Wednesday, September 25, 2013
KAGAME NA MUSEVENI NI NOMA
APRILI 6
mwaka 1994,Rais wa Rwanda, Juvenal Habyariana, na mwenzake wa BurundI,Ntaryamirwa Cyprian,
wakiwa ndani ya ndege aina ya Falcon-50, wakatunguliwa kwa kombora na Waasi wa
Kitutsi,RPF.
Huu ndiy
mwanzo wa mauaji ya Halaiki ya Rwanda,nakichocheo cha vita Burundi na hata
Mashariki mwa Congo,JK Kongo.
Migogoro ya
Watu-tsi na Wahutu,inayotiwa mafuta na Mabwana wa Vita(WAR-LORDS)Paul Kagame na
Yoweri Kaguta Museveni,sasa cheche zake hutishia hata amani ya Tanzania.
Wakimbizi
maelfu wanakimbilia hapa Tanzania,kufuatia vita baina ya Wahutu na Watu-tsi wa
Rwanda,Burundi na hata walewaliotimkia Jamhuri ya Kongo,kwa sababu na muda
tofauti.
Tuwatazame wanaojiita
Waasi wa Congo,M-23,CNDP na FDRL wanaosababisha Jenerali Kagame aanze
kututukana huku.
FDRL(Democratic
Forces for The Liberation of Rwanda) ni kikundi cha wanamgambo wa Kihutu ambao
ni adui wakubwa wa KAGAME na nduguze Watu-tsi.
Kama jina
lao lilivyo,baada ya mauaji ya halaiki, wakatimkia Congo ambako hata leo
wanaota kumtimua Kagame mamlakani.
Hawa,ni
Wahutu(raia wa Rwanda0 wanaompinga Kagame.
Sasa,Rais
Jakaya Kikwete akiwa Addis Ababa, akamshauri Kagame ambaye naye alihudhuria
moja ya mikutano ya AU kukaa meza ya mazungumzo na hao Waasi wa Kihutu wa FDRL
ili kuleta amani na utangamano Maziwa Makuu,likawa kosa kubwa kwa Kagame na kuanza
kurushamakombora ya kama alivyozoea.
Kingalipo
kikundi kingine cha wanamgambo wa Majimaj(Mai mai) ambacho pia kimejichimbia
misitu ya CONGO ,kinapeleka mauti huko Jamhuri ya Congo,kinaitwa ADC.
Ndani ya
Congo kuna jamaa zake Kagame na rafikiye,Museveni yaani M-23.
Jina hili
hutokana na tarehehe 23 Machi mwaka 2009,siku ambayo serikali ya Congo ilifikia
makubaliano ya Amani na kundi la Waasi wa CNDP,wakajumuishwa katika majeshi ya
serikali.
Naam, hawa
ndiyo M-23 Movement ambao ni kikundi cha Waasi kama 5,500 hivi waliojichimbia
Kivu ya Kaskazini na kuuza kifo kwa raia wa Kongo,na hapa kwetu wamesababisha
kilio kwa kupoteza wanaeshi wetu.
Wametokana
na misuguano isiyoisha baina ya serikali ya DRC na hawa wanaojiita Waasi kwenye
mipaka ya Uganda,Rwanda na Burundi.
Hawa M-23
wametokana na CNDP(Congress for the National Defence) kilichoanzishwa na ‘jamaa’
za akina KAGAME na Museveni,mmoja anaitwa Jenerali Nkundabatware,Desemba 2006
huko Kivu.
Januari,2009
CNDP Kilikosa umuhimu,kikaparaganyika,hadi eti Nkunda akakamatwa na majeshi ya
Rwanda,ambayo sote tunajua yalimpa chakula,nguo,fedha,silaha n.k
Sehemu ya
kundi hilo Iliongozwa General Bosco Ntaganda, ambacho kiliingia mkataba wa
amani na serikali ya Congo Machi 23, mwaka 2009.
Wapiganaji
hawa walipounganishwa na jeshi la Congo,CNDP kikawa chama cha siasa,wanachama
wao wakaachiwahuru magerezani.Rais wa kundi hilo akiitwa Askofu Jean-Marie
RUNIGA Lugerero!
Utaona ‘maaskofu’
wa siku hizi wakiongoza vikundi vya wanamgambo na kuua raia! Jihadhari sana na
wanaojiita Maaskofu,Manabii na Mitume wa siku hizi!!
Rais wa
kundi la M-23 akiitwa ‘General’Makenga Sultan-wote hawa mabwana wa vita
walikuwa CNDP.
Hawa hawakuwahi
kuaminiwa na serikali ya mjini Kinshasa,hata baada ya makubaliano,Rais Joseph
Kabila wa Kabange aliamuru Jenerali Nkunda akamatwe Aprili 11 mwaka 2012.
Hawa ni
Watu-tsi,ambao ni adui wakubwa wa kile kikundi cha Wahutu cha Democratic Forces
for the LIBERATION OF Rwanda(FDRL).Hawa wote wanaendesha harakati zao za
kigaidi ndani ardhi ya Congo,ndiyo maana kuna shida kila kukicha.
Bila shaka,
msomaji unapata picha kwamba, kuna vikundi vya Wahutu(FDRL) waliokimbia Rwanda
wakati wa genocide, walitimkia Cogon a huko wanaendesha harakati za kumpinga
Kagame.
Hawa Watutsi
walimsaidia Papaa Kabila(baba0kumwondosha Mobutu madarakani, na baada ya vita
hivyo,walijumuishwa katika majeshi ya serikali.
Hawa
Watu-tsi, wanapokea msaada kutoka Rwanda na Uganda, eti sasa mazungumzo ya
kuleta amani Congo hufanyika mjini Kampala chini ya usimamizi wa Kaguta Museveni!
Kichekesho kikubwa.
Majeshi ya
serikali ya mjini Kinshasa(FARDC) yamekuwa hayawezi kuwatimia hawa jamaa za
Kagame na Museveni huko Mashariki mwa Kongo,kwa sababu ambazo sasa tayari
umeziona kufuatia mfululizo wa makala haya.
Wakati
mwingine, majenerali wa FARDC walijidai kujisalimisha kwa Waasi,wakawapa zana
za vita na chakula katika kinachoitwa ‘mapigano makali’ ambamo Waasi wanawateka
askari wa serikali!
Wanafanya
usanii huo huku majeshi ya Umoja wa Mataifa(MONUSCO) yakiangalia hata ujambazi
unaofanywa kwa raia wa Congo.
Hawa MONUSCO
wakati mwingine kazi yao ni kupora madini na kuuza Ughaibuni,na wala siyo
kulinda raia wa Congo kama walivyotumwa na Umoja wa Mataifa,
Baada ya
majeshi ya Tanzania kujumuishwa katika jeshi la MONUSCO, sasa kampeni ya
kuwaswaga hao M-23 inaleta tija,wanapigwa ilivyo,ndiyo maana wanasisitiza
mazungumzo kuendelea Kampala,ili ikiwezekana warejeshwe jeshini
Kinshasa,viongozi wao wapewe mishahara na serikali ili wadumu kufanya ujambazi!
Watanzania
tunasema kwa uchungu mkubwa kwa sababu tumekwishamwaga damu ya askari wetu huko
Kongo, tayari M-23 ni adui yetu wa dhati,ndiyo maana Kagame anachuki ya wazi
kwetu.Ingekuwa heri Umoja wa Mataifa ungeongeza jeshi ili hawa waasi watwangwe
vilivyo,wanapoingia Rwanda kupewa chakula,nguo na bunduki,Rwanda wapewe kibano!
Kuna njia
tele za kuipa kibano serikali ya Kagame ikiwa ni pamoja na Vikwazo vya
kiuchumi, ama kunyimwa msaada wa kijeshi na kuuziwa silaha na mafuta.
Kuishinikiza
serikali ya Kinshasa kuzungumza na Waasi,wakati kukiwa na wakimbizi 200,000 au
zaidi wanaokimbia mapigano huko Goma,kuna leta ukakasi.
Kagame
akiambiwa kufanya mazungumzo na FDRL anakasirika;wakati hao M-23 wakitwangwa
vikali na maiti zao kubanikwa na majeshi ya serikali, kelele zinapigwa za
mazungumzo mjini Kampala!
Mazungumzo
hayo yalianza Desemba 9,mwaka 2012.
M-23
ilianzishwa rasmi Aprili 4,mwaka 2012 wakateka Goma kirahisi sana,kabla ya
Makomandoo wa Tanzania kuwachakaza vikali hao Waasi na kuwatimua Goma chini ya
mwamvuli wa MONUSCO.
Hawa jamaa
za Kagame sasa wamejificha Rwanda! Inasemwa wako mpakani,huku makombora
yanapodaiwa kutua Rwanda ili kuwasindikiza huko,ama wanafanya mchezo wa
kuchongea kwamba MONUSCO wameivamia Rwanda!
Rais Kikwete
anapotaka Rwanda inayoongozwa na serikali ya RPF(ya Watu-tsi) kukaa meza moja
na Waasi wa Kihutu,FRDL waliokimbilia Kongo ili kuongeza vurugu huko maana yake
nini?
· Kwamba,ni mazungumzo ya amani
wanayotaka Kagame na Museveni na jamaa zao wa M-23 waongee na serikali ya mjini
Kinshasa.Ni sawa na namna ambavyo Kagame angezungumza na FDRL ili kuleta amani
Maziwa Makuu.
· Hata RPF(Rwandan Patriotic Front)
walipokuwa Waasi wa Rwanda walianza kuzunguza na Habyarimana.
· Mazungumzo ya mani(Peace talk and
cease fire agreement)mwisho huweza kuzaa mikataba ya amani(peace accord) na
kuleta amani na utangamano kati ya nchi za migogoro.
Sasa tujiulize Kagame anapojidai kutuliza uhasama kati ya Watu-tsi na
Wahutumbaada ya genocide mwaka 1994, anaposhauriwa na Kikwete kuzungumza na
FDRL anakasirika nini?
Ili kuleta usalama Mashariki mwa Kongo Waasi wa M-23,CNDP,Maimai n.k
wanapozungumza na serikali ya Kabila mjini Kampala, si busara pia Kagame
kuzungumza na Wahutu wa FDRL mezani sasa ili kualiza vita Ukanda wa Maziwa
Makuu?
Mbona hata Waundi wamekuwa wakipatanishwa na akina Nyerere,Mandela,Bill
Clinton,Mwinyi n.k
Hawa walitia saini makubaliano ya
amani mjini Arusha mwaka 2000 chini ya Mandela na Clinton.
Ndiyo maana,wanamgambo wa Kitu-tsi walioko Kongo tunasema wametumumiwewa
kuangamiza Wahutu waliokimbiliahuko! Wahutu nao ni binadamu,wahurumiwe.
Rais Kikwete anajua mambo haya, alipomwambia Kagame kuzungumza na FDRL
ligusa kizinga cha moto wa visasi,moto ukalipuka.
Wapo watu wanasema:
“Kikwete,kama siyo kuropoka,imemhusu nini kuingilia Rwanda dhidi ya Waasi
wa FDRL?”
Swali la kijinga kwelikweli!
Hawa waasi ama Wakimbizi wa Rwanda wanapokimbilia Kongo,hususan Wahutu
wanapoleta balaa la vita huko, ama wanapokimbilia kwetu,Kagame na Museveni
hawatakuja hata huku kwetu kuwasaka Wahutu ili kulipa kisasi?
Tumeeleza kisa cha mauaji ya Kanungu zama za Kibwetere.
Tumezungumza umuhimu wa Amani Maziwa Makuu.
Wanamgambo wa Intarahamwe-adui za Kagame-ni wakimbizi wa vita kama
wakimbizi wengine.
Sheria gani inasema wawindwe na kuuliwa tena katika ardhi ya Kongo?
Kwa nini wasizungumze kama Kongo wanavyozungumza?
Mbona tunazuia genocide(1994) ili kufanya genocide nyingine dhidi ya
Wahutu wa FDRL?
R
TUNAHESABU MAITI ZA MAGAIDI
·
Al-Shabaab!
Al-Qaeda?
Tumechoka kuhesabu maiti
Na Conges Mramba
MATUKIO ya Ugaidi yaliyotokea jijini
London ,Uingereza, na kuua zaidi ya watu 50 mwaka 2005, yanaonyesha kuwa Tony
Blair na George Bush, wakati huo walikuwa wameshindwa kudhibiti ugaidi kwa
matumizi ya nguvu(Aggressive power); badala yake kilichotakiwa sasa ,ni njia za
kidiplomasia.
Diplomasia haikutumika wakati
huo,wala haikutumika wakati waSeptember 11 huko Marekani.
Dunia,ikiwemo Afrika,hususan Bara la
Afrika tenaMashariki huku,tumeumia maradufu kufuatia kipigo cha magaidi!
Tangu matukio ya Septemba 11,2001
yametokea matukio makubwa mengi sana ya ugaidi duniani; na nchi za Iraq
na Afghanistan ziliposhambuliwa na Majeshi
ya Uingereza na Marekani na kisha kupinduliwa, hakuna amani iliyopatikana.
Ulimwengu ulitegemea kwamba, baada
ya serikali za Wataleban na Saddam Hussein kupinduliwa Afghanstan na Iraq ,
sasa ulimwengu ungekuwa mahali salama, lakini badala yake sasa ni kiama cha
mabomu ulimwengu mzima.
Siyo ulimwengu ulioendelea kiulinzi,
na wala siyo nchi masikini kama hizi zetu, sote twagugumia machungu ya mabomu
mtindo mmoja!
Agosti 7,1998 mabomu yalipolipuliwa
katika ubalozi wa Marekani Nairobi na Dar es salaam, na kuua watu 224,ilisemwa
kuwa ni kwa sababu ya umasikini wetu, rushwa na miundo mbinu dhaifu ya ulinzi
dhidi ya magaidi.
Mwaka 2002,Machi 21, bomu
lililotegwa garini liliua watu tisa katika ubalozi wa Marekani mjini Lima ,
Peru .Ikasemwa hivyo, kwamba ni nchi dhaifu.
Oktoba 12,mwaka huo wa 2002, mabomu
yalilipuka katika klabu ya usiku mjini Bali , na kuua watu 202.
Wakati wa milipuko ya Septemba 11,
wakauawa zaidi ya watu 3,000 .hatua zilianza kuchukuliwa dhidi ya ugaidi.
Maana, ilionekana sasa magaidi hawakuwa wakitania.
Huu ni wakati WTC ilipogeuka Ground
Zero,na kifusi chake ni mnara wa kumbukumbu za magaidi,kifusi kimejaa ekari
moja!
Walishakamatwa magaidi kama akina
Riduan Isamadun, au Hambali, waliohisiwa kushiriki kiama hicho cha Septemba 11
. Alikamatwa pia Khalid Sheikh
Mohammed na wengine wengi.
Magaidi wengi walishakamatwa Iraq na
Afghanistan na kupelekwa Guantanamo Bay , lakini uovu unaendelea
tu.Ilichokipata Marekani, ni lawama za kukiuka haki za Binadamu.
Licha ya Osama Bin Laden, Mullah
Mohammed Omar na Abu Musab Al Zarqawi kusakwa sana , bado ugaidi ni kitisho
kikubwa kwa maendeleo ya watu Duniani.
Obama ameuawa na Carlos kafungwa
maisha,lakini ugaidi ungalipo.
Licha ya Tawala zilizodaiwa
kuwafadhili hawa majaili kupinduliwa, bado mabomu yanalipuka mahali popote
magaidi wanapoona panafaa yalipuke.
Agosti 19,2003 bomu lilipolipuka
katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, mjini Baghdad , na kuua watu 22,
akiwemo mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, De Mello, ulimwengu
ulipata kitisho kikubwa, kwamba ulimwengu mzima uko hatarini.
Hata Umoja wa Mataifa?
Hata hivyo, mabomu ya 2005 ya London
, yaliyoua zaidi ya watu 50, na kuharibu miundombinu ya reli katika jiji hilo
maarufu sana duniani, ni hatari zaidi!!
Msiseme Nairobi,Dar au Kampala!
Mbona New York,Washington na London ni miji iliyolipuliwa?
Tatizo watu hawana kumbukumbu,wamekalia siasa
za kuchoma magogo na matairi barabarani!
London, ni jiji lenye ulinzi wa hali
ya juu.Taasisi za ulinzi, upelelezi au ujasusi zilizopo London ni maarufu mno
duniani, na huogopwa ulimwengu mzima.
Lakini jinsi mtandao katili wa
Al-Qaeda ulivyojipenyeza na kupiga mabomu njia za reli za chini kwa chini(tube)
na mabasi, ni kitisho zaidi; na mashambulizi haya yanatosha kutufanya tuamini
kuwa mkakati wa Bush na Blair,Cameron na Obama kupambana na ugaidi kwa kutumia
nguvu(Aggressive Power) umepitwa na wakati.
Dunia ikae mezani kutazama
magaidi(ama wawe wanaharakati,walipa visasi n.k) wanatakaje ili kutuliza
mizuka?
.Magaidi wamesakwa sana, wameuawa
sana, lakini wamaomgezeka na kuua watu wengi mahali popote bila kuogopa umahiri
wa ulinzi, au utajiri!Marekani, Uingereza, Kenya na Tanzania zote zimepigwa na
Al-Qaeda!!
Kama majahili hawa wameweza kufanya
unyama mkubwa London , New York na Washington, ni wapi wataogopa?
Walipopiga Nairobi, Dar es salaam ,
Bali na ofisi za Umoja wa Mataifa, Baghdad , ilionekana ni udhaifu wa ulinzi.
Ilipopigwa miji ya Washington na New
York (Septemba 11) ilisemwa kuwa watakomeshwa.
Tumeona Osama akisakwa, utawala wa
Taleban na Saddam ukiangushwa, na kumfanya Saddam kuwa mateka na mfungwa katika
mji wake Mkuu aliotumia kuitawala Iraq , Lakini mabomu yanaendelea.
Saddam,Osama,Gaddafi wameuliwa
lakini mabomu na risasi vimerindima duniani,sasa West Gate,NAIROBI!!
Irak,Libya,Misri,SYRIA nk hamkani si
shwari tena.
Mtazamo wangu ni kuwa iko haja ya
Umoja wa Mataifa kujua kwamba Blair na Bush siyo majemadari tena wa vita dhidi
ya ugaidi duniani; wameshindwa vibaya; kwa kuwa miji yao mikuu imepigwa na
maelfu ya watu kuuawa.Iko siku nao watapigwa na kuuawa!
Hawa Cameron,Obama,Bush na Blair, sasa hawana jipya
la kuuhadaa ulimwengu kwamba ugaidi utatokomezwa.
Vita dhidi ya ugaidi, War Against
Terrorism, ni danganya toto!
Ni wajibu wa Umoja wa Mataifa kukaa na
kutafuta mbinu sahihi za kuondoa kitisho hiki, badala ya kuwategemea hawa akina
Bush, Obama,Hollande na Blair, walioshindwa vibaya na kwa aibu.
Hivi ulimwengu ungekuwaje mabomu ya London yangeelekezwa Gleneagles, walikokuwa
wakifanya mkutano wakuu wan chi tajiri zenye viwanda, G-8?
Bush, aliyeongoza vita dhidi ya
Afghanistan na Iraq , alikuwepo, na wengine wengi walikuwepo Scotland , mabomu
yalipolipuka.
Nataka kusema kuwa, kufuatia mkutano
huo mkubwa, na ulioandamwa na waandamanaji, kulikuwa na ulinzi mkali eneo zima
la Ufalme wa Uingereza, Lakini mabomu yalilipuka na kuua watu 52.
Hii ni kuonyesha kuwa iko siku
magaidi watapiga ikulu zote duniani, na kuleta msiba mkubwa.
Kwanini isitafutwe njia nyingine ya
kupambana na ugaidi, badala ya kutumia ubabe wa akina Bush na Blair?
Obama,Cameron,Hollande?
Miongo michache iliyopita, Uingereza
ilikuwa katika kitisho cha mabomu ya vikundi kama Irish Republican Army(IRA),
ambao sasa hawafanyi tena hujuma, kwa sababu Ireland inao uhuru na Haki
zilizokuwa zikitafutwa.
Serikali ya Uingereza ilitambua
madai ya magaidi hao wa IRA, na amani ikawepo.
Kwa mantiki hii magaidi ni binadamu
wanaofanya vitendo vya kinyama, ili kupata haki zao.
Ugaidi siyo ujambazi unaoandamana na
tamaa tu
. Bali , ugaidi ni harakati za
kutafuta maslahi Fulani.Wakati Fulani wanaharakati kama Martin Luther King,
Kanali John Garang, Museveni, Marehemu Samora Machel na wengine, walionekana
kama magaidi, lakini leo tuna waona mashujaa wa watu wao.
Hii ni kusema kuwa hawa magaidi
wanayomadai yao , ambayo Umoja wa Mataifa lazima uyatazame, na kuyatafutia
ufumbuzi.
Kama Kanali Gaddafi, wakati Fulani
ikulu yake ilipigwa mabomu na Marekani, hadi mwanaye akauawa, na leo
inasemekana nchi yake imekoma kuunga mkono ugaidi, hata Osama angeweza
kubadilika, kupitia meza ya mazungumzo!
Gaddafi baadaye aliuliwa kwa sababu
eti za kuwaita waasi mende,panya!
Ulimwengu unataka amani, hivyo
zitafutwe njia elfu kukomesha ugaidi, kwani Bush na Blair Obama na Cameron
wameshindwa sana ; hata miji yao yote mikuu imepigwa hadi maelfu kuuawa
.Magaidi hawana nchi, hawana mipaka,
hivyo wamepata ushindi wa kishindo, yapaswa wakabiliwe kidiplomasia, ili
kuondoa kitisho.
Tumecoka kusesabu maiti na ndoo za
damu inayomwagika!
Hivi leo mtu aweza kusema Bush na
Blair,Obama,Cameron na Hollande wataweza kuifanya dunia mahali pa salama?
La hasha… wameshindwa tangu Iraq , Afghanistan
, Afrika, Asia na hata jirani na Ikulu zao.
Shime, Umoja wa Mataifa utafute njia
mbadala ya kupambana na ugaidi; la sivyo tutateketea kwa mabomu ya majahili
hawa
0713 324 074.
J
|
AL SHABAAB NAIROBI PIGO KWETU TANZANIA
Na Conges Mramba
Jumatano, Agosti 7 mwaka huu
tulikumbuka mashambulizi ya magaidi yaliyofanywa katika Balozi za Marekani,
Dar es salaam na Nairobi ; mwaka 1998
.Na juzi tu,tukakumbuka matukio ya Septemba 11,mwaka
2001.Leo tunaomboleza,West Gate Nairobi.Watu takriban sabini wamekufa,wengi
wamejeruhiwa vibaya!
Zaidi ya watu
240 walikufa mwaka 1998; hawa hawakuwa wa Kenya pekee bali pia wa
Tanzania . Hawakuwa wa kabila moja au wa dini fulani, waliokuwa
wakisali msikiti mmoja ama kanisa fulani.
Magaidi ni hatari kwa raia wote wa
dunia.
Tunawaombolezea
waathirika wa tukio hilo la Agosti 7 mwaka huo wa 1998, ambalo msingi mkubwa
ni uadui kati ya Marekani na Waarabu walioamua kuisaka Marekani popote
duniani, ili kulipa kisasi.
Naam,kuisaka
Marekani katika ardhi yetu, kusababisha hasara ya maisha na mali za watu
wetu, ni vitu tunavyovipinga leo na kesho hata kama mbingu zishuke; ama jua
litue mchana saa saba!
Hata mgogoro wa Somali ni matokeo
ya Vita Baridi kati ya Urusi na Marekani na washirika wao,sisi tunapokwenda
kupambana na al-shabaab ama al-Qaeda,maana yake twapambana na mabaki ya
minyukano ya Mashariki na Magharibi.
Si lengo la ukurasa huu kusema kwamba magaidi ni Waarabu peke yao, ama watu
wa imani fulani. Nitajadili malengo ya ugaidi na chimbuko lake. Nitajadili
imani inavyoupa msukumo na nguvu ugaidi duniani.
Kuna vikundi tele vya kigaidi duniani. Usishangae, hakuna gaidi anayejiita
gaidi.
Wote
wanajiita, wanaharakati(activists) wa ‘Haki’ za ubinadamu wao. Ugaidi unakula
maisha ya watu na mali vinapopotea au kuharibiwa.
Kila
mmoja ana tafsiri yake ya ugaidi. Sitajali kusikia Rais George W. Bush wa
Marekani naye ni gaidi kama Osama bin Laden.
Hata hivyo,
najua, magaidi kama wale waliolipua Balozi la Marekani Dar es salaam na
Nairobi, Agosti 7 miaka 10 iliyopita, wote ni wauaji; wanastahili adhabu
kali.
Walioua watu
Nairobi nao wanastahili adhabu kali.
A-Qaeda ni kundi la harakati za kigaidi, bila kujali wanaharakati wake
wanatokana na itikadi gani. Japan, kuna kundi moja linaitwa, “Ukweli Mkuu”
kwa Kijapani, Aum shinrikyo-hawa nao hata wakifanya mauaji, watasema wameua
ili kuueneza huo Ukweli(The supreme Truth). Mauaji hayaenezi haki yoyote.
Uhispania, kuna kundi linaitwa, ETA(Freedom for The Bosque
Homeland), nalo linadai uhuru. Lebanon , kuna kundi maarufu sana kama ,
Hezbollah(Chama cha Bwana Mungu), wakati Ireland Kaskazini kuna kundi
liitwalo, Irish Republican Army(IRA).
Nchini Israeli,
kitovu cha uadui wa mgogoro wa Mashariki ya Kati, kuna kundi liitwalo, Kach
and Kahane Chai, Uturuki kuna PKK(Kurdistan Peoples Party), Sri Lanka kuna,
Liberation Tigers of Tamil Eelam(LTTE); wakati nchini Iran kuna Mujahedin-E-Khalq.
Ugiriki kuna kundi
linaitwa, November 17 Revolution.
Juzi tulisikia kundi la FARC(Revolutionary
Armed Forces of Columbia) likifanya utekaji nyara; lakini ni ‘Jeshi la
Kimapinduzi’.Jeshi la kimapinduzi hupindua raia?
Hakuna anayemaizi
kuwa matendo yake ni kinyume cha sheria za nchi, za kimataifa, ama ubinadamu.
Wengine wanajisingizia, wametumwa na Mungu ili kuwaua binadamu wenzao,
waabudu sanamu ama wapagani.
Wapo, Shining Path kule
Peru . Columbia pia kuna National
Liberation Army(ELN),
na Ufilipino kuna New People’s Army.
Tumjadili
kidogo tu, gaidi la kale, Ilych Ramirez Sanchez, ambaye kwa utani anaitwa,
Carlos The Jackal-mzaliwa wa mjini Caracas , Venezuela . Venezuela , ni nchi
aliyoongoza Hugo Chavez, ambaye alimtukana rais Bush, wakati anahutubia
Mkutano wa Umoja wa Mataija, jijini New York , akapewa saa chache awe
ameondoka nchini humo.
Chavez alishakufa akabaki Nicolas
Maduro.
Carlos, gaidi
anayetumikia kifungo cha maisha Ufaransa, ikifika Oktoba 12 mwaka
huu, atakuwa anaadhimisha miaka 59 ya kuzaliwa kwake.
Sasa, huyu jamaa
katika mafaili ya uhalifu na Jinai duniani, kuna mambo yake mengi, ambayo
yametokana na chuki za siku nyingi kati ya nchi za Amerika ya
Kusini(zilifuata siasa za Carl- Marx) na Marekani. Carlos, ambaye baba yake alikuwa
mjamaa, alimpeleka Chuo Kikuu cha Patrice Lumbumba, mjini Moscow , kusoma.
Huko alikutana na
Wapalestina, akaiva katika siasa za mrengo tofauti na ubeberu wa Kimarekani.
Hata jina
‘Ilych’ aliitwa na babaye ili kuwaenzi ‘makomredi’ wa Urusi ya Ujamaa,
akina Lenin.
Sasa Carlos anaipinga
Marekani hata huko jela, alishasema alimuunga mkono Osama bin Laden, kwa
asilimia 100; na kwamba anawataka watu wasiache kujitoa mhanga ili kufa na
Wamarekani, popote walipo!
Nitajadili kauli hii
baadaye kidogo. Hata hivyo, huyu jamaa aliyetiwa mbaroni na mashushushu wa
Ufaransa akiwa mjini Khartoum, Sudan alishakaa Urusi tangu 1968, amekaa
Ujerumani mwaka 79, amekaa Syria 91-93, na Ufaransa. Vituko vyake unaweza
kuvipata katika sinema za akina James Bond.
Hapa, nitajadili ugaidi, si
Carlos.
Naam, ugaidi wa Agosti 7 mwaka 1998, ulileta hadithi
nyingi. Lakini, tuseme kwamba wale magaidi walishambulia Balozi za Marekani
Dar es salaam na Nairobi , karibia muda uleule mmoja, kwa sababu nchi hizi
hazikuwa zimejiandaa.
Wengine wanasema hata
Kampala ingeshambuliwa. Kilichoiponya ati ujio wa Rais Bill Clinton wakati
ule mjini Kampala , ulivifanya vikosi vya usalama vya Uganda kuwa ‘more
alert’ kuliko Dar na Nairobi ! Hayo tuyaache.
Kampala
ilishambuliwa na al-Shabaab mwaka 2010 wakati wa Kombe la Dunia Afrika
Kusini.
Shambulizi lingine la magaidi Afrika Mashariki lilifika Novemba 28 mwaka
2002.
Magaidi waliua watu 16 mjini Mombasa, katika
hoteli ya Paradise iliyoko Kikambala. Ni kilomita 25 kutoka mjini Mombasa.
Hii hoteli ni ya Waisraeli; sasa unaweza kukisia hata wewe, kwamba ilishambuliwa
na adui zao Wapalestina. Wapalestina walikuja Afrika Mashariki kuwawinda adui
zao Waisraeli, katika ardhi ya Kenya. Hawakuua Waisraeli tu, waliua na
Wakenya, na raia wa mataifa mengine.
Sasa tuseme, vita vya kudai uhuru vinavyoendeshwa na Wapalestina dhidi ya
Mayahudi, vina leseni ya kuua na kuumiza binadamu wengine wasio na hatia?
Halafu, hao magaidi wa Kipalestina walifanya jaribio la kuilipua ndege ya
Arkia Airlines ya Israeli, iliyokuwa ikiruka kutoka uwanja wa ndege wa Moi,
mjini Mombasa. Bahati tu, lile kombora, bila shaka la Kirusi, liliikosa- kosa
ndege ile iliyokuwa na abiria 271 hivi.
Fikiria, kama kombora lile lingeipata ndege ile,wangekufa Waisraeli pekee?
Hata raia wa mataifa mengine, wasiojua uadui
waa Israeli na Wapalestina wangeungua katika miali ya moto wa mlipuko. Sasa
ugaidi unasura ya ukombozi au uokozi na uhuru wa wapi?
Narejea mada yangu ya madhara ya ugaidi Afrika Mashariki. Matukio yote ya
ugaidi yalisababisha watu mamia kufa, inakisiwa kulitokea hasara ya dola
mabilioni. Ili kuponya majeraha ya ugaidi, zimetumika dola matrilioni, ambazo
pengine zingetumiwa kuleta maendeleo-ugaidi ni adui wa maendeleo ya watu.
Nimesema magaidi wapo Wazungu kama IRA, na wa mataifa mengine kama akina
Carlos The Jackal; lakini ni magaidi. Magaidi hawana rangi, dini ama taifa
moja.
Ugaidi ni mauaji ya kinyama yanayoendana na matakwa ya ulipaji kisasi.
Pengine, magaidi kama Black Banners wa Iraki, wakati ule wa vita, waliwateka
jamaa watatu wa Kenya, ili kutafuta fedha kutoka kwa makampuni waliyofanyia
kazi.
Sasa nijadili jambo ambalo watu hupenda kunitolea matusi. Watoa lugha
chafu, hawana weledi juu ya lolote. Silaha yao ni matusi na vitisho.
Wanadhani, ukweli ni ule unaolingana na wanavyopenda, ama wanyofikiria wao.
Hata hivyo, ugaidi ni unyama, hata Mungu mahali popote hajawahi kusema watu
walipizane visasi. Sera za ‘Jino kwa Jino’ ama ‘TIT FOR TAT’ ni za Ibilisi.
Mungu anawataka watu kutong’oana meno, ili kulipa baya kwa baya?
ungu
anawataka watu wawe vibogoyo au chongo?
Juzi,
Papa Benedict XVI ameungama kwamba Kanisa Katoliki nalo lilishafanya ugaidi.
Ugaidi hauna rangi, kanisa, msikiti wala watu wa kabila moja.
Nilipata kutukanwa na hawa jamaa kwa kupinga kauli ya Carlos, kuwataka watu
kufuga midevu mingi kama shamba la miwa la Kilombero, halafu eti
wasiache kujilipua ili kuwakomesha Wamarekani, popote watakapowaona!
Sasa kama
Carlos kawaambia, kwa nini wasiende kujilipua New York au Washington ? Kwa
nini Mombasa , Nairobi au Dar? Huku Wamarekani hawapo!
Mkijilipua huku mnatuumiza sisi, wao hawapo.
Kama wapo ni mmoja tu au wawili-wafuateni Wamarekani kwenye uwanja wa
mapambano! Wenye uwezo walikwenda kulipua New York na Washington, Septemba 11
mwaka 2001; hadi leo historia inaelekea kuwasahau.
Sipendi kuamini kuwa,
mtu mwenye uwezo wa kufikiri anaweza kuwa’Shahidi’ mwaminifu wa imani
yake(uwe Ukristo,upagani ama Uislamu)kwa kujilipua, ili afe yeye na kumuua
adui!
Huku ni kushika dini
kupita kiasi(fanaticism), kunakogeuza dini kuwa vifo na mauti, kwamba ni ushahidi(martyr).
Hii si Jihad halali kuua hata watoto wasio na hatia, kwa sababu tu walikaa
meza moja na adui.Kwa nini kuua adui mmoja kati ya ndugu mamia?
Najua vita kati
ya Waisraeli na Waarabu wa Mashariki ya Kati, inaitwa ‘Vita kati ya wema na
uovu’. Sasa kama
pande mbili zinaua hata wasiohusika, mwema nani na mwovu ana alama gani?
George Bush na Tony Blair, wakati wanaishambulia Irak, walisema ni vita dhidi
ya watu wasiostaarabika. Wakati magaidi waliposhambulia London, wakasema ni
vita dhidi ya ustaarabu.Sasa tujiulize pia, kuua watu wasiohusika hata huko
Irak ni ustaarabu? Ni kwa sababu hii, safu hii inasisitiza kuwa mauaji ni
jinai, na kila muuaji ni Ibilisi mwenye mikia saba.
Hakuna kitabu kitakatifu kinachotuma watu kuwaua wenzao wasioamini ama
waabudu sanamu. Ndiyo maana hapa Tanzania si lazima kwa mujibu wa Katiba mtu
kuwa dini fulani.Hata wapagani na waabudu sanamu ni watu; wasiuawe kwa
kutokuwa na dini kwao.
Nasema hivi kwa sababu
rafiki yangu aliniambia, Allah kasema kuua hawa walao nguruwe ni kupata
thawabu hata akhera!(to be elevated to a higher plane of existence, where
life is an eternal bliss).
Ni kwa sababu hii,
msomi na mhadhiri, Imam mashuhuri anasema kila siku, kwamba Kuran
inakataza kabisa kuua au kujitoa mhanga-na kwamba wanaofanya hivyo, hawafanyi
kwa jina la Uislam; bali wanasaliti mafundisho ya Mtume Muhammad.
“Hatutaruhusu
imani yetu adhim kutekwa nyara na wahalifu”, alisema.
Maneno kama haya kayasema Kiongozi
wa Upinzani Bungeni juzi, Hamad Rashid Mohamed, alipokuwa akitoa hutuba fupi
wakati wa kuaga mwili wa Chacha Zakayo Wangwe, “Rasta” wa Tarime. Buriani
Chacha Wangwe.
Hamad Rashid,
alisema alikwaruzana na Marehemu Chacha Wangwe, lakini wakasameheana, kwa
sababu, Kuran inasema, ‘kusamehe ni lazima’ ili upate thawabu.
Biblia inasema kusamehe ‘saba x
sabini’ maana yake siku zote za maisha. Saba ni alama ya ukamilifu wa
utimilifu; hivyo tusichoke kusamehe.
Sasa
hata hapa mtanitukana na kutishia kunipiga kwa kuhimiza amani? Mungu gani
kawaambia kumpiga mwenye mawazo tofauti nanyi? Dini yenu ni ya amani,
kwa nini Jino kwa Jino?
Nilishasema katika makala mbili zilizotangulia, kwamba kuna upendeleo na
‘double standards’. Alichofanya Bush au Blair, akikifanya Mugabe au
Mpalestina, ataitwa gaidi, wao “Patriots”.
Hili
ni tatizo ambalo haliondolewi kwa watu kujilipua, lawama hizi haziondoki kwa
kujifunga mabomu. Hatupambani na ‘metropolitan power’ kwa kulipua Dar,
Mombasa na Nairobi.Tunatakiwa kuilipua Washington kisayansi, maana yake
kumlipua Bush pekee bila raia wasio na hatia.
Ukijifunga bomu utamlipua Blair au Bush? La hasha.
Utawalipua ndugu zako wa Dar, Mombasa ama Nairobi. Tutafute njia mwafaka ya
kuondoa ‘double standards’ duniani. Tusijiite,
“Liberators” ama ‘in the service of’ Allah’ kumbe wauaji wa ndugu zetu
wenyewe.
Tusidhani tunakomboa,
kumbe tunajiua! Kujiua ni dhambi kubwa na kosa katika sheria za binadamu na
Allah. Mashahidi
waaminifu wa imani, hawatoki msikiti fulani tu, hata sinagogi au kanisa.
Je,
hamjaona watu wakienda uwanja wa ndege na biblia pasipo nauli,hati za
kusafiria wala visa wakadhani Mungu atawapeleka Ulaya kuhubiri? Huku nako
kujifunga mabomu! Magaidi hawana dini moja.
Nimalize, kwa kusema
Kuzimu kumepanua kinywa chake. Kuna visasi vingi tangu matukio ya Septemba 11 mwaka
2001. Lakini, tuangalie faida yake nini? Nani kasema ukifa kwa kujilipua kwa
bomu na kuangamiza Mzungu mmoja na Waafrika wenzako 200 ni thawabu? Imani
zisitugawe;sisi ni wamoja hapa Tanzania ama Afrika.
Tutafakari msugoano uliopo kati ya Magharibi na Mashariki. Leo, siasa za
akina Hugo Chavez, zinashindwa. Akina Carlos The Jackal wanaonekana majambazi
tu, hata kama walifanya kazi bega kwa bega na makomredi kama Fidel Castro,
katika kuzuia ubeberu.
Hatuwezi kuupinga ubeberu kwa kuangamizana Paradise Mombasa, au katika
usafiri wa ndege kama ile ya Arkia Airline, ama wa treli London.
Hata
katika balozi za Wazungu, kama Dar, Kampala na Nairobi, ukijilipua hukosi
kuua Mzungu mmoja na Waafrika wenzako 300. Kuna thawabu gani hapo?
Tufanyeje sasa? Tufikiri kwa makini; tuepuke kutukana watu, kupandisha mizuka
ili kuhuisha roho ya kisasi. Tutaushinda uadui kwa akili na imani, si
imani bila busara. Busara hutoka kwa Mungu.Kwa mungu kuna haki na thawabu.
Mungu ni wa utaratibu, si wa machafuko.Palipo na machafuko, hapana Mungu. Na
sheria ni msumeno.
. Ukweli si ule unaomfrahisha mtu; ukweli ni mchungu lakini mtamu. Ukweli ni
ubinadamu. Tuimarishe ubinadamu-humanity.
Ndivyo
tunavyoikumbuka Septemba 11 mwaka 2001,tunawapa pole Nairobi kwa kipigo cha
al-SHABAAB,
www.congesmrambatoday.blogspot.com
0754 324 074,0786 324 074 |
Subscribe to:
Posts (Atom)