Wednesday, August 29, 2012
LEO NI JANA YA KESHO(3)
MIAKA SABA KAMILI
iliyopita,Kimbunga Katrina(unaweza kuita Catherine au
Katarina),kiliyakumba maeneo ya Pwani ya Ghuba yenye utajiri wa
nishati,nchini Marekani.
Ilikuwa Jumapili,Alasiri
majira ya saa 10. Ilikuwa siku ya Agosti 28. Mamlaka ya Hali ya
Hewa(National Weather Services) ikaonya raia wan chi hiyo juu ya
janga la Kimbunga Katrina kuvuruga eneo hilo,hususan New Orleans.
Agosti 30; saa 7:30 usiku,
tayari maji ya Ziwa yakisombwa na kimbunga kikali,yalishavuka kingo
na kuingia mitaani, ambako yaligharikisha watu.
Barabara Kuu ya
London(London Avenue) hapo New Orleans, zilipokuwa kingo zenye kimo
cha futi 300 zikagharikishwa na mawimbi yenye kubeba maji,yaliacha
makazi yake ya kawaida na kuhamia mjini.
Miundombinu kama umeme
ikaharibiwa vibaya,kukawa kiza totolo. Mawimbi ya maji yenye kina cha
futi hadi 10 yakagharikisha mji, wakazi wengi wakakwea katika mapaa
ya nyumba zao ili kujiokoa,wakisubiri msaada.
Msomaji, piga picha ya
Gharika ya Nuhu mwaka wa BC 4000,kasha tazama kilichotokea miaka saba
kamili iliyopita huko New Orleans.
Ilikuwa Agosti 28 hadi 30,
mwaka 2005.
Katrina, iliwafanya raia
25,000 wa New Orleans kuwa wakimbizi katika mji wao
wenyewe,wakalazimika kukwea katika mapaa ya nyumba zao,kusubiri
uokozi.Maji yenye kimo cha futi hadi 10 yalikuwa yakiotea maisha yao.
Hiki ni kiama cha Katrina
ama ‘Katarina’. Jumanne, Agosti 28 mwaka huu, Historia ikajirudia
wakati na mahali pale pale, safari hii wanakabiliwa na kimbunga
Isaac.
Nataka kukwambia
msomaji,zamani vimbunga vikibatizwa majina ya akina mama, Hellen,
Katrina,Katarina,Mitch n.k. Akina mama wa Haki za Wanawake wakaja juu
sana,kusema kwanini majanga yanabatizwa majina ya wanawake?
Ndiposa, utasikia kuna
Hurricane Isaac, Robert, Andrew ,Charles n.k
Sasa huko Louisiana na New
Orleans, tunasikia kuna Kimbunga Isaka. Hili ni eneo la njia ya
tufani na vimbunga,eneo la Kusini na Mashariki mwa Marekani.
Ni eneo lenye mito mikubwa
duniani,kama Mississippi, ambao ni wa kwanza kwa ukubwa hapa Duniani.
Unafuatiwa na Nile,unaoanzia Owen Falls, Jinja nchini Uganda,
unasafiri kilomita 6,900 hivi hadi Misri.
Naam,kufuatia
Katrina,visiwa jirani na New Orleans vilizama penye kinamansi.Maeneo
oevu ya ya Ghuba hii ya Pwani ya Marekani,yakazamishwa na kina cha
maji cha futi 30 hivi.
Mto Mississippi,
ukatapika maji, na Ziwa Pontchartrain,Kaskazini mwa mji likamwaga
gharika mjini. New Orleans uko chini ya usawa wa Bahari.
Tufani ama kimbunga chenye
kasi ya maili hadi 165 kwa saa,hadi kufika Agosti 31 mwaka huo 2005
kilishabeba mawimbi ya maji yenye futi hadi 29,mji ukazamishwa,uchumi
na biashara vikatiwa kiharusi.
Bidhaa zikapanda bei
kupindukia. Paketi ya sigara iliuzwa sasa kwa Dola 10(sawa na
shilingi 16,000 za Tanzania),magereza yakasombwa na maji,malango
yakafunguka,wafungwa na mahabusu wakajiendea zao.
Wahalifu walianza kutamba
mitaani. Sasa,kama maofisi ya serikali,polisi na mahakama
yaligharikishwa maji,mafaili yakasombwa na mafuriko,hata kama
ukikutana na kibaka au jambazi aliyetoroka jela,ungemkamata tena ili
ukamshitaki kwa ushahidi upi,midhali vielelezo vilishasombwa na
mafuriko?
Wahalifu walipotoroka
gerezani, wakasomba silaha zilizoachwa nyuma na skari, wakaanza
kufanya vitu vyao! Askari na raia wote walitoroka.
Nataka nikwambie msomaji.
Serikali ya Rais George
W.Bush ililaumiwa sana kwa kushindwa kuokoa maisha ya Watu Weusi
wengi. Helkopta za uokozi zilipofika eneo lile zikawatupia kamba
Wazungu kwanza,Weusi masikini wakaachwa!
Mji wenye wakazi 500,000
zoezi la uokozi likafanywa kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, ambao
hata sasa ungalipo.Waliuanza akina Adolf Hitler, wakaja makaburu wa
Afrika ya Kusini,hata sasa akina Samuel Eto’o Fils wanaushuhudia
huko Ulaya,na Olimpiki huko London kulikuwepo hali hiyo.
Uhalifu ulikuwa
mkubwa,magenge ya wakora yakanyatia polisi na kuwapokonya
silaha,bunduki na vilipuzi.Polisi nao waliasi kazi yao wakaanza
kupora kilichoachwa na Katrina-wengine walikwenda kuangalia majumba
yao na familia zao. Kumbe, wewe siku ya kiama utakumbuka kazi?
Nimesema,wafungwa
magerezani walitoroka wakaingia mjini,mafaili na vielelezo vya
ushahidi vilishasombwa na maji.
Makao Makuu ya Jeshi la
Marekani(The Pentagon) yalikuwa chini ya Ronald Rumsfeld wakati huo.
Yakalaumiwa kwa uzembe wa
kushindwa kuokoa watu na mali zao.
Huko Marekani, unapotaja,”
Hollywood” unazungumsa burudani; ukisema Wall Street unasema Pesa,
sasa ukisema eneo lililokumbwa na Katrina, maana yake ni mahali
inapopatikana nishati.
Katrina,ilileta kiharusi
kwa uchumi wa Marekani.Takriban asilimia 60 ya mafuta yanayoingizwa
Marekani,huingilia maeneo haya ya Ghuba ya Marekani.
Viwanda vya kusafisha
mafuta viko huko,uchumi wa taifa hilo ukatikiswa Agosti 28-31 mwaka
2005.
Niandikapo hapa,leo ni
Agosti 29,miaka saba kamili baada ya Katrina. Leo katika eneo
hilo,tarehe kama ya mwaka huo, kimbunga kingine sasa kilichobatizwa
jina la mwanaume, Isaka, kinalikumba eneo hilo!
Agosti 28-31 kimbunga
Katrina kikalikumba eneo hilo, leo tarehe hizo hizo,kimbunga Isaac
kinarejea nyuma kupitia njia yake.
Nataka kusema kwamba,
Historia inakawaida ya kujirudia-rudia.Yaliyotokea zamani, siku
huenda na kupita,hujirudia tena, nataka tujifunze Historia.
Nimerejea jambo hili,ili
msomaji wangu abaini kwamba mambo ya usoni yalishatokea huko
nyuma.Hata wanasiasa ghiliba tupu walishakuwepo huko nyuma,
yaliyowapata,yalitokea kutufundisha sisi wa sasa.
Ndiyo maana kichwa cha
makala haya hiutwa, “LEO NI JANA YA KESHO!”.Hakuna jambo jipya
hapa duniani. Suruwali za kubana zilikuwepo zamani, vijana wakora
walikuwepo,tabia mbaya ya kutoheshimu serikali na mamlaka ilikuwepo
tangu zama za Kaini!
Kaini, ndiye mwanzilishi
wa wakora na magangwe.Biblia,katika kitabu cha Kohelethi au Mhubiri
husema kwamba:
“Pepo huyarudia
mazunguko yake na mito hurejea inakotoka; wala hakuna jambo jipya
chini yajua”, Mhubiri 1:6-10.
Huyu Mhubiri, ambaye ni
Mfalme Suleiman mwana wa Mfalme Daudi wa Yese,(Tazama Mhubiri
1:12),aliishi kati ya mwaka 965-926 BC.
Msomaji mmoja ananiandikia
kwamba nirahisishe lugha ili wasome watu wa kawaida pia.
Hata hivyo, hiyo miaka ya
Kabla ya Kristo(Before Chris) inapungua na AD inaongezeka. Tujifunze
historia.
Kiwango cha elimu cha huyu
mtu aitwaye Suleiman, au nimwite Prof. Solomon, kilikuwa cha juu
sana, Falsafa yake ni kwamba mambo mengi hapa duniani hujirudia rudia
sana,yalikuwepo na yatakuwepo,ndiyo maana Leo ni jana ya kesho!
Tawala katili sana leo
duniani,zilishakuwepo hapo zamani sana,zikatoweka zitakuja nyingine
na kutoweka kama upepo.
Walikuwepo akina Julius
Caesar,Augustus(27BC-14 AD),Caligula(AD 37-41), hata watu wakawaabudu
kama miungu, akina Tiberius, wakati ule wa sensa, wakati Yesu
anazaliwa.
Sensa ipo hata sasa, na
watu wanasusa kwamba ni kinyume cha dini! Hata Yesu alihesabiwa,
maana Mariam mamaye alihesabiwa akiwa mjamzito wa kujifungua.
Tiberius alikusanya kodi
kubwa Rome hadi kufikia kama dola za Marekani1,700,000 katika mji
mmoja.
Walikuwepo akina Kaisari
Nero waliowakata vichwa mitume wa Yesu, watakuwepo wengine wakatili
kama hao. Gidion M. anatwambia jambo hili kwa kina.
Mathayo alichunwa ngozi
akiwa hai, Thomas alichomwa mkuki huko India, Marko alifia Ethiopia,
Mathayo alifia Alexandria,Misri,Luka akafia Ugiriki, Yohana
alichemshwa katika pipa la mafuta,Petro alisulubiwa kichwa
chini-miguu juu! Hapa ni mjini Rome.Yakobo alifia mjini Yerusalem n.k
Wamekuwepo hapa duniani
akina Farao,Nebchadnezzar, akina Malkia Cleopatra wa Misri.Hata sasa
kuna hadithi za kuhusu huyu mwanamama mrembo sana labda kuliko wote
duniani.
Historia inasema Malkia
Cleopatra aliwachanganya wanaume wawili wakuu sana-Julius Caesar na
Marc Anthony.Alitumia udhaifu wa ngono wa wanaume kuwamaliza,halafu
yeye akajiimarisha madarakani.
Kuhusu ngono, akina baba
wenye misuli na maarifa katika medani ya vita kama Julius Caesar, ni
dhaifu kwa wanawake- Strongest But Weak!
Cleopatra alikufa mwaka wa
BC 30,hakuacha hata maandishi yake. Cleopatra, “The Last Queen of
Egypt” ilidhaniwa kifo chake kingekuwa mwisho wa Misri?
Hata leo, wametoka akina
Gamal, akina Hosni Mubarak wako kolokoloni wakiwa mahututi,lakini
akina Mohamed Mursi, wapo!
Watu hutoweka na wengine
huja-hakuna mtu wa kudhaniwa mungu hapa duniani.
Cleopatra, alitumia mwili
wake kwa ghiliba ya ngono,kama silaha mithili ya misaili.
Hata leo wapo akina Joyce
Banda,leo ni kama jana.Wamekuja akina Joyce BANDA wanatumiwa na
madola makubwa kwa kisingizio cha demokrasia. Wameruhusu ushoga, sasa
wanataka kuchukua ziwa Nyasa lote ili makampuni ya Marekani,Uingereza
na Ufaransa wachote mafuta na gesi humo. Watu kama yeye wamekuwepo
zamani!
Namwonya Rais Jakaya
Kikwete, asiwasikilize sana hawa wakoloni,ni laghai na wasaliti,
wanajifanya rafiki,kumbe wafitini na wana hila.Tumkumbuke Julis
Caesar eti aliuliwa sababu ya udhaifu wa hila za mwanamke.
Nawaonya wanasiasa wa
Afrika. Wakiloni leo wanajidai kupromoti Demokrasia,kumbe leongo lao
ni kuchochea vurugu na vita Afrika, nchi inaposalia katika miali
mikali ya moto na mtutu wa bunduki,wao wachote rasilimali na
kuondoka!
Shime, wanasiasa hata wa
upinsani wasidhani wanatafuta haki na demokrasia,kumbe wanasababisha
nchi zetu zisitawalike.Wakoloni wametoka Libya, walikowachanganya
vichwa vijana wasio na ajira, wametoka Irak, sasa wako Syria baadaye
watakwenda Iran.
Wanaharakati wanalipwa
hela eti kuhamasisha demokrasia na haki za mashoga, wajiulize Yule
wanayemtumikia kwa yakini. Harakati siyo mbaya,ujira wa kufanya hivyo
wanatoa wapi?
Baadaye, watalipa nini?
Haya ya njama za akina Cleopatra kwa akina Julius Caesar na Marc
Athony yalishakuwepo mahali pengi duniani. Tuitazame historia.
Leo ni kama jana tu-Leo
ni jana ya kesho,leo na jana havina tofauti.
TAMATI
0786 324 074
Tuesday, August 28, 2012
GLOBAL WARMING AND CLIMATE CHANGE IN MWANZA
*Mabadiliko
ya Tabianchi yatishia meli kuparamia miamba na kuzama
Na Conges Mramba, Mwanza
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari(TPA),
imewapandisha kizimbani wamiliki wa meli binafsi, kwani wanazuia Mamlaka hiyo
kusimamia usalama wa abiria na mizigo, hata wakati huu wa kitisho cha magaidi
wa Al-Shabaab,Afrika Mashariki.
Mkuu wa Bandari(Port Master)Mwanza, John
Mutalemwa, katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi, alisema wamiliki hao wa
Bandari binafsi wanashindana na Sheria Na. 17(Tanzania Port Act) ya mwaka 2004.
Sheria hiyo
inaipa TPA nguvu ya kusimamia bandari
zote, zikiwemo za watu binafsi,ili kukagua usalama wa abiria na mizigo,kabla na
baada ya safari.
“Sheria inatupa Mamlaka ya kusimamia bandari
zote zikiwemo bubu, tukague na kujua
mizigo kiasi gani inasafirishwa; tunatakiwa kutazama abiria ikiwa wanalingana
na uwezo wa meli au boti,kulinganisha na uwezo wa chombo chenyewe, halafu tunatoa, “Port Clearance”
kabla ya meli kuanza safari”, Mutalemwa alisema.
Kwa mujibu
wa Mutalemwa, vipo vyombo vya usafiri majini,huchukua abiria na mizigo kuoita
uwezo. Hii ni kazi ya TPA kufanya ukaguzi makini,ili kuondokana na Ajali Ziwa
Victoria.
“Bandari ni mpaka wa nchi. Lazima tusimamie
hali ya usalama, meli inaweza kuleta Al-Qaeda ama Al-Shabaab, nap engine inaweza
kuingiza nchini silaha kutoka nchi za vita na migogoro. Eti wanakataa
tusiwasimamie…tumewafungulia kesi mahakamani”,Mutalemwa ameliambia gazeti hili
katika mahojiano Maalum ofisini kwake juzi.
Meli za mizigo za Jijini Mwanza, hufanya
safari zake hadi Port Bell, Uganda,na Kisumu nchini Kenya, ambako sasa magaidi
wa Al-Shabaab wanasaidia kuzimu kupanua kinywa chake.
Aidha, Mkuu huyo wa Bandari Mwanza amesema
nchi za Maziwa Makuu kama Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, na Burundi hazina
amani, na Kenya hamkani si shwari,kufuatia kitisho cha Al-Shabaab, wanaopinga
majeshi ya nchi hiyo kuingia Somalia kuwafulusha magaidi hao.
Kufuatia
hali tete ya usalama nchi jirani, Mutalemwa amesema lazima Mamlaka yake kuwa
macho na usalama wa abiria na mali zao dhidi ya hujuma za magaidi, wanaoweza
kupata upenyo wakaingiza silaha nchini kupitia Ziwa Victoria.
Mamlaka ya Bandari humiliki bandari za Mwanza
Kaskazini na Kusini,Nansio Ukerewe,Kemondo Bay na Musoma.
Vituo
vingine vidogo vinavyomilikiwa na TPA ni Maisome,Nkome,Bukondo,Kahunda,Miharaba,Kome,Buchosa,Solima,Karumo,Chato
na Nyamirembe(Kagera) na Kinesi mkoani Mara.
Bandari ya Mwanza ni kiungo muhimu kwa nchi za
Maziwa Makuu,hususan Uganda na Kenya,na
huchangia kwa kiwango kikubwa kukua kwa shughuli za uchumi,hata katika nchi
wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki(EAC).
Ripoti ya Malka hii iliyotolewa kwa Kamati ya
Bunge ya Miundombinu(nakala tunayo), inasema bandari ya Mwanza ingeweza
kusafirisha abiria milioni moja kwa mwaka.
Ingeweza kusafirisha tani mamilioni za moja za mizigo,kama Reli ya Kati ingekuwa
inafanya kazi kwa ufanisi. Hili ni eneo muhimu kwa ukuaji wa uchumi wan chi,lakini
kinyume chake ni hasara kila upande.
“Huduma hafifu za Reli zimesababisha shehena
ya kahawa kutoka Uganda na hata Bukoba,kubadili njia(route) na kupitia Bandari
ya Mombasa,Kenya “, Ripoti hii inasema.
Kufuatia huduma duni za Shirika la Reli,
Bandari za Mwanza ziko taaban,kwa sababu ya kupungukiwa mapato, zinaendeshwa
bila faida.
Kulingana na Ripoti hii kwa Kamati ya Bunge ya
Miundombinu,katika kipindi cha miaka mitano,kuanzia 2006/2007 hadi 2010/2011,
mizigo imepungua katika Bandari za Mwanza kutoka tani 480,568 hadi 248,860
mwaka 2011.
Utendaji
mbovu wa lililokuwa Shirika la Reli(TRL) ulisababisha treni iliyokuwa
ikisafirisha abiria na mizigo kati ya Mwanza na Bandari ya Dar es salaam
kusimamishwa.Hali hii husababishwa abiria na mizigo kubadili njia na kukosesha
mapato bandari za Mwanza.
Wafanyabiashara wa Uganda wanasafirisha bidhaa
zao kupitia bandari ya Mombasa,nchini Kenya.Shehena ya kahawa kutoka Uganda
iliyokuwa ikipitia bandari za Mwanza, inapitia Mombasa na hivyo kupunguza
kiwango cha mizigo kutoka tani 250,000 mwaka 2007 hadi tani 100,000 mwaka
2009/2010.
Kufuatia madudu ya TRL, hata abiria wamepungua
katika bandari za Mwanza kutoka abiria 891,634 mwaka 2007 hadi abiria
593,342.Huu ni upungufu wa asilimia 6.3 unaoikosesha nchi mapato na fursa za
ajira kwa watu wake.
Ripoti hiyo ya TPA, imebaini kwamba, wasafiri
wa vyombo vya majini Ziwa Victoria wamepungua kufuatia ushindani uliopo wa
barabara,hususan baada ya mtandao wa barabara kukamika ujenzi kwa kiwango cha
lami.
Kati ya Mwanza na Bukoba kuna usafiri wa ndege
ambao huchangia pia abiria wasisafiri kwa meli.
Kufuatia
hali hiyo,ripoti hiyo imebaini kuwa Kampuni ya Huduma za Meli,Marine Services
Company(MSC) iko hatarini kufilisika,kufuatia meli zake kuharibika mara kwa
mara,kitu kinachodaiwa na baadhi ya abiria kuwa ni hujuma za baadhi ya
wafanyakazo wa MSC ili kuwanufaisha wenye meli binafsi.
Kaimu Meneja Mkuu wa MSC, Projest Kaija,
ameliambia Mwanahalisi kwamba madai
hayo hayana ukweli, kwa kuwa kuhujumu kampuni unayofanyia kazi maana yake ni
kuhujumu mshahara na mapato yako.
“Je,
unahujumu Kampuni namna hiyo ili kampuni ikifa wewe utoe wapi mshahara?’ Kaija
alihoji.
Siku za karibuni MSC imewaondoa viongozi wa
Kampuni hiyo na kuwaweka wapya ili kuboresha ufanisi na kupunguza nakisi.
Kwa kipindi cha miaka mitano, idadi ya meli
zilizohudumiwa na Bandari za Mwanza, imepungua kutoka 2,684 hadi meli 1,900
mwaka jana.
Bandari ya
Mwanza pia huendeshwa kwa hasara ya mamilioni ya shilingi kila mwaka,nakisi ni
takriban shilingi bilioni 4.5
Mabadiliko
ya Tabianchi na Ongezeko la Joto Duniani,pia hutishia USALAMA wa usafiri Ziwani
Victoria.
Kwa kipindi
cha kati ya mwaka 1998 hadi 2006,maji ya Ziwa Victoria yamepungua kutoka mita
1,141.24 juu ya usawa wa bahari hadi mita 1,139.20. Upungufu ni wastani wa mita
2.04.
Kulingana na
Ripoti hiyo, meli nyingi zimekuwa zikishindwa kufungwa katika bandari za Mwanza
na Nansio,Ukerewe. Kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili pia huweza
kusababisha kuzuka kwa miamba ambayo huhatarisha usalama wa meli na boti na
usalama wa abiria,hasa wanaposafiri nyakati za usiku.
Meli
zinapoparamia miamba hutoboka na kujaa maji,ama kuwa katika hatari ya kuzama.
Ziwa Victoria ni chanzo cha Mto Nile, ambao
huanzia katika Maporomoko ya Owen,Uganda; maji husafiri umbali wa zaidi ya
kilomita 6,900 hadi Misri. Mvua za masika zinaponyesha Afrika ya Mashariki
hubeba rutuba mezi ya Aprili na Mei na rutuba hiyo hufika Misri kati ya Agosti
na Septemba na kuwawezesha Wamisri kupata rutuba jangwani.
Mto Nile ni mungu wa Wamisri. Miungu ya Misri
ina ‘mama’ yao Ziwa Victoria. Ni kwa sababu hii, mwaka 1929 na 1957 Misri
walitiliana saini mkataba na Wakiloni wa Kiingereza kuzuia matumizi ya maji ya
Ziwa Victoria kwa shughuli za kilimo na hata vyanzo vya umeme kama kilichopo
Jinja.
Aidha,kupungua kwa kina cha maji ya Ziwa hili
hufanya meli kutia nanga katika maji ya kina kirefu,na huku ni kuhatarisha
maisha ya abiria,hasa katika maeneo ya visiwa.
Mkuu wa Bandari ya Mwanza, John Mutalemwa
anasema Mamlaka yake imelazimika kuchimba mchanga katika bandari za Mwanza ili
kuongeza kina cha futi tatu ili kuwezesha meli kufunga gatini.
Mradi kama huu unafanyiwa upembuzi yakinifu
katika bandari ya Nansio,Ukerewe,lengo likiwa kujenga gati imara na salama.
Mpango wa
serikali wa kuunganisha Reli kutoka Tanga hadi Musoma kupitia Arusha, utaweza
kurejesha wingi wa abiria na mizigo katika Bandari za Mwanza, au abiria na
mizigo ya Uganda,Rwanda,Burundi na Congo wanaweza kutozifikia kabisa bandari za
Mwanza,na hivyo kuleta kifo cha mende kwa TPA na Meli za MSC.
Ziwa Victoria
ni fursa muhimu kwa Tanzania katika Soko la Pamoja la EAC,lakini fursa hii
inaachwa kwa wageni kupitia hujuma na ufisadi unaofanywa na maofisa wa
mashirika ya umma kama TRL na MSC.
www.congesmrambatoday.blogspot.com
0786 324 074
LEO NI JANA YA KESHO(2)
TUNAJADILI
ikiwa yupo kiongozi mahiri wa siasa hapa duniani, anayewapenda wananchi kiasi
cha kujitoa mhanga mithili ya mshumaa.
Mshumaa,huwaangaza wengine huku
ukijiteketeza wenyewe.
Mwandishi wa
Kigiriki, Euripides, aliandika takriban millennia tatu zilizopita kwamba,Mfalme
kijana mtanashati wa Thesaly aitwaye, Admetus aliugua.
Miungu ya
Ugiriki(Ugiriki ni nchi ya masanamu ya miungu wengi) ikawaambia nduguze kuwa
lazima Admetus afe, isipokuwa kama angepatikana mtu mwingine wa kufa badala
yake.
Kwa
Kiingereza mtu wa kufa badala ya mwingine ni “Substitute” ambaye kama
angepatikana kufa badala ya Mfalme Admetus, angeweza kupona maradhi yake na
kuendelea kuishi.
Wakaulizwa
baba na mama yake kama walikuwa radhi kufa badala ya Admetus,wakakataa. Ndugu
zake nao waliulizwa,wakakataa. Marafiki nao walisema, “Admetus, ni kijana
mzuri; ni mfalme mzuri,lakini hakuna wa kufa badala yake!”
Mwisho wa
siku, mkewe msichana mrembo sana aitwaye, Alcestis, akahiari kufa kwa niaba ya
Admetus,kwa sababu alimpenda na alikuwa mtu mwema.
Baada ya
kifo cha Alcestis, Mfalme Admetus alitambua ‘HASARA’ iliyomkuta ya kumkosa
kipenzi chake, Alcestis aliyekuwa na upendo wa dhati kwake.
Akamwombolezea ifuatavyo:
“Nitakulilia mpenzi wangu,siyo kwa
mwaka mmoja au miwili;bai katika siku zote za maisha yangu,mwanamke
uliyenipenda! Baba na mama walinichukia,walinipenda kwa maneno matupu,siyo kwa
vitendo”, Admetus aliomboleza.
Nataka
msomaji atambue kwamba, kumpenda mtu kwa maneno matupu siyo kumpenda-ni
kumchukia.Upendo wa dhati siyo wa maneno matupu; ni vitendo kama alivyofanya
Alcestis.
Naam, “Love in words, not deeds” ni unafiki
mtupu, siyo upendo,kama wanavyojidai siku hizi wanasiasa na wakoloni wetu wa
zamani.
Nakusudia
kuwaonya Waafrika wasiwe wepesi kulaghaiwa na wanasiasa na hata wakoloni wetu
wa Ulaya na Marekani, kwamba wana upendo kwa wananchi-si kweli ni unafiki na
ufalisayo mkubwa!
Hata
hivyo,Katika Warumi 5:7 Profesa Paulo
anasema, “Ni shida mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema,kama Admetus.
Biblia,
katika Warumi 5:8-10, inasema, “ Lakini,Yesu Kristo alikufa kwa ajili
yetu,tulipokuwa tungali “ADUI” zake.Alitupatanisha na Mungu tulipokuwa tungai
adui zake”(wenye dhambi ni adui wa Mungu).
Nataka
kujifunza hapa kwamba, Biblia inatwambia kwamba UPENDO ni dhidi ya adui, ambaye
kwa kawaida hawezi kuwa na faida yoyote-Upendo usio na faida!
Upendo wa
Alcestis kwa Admetus siyo huu usio na faida,bali ni upendo wa mke kwa mumewe,
“Philos’ au Philia-upendo wa familia,upendo wa kibinadamu wa kidugu-Brotherly
Love.
Baba
humpenda mama,mama humpenda baba, wazazi huwapenda watoto,hata mwingine hujitoa
mhanga kuwaopoa motoni.Ndugu hupendana wao kwa wao n.k
Upendo wa mtu kumpenda adui hata kuwa radhi
kufa kwa niaba yake ni Agape kwa Kigiriki, Prof. Ibrahim Lipumba, Dk.Wilbroad
Slaa au Rais Jakaya Kikwete, hawawezi kuwa na upendo wa jinsi hii, wala ule wa
Alcestis kwa raia.
Tuambizane
ukweli.Upendo wa kweli, “TRUE LOVE” Agape au Philos ni upendo wa mtu kuumia kwa
ajili ya kumpatia mema mtu mwingine. Upendo wa Agape hauna faida, “suffers long
and it thinks no evil”, hata kama unamwonyesha upendo huo jambazi au adui yako!
Tujiulize:Wanasiasa
wetu hawa, viongozi wa sasa wanaweza kujitoa mhanga wafe kwa ajili yetu
wananchi?
Wako tayari
sisi raia tuishi maisha bora kuliko wao?Wako tayari kuuza mashangingi,suti zao,
briefcase zao na rasilimali zao
nyingine, ili sisi wapigakura wao tuishi maisha bora?
Mtu
mbumbumbu anaweza kusema kwamba jibu la maswali haya ni Ndiyo! Haidhuru.
Tumjadili Mpigania Haki za Weusi wa Marekani, Martin Luther King Junior.
Kabla ya
kwenda kwa mtu huyu,tujisaili: Kwanini sisi masikini hatuna shule bora kwa
ajili ya elimu ya watoto wetu? Kwanini hatuna zahanati,dawa,vifaa na hatuna
hospitali?
Kwanini sisi vijijini hatuna barabara wala huduma
za jamii kama umeme,maji safi na salama n.k wakati wanasiasa hawa wao wana kila
kitu?Wanatembeleaje magari ya Milioni 60 wakati sisi hatuna zahanati wala dawa?
Viongozi wa
dini nao siku hizi wanatembelea magari ya fahari ya zaidi ya Bilioni 2, huku waumini
wao wakiwa hawana hata makubazi miguuni! Wanaimba Upendo! Mungu ni Upendoo,
aaameeen! Aibu tupu!!
Yawezekana
mtu “kuthubutu” kufa kwa ajili ya mtu mwema kama Admetus-huu upendo huitwa,Philosterges, kwa Kigiriki.
Lakini, kama
huna nasaba na mtu,humjui, naye ni adui yako na ukahiari kufa badala yake,
ndiyo AGAPE.
Wapo watu
wanakesha redioni na kwenye runinga wakiimba, “Nakupenda kama nyamachoma!” Huu siyo upendo, ni tamaa za
ngono(sexual drive, sexual affections, sexual love)ambazo mwisho wa ngono,hakuna
chochote,bali uchungu na majuto kwa aliyedanganyika.
Kumpenda mtu
usiyemjua,usiyewahi kukutana naye na hana faida kwako,ni “Impartiality Love”
upendo unaoitwa Agape ama Agapao kwa Kigiriki. Huu ndiyo upendo anaopaswa kuwa
nao kiongozi wa siasa-kuwapenda wananchi asiojua hata majina yao,na wanaishi
pembezoni kule,Masasi ama Saragana,Masinono na Bugwema,Musoma!
Siku hizi,
tunasikia kwamba kiongozi Fulani anawapenda wananchi, hadi wananchi wanakubali
kupigwa virungu,kupigwa machozi ama kupigwa risasi na polisi,kwa kutii shuruti
zake hata kuwapiga mawe polisi wenye SMG!
Polisi
wakizuia maandamano, kiongozi wa siasa akasema, Andamaneni, watu wanatii na
kupoteza maisha! Hii ndiyo Agape, watu kumfia kiongozi, siyo?
Agape, siyo
watu wafe kwa ajili yako ili uende Ikulu au uukwae ubunge ama madaraka Fulani.
Agape ni wewe kiongozi ufe kwa ajili ya masikini usio na nasaba nao,ili kwa
kifo chako wapate faida ya kukombolewa.
Tofautisha
upendo wa Alcestis,Martin Luther King Junior, Yesu na hawa jamaa. Tafakarini.
Tunajadili
upendo wa dhati.Viongozi wa siasa wanaonesha upendo huu kwa wananchi? Viongozi
wa kidini wanawapenda kwa dhati waumini wao? Mbona wao wanakula na kushiba,
wafuasi wao ni fukara?
Kwa nini
rushwa na ufisadi kama kuna upendo katika mtego uitwao siasa? Kwanini mishahara
ya wabunge na wafanyakazi iongezwe maradufu,halafu mazao ya wakulima yashuke
bei kwa visingizio vya kushuka kwa thamani ya shilingi au mtikisiko wa uchumi
duniani?
Kwa nini
hawa ambao hawajulikani kwa wanasiasa na viongozi wetu(wakulima),mazao yao
yanaposhuka bei,maisha yanapokuwa duni na hawana huduma za jamii,halafu
tunawachochea wafanye vurugu,wafe kwenye maandamano yaliyopigwa marufuku na
polisi,badaya ya kuwasaidia waishi,wanusurike kufa?
Tuambizane ukweli.Wanasiasa wote ni ndizi-ni
rangi moja na wamepinda! Msikubali wawatumie kama ngazi, wao wanaingia kula
maisha,nyie mwabaki kupigwa jua na mvua.
Acha upambe,
angalia maisha yako ni ya thamani kubwa. Kwanini umpige polisi kwa mawe wakati
yeye ana SMG yenye risasi 30?
Nahimiza
watu kuheshimu maisha yao,nahimiza watu kuheshimu mamlaka, nahimiza usamaria
wema,nahimiza utii wa sheria bila shuruti na kuheshimiana sisi kwa sisi.
Tusikubali viongozi wa siasa kutugawa kwa
misingi Fulani ili tuanze kupigana.Tukipigana wao wana mbawa,sisi tunakufa na
wake na watoto wetu wanateketea wakati wao huruka kwa ndege na kwenda zao!
Vita vya
wenyewe kwa wenyewe Kenya,ni mfano mzuri kwetu.Waliokufa walikuwemo watoto wa
Kibaki? Hapana. Walikuwemo wa William Rutto, ama wa Raila Amolo Odinga?
Watakuwemo
wa Dk.Slaa au Kikwete na wenzake? Anzisha amani, acha ujinga.
ZBIGNIEW
BZEZINSKI, alikuwa Mshauri wa Usalama wa Taifa, enzi za Rais Jimmy Carter wa
Marekani.
Huyu,mtu
mkubwa, wa Taifa babe sana hapa duniani ambalo husemwa lina demokrasia
iliyopevuka,ndiye hasa anayetuhumiwa kusimamia mradi wa kutengeneza virusi vya
Ukimwi,katika maabara za kijeshi huko kilomita 75 kutoka New York, mwaka 1975.
Naam,viongozi
wakubwa ni wenye ‘madudu nakubwa’.Wenye mamlaka makubwa wana madhambi makubwa
sana, kinachowaokoa ni uzuzu wa wafuasi wao kueneza propaganda kwamba hao
viongozi wao siyo binadamu wa kawaida,bali malaika au miungu.
Watu wadogo,
hasa viongozi wa Waafrika utaona wanasemwa walifanya upumbavu huu na ule!
Utaona unyama unafanywa Afrika,utadhani Ulaya na Marekani ni mbinguni!
Martin Luther King Junior, alitiliana saini
muswada wa Uhuru kwa Weusi wa Marekani,Julai 3,mwaka 1964.Mkataba huo ulikuwa
kati ya Dk. Luther King na Rais Lyndon Johnson, Martin Luther aliuawa na
Pentagon,Makao Makuu ya Jeshi la Marekani mwaka 1968.
Huyu, alitoa
maisha yake akipigania haki za watu wake, WEUSI wa Marekani, dhidi ya ubaguzi
wa rangi.
Tabia hii
ingalipo Marekani, na Ulaya. Namwonya
Rais Jakaya Kikwete awe macho na Uingereza, Marekani na Ufaransa.
Siku hizi
wameanza kumtumia Joyce Banda,kutaka kuleta chokochoko Maziwa Makuu,vita
vinapofumuka sisi kwa sisi,wao wachote rasilimali zetu na kuondoka. Nyuma ya
Joyce Banda lazima wapo hawa wameona kunaweza kuwepo mafuta ama gesi, ili
tuking’amua tuache kuwategemea!
Kama
alivyosema manafalsafa wa Ugiriki, Salon, sheria zilizowekwa ni ‘utando wa
Buibui’. Marekani hukiuka sheria na kwenda zao pasipo kunaswa na sheria hizo.
Wewe ‘mdudu’ mdogo ukicheza unanaswa.
Angalia
baadhi ya wadudu wadogo walionaswa katika “Spider’s Web” ni pamoja na akina
Muammar al- Qaddafi,Saddam,Osama,Charles Taylor,Laurent Gbagbo n.k
Tumjadili
kidogo Charles Ghankay Taylor.Ametumwa na Marekani kufanya unyama Sierra Leone
wakaja kumwacha penye mataa.
Walimtorosha
wenyewe gerezani huko Boston, akakimbilia Libya, akajifunza mbinu za medani za
kijeshi, akasaidiwa kupindua serikali Liberia, akaanza ‘biashara’ ya kusaidiana
na Revulutionary United Front(RUF) huko Sierra Leone, wakachukua almasi na
kumpa Marekani, wakapewa bunduki!
Mwisho wa siku, Taylor amekamatwa,
amefunguliwa kesi akashinda makosa yote 11, Marekani wakalazimishwa afungwe
miaka 50,tena Uingereza,ili abaki kimya gerezani maishani mwake, asipate kusema
siri!
BAFFOR
ANKOMAH,Mhariri wa jarida mahsusi la New African la Julai mwaka huu, katika
safu yake ya “Baffour’s Beefs” amesema uovu wa Marekani na mataifa babe
haya(Metropolitan Powers) ambao waliwashinikiza akina Louis Moreno Ocampo na
Fatou Bensouda, kumkomesha kicha maji kama Charles Taylor.
Nataka
kuwaonya viongozi wa Afrika,wanaotumiwa na Marekani,Ufaransa na Uingereza,kukoma
kuihujumu Afrika,la sivyo wanaelekea mahali walipo Taylor,Gbagbo, Osama,
Gaddafi n.k
Marekani
hawana rafiki,rafiki ni rasilimali kwa maslahi ya Marekani, siyo Afrika!
Nawaonya pia viongozi wa vyama vya siasa hapa
Afrika.Wanapewa vijisenti na silaha ili wafanye vurugu,nchi zetu
zisitawalike,mwisho wa siku ni hawa Marekani,Uingereza na Ufaransa
watakaofaidika na vita vya Kunguru!
Wametoka
Libya,Misri,Irak,Yemen na sasa wako mbioni kuiteka Syria,wakimaliza watakwenda
Iran. Qatar,Kuwait,UAE,Lebanon,Bahrain kumetulia kwa kwa sababu wamekubali
‘unono’ uende Ulaya na Marekani! Ukipinga tu,unaoneshwa mtutu wa bunduki na
unapelekwa kwenye utando wa bui bui utakaokunasa.
Sisi ni
wadudu wadogo,nzi-kwenye ‘spider’s web’ hatuwezi kuvuka.Tando zote za buibui
kama ICC huko Hague,ni mali yao.
Sasa
jidanganye kwamba Marekani na Ulaya kuna demokrasia au haki za binadamu. Wewe
naye binadamu,mtu mweusi?
Kamuulize
Caster Semenya, au Samuel Eto’o.
Angalia
madudu ya akina Nicolas Sarkozy huko Ufaransa, amefanya ufuska,uchafu akiwa
rais. Angekuwa RG Mugabe au mwingine,ungesikia maneno.Raia wangeshawishiwa
kuingia barabarani na kuchoma moto magari ya serikali,majengo na matairi
barabarani,kwamba ndiyo, “PEOPLES POWER”!!
Ufaransa,
‘scandal’ za akina Sarkozy za kufanyisha watoto ngono, huko Thailand na
Ufaransa eti ni ‘minor thing’, lakini viongozi kama Luiz Inancio da Silva wa
Barazil watasemwa hawana elimu,ni washona viatu! Hawaongei kuwa uchumi wa
Brazil ulipaa wakati wa Da Silva!
Wanaona sana
akina Jacob Zuma Mushorozi na Mfalme Muswati III wa Swaziland kuona vimwana
kila mwaka!
Lakini, ufuska wa akina Silvio Berlusconi huko
Italia ni ‘Minor thing’! Raia hawashawishiwi kuingia barabarani na mawe na
hawalipwi mishahara huko kushika bunduki,kama Syria.
Sisi
‘Madodoki’tunalishwa kila pumba na kuanza kupigana sisi kwa sisi. Hatujui
mwisho wake utakuwaje? Hatutazami kesho kwa kuchungulia historia ya hawa akina
Charles Taylor,Jonas Savimbi,Mobutu, Hosni Mubarak na vibaraka wengine walivyofanyiwa.
Nataka
kusema kwamba,tujiepushe na Marekani na wanasiasa wa Afrika ambao leo Marekani
na washirika wake wanawalipa posho kuja kufanya vurugu Afrika,ili tupigane sisi
kwa sisi,wao wachukue rasilimali.
Kumbe hata
mgogoro kati yetu na Malawi haufai kuishia kuwa vita vuya silaha,tunawanufaisha
hawa majahili walioanza kuchochea vita kwa kujua Ziwa Nyasa kuna mafuta au
gesi!
Nawashauri
Waafrika kuachana na kulishwa ‘kasumba’ ya kikoloni. Tuanze kupendana sisi kwa
sisi na kutatua matatizo yetu kwa amani,bila kuwaalika majahili hawa.
Nawaonya viongozi wa siasa hapa Afrika na
wapambe wao wanaopokea posho toka Ulaya na Marekani ili wawachochee vijana
kufanya vurugu kwa kisingizio cha ufisadi, na kukosa ajira!
Fikirini vizuri. Vita vikifumuka ndiyo
mtaajiriwa kwa risasi na mizinga?Ndugu zenu wakifa ama mama zenu na wadogo zenu
wakiwa wakimbizi,ndiyo mtapata ajira?
Itaendelea
0786 324 074,0754 324 074
Monday, August 27, 2012
LEO NI JANA YA KESHO(1)
TAI NI
NDEGE, anayeruka juu angani, umbali wa futi 10,000 ambazo hakuna ndege mwingine
aweza kufika.
Kwa sababu
hiyo, ndege tai ana uwezo wa kuona mbali kiasi cha kushangaza.Aweza kuona
mawindo akiwa mbali huko angani. Tunafundishwa sisi wanadamu kuona mbali
mithili ya ndege huyu. Tujifunze kufikiri kuliko kusema na kusoma, lengo ni
kupima faida na hasara ya kila jambo katika maisha.
Watanzania,
tumefika hapa tulipo kwa sababu hatuwezi kuona mbali kwa faida yetu.
Tumewaachia wafadhili na watu wengine kufikiri kwa niaba yetu-makosa makubwa.
Jicho la mtu halikuoneshi wewe hatari inayokukabili.
Sasa,
wasomaji wataniuliza:Wawezaje kuona mbali mithili ya ndege tai? Jibu ni rahisi.
Unatazama jana ili kujua ya kesho. Unatazama historia. Historia hutuonesha
kesho kuna nini?
Historia,
hutuonesha kesho kutatokea nini. Historia ni muhimu katika maisha. Historia
hutuambia siri za siku za usoni.
Mwandishi wa Kiingereza, George Orwell,ambaye
jina lake halisi ni Eric Arthur Blair, aliwahi kuandika hivi:
“He, who
controls the past, controls the future. He who controls the future, controls
the Present”
Tafsiri
yangu isiyo rasmi ni kwamba George Orwell,Yule mwandishi wa kejeli(satire) ya
SHAMBA LA WANYAMA, alisema hivi:
“Anayetawala
Historia,hutawala pia siku za usoni; na atawalaye siku za usoni hutawala hata
leo”.
Anaongeza kusema, “Today was Yesterday’s Tomorrow”-leo ni jana ya kesho!!
Anaongeza kusema, “Today was Yesterday’s Tomorrow”-leo ni jana ya kesho!!
Ndicho
kichwa cha makala haya,kutuonesha kwamba leo ni jana ya siku za usoni. Usione
leo ukadhani utakuwa hivi hivi kesho,leo itapita na itakuja kesho usiyodhani.
Ukitaka kujua ya kesho,tazama jana na leo-tafakari,jifunze kufikiri kwa kina.
Naam, leo
ilikuwa jana ya kesho.Ninapotazama historia nawaona watu wanaorejea tabia na
makosa ya jana.
Dola ya Rumi,
ilipinduliwa zamani kwa sababu ya ulevi,kukosa uzalendo,rushwa,ufisadi, raia
kupenda starehe na anasa, na hata leo Tanzania tunarejea yale yale tu.
Watu
wanafanya makosa yaliyowahi kutendwa katika historia, watu huchagua kufanya
yale yale yaliyofanywa katika historia,na hata kesho haina tofauti kubwa. Vita
vilikuwepo na hata sasa na kesho vitakuwepo,kwa sababu watu huyarejea yale
yaliyotendwa katika historia.
Historia
haiwarogi watu hata wayatende yale ya kale. Hatutaki kujifunza Historia,hatujui
na hatujui kuwa hatujui,ndiyo maana tunafanya makosa yaliyofanywa katika
historia.
Laiti tungejifunza Historian a kubaini makosa
ya wenzetu wa juzi na jana,leo tungetenda tofauti na kwa umakini na hekima.
Jumatano,
Agosti 22 mwaka huu, nilikuwa nikitazama kipindi cha STRAIGHT TALK AFRICA cha
Sauti ya Amerika(VOA) juu ya kifo cha Rais aliyekuwa Rais wa Ghana, John
Atta-Mills.
Nilitazama
kuapishwa kwa Rais Mpya, John Dramani Mahama, mahojiano kati yake na
Mtayarishaji wa kipindi hicho, Dk. Shaka Ssali, kwamba anaapishwa kumalizia
miezi mine iliyobaki,hadi kufikia Uchaguzi Mkuu.
Nikamaizi kuwa, Rais Mpya wa Ghana, John
Mahama, anafanana sana na wenzake waliomtangulia katika Ikulu ya mjini Accra.
Marais wote
waliapa kuiongoza vema Ghana;wote waliapa kuwajali raia,kuiendeleza nchi kwa
usawa na kutokuwa na upendeleo.
Naam, akina
Jerry John Rowrings ,John Kufour,John
Atta=Mills, na sasa John Dramani Mahama-naam,ni Ghana na utawala wa akina John!
Majina ni yale yale, watu walewale,kasoro ni
mbwembe za kuapishwa,suti walizovaa na wapambe waliowazunguka-maisha yale
yale,mambo yale yale tu,hakuna jipya.
Tujifunze
kuchungulia nyuma katika historia. Wanasiasa wakubwa siyo watu wa
kutegemea,kutumaini na kuegemea. Tunapaswa kuwatii,kuwaheshimu na kuwanyenyekea
kwa sababu wanashikilia mamlaka ambayo ni mithili ya upanga. Lakini siyo
kuwatumaini.
Mwanamuziki,
Roger Whittaker, alishaimba kwamba wanasiasa ni mithili ya ndizi mbivu katika
chane: Wote ni njano, wameshikilia pamoja,wanakula pamoja,wana rangi
moja,lakini hakuna aliyenyooka hata mmoja!
Nataka kuwaonya Watanzania wanaodhani
wanasiasa ni “Truvada” (dawa mpya ya Ukimwi iliyovumbuliwa),kwamba watamaliza
matatizo yao,wanajidanganya kuliko kawaida.
Watu wakubwa
wengi wamepinda mithili ya ndizi, hawana maadili. Wakisemacho hawakitendi na
wakitendacho sirini,hawakisemi. Wanapoapishwa,husema wataitii sheria na Katiba
ya Nchi, mara waingiapo madarakani,hujikuta wakitenda tofauti na walivyoapa.
Sasa, utaona watu wakivuja jasho jingi
kusukuma magari yao,kutandika mavazi yao chini,ili hawa mashujaa wao, “Role
Models” wapiti juu yake. Wengine wamefariki dunia kwa kukinzana na mamlaka kwa
sababu hao mashujaa wao wameagiza wafe!
Maisha yako ni ya thamani kuliko ya mwenzako.
Wanasiasa hawa watakuja na kuondoka,lakini
shida zetu zitabaki ikiwa sisi wenyewe hatuwezi kukaa na kutazama namna ya
kuziondoa.Wanasiasa wana kiu ya madaraka,na wala hawana nia ya kututumikia
mithili ya mshumaa. Mshumaa, hujiteketeza wenyewe kwa nia ya kuwaangaza
wengine. Nani mwanasiasa mshumaa?
Akiwepo
kiongozi mshumaa(na hayupo) huzimika mara kunako tufani. Elton John aliimba
kwamba , “Candle in Wind” mshumaa kunako upepo, wakati wa mazishi ya Princess
Diana, unakumbuka?
Naam, Candle in the Jungle!
Mshumaa mwituni,
utawaka,kunako tufani? Hata Princess Diana hajawahi kuwa mwema mithili ya
mshumaa,kujiteketeza wenyewe kwa nia ya kuwaangaza wengine? Huu ni Upendo wa
Agape.
Wanasiasa hawana upendo wa Agape.
Wanaweza
kuwaona raia wao mithili ya familia zao ama watoto wao wa kuzaa. Huu ni upendo
uitwao kwa Kigiriki, Philos,Phileo ama Philia.
Wengine wana
upendo wa kitoto,Storge, na wengine wana tamaa na ashiki za kimwili,Eros ama
Erao ambazo huzitumia kupora wake za raia wao na kuondoka!
Nakwambia
ukweli msomaji,amini usiamini. Usiwaamini wanasiasa hata ukajitoa mhanga
.Usifanywe ngazi ya kupandia ama kukwelea mamlakani,usigeuze mabega yako kubeba
wanasiasa hawa-heri kubeba zege,ili upate mlo wa usiku, sembuse wanasiasa hawa?
Watakuja na kuondoka,dhiki zetu zitabaki. Tena
wengine watakuja na kupandikiza chuki na ukabila kama Kenya,watawaachia
wananchi vita,umwagaji damu na visasi vya kurithi.
Mwanafalsafa
wa Athens,Ugiriki,Salon anasema hivi:
“The law is
like spider’s web. The small are caught ,but the great tear it up!”
Tafsiri
yangu:Sheria ni mithili ya utando(mtego) wa buibui,wadogo hunaswa
humo(wanyama,wadudu n.k)
Lakini,
wakubwa huutatulia mbali na kujiendea zao pasipo madhara yoyote! Nataka nikwambie
msomaji,watu wakubwa mnaowategemea(mnasukuma magari yao na kutandaza mashati na
khanga za akina mama ili wapiti juu yake) ni wahalifu sana. Hawana maadili
myoyoni mwao bali midomoni.
Wakubwa,
hujidai kuwapenda raia wao. Raia wako tayari kuwafia wanasiasa wao,lakini
wanasiasa ni nadra kufa kwa ajili ya raia.Wanakubali wafe kwa sababu ya tamaa
ya madaraka,na aslani siyo kwa ajili ya kuwapenda raia.
Kwa
wanasiasa,wanapokuwa akigombea uongozi,raia ni ngazi zao za kukwea uongozini.
Pindi wanapopata madaraka,raia hugeuka shubiri,mizigo ya kuwahoji kutimiza
ahadi. Raia hugeuka ‘adui’ za wenye mamlaka.
Sasa, nani
alikufa kwa ajili ya adui zake. Labda tusome Warumi sura ya 5,kwamba ni Yesu
aliyekufa kwa ajili ya adui zake!
Viongozi wengi wanaponyatia madaraka,hujidai
wema mithili ya mishumaa.Lakini pindi waingiapo mamlakani,hugeuka
mangimeza-hutawala kwa kutoa amri na
shuruti wakiwa mezani,kuliko kusikia kilio cha wananchi.
Uadilifu
hauji kwa maneno ya mdomoni,bali matendo yatokayo moyoni(Mathayo 21:23-32) hii
ni kusema, “To walk the talk”.
Watu wakubwa
sana duniani ni dhaifu kupindukia-Strongest but weak.
Nakusudia
kuchungulia historia ya watu wakubwa duniani kama Julius Caesar, Pharao wa
Misri,Malkia Cleopatra wa Misri, Kaisari Nero, Mfalme Herode,George Washington n.k
Hawa wote
walikuwa wavunja sheria,ambao kama umma ungemaizi, walistahili kukatwa vichwa
kwa uhaini, lakini kwa sababu ya wapambe, walishangiliwa sana.
Leo, nawashauri wasomaji wangu kuwaheshimu
wenye mamlaka(Warumi 13) ili ujiongezee uhai. Ni upumbavu wewe mwenye mawe
kujibizana na polisi wenye SMG zenye risasi za moto,ukijidai Mfalme Daudi kwa
Goriathi. Usijidanganye mwanaharakati kumtupia jiwe polisi mwenye silaha.
Mwanamuziki
Muhiddin Gurumo, na wenzake waliimba hivi zama za Ndekule:
“Usimkaribie
chatu, ooh chatu wee; gongo usimtupie utaukosa ushindi! Natoa onyo kwa yeyote
anayemchezea chatu, ni hatari, atakuja askikose lolote la manufaa na ajali
imkute bila ya kutegemea, atakuja adhirika ajute na duniaaa!”
Wanasiasa ni
chatu,hasa wawapo mamlakani. Ukitumwa kuwatupia gongo,ukinaswa na chatu mwenye
kiu ya damu,umejitoa kafara mwenyewe.
Najua watu
wajinga wapo wengi wenye kuchochea wenzao wafe ili wapige kelele nyingi kwamba
Haki za Binadamu zinavunjwa. Kila mtu atazame haki yake ya uhai kwanza.
Mara
nyingi,hawa wapiga domo wanaoitwa wa Haki za Mashoga, haki za akina mama, haki
sijui za Binadamu,huwavisha ngozi za kondoo raia wanaopenda kukaa-kaa vijiweni
saa za kazi, ili wakararuriwe na wanyama wakali!
Nawashauri watu kuwa ‘Busy’ na mambo yao na
kazi zao,tuachane na Politiki saa za kazi,maana hakuna mtawala atayekuja
kutugawia sembe na maziwa kila nyumba,bila kufanya kazi
Kanali
Muammar Gaddafi, alikaribia kuwagawia maziwa raia wake kila subuhi,lakini wapo
waliomkana, akauzwa kwa Wamarekani, na sasa yuko Kaburini, mtoto wake,Saif
al-Islam anakabiliwa na kitanzi.tazama historia ili kujua kesho.
George
Orwell anawafananisha nguruwewa SHAMBA LA WANYAMA na viongozi na unyama wao dhidi ya raia waliojidai
kuwapenda sana.
Mwanafalsafa
wa Ugiriki, Salon amewafananisha viongozi ho na wanyama wakubwa
wanaoichanachana sheria na katiba ya nchi na kujiendea zao wanakofuata maslahi
yao.
Sisi wadogo
ndiyo tunaswao na sheria. Usidanganywe kuvunja sheria na watu wakubwa-utanaswa
wewe wao watabaki. Utazame utando wa buibui ujifunze somo hili,wanaonaswa humo
ni akina nzi,mbu,sisimizi n.k Lakini,wakubwa hujiendea na kuuchana utando huo
wa bui bui. Tembo atanaswa katika ‘spider’s
web’?
Wakubwa
hukiuka maadili,na kwao si hoja.Hawnaswi na mkono wa sheria,hujiendea zao
salama. Usipoteze muda kuhoji jambo hilo,kafanye kazi zako, maana ni
historia,,bishana nayo upoteze muda na maisha bure!
Nawe wataka
kuvunja sheria za nchi?Wewe ni nzi, utanaswa katika mtedo wa
buibui(sheria),katika tawala za dhuluma, sheria wamewekewa wanyonge-wewe na
mimi, kutii ni njia ya kuokoa maisha,amini usiamini.
Tunisha
misuli uone,kesho utakuwa mshumaa katika tufani-Candle in Wind!
Usifuate
maoni ya watu wengi wajinga, Public Opinion. Jihadhari na maneno ya kijiweni.
Usimtupie fimbo chatu,utajuta. Utaumia. Usiwatupie polisi mawe wakiwa na
bunduki,utavuja damu puani. Usitumiwe kama kinyangarika.
Duniani,viongozi
wenye upendo na raia wao wanapokuwa madarakani,siyo wengi. Kiongozi hupenda
enzi na mamlaka yake kuliko raia,kuliko mke na wanaye. Sembuse wewe?
Nikupe
mfano. Karibia miaka 2,500 iliyopita,Mwanafalsafa aitwaye Euripides wa Ugiriki
aliandika kisa cha Admetus mfalme wa Thesaly kukabiliwa na mauti,hadi apatikane
mtu wa kujitoa mhanga ili afe badala yake.
Ndugu
zake,marafiki na baba na mama yake walikataa kufa kwa ajili yake. Ni msichana
mzuri,mpenzi wake aliyeitwa, Alcestis aliyekubali kufa badala ya Admetus.
Itaendelea
0786 324 074
Subscribe to:
Posts (Atom)