Wednesday, August 29, 2012

New Orleans, LA, USA
HUYU NDIYE MALKIA CLEOPATRA WA MISRI,alitumia ngono kama silaha ya kuwanasa wanume dhaifi wa ngono
CLEOPATRA
CLEOPATRA
hurricane Mitch,
MTU AKIWA KATIKA PAA AKISUBIRI WOKOVU
HURRICANE ISAAC

KATRINA

NEW ORLEANS WAKATI WA KATRINA,AGOSTI MWAKA 2005

LEO NI JANA YA KESHO(3)

  MIAKA SABA KAMILI iliyopita,Kimbunga Katrina(unaweza kuita Catherine au Katarina),kiliyakumba maeneo ya Pwani ya Ghuba yenye utajiri wa nishati,nchini Marekani.
Ilikuwa Jumapili,Alasiri majira ya saa 10. Ilikuwa siku ya Agosti 28. Mamlaka ya Hali ya Hewa(National Weather Services) ikaonya raia wan chi hiyo juu ya janga la Kimbunga Katrina kuvuruga eneo hilo,hususan New Orleans.
Agosti 30; saa 7:30 usiku, tayari maji ya Ziwa yakisombwa na kimbunga kikali,yalishavuka kingo na kuingia mitaani, ambako yaligharikisha watu.
Barabara Kuu ya London(London Avenue) hapo New Orleans, zilipokuwa kingo zenye kimo cha futi 300 zikagharikishwa na mawimbi yenye kubeba maji,yaliacha makazi yake ya kawaida na kuhamia mjini.
Miundombinu kama umeme ikaharibiwa vibaya,kukawa kiza totolo. Mawimbi ya maji yenye kina cha futi hadi 10 yakagharikisha mji, wakazi wengi wakakwea katika mapaa ya nyumba zao ili kujiokoa,wakisubiri msaada.
Msomaji, piga picha ya Gharika ya Nuhu mwaka wa BC 4000,kasha tazama kilichotokea miaka saba kamili iliyopita huko New Orleans.
Ilikuwa Agosti 28 hadi 30, mwaka 2005.
Katrina, iliwafanya raia 25,000 wa New Orleans kuwa wakimbizi katika mji wao wenyewe,wakalazimika kukwea katika mapaa ya nyumba zao,kusubiri uokozi.Maji yenye kimo cha futi hadi 10 yalikuwa yakiotea maisha yao.
Hiki ni kiama cha Katrina ama ‘Katarina’. Jumanne, Agosti 28 mwaka huu, Historia ikajirudia wakati na mahali pale pale, safari hii wanakabiliwa na kimbunga Isaac.
Nataka kukwambia msomaji,zamani vimbunga vikibatizwa majina ya akina mama, Hellen, Katrina,Katarina,Mitch n.k. Akina mama wa Haki za Wanawake wakaja juu sana,kusema kwanini majanga yanabatizwa majina ya wanawake?
Ndiposa, utasikia kuna Hurricane Isaac, Robert, Andrew ,Charles n.k
Sasa huko Louisiana na New Orleans, tunasikia kuna Kimbunga Isaka. Hili ni eneo la njia ya tufani na vimbunga,eneo la Kusini na Mashariki mwa Marekani.
Ni eneo lenye mito mikubwa duniani,kama Mississippi, ambao ni wa kwanza kwa ukubwa hapa Duniani. Unafuatiwa na Nile,unaoanzia Owen Falls, Jinja nchini Uganda, unasafiri kilomita 6,900 hivi hadi Misri.
Naam,kufuatia Katrina,visiwa jirani na New Orleans vilizama penye kinamansi.Maeneo oevu ya ya Ghuba hii ya Pwani ya Marekani,yakazamishwa na kina cha maji cha futi 30 hivi.
Mto Mississippi, ukatapika maji, na Ziwa Pontchartrain,Kaskazini mwa mji likamwaga gharika mjini. New Orleans uko chini ya usawa wa Bahari.
Tufani ama kimbunga chenye kasi ya maili hadi 165 kwa saa,hadi kufika Agosti 31 mwaka huo 2005 kilishabeba mawimbi ya maji yenye futi hadi 29,mji ukazamishwa,uchumi na biashara vikatiwa kiharusi.
Bidhaa zikapanda bei kupindukia. Paketi ya sigara iliuzwa sasa kwa Dola 10(sawa na shilingi 16,000 za Tanzania),magereza yakasombwa na maji,malango yakafunguka,wafungwa na mahabusu wakajiendea zao.
Wahalifu walianza kutamba mitaani. Sasa,kama maofisi ya serikali,polisi na mahakama yaligharikishwa maji,mafaili yakasombwa na mafuriko,hata kama ukikutana na kibaka au jambazi aliyetoroka jela,ungemkamata tena ili ukamshitaki kwa ushahidi upi,midhali vielelezo vilishasombwa na mafuriko?
Wahalifu walipotoroka gerezani, wakasomba silaha zilizoachwa nyuma na skari, wakaanza kufanya vitu vyao! Askari na raia wote walitoroka.
Nataka nikwambie msomaji.
Serikali ya Rais George W.Bush ililaumiwa sana kwa kushindwa kuokoa maisha ya Watu Weusi wengi. Helkopta za uokozi zilipofika eneo lile zikawatupia kamba Wazungu kwanza,Weusi masikini wakaachwa!
Mji wenye wakazi 500,000 zoezi la uokozi likafanywa kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, ambao hata sasa ungalipo.Waliuanza akina Adolf Hitler, wakaja makaburu wa Afrika ya Kusini,hata sasa akina Samuel Eto’o Fils wanaushuhudia huko Ulaya,na Olimpiki huko London kulikuwepo hali hiyo.
Uhalifu ulikuwa mkubwa,magenge ya wakora yakanyatia polisi na kuwapokonya silaha,bunduki na vilipuzi.Polisi nao waliasi kazi yao wakaanza kupora kilichoachwa na Katrina-wengine walikwenda kuangalia majumba yao na familia zao. Kumbe, wewe siku ya kiama utakumbuka kazi?
Nimesema,wafungwa magerezani walitoroka wakaingia mjini,mafaili na vielelezo vya ushahidi vilishasombwa na maji.
Makao Makuu ya Jeshi la Marekani(The Pentagon) yalikuwa chini ya Ronald Rumsfeld wakati huo.
Yakalaumiwa kwa uzembe wa kushindwa kuokoa watu na mali zao.
Huko Marekani, unapotaja,” Hollywood” unazungumsa burudani; ukisema Wall Street unasema Pesa, sasa ukisema eneo lililokumbwa na Katrina, maana yake ni mahali inapopatikana nishati.
Katrina,ilileta kiharusi kwa uchumi wa Marekani.Takriban asilimia 60 ya mafuta yanayoingizwa Marekani,huingilia maeneo haya ya Ghuba ya Marekani.
Viwanda vya kusafisha mafuta viko huko,uchumi wa taifa hilo ukatikiswa Agosti 28-31 mwaka 2005.
Niandikapo hapa,leo ni Agosti 29,miaka saba kamili baada ya Katrina. Leo katika eneo hilo,tarehe kama ya mwaka huo, kimbunga kingine sasa kilichobatizwa jina la mwanaume, Isaka, kinalikumba eneo hilo!
Agosti 28-31 kimbunga Katrina kikalikumba eneo hilo, leo tarehe hizo hizo,kimbunga Isaac kinarejea nyuma kupitia njia yake.
Nataka kusema kwamba, Historia inakawaida ya kujirudia-rudia.Yaliyotokea zamani, siku huenda na kupita,hujirudia tena, nataka tujifunze Historia.
Nimerejea jambo hili,ili msomaji wangu abaini kwamba mambo ya usoni yalishatokea huko nyuma.Hata wanasiasa ghiliba tupu walishakuwepo huko nyuma, yaliyowapata,yalitokea kutufundisha sisi wa sasa.
Ndiyo maana kichwa cha makala haya hiutwa, “LEO NI JANA YA KESHO!”.Hakuna jambo jipya hapa duniani. Suruwali za kubana zilikuwepo zamani, vijana wakora walikuwepo,tabia mbaya ya kutoheshimu serikali na mamlaka ilikuwepo tangu zama za Kaini!
Kaini, ndiye mwanzilishi wa wakora na magangwe.Biblia,katika kitabu cha Kohelethi au Mhubiri husema kwamba:
Pepo huyarudia mazunguko yake na mito hurejea inakotoka; wala hakuna jambo jipya chini yajua”, Mhubiri 1:6-10.
Huyu Mhubiri, ambaye ni Mfalme Suleiman mwana wa Mfalme Daudi wa Yese,(Tazama Mhubiri 1:12),aliishi kati ya mwaka 965-926 BC.
Msomaji mmoja ananiandikia kwamba nirahisishe lugha ili wasome watu wa kawaida pia.
Hata hivyo, hiyo miaka ya Kabla ya Kristo(Before Chris) inapungua na AD inaongezeka. Tujifunze historia.
Kiwango cha elimu cha huyu mtu aitwaye Suleiman, au nimwite Prof. Solomon, kilikuwa cha juu sana, Falsafa yake ni kwamba mambo mengi hapa duniani hujirudia rudia sana,yalikuwepo na yatakuwepo,ndiyo maana Leo ni jana ya kesho!
Tawala katili sana leo duniani,zilishakuwepo hapo zamani sana,zikatoweka zitakuja nyingine na kutoweka kama upepo.
Walikuwepo akina Julius Caesar,Augustus(27BC-14 AD),Caligula(AD 37-41), hata watu wakawaabudu kama miungu, akina Tiberius, wakati ule wa sensa, wakati Yesu anazaliwa.
Sensa ipo hata sasa, na watu wanasusa kwamba ni kinyume cha dini! Hata Yesu alihesabiwa, maana Mariam mamaye alihesabiwa akiwa mjamzito wa kujifungua.
Tiberius alikusanya kodi kubwa Rome hadi kufikia kama dola za Marekani1,700,000 katika mji mmoja.
Walikuwepo akina Kaisari Nero waliowakata vichwa mitume wa Yesu, watakuwepo wengine wakatili kama hao. Gidion M. anatwambia jambo hili kwa kina.
Mathayo alichunwa ngozi akiwa hai, Thomas alichomwa mkuki huko India, Marko alifia Ethiopia, Mathayo alifia Alexandria,Misri,Luka akafia Ugiriki, Yohana alichemshwa katika pipa la mafuta,Petro alisulubiwa kichwa chini-miguu juu! Hapa ni mjini Rome.Yakobo alifia mjini Yerusalem n.k
Wamekuwepo hapa duniani akina Farao,Nebchadnezzar, akina Malkia Cleopatra wa Misri.Hata sasa kuna hadithi za kuhusu huyu mwanamama mrembo sana labda kuliko wote duniani.
Historia inasema Malkia Cleopatra aliwachanganya wanaume wawili wakuu sana-Julius Caesar na Marc Anthony.Alitumia udhaifu wa ngono wa wanaume kuwamaliza,halafu yeye akajiimarisha madarakani.
Kuhusu ngono, akina baba wenye misuli na maarifa katika medani ya vita kama Julius Caesar, ni dhaifu kwa wanawake- Strongest But Weak!
Cleopatra alikufa mwaka wa BC 30,hakuacha hata maandishi yake. Cleopatra, “The Last Queen of Egypt” ilidhaniwa kifo chake kingekuwa mwisho wa Misri?
Hata leo, wametoka akina Gamal, akina Hosni Mubarak wako kolokoloni wakiwa mahututi,lakini akina Mohamed Mursi, wapo!
Watu hutoweka na wengine huja-hakuna mtu wa kudhaniwa mungu hapa duniani.
Cleopatra, alitumia mwili wake kwa ghiliba ya ngono,kama silaha mithili ya misaili.
Hata leo wapo akina Joyce Banda,leo ni kama jana.Wamekuja akina Joyce BANDA wanatumiwa na madola makubwa kwa kisingizio cha demokrasia. Wameruhusu ushoga, sasa wanataka kuchukua ziwa Nyasa lote ili makampuni ya Marekani,Uingereza na Ufaransa wachote mafuta na gesi humo. Watu kama yeye wamekuwepo zamani!
Namwonya Rais Jakaya Kikwete, asiwasikilize sana hawa wakoloni,ni laghai na wasaliti, wanajifanya rafiki,kumbe wafitini na wana hila.Tumkumbuke Julis Caesar eti aliuliwa sababu ya udhaifu wa hila za mwanamke.
Nawaonya wanasiasa wa Afrika. Wakiloni leo wanajidai kupromoti Demokrasia,kumbe leongo lao ni kuchochea vurugu na vita Afrika, nchi inaposalia katika miali mikali ya moto na mtutu wa bunduki,wao wachote rasilimali na kuondoka!
Shime, wanasiasa hata wa upinsani wasidhani wanatafuta haki na demokrasia,kumbe wanasababisha nchi zetu zisitawalike.Wakoloni wametoka Libya, walikowachanganya vichwa vijana wasio na ajira, wametoka Irak, sasa wako Syria baadaye watakwenda Iran.
Wanaharakati wanalipwa hela eti kuhamasisha demokrasia na haki za mashoga, wajiulize Yule wanayemtumikia kwa yakini. Harakati siyo mbaya,ujira wa kufanya hivyo wanatoa wapi?
Baadaye, watalipa nini? Haya ya njama za akina Cleopatra kwa akina Julius Caesar na Marc Athony yalishakuwepo mahali pengi duniani. Tuitazame historia.
Leo ni kama jana tu-Leo ni jana ya kesho,leo na jana havina tofauti.
TAMATI
0786 324 074






Tuesday, August 28, 2012

Musoma town ata shores of Lake Victoria
VIEW YA LAKE VICTORIA
KARIBU ROCKY CITY BWANA!

GLOBAL WARMING AND CLIMATE CHANGE IN MWANZA


          *Mabadiliko ya Tabianchi yatishia meli kuparamia miamba na kuzama
        Na Conges Mramba, Mwanza
   MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari(TPA), imewapandisha kizimbani wamiliki wa meli binafsi, kwani wanazuia Mamlaka hiyo kusimamia usalama wa abiria na mizigo, hata wakati huu wa kitisho cha magaidi wa Al-Shabaab,Afrika Mashariki.
 Mkuu wa Bandari(Port Master)Mwanza, John Mutalemwa, katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi, alisema wamiliki hao wa Bandari binafsi wanashindana na Sheria Na. 17(Tanzania Port Act) ya mwaka 2004.
Sheria hiyo inaipa TPA  nguvu ya kusimamia bandari zote, zikiwemo za watu binafsi,ili kukagua usalama wa abiria na mizigo,kabla na baada ya safari.
 “Sheria inatupa Mamlaka ya kusimamia bandari zote zikiwemo  bubu, tukague na kujua mizigo kiasi gani inasafirishwa; tunatakiwa kutazama abiria ikiwa wanalingana na uwezo wa meli au boti,kulinganisha na uwezo wa  chombo chenyewe, halafu tunatoa, “Port Clearance” kabla ya meli kuanza safari”, Mutalemwa alisema.
Kwa mujibu wa Mutalemwa, vipo vyombo vya usafiri majini,huchukua abiria na mizigo kuoita uwezo. Hii ni kazi ya TPA kufanya ukaguzi makini,ili kuondokana na Ajali Ziwa Victoria.
 “Bandari ni mpaka wa nchi. Lazima tusimamie hali ya usalama, meli inaweza kuleta Al-Qaeda ama Al-Shabaab, nap engine inaweza kuingiza nchini silaha kutoka nchi za vita na migogoro. Eti wanakataa tusiwasimamie…tumewafungulia kesi mahakamani”,Mutalemwa ameliambia gazeti hili katika mahojiano Maalum ofisini kwake juzi.
 Meli za mizigo za Jijini Mwanza, hufanya safari zake hadi Port Bell, Uganda,na Kisumu nchini Kenya, ambako sasa magaidi wa Al-Shabaab wanasaidia kuzimu kupanua kinywa chake.
 Aidha, Mkuu huyo wa Bandari Mwanza amesema nchi za Maziwa Makuu kama Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, na Burundi hazina amani, na Kenya hamkani si shwari,kufuatia kitisho cha Al-Shabaab, wanaopinga majeshi ya nchi hiyo kuingia Somalia kuwafulusha magaidi hao.
Kufuatia hali tete ya usalama nchi jirani, Mutalemwa amesema lazima Mamlaka yake kuwa macho na usalama wa abiria na mali zao dhidi ya hujuma za magaidi, wanaoweza kupata upenyo wakaingiza silaha nchini kupitia Ziwa Victoria.
  Mamlaka ya Bandari humiliki bandari za Mwanza Kaskazini na Kusini,Nansio Ukerewe,Kemondo Bay    na Musoma.
Vituo vingine vidogo vinavyomilikiwa na TPA ni Maisome,Nkome,Bukondo,Kahunda,Miharaba,Kome,Buchosa,Solima,Karumo,Chato na Nyamirembe(Kagera) na Kinesi mkoani Mara.
 Bandari ya Mwanza ni kiungo muhimu kwa nchi za Maziwa  Makuu,hususan Uganda na Kenya,na huchangia kwa kiwango kikubwa kukua kwa shughuli za uchumi,hata katika nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki(EAC).
 Ripoti ya Malka hii iliyotolewa kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu(nakala tunayo), inasema bandari ya Mwanza ingeweza kusafirisha abiria milioni moja kwa mwaka.
 Ingeweza kusafirisha tani mamilioni za  moja za mizigo,kama Reli ya Kati ingekuwa inafanya kazi kwa ufanisi. Hili ni eneo muhimu kwa ukuaji wa uchumi wan chi,lakini kinyume chake ni hasara kila upande.
 “Huduma hafifu za Reli zimesababisha shehena ya kahawa kutoka Uganda na hata Bukoba,kubadili njia(route) na kupitia Bandari ya Mombasa,Kenya “, Ripoti hii inasema.
 Kufuatia huduma duni za Shirika la Reli, Bandari za Mwanza ziko taaban,kwa sababu ya kupungukiwa mapato, zinaendeshwa bila faida.
 Kulingana na Ripoti hii kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu,katika kipindi cha miaka mitano,kuanzia 2006/2007 hadi 2010/2011, mizigo imepungua katika Bandari za Mwanza kutoka tani 480,568 hadi 248,860 mwaka 2011.
Utendaji mbovu wa lililokuwa Shirika la Reli(TRL) ulisababisha treni iliyokuwa ikisafirisha abiria na mizigo kati ya Mwanza na Bandari ya Dar es salaam kusimamishwa.Hali hii husababishwa abiria na mizigo kubadili njia na kukosesha mapato bandari za Mwanza.
 Wafanyabiashara wa Uganda wanasafirisha bidhaa zao kupitia bandari ya Mombasa,nchini Kenya.Shehena ya kahawa kutoka Uganda iliyokuwa ikipitia bandari za Mwanza, inapitia Mombasa na hivyo kupunguza kiwango cha mizigo kutoka tani 250,000 mwaka 2007 hadi tani 100,000 mwaka 2009/2010.
 Kufuatia madudu ya TRL, hata abiria wamepungua katika bandari za Mwanza kutoka abiria 891,634 mwaka 2007 hadi abiria 593,342.Huu ni upungufu wa asilimia 6.3 unaoikosesha nchi mapato na fursa za ajira kwa watu wake.
 Ripoti hiyo ya TPA, imebaini kwamba, wasafiri wa vyombo vya majini Ziwa Victoria wamepungua kufuatia ushindani uliopo wa barabara,hususan baada ya mtandao wa barabara kukamika ujenzi kwa kiwango cha lami.
 Kati ya Mwanza na Bukoba kuna usafiri wa ndege ambao huchangia pia abiria wasisafiri kwa meli.
Kufuatia hali hiyo,ripoti hiyo imebaini kuwa Kampuni ya Huduma za Meli,Marine Services Company(MSC) iko hatarini kufilisika,kufuatia meli zake kuharibika mara kwa mara,kitu kinachodaiwa na baadhi ya abiria kuwa ni hujuma za baadhi ya wafanyakazo wa MSC ili kuwanufaisha wenye meli binafsi.
  Kaimu Meneja Mkuu wa MSC, Projest Kaija, ameliambia Mwanahalisi kwamba madai hayo hayana ukweli, kwa kuwa kuhujumu kampuni unayofanyia kazi maana yake ni kuhujumu mshahara na mapato yako.
“Je, unahujumu Kampuni namna hiyo ili kampuni ikifa wewe utoe wapi mshahara?’ Kaija alihoji.
 Siku za karibuni MSC imewaondoa viongozi wa Kampuni hiyo na kuwaweka wapya ili kuboresha ufanisi na kupunguza nakisi.
 Kwa kipindi cha miaka mitano, idadi ya meli zilizohudumiwa na Bandari za Mwanza, imepungua kutoka 2,684 hadi meli 1,900 mwaka jana.
Bandari ya Mwanza pia huendeshwa kwa hasara ya mamilioni ya shilingi kila mwaka,nakisi ni takriban shilingi bilioni 4.5
Mabadiliko ya Tabianchi na Ongezeko la Joto Duniani,pia hutishia USALAMA wa usafiri Ziwani Victoria.
Kwa kipindi cha kati ya mwaka 1998 hadi 2006,maji ya Ziwa Victoria yamepungua kutoka mita 1,141.24 juu ya usawa wa bahari hadi mita 1,139.20. Upungufu ni wastani wa mita 2.04.
Kulingana na Ripoti hiyo, meli nyingi zimekuwa zikishindwa kufungwa katika bandari za Mwanza na Nansio,Ukerewe. Kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili pia huweza kusababisha kuzuka kwa miamba ambayo huhatarisha usalama wa meli na boti na usalama wa abiria,hasa wanaposafiri nyakati za usiku.
Meli zinapoparamia miamba hutoboka na kujaa maji,ama kuwa katika hatari ya kuzama.
 Ziwa Victoria ni chanzo cha Mto Nile, ambao huanzia katika Maporomoko ya Owen,Uganda; maji husafiri umbali wa zaidi ya kilomita 6,900 hadi Misri. Mvua za masika zinaponyesha Afrika ya Mashariki hubeba rutuba mezi ya Aprili na Mei na rutuba hiyo hufika Misri kati ya Agosti na Septemba na kuwawezesha Wamisri kupata rutuba jangwani.
 Mto Nile ni mungu wa Wamisri. Miungu ya Misri ina ‘mama’ yao Ziwa Victoria. Ni kwa sababu hii, mwaka 1929 na 1957 Misri walitiliana saini mkataba na Wakiloni wa Kiingereza kuzuia matumizi ya maji ya Ziwa Victoria kwa shughuli za kilimo na hata vyanzo vya umeme kama kilichopo Jinja.
 Aidha,kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili hufanya meli kutia nanga katika maji ya kina kirefu,na huku ni kuhatarisha maisha ya abiria,hasa katika maeneo ya visiwa.
 Mkuu wa Bandari ya Mwanza, John Mutalemwa anasema Mamlaka yake imelazimika kuchimba mchanga katika bandari za Mwanza ili kuongeza kina cha futi tatu ili kuwezesha meli kufunga gatini.
 Mradi kama huu unafanyiwa upembuzi yakinifu katika bandari ya Nansio,Ukerewe,lengo likiwa kujenga gati imara na salama.
Mpango wa serikali wa kuunganisha Reli kutoka Tanga hadi Musoma kupitia Arusha, utaweza kurejesha wingi wa abiria na mizigo katika Bandari za Mwanza, au abiria na mizigo ya Uganda,Rwanda,Burundi na Congo wanaweza kutozifikia kabisa bandari za Mwanza,na hivyo kuleta kifo cha mende kwa TPA na Meli za MSC.
Ziwa Victoria ni fursa muhimu kwa Tanzania katika Soko la Pamoja la EAC,lakini fursa hii inaachwa kwa wageni kupitia hujuma na ufisadi unaofanywa na maofisa wa mashirika ya umma kama TRL na MSC.
  www.congesmrambatoday.blogspot.com
    0786 324 074
 
  
 
 
Alcestis na Admetus,Mfalme wa Thesaly
ALCESTIS, anayedaiwa alikufa kwa ajili ya Admetus-hii ni hadithi ya kubuni ya Kigiriki iliyoandikwa na Euripides miaka 2,400 iliyopita
Zbigniew BrzezinskiHuyu hapa anayedaiwa kusimamia mradi wa kutengeneza Virusi vya Ukimwi,mwaka 1975

LEO NI JANA YA KESHO(2)


TUNAJADILI ikiwa yupo kiongozi mahiri wa siasa hapa duniani, anayewapenda wananchi kiasi cha kujitoa mhanga mithili ya mshumaa. 
Mshumaa,huwaangaza wengine huku ukijiteketeza wenyewe.
Mwandishi wa Kigiriki, Euripides, aliandika takriban millennia tatu zilizopita kwamba,Mfalme kijana mtanashati wa Thesaly aitwaye, Admetus aliugua.
Miungu ya Ugiriki(Ugiriki ni nchi ya masanamu ya miungu wengi) ikawaambia nduguze kuwa lazima Admetus afe, isipokuwa kama angepatikana mtu mwingine wa kufa badala yake.
Kwa Kiingereza mtu wa kufa badala ya mwingine ni “Substitute” ambaye kama angepatikana kufa badala ya Mfalme Admetus, angeweza kupona maradhi yake na kuendelea kuishi.
Wakaulizwa baba na mama yake kama walikuwa radhi kufa badala ya Admetus,wakakataa. Ndugu zake nao waliulizwa,wakakataa. Marafiki nao walisema, “Admetus, ni kijana mzuri; ni mfalme mzuri,lakini hakuna wa kufa badala yake!”
Mwisho wa siku, mkewe msichana mrembo sana aitwaye, Alcestis, akahiari kufa kwa niaba ya Admetus,kwa sababu alimpenda na alikuwa mtu mwema.
Baada ya kifo cha Alcestis, Mfalme Admetus alitambua ‘HASARA’ iliyomkuta ya kumkosa kipenzi chake, Alcestis aliyekuwa na upendo wa dhati kwake.
  Akamwombolezea ifuatavyo:
“Nitakulilia mpenzi wangu,siyo kwa mwaka mmoja au miwili;bai katika siku zote za maisha yangu,mwanamke uliyenipenda! Baba na mama walinichukia,walinipenda kwa maneno matupu,siyo kwa vitendo”, Admetus aliomboleza.
Nataka msomaji atambue kwamba, kumpenda mtu kwa maneno matupu siyo kumpenda-ni kumchukia.Upendo wa dhati siyo wa maneno matupu; ni vitendo kama alivyofanya Alcestis.
 Naam, “Love in words, not deeds” ni unafiki mtupu, siyo upendo,kama wanavyojidai siku hizi wanasiasa na wakoloni wetu wa zamani.
Nakusudia kuwaonya Waafrika wasiwe wepesi kulaghaiwa na wanasiasa na hata wakoloni wetu wa Ulaya na Marekani, kwamba wana upendo kwa wananchi-si kweli ni unafiki na ufalisayo mkubwa!
Hata hivyo,Katika Warumi 5:7   Profesa Paulo anasema, “Ni shida mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema,kama Admetus.
Biblia, katika Warumi 5:8-10, inasema, “ Lakini,Yesu Kristo alikufa kwa ajili yetu,tulipokuwa tungali “ADUI” zake.Alitupatanisha na Mungu tulipokuwa tungai adui zake”(wenye dhambi ni adui wa Mungu).
Nataka kujifunza hapa kwamba, Biblia inatwambia kwamba UPENDO ni dhidi ya adui, ambaye kwa kawaida hawezi kuwa na faida yoyote-Upendo usio na faida!
Upendo wa Alcestis kwa Admetus siyo huu usio na faida,bali ni upendo wa mke kwa mumewe, “Philos’ au Philia-upendo wa familia,upendo wa kibinadamu wa kidugu-Brotherly Love.
Baba humpenda mama,mama humpenda baba, wazazi huwapenda watoto,hata mwingine hujitoa mhanga kuwaopoa motoni.Ndugu hupendana wao kwa wao n.k
 Upendo wa mtu kumpenda adui hata kuwa radhi kufa kwa niaba yake ni Agape kwa Kigiriki, Prof. Ibrahim Lipumba, Dk.Wilbroad Slaa au Rais Jakaya Kikwete, hawawezi kuwa na upendo wa jinsi hii, wala ule wa Alcestis kwa raia.
Tuambizane ukweli.Upendo wa kweli, “TRUE LOVE” Agape au Philos ni upendo wa mtu kuumia kwa ajili ya kumpatia mema mtu mwingine. Upendo wa Agape hauna faida, “suffers long and it thinks no evil”, hata kama unamwonyesha upendo huo jambazi au adui yako!
Tujiulize:Wanasiasa wetu hawa, viongozi wa sasa wanaweza kujitoa mhanga wafe kwa ajili yetu wananchi?
Wako tayari sisi raia tuishi maisha bora kuliko wao?Wako tayari kuuza mashangingi,suti zao, briefcase zao na rasilimali zao nyingine, ili sisi wapigakura wao tuishi maisha bora?
Mtu mbumbumbu anaweza kusema kwamba jibu la maswali haya ni Ndiyo! Haidhuru. Tumjadili Mpigania Haki za Weusi wa Marekani, Martin Luther King Junior.
Kabla ya kwenda kwa mtu huyu,tujisaili: Kwanini sisi masikini hatuna shule bora kwa ajili ya elimu ya watoto wetu? Kwanini hatuna zahanati,dawa,vifaa na hatuna hospitali?
 Kwanini sisi vijijini hatuna barabara wala huduma za jamii kama umeme,maji safi na salama n.k wakati wanasiasa hawa wao wana kila kitu?Wanatembeleaje magari ya Milioni 60 wakati sisi hatuna zahanati wala dawa?
Viongozi wa dini nao siku hizi wanatembelea magari ya fahari ya zaidi ya Bilioni 2, huku waumini wao wakiwa hawana hata makubazi miguuni! Wanaimba Upendo! Mungu ni Upendoo, aaameeen! Aibu tupu!!
Yawezekana mtu “kuthubutu” kufa kwa ajili ya mtu mwema kama Admetus-huu upendo huitwa,Philosterges, kwa Kigiriki.
Lakini, kama huna nasaba na mtu,humjui, naye ni adui yako na ukahiari kufa badala yake, ndiyo AGAPE.
Wapo watu wanakesha redioni na kwenye runinga wakiimba, “Nakupenda kama nyamachoma!” Huu siyo upendo, ni tamaa za ngono(sexual drive, sexual affections, sexual love)ambazo mwisho wa ngono,hakuna chochote,bali uchungu na majuto kwa aliyedanganyika.
Kumpenda mtu usiyemjua,usiyewahi kukutana naye na hana faida kwako,ni “Impartiality Love” upendo unaoitwa Agape ama Agapao kwa Kigiriki. Huu ndiyo upendo anaopaswa kuwa nao kiongozi wa siasa-kuwapenda wananchi asiojua hata majina yao,na wanaishi pembezoni kule,Masasi ama Saragana,Masinono na Bugwema,Musoma!
Siku hizi, tunasikia kwamba kiongozi Fulani anawapenda wananchi, hadi wananchi wanakubali kupigwa virungu,kupigwa machozi ama kupigwa risasi na polisi,kwa kutii shuruti zake hata kuwapiga mawe polisi wenye SMG!
Polisi wakizuia maandamano, kiongozi wa siasa akasema, Andamaneni, watu wanatii na kupoteza maisha! Hii ndiyo Agape, watu kumfia kiongozi, siyo?
Agape, siyo watu wafe kwa ajili yako ili uende Ikulu au uukwae ubunge ama madaraka Fulani. Agape ni wewe kiongozi ufe kwa ajili ya masikini usio na nasaba nao,ili kwa kifo chako wapate faida ya kukombolewa.
Tofautisha upendo wa Alcestis,Martin Luther King Junior, Yesu na hawa jamaa. Tafakarini.
Tunajadili upendo wa dhati.Viongozi wa siasa wanaonesha upendo huu kwa wananchi? Viongozi wa kidini wanawapenda kwa dhati waumini wao? Mbona wao wanakula na kushiba, wafuasi wao ni fukara?
Kwa nini rushwa na ufisadi kama kuna upendo katika mtego uitwao siasa? Kwanini mishahara ya wabunge na wafanyakazi iongezwe maradufu,halafu mazao ya wakulima yashuke bei kwa visingizio vya kushuka kwa thamani ya shilingi au mtikisiko wa uchumi duniani?
Kwa nini hawa ambao hawajulikani kwa wanasiasa na viongozi wetu(wakulima),mazao yao yanaposhuka bei,maisha yanapokuwa duni na hawana huduma za jamii,halafu tunawachochea wafanye vurugu,wafe kwenye maandamano yaliyopigwa marufuku na polisi,badaya ya kuwasaidia waishi,wanusurike kufa?
 Tuambizane ukweli.Wanasiasa wote ni ndizi-ni rangi moja na wamepinda! Msikubali wawatumie kama ngazi, wao wanaingia kula maisha,nyie mwabaki kupigwa jua na mvua.
Acha upambe, angalia maisha yako ni ya thamani kubwa. Kwanini umpige polisi kwa mawe wakati yeye ana SMG yenye risasi 30?
Nahimiza watu kuheshimu maisha yao,nahimiza watu kuheshimu mamlaka, nahimiza usamaria wema,nahimiza utii wa sheria bila shuruti na kuheshimiana sisi kwa sisi.
 Tusikubali viongozi wa siasa kutugawa kwa misingi Fulani ili tuanze kupigana.Tukipigana wao wana mbawa,sisi tunakufa na wake na watoto wetu wanateketea wakati wao huruka kwa ndege na kwenda zao!
Vita vya wenyewe kwa wenyewe Kenya,ni mfano mzuri kwetu.Waliokufa walikuwemo watoto wa Kibaki? Hapana. Walikuwemo wa William Rutto, ama wa Raila Amolo Odinga?
Watakuwemo wa Dk.Slaa au Kikwete na wenzake? Anzisha amani, acha ujinga.
ZBIGNIEW BZEZINSKI, alikuwa Mshauri wa Usalama wa Taifa, enzi za Rais Jimmy Carter wa Marekani.
Huyu,mtu mkubwa, wa Taifa babe sana hapa duniani ambalo husemwa lina demokrasia iliyopevuka,ndiye hasa anayetuhumiwa kusimamia mradi wa kutengeneza virusi vya Ukimwi,katika maabara za kijeshi huko kilomita 75 kutoka New York, mwaka 1975.
Naam,viongozi wakubwa ni wenye ‘madudu nakubwa’.Wenye mamlaka makubwa wana madhambi makubwa sana, kinachowaokoa ni uzuzu wa wafuasi wao kueneza propaganda kwamba hao viongozi wao siyo binadamu wa kawaida,bali malaika au miungu.
Watu wadogo, hasa viongozi wa Waafrika utaona wanasemwa walifanya upumbavu huu na ule! Utaona unyama unafanywa Afrika,utadhani Ulaya na Marekani ni mbinguni!
 Martin Luther King Junior, alitiliana saini muswada wa Uhuru kwa Weusi wa Marekani,Julai 3,mwaka 1964.Mkataba huo ulikuwa kati ya Dk. Luther King na Rais Lyndon Johnson, Martin Luther aliuawa na Pentagon,Makao Makuu ya Jeshi la Marekani mwaka 1968.
Huyu, alitoa maisha yake akipigania haki za watu wake, WEUSI wa Marekani, dhidi ya ubaguzi wa rangi.
Tabia hii ingalipo Marekani, na  Ulaya. Namwonya Rais Jakaya Kikwete awe macho na Uingereza, Marekani na Ufaransa.
Siku hizi wameanza kumtumia Joyce Banda,kutaka kuleta chokochoko Maziwa Makuu,vita vinapofumuka sisi kwa sisi,wao wachote rasilimali zetu na kuondoka. Nyuma ya Joyce Banda lazima wapo hawa wameona kunaweza kuwepo mafuta ama gesi, ili tuking’amua tuache kuwategemea!
Kama alivyosema manafalsafa wa Ugiriki, Salon, sheria zilizowekwa ni ‘utando wa Buibui’. Marekani hukiuka sheria na kwenda zao pasipo kunaswa na sheria hizo. Wewe ‘mdudu’ mdogo ukicheza unanaswa.
Angalia baadhi ya wadudu wadogo walionaswa katika “Spider’s Web” ni pamoja na akina Muammar al- Qaddafi,Saddam,Osama,Charles Taylor,Laurent Gbagbo n.k
Tumjadili kidogo Charles Ghankay Taylor.Ametumwa na Marekani kufanya unyama Sierra Leone wakaja kumwacha penye mataa.
Walimtorosha wenyewe gerezani huko Boston, akakimbilia Libya, akajifunza mbinu za medani za kijeshi, akasaidiwa kupindua serikali Liberia, akaanza ‘biashara’ ya kusaidiana na Revulutionary United Front(RUF) huko Sierra Leone, wakachukua almasi na kumpa Marekani, wakapewa bunduki!
 Mwisho wa siku, Taylor amekamatwa, amefunguliwa kesi akashinda makosa yote 11, Marekani wakalazimishwa afungwe miaka 50,tena Uingereza,ili abaki kimya gerezani maishani mwake, asipate kusema siri!
BAFFOR ANKOMAH,Mhariri wa jarida mahsusi la New African la Julai mwaka huu, katika safu yake ya “Baffour’s Beefs” amesema uovu wa Marekani na mataifa babe haya(Metropolitan Powers) ambao waliwashinikiza akina Louis Moreno Ocampo na Fatou Bensouda, kumkomesha kicha maji kama Charles Taylor.
Nataka kuwaonya viongozi wa Afrika,wanaotumiwa na Marekani,Ufaransa na Uingereza,kukoma kuihujumu Afrika,la sivyo wanaelekea mahali walipo Taylor,Gbagbo, Osama, Gaddafi n.k
Marekani hawana rafiki,rafiki ni rasilimali kwa maslahi ya Marekani, siyo Afrika!
 Nawaonya pia viongozi wa vyama vya siasa hapa Afrika.Wanapewa vijisenti na silaha ili wafanye vurugu,nchi zetu zisitawalike,mwisho wa siku ni hawa Marekani,Uingereza na Ufaransa watakaofaidika na vita vya Kunguru!
Wametoka Libya,Misri,Irak,Yemen na sasa wako mbioni kuiteka Syria,wakimaliza watakwenda Iran. Qatar,Kuwait,UAE,Lebanon,Bahrain kumetulia kwa kwa sababu wamekubali ‘unono’ uende Ulaya na Marekani! Ukipinga tu,unaoneshwa mtutu wa bunduki na unapelekwa kwenye utando wa bui bui utakaokunasa.
Sisi ni wadudu wadogo,nzi-kwenye ‘spider’s web’ hatuwezi kuvuka.Tando zote za buibui kama ICC huko Hague,ni mali yao.
Sasa jidanganye kwamba Marekani na Ulaya kuna demokrasia au haki za binadamu. Wewe naye binadamu,mtu mweusi?
Kamuulize Caster Semenya, au Samuel Eto’o.
Angalia madudu ya akina Nicolas Sarkozy huko Ufaransa, amefanya ufuska,uchafu akiwa rais. Angekuwa RG Mugabe au mwingine,ungesikia maneno.Raia wangeshawishiwa kuingia barabarani na kuchoma moto magari ya serikali,majengo na matairi barabarani,kwamba ndiyo, “PEOPLES POWER”!!
Ufaransa, ‘scandal’ za akina Sarkozy za kufanyisha watoto ngono, huko Thailand na Ufaransa eti ni ‘minor thing’, lakini viongozi kama Luiz Inancio da Silva wa Barazil watasemwa hawana elimu,ni washona viatu! Hawaongei kuwa uchumi wa Brazil ulipaa wakati wa Da Silva!
Wanaona sana akina Jacob Zuma Mushorozi na Mfalme Muswati III wa Swaziland kuona vimwana kila mwaka!
 Lakini, ufuska wa akina Silvio Berlusconi huko Italia ni ‘Minor thing’! Raia hawashawishiwi kuingia barabarani na mawe na hawalipwi mishahara huko kushika bunduki,kama Syria.
Sisi ‘Madodoki’tunalishwa kila pumba na kuanza kupigana sisi kwa sisi. Hatujui mwisho wake utakuwaje? Hatutazami kesho kwa kuchungulia historia ya hawa akina Charles Taylor,Jonas Savimbi,Mobutu, Hosni Mubarak  na vibaraka wengine walivyofanyiwa.
Nataka kusema kwamba,tujiepushe na Marekani na wanasiasa wa Afrika ambao leo Marekani na washirika wake wanawalipa posho kuja kufanya vurugu Afrika,ili tupigane sisi kwa sisi,wao wachukue rasilimali.
Kumbe hata mgogoro kati yetu na Malawi haufai kuishia kuwa vita vuya silaha,tunawanufaisha hawa majahili walioanza kuchochea vita kwa kujua Ziwa Nyasa kuna mafuta au gesi!
Nawashauri Waafrika kuachana na kulishwa ‘kasumba’ ya kikoloni. Tuanze kupendana sisi kwa sisi na kutatua matatizo yetu kwa amani,bila kuwaalika majahili hawa.
 Nawaonya viongozi wa siasa hapa Afrika na wapambe wao wanaopokea posho toka Ulaya na Marekani ili wawachochee vijana kufanya vurugu kwa kisingizio cha ufisadi, na kukosa ajira!
 Fikirini vizuri. Vita vikifumuka ndiyo mtaajiriwa kwa risasi na mizinga?Ndugu zenu wakifa ama mama zenu na wadogo zenu wakiwa wakimbizi,ndiyo mtapata ajira?
 Itaendelea
0786 324 074,0754 324 074
  
                   


Monday, August 27, 2012

https://encrypted-tbn0.google.com/images?q=tbn:ANd9GcS_FKiJ5ptiUMNt8xnqf-M60J_CjaWsEF--YquXRWfO2JzqXUwRkg HUYU TAI HURUKA FUTI 10,000 ANGANI NA HUNA MBALI

TAI

tai

LEO NI JANA YA KESHO(1)


                            
TAI NI NDEGE, anayeruka juu angani, umbali wa futi 10,000 ambazo hakuna ndege mwingine aweza kufika.
Kwa sababu hiyo, ndege tai ana uwezo wa kuona mbali kiasi cha kushangaza.Aweza kuona mawindo akiwa mbali huko angani. Tunafundishwa sisi wanadamu kuona mbali mithili ya ndege huyu. Tujifunze kufikiri kuliko kusema na kusoma, lengo ni kupima faida na hasara ya kila jambo katika maisha.
Watanzania, tumefika hapa tulipo kwa sababu hatuwezi kuona mbali kwa faida yetu. Tumewaachia wafadhili na watu wengine kufikiri kwa niaba yetu-makosa makubwa. Jicho la mtu halikuoneshi wewe hatari inayokukabili.
Sasa, wasomaji wataniuliza:Wawezaje kuona mbali mithili ya ndege tai? Jibu ni rahisi. Unatazama jana ili kujua ya kesho. Unatazama historia. Historia hutuonesha kesho kuna nini?
Historia, hutuonesha kesho kutatokea nini. Historia ni muhimu katika maisha. Historia hutuambia siri za siku za usoni.
 Mwandishi wa Kiingereza, George Orwell,ambaye jina lake halisi ni Eric Arthur Blair, aliwahi kuandika hivi:
“He, who controls the past, controls the future. He who controls the future, controls the Present”
Tafsiri yangu isiyo rasmi ni kwamba George Orwell,Yule mwandishi wa kejeli(satire) ya SHAMBA LA WANYAMA, alisema hivi:
“Anayetawala Historia,hutawala pia siku za usoni; na atawalaye siku za usoni hutawala hata leo”.
Anaongeza kusema, “Today was Yesterday’s Tomorrow”-leo ni jana ya kesho!!
Ndicho kichwa cha makala haya,kutuonesha kwamba leo ni jana ya siku za usoni. Usione leo ukadhani utakuwa hivi hivi kesho,leo itapita na itakuja kesho usiyodhani. Ukitaka kujua ya kesho,tazama jana na leo-tafakari,jifunze kufikiri kwa kina.
Naam, leo ilikuwa jana ya kesho.Ninapotazama historia nawaona watu wanaorejea tabia na makosa ya jana.
Dola ya Rumi, ilipinduliwa zamani kwa sababu ya ulevi,kukosa uzalendo,rushwa,ufisadi, raia kupenda starehe na anasa, na hata leo Tanzania tunarejea yale yale tu.
Watu wanafanya makosa yaliyowahi kutendwa katika historia, watu huchagua kufanya yale yale yaliyofanywa katika historia,na hata kesho haina tofauti kubwa. Vita vilikuwepo na hata sasa na kesho vitakuwepo,kwa sababu watu huyarejea yale yaliyotendwa katika historia.
Historia haiwarogi watu hata wayatende yale ya kale. Hatutaki kujifunza Historia,hatujui na hatujui kuwa hatujui,ndiyo maana tunafanya makosa yaliyofanywa katika historia.
 Laiti tungejifunza Historian a kubaini makosa ya wenzetu wa juzi na jana,leo tungetenda tofauti na kwa umakini na hekima.
Jumatano, Agosti 22 mwaka huu, nilikuwa nikitazama kipindi cha STRAIGHT TALK AFRICA cha Sauti ya Amerika(VOA) juu ya kifo cha Rais aliyekuwa Rais wa Ghana, John Atta-Mills.
Nilitazama kuapishwa kwa Rais Mpya, John Dramani Mahama, mahojiano kati yake na Mtayarishaji wa kipindi hicho, Dk. Shaka Ssali, kwamba anaapishwa kumalizia miezi mine iliyobaki,hadi kufikia Uchaguzi Mkuu.
 Nikamaizi kuwa, Rais Mpya wa Ghana, John Mahama, anafanana sana na wenzake waliomtangulia katika Ikulu ya mjini Accra.
Marais wote waliapa kuiongoza vema Ghana;wote waliapa kuwajali raia,kuiendeleza nchi kwa usawa na kutokuwa na upendeleo.
Naam, akina Jerry John   Rowrings ,John Kufour,John Atta=Mills, na sasa John Dramani Mahama-naam,ni Ghana na utawala wa akina John!
 Majina ni yale yale, watu walewale,kasoro ni mbwembe za kuapishwa,suti walizovaa na wapambe waliowazunguka-maisha yale yale,mambo yale yale tu,hakuna jipya.
Tujifunze kuchungulia nyuma katika historia. Wanasiasa wakubwa siyo watu wa kutegemea,kutumaini na kuegemea. Tunapaswa kuwatii,kuwaheshimu na kuwanyenyekea kwa sababu wanashikilia mamlaka ambayo ni mithili ya upanga. Lakini siyo kuwatumaini.
Mwanamuziki, Roger Whittaker, alishaimba kwamba wanasiasa ni mithili ya ndizi mbivu katika chane: Wote ni njano, wameshikilia pamoja,wanakula pamoja,wana rangi moja,lakini hakuna aliyenyooka hata mmoja!
 Nataka kuwaonya Watanzania wanaodhani wanasiasa ni “Truvada” (dawa mpya ya Ukimwi iliyovumbuliwa),kwamba watamaliza matatizo yao,wanajidanganya kuliko kawaida.
Watu wakubwa wengi wamepinda mithili ya ndizi, hawana maadili. Wakisemacho hawakitendi na wakitendacho sirini,hawakisemi. Wanapoapishwa,husema wataitii sheria na Katiba ya Nchi, mara waingiapo madarakani,hujikuta wakitenda tofauti na walivyoapa.
 Sasa, utaona watu wakivuja jasho jingi kusukuma magari yao,kutandika mavazi yao chini,ili hawa mashujaa wao, “Role Models” wapiti juu yake. Wengine wamefariki dunia kwa kukinzana na mamlaka kwa sababu hao mashujaa wao wameagiza wafe!
Maisha yako ni ya thamani kuliko ya mwenzako.
 Wanasiasa hawa watakuja na kuondoka,lakini shida zetu zitabaki ikiwa sisi wenyewe hatuwezi kukaa na kutazama namna ya kuziondoa.Wanasiasa wana kiu ya madaraka,na wala hawana nia ya kututumikia mithili ya mshumaa. Mshumaa, hujiteketeza wenyewe kwa nia ya kuwaangaza wengine. Nani mwanasiasa mshumaa?
Akiwepo kiongozi mshumaa(na hayupo) huzimika mara kunako tufani. Elton John aliimba kwamba , “Candle in Wind” mshumaa kunako upepo, wakati wa mazishi ya Princess Diana, unakumbuka?
 Naam, Candle in the Jungle! 
Mshumaa mwituni, utawaka,kunako tufani? Hata Princess Diana hajawahi kuwa mwema mithili ya mshumaa,kujiteketeza wenyewe kwa nia ya kuwaangaza wengine? Huu ni Upendo wa Agape.
 Wanasiasa hawana upendo wa Agape.
Wanaweza kuwaona raia wao mithili ya familia zao ama watoto wao wa kuzaa. Huu ni upendo uitwao kwa Kigiriki, Philos,Phileo ama Philia.
Wengine wana upendo wa kitoto,Storge, na wengine wana tamaa na ashiki za kimwili,Eros ama Erao ambazo huzitumia kupora wake za raia wao na kuondoka!
Nakwambia ukweli msomaji,amini usiamini. Usiwaamini wanasiasa hata ukajitoa mhanga .Usifanywe ngazi ya kupandia ama kukwelea mamlakani,usigeuze mabega yako kubeba wanasiasa hawa-heri kubeba zege,ili upate mlo wa usiku, sembuse wanasiasa hawa?
 Watakuja na kuondoka,dhiki zetu zitabaki. Tena wengine watakuja na kupandikiza chuki na ukabila kama Kenya,watawaachia wananchi vita,umwagaji damu na visasi vya kurithi.
Mwanafalsafa wa Athens,Ugiriki,Salon anasema hivi:
“The law is like spider’s web. The small are caught ,but the great tear it up!”
Tafsiri yangu:Sheria ni mithili ya utando(mtego) wa buibui,wadogo hunaswa humo(wanyama,wadudu n.k)
Lakini, wakubwa huutatulia mbali na kujiendea zao pasipo madhara yoyote! Nataka nikwambie msomaji,watu wakubwa mnaowategemea(mnasukuma magari yao na kutandaza mashati na khanga za akina mama ili wapiti juu yake) ni wahalifu sana. Hawana maadili myoyoni mwao bali midomoni.
Wakubwa, hujidai kuwapenda raia wao. Raia wako tayari kuwafia wanasiasa wao,lakini wanasiasa ni nadra kufa kwa ajili ya raia.Wanakubali wafe kwa sababu ya tamaa ya madaraka,na aslani siyo kwa ajili ya kuwapenda raia.
Kwa wanasiasa,wanapokuwa akigombea uongozi,raia ni ngazi zao za kukwea uongozini. Pindi wanapopata madaraka,raia hugeuka shubiri,mizigo ya kuwahoji kutimiza ahadi. Raia hugeuka ‘adui’ za wenye mamlaka.
Sasa, nani alikufa kwa ajili ya adui zake. Labda tusome Warumi sura ya 5,kwamba ni Yesu aliyekufa kwa ajili ya adui zake!
 Viongozi wengi wanaponyatia madaraka,hujidai wema mithili ya mishumaa.Lakini pindi waingiapo mamlakani,hugeuka mangimeza-hutawala  kwa kutoa amri na shuruti wakiwa mezani,kuliko kusikia kilio cha wananchi.
Uadilifu hauji kwa maneno ya mdomoni,bali matendo yatokayo moyoni(Mathayo 21:23-32) hii ni kusema, “To walk the talk”.
Watu wakubwa sana duniani ni dhaifu kupindukia-Strongest but weak.
Nakusudia kuchungulia historia ya watu wakubwa duniani kama Julius Caesar, Pharao wa Misri,Malkia Cleopatra wa Misri, Kaisari Nero,  Mfalme Herode,George Washington n.k
Hawa wote walikuwa wavunja sheria,ambao kama umma ungemaizi, walistahili kukatwa vichwa kwa uhaini, lakini kwa sababu ya wapambe, walishangiliwa sana.
 Leo, nawashauri wasomaji wangu kuwaheshimu wenye mamlaka(Warumi 13) ili ujiongezee uhai. Ni upumbavu wewe mwenye mawe kujibizana na polisi wenye SMG zenye risasi za moto,ukijidai Mfalme Daudi kwa Goriathi. Usijidanganye mwanaharakati kumtupia jiwe polisi mwenye silaha.
Mwanamuziki Muhiddin Gurumo, na wenzake waliimba hivi zama za Ndekule:
“Usimkaribie chatu, ooh chatu wee; gongo usimtupie utaukosa ushindi! Natoa onyo kwa yeyote anayemchezea chatu, ni hatari, atakuja askikose lolote la manufaa na ajali imkute bila ya kutegemea, atakuja adhirika ajute na duniaaa!”
Wanasiasa ni chatu,hasa wawapo mamlakani. Ukitumwa kuwatupia gongo,ukinaswa na chatu mwenye kiu ya damu,umejitoa kafara mwenyewe.
Najua watu wajinga wapo wengi wenye kuchochea wenzao wafe ili wapige kelele nyingi kwamba Haki za Binadamu zinavunjwa. Kila mtu atazame haki yake ya uhai kwanza.
Mara nyingi,hawa wapiga domo wanaoitwa wa Haki za Mashoga, haki za akina mama, haki sijui za Binadamu,huwavisha ngozi za kondoo raia wanaopenda kukaa-kaa vijiweni saa za kazi, ili wakararuriwe na wanyama wakali!
 Nawashauri watu kuwa ‘Busy’ na mambo yao na kazi zao,tuachane na Politiki saa za kazi,maana hakuna mtawala atayekuja kutugawia sembe na maziwa kila nyumba,bila kufanya kazi
Kanali Muammar Gaddafi, alikaribia kuwagawia maziwa raia wake kila subuhi,lakini wapo waliomkana, akauzwa kwa Wamarekani, na sasa yuko Kaburini, mtoto wake,Saif al-Islam anakabiliwa na kitanzi.tazama historia ili kujua kesho.
George Orwell anawafananisha nguruwewa SHAMBA LA WANYAMA na viongozi  na unyama wao dhidi ya raia waliojidai kuwapenda sana.
Mwanafalsafa wa Ugiriki, Salon amewafananisha viongozi ho na wanyama wakubwa wanaoichanachana sheria na katiba ya nchi na kujiendea zao wanakofuata maslahi yao.
Sisi wadogo ndiyo tunaswao na sheria. Usidanganywe kuvunja sheria na watu wakubwa-utanaswa wewe wao watabaki. Utazame utando wa buibui ujifunze somo hili,wanaonaswa humo ni akina nzi,mbu,sisimizi n.k Lakini,wakubwa hujiendea na kuuchana utando huo wa bui bui. Tembo atanaswa katika  ‘spider’s web’?
Wakubwa hukiuka maadili,na kwao si hoja.Hawnaswi na mkono wa sheria,hujiendea zao salama. Usipoteze muda kuhoji jambo hilo,kafanye kazi zako, maana ni historia,,bishana nayo upoteze muda na maisha bure!
Nawe wataka kuvunja sheria za nchi?Wewe ni nzi, utanaswa katika mtedo wa buibui(sheria),katika tawala za dhuluma, sheria wamewekewa wanyonge-wewe na mimi, kutii ni njia ya kuokoa maisha,amini usiamini.
Tunisha misuli uone,kesho utakuwa mshumaa katika tufani-Candle in Wind!
Usifuate maoni ya watu wengi wajinga, Public Opinion. Jihadhari na maneno ya kijiweni. Usimtupie fimbo chatu,utajuta. Utaumia. Usiwatupie polisi mawe wakiwa na bunduki,utavuja damu puani. Usitumiwe kama kinyangarika.
Duniani,viongozi wenye upendo na raia wao wanapokuwa madarakani,siyo wengi. Kiongozi hupenda enzi na mamlaka yake kuliko raia,kuliko mke na wanaye. Sembuse wewe?
Nikupe mfano. Karibia miaka 2,500 iliyopita,Mwanafalsafa aitwaye Euripides wa Ugiriki aliandika kisa cha Admetus mfalme wa Thesaly kukabiliwa na mauti,hadi apatikane mtu wa kujitoa mhanga ili afe badala yake.
Ndugu zake,marafiki na baba na mama yake walikataa kufa kwa ajili yake. Ni msichana mzuri,mpenzi wake aliyeitwa, Alcestis aliyekubali kufa badala ya Admetus.
 Itaendelea
0786 324 074