Thursday, May 31, 2012

Mwanamke aketiye juu ya mnyama, tafadhali soma stori yake ndani
Mwanamke Goddes Europa ni sawa na yule wa Ufunuo 17
Huyu ndiye Adolf Hitler wa Ujerumani
http://t1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcRjjRt4OUPZD9pfIExWUIItRaKHKsnc-rTpjL4jSl49KBbXtgSXvwLondon Olympics Games, 2012


miduara mitano ya olimpiki ni mabara matano

Mwanamke wa Ufunuo 17 ni Kanisa la Rumi



    TUWEKE kumbukumbu zetu makini zaidi.
 Feburuari 26 mwaka 2009,William Shao aliandika katika Gazeti la Rai,kwamba mwanamke anayefanana na Yule wa Ufunuo wa Yohana 17:3-11, amejemgewa sanamu mbele ya Jengo la Bunge la Umoja wa Ulaya, huko Brussels,Ubelgiji.
Shao, alienda mbali zaidi kusema, hata jingo lenyewe la Bunge la Ulaya(EU) mjini Brussels, halina tofauti sana taswira yake na Mnara wa Babeli.

Shao, anasema sanamu ya mwanmke aliyeketi juu ya mnyama mbele ya ofisi za Bunge la Ulaya, haikuwekwa kwa bahati mbaya; inatafsiri jambo fulani muhimu wewe kuelewa.                     

 Ulaya, ilikuwa himaya ya Dola ya Rumi; na Mwanamke huyo wa mjini Brussels anayeitwa, “Europa Goddes” ni mungu mke wa Ulaya.
 Naam, mungu jike wa Ulaya ndiye mtawala wa Ulaya na makoloni yake duniani, na mji anaoketi huitwa kwa Jina la Siri, “Babeli” Ufunuo 17:5!!
Umeona picha ya mnara wa Babeli? Ni kama alivyosema mwandishi William Shao,kwamba inafanana sana na jingo la Bunge huko la Ulaya huko mjini Brussels, Ubelgiji.
‘Uropa Goddes’-mungu jike wa Ulaya,hufananishwa na jiji la kale sana Babeli ambayo ni Irak ya siku hizi.
 Kulingana na Biblia, mwanamke katika Unabii ni kundi la waabuduo-kanisa, waumini. Kuna wanawake wawili katika Ufunuo wa Yohana, Ufunuo 12 na 17; moja huwakilisha kundi nyoofu katika maadili ya kidini na, mwanamke wa Ufunuo 17 ni kundi kengeufu linalojichanganya na waabudu sanamu, anasa za dunia na uchafu wa kiroho.
Katika Hosea 2:10,Yeremia 3:14 na 2Korintho 11:2 uhusiano baina ya Mungu Mwenyezi na Kanisa lake hufananishwa na uhusiano wa ndoa,kati ya mume na mke.
Katika Ufunuo 21:2 mji wa Yerusalem umefananishwa na ‘Bibi Harusi’ yaani mwanamke safi. Kanisa la Mungu linapoungana na dunia na anasa na kuabudu sanamu, hufananishwa na UZINZI(Tazama Yakobo 4:4).
Naam, Yakobo anawaita watu wa Mungu waliomwacha na kuungana na Dunia ya dhambi kwamba ni Wazinzi, waasherati, makahaba!
 Ni hapa, tunapomaizi kwamba mwanamke wa Ufunuo 17:3 ambaye ni “mungu-jike wa Ulaya” ni Kanisa la Mungu lililoungana na Dunia na mivuto yake na anasa zake na kumwacha Mungu.
Anasa,ulevi,falsafa,ibada ya sanamu na miungu,ushoga,ulawiti hata wa watoto chekechea n.k
Mavazi ya ‘Mwanamke’ huyo ni rangi nyekundu na zambarau, ambayo yalivaliwa na makuhani wa miungu huko Babeli ya kale.
 Hawa ni kundi tajiri wenye madini,vito vya thamani na urembo ambalo linamvuto mkubwa kwa Wafalme wa Dunia. Kanisa hilo linasemwa kutawala miongoni mwa wafalme wa dunia(Marais, Mawaziri Wakuu,Wafalme n.k) yaani hubebwa na watawala wa Umoja wa Ulaya huko mjini Brussels(Tazama Ufunuo wa Yohana 17:4-6).
Muungano haramu wa Kanisa la Mungu na viongozi wa dunia(uzinzi) ndiyo kuungana kufanya yaliyo kinyume na Amri 10 za Mungu. Kuungana na upagani, kuabudu sanamu na miungu kama jua, sayari,nyota na mwezi.
Mwanamke wa mjini Brussels anao watoto wake nao ni ‘Makahaba’ yaani wazinzi wa kiroho.
Sasa, tutazame kwa makini; kama mji wa Brussels mwaka 96 AD wakati Mtume Yohana anaandika kitabu cha Ufunuo,ulikuwepo? Hasha!!
 Nchi nzima ya Ubelgiji ina watu wasiozidi milioni 12. Brussels siku hizi una wakazi milioni 1.5 tu.
Tuutafute mji wa kale sana Ulaya, ambao Yohana aliuita jina la mafumbo Babeli. Umejengwa juu ya milima saba(ufunuo 17:9).
 Mwaka 753 BC mji uliojengwa Ulaya ni Rome. Hata London haukuwepo, Uingereza ilikuwa kijiji kidogo mwaka 1000 AD. Hata mwaka 500 BC Rome lilikuwa jiji tena “SUPER POWER” Duniani, ulijengwa na Romulus.
 Katika mji huu ndiko yaliko mamlaka ya kidini,Vatican. Unaposema Vatican unasema kanisa la Mungu. Vatican imekuwa nchi Feburuari 11, mwaka 1929 zama za Benito Mussolini.
Habari zinazovuja(hata BBC wametangaza Jumatano iliyopita) kwamba kuna njama za mapinduzi baridi na mchakato wa kumsimika Papa mpya badala ya Benedict XVI.
Rome ni mahali ambapo wameishi ma-Baba Watakatifu(Popes) wa Katoliki wapatao 302. Mji huu ulikuwa makao makuu ya dola ya Rumi, hata zama za Yesu,mitume na zama za Biblia Takatifu yaani kati ya mwaka BC 1500 ZAMA ZA MUSA Hadi 96 AD alipofariki Yohana wa Patmo.
 Nataka msomaji atambue kwamba, waandishi wa Biblia waliposema Babeli,baada ya kuanguka kwa mji wa Babeli, walimaanisha MJI WA ROME(Isaya 21:9).
Fahari yake na ulikuwa mji mkuu wa biashara duniani. Kanisa Katoliki linadai Petro aliyefika mjini Rome mwaka 42 AD na akauliwa na Kaisari Nero Mkatili, mwaka AD 67,ndiye Papa wa Kwanza kwa Kanisa hilo.
 Tuwatazame mapapa. Huchaguliwa na Makadinari kama 131 hivi. Papa Benedict XVI yeye alichaguliwa na Makadinali 117, ambao hawakuwa na umri wa miaka 80. Papa ni Mwakilishi wa Yesu,mrithi wa Mtume Petro,Mkuu wa Mitume wote duniani,Papa ni Mamlaka na nguvu-Tazama Danieli 7:25.
 Rome, ni mahali Kanisa la Mt.Petro lilipojengwa juu ya Kanisa la Petro; linaitwa, St.Peter’s Basilica. Limejengwa KATIKA ENEO LA EKARI SITA.
Hili kanisa, St. Peter’s Basilica, lina urefu wa futi 700 na upana ni futi 450 na linaweza kuchukua watu 80,000 kwa wakati mmoja.
Rome ni jiji lililopo nyuzi sawa na New York kwa nyuzi za Latitude; ni jiji lenye Coliseum, ambamo yalifugwa masimba yaliyorarua Wakristo maelfu.
Rome,uko futi 40 hadi 270 juu ya usawa wa Bahari. Jiji lenye kelele nyingi kuliko mji wowote duniani,lipo kando ya Bahari ya Mediterranean.
 Zama za Papa Pius XII alibebwa kwenye kiti cha enzi kiitwacho, Sedia Gastatoria ambacho ni kiti cha enzi cha dhahabu chenye rangi nyekundu.Papa huketi hapa mara anapochaguliwa na Moshi  Mweupe, hutoa BARAKA Duniani- Urbi et Orbi.
Rome umejengwa juu ya milima saba: CAPITALINE, PALATINE, AVENTINE, QUIRINAL, VIMINAL, ESQUILINE, na CAELIAN.
Hapa, ndipo liketipo kanisa lile la Mungu ambalo sasa linataka kugeuka kuwa kama Yule mama wa mjini Brussels.
Mwanamke huyu ni kanisa. Kanisa linapoungana na dunia na kuacha usafi wa kiroho huitwa, ‘BABELI’ ya siri iliyoanguka na Mungu huwaita watu wake watoke humo(Ufunuo 18:2-4).
Kuanguka ni kuacha usafi wa kiroho,kumwacha Mungu na kuungana na uchafu kama unajisi,siasa za kugombea tawala za dunia,ufisadi,mapinduzi,ulawiti,ushoga n.k
Jiji lenye utajiri wa dhahabu na vito vya thamani lenye kuwakosesha watu kwa mafundisho yenye kuridhia dhambi(uasi wa sheria ya Mungu) kama jambo dogo tu-Uhuru na demokrasia,haki za binadamu n.k
Wapo wanaofuata kila jambo na ni ‘watoto’ wa Yule mama wa mjini Brussels. Tafakarini.
0786 324 074

MASKINI CHARLES TAYLOR

  TITANIC,
TUREJEE kidogo katika somo la Kuzama kwa Meli ya Titanic.
Kwamba, ilizama kwa maelekezo ya Freemasons. Nahodha wa Meli ya Titanic, E.J.Smith, alielekezwa kuizamisha meli ili kuwaulia mbali matajiri waliokuwemo.
Mhariri wa Makala wa Gazeti hili, Markus Mpangala,Mei 22 mwaka huu akawataja matajiri hawa walioangamia katika ajali hiyo kwamba ni John Jacob Astor,Archibald W.Butt,Charles M. Hayes,na mkewe na binzi zao, W.T.Stead,Benjamin Guggenheim, F.D.Millett na G.D.Widher.
Wengine walioangamia ni Isidor Strauss, na mkewe,J.B Thayer,J,Bruce Ismay,Henry B. Harris na mkewe na Washington A.Roebling.
Sina haja ya kulumbana na mtu kwamba Freemasons ambao kimsingi ni mawakala wa Ibilisi hawasababishi ama wanasababisha kutokea kwa majanga. Sote tunajua kuna nguvu mbili zinazoshindana duniani, nguvu ya wema na ile ya kufanya mabaya. Freemasons ni mawakala wa Ibilisi wenye kazi maalum ya kuhadaa watu,wakidhani wanafanya mema.
 Hata hivyo, Alex Mayoge wa Moshi,Kilimanjaro aliniandikia SMS kusema kwamba TITANIC ILIZAMA ili kuwaua matajiri hao ili Freemasons wapore fedha zao kwenda kugharimia VITA VYA KWANZA VYA DUNIA.
Titanic ilizama Aprili 1912 na ni miaka miwili baadaye,mwaka 1914 vita kuu ya kwanza ya Dunia ikaanza kwaka 1914.
 Vita vila lengo Fulani, na aghalafu vita wanavyoanzisha Freemasons ni vya kupora rasilimali ama kuweka mamlaka yao mahali wanapopingwa,nguvu za ushawishi zinaposhindikana.
Vita vya Pili vilianza 1939 vikakoma 1954. Tulishajadili jambo hili kwa kina,na anayetaka aangalie Blog yangu kuhusu vita hivi na matokeo yake.
Malengo ya maharamia hawa yangalipo duniani,ndiyo maana kuna vita leo Congo na maeneo mengine kama Sierra Leone, tuliona Revolutionary United Front wakipewa silaha kuharibu serikali ya mjini Freetown,ili wapore ALMASI ZA DAMU.
Mwisho wa siku Fodday Sankoh alikamatwa na kupelekwa The Hague ambako eti alifariki ama kunyamazishwa, leo niandikapo hapa Taylor anahukumiwa kifungo cha miaka mingi huko jijini London,Uingereza?
 Soma  tamthilia hii kama kichekesho tu(Satire) cha Taylor huko Mahakamani Hague, dhidi ya wakubwa.
     CHARLES TAYLOR 64 + 80
 
 
ASKARI:           Koooortiiiii?
 
(Mahakama ya Umoja wa Mataifa,ICC,inaanza kikao chake, ‘session’ mjini The Hague, Uholanzi.
Washitakiwa, maofisa wa Mahakama wanaingia,na watu  wote ndani ya mahakama hiyo wanasimama wakati wa majaji kuingia kortini, ambamo Taylor anashitakiwa kwa makosa 11 ya uhalifu wa kivita huko Sierra Leone tangu 1991 hadi 2002, akiwasaidia United Revolutionary Front).
 
KARANI:       Charles Ghankay Taylor dhidi ya Haki za Binadamu?
 
TAYLOR:      Timamu, Mheshimiwa Jaji, Lussick. Hata hivyo nashangaa,katika kesi hii washitakiwa wenzangu, akina mabwana George W.Bush na Tony Blair wameachwa. Haidhuru! Nimamaizi Mheshimiwa Jaji, mahakama hii ya ICC hapa Hague ina makengeza!
 
JAJI  LUSSICK:    Mwendesha Mashitaka una hoja?
 
MWENDESHA MASHITAKA:    Mshitakiwa aliwafadhili Waasi wa RUF walipoua watu huko Sierra Leone, akawatumikisha watoto maelfu jeshini kwa muda wa miaka 11; naye ana makosa 11.
 
JAJI LUSSICK:    Mshitakiwa, Charles Taylor,Rais wa zamani wa Liberia, unapaswa kuieleza mahakama hii tukufu, una maanisha nini kusema mahakama ina makengeza? Mahakama ina macho?
(kicheko cha kwikwi toka kwa wasikilizaji)
 
TAYLOR:   Mheshimiwa, sina maana kwamba mahakama ni kipofu; ila ina makengeza! Haina macho, mahakama ina ‘double standards’ yaani upendeleo, haiwaoni Wazungu tuliosaidiana nao kuwafadhili United Revolutionary Front(RUF) ili wapore ALMASI ZA DAMU ili ‘deal’ hii itupe utajiri? Sasa mheshimiwa, kazi tumefanya wote na akina Bush na Blair, eti ‘zengwe’ nasukumiwa mimi peke yangu. Hiyo noma Mheshimiwa!
JAJI LUSSICK: Okay! Okay! Nimekupata Mr. Taylor, ohh..samahani, Mr. X-President! Hata hivyo hujakana shitaka lolote kati ya haya 11 unayokabiliwa nayo?
TAYLOR:      Nikanushe nini Mheshimiwa wakati mlikwishaamua kunitosa?
JAJI LUSSICK:   Tumuulize Mwendesha Mashitaka Mkuu,Louis Mareno-Ocampo. Kwanini Taylor? Why Taylor, and why not Wazungu in this TRIAL?
OCAMPO:    Mheshimiwa Jaji,Lussick, Rais Mstaafu wa Liberia, Bwana Caharles Taylor alishatakiwa na wenzake kama Fodday Sankoh,kiongozi wa RUF.
 TAYLOR:  Mheshimiwa, nataka Ocampo aieleze hii mahakama ya Fisi ambako mimi Mbuzi leo nasulubiwa kinyama! ‘Poppy’ Sankoh ni mshitakiwa namba ngapi katika kesi hii?
 OCAMPO: Sankoh hayupo hapa mahakamani. Kama mahakama inakumbuka, alifariki akiwa rumande hapa mjini Hague.Waasi wengine wakikamatwa upelelezi ukikamilika nao tutawashitaki, hakuna ‘impunity’ kwa mkosaji yeyote.
TAYLOR:  Mheshimiwa, inakuingia kichwani kwamba mimi peke yangu ningeweza kufadhili RUF kuua watu,kubaka,kukata raia viungo na kupeleka watoto 200,000 vitani,kama siyo msaada wa Bush,Blair na ‘Wadosi’ wengine wa huku ‘majuu’ mheshimiwa, kama siyo kunionea?
JAJI:                   Swali jingine?
TAYLOR:       Mimi peke yangu ningewezaje kumpa Poppy Sankoh ‘shavu’ kwa miaka thenashara, hadi akombe ALMASI ZA DAMU Sierra Leone? Eti wanasema mjini Johannesburg nilimhonga yule kimwana, Naomi Campbell bonge la almasi ghafi. Hizo almasi nilizipataje na nilikuwa namuuzia nani, Mzungu au Mwafrika,Mweupe au mfupi, mnene au kimbaumbau? Ebo! Noma mheshimiwa!!
(kicheko cha kwikwi kutoka kwa wasikilizaji mahakamani)
BRENDA HOLLIS:    Taylor na Sankoh walishirikiana kufanya uhalifu Sierra Leone,KWA MTUTU WA BUNDUKI, walipora almasi za damu na kuziuza kwa wateja wao Ulaya na Marekani
TAYLOR:    Tena huyu Brenda Hollis,Mwendesha Mashitaka ni mpuuzi kabisa, afadhali Ocampo, tuliua watu kwa bunduki? Umesikia Liberia kulikuwa na kiwanda cha bunduki kama AK 47?
OCAMPO: (anasimama) Mheshimiwa Jaji, ALMASI ZA DAMU zilisafirishwa kwa magendo hadi Afrika Kusini hadi Ulaya na Marekani ambako walibadilishana na Wazungu kwa almasi kwa bunduki yaani Guns for Diamonds mheshimiwa!
 TAYLOR:   Basi poa, Mheshimiwa Jaji, sasa wanataka mimi nikanushe nini kama hata wao wanajua Mzungu alifanya vikao vya G-8 vya kinafiki huko Antwerp, kukataza biashara ya almasi za damu,kumbe naye alizimaindi?
  JAJI:          kama sijakosea, swali la mshitakiwa ni kwamba, kwa nini upande wa mashitaka haujawaleta mahakamani walionunua almasi za damu toka Sierra Leone,badala yake wamewaleta wauzaji peke yao?
TAYLOR:   Hewaa! Jaji,kumbe hukusoma mwembeni na kupata digrii za ‘madensa’ ila umebukua sheria! Umenipata! Huyu Ocampo kwao ni Buenos Aires, Argentina, sasa ni kibaraka wa Mzungu wa Ulaya hajui EU walipora almasi za damu licha ya sheria kupiga marufuku biashara hiyo, halafu anatukamata Waafrika tu! Wapi Wazungu hapa bwana? Hiyo siyo ‘Fair Play’ ni Unfair kabisa, Noma msikaji!!
  (minong’ono na miguno inasikika mahakamani)
OCAMPO:    Waheshimiwa Jopo la Majaji, mshitakiwa athibitishe kauli yake kama ICC inawashitaki Waafrika tu,na aslani hakuna Mzungu hata mmoja! Hiki siyo chombo cha Umoja wa Mataifa(UN) na nchi 54 za Afrika hazijaridhia Mahakama hii tukufu?
TAYLOR:    Hawa mabwana wanatutuma kazi,tunatesa raia,tunakwiba rasilimali na fursa zao nyingi,ili Punda afe Mzigo ufike! Halafu baadaye wakitosheka wanaanza kutuchonganisha na raia na maandamano kama walivyofanya Libya,Misri kwa Mubarak,Tunisia kwa Ben Ali n.k Je huu ni uungwana Mheshimiwa? Tunapora nchi zetu kwa ufisadi na kuleta mzigo halafu kisha wanatusaliti! Huu siyo uungwana mheshimiwa!
JAJI: Hujaitajia mahakama Waafrika wangapi wamekamatwa peke yao na kushitakiwa The Hague?
TAYLOR:  Mimi ningali Rais halali wa Liberia, huyo Hellen Johnson Sielief, wamemleta wao ili atawale kisha mimi waninyonge! Wanasema hakuna ‘Impunity’ wakati Blair,Bush wanavamia na kuua hakuna mashitaka! Mnataka nife kama Gaddafi na Saddam?
JAJI:  Enhe, wewe na wengine kina nani? Wataje mlioshirikiana kuua raia mkapora utajiri wa Afrika na kuuficha Ulaya na Marekani.
 TAYLOR: Simple, Fodday Sankoh, Laurent Nkundabatware, Jean-Pierre Bemba, Laurent Gbagbo, hawa ‘Ocampo Six’ mmewaacha mkachagua ‘Ocampo Four’, halafu mnamtaka Omar Hassan Al Bashir, Tomas Lubanga,Joseph Kony,Paschal Ntaganda.
JAJI:                  Umemaliza?
TAYLOR: Mobutu, Savimbi,mbona hamsemi mliwasaidia hawa kupora utajiri wa Afrika na kuuhamishia Ulaya na Marekani sasa Afrika ni The Shame of poverty in   Plentiful?
OCAMPO:  Mheshimiwa,huyu jamaa sijui hamnazo, au kachapa kilaji! Amesahau Slobodan Milosevic wa Serbia naye alishakamatwa mwaka 2000? Atasemaje kwamba tunawakamata Waafrika tu?
TAYLOR: Mimi siyo mlevi,ninakupa ‘facts’ usianze chuki zenu hapa. Mimi ni Rais halali Liberia wananchi wananipenda, Marekani wamenitumia nikapora almasi za damu na kuwapelekea,sasa wanasema mimi
 muuaji. Guns for Diamond ningefanyaje miaka 11 bila kushirikiana nao? Wazungu, acheni kufikiri Mwafrika zoba, hamnazo?
(kicheko mahakamani, zinasikika kelele za mashabiki wake nje ya mahakama wakishangilia)
 
  JAJI: Order! Hapa tuko mahakamani,hatupo baa! Utulivu tafadhali! Enhe, Taylor endelea kuuliza swali kama unalo; lakini wewe siyo among the wealthiest in the world?
TAYLOR:   Umbeya tu mheshimiwa. Hawa wanatuchonganisha na wananchi wetu halafu wanasanua deal kwa mitandao yao kama weakleaks, wanachochea maandamano kwa facebook na twitter
OCAMPO: Kwani Wazungu hawakamatwi?
TAYLOR: Baada ya Adolf Hittler baada ya Vita ya Pili ya dunia nani aliyehukumiwa Hague,kama siyo mimi mnataka kunionea eti nifungwe miaka 80,sasa nina 64, ndiyo nini kama siyo kuniziba mdomo nisiseme mlivyopora ALMASI ZA DAMU huko Kono, Sierra Leone? Eti mnataka kunifunga Uingereza!!
  JAJI: Hoja yako ni ipi hapa?
TAYLOR:   Ukiacha wale NAZIS, hawa jamaa ni matapeli hawajamkamata Mzungu, wanatukamata sisi Waafrika tu, wana ‘double standards’ mheshimiwa Jaji na mambo haya hapa siyo kesi ni siasa tupu-This massive inequality can be traced back to cold war politics!!Sikubaliani na ukoloni wa ICC,WALA hakuna human rights wala transparency international wala nini!!
JAJI:  Wakili wa mshitakiwa una swali?
WAKILI: Taylor, kina nani wengine wanaonewa na ICC?
Taylor:  Hata mashirika ya wakimbizi na mengine ya Umoja wa Mataifa Congo,Dafur, Sierra Leone n.k wizi mtupu, dunia haina amani ni utapeli tu,vita wachochee wao,tushitakiwe sisi akina Taylor, Mobutu Sseseseko,Jonas Savimbi, Bosco Ntaganda,Thomas Lubanga,Jonas Kony,orodha ni ndefu mheshimiwa! Hawa wote husaidiwa na Wazungu kuharibu amani,uchumi na usalama wa Afrika,halafu hugeuka chameleon?
(anainamisha kichwa kuonesha ameridhika, anaketi)
JAJI:   Badala ya kukanusha mashitaka  unalalamika sana kwamba umeonewa,kwamba ICC inawaonea Waafrika tu. Mahakama imeona una hatia ya mashitaka yote thenashara! Upande wa Mashitaka una hoja?
 
BREBDA HOLLIS:    Huyu jamaa afungwe miaka 80, ukijumlishe umri wake wa miaka 64 maana yake ni kwamba afie ‘nondo’ ama mangenge ili liwe fundisho kwa ‘masera’ wenzake wanaoua raia!
JAJI:      Hukumu KAMILI Mei 30 mwaka huu 2012.
ASKARI:       Kooooortiii!!
 Mei 30, magazeti ya Tanzania yanaandika, “Taylor anyeshewa mvua ya miaka 80 jela!” mara, ‘Taylor kunyea mtondoo!”
                                   TAMATI
0786 324 074 ama www.congesmrambatoday.com
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

UBAGUZI WA RANGI OLIMPICS


Mwaka 1936 Dikteta wa Ujerumani, Adolph Hitler, alikataa kutambua ushindi wa Mtu mweusi, Jesse Owens, aliyeshinda medali nne za dhahabu kwa dakika 45 tu, katika Mashindano ya Olimpiki ya Majira ya Kiangazi mjini Berlin .
   Hitler, alisema Jesse Owens(Mmarekani mweusi) alikuwa mnyama. Kulingana na Hitler, haikuwa haki mnyama(Owens) kushindana na Binadamu(Mzungu) katika mashindano yoyote! Binadamu hushindanishwa na binadamu na wanyama na wanyama wenzao.
  Viongozi wetu wanaweza kujidai kusahau dharau za akina Hitler, wakadhani ubeberu na unyang’au wa Wazungu umekoma. Wanafikiri ubaguzi wa rangi haupo. Huku ni kujidanganya sana ...huyo Watson hajakurupuka, kasema wanavyoamini wao.
   Jumapili, Julai 9, mwaka 2006. Italia ikapambana na Ufaransa katika Fainali ya Kombe la Dunia, katika uwanja huohuo wa Berlin aliojenga Hitler miaka 70 iliyopita na kusimika hirizi ya unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya mtu mweusi.
    Marco Materazzi wa Italia akamtukana Zenedine Zidane ‘Zizou’ matusi yanayokaribiana na ubaguzi wa rangi. Zizou, akamtwanga Materazzi na kumwangusha chini…kapewa kadi nyekundu na mwamuzi na kutolewa nje. Alizua mjadala mkali wa kisiasa.
Zizou ni raia wa Ufaransa, mwenye asili ya Algeria , Afrika.
   Siyo Berlin tu ilikozikwa hirizi ya ubaguzi wa rangi; hata Uhispania akiana Samuel Eto’o Fils hudhaniwa nyani. Hata Seneta wa Italia, Roberto Calderoli anaamini watu weusi ni mkosi, tena si binadamu wenye akili kama Mzungu.
    Seneta Calderoli, alisema Timu ya Taifa ya Ufaransa iliyoundwa na weusi wengi, akina Eric Abidal, Claud Makelele, Thierry Henry, William Gallas, Louis Saha, Patrick Vieira, Djibril Cisse , Zizou na wengineo ndio walioitia mkosi Ufaransa ikashindwa na Italia mwaka 2006.Laiti ingeundwa na binadamu, Wazungu! Kujaza weusi wengi katika kikosi chake kukasemwa kuwa ni sababu ya Ufaransa kushindwa mjini Berlin hata miaka 70 baada ya Hitler kuujenga uwanja huo!
    Haya yalishasemwa na akina Ian Douglas Smith wa Rhodesia ya zamani sasa Zimbabwe ya Mugabe, Kaburu Balthazar Johannes Voster na P.W. Botha wa Afrika Kusini. Wanafunzi 250 wa Kiafrika waliouawa na polisi wa Makaburu mwaka 1976 kwa sababu ya kukataa kuimba Kiafrikana(lugha ya binadamu) wamesahaulika akilini mwa vigogo wetu?
   Naam, hawa ndio akina James Watson leo wanaosema Mwafrika hana akili; na huwezi kumfanya daraja moja na Mzungu!
Wazungu wengi wanaamini Mwafrika nyani; hayawani. Tunadhihirisha hili kwa kujikomba na kuwapa rasilimali zetu ili wauze na kutugawia kidogo.
   Rasilimali zetu zinajenga kwao, wanakula minofu sisi mifupa halafu tunampigia magoti Malkia, akina Gordon Brown na akina Bush. Tunakosa cha kwetu.
Tunajidai kusahau kuwa Wazungu ni walewale jana hata leo. Wao wanaona ni daraja la kwanza sisi mwisho; chetu chao, chao si chetu…kwanini hatung’amui?
   Enzi zile tulisema tumeonewa kiasi cha kutosha, tumedharauliwa sasa tunataka mapinduzi. Mbona mapinduzi hayaonekani, isipokuwa tunarejea utumwani? Itaenelea tolea lijalo.
   0786 324 074
 

Looking for last minute shopping deals? Find them fast with Yahoo! Search.
   

Kuelekea Olimpic London, 2012


 
MASHINDANO ya Olimpiki ya majira ya kiangazi yanayotarajiwa kufanyika London, mwezi Julai,  mwaka huu, yalianza zamani sana, karne tano kabla ya Kristo.
   Yale mashindano ya Olimpiki tunayoshuhudia siku hizi, yalianza Athens huko Ugiriki mwaka 1896
.Hufanyika kila baada ya miaka minne, wakati leo wanariadha wanaoshiriki wameongezeka kutoka nchi 13 mwaka 476 BC hadi zaidi ya 200 hii leo.
    Alama ya mashindano haya ya Olimpiki ni miduara mitano iliyoungana; inayowakilisha urafiki na udugu wa kimichezo wa watu wa mabara yote.
Miduara hii pia huwakilisha mabara natano ya kijiografia, ambayo ni Afrika, Asia, Ulaya, Australia na Amerika.
  Kila mduara una rangi tofauti kulingana na rangi ya watu wake. Miduara hii ina rangi nyeusi(Afrika), bluu(Ulaya), njano(Asia),kijani( Australia ) na Amerika wanawakilishwa na rangi nyekundu.
 Miduara hii mitano huwa katika bendera nyeupe ya Olimpiki.
   Madhumuni ya ushiriki wa mashindano haya si kushinda medali peke yake, bali ni kushiriki. Maisha ya kawaida ya mwanadamu si shangwe ya ushindi; ni kupambana.Yaani, kitu muhimu si kushinda bali ni kupambana kwa ari kubwa.
    Kauli mbiu ya mashindano ya Olimpiki ni “Citius, Altius, na Fortius” ambayo ni maneno ya Kilatini, maana yake, ‘Kupaa haraka, Juu na kwa Nguvu’. Afrika haina budi kushinda mafashisti mamboleo na kupaa juu kwa haraka na nguvu katika nyanja zote za maendeleo.
   Kiapo cha kila mwanamichezo anayeshiriki kushindana katika mashindano ya Olimpiki, ni kushindana kwa heshima kulingana na sheria na kanuni zinazoongoza mashindano; kuwa na uanamichezo na utukufu wa kweli wa mashindano, bila kusahau kuipa heshima timu ya kila mwanamichezo anayehusika.
    Mwenge wa Olimpiki uliotua Dar es salaam mwaka 2008, ukishuka kutoka dege kubwa la rangi ya ‘Pinki’ hivi, ulianza kukimbizwa mwaka 1936. Tayari mwenge huu umewashwa huko Athens.
.Zamani, mwenge huo uliwashwa kwa miali ya jua huko Olimpia(asili ya mashindano yenyewe), huko Ugiriki. Badaye, mwenge ulichukuliwa kupelekwa uwanja wa mashindano kwa meli au ndege.
    Dar es salaam mwenge huo ulikimbizwa kwa amani bila kitisho cha waandamanaji, ama al-Qaeda. Mashindano ya kisasa ya Olimpiki yalianza Athens mji mkuu wa Ugiriki mwaka 1896; miaka minne baadaye yalifanyika jijini Paris.
    Mwaka 1904 mashindano haya yalifanyika  St. Louis , Marekani. Mwaka 1906 yalifanyika Athens , lakini hayakutambuliwa na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa(IOC). Mwaka 1908 yalifanyika mjini London kwa mara ya kwanza.
   Mwaka 1912 mashindano ya Olimpiki yalifanyika Stockholm nchini Sweden , 1920(Antwerp-Ubelgiji); 1924(Paris-Ufaransa);1928(Amsterdam-Uholanzi);1932(Los Angeles-Marekani);1936(Berlin-Ujerumani ya enzi ya Hitler);1948(London- Uingereza);1952(Helsinki-Finland);mwaka 1956 yalifanyika Melbourne-Australia, 1960 yalifanyika Rome mji mkuu wa Italia.
   Mwaka 1964 mashindano yalifanyika Tokyo , Japan , wakati yale ya 1968 yalifanyika Mexico City nchini Mexico . Mwaka 1972 mashindano yalifanyika jijini Munich , Ujerumani Magharibi wakati huo; yaliacha alama ya kitisho cha magaidi, kama ilivyo zama hizi za al-Qaeda.
   Septemba 5, mwaka huo wa 1972 magaidi wanane wa Kipalestina kutoka kundi liitwalo, Black Septemba, walidhamiria kulipa kisasi dhidi ya adui zao Waisraeli.
Walijipenyeza katika mabweni ya wanariadha katika kijiji cha Olimpiki(wakati wa ufunguzi wa mashindano); wakiwa wamevalia viruwiruwi(mask) nyusoni mwao, waliwatwanga risasi wanariadha wawili wa Israeli, kabla ya kuwateka nyara wengine tisa.
   Magaidi hao wa Black September walikuwa wakiwadai Waisraeli kuwaachia huru mateka wanamgambo 200 wa Kipalestina waliokuwa wamekamatwa na majeshi ya Israeli wakati huo.
    Black September, wakaitaka serikali ya Ujerumani Magharibi kuwasafirisha kwa helkopta wao na mateka wao hadi katika uwanja wa ndege ulio nje ya Munich.
Waliitaka serikali baadaye iwapeleke katika nchi yoyote ya Kiarabu, iliyokuwa ikiunga mkono Wapalestina kujitawala katika ardhi yao .
   Naam.Wapalestina waliwateka nyara wanariadha wa Uzayuni kama kisasi cha kutaka mateka wa Kiarabu kuachiliwa huru; wakijua wakati huo wa michezo ya Olimpiki, suala lao lingetangazwa sana na vyombo vyote vya Habari vya dunia nzima.
   Baada ya majadiliano makali Wajerumani waliamua kuwachukua magaidi wale(nisihukumiwe kuwaita hivi hata kama ni wanaharakati) na mateka wao hadi katika uwanja wa Furstenfeldbruck.
   Vikosi vya usalama vya Ujerumani vilifanya ujanja wa hali ya juu, vikauzingira uwanja huo na kuwasubiri. Walipotua tu uwanjani, kabla ya kushuka ndegeni, mapambano ya silaha yakaanza.
    Magaidi watano wa Kiarabu waliuliwa, wengine watatu wakatiwa  mbaroni. Hata hivyo, walikwisha waua wale wanariadha wote tisa wa Israeli, waliotekwa nyara mabwenini, kule Munich katika kijiji cha Olimpiki.
    Tukio hilo liliidhalilisha sana serikali ya Ujerumani Magharibi, baadhi ya mataifa yakatishia kususia mashindano. Huu ni wakati gaidi la kale sana la kimataifa, Carlos The Jackal, linalotumikia kifungo cha maisha Ufaransa, lilipotuhumiwa kupanga mashambulizi hayo.
   Sakata hilo lilipita, mashindano hayo ya Munich yakaendelea kama ilivyopangwa.
 Mwaka 1976 mashindano ya Olimpiki yalifanyika Montreal Alberta Canada .
Mwaka 1980 yalifanyika Moscow Urusi ya zamani, ambako Tanzania iliwakilishwa na mabalozi wengi wakiwemo akina Luliga Musa, Mwinga Mwanjala n.k
   Mwaka 1984 yalifanyika Los Angeles, Marekani. Mwaka 1988(Seoul-Korea Kusini); 1992(Barcelona-Uhispania); mwaka 1996(Atlanta-Marekani);mwaka 2000(Sydney-Australia); mwaka 2004 yalifanyika tena Athens, Ugiriki yalikozaliwa; lakini chini ya ulinzi mkali sana, kufuatia kitisho cha magaidi wa al-Qaeda.
   Mwaka huu wa 2008 mashindano haya yalifanyika Beijing nchini Uchina, huku kukiwa na kitisho cha matetemeko na magaidi wa al-Qaeda na wa Tibet.
 Mwaka 2012 mashindano haya yatafanyika mjini London. Hata huko London kitisho cha magaidi kingalipo…Afrika haijawahi kuandaa mashindano haya adhimu duniani. Kwa nini na kwa sababu gani? Kama ni suala la usalama, mbona hata Munich magaidi walitamba? Afrika itaandaa mashindano haya lini?
    Zamani, mabingwa wa Olimpiki walituzwa taji ya majani ya mizeituni
.Leo, mashindano haya huandamana na tuzo za kitajiri. Mashindano ya sasa yanapoteza maudhui ya Olimpiki, kama tulivyokwishakuona. Uzalendo unapotea, Olimpiki ni mnada tu wa kusaka utajiri.Mabingwa wa Afrika hurubuniwa kwa rushwa na Wazungu!
   Mraba huu unawakumbuka mabingwa wa Olimpiki, hususan askari shujaa sana wa Kigiriki aitwaye, Pheidipides.
Huyu, alitimka umbali wa mali kama 29 hivi, kutoka mahali paitwapo Marathon kwenda mjini Athens.
   Mwaka 490 BC Majeshi ya Waperizi(Iran ya leo) yalikwenda mahali paitwapo Marathon na kutaka kuivamia Ugiriki. Walikuwa na majeshi makubwa sana, kwa bahati jeshi dogo la Ugiriki likafanikiwa kuwapiga na kuwafukuza kabisa.
   Jemadari wa Jeshi la Ugiriki akamtuma Pheidipides kwenda mjini Athene(wakati huo) kwenda kupeleka Habari njema za ushindi.Ulikuwa wakati wa Mfalme Dario wa Umedi-Soma kitabu cha Danieli sura 2-3
  Basi, alipofika mjini Athens, sokoni kwenye mkusanyiko wa watu wengi, alifanikiwa kusema kwa shida sana kwamba jeshi lao lilikuwa limelishinda jeshi la wavamizi.
   Alipomaliza kusema, akaanguka mchangani na kufa!
 Mbio za Marathon zikaanzishwa kwa lengo la kumkumbuka shujaa, Pheidipides.Hizo zilikuwa enzi za Mfalme Dario anayesimuliwa Habari zake katika Biblia, katika Danieli.
 Utaona kuwa neno Olimpiki limetokana na Olympia, neno Marathon ni mahali alipoanza kutimka shujaa huyo kwenda Athens.
    Mabingwa wengine wa Marathon ni pamoja na Joan Benuit wa Marekani mwaka 1984,Rosa Mota wa Ureno(1988); Valentina Yegorova(1996), Fatuma Roba wa Ethiopia(1996) na Naoko Takahashi wa Japan mwaka 2000.
   Afrika inang’ara ipasavyo katika bendera nyeupe ya OIlimpiki. Mabingwa wa Marathon wa Afrika ni pamoja na  Abebe Bikila wa Ethiopia(1960,64); Marmo Wolde wa Ehiopia(1968);Josia Thugwane wa Afrika Kusini(1996); na Gezahgne Abera wa Ethiopia mwaka 2000. Rekodi za 2004 hazikuwekwa.
   Waama, mraba huu unamkumbuka sana kaka yetu, Jesse Owens, Mmarekani mwenye asili ya Afrika aliyeshinda medali nne za dhahabu katika mashindano ya Olimpiki ya mwaka 1936 mjini Berlin.
 Jesse Owens, alitimka kwa dakika 45 akawa na medali hizo nne,  pamoja na kushinda mita 200.Aliyekuwa mgeni wa heshima wa mashindano hayo, Dikteta Adolf Hitler, aliamua kususa kutazama mtu mweusi akishinda
 Aliondoka uwanjani hapo na kusema kwamba hakuwa tayari kuona ‘mnyama’ Owens, akiwanyanyasa binadamu(Wazungu).Wangalipo wenye mawazo kama Hitler hata sasa, wengine wamezaliwa Afrika.
   Hitler, ndiye mjenzi wa uwanja huo wa Berlin ilikokuja kuchezwa fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2006(miaka 70 baadaye) kati ya Ufaransa na Italia.
Ufaransa iliyokuwa na Weusi wengi katika kikosi chake, ilitukanwa kwamba ilishindwa kwa sababu ya hao Weusi!
   Tena, Michael Materrazi alimtukana Zenedine Zidane “Zizou” kwamba alikuwa gaidi, kutokana na asili yake ya Algeria.Zidane alimtwanga kichwa kikali, akatolewa nje kwa kadi nyekundu! Naam, mzimu wa unyanyapaa na  ubaguzi  wa rangi ungalipo mjini  Berlin hata baada ya Dikteta, Fashisti Adolf Hitler kujiua.
   Mabingwa wengine wa Olimpiki kutoka Afrika ni pamoja na Paul Erang wa Kenya aliyeshinda mita 800 mwaka 1988, William Tanui pia wa Kenya(1992). Mwaka 2000 Noah Kiprono Ngenyi wa Kenya alishinda mita 1,500, Mirutus Yifter wa Ethiopia alishinda mita 5000 mwaka 1980, Said Aouita wa Morocco alishinda 1984 hizo mita 5000, Venuste Niyongabo wa Burundi alishinda 1996 na Milton Wolde wa Ethiopia aliwika katika mashindano hayo mwaka 2000.
    Katika mita 10,000 Naftali Temu wa Kenya alishinda 1968, Miruts Yifter wa Ethiopia akashinda mwaka 1980. Haile Gebrselassie wa Ethiopia aliwika mita 10,000 mwaka 1996 na 2000.Nigeria ya akina Nwankwo Kanu ilipata kushinda kombe la Olimpiki la soka, kwa kuwachapa vigogo kama Brazil na Argentina. Afrika,  ni kichwa si mkia katika ramani ya Olimpiki.
    Mabingwa wengine wa Olimpiki ni Amos Biwott wa Kenya mwaka 1968, Kipchoge Keino pia wa Kenya mwaka 1972,Julius Korir wa Kenya mwaka 1984,Julius Kariuki wa Kenya mwaka 1988, Mathew Birir wa Nyayo mwaka 1996, Joseph Kater pia wa Nyayo mwaka 1996 na Robert Kosgei mwaka 1996. Maria Mutola wa Musumbiji alishinda mita 800 mwaka 2000. Afrika ni bara la mabingwa wenye ari ya kushinda.
    Tanzania imewahi kushiriki mashindano mengi ya kidunia; inajivunia rekodi za mabingwa wake kama Filbert Bayi, Suleiman  Mujaya Nyambui, Juma Ikangaa na wengine wengi.
    Afrika Kusini iliaandaa Kombe la Dunia mwaka 2010.
Baadaye Afrika itataka kuandaa mashindano makubwa ya kimataifa, licha ya kampeni chafu sana za Wazungu, kwamba Afrika hakuna usalama, hususan zama hizi za magaidi.
Mbona Black September waliteka wanariadha Munich ? Watasema, Afrika kuna miundo mbinu dhalili n.k
    Mwisho, Afrika si mshiriki bali mshindani wa dhati kama tulivyoona. Mtu mweusi si mtumwa, bali ‘championi’ katika nyanja anuwai kama tulivyoona akina Jesse Owens.
Wapo mabingwa wengine weusi katika nyanja tofauti za maisha-Afrika inastahili nafasi sawa.
    Shime, Waafrika wenye maradhi ya kutokujiamini ama kujidharau(inferiority complex) waone kuwa mtu Mweusi yuko juu sana .
Akina Hitler wa kizazi hiki wazomewe kwa sababu Afrika inakwea juu sana . Afrika, “Citius, Altius….Afrika Fortius”, ina  kwea Haraka, Juu na kwa Nguvu. Afrika  kilele cha utukufu.
Mwaka 2008 mashindano ya Olimpiki yalifanyika Uchina, mwaka huu 2012 yatafanyika London,siku chache zijazo kuanzia sasa. Je kutatokea ubaguzi wa rangi wa kuwabagua akina Caster Semenya?
     0786 324 074
   
   
   


Tuesday, May 29, 2012

SUMATRA DAR NOMA!!

*Abiria wahofia kitisho cha Al Shabaab
Na Conges Mramba, Nansio
MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri Nchi Kavu na Majini(SUMATRA) inadaiwa kushindwa kusimamia ukaguzi wa vyombo vya majini Ziwa Victoria, hivyo kusababisha hofu ya kuweza kutokea   ajali.
  “Maofisa wa SUMATRA wanapotoka Dar es salaam kuja Ziwa Victoria kuendesha zoezi la ukaguzi,wanawashurutisha wamiliki wa vyombo vya majini kuwalipia gharama za chakula na malazi hotelini”, Gazeti hili limedokezwa.
Nahodha wa Meli moja ya kampuni binafsi, ameliambia Gazeti hili kwamba,kitendo cha maofisa wa SUMATRA kupewa hisani ya gharama za chakula,malazi na maburudisho wakati wanapofanya ukaguzi wa vyombo vya usafiri majini Ziwa Victoria,huhafifisha ubora wa vyombo husika,na changamoto kwa manahodha na mabaharia.
“SUMATRA, wanapofika Mwanza,toka Dar es salaam, wanakula na kulala kwa gharama za wamiliki wa meli na boti hapa Ziwa Victoria, sasa watakagua nini kama siyo kulipa fadhila kwa yale waliyotendewa na wamiliki wa meli ama boti?” Amehoji Nahodha wa Meli moja kwa masharti ya kutotajwa jina wakati wa mahojiano na gazeti hili.
 Tumemtafuta    Ofisa Uhusiano wa SUMATRA, David Mziray, kwa takriban juma zima,ili kujibu tuhuma hizo, lakini simu yake ya mkononi ama iliita pasipo majibu, ama ilikuwa imefungwa.
 Hata hivyo, Ofisa Mfawidhi wa SUMATRA,Mkoani Mwanza, Alfred Wariana, amesema maofisa wa SUMATRA kutoka Dar es Salaam,hufika Mwanza kufanya ukaguzi wa kila mwaka,na hulipiwa gharama za usafiri,malazi na chakula na Mamlaka, na wala siyo wamiliki wa vyombo vya usafirishaji Ziwa Victoria.
  Jumapili, Mei 27 mwaka huu,mwandishi wa makala haya alisafiri kutoka Jijini Mwanza,kwenda Nansio,Ukerewe kwa Meli ya Mv. Samar II inayomilikiwa na Kampuni na Kampuni ya Samar Filling Station,ya Mwanza.
Hii ni meli iyojengwa mwaka 2009 na Kampuni ya Songoro Marine Transport pia Jijini Mwanza,kama meli ya mizigo. Ilikuwa ikifanya safari zake kati ya Mwanza na Uganda.
 Meli hiyo ilibadilishwa matumizi mwaka huu, ikawekewa viti na kuanza kusafirisha abiria kutoka Mwanza hadi Nansio,Ukerewe. Uwezo wake ni kuchukua abiria 248 na tani kati ya 101 na 138 za mizigo.
 Nilimuuliza Nahodha wa meli hii,Kapteni Adam Andrew Alex, “Meli ina vifaa vya uokozi kwa kiwango gani?”
“Ina maboya(life rings) 60 na life jackets 350.Tuna mashua moja na vifaa 10 vya kuzimia moto”, Kapteni Alex alisema.
Kutoka Jijini Mwanza hadi Nansio, mji mkuu wa wilaya ya Ukerewe yenye visiwa 27 na vingine 11 visivyokaliwa na watu kuna umbali wa mali 29 za majini.
Kapt.Alex anasema alihitimu katika Chuo cha Mabaharia, Dar es salaam Maritime Insitute, na alikuwa na uzoefu wa mwaka mmoja kazini. Akasema meli yake ilikuwa na mabaharia tisa wenye uzoefu wa kati ya miezi sita na mwaka mmoja kazini.
 Akizungumzia mazingira ya kazi, amesema mikataba ya ajira katika vyombo hivi vya binafsi haiendani na kazi, “Hakuna hata malipo ya muda wa ziada wa kazi(over time),wala hakuna usafiri baada ya kazi”, Kapt. Alex amedai.
 Eferi Bulongo(75) ni miongoni mwa abiria waliosafiri na meli hiyo, Samar II kwenda Nansio. Nilimuuliza, “Una maoni gani kuhusu usafiri Ziwa Victoria?”
 “Sipendi kusafiri kwa meli binafsi;zinasumbua, ratiba ya safari haieleweki,ni namna wanavyojisikia wao, na melini hakuna mahitaji ya lazima ya kuaminika kama chakula na vinywaji;kuna chai”, Bulongo amedai.
 Amesema, meli za Mashirika ya Umma,kama Marine Services Company(MSC) ni bora kabisa, ratiba ya safari huzingatiwa.
“Hizi meli za MSC zinahujumiwa na baadhi ya wafanyakazi wake.Labda wanapewa rushwa na wamiliki wa meli za binafsi ili meli za MSC ziache kufanya huduma ili  wafanye biashara, abiria wengi hawazipendi hizi meli binafsi”, Bulongo amesisitiza, huku akihoji, “Kwanini Meli za MSC ndizo ziharibike kila kunapokucha? Mv.Clarias haijafanya kazi kwa zaidi ya miezi minne; sasa wamesikia Bunge la Bajeti karibu kuanza, ndiyo tunasikia itaanza kati ya kesho(Mei 27) na kesho”, anasema Bulongo.
  Nikampigia simu Kaimu Meneja Mkuu wa MSC,Projest Kaija kujibu tuhuma hizo.
“Leo, Jumapili Mei 27, tunaifanyia majaribio Mv.Clarias. Baada ya siku chache itaanza safari zake kwenda Ukerewe”, Kaija anasema.
 Anakanusha kuwepo kwa tuhuma zenye lengo la kuhujumu Kampuni ya umma kwa nia ya kuwanufaisha wenye meli binafsi.
“Wafanyakazi wa MSC wanawezaje kuhujumu kampuni inayowapa mshahara?” Anahoji,huku akisisitiza kuwa tuhuma hizo zitachunguzwa,kwa kuwa uongozi wa kampuni hiyo ya umma umebadilishwa siku chache zilizopita; kampuni inafanya matengenezo(reform) anuwai.
 Nikampigia simu  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Everest Ndikilo,ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa,  kumsaili:
“Kwanini abiria wanapopanda katika vyombo vya majini Ziwa Victoria hawakaguliwi, ili kubaini uwezekano wa kuwepo kwa magaidi kama  Al-Qaeda na Al-Shabaab, wanaotishia maisha ya watu nchi jirani ya Kenya?”
Magaidi waliwahi kuteka nyara ndege ya Air Tanzania(ATC)mwaka 1988 , yenye maandishi ubavuni, ‘Tango Charlie” wakati ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza,ikalazimishwa kwenda Jijini London ambako hatimaye jumla ya wateka nyara watano raia wa Tanzania walihukumiwa kifungo cha kati ya miaka mitatu na mitano jela,Jijini London.
 “Ulinzi na Usalama ni Ajenda ya  kudumu na siyo majini tu, hata kwenye majengo,mahoteli na makazi ya raia”, Mkuu wa Mkoa Ndikilo anasema.
Kuhusu maofisa wa SUMATRA,kutoka Dar es Salaam kulazimisha kulipiwa gharama za ukaguzi na wamiliki wa vyombo ziwa Victoria, Ndikilo akasema, “Kama jambo hilo lipo,basi ni tatizo kubwa,nitafuatilia ili hili likemewe”, Ndikilo akasema.
 Gazeti moja litolewalo kila siku hapa nchini kwa lugha ya Kiingereza, katika toleo lake la Mei 23 mwaka huu lilisema kwamba,mwaka 1996 Mv.Bukoba ilipozama na kupoteza maisha ya abiria wake takriban 1,000; miongoni mwao alikuwemo Abu Ubaidah al-Banshiri, ambeye alikuwa nambari mbili wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda.
Naam, kundi hili la AlQaeda, lilianzishwa na Osama bin Muhammad bin Awad bin Laden,Feburuari mwaka 1998 kwa jina la WORLD ISLAMIC FRONT,ili kuhujumu maslahi ya Marekani na washirika wake mahali popote duniani,hata kama ni Ziwa Victoria,
Osama alikuwa mshirika wa Marekani na shirika lao la Ujasusi(CIA) mwaka 1979 wakati majeshi ya Warusi walipovamia Afghanistan.CIA walimfadhili mabilioni ya Dola za Marekani kuanzisha kambi ya mafunzo ya Makhtab al-Khidamat(MAK).
Lakini,baada ya Urusi kuondoka Kabul mwaka 1989, Osama akageuka kuwa adui wa MAREKANI na washirika wao, akaungana na Taliban na Mullah Muhammad Omar kuendesha ‘Jihad’ dhidi ya Marekani na washirika.
Nataka kusema kwamba,mwaka 1996 wakati Mv.Bukoba inazama ziwa Victoria, al-Qaeda tayari walikuwepo,na wangeweza kufanya madhara hapa nchini kwa mashambulizi yenye kulenga shabaha Wamarekani ama maslahi yao hapa Tanzania.
Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Everest Ndikilo, amesema serikali imeimarisha ulinzi katika Ziwa Victoria,kwa kuwa zipo boti za doria zinazozunguka ziwani, na raia wanapaswa kutoa taarifa pindi wanapoona mienendo yenye mashaka ama kitisho cha magaidi wa al-Qaeda ama al-Shabaab!
0786 324 074
  
         

MAGAIDI HATARINI KUVAMIA ZIWA VICTORIA

Mwangwi wa A-Shabaab Nairobi, watikisa wasafiri Ziwa Victoria

          *Mabadiliko ya Tabianchi yatishia meli kuparamia miamba na kuzama
        Na Conges Mramba, Mwanza
   MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari(TPA), imewapandisha kizimbani wamiliki wa meli binafsi, kwani wanazuia Mamlaka hiyo kusimamia usalama wa abiria na mizigo, hata wakati huu wa kitisho cha magaidi wa Al-Shabaab,Afrika Mashariki.
 Mkuu wa Bandari(Port Master)Mwanza, John Mutalemwa, katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi, alisema wamiliki hao wa Bandari binafsi wanashindana na Sheria Na. 17(Tanzania Port Act) ya mwaka 2004.
Sheria hiyo inaipa TPA  nguvu ya kusimamia bandari zote, zikiwemo za watu binafsi,ili kukagua usalama wa abiria na mizigo,kabla na baada ya safari.
 “Sheria inatupa Mamlaka ya kusimamia bandari zote zikiwemo  bubu, tukague na kujua mizigo kiasi gani inasafirishwa; tunatakiwa kutazama abiria ikiwa wanalingana na uwezo wa meli au boti,kulinganisha na uwezo wa  chombo chenyewe, halafu tunatoa, “Port Clearance” kabla ya meli kuanza safari”, Mutalemwa alisema.
Kwa mujibu wa Mutalemwa, vipo vyombo vya usafiri majini,huchukua abiria na mizigo kuoita uwezo. Hii ni kazi ya TPA kufanya ukaguzi makini,ili kuondokana na Ajali Ziwa Victoria.
 “Bandari ni mpaka wa nchi. Lazima tusimamie hali ya usalama, meli inaweza kuleta Al-Qaeda ama Al-Shabaab, nap engine inaweza kuingiza nchini silaha kutoka nchi za vita na migogoro. Eti wanakataa tusiwasimamie…tumewafungulia kesi mahakamani”,Mutalemwa ameliambia gazeti hili katika mahojiano Maalum ofisini kwake juzi.
 Meli za mizigo za Jijini Mwanza, hufanya safari zake hadi Port Bell, Uganda,na Kisumu nchini Kenya, ambako sasa magaidi wa Al-Shabaab wanasaidia kuzimu kupanua kinywa chake.
 Aidha, Mkuu huyo wa Bandari Mwanza amesema nchi za Maziwa Makuu kama Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, na Burundi hazina amani, na Kenya hamkani si shwari,kufuatia kitisho cha Al-Shabaab, wanaopinga majeshi ya nchi hiyo kuingia Somalia kuwafulusha magaidi hao.
Kufuatia hali tete ya usalama nchi jirani, Mutalemwa amesema lazima Mamlaka yake kuwa macho na usalama wa abiria na mali zao dhidi ya hujuma za magaidi, wanaoweza kupata upenyo wakaingiza silaha nchini kupitia Ziwa Victoria.
  Mamlaka ya Bandari humiliki bandari za Mwanza Kaskazini na Kusini,Nansio Ukerewe,Kemondo Bay    na Musoma.
Vituo vingine vidogo vinavyomilikiwa na TPA ni Maisome,Nkome,Bukondo,Kahunda,Miharaba,Kome,Buchosa,Solima,Karumo,Chato na Nyamirembe(Kagera) na Kinesi mkoani Mara.
 Bandari ya Mwanza ni kiungo muhimu kwa nchi za Maziwa  Makuu,hususan Uganda na Kenya,na huchangia kwa kiwango kikubwa kukua kwa shughuli za uchumi,hata katika nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki(EAC).
 Ripoti ya Malka hii iliyotolewa kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu(nakala tunayo), inasema bandari ya Mwanza ingeweza kusafirisha abiria milioni moja kwa mwaka.
 Ingeweza kusafirisha tani mamilioni za  moja za mizigo,kama Reli ya Kati ingekuwa inafanya kazi kwa ufanisi. Hili ni eneo muhimu kwa ukuaji wa uchumi wan chi,lakini kinyume chake ni hasara kila upande.
 “Huduma hafifu za Reli zimesababisha shehena ya kahawa kutoka Uganda na hata Bukoba,kubadili njia(route) na kupitia Bandari ya Mombasa,Kenya “, Ripoti hii inasema.
 Kufuatia huduma duni za Shirika la Reli, Bandari za Mwanza ziko taaban,kwa sababu ya kupungukiwa mapato, zinaendeshwa bila faida.
 Kulingana na Ripoti hii kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu,katika kipindi cha miaka mitano,kuanzia 2006/2007 hadi 2010/2011, mizigo imepungua katika Bandari za Mwanza kutoka tani 480,568 hadi 248,860 mwaka 2011.
Utendaji mbovu wa lililokuwa Shirika la Reli(TRL) ulisababisha treni iliyokuwa ikisafirisha abiria na mizigo kati ya Mwanza na Bandari ya Dar es salaam kusimamishwa.Hali hii husababishwa abiria na mizigo kubadili njia na kukosesha mapato bandari za Mwanza.
 Wafanyabiashara wa Uganda wanasafirisha bidhaa zao kupitia bandari ya Mombasa,nchini Kenya.Shehena ya kahawa kutoka Uganda iliyokuwa ikipitia bandari za Mwanza, inapitia Mombasa na hivyo kupunguza kiwango cha mizigo kutoka tani 250,000 mwaka 2007 hadi tani 100,000 mwaka 2009/2010.
 Kufuatia madudu ya TRL, hata abiria wamepungua katika bandari za Mwanza kutoka abiria 891,634 mwaka 2007 hadi abiria 593,342.Huu ni upungufu wa asilimia 6.3 unaoikosesha nchi mapato na fursa za ajira kwa watu wake.
 Ripoti hiyo ya TPA, imebaini kwamba, wasafiri wa vyombo vya majini Ziwa Victoria wamepungua kufuatia ushindani uliopo wa barabara,hususan baada ya mtandao wa barabara kukamika ujenzi kwa kiwango cha lami.
 Kati ya Mwanza na Bukoba kuna usafiri wa ndege ambao huchangia pia abiria wasisafiri kwa meli.
Kufuatia hali hiyo,ripoti hiyo imebaini kuwa Kampuni ya Huduma za Meli,Marine Services Company(MSC) iko hatarini kufilisika,kufuatia meli zake kuharibika mara kwa mara,kitu kinachodaiwa na baadhi ya abiria kuwa ni hujuma za baadhi ya wafanyakazo wa MSC ili kuwanufaisha wenye meli binafsi.
  Kaimu Meneja Mkuu wa MSC, Projest Kaija, ameliambia Mwanahalisi kwamba madai hayo hayana ukweli, kwa kuwa kuhujumu kampuni unayofanyia kazi maana yake ni kuhujumu mshahara na mapato yako.
“Je, unahujumu Kampuni namna hiyo ili kampuni ikifa wewe utoe wapi mshahara?’ Kaija alihoji.
 Siku za karibuni MSC imewaondoa viongozi wa Kampuni hiyo na kuwaweka wapya ili kuboresha ufanisi na kupunguza nakisi.
 Kwa kipindi cha miaka mitano, idadi ya meli zilizohudumiwa na Bandari za Mwanza, imepungua kutoka 2,684 hadi meli 1,900 mwaka jana.
Bandari ya Mwanza pia huendeshwa kwa hasara ya mamilioni ya shilingi kila mwaka,nakisi ni takriban shilingi bilioni 4.5
Mabadiliko ya Tabianchi na Ongezeko la Joto Duniani,pia hutishia USALAMA wa usafiri Ziwani Victoria.
Kwa kipindi cha kati ya mwaka 1998 hadi 2006,maji ya Ziwa Victoria yamepungua kutoka mita 1,141.24 juu ya usawa wa bahari hadi mita 1,139.20. Upungufu ni wastani wa mita 2.04.
Kulingana na Ripoti hiyo, meli nyingi zimekuwa zikishindwa kufungwa katika bandari za Mwanza na Nansio,Ukerewe. Kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili pia huweza kusababisha kuzuka kwa miamba ambayo huhatarisha usalama wa meli na boti na usalama wa abiria,hasa wanaposafiri nyakati za usiku.
Meli zinapoparamia miamba hutoboka na kujaa maji,ama kuwa katika hatari ya kuzama.
 Ziwa Victoria ni chanzo cha Mto Nile, ambao huanzia katika Maporomoko ya Owen,Uganda; maji husafiri umbali wa zaidi ya kilomita 6,900 hadi Misri. Mvua za masika zinaponyesha Afrika ya Mashariki hubeba rutuba mezi ya Aprili na Mei na rutuba hiyo hufika Misri kati ya Agosti na Septemba na kuwawezesha Wamisri kupata rutuba jangwani.
 Mto Nile ni mungu wa Wamisri. Miungu ya Misri ina ‘mama’ yao Ziwa Victoria. Ni kwa sababu hii, mwaka 1929 na 1957 Misri walitiliana saini mkataba na Wakiloni wa Kiingereza kuzuia matumizi ya maji ya Ziwa Victoria kwa shughuli za kilimo na hata vyanzo vya umeme kama kilichopo Jinja.
 Aidha,kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili hufanya meli kutia nanga katika maji ya kina kirefu,na huku ni kuhatarisha maisha ya abiria,hasa katika maeneo ya visiwa.
 Mkuu wa Bandari ya Mwanza, John Mutalemwa anasema Mamlaka yake imelazimika kuchimba mchanga katika bandari za Mwanza ili kuongeza kina cha futi tatu ili kuwezesha meli kufunga gatini.
 Mradi kama huu unafanyiwa upembuzi yakinifu katika bandari ya Nansio,Ukerewe,lengo likiwa kujenga gati imara na salama.
Mpango wa serikali wa kuunganisha Reli kutoka Tanga hadi Musoma kupitia Arusha, utaweza kurejesha wingi wa abiria na mizigo katika Bandari za Mwanza, au abiria na mizigo ya Uganda,Rwanda,Burundi na Congo wanaweza kutozifikia kabisa bandari za Mwanza,na hivyo kuleta kifo cha mende kwa TPA na Meli za MSC.
Ziwa Victoria ni fursa muhimu kwa Tanzania katika Soko la Pamoja la EAC,lakini fursa hii inaachwa kwa wageni kupitia hujuma na ufisadi unaofanywa na maofisa wa mashirika ya umma kama TRL na MSC.
  www.congesmrambatoday.blogspot.com
    0786 324 074