Monday, November 25, 2013

SHAMBA LA WANYAMA TANZANIA HII?




Mwandishi wa kitabu maarufu, ‘SHAMBA LA WANYAMA’,George Orwell,jina lake halisi ni Eric Blair.
Alizaliwa India mwaka 1903, ambako babaye alifanya kazi kama Ofisa wa serikali huko Bengal.Akiwa mtoto,Eric Blair alipelekwa Uingereza, akasoma shule binafsi ya Eton, ambayo ilikuwa bora sana zama hizo.
Wazazi wake walikuwa makabwela.Hivyo, Blair akaishi katika madhila ya ufukara;maisha ambayo yalimfanya kudharauliwa na jamii ya Kiingereza yenye ukwasi.
Mwaka 1922, akajiunga na jeshi la polisi Burma, siku hizi nchi hii huitwa Myanmar.
Burma, ilitawaliwa na Uingereza kwa mkono wa chuma,kinyume na matakwa ya raia.Siku hizi Uingereza inaimba wimbo wa ‘Demokrasia’ kumbe kawimbo ‘demokrasia’ katamu,lakini waimbaji wake hunuka mithili ya kwapa la Ibilisi! Unafiki tu!!
Eric, alipopata likizo akarejea Uingereza ambako alikaa muda wa likizo ukapita-hakurejea Burma.Alijisikia vibaya sana kutumika katika jeshi la Kiingereza kuwakandamiza raia wa nchi hiyo na matakwa yao.
Naaam, ilikuwa mwaka 1927.Eric Blair aliishi London,na wakati mwingine mjini Paris,Ufaransa ambako aliishi katika lindi la ufukara wa kupindukia.
Aliishi sanjari na watoto wa mitaani, ‘chokoraa’ na wasio na ajira waliolala vibarazani katika mitaa ya kitajiri.Na wakati mwingine aliishi na wasio na ajira, na waliolipwa  kiduchu mithili ya ujira wa mtwangaji.
Wakati mwingine, akaosha vyombo hotelini ili kujipatia mlo wa usiku hususan huko mjini Paris,Ufaransa.
Ni hapa, Eric Blair alipoanza kuandika kuhusu maisha yake ya kijungujiko.Kitabu chake cha awali kilichapwa kwa jina la GEORGE ORWELL,kwa sababu alisema alionea aibu jina lake halisi,Eric Blair! Ufukara!
Amewahi kuwa mwalimu, akaacha.Alifanya kazi dula la vitabu.Mwaka 1936 alimuoa Eileen Hertfordshire, wakaanzisha duka dogo la reja-reja.
Wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Hispania, alikwenda huko ili kupata cha kuandika kuhusu vita; akajikuta katika mapigano makali.Alijikuta akipigana bega kwa began a Republican-akajeruhiwa vibaya, akatimkia Ufaransa na mkewe ambaye waliandamana naye.
Mwaka 1938 George Orwell alikuwa mgonjwa sana, hata vita vya Pili vya Dunia vilipozuka(1939-44) alitamani kujiunga jeshini,lakini hakufanya hivyo.
Alifanya kazi kama Mwandishi wa habari.Mkewe alifariki ghafla mwaka 1944;wakati mwandishi huyu mahiri alipokuwa yungali mwenye afya mbovu.Wakati huo, alitumia muda mwingi katika korido za hospitalini ili kutafuta tiba.
Mwaka 1949,Orwell alimuoa Sonia Brownwell.Walipanga kwenda Switzerland, lakini Orwell akafariki dunia mwaka 1950.
Vitabu vingi vya mwandishi huyu mahiri duniani vinahusu madhila yaliyompata katika taabu,dhiki,kudharauliwa sababu za ufukara.
Baadhi ya vitabu vyake ni  Burmese Days, Down and Out in Paris and London vilivyohusu maisha ya ufukara katika miji mikuu ya Ulaya.
Homage to Catalonia, kinahusu vita Hispania, A Clergyman’s Daughter ni uzoefu wake katika kazi ya ualimu.
Aliandika Keep the Aspidistra Flying kama uzoefu wake katika duka la vitabu.The Road to Wigan Pier ni stori zake kuhusu maisha ya wasio na ajira Kaskazini mwa England, eneo la viwanda vikubwa.
Hata hivyo,George Orwell ni maarufu sana duniani kwa vitabu vyake viwili alivyoandika mwishoni mwa uhai wake.
“1984” ni kitabu cha kuogofya kuhusu maisha ya usoni(Future),wakati fikra za watu na maisha yao yatakapotawaliwa na serikali. Kwamba mwaka huo 1984 watu wasingeamua hatma ya maisha yao wenyewe-Udikteta.
‘ANIMAL FARM’ ni riwaya kali ya kejeli(satire) kuhusu wanyama-watu,akizungumza dhima ya Mapinduzi yaliyoshindwa ya Joseph Stalin huko Urusi.Si Urusi tu,kitabu hiki Animal Farm huonesha yanayojiri hata sasa hapa Tanzania.
Ujumbe mahsusi ni kwamba,tama ya madaraka ya viongozi huwaingiza walalahoi katika matumaini makubwa,kisha hugeuka watumwa wa kupindukia-hata humwaga damu yao ya thamani.
Baadhi ya “wanyama” katika riwaya hii kali huwakilisha watu muhimu sana katika taifa(Public Figures) na ambao hupendwa sana na mashabiki wao utadhani miungu-sacred cows ,kuwagusa inakuwa laana na kifo!
Ni maisha halisi ya wanyama hawa hata hapa unapopenda sana wewe bila akili tunduizi(critical mind).Nguruwe wajanja,wasomi waliojitia ku-“organize” wanyama wenzao ili kuondokana na utumwa ulioendeshwa na BINADAMU-Madhila ya utumwa na ukandamizaji hata leo tunao hapa hapa kijiweni petu-kila mtu na kijiwe chake.
Wanyama walikusudia kufanya MAPINDUZI uili kujenga JAMII YENYE USAWA! Jamii yenye usawa katika dunia hii hii eeh??
Taifa jipya la Wanyama walilokusudia baada ya mapinduzi ni lenye haki tupu,kweli,ubora na usawa, ambalo lingeleta Maisha Bora kwa Kila (Mtanzania)! Hapana, maisha bora katika shamba la wanyama-ANIMA FARM.
Kufuatia mawazo haya ya kimapinduzi, zilitungwa sheria, ama AMRI SABA(The seven commandments) ili kuwalinda wanyama.
Amri zote saba zilibeba maudhui na muktadha ya USAWA- “ALL ANIMALS ARE EQUAL”.Naam, usawa,usawia.
Nadhani msomaji umepata kusikia au kuona, ama vyote viwili-kuona na kusikia baadhi ya wanyama ambao ni ‘Public Figures’ katika Tanzania hii hii wanapotokwa mapovu mdomoni kuhubiri juu ya Tanzania yenye usawa,wakati ukweli halisi ni ubeberu na udikteta uliokamaa kuzidi wa mkoloni katili!
Nianze kukutajia AMRI SABA za wanyama wa George Orwell.Shamba la wanyama la Uingereza!
1.Kila aendaye kwa miguu miwili(binadamu) ni adui wa wanyama.
2.Kila aendaye kwa miguu minne au mbawa ni rafiki
3.Ni marufuku mnyama kuvaa nguo!
4.Ni marufuku wanyama kulala kitandani
5.Hakuna mnyama kufakamia kilaji(pombe,masanga,ulabu n.k)
6.Marufuku mnyama kuua mnyama mwenzake
7.WANYAMA WOTE WAKO SAWA
Amri hizi zote zilitundikwa ukutani,ili wanyama wote katika shamba hili la wanyama waishi na kuzifuata, na wanyama wote walisomewa kwa sauti ili wazisikie.
Kusudi ni kila mnyama kuondokana na utumwa,udikteta,ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka katika jamii ya wanyama-haki stahiki.
Ni ufisadi wa kutisha kwa wanyama hao wa George Orwell ulioendeshwa na binadamu.
Binadamu(binadamu mniwie radhi kusema haya) alikula bila kuzalisha chochote!(MAN IS ONLY CREATURE THAT CONSUMES WITHOUT PRODUCING)!
Binadamu HAMKAMULIWI MAZIWA,wala hamtagi mayai;ninyi ni dhaifu kupindukia hata hamwezi kukokota jembe linalokokotwa na wanyama kazi(plough).
Binadamu wala hamwezi hata kufukuza kasungura,mpaka msaidiwe na mbwa!
Mbwa akifukuza sungura,hutokwa jasho jingi na povu mdomoni; lakini mara anapokamata ‘Apwoyo’ sungura, binadamu humpora kasha huchukua minofu na kumtupia mbwa mifupa na matumbo! Mbwa hula makombo,pamoja na kulinda mali ya binadamu utadhani yake, wakati wa hatari, wa baridi,mvua-jua lake mvua yake!!
Eti huyu binadamu ndiye “Lord of all animals”, KATILI,mbinafsi ndiye anayeamrisha wanyama wote kufanya kazi na kumpa yeye chakula,kiburi na utajiri,anasa!
“Hata kinyesi cha wanyama ni mbolea.Kazi ya binadamu ni kulewa pombe na machangudoa,kulewa sifa na mafanikio hewa.”
Hizi kauli za wanyama zilitia simanzi.
Kwamba, ingawa wanyama ni chanzo cha mapato na kiburi cha mwanadamu katili, bado wanyama hawamiliki chochote wanachozalisha kasoro ngozi zao tu!
Ng’ombe hawamiliki hata galoni moja ya maziwa,miongoni mwa mabilioni ya papipa ya maziwa yanayokamuliwa kila mwaka na kuuzwa ama kunywewa kila siku!Kuku hawakuwa na haki hata ya kula yai moja.
Vyote,binadamu akafakamia.Kuku akila yai hata moja alilotaga, ni kosa. Mwisho wa siku hakuna mnyama anayenusurika kwa makali ya jisu! Kuchinjwa!!
Hata mbwa aliyejitia ‘rafiki’ wa binadamu,pindi anapozeeka na kuishiwa meno mdomoni, anaposhindwa kubwekea adui kwa maradhi na kuachwa nje kila siku, hufungwa kamba nene shingoni na kutupwa katika shimo refu, asiweze kuokoka!
Wenye masikio na wasikie.
Naam, kwa kifupi, sera za shamba la wanyama zilikuwa na mashiko,ili kuuelekeza umma wa SHAMBA LA WANYAMA kufanya mapinduzi=mabadiliko.
Maslahi ya wanyama hayakuwepo isipokuwa dhuluma,kudharauliwa,utumwa na unyang’au wa binadamu.
Binadamu walijiona “Aloof” walijiona wako juu kuliko wanyama,walijiona “Better than Animals”.
                                   UNAFIKI WA KUTISHA
Hata hivyo,licha ya sera za wanyama kuitikisa nchi,mapinduzi yalipokuja(mabadiliko) viongozi wa shamba la wanyama wakayateka nyara.Wakabadili amri muhimu za usawa,amri zikaanza kusomeka hivi:
“ALL ANIMALS ARE EQUAL, BUT SOME ANIMALS ARE MORE EQUAL THAN OTHERS!”
Kwamba, ingawa wanyama wote ni sawa, baadhi yao(viongozi wateule wa mungu) walikuwa na usawa zaidi kuliko wenzao!
Nguruwe walipofanikiwa kuongoza mapinduzi ya kumtimua binadamu kwa mapinduzi makali, walianza kulewa pombe, afadhali ulevi wa pombe kuliko kulewa madaraka!
WALIVAA SUTI za binadamu!Mnyama kuvaa suti ya binadamu mkia nje!!Kanuni za usawa zikatupwa chini,wanyama wakakosa haki na usawa waliotegemea wakati wakifanya uasi dhidi ya mwanadamu.
Ndoto ya ukombozi ikaanza kupotea,demokrasia ikatupwa shimoni, wanyama wakaanza kusema, “Heri utumwa wa kwanza kuliko wa sasa!”Wenye masikio na wasikie.
Nguruwe, walioongoza mapinduzi,wakidai usawa na demokrasia,wakaanza kukataa kuulizwa ‘Mapato na Matumizi’ ya Shamba la Wanyama! Kuhoji hesebu za shamba la wanyama ikawa kujitafutia kifo ama kuchapwa mijeledi!
 Ukihoji kwanini hata uchaguzi wa viongozi ndani ya shamba la wanyama, hakuna? Unaambiwa msaliti! Umetumwa na binadamu kuvuruga shamba la wanyama!
Unatimliwa kinyama,unavuliwa hata ngozi yako uliyopewa na Mungu! Unachapwa bakora!Wenye masikio na wasikie.
Uhaini! Eti kuhoji hesabu za shamba la wanyama ni uhaini,usaliti! Ufisadi? Hamtaki kuulizwa Mapato na Matumizi ya SHAMBA LA WANYAMA?
Nguruwe, hamtaki uchaguzi huru wa uhuru na haki? Hamtaki kuulizwa mhula wenu wa uongozi utakoma lini? Mnaanza kusingizia wanyama wenzenu kusaliti SHAMBA LA WANYAMA? Mizengwe,kuvuliwa ngozi yako uliyopewa na Mungu-This is abuse of political power.
For this reason animals have even less freedom than before. Wenye masikio na wasikie kilio cha shamba la wanyama Tanzania hii!
Itaendelea
0713 324 074







Wednesday, November 13, 2013

habari zenu nazo!



RAIS THOMAS JEFFERSON, wa Marekani(1801-1809) aliposhambuliwa sana na magazeti, wakati wa Awamu yake ya Tatu ya utawala wa Taifa hilo kubwa duniani, alisema hivi:
   “Mtu asiyechungulia kabisa katika kurasa za magazeti ,yu na taarifa sahihi kuliko anayesoma magazeti hayo kila siku. Maana yake ni kwamba, asiyejua chochote yu jirani na ukweli, ukilinganisha na yule ambaye akili zake zimejazwa uongo na upotovu”.
   Hii ni barua ya Rais Jefferson, kwa John Norvell, Juni 14, mwaka 1807.
 Hapa,  nakusudia kusema kwamba, mtu mzito sana katika nchi inayoongoza kwa demokrasia duniani, na uhuru wa vyombo vya habari, akavilaumu na kuvilaani sana vyombo hivyo, kwamba heri visingekuwepo aslani.
    Mwahahistoria wa Kiingereza, Thomas Babington Macaulay, ndiye aliyevibatiza vyombo vya habari wadhifa mtukufu wa “MHIMILI WA NNE WA DOLA”.
 Vyombo vinavyolalamikiwa kuwaongezea  mahluki ujinga, hadi watu wakubwa namna hii wakasema, ‘Heri visingekuwepo’!
Ni vyombo hivi vinavyowapigia debe wakubwa kuingia kwenye ulaji, halafu vinapoanza kuwaponda.vinageuka ‘Shetani’ kheri visingekuwepo duniani?
  Spika wa zamani wa  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa zamani, George Mkuchika, zamani kidogo walilaumu baadhi ya magazeti(siyo Mwanahabari), kana kwamba ingekuwa heri wananchi kutojua kitu chochote, kuliko kuyasoma magazeti hayo,ili kujazwa ujinga!
   Sitta na Mkuchika wanakubaliana na Thomas Jefferson kwamba,
   “The man who never looks into newspapers is better informed than who reads them inasmuch as who knows nothing is nearer the truth than he whose mind is filled with falsehood and errors”.
   Yapo mambo yaliyoandikwa na magazeti ,yametia ukakasi katika vichwa vya mihimili mingine ya Dola, yaani Bunge na serikali.
 Bila shaka magazeti hayo yalibeba ajenda za wahariri na wamiliki wake, waandishi na zaidi sana yalitafuta kupambana na matatizo binafsi ya kisiasa(political problems) zaidi ya kufahamisha na kuelimisha umma.
Lakini, wakubwa huwa hawataki kuelezwa udhaifu wao,wanataka sifa tu.
    Waziri mwenye dhamana ya Habari, wakati huo George Mkuchika,  alitishia kutumia ‘rungu’ alilopewa na Katiba kutaka kufungia magazeti hayo.
Hata siku hizi za akina Fenela Mkangala,magazeti yalishafungiwa,yanagugumia kwa maumivu,ingawa mwanzoni mwa Kikwete yalisemwa kumlamba miguu rais!!
Kufungia vyombo vya habari?
  Kwa sababu, kufanya hivyo si kuchimbua mizizi ya tatizo la ukiukwaji wa maadili ya taaluma ya Uandishi wa Habari nchini. Ni kufukia uoza usionekane, tena kuahirisha riha mbaya ya uandishi isifike puani mwa wasomaji.
   Lipo tatizo la msingi la baadhi ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi, kwamba wamesajili magazeti yao ili yafunike madhambi yanayosemwa sana juu yao .
   Ushahidi unaoonekana ni kwamba baadhi ya magazeti siku hizi yamekuwa yakimshambulia mtu mmoja kiasi kwamba ni nadra kukuta ‘Maslahi ya Taifa’ ndani ya mashambulizi hayo.
   Nachelea kumuunga mkono Mfanya biashara, Reginald Mengi, na kauli zake kwamba, ‘Mafisadi wameanzisha vipeperushi’ ili kumshambulia, kwa sababu hata yeye mageti yake ya Taifa Letu na Sema Usikike, yametajwa na Waziri Mkuchika kuandika habari zinazotia kichefuchefu!
    Sina hakika kama wakati ule ofisi ya Waziri Mkuchika ingeweza kuingia mkenge, ikasajili vipeperushi zaidi ya magazeti, wakati kuna sheria, kanuni na taratibu za kusajili magazeti.
 Sheria hizo huainisha magazeti, vipeperushi, majarida n.k
    Niunge mkono hoja kwamba yapo magazeti yaliyoanzishwa karibuni, yana lengo la kunyamazisha kelele za umma dhidi ya ufisadi na mafisadi kwa njia ya kutangaza ‘Privacy’ za watu, ili wasahahu kwamba kuna mafisadi.
Mengine huanzishwa na wanasiasa kuelekea 2015.kazi ni kuudanganya umma na kuwachafua adui zao wa mapambano ya siasa.
   Magazeti ya kale yamekuwa yakiandika kwamba kuna watu wanatumia vibaya madaraka waliyopewa, wanakiuka maadili ya uongozi na kutumia vibaya rasilimali za umma.
   Wakati, magazeti ya sasa yanajaribu kutwambia kwamba wapigao kelele sana dhidi ya ufisadi ni ‘mabingwa wa kuoa na kutaliki’; tena wapo vigogo ni ‘manchampioni’ wa kuwaweka kinyumba wanaume wenzao, naam mashoga!
   Bila shaka hivi ni vita kati ya mtu na mtu, kati ya kundi moja na jingine.Yapo magazeti hayana ajenda,ila kutangaza pumba,yanaapisha!
 Hata hivyo, wapigao ‘panda sana ’ hawana tofauti kubwa sana na kigenge cha matapeli, ambao licha ya kuendesha kampeni dhidi ya wapigao kelele dhidi ya ufisadi, huwadhulumu sana waandishi; huwapiga ‘danadana’ kila kunapokucha.
    Vyombo vya habari vina jukumu begani mwake kufichua uovu na uhalifu. Vyombo hivi ni Kioo cha Jamii.
Kazi ya kioo ni kuonesha uso ama sura ya mtazama kioo.Kukosoa kwa nia ya kujenga Taifa imara na safi.
   Kioo hakimsingizii mtu makasoro yake. Kioo hakimsemi mtu kwamba ana kunyanzi ama udelele na madevu mithili ya shamba la Miwa la Kilombelo, wakati hana.Kioo hakiwezi kusema kwamba Shetani ni Mungu na Mungu ni Shetani ama Obama ni Osama, ingawa majina yao hufanana na hulingana kasoro herufi ‘B’ na ‘S’ katikati ya majina yao.
Vyombo vya habari hutakiwa kuwa makini na wakweli na walinganifu.
   Kazi ya kioo ni kusema ukweli kama fisadi anayo matongotongo, udelele, makunyanzi na hata midevu inayotisha watoto na kuonja michuzi.
   Mtazama kioo, awe na udelele, tongotongo, makengeza ama makunyanzi, hapaswi kukasirika na kukivunja kioo chake pindi kimwonyeshapo taswira ama mwonekano wake. Anapaswa kutumia maji na sababuni kujitakasa.
    Mafisadi hawataki kujitakasa  ili waonekane safi mbele ya kioo na mbele ya jamii.
Wanavunja kioo halisi, kisha hutengeneza vioo feki na bandia ili kuwageza wananchi kuona makengeza na maruweruwe!
   Nataka kusema kwamba, wakati maadili ya uandishi wa Habari yanataka habari ziwe ‘Objective, Fair na Accurate', siku hizi twasoma habari za kushambuliana, kutetana na kulumbana  wenyewe kwa wenyewe.Tunasoma ushabiki mwingi. Upuuzi,vita uongo na chuki na uchimvi hasa kwenye mitandao ya kijamii.
   Zaidi sana , twasoma ‘kati kati ya mistari’ wamiliki wa magazeti hayo wakimwagiana uvumba, matusi na fitina ili kuvuana nguo na kubakizana utupu-uchuro na mambo ya kijingajinga!
   Tunauliza:
 “How can they balance freedom of the press with the rights of individuals to privacy and their good names?”
   Lini uhuru wa Habari ulifikisha mwisho Haki za watu zinakoanzia, hadi tuambiwe mambo ya kupigana denda wakati hayahusiani kabisa na ajenda ya wizi wa mali ya umma?
    Waama, huu uandishi wa ‘sensationalism’ na vita dhidi ya mtu na mtu au kundi moja linalojidai safi dhidi ya jingine linaloitwa fisadi, faida yake nini kwa umma wa Watanzania?
   Heri magazeti haya yasingekuwepo, kama alivyosema Rais wa Tatu wa Marekani, Thomas Jefferson..
   Mhimili wa nne wa Dola(vyombo vya habari) una dhima ya kuonyesha makosa ya watu na serikali yao katika kujiletea mafanikio. Vyombo hivi vifanyapo kazi sawa sawa ni  kama kioo cha kuonyesha watu wapi wana mapungufu, ili wayarekebishe.
  Naam, vyombo vya habari ni sawa na kioo kikubwa ukutani, ambacho watu wote wan chi hupita kujitazama.
    Ni aibu kundi Fulani la watu( sijui ndiyo mafisadi kweli) wanapojitazama katika kioo hiki kilichopo njia kuu, hubaini tabia zao chafu, lakini badala ya kujisafisha udelele na tongotongo, huwaleta  mafundi vishoka ili wakavunje kioo kinachoonyesha makunyanzi na  makengeza yao na kutengeneza vioo vipya vipya feki.
   Lengo ni kuwachanganya watu wasione makunyanzi na matongotongo yao ? Lengo ni kuifanya jamii ya Tanzania iwe makengeza?
   Nakusudia kusema kwamba, hawa hawana nia nyingine ila kutaka umma wa Watanzania useme kwamba vyombo vya habari vya Tanzania (kioo cha jamii) havina maana kwa kuwa vimejitia unajisi na vinachafua watu badala ya kuonyesha kasoro.
   Watu hawa, wanataka umma wa Watanzania uone kwamba ni heri kutosoma magazeti kabisa kuliko kuyasoma na kujazwa ujinga!
 Kwamba, eti mawaziri wetu wakuu wanapostaafu, hujitwalia madume menzao kuwa ‘vimada’ wao; kwamba Tanzania kuna ma “Retired” PM(But not tired) viwembe 'Chapa mamba' katika ngono za jinsia moja! Uchuro.
    Nazungumzia ulazima wa kuwepo ama kutokuwepo kwa vyombo vya habari, kama habari zenyewe zinatia ukakasi kiasi cha macho kupatwa kiwi na meno kuota ganzi!
  Thomas Jefferson, kabla ya kuwa Rais wa Marekani alimwandikia barua Kanali Edward Carrington, Januari 16, mwaka 1787 kusema, angepewa kuamua kuhusu kuwepo au kutokuwepo vyombo vya habari asingesita kuchaguwa kuwepo kwa vyombo vya habari hata mahali ambapo hakuna serikali.
   Vyombo vya habari vifanyavyo kazi sahihi ni muhimu kuliko serikali.
Ewe Fisadi, unapovunja ‘Kioo’ nani akuoneshe udelele wako? Tatizo siyo kioo, ni udelele na ufisadi(uchafu) wako. Je, kioo bora kisiwepo ili udelele wako usionekane?
   Vyombo vya habari(kioo) ni muhimu kuonyesha uchafu wa mafisadi, ili wajisahihishe.Waache kujenga chuki dhidi ya kioo kionyeshacho makunyanzi na udelele wao.
      0786/0713-324 074



Marekani, magazeti kama, Wall Street Journal, USA Today, Los Angeles Times, New York Daily Times, New York Times, Washington Post, New York Times, Tribune, Newsday n.k yanaongoza mauzo.
Huku kwetu Tanzania, jamii haipendi kusoma vitabu na magazeti yenye kuelimisha juu ya uchumi,ujasiliamali, elimu ama taaluma Fulani,kama kilimo bora n.k
Watu hupenda tetesi,picha zenye ladha mbaya(Bad taste),habari za kuvunjia watu heshima, zilizokolezwa na kuongezewa chumvi(exaggerated) ,uchochezi na mambo ya hihi-hivi tu,yasiyo na kichwa wala miguu,hushabikiwa sana.
Tovuti, blogs, face book, twitter zenye picha za kingono-ngono(pornography) hutembelewa na watuy wengi. Kamera za simu za mikononi siku hizi humfanya kila mtu kupiga picha bila hata kufuata taaluma, na kuzichapisha kwenye blogs,facebook n.k
Dhima, “Role” ya vyombo vya habari, “Kutaarifu/kuhabarisha,kuelimisha,kurekebisha jamii,kuburudisha,kukemea(to inform, to educate, to reform, to entertain, to incite) ilishatupwa na vyombo hivi siku nyingi.
Juma lililopita,tukagusia kuheshimu haki za watu,faragha zao(privacy),pasipo kisingizio kwamba eti wanahabari wana uhuru na kwamba kila kitu ni habari,hata kama mtu analalia jamvi. Jamii haina haja kujua kwamba mtu Fulani anaringa,lakini hulala penye jamvi!
Pana sheria zinazokataza vyombo vya habari kuchafua heshima za watu. “Libel” ni kosa linaloweza kuwa, ‘civil’ au ‘criminal offense’ .Kosa la madai au Jinai. Wanahabari wanategemewa kutangaza habari za kujenga na ziwe za kweli, sahihi na za kutegemewa na jamii,pasipo kuwa na upendeleo-habari zisiwe biased, ziwe ‘credible’ na ‘accurate’. Wanahabari hushauriwa kuchungulia katika pande zote za habari -checks and balances.
Tunataka jamii ipate habari ili iamue ifanye nini, na jamii ione mantiki na kuamua aidha kukubaliana au kutokubaliana.
Siku zetu hizi, DALADALA ya vyombo vya habari-MEDIA- inatumia haki ya kikatiba ya watu kujieleza- Freedom of expression, kuhukumu watu kwamba ni wezi,mafisadi na majambazi, na wengine kwamba ni miungu na malaika na mitume!
Vyombo vya habari vinalazimisha hata watu wote wafanye nini! Vimekuwa mgambo, mahakama,polisi, waendesha mashitaka,mahakimu na magereza kwa pamoja!!
Nakiri, vyombo vya habari ni muhimu sana katika taifa lolote, vina wajibu mtukufu kuifanya serikali ijitazame,ione makosa yake ili kujirekebisha,na watawaliwa wanapaswa kuhabarishwa ili waamue wao wenyewe nini cha kufanya.
Hata hivyo,vyombo vya habari vina jukumu mahsusi kuikosoa jamii ili ifuate sheria,taratibu siyo kuishia kuikosoa serikali tu na kuiacha jamii kuangamia kwenye majanga anuwai kama uchangudoa,ujinga,ukimwi,ugaidi n.k
Ukosoaji wa wanahari usiilenge tu serikali kutumia vibaya madaraka,’Abuses of power’ bali pia vyombo vyetu vitafute kuona yalipo maslahi ya taifa zima,na maslahi ya walio wengi.
 Tazama kauli hii:
“The Press is too quick to criticize authority, and does not support national interests”
Vyombo vya habari leo huishia kulalama na kuikosoa serikali, wakati vimesahau wajibu wa kuunga mkono maslahi ya taifa.Yako mengi, hata nchi inapoingia vitani, wanahabari hawapaswi kuunga mkono adui n.k
Kila mtu anajua sasa hatuna MAADILI,ndiyo maana maslahi ya taifa yanatupwa,na maslahi binafsi yanakumbatiwa na kila mtu,mimi hata wewe tukiwemo.
Nipewahi kuandika kwamba Maadili ni SHERIA ambayo kwa Kigiriki huitwa, “Nomos”, ama    ‘Torah’ kwa Kiebrania. Mana yake ni ‘Directions” maelekezo,mwongozo, “Guidance” utaratibu wa kufuata, ‘instructions’, ili watu wote waufuate kwa nia ya kuepuka makosa ama jambo Fulani muhali-baya.
Ni kutokana na Sheria, ‘Torah’ ama ‘Nomos’ tunapata uadilifu. Ikiwa watu watatii sheria na kuwa wanyoofu,tutakuwa na uadilifu. Kumbe, uadilifu hujenga unyoofu. Sheria za unyoofu(Moral Laws) ndiyo hasa maadili yanayolalamikiwa siku hizi kwamba yamepotea sana.
Ukweli ni kwamba, ‘Moral Laws’ ni AMRI 10 ZA MUNGU  ambazo ni kiwango bora cha maadili.
God’s legal standard for morality” kiasi hata vyombo vya habari hatuwezi kuzishika hizo amri 10 za Mungu, kwa sababu wengine hawaamini kama kweli yupo, au ana itawala dunia hii. Labda alishakufa n.k!
Waandishi wa habari wengine licha ya kutokubali kwamba Mungu yupo, wengine hawampendi,na hakuna juhudi za kuwahimiza kuzitii sheria zake zinazojenga maadili katika taifa lolote. Kwa sababu hiyo, hata vipindi vya dini havipendwi na vimepuuzwa sana.
Nataka kusema kwamba uhuru wa habari ni mzuri sana. Hata hivyo, uhuru wa kusema chochote na mwandishi yeyote, au kunakilicho chote kutoka kwa mtu yeyote kwamba ndiyo haki  za binadamu kwa mujibu wa katiba ya nchi(Freedom of expression), ndiyo mwanzo hata wa kutangaza habari za Ibilisi, za uchochezi, maneno mabaya,picha mbaya za kutisha(bad taste);tunapotosha hata watoto wadogo na kuwafunza uchafu,kwa kisingizio cha demokrasia.
Tumeona kwamba, Shetani alimtumia Nyoka kama “MEDIUM”Chombo chake cha mawasiliano kupeleka uchochezi kwa Adamu na Hawa ili wachukie SHERIA/MAADILI’TARATIBU/MWONGOZO/KANUNI kwamba ni vitu visivyotekelezeka; na kwamba mambo hayo yote hapo juu ni ukatili,udikteta na ubinafsi wa Mungu! Mwanzo 3:1-5.
Je, sisi vyombo vya habari na wanahabari katika nchi hii,siku hizi tunatumia demokrasia na uhuru  aliodai Ibilisi dhidi ya sheria za Mungu KUFANYA NINI?
Au ndiyo sababu tunapotosha watu makusudi?
Sisi Media, tumeamua kuwa njia ya Ibilisi kufundisha ajenda yake, ili kuwapotosha watoto,kuwafundisha maneno mabaya,ngono, matusi,kuvaa nguo za uchi,nyimbo za uchi,picha za ngono,uchafu mwingi usiosemeka!
Tazama televisheni nyingi uone michezo ya kuigiza ya uchi uchi,muziki wa ovyo wa wabwia unga na wavuta bangi, maneno machafu ya kingono,ulevi, uvuta bangi, umalaya, halafu tunapiga kelele za kijinga:
“Taifa linaangamia kwa kukosa maadili! Mafisadii!”
Nini chimbuko la mafisadi na walevi, wabwia unga, kama si vyombo vya habari kuwahusudu sana wavuta bangi,Malaya,machangudoa na majambazi na wauaji wa Marekani na Ulaya?
Mauaji ya kinyama watoto wameyaona kwenye televisheni,kwenye sinema, uchangudoa watoto wametazama kwenye twitter,facebook,blogs n.k maadamu siku hizi tumewanunuliwa vijisimu vingi vya China, vinawaharibu wawapo hata vitandani vyumbani mwao. Adui namaba moja wa Maadili ni vyombo vya habari!
Kimsingi,vyombo vya habari visipotumika vizuri,ni DALADALA inayopeleka kizazi hiki Jehanum ya moto; vyombo vya habari vinamsaidia SHETANI KUTANGAZA uhalifu kuliko vinavyotumika kuelimisha watu na kuwaondoa kwenye giza.
Kuna vipindi vingapi vya dini? Nani anafuatilia vipindi vya dini kwenye televisheni? Muda wa habari ukifika watu wana tune kwenye michezo,muziki na kwenye comedy!
Matangaza ya pombe,sigara huwavutia hata watoto kupeperusha moshi angani kama treni, na kusema maneno machafu ya mastaa wa Ulaya au wa hapa Bongo! Nguo za nusu uchi,mapenzi,ngono,filamu za mauaji,za ngono,michezo ya kiwenda wazimu,ukatili,uvuta bangi n.k ndiyo vipindi vinavyopendwa sana!
Vyombo vya habari-MEDIA-vinapeleka habari namna hii kwa watazamaji,wasikilizaji na wasomaji, wau wanaita, Mass Audience. Nakwamba vyombo vya habari ni kama kisu,kikitumika vibaya kitakata nyanya,vitunguu na nyama mekoni nawe utakula chakula bora na kitamu sana. Kikitumika vibaya hiki kisu utaua watu!
Shetani, ametumia MEDIA au kimoja MEDIUM tangu Edeni. Nyoka alitumika kama chombo cha habari kuwasilisha uchochezi kwa Hawa.
Sasa, angalia kama vyombo hivi vya habari vinatekeleza hiyo dhima, “Role” ya vyombo vya habari: To inform, to educate, to reform, to entertain, to incite and to set an agenda!
 Kuhabarisha,kufundisha, kurekebisha jamii,kuburudisha,kuonya na kuweka jukwaa la mjadala wa manufaa kwa jamii.
Je, msomaji, wewe redio yako,televisheni yako na magazeti yako yanakusaidia kwa haya na watoto wako wanafaidika?
Sisi wanahabari tujiulize,tunahabarisha nini? Tunawapa watu jukwaa la kusema nini kama siyo utumbo?
 Sikiliza hata vituo vya redio, utasikia Kiswahili cha ovyo sana, “Masaa masita!!” badala ya saa sita, “Hiko” badala ya Hiki kijiko au hichi kijiti!
Eti lisaa limoja! Kuna lisaa  limoja jamani? Kuna saa moja,basi, Uchafu gani huu? Sikiliza nyimbo zao sasa, wasela wanaimba huku wakishika sehemu zao za siri utadhani wanawashwa upupu! Eti ‘hiko kikombe!’
Eti burudani, utasikia mtangazaji anawachochea manazi wa Yanga au Simba kumdunda mwamuzi kwamba hayuko ‘Fair’ kabisa!
Hivi wewe mtangazaji au mchochezi? Unataka manazi wafanye nini kama unasema goli lilikuwa si halali mwamuzi kaiua timu yenu? ‘sisi moja-wao bila!!
Watangazaji hao wa siku hizi.Muziki wa matusi ya nguoni, taarabu za kusimangana na kuoneshana viuno, hata kwa watoto under age. Katika Biblia, katika Amosi 6:5 Mungu anasema, “Niondoleeni nyimbo zenu za upuuzi” wanaimba Nakupenda tangu asubuhi hadi usiku wa manane, hakua kingine!
Siku hizi,nyimbo kama “Kabwe rudi nyumbani ushirikiane nasi kulijenga taifa” hakuna, hakuna uzalendo wowote,ni ngono tu na viroba!
Hakuna vitabu,hakuna maktaba.Kila mtaa kuna baa,saloni na stoo bubu,hakuna maktaba wala watu kujisomea. Vitabu tunavyopenda ni vyenye mapaja manene ya akina mama na uchawi. Hakuna maarifa, magazeti ya ngonongono ndiyo yanayopendwa.
Sasa, tunasema vyombo vya habari Media ni mhimili wa Nne wa Dola.
Mwanahistoria wa Kiingereza,Thomas Babington Macaulay ndiye aliyeita Media kwamba ni “The Fourth Estate” kwa sababu, ni mithili ya mbwa mlinzi kwa jamii. Vyombo vya habari vina jukumu mahsusi kama mbwa mlinzi –Watchdog Role.
Mihimili mingine ya Dola ni Mahakama,Serikali na Bunge.Sasa vyombo vya habari vinafuata,lakini vinaongoza kuchafua maadili ya watu na vinachangia sana kuwaambia watu kutofauata sheria.Wewe unamnunulia mwanao toy  la bunduki, si unataka awe jambazi?
SHERIA hufunua Mungu na tabia njema aliyo nayo na utakatifu na usafi wake.Sheria ni nakala ya upendo wa Mungu,ni kiwango cha maadili bora,maadili yametupwa kwa sababu vyombo vya habari ni Daladala iliyowasomba wengi na kuwatupa shimoni.
Siku hizi kuna ‘Yellow Journalism’ ambamo kuna ‘cooked stories’ mtu ana kaa anatunga story na kuwagutua watu anaongeza chumvi habari, sensationalism, basi vijana wanaamua kubeba rungu na kufanya vurugu,hapo mwandishi anapata Lead story! ‘Kiama chatokea Mwanza,Arusha au Dar!!’
Watazame baadhi ya wahariri wa vyombo hivi, chungulia maisha yao nje ya ofisi,yanatia kinyaa,Siyo waadilifu.Wao na wakuu wao wa vyombo vya habari,wameshiriki sana kupora malipo ya waandshi wao wa mikoani, ambao sasa ni omba omba,wanaoingilia hata harusi za watu-trespassing- na kudai posho!!
Wakuu wa tasnia ya habari baadhi yao ni wa ajabu mno, wanakula mgongoni mwa wanahanari! Kuna maadili wapi na yapi kwenye tasnia ya habari,kama mwandishi anaomba nauli kila siku,ili kujinusuru maana hajalipwa malipo yake miaka mitatu

Mwandishi wa safu hii(wa kwanza kulia) akiwa na wenzake walipokuwa wakiendesha kipindi katika studio za televisheni ya Barmedas Jijini Mwanza

 Hapa ndiyo mwanzo wa kutegemea vijizawadi-Payola-kutoka kwa vyanzo vya habari zake ili apate kujikimu! Hapo unategemea habari gani,kama siyo watu kilishwa uongo na uchochezi,na blahblah tu.
Amini usiamini,vyombo vya habari ni DALADALA inayopeleka watu SHIMONI -shimo la Tewa, aliloimba Samba Mapangala.
Nimekumbushia ile ya Kikwete kulambwa miguu na waandhi wa TZ.
0713 324 074