Tuesday, April 24, 2012

UNATAKA UTAJIRI?-5

                                            *Mtafute nyoka aitwaye Asclepius
DESEMBA 21, MWAKA 1988, Boeing 747 ya Pan American World Airways (Pan Am) ililipuliwa na waliodhaniwa magaidi,kutoka Libya.
Ilianguka eneo la Lockerbie, nchini Scotland, na kuua watu 270, kati ya hawa 11 walikutwa ardhini.
 Hiyo ndege, Flight 103 ya Pan Am,kumbe haikulipuliwa na akina Basset Ali al-Meghri, kama ilivyokuja kujulikana hivi karibuni.
 Freemason, walipanga ajali hiyo, Shetani akalamba damu za watu hao 270,kisha wakasingiziwa ‘Mashushushu’ hao wa Libya.
 Kanali Muammar al-Gaddafi akitaka kujikomba Magharibi, akamkabidhi al-Meghri, Aprili 5 mwaka 1999 kwa Wamarekani, wakamhukumu kifo  Januari 31 mwaka 2001 kwa kosa ambalo wamekuja kusema hivi karibuni kwamba al-Meghri na wenzake hawakuhi kulifanya-Walionewa!
 Basset al-Meghri, ameachwa huru,yupo Tripoli ambako anagugumia kwa maumivu ya Saratani.
 Nimerejea kisa hiki hapa, ili msomaji makini atafakari vitu vingi sana hapa,hata kumaizi nyumerali hizi hapa ambazo pia hutumiwa na Freemasons.Halafu, nataka kufafanua utajiri unaopatikana kupitia UTATU MTAKATIFU wa Ulaya,Marekani na Mfumo Mpya wa dini unaokuja duniani, ambao nitauita, Yezebeli.
 Naam, leo najadili ‘UTATU MTAKATIFU’ ambao pia ni “UTATU MTAKAVITU” ambao ulitumiwa na Biblia katika kueleza matendo ya Balaam, Balaki na Yezebeli,katika Ufunuo 2:14-20.
Hawa, Balaam,Balaki na Yezebeli, wametajwa kuishi miongoni mwa watumishi wa Mungu,katika makanisa  ya Pergamo na Thiatira,huko Asia Ndogo.
 Balaam, Balaki na Yezebeli huwakilisha watu wa ‘tabia tatu’ tofauti ambazo nakusudia kujadili katika sehemu hii. Bahati mbaya, watu wengi wanenipigia simu kutaka niwaoneshe namna wanavyoweza kujipatia utajiri kwa kutumia Freemasons. Hawa wazingatie maelekezo haya hapa chini.
  Kwanza, Balaki alikuwa Mfalme wan chi ya waabudu sanamu na mizimu ya Moabu. Balaki alimshauri Nabii Balaam ‘Kuwalaani ‘ Waisraeli bila kupata mafanikio. Tazama Kitabu cha Hesabu sura mbili za 23 na 24.
Yezebeli, alikuwa ‘MALKIA’ alifefadhili Manabii wa Baali na Ashtoreth(1Wafalme18:19),Miungu hii ingalipo na huabudiwa katika ulimwengu wa sasa na watu pasipo kujua,kama nitakavyofafanua.
Badala ya Nabii Balaam kuwabariki hao watu wa Mungu, badala yake laana alizoitwa kutoa kwa ujira wa fedha ili awe tajiri, zikageuka Baraka maridhawa.
 Kupenda pesa kupita kiasi, ni chimbuko la uhalifu na mabaya tele duniani(1Timotheo6:10).
Huyu nabii Balaam hutajwa pia katika AGano Jipya mara tatu(2Petro2:15,Yuda 11,na Ufunuo 2:14),Balaam ni kielelezo cha tamaa ya utajiri haramu,fedha chafu na dhambi.
 Alikuwa tayari kufanya jambo lolote,mradi ajipatie fedha-hata kama ni kutoa kafara watoto na jamaa zake kwa Shetani-ndivyo dunia ilivyo leo.
Alikuwa kufanya chochote alichoambiwa na Mfalme wa Moabu,Balaki, mradi alipwe fedha, bila kujali madhara yake. Biblia inamwita Balaam ‘mkichaa’ ambaye hadi alikaripiwa vikali na punda aliyekuwa akisafiria.
Kwa mara ya kwanza,punda aliweza kusema kwa lugha ya kibinadamu,ili kuonya tama ya Nabii mpenda utajiri. Punda alisema mithili ya mwanadamu za za Nabii huyu chakaramu, mwenye tama ya utajiri.
 Hata siku hizi wangalipo manabii wengi bandia wanaomwakilisha Balamu, ambao kwao pesa ni bora kuliko chochote. Siku hizi, wangalipo akina ‘Balaam’ lukuki ambao husababisha vikwazo mbele ya watu wa Mungu lukuki.
 Biblia ya Kiingereza husema, hawa manabii uchwara wanaleta ukwazo, “Who taught Balak to cast a stumbling block before God’s people”.
Manabii wa zama hizi hupenda fedha maradufu kuliko Balaam, na huwafundisha wafalme(akina Balaki) kuleta vikwazo kwa  watu wa Mungu siku hizi ili wasujudie sanamu, mashetani na miungu kusudi lao likiwa kupata chakula na mahitaji ya kimwili. Tazama Ufunuo 2:14
Najadili utajiri haramu wanaotafuta manabii wa siku hizi na mitume wanaozuka kila siku na kuanzisha vijikanisa.
“To love gain from wrongdoing” ni kupenda fedha kwa njia haramu sana,kama kuuza wokovu kwa njia ya maji ya Baraka, vitambaa vya upako ambako ni sawa na ufisadi wa kiroho, rushwa,wizi n.k
Iko siku punda   watasema kwa sauti ya kibinadamu kuwakemea hawa Manabii na mitume uchwara, ambao wakati mwingine wamevunja ndoa za watu kwa uzinzi, wamebaka akina mama.
Yule punda aliyemkemea Balaam, atawakemea hawa ambao siku hizi wamezidi kufanya ufisadi wa kiroho na kimwili kuliko allivyofanya Nabii Balaam. Wameanzisha vijikanisa utatiri,kila mmoja na upako na kakanisa kake,ili ajipatie chakula,gari na maisha ya anasa.
 Wanajidai ‘kubariki’ watu wa Mungu kumbe ni laana tupu, watu wamejikuta wakizini na mijoka na pepo wachafu huko makanisani! Serikali ipo,lakini imewaacha hawa akina Balaam kuendeleza u-Balaam wao, na wanaposhuka madhabahuni, hulalama kwamba serikali imejaa ufisadi na wizi!!
 Naam, hawa ni ‘Mabinti’ wa Yule Kahaba aketiye juu ya mnyama mwekundu sana katika Ufunuo 17:1-11.
Hii hapa ni sauti ya punda( a dump ass speaking  with human voice) imekuja kutuliza kichaa cha manabii uchwara hawa, na mitume bandia wa Kristo uchwara na Ibilisi. Hawa waache kughilibu watu wa Mungu kwamba huwapa Baraka,kumbe laana tupu.
Waumini wajinga wametoa mali zao katika madhabau za Freemasons wakitegemea utajiri bandia, wengine wametoa kafara wake,waume, watoto na wazazi kwa taraja ta utajiri na Baraka, kumbe walidhani wamepata,wakapatikana!!
 Hii ni pata potea ya manabii na mitume wa siku hizi wenye tama ya pesa na tama ya utajiri wa haraka. Wamemgeuza kila mtu Balaam-watu wako machopima kuchuchumilia utajiri wasiojua chanzo chake-kazi zimeachwa,mashamba yameota magugu, watu wote wamewageukia manabii na mitume ili kupata utajiri!
  Serikali inahangaika kutafuta mafisadi katika Baraza la Mawaziri la Rais Kikwete? Wengine wako makanisani, wana utajiri usiojulikana, wanaendesha magari ya fahari kuliko wabunge, makatibu wakuu wa wizara, wakurugenzi n.k
Fedha na fahari wametoa wapi? Wameuza kitu gani kama siyo biashara haramu ya maji ya Baraka, vitambaa vya upako na utapeli kwa kutumia majoka?
 Juzi, Bunge liliwaka moto,wabunge wakilaani ufisadi, mwingine uko ndani ya vijikanisa,kwa manabii wa siku hizi na mitume bandia wa Kristo!
 Waziri Mkuu Pinda, akiachia ngazi kwa sababu ya ufisadi wa mawaziri wake, na hawa wasiachwe kuendelea kutapeli raia kwa jina la Yesu!
 Tamaa ya utajiri ilimfanya Balaam kushindwa kumwona Malaika wa Bwana,lakini Punda akamwona. Hawa ni vipofu,na wasithubutu kuniombea vibaya kwa miungu yao,Freemasons, watanibariki mno!!
 Naam, manabii wengi na mitume wa siku hizi ni vipofu,hawaoni na afadhali punda wana macho ya kuona vitu vitakatifu. Hujipendekeza kwa wafalme akina Balaki,mradi wapewe fedha, hata kama kwa kufanya hivyo ni kumkosea Mungu wanayejidai kumtumikia.
 Ndiyo maana siku hizi utasikia ubakaji misikitini na makanisani,kuvunja ndoa za watu,makasisi kuwatia mimba wake za watu na kutelekeza watoto! Kuna Mungu wapi bwana huko siku hizi?
Ukiwaambia wanakutafuta kukuua kwa jina la masangoma!Sasa, hawa watu wa Mungu wa wapi, serikali nayo inaacha kuwatia mbaroni ili wafungwe jela kwa makosa mengi ukiwemo utapeli, rushwa na mauaji ya watu wasio na hatia.
 Kazi yao siku hizi ni kugombania waumini. Hawa ni waabudu sanamu,ni wachoyo kama Akani, ni akina Gehazi wanaoenda vileleni mwa milima katika madhabahu za Baali kujipatia chumo la faida. Naam chumo la aibu kwa kutumia vijikanisa utitiri ambamo hakuna kitu bali kuwanga kwa makelele ya kiruu na aibu-serikali haioni?
 Hawa ni manabii wa Yezebeli, Ibilisi na Joka. Tumjadili kidogo Yezebeli wa kanisani Thiatira.Aliwafundisha watu kuabudu sanamu.Sanamu ni uzinzi wa kiroho, hivyo hata watumishi wa Mungu wakaanza kuabudu Baal-Peori! (Hesabu 25:1-3)
Yezebeli wa leo ni MALKIA aketiye migongoni mwa wafalme wa dunia(Ufunuo 17:3-18), hawa ni kundi la watu wanaojidai kumwabudu Mungu kumbe wana ajenda ya UTAJIRI na MAMLAKA YA ULIMWENGU.Makusudi yao ni kuwakosesha watu wajikwae na kula vyakula vilivyotolewa kwa sanamu(Ufunuo 2:20).
 Tumjadili pia mfalme wa Moabu,yaani Balaki.Balaki ni tajiri, ana fedha na huwalipa manabii hawa uchwara fedha na utajiri ili walete Baraka bandia kwa watu duniani-hizi ndizo ishara zidanganyazo.
 Mfalme Balaki wa Moabu ya siku hizi anafanya kila jambo hata kama kuwasingizia watu ili wapate kuwafunga jela,kama walivyowafanya wale mashushushu wa Libya, akina Basset Ali al-Meghri.Watazidi kuwaua watu huko mbele ya safari Ufunuo 13:14-17.
 Mfalme wa Moabu Balak hana tofauti kubwa na Barack(OBAMA) wa Marekani(Moabu ya kiroho) ambaye huwalipa fadhila manabii utitiri. Aina hii ya madhehebu imezuka kwa wingi Marekani,na huchangiwa fedha kuja kuendesha hadaa na utapeli huku.
  Hawa, watashirikiana na Ibilisi na Freemasons ili kujidai kuleta Baraka kwa dunia. Mfalme Balak wa Moabu ya kiroho atakubaliana na UTATU MTAKAVITU wa Yezebeli,Balaam  ili kutengeneza sanamu(Ufunuo 13:14) watafanya biashara kwa vibali maalum na wasiotaka wamewekewa vikwazo vya uchumi ili wasifanye biashara Ufunuo 13:17.
 Dunia nzima itaabudu sanamu Ufunuo 13:12. Utatu Mtakavitu wa Yezebeli, Balaki na Balaam utakusanya watu kwa vita ya Har-Magedon(Ufunuo 16:13-16) lengo ni kumpinga Mungu wa kweli kwa ishara na maajabu!
  Miujiza! Balaki, Balaam na Yezebeli, watasababisha Mapigo Saba ya Mwisho- haya ni majanga ya kiasili ambayo ukiyachunguza yataletwa na kiburi cha Moabu na washirika wako,kwa kuchafua sana anga la dunia,kukataa kusaini mikataba kama ule wa Kyoto(Kyoto Protocol) ili maji yachafuke,viumbe wafe kwa Ongezeko la joto na mabadiliko ya tabianchi, mafuriko kila mahali, vifo majanga, kansa, ukimwi,vyanzo vya maji kuwa damu,kutoboka kwa utando wa Ozone n.k
 Moabu ya kiroho(Marekani) iligoma kutia saini Mkataba wa Kyoto mwaka 1997,kwa sababu kufanya hivyo kungeleta hasara kwa wafanyabiashara wan chi hiyo-Wakaona heri kuongeza madhara kwa kumwaga hewa chafu angani ili wajipatie UTAJIRI.
Soma Ufunuo 16:1-20 uone majanga haya ambayo yanaitwa MAPIGO SABA YA MWISHO-ambayo kimsingi chanzo chake ni kiburi cha hawa Freemasons na utatu mtakavitu wao.
 Hivyo, Balak, Balaam na Yezebeli na mawakala wa Freemasons,mwisho wao umeandikwa katika Ufunuo 18:8-17. Utajiri haramu huu utakomeshwa Ufunuo18:17-19.
Balak ni Mfalme na Balaam ni nabii, wote huwakosesha waumini wa kidini na kuwapeleka kwa Yezebeli ili awalee na kuwakosesha.
 Naijadili kidogo miungu iliyowahi kuishi Mlima Olympus. Iliishi pamoja na waliokufa-mizuka!
Zeus,Titan,Poseidon ambaye ni mungu wa maji,Hades ambaye ni Pluto ambaye pia ni munguwa wafu,Hestia,Hera,Ares ambaye ni mungu wa vita-orodha ya miungu ni ndefu.
Siku hizi tunamwabudu mungu wa dawa wa Ugiriki Aesculapius (Kilatini huitwa ASCLEPIUS) ambaye huonekana akiwa kashika fimbo huku nyoka akiwa amezinga hiyo fimbo.
Nyoka ni ishara ya upya unaoleta ujana kwa sababu hujivua magamba. Siku hizi kuna falsafa ya kujivua gamba,chanzo chake ni nyoka.
 Fimbo aliyojizinga huyu ni ishara ya uponyaji kutoka kwa huyu mungu wa dawa Aesculapius-Compton’s a  Britannica Publications, Vol. 1 ukurasa wa 87.
 Huyu ndiye Yule nyoka aliyeko katika nembo ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa(WHO) na ndiye nyoka Yule Yule aliyeko katika noti ya zamani ya shilingi 500. Huyu ndiye nyoka ambaye huponya ukata,umasikini,ufukara n.k Mimi sijui aliko,msiniulize namba zake za simu!!
0786 324 074
 
 
 
 
 
 
 

Thursday, April 19, 2012

UNATAKA UTAJIRI?


                                                                       Unataka Utajiri? (4)
                                *Laana ya Rasilimali ni zao la hujuma za Freemasons
RAIS Barack Obama, amemteua Mmarekani mwingine, Jim Yong Kim(52) kuwa Rais wa Benki ya Dunia(WB).
Lengo mahsusi, ni ili kushikilia uchumi, mipango  ya maendeleo na fedha za Dunia nzima-hii ni AJENDA YA SIRI ya Freemasons.
Fuko la Fedha la Kimataifa(IMF) linaongozwa na Mfaransa, Christine Lagarde, baada ya ile kashfa ya Mfaransa mwenzake, Dominique Stauss-Khan(DSK).
Hii ni kusema kwamba, mataifa  ya Dunia ya Pili, Brazil,Russia,India,China na South Africa(BRICS) nyendo zao za kutaka kuzipokonya Marekani na Ulaya uongozi wa Taasisi hizi nyeti za kifedha dunia,IMF na WB zimekwama sana.
BRICS, wanadhaniwa kutaka kuanzisha Benki yao ili wakopeshane wenyewe pasipo kuwekewa masharti na kuingiliwa sana kama inavyofanya Benki ya Dunia(WB) na IMF. Masharti ya IMF na WB ni kwamba lazima wakuingilie sana na wakupe masharti wayatakayo wao, ambayo mengi ni ya kitapeli na yamejaa matokeo hasi yaliyozaa umasikini na ukosefu wa ajira hata hapa kwetu baada ya kuuza viwanda na mashirika ya umma.
Ukitaka mikopo,lazima kuzipigia goti IMF na WB. Ukikosana nao kama Mugabe, Ayatollah Ali Khamenei, Gaddafi n.k unawekewa vikwazo vikali na hawa mabwana wa Ulaya na Marekani.
 Ukomunisti unakwisha; unapotoweka, sasa nafasi yake inachukuliwa na kitu kingine,na ni UKATOLIKI unaofika mahali ambapo haukuwepo kama Cuba,Korea Kaskazini,China, Japan na utafika Libya,na nchi nyingine.
 Dunia inakaribia wakati wa utatu mtakatifu wa Muungano wa siasa, dini na sera moja ya uchumi duniani.
Siku hizi, Makao Makuu ya Uchumi wa Dunia ni Washington Dc.Zamani, Makao Makuu ya uchumi wa dunia yalikuwa mjini Rome,jiji hili lilijengwa mwaka 753 BC na Romulus.
Bila shaka,tutajadili Rome na Washington DC watakavyobadilishana kuukalia uchumi wa dunia kwa mara nyingine, siku chache za usoni mwetu.
Nataka kusema kwamba, Benki ya Dunia(WB) na Fuko la Fedha la Kimataifa(IMF) ni mambo yote siku hizi.
 Hata Kombe la Dunia na mashindano kama Olimpiki yatakayoanza jijini London, siku 100 zijazo kuanzia siku ninapoandika hapa, yamewekewa mikono  na mawakala wa Freemasons. Kombe la Dunia(FIFA WORD CUP) yalianza mwaka 1930; leo ni mradi unaoingiza mabilioni ya Dola za Marekani.
 Na tabia za ubaguzi wa rangi,unyanyasaji hasa dhidi ya Afrika hudhihiri sana wakati wa Kombe la Dunia,na mashindano kama Olimpiki.
Katika makala zilizotangulia, nikaandika kwamba,Hitller, naam Yule Dikteta wa Ujerumani, Adolf Hitler, ndiye alijenga uwanja wa Olimpiki wa Berlin mwaka 1936 yalikofanyika mashindano ya Olimpiki ya mwaka huo wa 1936,Hittler akamwita Mweusi,Jesse Owens wa Marekani kwamba ni mnyama.
Miaka 70 baadaye, katika mwaka 2006, wakati wa Fainali za Kombe la Dunia, kati ya Ufaransa na Italia, Marco Materrazzi akamtukana Zenedine Zidane matusi ya kibaguzi katika siku ya fainali uwanjani hapo hapo Berlin.
 Ubaguzi ungalipo hata leo, hata WEUSI wa Marekani wamebaguliwa kila mara hata wakati wa janga la Katrina. Freemasons ndiyo wanaoongoza mambo haya machafu duniani. Kombe la Dunia lenye umri wa miaka 82, mwaka 2010 lilifanyika Afrika ya Kusini kwa mara ya kwanza kabisa,na liliingiza Dola za Marekani Billioni 10,huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) akisema ni ‘nyenzo ya kutengeneza fedha’.
Naam, nazungumzia fedha, zinazoshikiliwa na taasisi nyeti duniani ambazo ni mawakala wa Freemasons. Mimi sizungumzii utajiri wa mtu mmoja, msinisumbue kwa visimu, mimi siyo Freemasons.
 Nazungumza utajiri wa rasilimali za dunia. Dunia nzima inapokwenda kutumia fedha moja. Ulaya sasa wanakwenda kutumia euro ingawa Uingereza haijatia mguu wake kwa pesa hii,kwa kuwa Pound  yake ingali na thamani kubwa dhidi yah ii Euro ambayo inaizidi Dola ya Marekani.
 Jumuiya ya Afrika Mashariki nayo iko mbioni kutumia fedha moja ama sarafu moja katika itifaki iitwayo, THE EAST AFRICAN MONETARY UNION (EAMU).
Hii EAMU, ilitazamiwa kuanza mwaka huu 2012,bahati mbaya haitaanza, walitumwa wataalamu kujifunza huko Ulaya ili kufuatisha namna ya euro ilivyoanzishwa na inavyofanya kazi. Yumkini EAMU ikaanza kazi baadaye mwakani.
 Sekretariati ya Jumuia ya Afrika Mashariki(EAC) na Benki Kuu ya Ulaya(European Central  Bank)walishakaa pamoja,wakatoa tamko kwamba sasa kila kitu tayari ili sarafu ya Afrika Mashariki ianze,kilichobaki ni raia watoe maoni tu,na wadau waseme ili maoni haya yapelekwe kwenye sekretarieti ya EAC.
 Naam, sarafu moja ya EAC kusimamiwa na kuratibiwa na Ulaya,yaani  Central Bank of Europe?!! Kwamba, nchi tano za Afrika Mashariki, Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi wataanza kutumia itifaki ya sarafu moja hivi karibuni sana, sarafu inayolingana na kile Central Bank of Europe wamekitaka sana!
 Kichekesho ni kwamba, hata Uingereza ambayo imesita sana kujiunga kutumia euro, nao wangependa sisi kutumia sarafu ya pamoja ya Afrika Mashariki, eti ili kuinua uchumi wa watu wetu,ili kutumia mfumo mmoja wa kibenki(Union of Banking System).
Muungano wa kidunia wa biashara ulikuwepo zamani jijini Rome, na Rome uliitwa kwa jina siri kwamba ni “Babeli ya Siri”(Ufunuo 18:1-19). Itifaki hii ya ‘Single Currency” ina Baraka ya Freemasons,na lengo ni kushikilia mabenki yote, biashara zote duniani, rasilimali zote na ndiyo utajiri wote wa watu wote.
 Mipango yote ya maendeleo na uchumi wa dunia hufanywa na mawakala hawa wa Ulaya,Marekani na Freemasons,na asiwepo wa kuwapinga.
Huu mji wa siri ambao ni ‘Center of economic life of Modern World’ yaani Rome mambo sasa, watakuwa kitovu cha uchumi wa dunia-mabenki na fedha zote za dunia vitakuwa mikononi mwake,na kutolewa kwa masharti yake.
 Makao ya hawa Freemasons ndiyo yatakuwa makao makuu ya mabenki haya na mashirika haya ya fedha na mipango ya uchumi duniani.
 Haya makao makuu ya uchumi ni Babeli ya kiroho iliyoanguka kwa kuacha usafi na utakatifu sawa sawa na neon la Mungu(Ufunuo 19:1-5,Ufunuo 18:2-3 na Isaya 21:9). Babeli hawa wameacha usafi,wamekuwa ngome ya pepo wachafu na ndege wachafu kama bundi na kuna machafuko na chimbuko la ushetani mwingi duniani.
 Nataka kusema kwamba, wanachofanya Benki ya Dunia na Fuko la Fedha la Kimataifa(IMF) baada ya Mungu wa mbinguni kuacha kuidhibiti dunia,na roho wake kupingwa vikali na watu siku hizi, ni mipango kamambe ya kuiangamiza na siyo kuiimarisha dunia.
 Ndiyo maana, nchi za BRICS (Brazil,Russia,India,China na South Africa) wamechekecha vichwa,wakaona IMF na WB hawana mpango wa kuendeleza nchi yoyote, wanampango wa kuanzisha Benki yao ili kuepukana na ujanja ujanja wao na ukoloni wao.
  Ili upewe msaada ama mkopo,lazima uwapigie hawa magoti na ulambe madole gumba yao. Misaada yao ni ghiliba tupu na ufisadi na mipango kama ya Milenia (MDGs) ni maneno matupu na ghiliba kwa raia masikini, amini usiamini.
  Kwa bahati mbaya sana, hata madhehebu ya dini yanajidanganya na mabenki yao waliyoanzisha ambayo sharti kupewa Baraka za taasisi hizi nyeti kwa ukoloni,ushetani na ufreemason.
Dhambi za Babeli,ni kuuhadaa ulimwengu, wakati hao hao hao wanapopanga mauaji makubwa kwa raia masikini duniani kwa sera za ghiliba zilizojaa ufisadi mkubwa. Mashirika ya dini kumiliki mabenki kwa sera na sheria za IMF na WB?
 Jiji la Rome,limejulikana sana kwa ibada ya sanamu na miungu kama Venus aliye binti wa Zeus, Ares,Diana, Saturn, Pluto, Mercury, Neptune, Uranus, Jupiter na Juan a hata Mwezi! Huu mfumo wa ibada ya jua,nyota na sayari ulipoabudiwa Misri uliitwa Isis,Waperizi waliita Mithras na ndiyo Tamuzi aliyeitwa Ugiriki Demeter.
 Duniani siku hizi, haya masanamu ya Mungu jua,Helios, Artemi(Diana),Zeusi(Jupiter) na Mapiramidi ya Misri yaliyoabudiwa hata miaka 2500 BC KANDONI mwa Mto Nile huko Khufu,na Bustani za Babeli,ndiyo MAAJABU SABA YA DUNIA.
 Sasa,kama unabisha, kawaambie Wazungu waabudu Ziwa Nyanza,maana ndiyo baba mzazi wa Mungu wa Wamisri yaani Mto Nile, “Ra” Wanapinga.Kwanini Ziwa Nyanza mnaloita Victoria halimo kwenye maajabu saba ya Dunia, sembuse Mlima Kilimanjaro?
 Freemasons wanaujua Mlima Kilimanjaro?Wanazijua mbuga za Serengeti? IMF na Benki ya Dunia(WB) wanataka madini,mafuta,gesi na rasilimali za thamani kubwa-zinapogunduliwa kwako wewe hauwi tajiri,ila watakuhujumu hadi wao wawe tajiri kupitia hata vita. Jambo hili tumeliona Nigeria, tunaliona mahali pengi na huitwa, The Resources Curse.
 Nataka nikwambie msomaji, maboss wa IMF na WB wengi ni mawakala wa kifo walioteuliwa kushikilia taasisi hizi kuua watu masikini wa dunia.
Bahati mbaya,tunashabikia kila uchafu toka ng’ambo,tunashabikia timu zao, sinema zao kama Jaws,Star Wars,Pscho,Silence of the Lambs,Godfather n.k.Tunashangilia hata Bigbrother Africa(BBA) na kila mitindo michafu ya kutumaliza kabisa.
 Niijadili kidogo dini ya marasta(Rastafarianism) huko Jamaica, na wanasema asili yake ni Ethiopia, yaani walimwabudu Mfalme(emperor) Haile Selassie?
 Wanamuziki nguli kama Mr.Robert(Bob) Marley WALIABUDU kwa kuadhimisha kwa mitindo ya nywele ya rasta(drearock),hata Tanzania kuna rasta wengi, hawali nyama na wanavuta bangi!
 Hawa Rastafarians walipinga ubeberu wa WEUPE,wakiloni dhidi ya WEUSI na walitunga nyimbo tamu kuwaita Wazungu-Babylon!
 Babylon ni Babeli,yaani machafuko, ule mji ulioanguka, ambao Babilia inataka tuuache.Bahati mbaya, hawa Rastafarians wanarejea kosa la ibada ya sanamu na wanadamu kama Emperor Haile Selassie, ambaye wanasema ni mungu!? Hii ni ibada ya sanamu.
Tunaujadili ukweli na haki,bila kuacha kitu hata kama wengine watatukemea sana. Tunakemewa hata na wachungaji makanisani.
 Ufisadi wa kiroho na kiuchumi ni tawi la Freemasons na Illuminati.Vyombo vya habari kila siku humshangilia Ibilisi anavyofanya mauaji,vituko na unyama wake. Bunge la Tanzania linajadili ufisadi wa mali unaoletwa na ufisadi wa kiroho.
 Hata masheikh na makasisi wameacha kuujadili na kukemea ufisadi wa kiroho wanakemea zao la ufisadi huu yaani wizi na uporaji wa mali ya umma,dhuluma(Isaya 59:14).
Wenye kudhulumu wana zidi sana kudhulumu,wakati hakuna juhudi za kutakasa myoyo kama Mungu apendavyo. Kuna wizi hata wa sadaka, zaka, watu wanabuni kuiba kupitia mafuta ya Baraka ya mizeituni, vitambaa vya Baraka, uzinzi, ushoga,hata maaskofu ni mashoga na wafiraji. Mbona hata Papa anaomba radhi kwa ufisadi huu?
 Itaendelea
0765 324 074