wanaweza kwenda baa na vimwana na kuuchapa mtindi, halafu waumini wanapoandamana kupinga wazinzi kuwa wachungaji, maaskofu wanawatetea!
 Huu ndiyo uhuru ulioko Uingereza,Marekani na Ufaransa..uhuru wa kumomonyoa maadili na sheria za Bwana Mungu.
            www.congesmrambatoday,blogspot,com
            0896/0754-324 074

Obama kamuua Osama, au geresha na janja ya Marekani?

                       
WAMAREKANI wanashangilia sana,Rais Barack Obama kafanikiwa kumuua Osama bin Laden.
Marekani sasa wameushinda Ulimwengu.
Mwanzoni, Osama alikuwa ‘rafiki’ yao na mshirika wao katika vita vya kuyapinga majeshi ya Urusi nchini Afghanistan.
Marekani, sasa wamewaua adui zao karibu wote katika vita vinavyoitwa vya ugaidi-WAR AGAINST TERRORISM- na wanakaribia kuwatia mbaroni wote wanaowapinga,walioko katika ‘Mhimili wa Uovu’ Duniani.
Saddam Hussein,mtawala wa nchi iliyo na mito miwili ya Tigris na Euphrates, nchi ya Irak, alinyongwa kwa kamba nene shingoni, katika jingo la Camp Justice, Alfajiri ya Jumamosi,Desemba 30 mwaka 2006,mjini Baghdad.
Awali, walitangulia kuwaua wanaye,Udday na Qussay,kwa mvua ya mabomu iliyomwagwa na madege ya kivita, na vikosi maalum kama Delta Force.
 Naam. Tunaweza kusema, ‘Mto Frati ulikauka’ hiyo Desemba 2006, pale sanamu ya Saddamu Hussein ilipoangushwa mjini Baghdad,kabla ya yeye kunyongwa.
 Sura ya Pili ya kitabu cha Danieli katika Biblia Takatifu,hutuambia kwamba Babeli ambayo sasa ni Irak ilikuwa nchi ya sanamu kubwa za madini yenye thamani kubwa,zilizoabudiwa.
Sanamu ya Saddam ilibomolewa na kushushwa mahali pake,kuonesha enzi ya Babeli ama Irak ya Saddam ilishakoma mwaka 2003, ili kutoa nafasi na njia kwa mataifa ya Mashariki yaliyowapinga Marekani na washirika wake wa NATO,kuvuka mto na kuungana na Ulaya Magharibi.
Mto mkubwa, Frati, ‘ulikaushwa’ kabisa mwaka 2006, wakati Dola kuu duniani, Marekani ilipojizatiti kuitawala dunia baada ya dola ya Urusi ya Kisovieti(USSR) kusambaratika mwanzoni mwa miaka ya 1990.
Marekani sasa ni ‘baba’ wa Ulimwengu, na anayewapinga anaishia kukamatwa na kufungwa jela ama kuuawa kwa mabomu makali,kama siyo kutiwa kitanzi.
Mabaki ya Ukomunisti yangalipo,ndiyo Uislam wenye msimamo mkali; na ndiyo akina Kanali Muammar al-Gaddafi wa Libya, Hugo Chavez wa Venezuela,  Mugabe wa Zimbabwe, Fidel Alejandro Castro Ruz na nduguye Raul Castro Ruz wa Cuba na wenzao.
Siku zao zinahesabika,kwa sababu tayari mtoto wa Gaddafi,Saif al-Arab ameualiwa pamoja na wanaye watatu mjini Tripoli.
Mauti yanamkaribia Gaddafi,kama siyo kifungo jela,kasha kunyongwa kwa kamba hadi kufa kama Marehemu Saddam.
Basi, ulimwengu wa Kikomunisti umekoma,na Gaddafi anakaribia ukingoni,kwa kuwa madege ya vikosi vya majeshi ya Umoja wa Kujihami Ulaya Magharibi,NATO, wanamvizia kama walivyomwotea Osama bin Laden na kumlipua usiku wa kuamkia Mei Pili,jirani na Islamabad, Pakistan.
Osama bin Laden(54) ameuawa na vikosi maalum vya Marekani,vikishirikiana na majasusi wa Central Intelligence Agency(CIA). Ilikuwa siku chache tu, baada ya mtoto wa Gaddafi, Saif al- Arab kuuawa pamoja na wanaye watatu.
Naam.Kupitia kituo cha televisheni cha sky news,nimeuona uso unaodaiwa wa Osama bin Laden,ukiwa umefumuliwa,macho yamefumbwa,hana kilemba cheupe tena,madevu yamesawajika!
Hakika, alikuwa amekufa, na mtu Yule alifanana sana na Osama-Amekufa. Naam, Osama bin Laden amekufa,ingwa wengine bado wanasema ni Propaganda za Marekani tu,Osama yungali hai!
Rais  wa Marekani, Barack Obama, amaeutangazia ulimwengu kwamba, Osama ameuawa na mwili wake ulikuwa chini ya ulinzi wa vikosi maalum vya Marekani.
 Kichwa chake kiliwekewa dhamana ya dola za Marekani milioni 50; na inawezekana Wapakistan wamemsaliti kwa majeshi ya Marekani au majasusi wa CIA.
Vita vya Marekani dhidi ya Ugaidi, viko ukingoni; na upinzani wa kweli dhidi ya Marekani na washirika wake unakoma, kwa hiyo nchi za Mashariki mwa Mto Frati, zinakwenda kuungana na Magharibi yaani NATO na soko la pamoja Common Market, matarijio ni nchi nyingi duniani kama siyo zote kuanza kutumia pesa moja iitwayo Euro,ambayo ina picha ya Askofu Mkuu wa Rumi,Baba Mtakatifu au Papa.
Osama bin Muhammad bin Awad bin Laden, alikuwa mshirika wa zamani wa Marekani wakati wakiyapiga majeshi ya Urusi(USSR) ya Kisovieti,yalipoivamia Afghanistan.
 Alizaliwa mwaka 1957,na alikuwa mtoto wa 17 kati ya watoto 50 wa Muhammad bin Laden,kibarua wa Yemen aliyekwenda Saudi Arabia akawa tajiri mno kupitia miradi ya ukandarasi.
 Huyu, babaye Osama alikufa kwa ajali ya ndege mwaka 1968, Osama akarithi kitita cha dola za Marekani kati ya milioni 50 hadi 300 hivi.
Ilikuwa Desemba, 1979 Osama alipoungana na Mujahedin wa Afghanistan kuipinga Urusi kuivamia Afghanistan.
Wakati ule wa VITA BARIDI,Marekani walipigana bega kwa began a Osama dhidi ya majeshi ya Muungano wa Kisovieti wa Urusi(USSR).
Shirika la Ujasusi la Marekani(CIA) lilimfadhili Osama mabilioni ya dola ili kuwashirikisha Waafaghan kuwapinga Warusi kuingia kijeshi mjini Kabul na kufanya uvamizi.
Osama, akawa na fedha,akaanzisha kambi ya mafunzo ya Mukhtab al-Khidemat(MAK), AKAFUNDISHA maelfu ya vijana kutoka nchi dazeni kupigana vita dhidi ya uvamizi wa Kirusi huko Afghanistan.
Fedha, alipewa na Marekani. Hivyo kambi ya MAK ndiyo chimbuko hasa la al-Qaeda miaka ile ya 1980.Osama alirejea Saudi Arabia baada ya majeshi ya Urusi kuondoka Afghanistan mwaka 1989.
Msomaji,unajua sababu za Osama kukosana na Marekani na kuanza kumpinga Mfalme wa Saudi Arabia?
Saudi Arabia,iliungana na majeshi ya washirika wa Marekani katika Vita vya Ghuba ya Uajemi,dhidi ya Irak,mwanzoni mwa miaka ile ya 1990.
 Yaani,Mfalme wa Saudi Arabia aliungana na Marekani kupigana vita dhidi ya Marehemu Saddam Hussein,katika vita vya kwanza vya Ghuba, Irak ilioishambulia Kuwait,wakati wa George Herbert   Walker Bush(Bush Baba)wakati ule akipigana na Saddam.
Osama ali ‘waasi’ Marekani wakati wa vita vya kwanza vya Ghuba,vilivyopiganwa kwa sababu ya mafuta. Chimbuko la uasi wa Osama dhidi ya Marekani ni maslahi ya mafuta ya Waarabu wa Irak,dhidi ya vibaraka wa Marekani wa Kuwait-zote hizi ni nchi zinazozalisha sana mafuta,naam Mafuta!
Vita vya kwanza vya Ghuba vilipokwisha,Bin Laden alitimkia Sudan.
Nataka nikwambie msomaji,Sudan ni nchi kimbilio la magaidi ambao wakati mwingine tuwatazame kama wanaharakati!
Namkumbuka Ilich Ramirez Sanchez, maarufu kama Carlos The Jackal wa Venezuela, aliyehitimu Chuo Kikuu cha Patrice Lumumba,mjini Moscow, akapinga sera za Marekani za kibabe juu ya Palestina inayopambana siku nyingi na Israeli.
Carlos The Jackal alikimbilia Sudan kujificha, akajakukamatwa na majasusi wa Kifaransa mjini Khartoum,wakampeleka Paris alikofungwa kifungo cha maisha.
Carlos, alipinga ubeberu wa Kimarekani na Uzayuni wa Israeli kwa njia za kigaidi kwa kutumia vikundi kama Balack Septemba, kilichowateka nyara Wanamichezo wa Israeli wakati wa    michezo ya Olimpiki,mjini Munich,mwaka 1972.
Naam, Osama naye alikimbilia mafichoni Sudan kama Carlos The Jackal
.Akaanza Operesheni za kigaidi dhidi ya maslahi ya Marekani,kama mwaka 1993 aliposhambulia jirani na jengo la WTC, mjini New York na kuua watu 18.
Nataka kusema kwamba, Osama alisaidiwa na Marekani dhidi ya Urusi,mafunzo ya kijeshi. Akaja kuwageuka kama Saddam Hussein alivyowageuka wakati ule akishirikiana nao kupigana vita dhidi ya Iran, zama za Ayatollah Khomeini.
 Unakumbuka, Ayatollah Khomeini, alitoka Paris Ufaransa,uhamishoni, akampindua Shah kibaraka wa Marekani huko Iran, zama za uporaji wa mafuta. Tumeeleza jambo hili katika makala zetu zilizotangulia.
Osama, alinyang’anywa Hati ya kusafiria ya Sudan na Saudi Arabia mwaka 1994,akatimkia Afghanistan alikoanza kushirikiana na Taliban waliouteka mji wa Kabul,Septemba mwaka 1996.
 Osama, aliwapa pesa Taliban kwa sababu kiongozi wa Taliban,Mullah Muhammad Omar alikuwa swahiba wake.
Wakaanzisha mafunzo kwa wanamgambo,wakapigana dhidi ya India huko Kashmir.
Agosti mwaka 1998 Bin Laden akatangaza ‘Jihad’ dhidi ya Marekani huko Peninsula ya Arabia,tumesema huko Marekani ilikwenda kutafuta mafuta inayosaka sana.Kila kwenye mafuta mengi,kuna majeshi ya Marekani karibu.
Marekani wakaanza kumsaka Osama huko Afaghanistan,wakapindua serikali ya Wataliban na Mullah Muhammad Omar akakimbia kujificha mvua ya madege ya NATO na washirika wao.
‘Fatwa’ dhidi ya Marekani ilitolewa na akina Osama Feburuari 23 mwaka 1998. Mashambulizi dhidi ya Balozi za Marekani mjini Dar es salaam na Nairobi yakafanywa Agosti 7 mwaka 1998 yakasababisha zaidi ya watu 200 kufa.
Aidha,yamefanywa mashambulizi mengi dhidi ya maslahi ya Marekani duniani,na vikundi vya kigaidi vya al-Qaeda na al Shabab,hasa shambulizi la Septemba 11 mwaka 2001 lililoua watu zaidi ya 5,000 huko New York na Washington na Pennsylvania
 Hata mwaka jana waliuawa watu mjini Kampala wakati wakitazama Kombe la dunia kwenye televisheni.
Nataka kusema kwamba,Osama na Saddam Hussein walikuwa ‘washirika’ wa Marekani,maslahi yakafika ukingoni,wakageuka maadui wakubwa.
 Osama aliwasaidia Marekani kupambana na majeshi ya Urusi mjini Kabul mwaka 1979,wakati Saddam alipewa jukumu la kupambana na Iran zama za Marehemu Ayatollah Khomeini,mfuasi wa itikadi kali na Ukomunisti.
Sasa, Osama na Saddam, washirika wa zamani wa Marekani waliogeuka adui, wamekufa katika mkono wa Marekani.
 Je, ugaidi umekwisha?
 Barack Obama kawatangazia Marekani kwamba vita vimefika ukingoni, mabaki ya ugaidi na ukomunisti yatamudu kupingana na Marekani?
 Akina Saif al-Arabu wamekufa mjini Tripoli, Gaddafi anawindwa, siku na saa yoyote anawafuata akina Saif,kama Saddam alivyowafuata Qussay na Udday!
 Ni shangilizi Marekani. Huenda sasa joto la Obama kupingwa kwamba siyo raia wa Marekani litapoa na huenda akapewa mhula wa pili wa utawala hapo Novemba mwaka kesho,2012.
Rais Obama, anapingwa na wabaguzi wa rangi wa Republican kwamba hakuzaliwa na Hussein Obama na mama yake Ann Dunham Stanley huko Hawaii. Kwamba, eti alizaliwa Kenya na siyo  Mmarekani!
Sasa,kifo cha Osama Mei Pili mwaka huu wa 2011,usiku wa kuamkia Jumatatu huko Pakistan kitamwokoa Obama asizame 2012?
 Osama atamwokoa Obama? Ni mwisho wa vita vya ugaidi na mwanzo wa Marekani kuwakamata watu wanaoipinga na mipango yake ya uporaji wa rasilimali za dunia na hata za sayari nyingine kama Mars na Mwezi?
Ni mwanzo wa Marekani kulazimisha watu wa Dunia nzima kutumia euro yenye sura ya Papa? Ama, ni mwanzo wa amani ya kudumu duniani,kwa kuwa magaidi kama Osama hawapo tena?
Ni vita vikali vilivyodumu kwa muongo mmoja na kuwajeruhi na kuwaua watu wengi duniani kote-vita vya maslahi ya Marekani dhidi ya maslahi ya waarabu,mabaki ya ukomunisti.
 Hata Bush alishatangaza kwamba Osama alikwishauawa na Majeshi ya Marekani huko Tora Bora, sasa ni Osama gani aliyeuliwa Pakistan?
    0786/0754-324 074