Monday, October 29, 2012

AKINA NANI WALIMUUA BARLOW?



                 

JAMII ya Jijini Mwanza ilisema kuwa  “motive” ya mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi,ACP Liberatus Barlow,ni wivu wa kimapenzi.
Kikosi maalum cha upelelezi(TASK FORCE) kiliundwa ili kupeleleza mauaji haya ya tashtiti.Kilihusisha makachero wa kimataifa,”Interpol”, na miongoni mwao wataalam wa Kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,
Kabla ya majuma mawili kwisha, tangu mauaji ya Barlow, Oktoba 13 mwaka huu,tayari watu zaidi ya 10 walikuwa wamenaswa,wengine kwa mahojiano na wengine ndiyo hasa waliomuua Barlow jijini Mwanza,wakajakutimkia Dar es Salaam.
Dorothy Moses, ama Dorothy Lymo(42) ndiye mwanamama aliyekuwa na Kamanda Barlow(55) dakika chache kabla ya mauaji ya kinyama kumkumba.Alipigwa kwa risasi ya bunduki nzito, Shotgun, “Greener”shingoni,shingo likafumuliwa kabisa.
Felix Felician(50) ama maarufu Jijini kama ‘Pepe’ alitiwa mbaroni kwa tuhuma kuwa ndiye aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi na Dorothy, ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi ya Nyamagana B,Jijini.
Ilihisiwa kuwa, pengine mwanamama huyu mfuauji, alikuwa akigawanya penzi la tashtiti kwa Marehemu Barlow na ‘Pepe’yumkini kiasi cha kuleta wivu na visasi.
Kufuatia tuhuma hizo ambazo polisi wangali wakifanyia kazi kwa umakini, alikamatwa pia Fumo Felician(46),mchezaji wa zamani na ‘striker’ mwenye mashuti makali katika timu ya Pamba ya Jijini Mwanza na Dar es salaam Young Africans. Pepe ni nduguye Fumo.
TASK FORCE ya makachero wa polisi iliongozwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini(DCI)Robert Manumba, iliwakamata pia Bahati Agostino na Waibe Maboto, kwa sababu Barlow alipouawa huko Kitangiri usiku wa kuamkia Oktoba 13, majahili wale walimpora redio ya upepo(Radio Call), na kasha walipora simu ya Dorothy.
Nataka kusema kuwa,bado watu hawajajifunza kwamba sasa kuiba simu ya mtu,hususan katika matukio ya ujambazi na mauaji namna hii ni kujiweka hatarini.
Nataka kuandika hapa kwamba, hisia za watu kwamba kundi hili la majambazi lilikuwa na watu werevu, ni uongo tu. Kama walitoweka na simu ya Dorothy wakaendelea kuitumia hata kama walishanyofoa laini, hawa walikuwa majambazi waliojua kufyatua risasi, na wala hawakujua chochote kuhusu teknolojia ya leo.
Hawa walivyo mazuzu, eti walitupa laini ya Dorothy, wakaendelea kuitumia simu ile wao wenyewe, ama mtu mwingine waliyemuuzia, huku wakijua simu ile ilisajiliwa na hata namba ya simu iitwayo ‘IMEI’ ilisajiliwa?
Kulingana na teknolojia ya siku hizi, ilikuwa rahisi kama nini kwa makachero wa ‘Interpol’ wenye utaalam wa hali ya juu katika ‘Information Technology’ kuiona simu hiyo na kujua mahali ilipokuwa ikiitia hata kama laini ya awali ilishanyofolewa na kutupwa.
Makachero waliifuatilia simu hiyo na kufanya mtego mdogo tu,tayari aliyekuwa nayo akatiwa mbaroni,ili akaeleze alikoipata na ilikuwa rahisi mno kuwasema waliompa au mahali wenzake walipokuwa.
Hivyo,tusiwape sifa majahili hawa kwamba walikuwa mauaji wa kimataifa, “Executioners’” kumbe majangili tu, wanaomea Tanzania kwa sababu ya uzembe wa polisi wetu na tabia ya jamii hii ya kufumbia macho watoto wao wahalifu.
Kwa kutumia IT makachero waliwanasa akina Bonge(30) na Amos Waibe Maboto; walikamatwa jijini Mwanza,kwa kutumia TEKNOHAMA.
Nataka kusema kwamba, umefika wakati sasa kutumia kompyuta kuwanasa wahalifu,badala ya kutumia mashushushu ambao wengine si waadilifu,nao hujiingiza katika usaliti na kuwaumiza raia.
ALHAMISI,Oktoba 25 mwaka huu,Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai,Kamishna Mwandamizi wa Polisi,Robert Manumba, akawaambia waandishi wa habari jijini Mwanza kwamba,kundi la watu waliokamatwa jijini Mwanza likihusishwa na mauaji ya Kamanda Barlow, hawa kuwa hasa wauaji.
Kwamba, walishikiliwa na jeshi hilo na kuhojiwa kwa sababu katika medani ya upelelezi,ni muhimu kama nini kuwahoji mashuhuda wengi,kama huyo Dorothy Lymo,ambaye alikuwa na marehemu wakati wa tukio la mauaji na hata hao ‘jamaa’ zake, akina Pepe na Fumo na wengine.
Wakikutwa hawana hatia,basi wataachwa huru.Ni muhimu polisi kuwahoji washukiwa wote na si mara moja au mbili,ili wakupe mwelekeo wa upelelezi nap engine sababu za kifo cha mtu kama huyo RPC Liberatus Barlow.
Kauli ya DCI Robert Manumba,kwamba hawa waliotajwa wangali wanapelelezwa,hata kama uchunguzi wa awali umebaini kuwa hawana uhusiano wa moja kwa maja na mauaji ya Kamanda,inaondoa tu ‘Motive’ kwamba aliuliwa kwa wivu wa kimapenzi, lakini bado tuhuma zingalipo dhidi yao.
Manumba, aliwaambia waandishi wa habari Alhamisi,Oktoba 25 kwamba waliomuua Barlow ni majambazi wazoefu(wa uhalifu,siyo weledi),na kwamba inawezekana lilikuwa tukio la ‘nasibu’ na bahati mbaya hivi.
Kundi la majahili saba, miongoni mwao watano: Muganyizi Michael Peter(36) mkazi wa Isamilo,Mwanza,Chacha Mwita(50),Edward Bugazi Kusuta,Bhoke Marwa Mwita(42)nz Magige Mwita Marwa, ambao wengine walikuwa wakazi wa Gongo la Mboto,Dar ndiyo hasa walioshiriki katika mauaji.
Watu hawa, majira ya saa nne hivi  usiku, siku ya tukio, walitangulia kupora mali za watu katika ‘grocery’ ya New Tuliza Inn,Pasiansi, waliwateka wanywaji na kuwapora vitu na simu ya mama mmoja.
Usiku huo wa Oktoba 12,Ijumaa saa sita hivi usiku walifika Kiseke katika baa iitwayo,Green Corner, waliwapora wateja,walipora hata Konyagi,wakabugia.
Sasa, wakati wanafika Kitangiri eneo lile la tukio,wakakutana na Barlow ambaye alikuwa akimsindikiza Dorothy nyumbani kwake, akawamulika kwa taa za gari.
Dorothy, anasema aliwaona wakiwa wamevalia vivazi vile vya Polisi Jamii ama Ulinzi Shirikishi, sasa Kamanda Barlow akidhani ni hao walinzi wa kijamii, akawamulika ili awaone vizuri.
Dorothy akamwambia Barlow, “Unawamulika unawajua?” Basi, kuona hivyo hgao jamaa wakamfuata Barlow haraka na kumzingira, wakaanza kufanya matata, Barlow akachukua ‘Radio Call’ ili awaite polisi.
Muganyizi Peter akamfatulia risasi ya Shotgun shingoni, ikamfumua shingo kabisa, ilimvunjilia mbali shingo lake.
Walichukua hiyo Radio Call ya Barlow na simu ya Dorothy,wakajitoma gizani.Keshoye, wakajiondokea kwenda Dar es Salaam,bila shaka walishajua walimuua nani!
TASK FORCE ya makachero wa polisi ya KIKOSI  CHA KISASI DHIDI YA MAUAJI YA BARLOW kiliwasili jijini Mwanza jioni Oktoba 13. Hata Inspekta Jenerali wa Polisi, Said A. Mwema, mtikiso wa mauaji hayo ulimleta Mwanza siku hiyo.
Makachero wa polisi, wakiwamo hao wa kimataifa, Interpol waliwasili Mwanza, wakasambaa Mara,Shinyanga,Mwanza, Geita,Bukoba na Dar es salaam, ili kufanya mtandao mkubwa katika medani ya upelelezi.
IGP Mwema, amewaambia wanahabari kuwa,waliomuua Barlow walikuwa saba, hao watano wamekamatwa tayari na wengine wawili wananyatiwa bado, na kwamba hata kama waende Uingereza watatiwa mbaroni na Interpol na watashushwa hapa nchini ili wakabiliane na mashitaka,ili kuwa fundisho kwa wenzao. Hiki ndicho KISASI alichosema Mwema, dhidi ya mauaji ya Barlow.
Nataka kusema kwamba, kulingana na Mwema,makachero wa hiki KIKOSI MAALUM CHA KISASI, walifanya kazi yao kabla ya siku 12 kwisha na kuwatia mbaroni wahusika, kama wanavyofanya kazi Federal Bureau of Investigation, Scotland Yard   ama  Military Intelligence 5(MI5)!
Majambazi hao walikamatwa Dar,Gongo la Mboto,wakakutwa na silaha mbili,Shotgun hiyo waliyotumia kumuua Barlow,ilikatwa kiatako na nyingine ni ‘Pump Action’.
Hadi Oktoba 25 redio ya upepo ya Barlow waliyopora eneo la tukio,ilikuwa bado kukamatwa,ndiyo iliyochongea Barlow kuvunjwa shingo kwa Shotgun Greener iliyofyatuliwa na huyo Muganyizi Peter,Mhaya kutoka Kagera!
Walipomuua Barlow wakatorokea Dar es salaam ambako pia hawakulala,walipora mali za raia hadi siku walipokamatwa. Nakwambia Jasiri haachi asili.
Kufuatia maelezo ya IGP Mwema na DCI Manumba, nataka kutafakari mambo machache hapa. Sina ubishi na kauli kuwa Barlow hakuuliwa kwa wivu na  visasi vya kimapenzi.
Nataka msomaji ajiulize maswali yafuatayo:
Mwanza,kuna majambazi mwazoefu wenye bunduki kama Shotgun, wanatamba tangu saa nne tu za usiku kuanzia Pasiansi,Lumala hadi Kiseke?
Polisi wa doria wanakuwa wapi hadi baa ziporwe hata Konyagi na majambazi,hata waanze kujipongeza,Kazi na Dawa, utadhani nchi haina mwenyewe?
Akina Muganyizi, walipokamatwa eti walikutwa na simu nyingi walizopora wananchi, bila shaka mchana kweupe!
Polisi walikuwa wapi wakati vibaka, wezi na majambazi wanapotishia maisha ya watu na mali zao?
Hivi Mwanza nako kuna  ‘Security Service’? Mbona raia wanatishiwa na vibaka na majambazi ambao sasa hawana hofu tena na doria za polisi?
Niliandika katika sehemu iliyotangulia kwamba, hapa Mwanza ndipo hakimu mmoja aliwahi kumtorosha jambazi sugu kwa ‘removal order’, siku ya kesi RCO Goodluck Mongi, akaambiwa na askari wake kwamba,mshitakiwa hakuwepo rumande!
Hapa Mwanza,ndipo jamaa mmoja mwaka 2005, alijipenyeza katika msitu wa wana usalama pale CCM Kirumba, akampiga mweleka Jakaya Kikwete wakati huo akiwa mgombea mteule wa Chama cha Mapinduzi! Kesi hii ilifika mahakamani,jamaa akanyeshewa mvua ya miaka jela.
Aliyekuwa Mbunge wa Shinyanga Mjini, Leonard Derefa, aliwahi kusema Bungeni kwamba jeshi la polisi livunjiliwe mbali,kwa kuwa lilishashindwa kulinda raia na mali zao-limewaacha majambazi na vibaka kutamba!
Mimi sitaki jeshi hili livunjwe,ili kuwe na “Vacuum” ama Ombwe ambalo linaweza kuleta kiama zaidi ya hapa tulipo.
Nataka kumwambia rafiki yangu Mwema ajiulize kama raia tunavyojiuliza: Kwanini Barlow alikuwa peke yake usiku wa manane,bila ulinzi? Kwanini alitembelea gari la kiraia tena lenye stika bandia ya Bima?
RPC hakuwa na walinzi? Je,polisi wa Mwanza wanafanya nini kuwakamata vibaka hata wanamiliki silaha na kumuua RPC? Polisi wanakamata wahalifu au wanafanya biashara ya daladala mjini? Kwa nini polisi wawe na vitambi? Mbona hata Bill Gates, Carlos Slim, Warren Buffett na wenzao hawana vitambi? Eti Polisi wa Mwanza wana vitambi!!
Nataka kumwambia IGP Said Mwema akumbuke kwamba, nilimuuliza katika mkutano na waandishi wa habari kwamba, Barlow aliuawa Oktoba 13, ilipofika Oktoba 25 tayari majahili hao walikwishatiwa mbaroni-siku 12 tu  za Operesheni ‘LIPA KISASI DHIDI YA MAUAJI YA BARLOW’.
Nika mkazia macho ya kidadisi IGP Mwema na kumbandika swali,
“Kwanini kasi hiyo ya majuma mawili ya kuwakomesha majambazi waliomuua Barlow isitumike pia kuwakomesha majahili wanao ua raia na kuwapora mali zao?”
Kwa nini kasi hiyo, “Supersonic Speed” isitumike katika upelelezi wa kesi nyingine za raia wa kawaida, wanaohujumiwa na majahili hawa na kuporwa mali na maisha?
Kwa nini polisi wanashindwa kufikisha kesi hata ya vibaka mahakamani, eti upelelezi haujakamilika? Kwanini kesi ya Barlow upelelezi ufanywe kwa kasi za viwango kama zile za Samuel Sitta-Standard and Speed!
“Polisi na raia wema lazima kuunganisha nguvu na talanta zao ili kuongeza ‘speed’ ya kuwakomesha wahalifu,ili nchi iwe salama”, alinijibu IGP Mwema,pale ukumbi wa Jini,Mwanza.
Said Mwema, anatishwa na jamii kukosa uzalendo kwa Taifa letu, na kushindwa kutimiza wajibu wa kizalendo kwa Taifa.
Oktoba 25,ndiyo siku nilipobaini kuwa Said A.Mwema, ni mwanafalsafa wa kiwango cha juu sana.Alianza kueleza kauli za marais wa Marekani akina John Fitzgerald “J.F” Kennedy na Abraham Lincoln, juu ya maslahi ya nchi kuwa kipaumbele cha kwanza,na uzalendo kwanza kuliko matumbo. Siku hizi Tanzania raia na polisi ni wazalendo wa matumbo yao!
Naam, Mwema akauliza hivi, “Usiulize Tanzania itakufanyia nini,uliza utaifanyia nini Tanzania?” Mwema amesema uzalendo unatoweka katika nchi yetu na maslahi ya taifa yametupwa,ndiyo maana polisi na raia wameshindwa kuunganisha nguvu na vipaji vyao ili kuwatoa kamasi majambazi!
Nitaichambua hotuba ya IGP Mwema, juma lijalo , Itaendelea.










Monday, October 22, 2012

MAUAJI YA KAMANDA BARLOW-FULL STORY 2



                       
JULAI 28,mwaka 2003, aliyekuwa Mkuu wa kituo  kikuu cha Polisi  (OCS) Jijini  Mwanza, Daniel Maburuki Mahende(45) aliuawa  kwa risasi na majambazi,katika eneo la Bugando,jijini Mwanza.
Serikali iliahidi kuwatia mbaroni wauaji hao, waliohisiwa majambazi kutoka Burundi. Haikujulikana baadaye kwamba wauaji hao walichukuliwa hatua gani na mahakama.
Mwanza,kumetokea matukio ya mauaji ya kinyama sana.Lakini umma haukujulishwa hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika ili liwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama zao.
Katika makala yaliyotangulia, nikaeleza kwamba, aliwahi kupigwa risasi ya kichwa ‘cashier’ wa Tanzania Breweries Limited(TBL),Pasiansi, Jijini,zikaporwa zaidi ya shilingi milioni 200.
Baadaye,nilipomuuliza aliyekuwa Wakili wa Serikali Mfawidhi,katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP)Kanda ya Ziwa, Anselm Mwampoma, akaniambia:
“Kesi hiyo ya mauaji ya ofisa wa TBL,huko Pasiansi,haikuwa na ushahidi wa kutosha kuwatia watuhumiwa hatiani”, alisema Mwampoma.
Tuseme, kesi hiyo “Ilivurugwa” ama ilichakachuliwa,hata ushahidi uliokuwepo haukutosha hata kuwafikisha mahakamani washitakiwa. Hili Mosi.
Pili, aliyewahi kuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mwanza,(RCO) Goodluck Mongi, aliwahi kusema katika semina iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) kwamba wapo maofisa wa Mahakama Mwanza, waliwahi kumtorosha mtuhumiwa wa ujambazi ,gerezani Butimba,kwa ‘removal  order’ akatoweka rumande, na siku ya kesi mahakamani mshitakiwa  hakuonekana!
 Yaani, wakati maofisa wa polisi wakihaha kumfikisha mtuhumiwa wa ujambazi mahakamani, alishayeyuka rumande!
Sipendi kusema kilichotokea, lakini msomaji unaweza kujua inakuwaje mtuhumiwa wa ujambazi anapewa dhamana, kwa “removal order” ya   Mheshimiwa Hakimu, pasipo hata polisi kujua?
Kuna matukio lukuki  ya ujambazi Mwanza,wizi,uhalifu,mauaji ya kutatanisha n.k Hata hivyo, umma haujui kwa nini wahusika hawajakamatwa na kufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.
Hii ni HATARI!! Matukio ya karibuni sana ambayo hata Marehemu Kamanda Liberatus Barlow aliyashuhudia,ni ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Gazeti la Kasi Mpya, Richard Masatu, ambayo licha ya ripori ya daktari kuoneshwa kuwa aliuawa, polisi waliendelea kusema aligongwa gari!
Kuna mauaji ya mmiliki wa nyumba moja ya wageni Jijini Mwanza anayejulikana kwa jina la Manumbu, aliuliwa kwa risasi,lakini umma haujafahamu kilichotokea, na wala hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Kuna kawaida ya matukio ya mauaji kutokea Mwanza,lakini sijui polisi wanashindwa kuwabaini wauaji ili wafikishwe mahakamani?
Kuna watu wanakufa katika mazingira ya kutatanisha,lakini mwisho wa siku hakuna mtu anayekamatwa na polisi ili ashitakiwe mahakamani.
 Mwanza,kuna historia ya Mbunge mmoja, kumwagiwa tindikali,lakini ‘kesi iliyeyuka’ kwa njia zisizofahamika,kufuatia mtuhumiwa kuyeyuka,kama walivyoyeyuka  mashahidi wa kesi ya mauaji ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa huko Kenya,zama za NYAYO,Dk.Robert Ouko.
Aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza, Leonard Bihondo, alituhumiwa kumuua aliyekuwa Katibu wa CCM wa Kata ya Isamilo, Bahati, alitiwa mbaroni na kesi yake ingali ikisubiri kuanza kusikilizwa.
Jumatano, Oktoba 17,mwaka huu,nikaazimu kumuuliza Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini(DCI)Robert Manumba,kama alijua mauaji ya Kamanda Barlow yalifuatiwa na mauaji ya watu wengine hapo Mwanza,lakini haikufahamika hatma ya mauaji hayo?
Na kwamba, Je, polisi wamefikia hatua ya ku  “compromise” na hali hiyo? Nilimkuta Robert Manumba,mbele ya jengo la ofisi ya Kamanda wa Polisi Mwanza,nikamsalimia kasha nilipomgusia jambo hilo akaniambia:
“Rafiki yangu,mimi ni mgeni hapa! Wenyeji mbona wapo ofisini unaweza kuwauliza hata wakasema kuhusu kilichopo?’ Manumba aliniambia. Nilicheka,kasha nikamuaga,maadam alikwisha pangua ‘ngumi’ za uso nilizotaka kumtupia!
Nilimpata Mkuu wa Upelelezi (RCO)Mkoani Mwanza,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi(SSP)Joseph Konyo(siyo Joseph Kony wa  Lord’s Resistance Army wa Uganda).Siku hiyo, Oktoba 17,nikamwambia Joseph Konyo, juu ya migogoro Rwanda,Burundi na Jamhuri ya Congo(DRC) ilivyosababisha wakati Fulani huko mkoani Kigoma bunduk,SMG,i kuuzwa kwa kubadilishana na  DEBE LA MAHINDI au MTAMA!
Nilimuuliza Konyo, kama hakujua kwamba wakati Fulani wananchi kutoka Kigoma walihudhuria semina moja ya Upunguzaji silaha, wakasema  Mwanza ndilo lilikuwa soko kuu la silaha?
Na kwamba, polisi waliposhindwa kuchukua hatua sasa silaha haramu zinapatikana mikononi mwa wahalifu hata kuweza kuua raia na hata maofisa wa polisi kama Kamanda Liberatus Barlow?
“Nilikuwa Kigoma, wakati huo mwaka 2004,iliposemwa kwamba bunduki moja ya SMG ilibadilishwa kwa debe la mtama au mahindi katika magulio.Haikuwa na ushahidi kwamba wanunuzi wa silaha hizo walitokea Mwanza, hata hivyo polisi lazima washirikiane na raia ili kutokomeza uhalifu”, Joseph Konyo alisema.
“Nawashauri raia wema wa Mwanza,wasiache kushirikiana na polisi ili kusaidia kuondoa kitisho cha amani. Bila amani,hakuna kitakachofanyika. Wasikate tamaa,raia wanapaswa kutoa taarifa hata katika ngazi za juu za polisi,wanapaswa kutuamini kama wanataka tupambane na uhalifu na kuushinda”, Konyo alisema.
Akasisitiza kuwa, kumkamata mtuhumiwa ni jambo moja,lakini kumfikisha mahakamani na kuthibitisha kosa, ni jambo la pili linalohitaji ushiriki wa raia wema kutoa ushahid, ili kuthibitisha kosa pasipo shaka yoyote.
Nikamkumbusha RCO,Konyo madai ya wananchi wa Mwanza,kwamba wakitoa taarifa za uhalifu,mara wahalifu hukamatwa kasha kuachwa huru ambapo kitendo cha raia kuwajulisha polisi wahalifu hugeuka jambo hatari kwa maisha yao?
Siku tano baadaye, RCO,Joseph Konyo akafanya mkutano na maofisa wa Polisi na kuwataka kushirikiana ipasavyo na wananchi katika vita dhidi ya uhalifu nchini.
“Polisi tunapofuatilia uhalifu,tunapowajibika ipasavyo katika matukio ya uhalifu,tukishirikiana na raia wema tutatokomeza uhalifu”, Konyo alisikika akiwaambia maofisa wa Polisi.
Mkutano huo,ulihusisha maofisa wakaguzi wa polisi, maofisa wa idara ya upelelezi na maofisa wa kawaida.
 Kauli hiyo ya Konyo imekuja siku chache baada ya kifo ca Barlow, ambaye pia ameuliwa katika mazingira ya kutatanisha, ambayo raia wanadhani kulikuwa na uzembe na tabia ya kuwalea wahalifu iliyojengwa muda mrefu hata kusababisha mazingira ya ‘Mdharau Mwiba Guu likaota tende!”
Kufuatia hali hiyo, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Nchini,Robert Manumba, anasaidiana na makachero wa Polisi wa Kimataifa, Interpol, kuwawinda majahili hao waliomuua Barlow,na inshallah, baada ya kitambo watakuwa wametiwa mbaroni na kufikishwa mbele ya sheria.
Hadi sasa watu takriban 15 wamehojiwa na polisi,na watu kadhaa wanashikiliwa kufuatia mauaji hayo ya kuamkoa Jumamosi,Oktoba 13, majira ya saa 7-8 huko Kitangiri.
Mwanza ni mahali ambapo motto aliwahi kutekwa nyara, watekanyara wakaomba wapewe mamilioni ya fedha ili wamwachie mtoto huyo. Uliwahi kusikia hadithi za utekaji nyara na watekaji kuomba fedha nyingi za ‘kikombozi’?
     Haili liliwahi kutokea huko Bwiru,mtoto akatekwa nyara, wateka nyara wakaomba pesa, polisi walipojaribu kumwokoa wakishirikiana na babaye, mtoto alitoswa Ziwa Victoria na kufa!
Haya mambo ya Palestina, Ulaya na Afghanistan,yaliwahi kutokea bwiru,Mwanza. Mwanza watu waliwahi kuteka msichana wa baa,wakachinja, wakachukua kichwa,shavu la kulia wakanyofoa sehemu zake za siri,kasha kiwiliwili kikasokomezwa kwenye sandarusi na kuachwa penye pagala!
Wauaji wengine walitoroka,polisi hawakuwahi kuwakamata na kuwasweka hata rumande. Hapa Mwanza, ndipo mahali ambapo mwanamke anachinjwa chumbani, hata majirani wakashindwa kujua hadi walipoalikwa na mainzi ya kijani asubuhi,maiti akiwa ndani ya kiroba,katika pagala la mitaa ya Kiyungi!
Hapa ndipo jamaa mmoja wa Kenya alitaka kumuuza albino kwa shilingi milioni 400,ikawa bahati polisi wakamnasa na kumwokoa albino aliyekuwa hatarini kuchinjwa ili viungo vyake vikauzwe kwa watu wanaotaka utajiri kwa kutumia  ‘ndaku’ au bahati Fulani za utajiri.
 Huku ndiko albino huwindwa kama wanyama,hata sasa wapo wanaoishi katika kambi maalum wasije kuuliwa. Hapa ndipo vikongwe wanauliwa kwa tuhuma za ushirikina.
Hapa ni mahali ambapo wahalifu wana ‘confidence’ hata walipomaliza kumuaa Kamanda Barlow, walitoroka na Radio Call na bastola yake.Walivalia majazi ya polis Jamii.Waliyatoa wapi?
Hata hivyo, katika medani ya upelelezi,ni mapema mno kusema nani alimuua Kamanda Barlow ambaye tayari amezikwa kwao Kilimanjaro.
Katika medani ya ukachero,siyo kila anayekutwa na kamba shingoni akiwa amekufa,basi kajinyonga! Polisi wana kazi ya kuchuja habari,kuzikagua na kugundua wahalifu wapya,kasha kutafuta ushahidi na kuutetea mahakamani,ili  kuithibitishia mahakama pasipo shaka yoyote(beyond reasonable doubt) kwamba muuaji ni Fulani.
Itaendelea


Tuesday, October 16, 2012

BARLOW FULL STORY!!




IJUMAA,Oktoba 12 mwaka huu,yaani siku moja kabla ya mauaji ya kinyama dhidi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Liberatus Barlow(55), Mrakibu Mwandamizi wa Polisi(SSP) Lily Matola, anawaambia waandishi wa Habari:
“Kesho Jumamosi(Oktoba 13) Kamanda,Liberatus Barlow) anataka kuzungumza nanyi kitu nyeti”, SSP Liliy Matola, anasema.
“Unajua, yeye anakawaida ya kushiriki Doria yeye binafsi bila kuhusisha askari; ana cha kuwaambia, baadhi yenu ana namba zenu za simu, atawajulisha muda wa kukutana naye,lakini ni kama saa tano hivi asubuhi”, anasema SSP Matola,Ofisa Mnadhimu wa Polisi(Staff One) Mwanza.
Asubuhi, siku ya Jumamosi, zikasikika habari kuwa Barlow alikuwa kauliwa na majambazi,katika eneo la jirani na Hoteli ya Tai Five, karibu na Kona ya Bwiru,Kitangiri,Jijini Mwanza.
Nilikutana na ACP Liberatus Barlow(55) mara ya mwisho Oktoba 19,siku ya Jumatano mwaka huu. Ilikuwa takriban saa 50 kabla ya mauti kumkumba.Alikuwa ndani ya sare zake za kipolisi na kofia kichwani.
Ilikuwa saa saba hivi mchana, akiwa nje ya jingo la ofisi yake.Alikuwa akiwaambia wanahabari juu ya tukio la kukamatwa vibaka watatu waliojaribu kupora maberamu ya mafuta katika matangi ya Kampuni ya ENGEN, Igogo,Jijini Mwanza.
Naam, Kamanda Barlow ameuawa na watu wanaosadikiwa majambazi,huko Kitangiri,jijini Mwanza,majira ya kati ya saa saba na saa nane za usiku, alipokuwa akitokea kumsindikiza Doroth Moses, ambaye ni Mwalimu katika shule ya Msingi ya Nyamagana B,mara baada ya kikao cha watu wa mkoa wa Kilimanjaro.
Baada ya kupata  habari za kifo cha Barlow, mara nakumbuka kauli ya SSP Lily Matola:
“Kesho, Jumamosi waandishi mje hapa ofisini Kamanda Barlow anawahitaji,atakuwa na jambo muhimu kuwapasheni habari wananchi”.SSP Lilian Matola, alikuwa akisema kwa utulivu mkubwa,kama ilivyo kawaida yake,huku akitoa tabasamu tamu la asali.
Sijui,Kamanda Barlow aliwaalika waandishi lufika ofisini kwake Jumamosi hiyo kufanya ‘coverage’ ya kitu gani? Labda, alitabiri kitakachomkuta?!
Sikufika ofisini kwa Kamanda asubuhi hiyo ya Jumamosi,kwa kuwa nilikuwa nikihudhuria Ibada, kanisani Kirumba.Napenda kumwabudu Mungu.
Mkurugenzi wa kituo cha televisheni cha Barmedas cha jijini Mwanza na Meneja wa Kituo, Charles Sokoro, walinigutua kusema kanisani hapo kwamba,Kamanda Barlow alikuwa kauliwa na majambazi usiku wa kuamkia hiyo Jumamosi!
Hili siyo tukio la kwanza la majambazi kuwaua maofisa wa ngazi za juu wa   Polisi jijini Mwanza. Jiji la Mwanza linao raia wema na pia wapo majambazi,mashetani hayawani na majahili waliozowea kupokonya maisha ya watu kwa kuwamwagia tindikali,kuwaua kwa risasi na sumu.
Julai 28,mwaka 2003, aliyekuwa Mkuu wa kituo kikuu cha Polisi Jijini Mwanza(OCD)Daniel Maburuki Mahende(45) alipigwa risasi kichwani na majambazi.
Ilikuwa majira ya saa 3 usiku, Mahende na askari wake wakijaribu kufuatilia majambazi waliotaka kupora huko Bugando, akajikuta katikati ya mvua ya risasi za rashasha za majahili hao,wakamuua.
Mrakibu Msaidizi wa Polisi(ASP) Mahende, alikuwa katika doria ya kuwakabili majahili hao wanaotishia amani ya raia na mali zao, ilisadikiwa walikuwa ageni kutoka Burundi,walitumia bunduki ya rashasha,SMG  kummaliza Mahende.
Wakati huo, SMG na risasi zake vilibadilidhwa katika magulio ya mkoani Kigoma kwa debe la mahindi au mtama, amini usiamini.
Taarifa kutoka Kigoma zilisema kwamba vita huko Burundi vilifanya silaha na risasi kuuzwa magulioni,na wanunuzi wakubwa walitajwa kutokea Jijini Mwanza.Aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wakati huo, Adadi Rajabu, hakusadiki taarifa hizo zilizotolewa na watu wa mkoa wa Kigoma katika semina moja katika Hoteli ya New Mwanza.
Kulitokea majibizano ya risasi kati ya majahili hao kutoka Burundi(walikuwa Mwanza baada ya kukaribishwa na wenyeji)kati yao na polisi, ASP Mahende akapigwa risasi ya kichwa na kufariki.
Polisi waliandaa mtego wa kuwanasa majahili hao baada ya kupata taarifa kwa raia wema,kama majira ya saa tatu hivi usiku.Polisi walimuua jambazi moja na kumpora SMG iliyosheheni risasi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, wakati huo Daniel Ole Njoolay akatangaza kiama cha majambazi, kama sasa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini(DCI) Robert Manumba, anavyotangaza kiama cha majahili hao.
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Zelothe Stephen, akatangaza vita dhidi ya majambazi na wahamiaji haramu jijini Mwanza. Mwanza,kuna   wahamiaji haramu,wengine  Wabembe nao hujiita Waha kutoka Kigoma,kumbe hutoka Congo-DRC.Wengine ni    Warundi nao hujiita Waha wa Kigoma, si ulisikia baadhi yao wakitimkia porini, walipogomea sense ya watu na makazi?
Wengine Wasomali, wanahonga-honga maofisa wa uhamiaji na polisi, na kusalia mjini kuendesha ukiranga wao. Nataka kusema kwamba, Mwanza ilishaingiliwa!
Wakati huo,matukio ya uharamia yalikuwa mengi Ziwani Victoria, wizi wa shilingi milioni 90 katika Benki ya NBC,Misungwi, shilingi bilioni 2 zilizporwa wakati huo CRDB Dar es salaam, mamilioni ya fedha,kama milioni 200 ziliporwa katika kiwanda cha bia, Pasiansi Jijini Mwanza na   cashier akafumuliwa kichwa kwa risasi. Kesi yake,bila shaka iliharibiwa baada ya ushahidi kukosekana kuwatia hatiani waliotuhumiwa!
Jijini Mwanza pia ziliporwa milioni 12 katika kiwanda cha samaki cha Omega,Ilemela,Jijini Mwanza.Wakati huo migodi mingi ilivamiwa,Geita,Nyamongo,mabasi yalitekwa Ngara, Geita,Kahama,Kibondo,Sirari n.k
Siku moja kabla ya kifo cha Hayati Liberatus Barlow, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP),nilimuuliza SSP Lily Matola,wakati wa mkutano wa kawaida na wanahabari:
“Umesema leo(Ijumaa 12)hakuna taarifa za uhalifu mkoani Mwanza. Jambo hili lina weza kuwa na maana mbili tofauti: Kwamba,Polisi wanafanya kazi zao vizuri sana,hadi uhalifu na wahalifu wametokomezwa? Au, raia wema wamekosa kuliamini jeshi la polisi,hata wameshindwa kulisaidia kuwabaini wahalifu,na sasa majahili hao wameachwa watambe?”
SSP Lily Matola, akitabasamu tabasamu tamu kama asali, akanijibu hivi:
“Swali ni zuri na muhimu, ila hatuwakatishi tamaa raia wema wanaotaka kutoa taarifa za wahalifu,tunategemea taarifa za raia wema ili tushirikiane kutokomeza majambazi na wahalifu”, SSP Matola alisema.
 Ni ukweli usiofichika kwamba, Hayati Liberatus Barlow alikuwa mwiba mchungu kwa wahalifu, baadhi yao waliuliwa kwa risasi na polisi,na wengine ni ndege wa jela.
Barlow, alifika Mwanza takriban mwaka mmoja unusu uliopita. Ilikuwa baada ya ACP  Simon Nyankoro Sirro kuhamishiwa Dar es salaam,Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, anakoshikilia wajibu mtukufu.
Sirro, aliwahi kujipenyeza katika biashara haramu ya viungo vya binadamu,hususan walemavu wa ngozi, Albino, raia mmoja wa Kenya,Nathan Mtei(28) akajikuta akiishia mikononi mwa polisi,katika nyumba ya kulala wageni.
 Ilikuwa Agosti 15 mwaka 2010, Nathan Mtei alimhadaa Robinson Mkwana mlemavu wa ngozi naye raia wa Kenya,kuja jijini Mwanza,kwamba angemtafutia kazi ya utingo katika malori,kumbe kuuza viungo vyake.
Polisi walinasa mazunguzo yao na wafanyabiashara hao haramu, wakamhadaa Mtei ili amlete Mkwana akiwa mzima,ili wao ‘washughulike naye’. Walikubaliana kwamba Mtei angelipwa milioni 400. Basi Polisi wa Kamanda Sirro, wakamfuata Mkwana katika nyumba moja ya wageni, Nyakato,Jijini Mwanza walikofikia.
Nathan Mtei alipofungua mlango wa chumba walimofikia na albino Robinson Mkwana, polisi walijitoma ndani wakiwa na silaha mkononi!
Mtei alitekewa, akafungwa pingu.Albino, Robinson Mkwana akashangaa, polisi wakamwambia kwamba huyo Mtei hakuwa rafiki bali jambazi aliyetaka kumuua ili wamnyofoe viungo kwa milioni 400 ambazo polisi walifika nazo mahali hapo.
“Aliniambia tujenaye TZ angenitafutia kazi kwa Truck…”Robinson Mkwana alisema,wakati polisi walipowatia mbaroni.
Mauaji ya RPC,Barlow hapa jijini Mwanza ni kitisho kwa wananchi wa kawaida. “Sasa, kama RPC anauliwa namna hii, sisi raia wa kawaida tutapona?” mama mmoja anasikika akisema.
Mwanza ni miongoni mwa maeneo yenye kuwavutia wahalifu,ni mkoa ambao una rekodi ya juu ya kumiliki silaha kinyume cha sheria. Mikoa mingine ni Kigoma,Kagera,Geita,Arusha,Dar es salaam,Rukwa,Iringa na Mbeya.
Mwaka 2000 debe moja la mahindi ama mtama liliweza kubadilishwa kwa SMG ama debe la risasi katika magulio ama minada ya wananchi huko Kigoma.Wakati huo Tanzania ilikuwa na wakimbizi 500,000 ambao sasa wamerejeshwa kwao.Walikuja na bunduki.
Ukiacha Mwanza kuwa na watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria, na wauaji wa albino na wafanya biashara hiyo haramu kutoka hata Kenya,Mwanza hamkani si shwari.
Niliwahi kumuuliza ACP  Simon Sirro, “Kwanini Mwanza,silaha zinazofanya uhalifu hazikamatwi?”
“Wanaficha hata Sirari au Nzega. Huwezi kuamini,tulimfuatilia jambazi mmoja tukamkamata akatupeleka Nzega ambako walikuwa wameficha SMG ardhini. Hiyo SMG ilikuwa ikitumika kufanya uhalifu Kanda nzima ya Ziwa”, alisema Simon Sirro Nyankoro.
Majangili wa Kisomali waliwahi kumuua OCD huko Ngorongoro, eneo ambalo sasa lipo mkoa wa Manyara.
 Mauaji ya Barlow, Mwanza yanazungumzwa kuhusishwa pengine na wivu wa kimapenzi,lakini walimu wa shule ya Nyamagana B wanakanusha Barlow kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwalimu mwenzao, Doroth Moses.
Doroth Moses, anashikiliwa na polisi kwa mahojiano, kwa kuwa ndiye mwanamke aliyekuwa akisindikizwa nyumbani kwake, usiku huo na Barlow. Doroth anaishi huko Kitangiri ambako ni eneo tukio la kumuua Kamanda Barlow lilitokea.
Mwili wa Barlow, uliagwa katika uwanja wa Nyamagana, Jumatatu iliyopita, ukasafirishwa kwa ndege hadi Dar es salaam ilikokuwa familia yake.
Tayari ACP Barlow amezikwa kwao mkoani Kilimanjaro, wakati Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(DCI)Robert Manumba, angali anaongoza Kikosi cha    makachero wa polisi,ili kuwabaini wahusika wa tukio hili la kinyama.
Makala hii itaendelea


KUZIMU KUNA NJAA YA BARLOW!!

SAFARI YA BARLOW KUELEKEA KUZIMU

Mkuu wa Mkoa anapomsikitikia Barlow

Evarist Ndikilo: Nakulilia Barlow,ooh..

Makachero kuwasaka waliomuua Barlow

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini(DCI)Robert Manumba(wa pili toka kulia,Mwanza juzi

Kamanda Barlow

jeneza la Kamanda

Barlow umetuacha

Watu wakifuatilia kwa makini kuaga mwili wa Barlow Mwanza

SPECIAL BARLOW ASSASSINATION IN MWANZA

Mwili wa Barlow

Siri za kifo cha Barlow zitapatikana hapa

hayati Liberatus Barlow

THE LATE ACP BARLOW

Simon Nyankoro Sirro(kushoto) akiwa na   Marehemu Barlow

Siri za kifo cha Liberatus Barlow




IJUMAA,Oktoba 12 mwaka huu,yaani siku moja kabla ya mauaji ya kinyama dhidi ya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Liberatus Barlow(55), Mrakibu Mwandamizi wa Polisi(SSP) Lily Matola, anawaambia waandishi wa Habari:
“Kesho Jumamosi(Oktoba 13) Kamanda,Liberatus Barlow) anataka kuzungumza nanyi kitu nyeti”, SSP Liliy Matola, anasema.
“Unajua, yeye anakawaida ya kushiriki Doria yeye binafsi bila kuhusisha askari; ana cha kuwaambia, baadhi yenu ana namba zenu za simu, atawajulisha muda wa kukutana naye,lakini ni kama saa tano hivi asubuhi”, anasema SSP Matola,Ofisa Mnadhimu wa Polisi(Staff One) Mwanza.
Asubuhi, siku ya Jumamosi, zikasikika habari kuwa Barlow alikuwa kauliwa na majambazi,katika eneo la jirani na Hoteli ya Tai Five, karibu na Kona ya Bwiru,Kitangiri,Jijini Mwanza.
Nilikutana na ACP Liberatus Barlow(55) mara ya mwisho Oktoba 19,siku ya Jumatano mwaka huu. Ilikuwa takriban saa 50 kabla ya mauti kumkumba.Alikuwa ndani ya sare zake za kipolisi na kofia kichwani.
Ilikuwa saa saba hivi mchana, akiwa nje ya jingo la ofisi yake.Alikuwa akiwaambia wanahabari juu ya tukio la kukamatwa vibaka watatu waliojaribu kupora maberamu ya mafuta katika matangi ya Kampuni ya ENGEN, Igogo,Jijini Mwanza.
Naam, Kamanda Barlow ameuawa na watu wanaosadikiwa majambazi,huko Kitangiri,jijini Mwanza,majira ya kati ya saa saba na saa nane za usiku, alipokuwa akitokea kumsindikiza Doroth Moses, ambaye ni Mwalimu katika shule ya Msingi ya Nyamagana B,mara baada ya kikao cha watu wa mkoa wa Kilimanjaro.
Baada ya kupata  habari za kifo cha Barlow, mara nakumbuka kauli ya SSP Lily Matola:
“Kesho, Jumamosi waandishi mje hapa ofisini Kamanda Barlow anawahitaji,atakuwa na jambo muhimu kuwapasheni habari wananchi”.SSP Lilian Matola, alikuwa akisema kwa utulivu mkubwa,kama ilivyo kawaida yake,huku akitoa tabasamu tamu la asali.
Sijui,Kamanda Barlow aliwaalika waandishi lufika ofisini kwake Jumamosi hiyo kufanya ‘coverage’ ya kitu gani? Labda, alitabiri kitakachomkuta?!
Sikufika ofisini kwa Kamanda asubuhi hiyo ya Jumamosi,kwa kuwa nilikuwa nikihudhuria Ibada, kanisani Kirumba.Napenda kumwabudu Mungu.
Mkurugenzi wa kituo cha televisheni cha Barmedas cha jijini Mwanza na Meneja wa Kituo, Charles Sokoro, walinigutua kusema kanisani hapo kwamba,Kamanda Barlow alikuwa kauliwa na majambazi usiku wa kuamkia hiyo Jumamosi!
Hili siyo tukio la kwanza la majambazi kuwaua maofisa wa ngazi za juu wa   Polisi jijini Mwanza. Jiji la Mwanza linao raia wema na pia wapo majambazi,mashetani hayawani na majahili waliozowea kupokonya maisha ya watu kwa kuwamwagia tindikali,kuwaua kwa risasi na sumu.
Julai 28,mwaka 2003, aliyekuwa Mkuu wa kituo kikuu cha Polisi Jijini Mwanza(OCD)Daniel Maburuki Mahende(45) alipigwa risasi kichwani na majambazi.
Ilikuwa majira ya saa 3 usiku, Mahende na askari wake wakijaribu kufuatilia majambazi waliotaka kupora huko Bugando, akajikuta katikati ya mvua ya risasi za rashasha za majahili hao,wakamuua.
Mrakibu Msaidizi wa Polisi(ASP) Mahende, alikuwa katika doria ya kuwakabili majahili hao wanaotishia amani ya raia na mali zao, ilisadikiwa walikuwa ageni kutoka Burundi,walitumia bunduki ya rashasha,SMG  kummaliza Mahende.
Wakati huo, SMG na risasi zake vilibadilidhwa katika magulio ya mkoani Kigoma kwa debe la mahindi au mtama, amini usiamini.
Taarifa kutoka Kigoma zilisema kwamba vita huko Burundi vilifanya silaha na risasi kuuzwa magulioni,na wanunuzi wakubwa walitajwa kutokea Jijini Mwanza.Aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wakati huo, Adadi Rajabu, hakusadiki taarifa hizo zilizotolewa na watu wa mkoa wa Kigoma katika semina moja katika Hoteli ya New Mwanza.
Kulitokea majibizano ya risasi kati ya majahili hao kutoka Burundi(walikuwa Mwanza baada ya kukaribishwa na wenyeji)kati yao na polisi, ASP Mahende akapigwa risasi ya kichwa na kufariki.
Polisi waliandaa mtego wa kuwanasa majahili hao baada ya kupata taarifa kwa raia wema,kama majira ya saa tatu hivi usiku.Polisi walimuua jambazi moja na kumpora SMG iliyosheheni risasi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, wakati huo Daniel Ole Njoolay akatangaza kiama cha majambazi, kama sasa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini(DCI) Robert Manumba, anavyotangaza kiama cha majahili hao.
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Zelothe Stephen, akatangaza vita dhidi ya majambazi na wahamiaji haramu jijini Mwanza. Mwanza,kuna   wahamiaji haramu,wengine  Wabembe nao hujiita Waha kutoka Kigoma,kumbe hutoka Congo-DRC.Wengine ni    Warundi nao hujiita Waha wa Kigoma, si ulisikia baadhi yao wakitimkia porini, walipogomea sense ya watu na makazi?
Wengine Wasomali, wanahonga-honga maofisa wa uhamiaji na polisi, na kusalia mjini kuendesha ukiranga wao. Nataka kusema kwamba, Mwanza ilishaingiliwa!
Wakati huo,matukio ya uharamia yalikuwa mengi Ziwani Victoria, wizi wa shilingi milioni 90 katika Benki ya NBC,Misungwi, shilingi bilioni 2 zilizporwa wakati huo CRDB Dar es salaam, mamilioni ya fedha,kama milioni 200 ziliporwa katika kiwanda cha bia, Pasiansi Jijini Mwanza na   cashier akafumuliwa kichwa kwa risasi. Kesi yake,bila shaka iliharibiwa baada ya ushahidi kukosekana kuwatia hatiani waliotuhumiwa!
Jijini Mwanza pia ziliporwa milioni 12 katika kiwanda cha samaki cha Omega,Ilemela,Jijini Mwanza.Wakati huo migodi mingi ilivamiwa,Geita,Nyamongo,mabasi yalitekwa Ngara, Geita,Kahama,Kibondo,Sirari n.k
Siku moja kabla ya kifo cha Hayati Liberatus Barlow, ambaye alikuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP),nilimuuliza SSP Lily Matola,wakati wa mkutano wa kawaida na wanahabari:
“Umesema leo(Ijumaa 12)hakuna taarifa za uhalifu mkoani Mwanza. Jambo hili lina weza kuwa na maana mbili tofauti: Kwamba,Polisi wanafanya kazi zao vizuri sana,hadi uhalifu na wahalifu wametokomezwa? Au, raia wema wamekosa kuliamini jeshi la polisi,hata wameshindwa kulisaidia kuwabaini wahalifu,na sasa majahili hao wameachwa watambe?”
SSP Lily Matola, akitabasamu tabasamu tamu kama asali, akanijibu hivi:
“Swali ni zuri na muhimu, ila hatuwakatishi tamaa raia wema wanaotaka kutoa taarifa za wahalifu,tunategemea taarifa za raia wema ili tushirikiane kutokomeza majambazi na wahalifu”, SSP Matola alisema.
 Ni ukweli usiofichika kwamba, Hayati Liberatus Barlow alikuwa mwiba mchungu kwa wahalifu, baadhi yao waliuliwa kwa risasi na polisi,na wengine ni ndege wa jela.
Barlow, alifika Mwanza takriban mwaka mmoja unusu uliopita. Ilikuwa baada ya ACP  Simon Nyankoro Sirro kuhamishiwa Dar es salaam,Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, anakoshikilia wajibu mtukufu.
Sirro, aliwahi kujipenyeza katika biashara haramu ya viungo vya binadamu,hususan walemavu wa ngozi, Albino, raia mmoja wa Kenya,Nathan Mtei(28) akajikuta akiishia mikononi mwa polisi,katika nyumba ya kulala wageni.
 Ilikuwa Agosti 15 mwaka 2010, Nathan Mtei alimhadaa Robinson Mkwana mlemavu wa ngozi naye raia wa Kenya,kuja jijini Mwanza,kwamba angemtafutia kazi ya utingo katika malori,kumbe kuuza viungo vyake.
Polisi walinasa mazunguzo yao na wafanyabiashara hao haramu, wakamhadaa Mtei ili amlete Mkwana akiwa mzima,ili wao ‘washughulike naye’. Walikubaliana kwamba Mtei angelipwa milioni 400. Basi Polisi wa Kamanda Sirro, wakamfuata Mkwana katika nyumba moja ya wageni, Nyakato,Jijini Mwanza walikofikia.
Nathan Mtei alipofungua mlango wa chumba walimofikia na albino Robinson Mkwana, polisi walijitoma ndani wakiwa na silaha mkononi!
Mtei alitekewa, akafungwa pingu.Albino, Robinson Mkwana akashangaa, polisi wakamwambia kwamba huyo Mtei hakuwa rafiki bali jambazi aliyetaka kumuua ili wamnyofoe viungo kwa milioni 400 ambazo polisi walifika nazo mahali hapo.
“Aliniambia tujenaye TZ angenitafutia kazi kwa Truck…”Robinson Mkwana alisema,wakati polisi walipowatia mbaroni.
Mauaji ya RPC,Barlow hapa jijini Mwanza ni kitisho kwa wananchi wa kawaida. “Sasa, kama RPC anauliwa namna hii, sisi raia wa kawaida tutapona?” mama mmoja anasikika akisema.
Mwanza ni miongoni mwa maeneo yenye kuwavutia wahalifu,ni mkoa ambao una rekodi ya juu ya kumiliki silaha kinyume cha sheria. Mikoa mingine ni Kigoma,Kagera,Geita,Arusha,Dar es salaam,Rukwa,Iringa na Mbeya.
Mwaka 2000 debe moja la mahindi ama mtama liliweza kubadilishwa kwa SMG ama debe la risasi katika magulio ama minada ya wananchi huko Kigoma.Wakati huo Tanzania ilikuwa na wakimbizi 500,000 ambao sasa wamerejeshwa kwao.Walikuja na bunduki.
Ukiacha Mwanza kuwa na watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria, na wauaji wa albino na wafanya biashara hiyo haramu kutoka hata Kenya,Mwanza hamkani si shwari.
Niliwahi kumuuliza ACP  Simon Sirro, “Kwanini Mwanza,silaha zinazofanya uhalifu hazikamatwi?”
“Wanaficha hata Sirari au Nzega. Huwezi kuamini,tulimfuatilia jambazi mmoja tukamkamata akatupeleka Nzega ambako walikuwa wameficha SMG ardhini. Hiyo SMG ilikuwa ikitumika kufanya uhalifu Kanda nzima ya Ziwa”, alisema Simon Sirro Nyankoro.
Majangili wa Kisomali waliwahi kumuua OCD huko Ngorongoro, eneo ambalo sasa lipo mkoa wa Manyara.
 Mauaji ya Barlow, Mwanza yanazungumzwa kuhusishwa pengine na wivu wa kimapenzi,lakini walimu wa shule ya Nyamagana B wanakanusha Barlow kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwalimu mwenzao, Doroth Moses.
Doroth Moses, anashikiliwa na polisi kwa mahojiano, kwa kuwa ndiye mwanamke aliyekuwa akisindikizwa nyumbani kwake, usiku huo na Barlow. Doroth anaishi huko Kitangiri ambako ni eneo tukio la kumuua Kamanda Barlow lilitokea.
Mwili wa Barlow, uliagwa katika uwanja wa Nyamagana, Jumatatu iliyopita, ukasafirishwa kwa ndege hadi Dar es salaam ilikokuwa familia yake.
Tayari ACP Barlow amezikwa kwao mkoani Kilimanjaro, wakati Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai(DCI)Robert Manumba, angali anaongoza Kikosi cha    makachero wa polisi,ili kuwabaini wahusika wa tukio hili la kinyama.
Makala hii itaendelea