Monday, December 19, 2011

WHAT WAS THE MIRACLEOUS 'STONY' BABY AT KUNZUGU BUNDA?

ON JULY 25th in 1978 at Oldham, Lancashire in The US, a girl called Louise Brown, became the World’s first “test tube baby”.
An egg from her mother’s body had been fertilized in a laboratory. It was the matter of science, and it occurred during the scientist’s development of human ‘cloning’ take off.
Scientists do manage to clone frogs, sheep, chickens and it is possible to clone human being.
But, what about a woman to bear a  small round stone at Kunzugu village in Bunda District, on August 23rd this year?
Dr. Rwakyendera Onesmo(MD, MMED)who is the Mwanza’s  Sekou Toure Regional Medical In charge, during  an exclusive interview with The Lake Zone Today Magazine
very recently, said that human beings cannot bear  stones, but something similarly to  stone, or the very hard material in the  round form of a ball.
Dr. Rwakyendera Onesmo  who is also a Medical Specialist in Obstetrician( a doctor who is an expert in a branch of medicine dealing with pregnancy, child birth and the period immediately after child birth) and Gynecologist (a study of  female sex organs and  the treatment for disease of women) said during  an interview that, even geologists cannot prove that the stony baby born  was really a stone.
“ But, In Medical  field, this  is the ‘Mummifying’ or the Calcification”, Dr. Rwakyendera explained.
He added that, the  circumstances occurs when a pregnant woman unfortunately her baby is dying within the Uterus or the mother’s womb, and when its life get ends.
“When unborn baby  dies within, and when the fertilized egg is living no more,  if this baby is not  being born, the Mummifying process takes place” ,Says The Medical Specialist.
According to Dr. Rwakyendela, Mummies in the ancient Egyptians  treated with chemicals in order to stop  the dead bodies  decaying. Even the present, you can see the Mummies in their Museums all over the World.
“The Mummifying” process takes place after the  fetus  dies , and when such  non developing cells are clotting and amalgamating, it results in a stony like thing material.   Via an X-Ray, you can see the amalgamated bones in the womb of the mother whose baby is already dead,   and normally she never  has  regular menstruation period.”, The Doctor insisted.
  Any mother with  such symptoms, must  seek  for medical  advice  or checkups, and is much better to abort  in order  to end  out the   affected woman’s pregnancy; for the infant shall never be born alive.
Another cause for  the  a dead fetus   to get  a hard deposit form in  the mother’s womb, is the Calcium-a chemical element which is found in bones - when it amalgamating, and  doing  idle in Uterus for so long without giving birth. 
Fetuses,  have bones    which has  such an  element, and  bones with calcium tends to  clot and get  a hardening form  like small round stone during this abnormalities, as it occurred in the case of Ngeme Makalla(20)who is the Kunzugu  village resident, in Bunda District, in Mara Region.
“Even men who having problems in their bladders.  When a  male  patient who cannot  urinate effectively and  regularly , the Calcium elements can form a stony  egg- like  within the bladder. This is The Urinary Bladder Stone.” Dr. Rwakyendera explained.
“Bladder stone is very hard deposit formed in the kidney or bladder”, He   stated, “But Geologists cannot proclaim   that, these bladder and kidney stones are stones we customary sees  everywhere. It’s impossible a woman either  to conceive, or   to bear and   at last   to give birth a stony child…Never ever!!”
 In fact, the Doctor said, when unfortunately the child dies in the mother’s womb, changes begins, and the  cells are  also  dies within the Uterus, even  every baby  organs dies, i.e. the legs, the skull, the brain, the flesh ,other bones and particles of the human body, etc  are  amalgamating  to form a  very hard deposit, which laymen used to say,  it  is  stone baby births. It is like a blood clot which forms a hardened material.
The Doctor’s explanation on this condition is either the “Mummifying” or the “Calcification” but not stone child birth.
Ngeme Makalla(20) The Kunzugu resident   alleged  to  conceive in her womb a stone,  which she gave birth last month.
She and her husband, Nyamulekela Kennedy(33) during an incident,  assured their colleague villagers that, the baby born was a round stony which at last  they wrapped in a piece of newspaper and displaying to spectators. It was 23rd of August, this year when the marvelous  stone babe was born.
However, Ngeme has been insisted, her  pregnancy was in trouble since the incubation period, and she and his couple went to the traditional healers to seek medical advice , but had  never success.
“The baby never leaps and I decided to see traditional doctors who never succeeded, and during the labour -at the final stage of my pregnancy leading to childbirth, we found a marvelous ‘pebble’-like babe which I conceived for more than 12 months”, Ngeme Makalla said
The Clinical Doctors (Dr. Kajiu Mhando, and Dr.Bandhihai Tefurukwa)  says: the situation is never a miracle, or marvel baby born, but an infirm within the Mother’s womb, that causes abnormalities.
They insisted  that, women when conceived in their womb  should  seek  medical  check-ups and  should never give up  clinical  advices.
 



Ngeme Makalla(Right) with her husband while holding the stone in hand
  










UTATU MTAKATIFU WA FREEMASONS?

NGO zinazobebwa  Ulaya na  Marekani ,zinajitoa mhanga kutangaza  ‘Injili’ ya “Utatu Mtakatifu” wa Ushoga?
     *Huu Utatu Mtakatifu (Evil Trio) una Baraka za vyura wa Farao wa Misri
SEPTEMBA  mwaka huu,nilikuwa miongoni mwa waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya kuongeza uelewa wa kupinga  unyanyapaa, “Anti Stigma Awareness”.
Tukajifunza kwamba, unyanyapaa ni mbaya; ni chimbuko la majanga makubwa kitaifa na kimataifa, na kwamba aslani, hakuna unyanyapaa chanya duniani.
Hata hivyo, nikajikuta nikibishana mno na Mwalimu juu ya Jamii za Kiafrika kuachana na  UNYANYAPAA juu ya wanaume wanaoingiliwa kimwili,yaani mashoga ama wanawake wanaowaoa wanawake wenzao, wasagaji.
Tulifundishwa kwamba, unyanyapaa hata dhidi ya mashoga ni ukatili, ni kinyume cha ‘Haki za Binadamu’ ni ubaguzi,ni kutenga watu ni udhalilishaji.
 Kwamba, Afrika,imeshindwa kushughulikia watoto waishio mazingira hatarishi, imeshindwa kupambana na umasikini,ufisadi na utawala mbovu, inakazania kunyanyapaa watu wa ndoa za Jinsia Moja-Mashoga na Wasagaji!
 Naam, hii ndiyo Sauti ya Marekani,Ulaya na NGO zetu na Wanaharakati wa Haki za Binadamu. Bado kitambo kidogo, hata vyama vya siasa vitakuwa na sera hizi ili vipate kuungwa mkono na Mabwana wakubwa wa Magharibi.
Ni kwa sababu hii, msomaji ajue, Marekani na Ulaya wameamka ili watufundishe sisi Waafrika kubadili mtazamo wetu ili tusiwanyanyapae mashoga!
Katika mafunzo haya(siwaambii yaliwezeshwa na mashirika gani) tukafundishwa wimbo ufuatao:
“Unyanyapaa,kejeli,viboko,dharau na manyanyaso dhidi ya watoto na Jamii ya mashoga ni janga-unyanyapaa tuulete,tuuchane-chane,tuutupe!”
Ubeti wa Pili tuliuimba hivi:
 “Watoto wetu(wakiwa mashoga) vipaji vyao,busara zao,hekima zao-tuwalete,tuwakumbatie tuwabusu!”
Hakika, huu ndiyo mtazamo wa Bara la Ulaya na Marekani katika kuwashughulikia vijana wetu wanaojiingiza katika  usagaji na ushoga. Kwa Wazungu, ushoga siyo janga(janga ni watoto wa mitaani)ushoga ni uhuru zaidi na maamuzi ya mtu mwenyewe-hakuna  kubeza na kuhukumu!
Katika Unabii wa Biblia, katika Ufunuo wa Yohana 16:13 kumetabiriwa ‘Roho Tatu za Uchafu’(Utatu Mtakatifu wa Uovu) za vyura, zinapotoka kinywani mwa Shetani,Mamlaka kuu za Dunia na Muungano wa Dini na Serikali za Dunia.
Kumbe Biblia inatabiri kwamba mambo haya yatatoka katika kinywa cha Mamlaka za Dunia zitakapoungana na Mamlaka za Madhehebu ya Dini, ambayo ni pamoja na Umizimu, Teknolojia na ukisasa utakaokwenda kuandaa ‘Vita vya kiroho’ vya Har Magedon.
   Roho Tatu mfano wa vyura,maana yake nini?
Chura, ni alama ya uchafu. Katika Misri ya kale,chura alikuwa nembo ya mungu mke,Heget, aliyeaminiwa kwamba alikuwa chimbuko la uhai kwa watoto wanaozaliwa-nguvu kwa vijana.
Huu Utatu Mtakatifu wenye sura ya chura(Evil Trio) umevaa umizimu wa kisasa,uasi wa kidini, na hali ya vijana kuona DHAMB( uasi wa sheria za Mungu) kama kitu cha kawaida tu.
Leo, vijana wengi wakifanya makongamano,hujiuliza,”Hivi Mungu yupo kweli?”
Ndivyo alivyouliza Farao wa Misri zama zile za Nabii Musa, kama miaka 1500 BC.
Vijana wanataka kuwa huru kutoka hofu ya kuwapo kwa Mungu; wanakusudia kuishi huru, na wanamwona Mungu na sheria zake Dikteta-vijana wanataka haki zaidi katika kufanya mambo yao.Ndivyo zilivyokuwa siku za Nuhu na Loti.
Mila na desturi nyingi za Afrika zinakinzana na vijana wa kileo wa kizazi hiki cha ‘dot com’ katika zama za utandawazi za karne hii.
Mila na desturi za Afrika,zingali zikiheshimu sana ndoa ya Jinsia tofauti(heterosexual couples).
Ndoa kati ya mume na mke, ndiyo mwanzo wa familia bora na imara iliyoasisiwa na Mungu katika Bustani ya Edeni, kadiri ya miaka 4004 BC.
Roho Tatu za vyura zinapinga kwa dhati uhalali wa ndoa za Jinsia Tofauti pekee. Roho hii inayotoka mdomoni mwa watawala wa dunia walioungana na Freemasons na teknolojia, wanataka kuwe na ushoga, usagaji, ndoa za mikataba, useja wa kudumu maishani,kuasili(adopt) watoto, ama kupata watoto kwa njia ya maabara (test-tube babies); na hata binadamu kutengenezwa katika maabara,yaani human cloning.
Maisha ni magumu, Haki za Binadamu hizi zinawapigia debe wanaume na wanawake kufanya biashara ya ngono(Commercial Sex Work) ili kujipatia kipato.
 Ndiyo maana, ukienda katika vilabu vya usiku na madanguroni utawakuta wasichana wetu “Dada Poa” wakijidaki ili wapate ujira. Wanashindana na makaka poa(mashoga) katika biashara hii, inayopingwa huku wakati imehalalishwa tayari na Wazungu,Mashirika yao na NGO na wanaharakati wa huku kwetu.
Kwa sababu lipo wimbi kubwa la watu kuhamia mijini(Urbanization) huu Utatu Mtakatifu wa vyura utawakuta vijana wengi wanaohama vijijini kwenda mijini,wakiwa waongufu wapya. Maadili ya Muafrika yataondoka na Wazee ambao sasa wana miaka kuanzia 55 na kuendelea na ni wachache tu.
 Afrika,kuna vijana wengi na watoto kuliko hawa watu wazima wanaojidai kupinga ushoga na mmomonyoko  wa maadili siku hizi.
Vijana, kupata watoto waliozalishwa katika maabara kama Marehemu Michael Jackson, hapo sawa. Kwanza ,wasichana na wavulana hawataki watoto-wanawatupa kwenye madampo.Heri wabebe midoli  hata ya ‘dogi’na kutembea nayo mitaani.
 Sasa, nani atalea watoto na maisha haya magumu? Hata kilimo sasa hatutaki,tutakula mchele wa maabara. Ni kuongea na simu na kutazama ngono mtandaoni,kusikiliza muziki kwenye simu, asubuhi hata jioni.
Hata  wasichana wakizaa hawataki kuwanyonyesha  watoto ziwa la mama, wasije kuzeeka bure na kukosa starehe.Wengine wanawatupa chooni ama dampo kwenye mifuko ya Rambo! Nani alee, sasa?
Vijana wanachelea kuwa wazee, wanakazana hata kumeza vidonge wasizeeke, na wazee wengine wanameza dawa za kuwarejesha ujanani-Afrika uzee sasa ni janga kuliko Ukimwi! Hawataki kukonda, wananunua dawa za Ki-China.
Wasichana wakizaa kabla ya ndoa, hawanyonyeshi watoto titi la mama.Wengi wao wameingia katika ndoa za mikataba,kwa sababu wanasema ndoa siku hizi ni utumwa. Nani aolewe? Kuoa ama kuolewa eti ni utumwa, sababu ni uchumi wa dunia kuwa mgumu.
Hata kuosha vyombo ni utumwa.
He! Mwe!! Msichana mrembo aache kujipamba na kwenda kujiuza mitaani apate maisha, eti aolewe?
 Ndiyo maana ndoa inafungwa saa sita mchana, inavunjika saa 12, jioni saa za kwenda Villa Park!!
Ndoa ni ndoano.
Hata walioko kwenye ndoa nao wanakwenda kujiuza katika  ‘Viwanja vya Fisi’ kwa sababu maisha siku hizi ni magumu. Ndoa ni utumwa siku hizi kwa watoto wa siku hizi.
 Wanaharakati wanatufundisha kwamba Baba  ‘Siku hizi’ hana watoto, hawa ni watoto wetu!
Naam, vijana wetu hawa tunaowaita “wa Siku Hizi” wanatafuta maisha namna hii kwa sababu wazee wameng’ang’ania ajira, wanafanya ufisadi na kuhujumu uchumi ;sasa ‘Kaka-Poa’ na ‘Dada-Poa’ ni wasomi hasa wa vyuo vikuu, na wanafanya umalaya wa mtandaoni kupitia simu za mikononi ,zenye internet kama Broad band, sijui Twitter, Face book n.k
Hata watoto wa kiume wanatamani kubadili jinsi zao za kiume ili wawe wake(Trans Gender) ili ,wajiuze na kufaidi maisha. Akina mama nao wanajibadili jinsi ili wawe waume waoe na kuolewa kwa pamoja! Wamiliki jinsi mbili tofauti,“Two in One” Ili akipatikana  sugar mammy au sugar daddy, sawa. Kaka Poa au Dada poa, ni poa tu.
 Hizi ndizo sera za akina David Cameron na Barack Obama, kama mtu anapinga atanyimwa msaada! Kawaulize wenye NGO kama hawatachangamkia ‘deal’ hii ya kutetea  ‘Haki hizi za Binadamu za mashoga?
 Hili niliache, wasije kunitoa nyongo bure.Tumempinga David Cameron juu juu tu.
Thomas Beatie(37) ni :Dume-Jike” ,Mmarekani, aliyezaliwa Hawaii mwaka 1974 akaitwa Tracy Logondino.
Alipofikisha umri wa miaka 20 akadungwa sindano zenye hormone za kiume(testosterone Injections) ili awe na nywele za kiume tabia ya kiume na sauti nzito.
Mwaka 2002, alifanyiwa operesheni ya kuondolewa matiti(Mastectomy) kwa sababu alitamani kuwa mwanamume. Aliwekewa uume; lakini uke wake haukuondolewa mwilini mwake. Alioa mwanamke aitwaye Nancy, akazaa naye watoto; Susan, Austina na Jensen.
Beatie, akawa ‘Dume-Jike’ ingawa matiti yalishaondolewa kifuani pake. Nataka kusema kwamba, ingawa alioa mke,Nancy, alikuwa pia mke aliyefanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine! Yaani alikuwa mume na mke kwa pamoja!! Hii ndiyo Marekani sasa.
Jamaa huyu sasa amepata ujauzito, anakaribia kujifungua mtoto. Licha ya kuwa baba wa hao watoto watatu: Susan, Austin na Jensen, sasa atajifungua mtoto wa baba mwingine- atakuwa Baba na Mama kwa mpigo!!
Anaishi Arizona, na akijifungua anasema ataondolewa kizazi. Mkewe naye alishaondolewa kizazi- hysterectomy!
Sasa, atakapoondolewa kizazi, anasema atakuwa “Dume la Mbegu” maana anapopata ujauzito basi hormone za kiume huacha kufanya kazi ili kumpa fursa mtoto aliye tumboni kuwa na afya njema. Shaabash!!
Nataka kusema kwamba, Barack Obama , David Cameron, Mashirika yao ya misaada na NGO ZETU(ZIKIWEMO ZA MFUKONI) wanaingia vitani kufanya semina ili sote tubadili “Mind sets” kuuinamia ushoga, usagaji,kubadili jinsi(transgender) n.k
Hakuna noma, eti?! Basi, Poa kaka, lakini siyo wewe kaka poa..
Roho Tatu za vyura zinahamasisha uchafu huu, miujiza ikiwemo ya kisayansi na kishetani, ishara, maajabu, ibada bandia,utajiri wa haraka,picha za uchi(pornography)ngono za mtandaoni, sinema chafu,hadithi za ngono, magazeti ya ngono-ngono,vijarida vya uchi-uchi,kutembea uchi,vivazi vya ajabu vya nusu uchi,miziki ya ngono-ngono ya siku hizi,mitindo ya kidunia n.k
Makanisa na misikitini hawako salama. Madawa ya kulevya,ulawiti,ufisadi na uchafu,madawa ya kulevya yako huko. Rais Kikwete aliposema kuna madawa ya kulevya makanisani na misikitini, watu wakabisha, kumbe ndiyo biashara yao ya siku nyingi, na wametajirika kimiujiza.
Hata makanisani siku hizi, kuna ma-Disko kuliko vilabu vya usiku.
 Eti “disko la Yesu”… Yesu ana disko? Anapigia ukumbi gani nyie? Kuongea na wafu(spiritualism) miujiza ,ya uponyaji kwa fedha ni nini kama siyo nguvu ya  Freemasons, mizimu na dini bandia hizi?
Misikiti inayumba,makanisa yanapoyumba.Maaskofu na makasisi ni walawiti,hata Baba Mtakatifu, Benedicto XIV anaomba radhi kila siku. Viongozi wa dini wanamwaga damu kama Kibwetere wa Kanungu,Uganda. Niliandika siku chache zilizopita juu ya Yunus Santy, kasisi toka Italia kuwabaka wasichana wa shule Mwanza, serikali ikagwaya  kumfunga miaka 30 jela.
Roho Tatu za Vyura huhamasisha uhuru na Haki za Binadamu zaidi na kumwona Mungu ‘Jambazi sugu’ na Dikteta.
Laiti wangejua Mungu anakaa mtaa gani,leo wangekwisha mshitaki The Hague,Uholanzi, kwa kosa la kutishia kuleta kiama duniani, siku ya mwisho.
Watu wanageukia teknolojia kuwa mungu wao, aliye muumbaji wa wanyama,watu na mimea bandia.’Thiories’ kama uibukaji, evolution huondoa hofu kwamba kuna Mungu, sasa wanaume nao wanapata mimba?Wanawake nao wanaoa!
Hata hivyo, najua kuna watu wana NGO za kupinga unyanyapaa dhidi ya wanaume watakaoolewa na wanaume wenzao,wanawake watakaoolewa na wenzao na wanaobadili jinsi zao,ili waoe au kuolewa, machangudoa,kaka poa n.k
Haki za Binadamu wanatwambia ,TUSIWANYANYAPAE! Hili ndilotangazo la Desemba 10 mwaka 1948.
Mtu mmoja hunisumbua  sana nimwambie namba za simu za Freemasons; mimi siwajui Freemason na simo. Mimi ni maskini;sina kitu.
 Bila shaka, hawa nia yao ni kupata utajiri wa haraka,  katika fahamu zao walisha mkataa Mungu, Mungu wao ni tumbo.
 Hii ndiyo Injili Mpya ya Utatu Mtakatifu(Evil Trio)  iliyopata kibali Marekani na Uingereza, na mtu akiikubali anapewa msaada, ama analipwa utajiri. Wapo wengi wanaopenda utajiri wa namna hii; wasinisumbue. Mimi sijui Freemasons wanaishi nyumba namba ngapi?
Mtaa gani…sijui!! Na huyo  ‘Jike-Dume’ simjui, msisumbuke kuniuliza!! Alamsik.
0754/0786-324 074
 

BURIANI KIM JONG IL

 
 KIFO CHA KIM JONG IL NI 'SHANGWE' MAREKANI?
*mwoga wa kupanda ndege amekufa ajalini ndani ya treni!
 
KULIKUWA na watawala ‘magangwe’ ambao hawajawahi kuichelea(kuiogopa) Marekani wakati wowote, katika historia ya Ulimwengu:
  Field Marshal Fidel Alejandro Castro Ruz na mdogoye, Raul Castro wa Cuba, Robert Gabriel Mugabe wa Zimbabwe, Hugo Chavez wa Venezuela, Mahmoud Ahmadnejad wa Iran na Kim  Il Sung na baadaye Kim Jong Il wa Korea Kaskazini.
   Kwa uchache, ni viongozi machachari, “magangwe” waliowahi kuitukana Marekani katika mabaraza ya Umoja wa Mataifa,huko New York, na wakati mwingine walipotukana na kuigomea Marekani wakakabiliwa na vikwazo cha kiuchumi,ndiyo kunyimwa misaada na kushindwa kuuza fursa zake n.k
   Siku za karibuni , vyombo vya habari vya kimataifa  vimekuwa vinajadili  mchakato wa kung’atuka madarakani kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Il, kufuatia afya mbaya, na mchakato wa kumrithisha mwanaye mdogo kuliko wote, Kim Jong Un.
 Ndivyo ilivyotokea, baada ya Kim Jong Il kufariki dunia Jumamosi, Desemba 17 mwaka huu wa 2011.
 Kim Jong Il, alikuwa hazungumzwi vizuri na nchi za Magharibi, kufuatia kiburi chake,wakati mwingine akakisiwa gaidi,mlevi, chakaramu,mpenda vidosho na starehe.
  Inakisiwa kwamba,kwa mwaka mmoja, Kim Jong Il alikuwa akibugia yeye peke yake, konyagi kali na mvinyo wenye thamani ya Dola za Marekani 800,000.
Ni kama  zaidi ya shilingi bilioni moja za Tanzania, alizotumia kupata ‘kilaji’.
 Mwoga wa kupanda ndege, amekuwa akisafiri mara chache mno Uchina na Russia,lakini kwa treni la fahari sana lenye ulinzi mkali. Amekufa safarini akiwa katika treni hilo hilo.
 Kim Jong Il, anatajwa kupenda sana sinema, aliwahi kuandika kitabu kiitwacho, On The Art of Cinema.
 Kim Jong Il ambaye anaachia madaraka ya kuiongoza Jamhuri hiyo ya Korea , kufuatia mauti alizaliwa Baekdu, katika kibanda katika mlima mrefu huko Peninsula ya Korea, zama za Kisovieti.
 Nyaraka za Kisovieti hueleza alizaliwa katika kijiji cha Siberia ambako babaye, Kim Il Sung alikuwa Kapteni wa Brigedi maalum ya Wachina na wakimbizi wa Kikorea.
 Amesoma Pyongyang katika shule ya watoto wa vigogo, Namsam ambako watoto wa vigogo wa vyama vya Wafanyakazi kilichoongoza Kora tangu 1948, walikuwa wakisoma.
 Akasoma chuo Kikuu cha Kim Il Sung na kutunukiwa shahada ya siasa na uchumi mwaka 1964.
 Baada ya chuo kikuu ali pandishwa vyeo katika chama cha wafanyakazi, mwaka 1974 ilishajulikana angemrithi babaye.
 Ni kweli, Julai 8 mwaka 1994 babaye Kim Il Sung akafa, yeyeakachukua madaraka.
Tabia hii hata Afrika tumeiona Gabon, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo(DRC) na mahali pengine, na tunawaona vigogo wetu hapa wakijaribu kuwakweza watoto wao katika nyadhifa nyingi.
 Huyu Kim Jong Il alitazamiwa kumritisha mwanaye wa kwanza, Kim Chul,lakini sasa upepo mwanana unamwelekea Kim  Jong Un.
Mzee huyu ameoa mara tatu, ana watoto watatu, ana dada mmoja.
 Nakupa vimbwanga vya Mzee Kim Jong Il. Aliwahi kuhusishwa na ugaidi na biashara ya madawa ya kulevya.
Kumbuka pia kuna Propaganda za Marekani kwa wale wasiotakiwa;hupakwa matope.
 Kim Jong Il mwaka 1983 alikisiwa na Korea Kusini(Korea Kusini ni adui wa Korea Kaskazini sababu ni kibaraka wa Magharibi) kwamba ndiye aliyepiga mabomu Burma(Myanmar siku hizi) na kuua viongozi 17 wa Korea Kusini waliokuwa huko.
 Mwaka 1987 pia Korea Kusini walimtuhumu kupiga mabomu ndege yao na kuua watu 115 waliokuwemo. Mawakala wa usalama(mashushushu) walitoa siri kwamba eti Kim Jong Il aliamuru ipigwe.
 Huyu jamaa anayeondoka madarakani na kumrithisha mwanaye huyo Kim Jong Un, alikuwa akiongea kwa nadra.
Wengine walidhani ni mbumbumbu ama mkichaa tu.
Aliyekuwa Waziri wa Mambe ya Nje wa zamani wa Marekani, Madeleine K. Albright alifika mjini Pyongyang, Oktoba mwaka 2000 ,akasema baadaye kwamba Kim hakuwa zoba, na siyo mwango kama walivyosema.
       Kiini cha uadui na Marekani
Alianza kurutubisha Uranium mwaka 1990.Wamekuwa wakifanya majaribio ya makombora ya Nyuklia miaka ya karibuni, Marekani kawashawishi kwa pesa nyingi waachane na mpango wao wa Nyukilia,wanasema wanataka kurutubisha Uraniu ili wapate nishati ya umeme.
 Sasa, Marekani ilitaka kuwahonga mapipa mengi tu ya mafuta, imeshindikana, wakaanza kufanya majaribio ya makombora ya Nyuklia chini ya ardhi na baharini,kitendo ambacho hakikupendwa na Korea Kusini na Japan.
 Hata hivyo, Septemba 11 mwaka 2001 Kim Jong Il alimtumia salamu za rambirambi George W. Bush kulaani kiama cha ndege zilizoangamiza WORLD TRADE CENTRE,iliyotaka kulipua Pentagon na ile iliyotua huko Pennsylvania.
 Hata hivyo,
Bush akatangaza kuiondosha Korea Kaskazini katika nchi za mhimili wa Uovu Dunini(Axis of Evil) sambamba ya Iran ya Ahmadnejad na Irak ya Marehemu Saddam Hussein.
 Mrakani iliirejesha Korea hii katika mhimili wa uovu ‘The Axis of Evil”miaka michache iliyopita, mara Korea hii ilipoanza kufanya majaribio ya Nyuklia.
Kim Jong Il alizaliwa Feburuari 16 mwaka 1942 akarithi rasmi madaraka kutoka kwa babaye Oktoba 8 mwaka 1997. Kora ina wanajeshi 1,082,000.
 Baba yake, Kim Il Sung, alikufa mwaka 1994 na aliiongoza nchi hii kwa mkono wa chuma kwa miaka 40. Utaona kwamba Kim Jong ameongoza kutoka mwaka 1994 hadi Jumamosi, Desemba 17 mwaka huu wa 2011 kwa maradhi ya moyo.
  Baba yake, alifanyiwa maombolezo ya kitaifa kwa miaka mitatu hadi 1997 ndipo huyo Kim Jong Il aliyefariki baada ya kuugua muda mrefu alipokuwa mtu wa mwanzo katika nchi za Kikomunisti kumrithi babaye katika kitu cha urais.
 Akachaguliwa kuwa rais mwaka 1998 bila kupingwa. Hata huku watu wanapita bila kupingwa hata katika chaguzi za vyama!
   Umoja wa Mataifa unasemaje?
 Mwaka 2003; ilikuwa Agosti 29 mtangazaji mahiri wa BBC, Tim Sebastian katika kile kipindi chake maarufu, HARDtalk, akamuuliza kiongozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Nguvu za Atomiki(IAEA),Mohammed El Baradei, kwamba ni nchi ipi ya kuogofya sana duniani?
 Ni Korea Kaskazini ama Iran? Dk.El Baradei akasema nchi sita ikiwemo Marekani, zilipokutana Beijing kujadili kitisho cha Nyuklia ulimwenguni,ziliiofia sana Korea hii na mpango wake wa kurutubisha uranium.
Kwamba walitumia mpango huo kujipatia chumo duniani. Halafu alisema Iran nayo ilikuwa inaanza kurutubisha Uranium, lakini Dk. El Baradei akaitaka Iran kufuata mkataba wa NPT(Nonproliferation Treaty) unaopinga ukaguzi kufanyika wa miradi ya Nyuklia.
 
           Korea Kaskazini  hakuna Mungu ila kuna Rais tu!
 Korea Kaskazini  kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa(UN) Mwaka 2005 ilikuwa na watu milioni 29.5 katika maili za mraba 47,399.
 Hapa wanaongea Kikorea na dini zao ni Budha, Chondogyo, na wanaamini Mungu hayupo kabisa duniani, sembuse Korea?!
 Marekani wanasema huko kuna wafungwa wa kisiasa 200,000 na wapinzani wa serikali huteswa na kunyongwa na wengine husota jela kwa kipigo kama watumwa.
 Nimeleta kisa hiki ili kujifunza kwamba hata katika nchi zetu hizi bado kuna matumizi mabaya ya fedha za umma, ulevi wa vigogo kwa pesa za umma na udikteta usio na faida kwa umma.
 Watoto wa vigogo huwarithi baba zao wanapofariki kama huyo Kim Jong Un; wakati huku watoto wa vigogo hurithi kila lililojema, wakati raia wanaponyauka kama maharage wakati wa hari.
 Wakati Kim akitumia bilioni moja kupiga mtindi, huku kwetu bajeti ya shilingi bilioni 30 kwa mwaka, ni za chai ya 'wazee'.na zaidi ta bilioni 20 ni posho za wabunge,bado za vigogo!!
   0786/0754 324 074
 

KIFO CHA KIM JONG IL KITUPE SOMO AFRIKA

Korea Kaskazini,  baada ya kifo cha Rais kuna kituko cha mchakato wa kurithishana madaraka, kutoka kwa  Marehemu Kim Il Jong kwenda kwa mwanaye wa mwisho, Kim Jong-UN. 
 Kim Jong IL naye alirithi utawala kutoka kwa babaye, Kim Il Sung, mwaka 1994.
 Wakati hata hapa Afrika Mashariki, tunayaona sana haya.
 RAIS Yoweri  Kaguta Museveni, Aliuanza mwaka 2009 kwa kumteua mkewe, Janet, kuwa Waziri wa    eneo la Karamoja.
   Watu walipompinga sana kuifanya Uganda kama kampuni binafsi ya familia, akasema Janet ndiye mtu pekee Uganda , ambaye anaweza kukabali kumsaidia kuunganisha eneo hilo lenye kero na dhiki nyingi.
  Kwamba, hapakuwa na mtu Uganda , ambaye angekubali kufanya kazi eneo lenye njaa, vita na machafuko, isipokuwa Janet Museveni. Rais Museveni pia alishalalamikiwa kuwapa vyeo kaka yake na mwanaye, kana kwamba serikali ya Uganda ni kampuni ya familia.
  Familia nyingi za Marais hapa Duniani zina kawaida ya kurithishana madaraka na vyeo serikalini, hata raia wanaposimama kupinga mtindo huo.
   Afrika, inashuhudia marais wakifa, watoto wao wanatawazwa kuchukuwa mahali pao, utadhani hakuna watu wengine wenye utashi, busara ama uwezo.Hata chaguzi za kiini macho zinapofanyika, bado hao watoto wa marais waliofariki, hushinda kwa kishindo na tsunami na kuzima ngebe za wapinzani.
  Mwaka 1979 kulikuwa na wimbi la kuwapindua madikteta.
Na mwanzoni mwa mwaka 2011 wamepinduliwa Madikteta tangu Tunisia,Libya na Misri na upepo bado unavuma Kaskazini,labda utashuka Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Ni wakati  huo  mwaka 1979  akina Amin Dada na Marcius Nguema Biyogo waliondoka madarakani ili kupisha mabadiliko.
   Nataka kusema kwamba, siyo Korea Kaskazini tu ambako Dikteta Kim Il Sung alikufa mwaka 1994 akamwachia mwanaye, Kim Jong Il madaraka na sasa hata Kim Jong Il    alipofariki akawachia Kim Jong-UN.
.Na wala siyo Uganda tu, ambako Janet Museveni amepewa uwaziri na mumewe, ili pengine akiondoka, baadaye apate kumrithi.
   Katika ulimwengu huu watu hutaka kuwarithisha wana, mabinti,ndugu, jamaa na rafiki madaraka ili kulindiana heshima kufuatia wimbi la kuumbuana na kushitakiana kama Zambia na Malawi ambako akina Frederick Chiluba na Bakil Muluzi wamekumbwa na kitisho cha kuishi nyuma ya nondo za magereza.
   Siyo neno kama Janet au jamaa yeyote wa Rais watakuwa wanamapinduzi na wazalendo waliouza mali zao kuikomboa nchi kama Fidel Alejandro na Raul Castro Ruz, huko Cuba .
  Nazungumzia hatari ya viongozi tulio nao hapa Afrika kutumia fedha za walipa kodi, kujijengea himaya za kinasaba au miliki za kifalme na kisultani, katika nchi zetu zinazoitwa eti za kidemokrasia.
   Hawa viongozi wetu hawataki kuondoka madarakani kwa sababu waliikomboa nchi kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza.
WANARITHISHANA MARAKA ili wakiondoka wao maslahi yao yalindwe kama ilivyo Zimbabwe kwa akina Morgan Tsvangirai na R.G. Mugabe.
   Ukichunguza kwa makini, utaona aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika(AU) ,Muammar al-Qaddafi wa Libya alikuwa  hajaondoka madarakani tangu apindue serikali mwaka 1969.
Hata hivyo napingana na maguvu ya NATO kumpindua Gaddafi na kumuua. Afrika yenyewe inapaswa kujadili jambo hili kwa kina,ili kuepuka ukoloni.
Huyu  Gaddafi ndiye aliyesema Uganda kwamba ingekuwa heri ‘wanamapinduzi’ kama Museveni au Mugabe wasiondoke MADARAKANI!
  Hata Misri, Hosni Mubarak aliingia madarakani baada ya Rais Anwar Sadat kuuawa kwa risasi Oktoba 6, mwaka 1981. Alikaa madarakani hadi mwaka huu 2011 alipoondoka kwa NGUVU YA UMMA.
 Kuna maneno maneno kwamba Qaddafi na Mubarak nao walitaka kuwarithisha watoto wao pindi wangeondoka, ili kuweka mambo yao sawa sawa.
   Nchini Kenya , mbio za Uhuru Kenyatta kuingia madarakani zilikitumbukia nyongo chama tawala cha zamani KANU, kikashindwa na Muungano wa Upinde wa Mvua, NARC.
   Naam, katika Tanzania yetu, uataona kitu hiki kurithishana madaraka serikalini na chama tawala baina ya ndugu, watoto na jamaa za vigogo na wenye nasaba.
  Tulishaona watoto wa vigogo wakipigana vikumbo kugombea vyeo, hususan Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM(NEC) na hata wamejaribu kuingia Kamati Kuu(CC) ya Chama ili kulinda huko maslahi, milki na himaya ya baba zao.
   WANAWANIA UBUNGE na nyadhifa nyingine, si kwa sababu wanataka sana kuwatumikia wananchi, bali wanataka kurithi madaraka ya baba zao wanapostaafu.
   Naam, Tanzania kama nchi nyingine nilizotaja, inakuwa vigumu masikini wa vijijini kugombea nafasi za uongozi, wakapata kura za kutosha.
   Kwa sababu, walioko juu wanataka kurithishana madaraka na ndugu na wapambe,kama si marafiki ama wenye nasaba.
. Wanaotaka kudumu kuwa wabunge na mawaziri ni wale wanaoitwa ‘mtoto wa fulani’ ili kulinda milki yao .
 Hawa, ni wake, jamaa, watoto na marafiki za wakubwa, ambao hata Benki Kuu(BoT) tulisikia juzi hapa wakiwa wameajiriwa bila kuwa na sifa.
   Dikteta wa zamani wa Argentina , Juan Peron alitawala mwaka 1946 hadi 55 akapinduliwa na jeshi.
   Mwaka 1973 akarejea toka uhamishoni Uhispania na kuwa rais tena. Alimfanya mkewe wa pili, Isabel kuwa Makamu wake. Huyo Isabel hakupendwa na raia kama mkewe wa kwanza, Eva ama kama walivyomwita, Evita.
   Peron alikufa mwaka 1974, Isabel akawa rais.
 Nchi ikawa ‘wizi mtupu’ kwa sababu ya utawala mbovu, watu kuingia madarakani kwa upendeleo bila uwezo. Mfumuko wa bei ulipanda hadi asilimia 500 hadi akapinduliwa na jeshi.
  Huu upendeleo na ubinafsi natawala za wapambe na unasaba, ndio unaoipeleka Afrika kaburini.
 Kwa sababu wenye uchungu na nchi wananyimwa fursa za kujitawala. Hawana fedha, hawana mvuto kwa wapiga kura wa 'kura za kula'.
Waliorithishwa utawala huwa hawana uchungu na nchi; hawana tofauti na Isabel.Nikuponda maraha tu,kwa fedha za walipa kodi, wanakwenda kujifungua Paris,London au New York wakati raia wanapolazwa wanne kitanda kimoja, ama wanapokufa kwa kukosa tiba.
Wake zao na hawa watoto wao wanakula maisha kwa jasho la walala hoi.
 
   Wana kula maraha mpaka nchi inakauka-wao hawana habari-gharama za maisha zinapanda, wizi wa fedha za umma, ufisadi unakuwa mkubwa ili kugharimia starehe.
 Hata Chadema hawako salama sana na tabia hii ya kurithishana madaraka na vyeo kinasaba-huu ni ukoloni usiovumiliwa hata chembe!
    0786-324 074
congesdaima@yahoo.com
 
 
 

Marehemu Kim Jong Il anapofariki anatuachia Tanzania somo gani?

Korea Kaskazini, siku hizi kuna kituko cha mchakato wa kurithishana madaraka, kutoka kwa  Marehemu Kim Il Jong kwenda kwa mwanaye wa mwisho, Kim Jong-UN. 
 Kim Jong IL naye alirithi utawala kutoka kwa babaye, Kim Il Sung, mwaka 1994.
 Wakati hata hapa Afrika Mashariki, tunayaona sana haya.
 RAIS Yoweri  Kaguta Museveni, Aliuanza mwaka 2009 kwa kumteua mkewe, Janet, kuwa Waziri wa    eneo la Karamoja.
   Watu walipompinga sana kuifanya Uganda kama kampuni binafsi ya familia, akasema Janet ndiye mtu pekee Uganda , ambaye anaweza kukabali kumsaidia kuunganisha eneo hilo lenye kero na dhiki nyingi.
  Kwamba, hapakuwa na mtu Uganda , ambaye angekubali kufanya kazi eneo lenye njaa, vita na machafuko, isipokuwa Janet Museveni. Rais Museveni pia alishalalamikiwa kuwapa vyeo kaka yake na mwanaye, kana kwamba serikali ya Uganda ni kampuni ya familia.
  Familia nyingi za Marais hapa Duniani zina kawaida ya kurithishana madaraka na vyeo serikalini, hata raia wanaposimama kupinga mtindo huo.
   Afrika, inashuhudia marais wakifa, watoto wao wanatawazwa kuchukuwa mahali pao, utadhani hakuna watu wengine wenye utashi, busara ama uwezo.Hata chaguzi za kiini macho zinapofanyika, bado hao watoto wa marais waliofariki, hushinda kwa kishindo na tsunami na kuzima ngebe za wapinzani.
  Mwaka 1979 kulikuwa na wimbi la kuwapindua madikteta.
Ni wakati huo akina Amin Dada na Marcius Nguema Biyogo waliondoka madarakani ili kupisha mabadiliko.
   Nataka kusema kwamba, siyo Korea Kaskazini tu ambako Dikteta Kim Il Sung alikufa mwaka 1994 akamwachia mwanaye, Kim Jong Il madaraka na sasa hata Kim Jong Il    anataka kumwachia Kim Jong-UN.
.Na wala siyo Uganda tu, ambako Janet Museveni amepewa uwaziri na mumewe, ili pengine akiondoka, baadaye apate kumrithi.
   Katika ulimwengu huu watu hutaka kuwarithisha wana, mabinti,ndugu, jamaa na rafiki madaraka ili kulindiana heshima kufuatia wimbi la kuumbuana na kushitakiana kama Zambia na Malawi ambako akina Frederick Chiluba na Bakil Muluzi wanakumbwa na kitisho cha kuishi nyuma ya nondo za magereza.
   Siyo neon kama Janet au jamaa yeyote wa Rais watakuwa wanamapinduzi na wazalendo waliouza mali zao kuikomboa nchi kama Fidel Alejandro na Raul Castro Ruz, huko Cuba .
  Nazungumzia hatari ya viongozi tulio nao hapa Afrika kutumia fedha za walipa kodi, kujijengea himaya za kinasaba au miliki za kifalme na kisultani, katika nchi zetu zinazoitwa eti za kidemokrasia.
   Hawa viongozi wetu hawataki kuondoka madarakani kwa sababu waliikomboa nchi kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza.
WANARITHISHANA MARAKA ili wakiondoka wao maslahi yao yalindwe kama ilivyo Zimbabwe kwa akina Morgan Tsvangirai na R.G. Mugabe.
   Ukichunguza kwa makini, utaona aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika(AU) ,Muammar al-Qaddafi wa Libya akiwa hajaondoka madarakani tangu apindue serikali mwaka 1969.  Gaddafi amepinduliwa na kuuawa.
Huyu ndiye aliyesema Uganda kwamba ingekuwa heri ‘wanamapinduzi’ kama Museveni au Mugabe wasiondoke MADARAKANI!
  Hata Misri, Hosni Mubarak aliingia madarakani baada ya Rais Anwar Sadat kuuawa kwa risasi Oktoba 6, mwaka 1981. Mubarak tayari kapinduliwa na anasubiri mashitaka,kwa kuwa hata Rais wa Tunisia, Ben Ali na Laurent Gbagbo wa Ivory Coast wanasubiri mashitaka, The Hague.
 Kuna maneno maneno kwamba Qaddafi na Mubarak nao wanataka kuwarithisha watoto wao pindi wakiondoka, ili kuweka mambo yao sawa sawa.
   Nchini Kenya , mbio za Uhuru Kenyatta kuingia madarakani zilikitumbukia nyongo chama tawala cha zamani KANU, kikashindwa na Muungano wa Upinde wa Mvua, NARC.
   Naam, katika Tanzania yetu, uataona kitu hiki kurithishana madaraka serikalini na chama tawala baina ya ndugu, watoto na jamaa za vigogo na wenye nasaba.
  Tulishaona watoto wa vigogo wakipigana vikumbo kugombea vyeo, hususan Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM(NEC) na hata wamejaribu kuingia Kamati Kuu(CC) ya Chama ili kulinda huko maslahi, milki na himaya ya baba zao.
   WANAWANIA UBUNGE na nyadhifa nyingine, si kwa sababu wanataka sana kuwatumikia wananchi, bali wanataka kurithi madaraka ya baba zao wanapostaafu.
   Naam, Tanzania kama nchi nyingine nilizotaja, inakuwa vigumu masikini wa vijijini kugombea nafasi za uongozi, wakapata kura za kutosha.
   Kwa sababu, walioko juu wanataka kurithishana madaraka na ndugu na wapambe,kama si marafiki ama wenye nasaba.
. Wanaotaka kudumu kuwa wabunge na mawaziri ni wale wanaoitwa ‘mtoto wa fulani’ ili kulinda milki yao .
 Hawa, ni wake, jamaa, watoto na marafiki za wakubwa, ambao hata Benki Kuu(BoT) tulisikia juzi hapa wakiwa wameajiriwa bila kuwa na sifa.
   Dikteta wa zamani wa Argentina , Juan Peron alitawala mwaka 1946 hadi 55 akapinduliwa na jeshi.
   Mwaka 1973 akarejea toka uhamishoni Uhispania na kuwa rais tena. Alimfanya mkewe wa pili, Isabel kuwa Makamu wake. Huyo Isabel hakupendwa na raia kama mkewe wa kwanza, Eva ama kama walivyomwita, Evita.
   Peron alikufa mwaka 1974, Isabel akawa rais.
 Nchi ikawa ‘wizi mtupu’ kwa sababu ya utawala mbovu, watu kuingia madarakani kwa upendeleo bila uwezo. Mfumuko wa bei ulipanda hadi asilimia 500 hadi akapinduliwa na jeshi.
  Huu upendeleo na ubinafsi natawala za wapambe na unasaba, ndio unaoipeleka Afrika kaburini.
 Kwa sababu wenye uchungu na nchi wananyimwa fursa za kujitawala. Hawana fedha, hawana mvuto kwa wapiga kura wa 'kura za kula'.
Waliorithishwa utawala huwa hawana uchungu na nchi; hawana tofauti na Isabel.
Nikuponda maraha tu,kwa fedha za walipa kodi, wanakwenda kujifunguaaa Paris,London au New York wakati raia wanapolazwa wanne kitanda kimoja, ama wanapokufa kwa kukosa tiba.
 
   Wana kula maraha mpaka nchi inakauka-wao hawana habari-gharama za maisha zinapanda, wizi wa fedha za umma, ufisadi unakuwa mkubwa ili kugharimia starehe.
 Hata Chadema hawako salama sana na tabia hii ya kurithishana madaraka na vyeo kinasaba-huu ni ukoloni usiovumiliwa hata chembe!
    0786-324 074
congesdaima@yahoo.com
 
 

Tuesday, December 13, 2011

UTATU MTAKATIFU WA FREEMASONS,SHETANI NA DINI

SEPTEMBA  mwaka huu,nilikuwa miongoni mwa waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya kuongeza uelewa wa kupinga  unyanyapaa, “Anti Stigma Awareness”.
Tukajifunza kwamba, unyanyapaa ni mbaya; ni chimbuko la majanga makubwa kitaifa na kimataifa, na kwamba aslani, hakuna unyanyapaa chanya duniani.
Hata hivyo, nikajikuta nikibishana mno na Mwalimu juu ya Jamii za Kiafrika kuachana na  UNYANYAPAA juu ya wanaume wanaoingiliwa kimwili,yaani mashoga ama wanawake wanaowaoa wanawake wenzao, wasagaji.
Tulifundishwa kwamba, unyanyapaa hata dhidi ya mashoga ni ukatili, ni kinyume cha ‘Haki za Binadamu’ ni ubaguzi,ni kutenga watu ni udhalilishaji.
 Kwamba, Afrika,imeshindwa kushughulikia watoto waishio mazingira hatarishi, imeshindwa kupambana na umasikini,ufisadi na utawala mbovu, inakazania kunyanyapaa watu wa ndoa za Jinsia Moja-Mashoga na Wasagaji!
 Naam, hii ndiyo Sauti ya Marekani,Ulaya na NGO zetu na Wanaharakati wa Haki za Binadamu. Bado kitambo kidogo, hata vyama vya siasa vitakuwa na sera hizi ili vipate kuungwa mkono na Mabwana wakubwa wa Magharibi.
Ni kwa sababu hii, msomaji ajue, Marekani na Ulaya wameamka ili watufundishe sisi Waafrika kubadili mtazamo wetu ili tusiwanyanyapae mashoga!
Katika mafunzo haya(siwaambii yaliwezeshwa na mashirika gani) tukafundishwa wimbo ufuatao:
“Unyanyapaa,kejeli,viboko,dharau na manyanyaso dhidi ya watoto na Jamii ya mashoga ni janga-unyanyapaa tuulete,tuuchane-chane,tuutupe!”
Ubeti wa Pili tuliuimba hivi:
 “Watoto wetu(wakiwa mashoga) vipaji vyao,busara zao,hekima zao-tuwalete,tuwakumbatie tuwabusu!”
Hakika, huu ndiyo mtazamo wa Bara la Ulaya na Marekani katika kuwashughulikia vijana wetu wanaojiingiza katika  usagaji na ushoga. Kwa Wazungu, ushoga siyo janga(janga ni watoto wa mitaani)ushoga ni uhuru zaidi na maamuzi ya mtu mwenyewe-hakuna  kubeza na kuhukumu!
Katika Unabii wa Biblia, katika Ufunuo wa Yohana 16:13 kumetabiriwa ‘Roho Tatu za Uchafu’(Utatu Mtakatifu wa Uovu) za vyura, zinapotoka kinywani mwa Shetani,Mamlaka kuu za Dunia na Muungano wa Dini na Serikali za Dunia.
Kumbe Biblia inatabiri kwamba mambo haya yatatoka katika kinywa cha Mamlaka za Dunia zitakapoungana na Mamlaka za Madhehebu ya Dini, ambayo ni pamoja na Umizimu, Teknolojia na ukisasa utakaokwenda kuandaa ‘Vita vya kiroho’ vya Har Magedon.
   Roho Tatu mfano wa vyura,maana yake nini?
Chura, ni alama ya uchafu. Katika Misri ya kale,chura alikuwa nembo ya mungu mke,Heget, aliyeaminiwa kwamba alikuwa chimbuko la uhai kwa watoto wanaozaliwa-nguvu kwa vijana.
Huu Utatu Mtakatifu wenye sura ya chura(Evil Trio) umevaa umizimu wa kisasa,uasi wa kidini, na hali ya vijana kuona DHAMB( uasi wa sheria za Mungu) kama kitu cha kawaida tu.
Leo, vijana wengi wakifanya makongamano,hujiuliza,”Hivi Mungu yupo kweli?”
Ndivyo alivyouliza Farao wa Misri zama zile za Nabii Musa, kama miaka 1500 BC.
Vijana wanataka kuwa huru kutoka hofu ya kuwapo kwa Mungu; wanakusudia kuishi huru, na wanamwona Mungu na sheria zake Dikteta-vijana wanataka haki zaidi katika kufanya mambo yao.Ndivyo zilivyokuwa siku za Nuhu na Loti.
Mila na desturi nyingi za Afrika zinakinzana na vijana wa kileo wa kizazi hiki cha ‘dot com’ katika zama za utandawazi za karne hii.
Mila na desturi za Afrika,zingali zikiheshimu sana ndoa ya Jinsia tofauti(heterosexual couples).
Ndoa kati ya mume na mke, ndiyo mwanzo wa familia bora na imara iliyoasisiwa na Mungu katika Bustani ya Edeni, kadiri ya miaka 4004 BC.
Roho Tatu za vyura zinapinga kwa dhati uhalali wa ndoa za Jinsia Tofauti pekee. Roho hii inayotoka mdomoni mwa watawala wa dunia walioungana na Freemasons na teknolojia, wanataka kuwe na ushoga, usagaji, ndoa za mikataba, useja wa kudumu maishani,kuasili(adopt) watoto, ama kupata watoto kwa njia ya maabara (test-tube babies); na hata binadamu kutengenezwa katika maabara,yaani human cloning.
Maisha ni magumu, Haki za Binadamu hizi zinawapigia debe wanaume na wanawake kufanya biashara ya ngono(Commercial Sex Work) ili kujipatia kipato.
 Ndiyo maana, ukienda katika vilabu vya usiku na madanguroni utawakuta wasichana wetu “Dada Poa” wakijidaki ili wapate ujira. Wanashindana na makaka poa(mashoga) katika biashara hii, inayopingwa huku wakati imehalalishwa tayari na Wazungu,Mashirika yao na NGO na wanaharakati wa huku kwetu.
Kwa sababu lipo wimbi kubwa la watu kuhamia mijini(Urbanization) huu Utatu Mtakatifu wa vyura utawakuta vijana wengi wanaohama vijijini kwenda mijini,wakiwa waongufu wapya. Maadili ya Muafrika yataondoka na Wazee ambao sasa wana miaka kuanzia 55 na kuendelea na ni wachache tu.
 Afrika,kuna vijana wengi na watoto kuliko hawa watu wazima wanaojidai kupinga ushoga na mmomonyoko  wa maadili siku hizi.
Vijana, kupata watoto waliozalishwa katika maabara kama Marehemu Michael Jackson, hapo sawa. Kwanza ,wasichana na wavulana hawataki watoto-wanawatupa kwenye madampo.Heri wabebe midoli  hata ya ‘dogi’na kutembea nayo mitaani.
 Sasa, nani atalea watoto na maisha haya magumu? Hata kilimo sasa hatutaki,tutakula mchele wa maabara. Ni kuongea na simu na kutazama ngono mtandaoni,kusikiliza muziki kwenye simu, asubuhi hata jioni.
Hata  wasichana wakizaa hawataki kuwanyonyesha  watoto ziwa la mama, wasije kuzeeka bure na kukosa starehe.Wengine wanawatupa chooni ama dampo kwenye mifuko ya Rambo! Nani alee, sasa?
Vijana wanachelea kuwa wazee, wanakazana hata kumeza vidonge wasizeeke, na wazee wengine wanameza dawa za kuwarejesha ujanani-Afrika uzee sasa ni janga kuliko Ukimwi! Hawataki kukonda, wananunua dawa za Ki-China.
Wasichana wakizaa kabla ya ndoa, hawanyonyeshi watoto titi la mama.Wengi wao wameingia katika ndoa za mikataba,kwa sababu wanasema ndoa siku hizi ni utumwa. Nani aolewe? Kuoa ama kuolewa eti ni utumwa, sababu ni uchumi wa dunia kuwa mgumu. Hata kuosha vyombo ni utumwa.
He! Mwe!! Msichana mrembo aache kujipamba na kwenda kujiuza mitaani apate maisha, eti aolewe? Ndiyo maana ndoa inafungwa saa sita mchana, inavunjika saa 12, jioni saa za kwenda Villa Park!!
Ndoa ni ndoano.
Hata walioko kwenye ndoa nao wanakwenda kujiuza katika  ‘Viwanja vya Fisi’ kwa sababu maisha siku hizi ni magumu. Ndoa ni utumwa siku hizi kwa watoto wa siku hizi.
 Wanaharakati wanatufundisha kwamba Baba  ‘Siku hizi’ hana watoto, hawa ni watoto wetu!
Naam, vijana wetu hawa tunaowaita “wa Siku Hizi” wanatafuta maisha namna hii kwa sababu wazee wameng’ang’ania ajira, wanafanya ufisadi na kuhujumu uchumi ;sasa ‘Kaka-Poa’ na ‘Dada-Poa’ ni wasomi hasa wa vyuo vikuu, na wanafanya umalaya wa mtandaoni kupitia simu za mikononi ,zenye internet kama Broad band, sijui Twitter, Face book n.k
Hata watoto wa kiume wanatamani kubadili jinsi zao za kiume ili wawe wake(Trans Gender) ili ,wajiuze na kufaidi maisha. Akina mama nao wanajibadili jinsi ili wawe waume waoe na kuolewa kwa pamoja! Wamiliki jinsi mbili tofauti,“Two in One” Ili akipatikana  sugar mammy au sugar daddy, sawa. Kaka Poa au Dada poa, ni poa tu.
 Hizi ndizo sera za akina David Cameron na Barack Obama, kama mtu anapinga atanyimwa msaada! Kawaulize wenye NGO kama hawatachangamkia ‘deal’ hii ya kutetea  ‘Haki hizi za Binadamu za mashoga?
 Hili niliache, wasije kunitoa nyongo bure.Tumempinga David Cameron juu juu tu.
Thomas Beatie(37) ni :Dume-Jike” ,Mmarekani, aliyezaliwa Hawaii mwaka 1974 akaitwa Tracy Logondino.
Alipofikisha umri wa miaka 20 akadungwa sindano zenye hormone za kiume(testosterone Injections) ili awe na nywele za kiume tabia ya kiume na sauti nzito.
Mwaka 2002, alifanyiwa operesheni ya kuondolewa matiti(Mastectomy) kwa sababu alitamani kuwa mwanamume. Aliwekewa uume; lakini uke wake haukuondolewa mwilini mwake. Alioa mwanamke aitwaye Nancy, akazaa naye watoto; Susan, Austina na Jensen.
Beatie, akawa ‘Dume-Jike’ ingawa matiti yalishaondolewa kifuani pake. Nataka kusema kwamba, ingawa alioa mke,Nancy, alikuwa pia mke aliyefanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine! Yaani alikuwa mume na mke kwa pamoja!! Hii ndiyo Marekani sasa.
Jamaa huyu sasa amepata ujauzito, anakaribia kujifungua mtoto. Licha ya kuwa baba wa hao watoto watatu: Susan, Austin na Jensen, sasa atajifungua mtoto wa baba mwingine- atakuwa Baba na Mama kwa mpigo!!
Anaishi Arizona, na akijifungua anasema ataondolewa kizazi. Mkewe naye alishaondolewa kizazi- hysterectomy!
Sasa, atakapoondolewa kizazi, anasema atakuwa “Dume la Mbegu” maana anapopata ujauzito basi hormone za kiume huacha kufanya kazi ili kumpa fursa mtoto aliye tumboni kuwa na afya njema. Shaabash!!
Nataka kusema kwamba, Barack Obama , David Cameron, Mashirika yao ya misaada na NGO ZETU(ZIKIWEMO ZA MFUKONI) wanaingia vitani kufanya semina ili sote tubadili “Mind sets” kuuinamia ushoga, usagaji,kubadili jinsi(transgender) n.k
Hakuna noma, eti?! Basi, Poa kaka, lakini siyo wewe kaka poa..
Roho Tatu za vyura zinahamasisha uchafu huu, miujiza ikiwemo ya kisayansi na kishetani, ishara, maajabu, ibada bandia,utajiri wa haraka,picha za uchi(pornography)ngono za mtandaoni, sinema chafu,hadithi za ngono, magazeti ya ngono-ngono,vijarida vya uchi-uchi,kutembea uchi,vivazi vya ajabu vya nusu uchi,miziki ya ngono-ngono ya siku hizi,mitindo ya kidunia n.k
Makanisa na misikitini hawako salama. Madawa ya kulevya,ulawiti,ufisadi na uchafu,madawa ya kulevya yako huko. Rais Kikwete aliposema kuna madawa ya kulevya makanisani na misikitini, watu wakabisha, kumbe ndiyo biashara yao ya siku nyingi, na wametajirika kimiujiza.
Hata makanisani siku hizi, kuna ma-Disko kuliko vilabu vya usiku.
 Eti “disko la Yesu”… Yesu ana disko? Anapigia ukumbi gani nyie? Kuongea na wafu(spiritualism) miujiza ,ya uponyaji kwa fedha ni nini kama siyo nguvu ya  Freemasons, mizimu na dini bandia hizi?
Misikiti inayumba,makanisa yanapoyumba.Maaskofu na makasisi ni walawiti,hata Baba Mtakatifu, Benedicto XIV anaomba radhi kila siku. Viongozi wa dini wanamwaga damu kama Kibwetere wa Kanungu,Uganda. Niliandika siku chache zilizopita juu ya Yunus Santy, kasisi toka Italia kuwabaka wasichana wa shule Mwanza, serikali ikagwaya  kumfunga miaka 30 jela.
Roho Tatu za Vyura huhamasisha uhuru na Haki za Binadamu zaidi na kumwona Mungu ‘Jambazi sugu’ na Dikteta. Laiti wangejua Mungu anakaa mtaa gani,leo wangekwisha mshitaki The Hague,Uholanzi, kwa kosa la kutishia kuleta kiama duniani, siku ya mwisho.
Watu wanageukia teknolojia kuwa mungu wao, aliye muumbaji wa wanyama,watu na mimea bandia.’Thiories’ kama uibukaji, evolution huondoa hofu kwamba kuna Mungu, sasa wanaume nao wanapata mimba?Wanawake nao wanaoa!
Hata hivyo, najua kuna watu wana NGO za kupinga unyanyapaa dhidi ya wanaume watakaoolewa na wanaume wenzao,wanawake watakaoolewa na wenzao na wanaobadili jinsi zao,ili waoe au kuolewa, machangudoa,kaka poa n.k
Haki za Binadamu wanatwambia ,TUSIWANYANYAPAE! Hili ndilotangazo la Desemba 10 mwaka 1948.
Mtu mmoja hunisumbua  sana nimwambie namba za simu za Freemasons; mimi siwajui Freemason na simo. Mimi ni maskini;sina kitu.
 Bila shaka, hawa nia yao ni kupata utajiri wa haraka,  katika fahamu zao walisha mkataa Mungu, Mungu wao ni tumbo.
 Hii ndiyo Injili Mpya ya Utatu Mtakatifu(Evil Trio)  iliyopata kibali Marekani na Uingereza, na mtu akiikubali anapewa msaada, ama analipwa utajiri. Wapo wengi wanaopenda utajiri wa namna hii; wasinisumbue. Mimi sijui Freemasons wanaishi nyumba namba ngapi?
Mtaa gani…sijui!! Na huyo  ‘Jike-Dume’ simjui, msisumbuke kuniuliza!! Alamsik.
0754/0786-324 074





Monday, December 12, 2011

WABUNGE WA TANZANIA NA POSHO NA SHAMBA LA WANYAMA


WABUNGE ni wanasiasa.
Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muunganoi wa Tanzania ni wanasiasa.Wanasiasa wote(kasoro wachache tu) hufanana; hulingana na wote wana malengo mamoja ya kupata madaraka,kujiongezea vyeo na ukwasi na kasha kutumia madaraka waliyopata kwa fedha zao ili kujiongezea fedha.
Wanasiasa hutumia madaraka wanayopata ili kujiongezea utajiri, na kasha hutumia utajiri ili kujilimbikizia vyeo,madaraka na ‘uheshimiwa’. Wanasiasa wote duniani hufanana; ni wachoyo na wabinafsi.
Mwanamuziki , Roger Whittaker, alipata kuimba hivi:
“Politicians are like a bunch of bananas. They hang together, they all are yellow, and there is not a straight one”.
Kwa tafsiri yangu, Whittaker angeimba hivi kwa Kiswahili. “Wanasiasa ni mithili ya ndizi katika chana moja.Hushikana mahali pamoja; ndizi zote zina rangi moja ya njano; na kati ya hizi hakuna hata moja iliyonyooka!”.
Ndizi zote zimepinda! Na wanasiasa wote wamepinda; ni kama walizaliwa pamoja, wanashikiliwa pamoja(kwenye uchu wa madaraka,ukwasi na tama ya kila jambo)pamoja na vyeo na maslahi. Rangi yao ni moja-NJANO-ni wapenda maslahi na hawatabiriki, na hakuna hata mmoja kati yao aliyenyooka.
Lesoni ya Waadventista wa Sabato ya Oktoba-Desemba,mwaka huu 2011,ukurasa wa 105, kumeandikwa hivi:
“Politicians say one thing when seeking election, and then do the opposite once in office, all the while accepting thinly veil bribes from special interests”.
Wanasiasa wote duniani, wakisemacho wakati wanapotafuta kuchaguliwa wakati wa chaguzi anuwai, pindi wakipata madaraka hufanya kinyume chake; na wanachotazama ni maslahi yao hata kama yamekuja kwa njia haramu.
Wanasiasa, wakisemacho hawakitendi; wakitendacho hawakisemi. Unaweza kusema hivi kwa Kiingereza, “They never Walk the Talk” wana maneno matupu yasiyo na vitendo, wana ahadi hewa na matumaini ya bure kwa wale wanaowaongoza. Ghiliba Ghilibu?
Twapaswa kutowaamini wanasiasa. Tunao wengi duniani, hata hapa Tanzania wanasiasa hata wa kusoma wapo wengi,lakini hawana faida. Shida yetu ni ombwe la uongozi. Viongozi ama hawapo, au hata kama wapo hawajulikani walipo.
Kwa sababu ya kukosekana viongozi, ndiyo maana wanasiasa wale wote tunaowaita viongozi(kwa ujumla wao) wanakubalina kwa pamoja bila kujali itikadi zao kwamba wajiongezee posho za vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kutoska shilingi 70,000 hadi 200,000 kwa siku.
Hili ni ongezeko lazaidi ya asilimia 180. Spika wa Bunge, Anne Makinda, anasema sababu ya kufanya hivi ni kupanda kwa gharama za maisha,hususan Dodoma, mahali waheshimiwa hawa(wanasiasa-wabunge) wanakoishi nyakati za vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Gharama za maisha zimepanda Dodoma(siyo nchi nzima?),halafu kwa waheshimiwa wabunge tu? Gharama za maisha hazijapanda katika maeneo mengine ya nchi wanakoishi Watanzania wengine zaidi ya milioni 42?
Majibu ya maswali haya ni rahisi mno.Kwamba, kwa tabia ya wanasiasa, wao hujijua wao peke yao, Watanzania waliobaki huwa hawajulikani.
Kila siku waheshimiwa hawa husikika wakisema, “Mimi na watu wangu!” Yaani sisi(Watanzania) ni watu wao!
Halafu husema, “Jimboni kwangu” yaani majimbo yote na watu wote ni mali zao, kwa sababu hiyo wamepewa mamlaka ya kuamua chochote kwa niaba yetu, wanafikiri kwa niaba yetu, na hata wao wakishiba wakati sisi tuna njaa kwao wanaona ni sawa sawa!
Dodoma, wakati wa vikao vya Bunge,kuna waheshimiwa na wapambe na familia zao wanapotambulishwa na Mheshimiwa spika. Kuna watu wengi wanaoandamana Dodoma na kufanya maisha yapande huko, halafu akina David Jairo wanakusanya pesa za umma na kuwalipa posho nono,kwa kile ambacho wala hakina maslahi ya taifa.
Dodoma, wakati wa vikao vya Bunge, kuna watu wengi,kuna ‘ma kaka poa’ na  ‘ma dada-poa’ wanaozengea zengea pesa za posho zitokanazo na kodi zetu. Hili niliache.
Nataka kusema kwamba, waheshimiwa Wabunge wao wanajiona ni muhimu sana kuliko wananchi wa kawaida.
Kama msomaji unabisha,nenda kasome kitabu kiitwacho, ANIMAL FARM(Shamba la Wanyama) cha Mwandishi wa Kiingereza, George Orwell.
Orwell, aliandika kejeli(satire) kwamba,katika Shamba la Wanyama, viongozi wa wanyama wao walijiona, “More equal than others” wanao usawa zaidi ya wanyama wenzao;yaani walistahili maslahi zaidi ya wanyama wa kawaida katika haka ‘kasungura kadogo’!!
Naam, waheshimiwa wabunge wetu wanafanana mno na waliokuwa viongozi wa Shamba la Wanyama wa George Orwell.Kwamba wao “ are more equal than other Tanzanians” tuseme wao ni bora zaidi kuliko sisi,ndiyo maana maisha yanakuwa magumu kwao zaidi kuliko sisi,tena ni magumu zaidi Dodoma kuliko majimboni kwao!
Nimuunge  Mkono David Kafulila, Mbunge wa Kigoma Kusini, kwamba wanalipwa mshahara kwa sababu ya vikao huko Dodoma, Bungeni, sasa posho za vikao za nini wakati tayari wamelipwa mshahara kwa kazi hiyo?
Ukiacha Kafulila na wengine wachache, wabunge wote wameweka itikadi zao pembeni kuchukua posho nono,kwa hiyo hawana tofauti sana na ‘Nguruwe’ wa George OIrwell katika Shamba la Wanyama.
George Orwell hakukusudia kumwita mtu yeyote nguruwe, hii ni kejeli name sikusudii kuwaita viongozi wetu nguruwe, ila nguruwe walikuwa viongozi katika Shamba la Wanyama la George Orwell ambalo nimechukua mfano kuwasilisha ujumbe wangu.
George Orwell, alilenga kuwasema wanasiasa ‘tamaa mbele-mauti nyuma’ na mabeberu ambao walidhani uongozi ni kujitofautisha na umma, ni kustahili heshima zaidi,maslahi,zaidi mafao manono zaidi na stahili zaidi kuliko wananchi wa kawaida.
Tunajadili Haki za Binadamu na usawa na uhuru wa kweli katika hii miaka 50 ya Uhuru iliyosherehekewa kwa mbwembwe juzi.
Tunajadili usawa, ambao tunasema Katiba yetu inasema, ‘Binadamu wote ni sawa”.
 Je, kuna usawa katika Shamba la Wanyama, wakati viongozi wanapojiona kuwa na ‘usawa zaidi’ kuliko sisi wengine?
Kwa mfano, wananchi sisi wa vijijini, ambao maisha ni magumu mara dufu kuliko mji wowote, achilia mbali Dodoma, tunaambiwa ‘kasungura ni kadogo’ hata wanafunzi wanaketi sakafuni, tuseme mchangani maana hata hiyo sakafu hakuna, wanapokuwa madarasani.
Tunaambiwa ‘kasungura ni kadogo’ wakati hatuna barabara, hospitali, zahanati,maji salama n.k
Halafu, watu wanadhani hawa wanasiasa wabaya ni wa chama Fulani tu. Kwa ujumla kwenye maslahi wote hufanana,( labda kasoro Kafulila na wenzake); ndiyo maana Whitteker akaimba kwamba, “They are like a bunch of bananas. They hang together, they all are yellow and there is not a straight one”
Siyo Mbowe, Siyo Shibuda, Mizengo Pinda na wenzao, woote ni wamoja na wameshikiliwa na moyo mmoja(maslahi ya wabunge na posho zaidi) na wote ni rangi moja-NDIZI- na hakuna aliyenyooka!!
  congesdaima@yahoo.com
0786/0754-324 074