Monday, January 28, 2013

Ulaya na Marekani hakuna haki za binadamu

KAMPUNI ya Shell ya Uingereza,iliwalipa fedha wanamgambo kuwaua wanaharakati wakati walipoandamana huko Niger Delta, kupinga makampuni hayo ya kigeni kuchimba mafuta  eneo hilo wakati wakiharibu mazingira,bila kulipa fidia.
Tumeona juma lililopita,kwamba Niger Delta hakukuwa na mafuta na huduma za kiuchumi hazikuwepo licha ya mapipa mengi kuchimbwa eneo hilo  la Kusini mwa Nigeria.
Kampuni ya Chevron ya Marekani,iliwalipa mishahara polisi na jeshi kuwaua wanaharakati kama Ken Saro-Wiwa, kwa sababu walipinga uhalifu wa makampuni haya kwa maandamano makubwa ya amani.
Watu wajinga wanapoona Afrika polisi wakikabiliana na waandamanaji,akili inawatuma Ulaya hawakabiliwi. Kumbe, Ulaya na Marekani walikuwa nyuma ya vikosi vya Sani Abacha kuwaua wanaharakati waliopinga makampuni ya kigeni kuharibu mazingira bila kuleta maendeleo kwa raia hata licha ya kuchimba mafuta katika eneo hilo.
Sasa, kama Gaddafi alishambulia waandamanaji wa Benghazi,akapinduliwa kasha kuuliwa kwa risasi, Kiongozi wa Syria, Bashar al Assad naye anawashambulia raia wanaompinga anashughulikiwa na Ulaya na Marekani,kwanini Shell na Chevron yalishinikiza serikali ya Nigeria kuwaua waandamanaji?
Huko Burma,(siku hizi ni Myanmar) kampuni kubwa la Unocal la Marekani, lilitiliana saini mkataba na jeshi kuilinda,ilipokuwa ikitekeleza ujenzi wa Bomba la gesi asilia kama hiyo ya Mtwara, kupelekwa nchi nyingine.
Bomba hilo lilikuwa likijengwa kutoka Yadana,wanakijiji walitumikishwa pasipo ujira,walibakwa,waliuliwa.Waliteswa na wanajeshi,Marekani wakiwa pembeni,wakatumikishwa kitumwa.
Wapo wajinga,wataanza kusema,ilikuwa kampuni siyo serikali ya Marekani,subiri uone!
Wanakijiji walifungua kesi ya madai dhidi ya kampuni hilo la Unocal,kulitumia jeshi la Yangon kuua vibarua,kubaka na kuwatumikisha kitumwa,pasipo malipo ili gesi iende nchi nyingine.
Shirika la Habari la Agence France Presse(AFP) likasema miaka saba iliyopita kwamba, Unocal walipobanwa wakasema ukweli,wakakubali kuzungumza na wanavijiji wa Burma ili kesi iondolewe mahakamani,walikubali kuwalipa fidia na kuwasaidia kuimarisha maendeleo.
Nimesema Unocal; ni kampuni la Kimarekani la kuchimba gesi.Mahakala ilikuwa inakaribia kuwapa ushindi wanavijiji wa Burma waliofungua kesi Califonia.
Nikusimulie kidogo.Jumanne,Desemba 10, mwaka 2003 kampuni hili katili la Kimarekani lilipandishwa kizimbani huko California ili kujibu mashitaka ya hao wanavijiji wa Burma, na kuhalifu haki za Binadamu.
Nchi ya Burma wakati huo ilikuwa chini ya utawala wa kiimla wa kijeshi ambao Marekani hujidai sana kuupinga hapa Barani Afrika,kumbe sehemu nyingine wanajali maslahi tu.
Hii ‘Brutal Military Junta’ waliwalazimisha raia kujenga bomba la urefu wa kilomita 62,waliokataa waliuliwa,akina mama wakabakwa na kuumizwa bila fidia.
Bomba lenyewe lilikuwa la kilomita 62 sawa na maili 39 ili kupeleka gesi kutoka Myanmar kwenda Thailand.
Basi, Unocal walipobanwa wakakubali kulipa fidia maana kazi waliyofanya wanavijiji hawa wa Myanmar mwaka 1990s ilikuwa ya thamani ya Dola bilioni 1.2.
Sasa jiulize,wewe shabiki wa hawa Marekani na Ulaya, Utumwa kwa wananchi waaa      Burma ndiyo Haki za Binadamu? Utumwa huu katika karne ya karibuni?
Unocal walishirikiana na kampuni la Ufaransa,Total kupeleka gesi Thai.
Tutazame wanavyoharibu mazingira ya dunia,hasa nchi za dunia ya tatu na kukataa kusaini mikataba ya upunguzaji wa hewa za sumu angani,ili tupatwe majanga ya asili.
Mapigo Saba ya Mwisho-
haya ni majanga ya kiasili ambayo ukiyachunguza yataletwa na kiburi cha Moabu,Marekani na washirika wake,kwa kuchafua sana anga la dunia,kukataa kusaini mikataba kama ule wa Kyoto(Kyoto Protocol) ili maji yachafuke,viumbe wafe kwa Ongezeko la joto na mabadiliko ya tabianchi, mafuriko kila mahali,
vifo majanga, kansa, ukimwi,vyanzo vya maji kuwa damu,kutoboka kwa utando wa Ozone n.k
 Moabu ya kiroho(Marekani) iligoma kutia saini Mkataba wa Kyoto mwaka 1997,kwa sababu kufanya hivyo kungeleta hasara kwa wafanyabiashara wan chi hiyo-Wakaona heri kuongeza madhara kwa kumwaga hewa chafu angani ili wajipatie UTAJIRI.
 
Miongoni mwa shughuli za kiuchumi za binadamu zinazoharibiwa sana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi ni pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi n.k
    Mkutano wa New York ulioanza Septemba 22 mwaka huu wa 2009, umefanyika takriban miaka 12 kamili tangu mkutano wa Kyoto, Japan ufanyike Desemba mwaka 1997.
   Katika mkutano wa Kyoto, viongozi wa mataifa zaidi ya 150 duniani walikutana wakaweka  itifaki ambayo ingewezesha kupunguza hewani kiwango kikubwa cha gesi au hewa chafu ya sumu zinazoletwa na hewa ya ukaa(C02) na gesi nyingine kama     CH4,N20, HFC8, PFC8  na SF6.
   Mkataba huo uliojulikana kama  itifaki ya Kyoto(Kyoto Protocol) uliokusudia kupunguza gesi za sumu duniani kwa silimia 5.2 kabla ya kufika mwaka 2012.
  Mataifa yaliyoshurutishwa kusaini mkataba huo wa Kyoto ni nchi zote 38 zenye viwanda duniani..
Mataifa yote 15 ya Umoja wa Ulaya(EU) yakakubali kupunguza asilimia nane ya taka hewa zake duniani. Marekani ilitakiwa kupunguza asilimia saba ya gesi zake inazotupa angani.
 
 Japan, ilitakiwa kupunguza asilimia sita ya taka sumu inazotupa angani, na nchi zinazoendelea zilitakiwa kupunguza kiwango chochote kwa uhuru wake.
 Marekani ilisaini mkataba huo Novemba 12, mwaka 1998, lakini kutokana na kitisho kutoka kwa matajiri wenye viwanda nchini humo, serikali ya Rais Bill Clinton ilichelea kupeleka ajenda hiyo katika Bunge la seneti.
 Kwa sababu, kusaini mkataba wa Kyoto na kuutekeleza, maana yake ni kwamba viwanda vya Marekani vingelazimika kupunguza uzalishaji.
Ni kwa sababu hii serikali ya Clinton iliufyata.
  Mkutano mwingine wa kujadili upunguzaji wa taka za sumu hewani ulifanyika Bonn, Ujerumani Julai 2001.Utawala wa George .W. Bush ulitangaza kujitoa katika mkataba wa Kyoto kwa madai kwamba uliweka zigo kubwa katika nchi zilizoendelea bila kuzingatia usawa.
 Marekani, waligeuka wapinzani wakubwa katika ajenda za kupunguza hewa za sumu duniani, tangu huko mjini Bonn, Ujerumani na mahali pengine, kwa sababu ya maslahi yake na ya viwanda vyake, bila kujali madhara makubwa yaliyotokana na wingi wa viwanda vyake kutupa angani hewa chafui zenye kusababisha majanga makubwa kwa Ulimwengu mzima..
Hizi ndizo haki za binadamu Ulaya na Marekani?
  Kwa shingoupande, walikubali kupunguza hewa hizo za sumu ili kutekeleza huo mkataba au itifaki ya Kyoto ya 1997.
  Katika makubaliano ya mjini Bonn, mataifa makubwa yenye viwanda yanayomwaga kwa wingi hewa za sumu angani, yalishauriwa kufuata malengo waliyowekewa ya kupunguza hewa ya ukka katika anga.
 Kulingana na Shirika la Kudhibiti Uharibifu wa mazingira, hewa ya ukaa(carbon dioxide) imeongezeka sana angani kutoka mwaka 1990 hadi sasa; na hii ni kutokana na shughuli za binadamu, ikiwa ni  pamoja na viwanda na migodi.
  Wakati hewa za sumu zinapoongezeka sana duniani, misitu ama miti inayopunguza kwa kiwango kikubwa hewa ya ukaa kwa kutengenezea chakula chake(starch) inatoweka kwa kasi na kwa kiwango cha kutisha sana.
  Tazama nchi zinavyoongeza sana kiwango cha hewa za sumu angani.
 Mashariki ya Mbali pamoja na Oceania wanachafua anga kwa kiwango cha asilimia 28.9.
Amerika ya Kaskazini huchafua anga kwa kiwango cha asilimia 28.8.
 Marekani pekee inachafua anga la dunia nzima kwa moshi wa magari na viwanda vyake kwa asilimia 24.7.
   Ulaya Magharibi, kwa pamoja huchafua anga la dunia kwa asilimia 16.5, wakati Amerika Amerika ya Kusini nzima na Kati huchafua anga la dunia kwa kiwango cha asilimia 4.3.
   Ulaya Mashariki, na iliyokuwa Jamhuri ya Kisovieti(USSR) huchafua anga la dunia nzima kwa kiwango cha asilimia 12.8. Mashariki ya Kati huchafua anga kwa kiwango cha asilimia 4.7.
 Afrika, inachangia katika uchafuzi wa anga la dunia kwa asilimia 3.9 tu.
Hii ni kwa mujibu wa Ripoti za Energy Information Administration, kuanzia mwaka 1999.
 Afrika inayochangia kwa kiwango kidogo sana katika uchafuzi wa hewa angani, ndiyo inayoathiriwa sana na madhara makubwa ya uchafuzi wa hewa angani unaoleta mabadiliko ya tabia ya  nchi.
 Mifugo ya Afrika, hususan Kenya  na hapa kwetu hufa kwa ukame unaoletwa na uchafuzi wa mazingira ya anga. Uchafuzi wa anga ndiyo chanzo cha ukame huko kwetu Afrika. Ukamwe huu ndiyo unaochangia jangwa kuongezeka, ukame na njaa na vifo vya watu pia.
 Kulingana na uchafuzi huo wa hewa angani, Benki ya Dunia(WB) ilishasema mwaka 2001 kwamba kila mwaka watoto wachanga wapataao 500,000 wangepoteza maisha duniani pote kwa sababu ya uharibifu huu mkubwa wa anga.
Vifo huletwa na viwanda vya Ulaya na Marekani siyo? Kumnyang’anya mtu uhai siyo haki za binadamu sawa?
  Kunatokea mvua za sumu(acid rains) zitakazosababisha uharibifu mkubwa sana wa misitu hasa ya Afrika, na wala mvua za sumu hizi za viwanda vya mataifa makubwa haziharibu huko kwao peke yake.
 Nataka kusema kwamba, Marekani inaongoza duniani kwa uchafuzi wa anga, lakini athari zake tunapata sisi huku; tunakufa kwa njaa na matokeo ya ukame na hata vimbunga kama Mitch, tsunami na Katrina ambavyo vikitokea, huua maelfu ya watu bila kujali mipaka ya nchi za viwanda na zisizokuwa na viwanda.
  Ni kwa sababu hii, ubeberu wa Marekani wa kukataa kutia saini mikataba ya upunguzaji wa hewa na taka za sumu, kama huo wa Kyoto wa mwaka 1997, ni hatari kwa maisha ya watu, hasa tuishio nchi masikini.
  Ingekuwa heri kama Mkutano wa New York  na Afrika ya Kusini ungeipa kibano kikali Marekani kwa kiburi chake na kuwelka mbele maslahi binafsi ya viwanda vyao, huku ng’ombe wa masikini wanapokufa kwa maelfu huku kwetu, pasipo fidia.
  Marekani, hukimbilia kuliburuza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuzitenga nchi nyingine kaidi kutekeleza mikata kama ya Nyuklia n.k Ni  Marekani hiyo hiyo inayotaka Iran na Korea Kaskazini na Iran zitengwe au zishambuliwe kijeshi kwa kukataa kutia saini mkataba wa kupunguza silaha za nyuklia.
 Mbona yenyewe inakataa kwa  ubabe kutekeleza mkataba wa Kyoto, unaotaka hewa za sumu zinazoleta majanga duniani kudhibitiwa. Ongezeko la joto duniani linaloleta hayo majanga kama tsunami, huleta madhara hadi huku Bahari ya Hindi na kusababisha vifo hata Kenya, Tanzania na Somali. Kwa nini Marekani haidhibitiwi ama kupewa kibano au kushambuliwa kijeshi, kama yenyewe ilivyozishambulia Irak na Afghanistan,  na iko mbioni kuzishambulia Iran na Korea Kaskazini kwa kukataa kutekeleza mikataba ya upunguzaji silaha za sumu?
 Sumu inayoua watu si ndiyo iliyo,o pia katika silaha za atomiki na ndiyo ile inayorushwa angani na viwanda vya Marekani na Ulaya, bila kudhibitiwa na mtu, tena kibabe?
 Ni kwa sababu hii, viongozi wa Afrika waliokwenda New York kujadili kitisho cha hewa za sumu angani na mabadiliko ya tabia  ya nchi, wanapaswa kutoa tamko kali la kuikemea Marekani au ikibidi kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kuitenga na Jumuiya za Kimataifa, kwa vitendo vyake vya kibabe vya kuleta maafa Ulimwenguni.
 Dunia haina ubavu wa kuitenga Marekani?
Marekani haiwezi kushambuliwa kijeshi na dunia nzima ili kuishikisha adabu iache kuiangamiza dunia kwa kumwaga sumu tani mamilioni kwa siku, huku ikikataa kutia saini kila mkataba unaowataka kupunguza sumu?
  Wakuu wa nchi za Afrika(akiwemo Rais Kikwete) wanaporejea kutoka New York, wanapaswa kuwaambia wananchi wao, ni namna gani wamembana Barack Obama, kwa sababu nchi yake ina kiburi cha ubeberu, kuendeleza uzalishaji wa taka sumu, zinazoleta saratani ya ngozi huku, kuleta jangwa ama ukame na kuua mifugo Afrika, hususan Tanzania na Kenya.
 Shughuli za kilimo na ufugaji, ambazo hufanywa na masikini huku Afrika Mashariki zinatatizwa sasa na mabadiliko ya tabia ya nchi na ukame. Chakula cha binadamu hakuna, kwa sababu Afrika inakuwa jangwa, kwa sababu Jangwa la Sahara lililoko Kaskazini linakaribia kushikana na lile la Kalahari, lililopo Kusini.
 Sasa, mvua itanyesha jangwani?
 Ni kwa sababu hii, tunasema, kiburi cha Marekani kimekwisha kuleta majanga makubwa hapa Kwetu Tanzania tangu wakate kusaini Mkataba wa Kyoto Desemba 1997 hadi mkutano huo ulipofanyika New York, Septemba, 2009.
  Ni kwa sababu hii, Rais Kikwete na ujumbe wake, wanapaswa kuwaambia Watanzania, Rais Obama wa Marekani, ameambiwa kwa kiwango gani kulipa fidia ya mifugo ya Wamasai, Wajitta, Wasukuma, Wakurya na wafugaji wengine ambao mifugo yao inaangamia kwa sababu ya ukame ulioletwa na sumu na taka za hewani kutoka viwanda vya Mabwanyenye wa Marekani?
 Vinginevyo, Obama ana kesi ya kujibu Dar es salaam, asijidai kukemea utawala mbaya huku na ufisadi, kumbe nchi yake huchangia mvua kukoma kunyesha na vifo vya mifugo huku.
Je,huu ni uungwana? Ni haki za Binadamu?
   0713 32 40 74

afrika kizimbani 9

Novemba 10 mwaka 2004, askari wa Kiingereza, Brett Richard(20) na Nigel David(23) walidaiwa kumbaka kwa zamu na kumsababishia kifo msichana wa Kitanzania, Conjesta Ulikaye.
   Nigel David na Brett Richards, walikuwa mapumzikoni jijini Dr es salaam.
  Waitokea vitani, Irak, hivyo wakawa wanajiburudisha katika fukwe za jiji la Dar es salaam .
 Wakiwa katika fukwe za Hoteli ya Silver Sands, tukio la mauaji ya msichana huyo likatokea.Walitiwa mbaroni, shauri lao likashughulikiwa kwa siku 36 tu.
  Walifikishwa mahakani Novemba 16 mwaka huo; yaani kesi yao ilifika mahakani siku sita tu baada ya tukio.
 Ilipofika Desemba 22 mwaka huo wa 2004, kesi dhidi yao ikafutwa na Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kwa mujibu wa  kifungu namba 91(1) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 1985.
  Aliyekuwa DPP wakati huo, Godfrey Shaidi, alisema ushahidi uliokuwepo haukutosha, hivyo hao Wazungu, askari wa Uingereza vitani Irak wakaachwa huru huria.
  Ofisi ya DPP imekuwa ikisema kesi zinacheleweshwa mahakamani zinapokuwa zikingoja kupangiwa tarehe ya kusikilizwa, wala hazicheleweshwi na ofisi ya DPP.
   Mahakama inadaiwa kuchelewesha kusikiliza kesi hasa kwa watu Weusi tena masikini wasio na ukwasi na mvuto wowote katika jamii.
  Wakati, zile kesi zinazowahusu vigogo kama akina Marehemu ‘Ditto’, Abadallah Zombe na wengine wa kariba hiyo, na Wazungu kama hao askari wa Uingereza, kesi huendeshwa kwa kasi ya ‘supersonic’ hadi wanapoachiliwa huru.
  Ni hapa, inapokuja dhana kwamba, mfumo wa sheria wan chi hii, haujali usawa kwa raia, bali unazingatia rangi, kipato, vyeo n.k
  Pia, inasemwa magereza ni kama yalijengwa kwa ajili ya wahalifu masikini Weusi, na kamwe siyo kwa Wazunagu na wenye ukwasi.
!
  Mzungu, Yunus Santy(67) ambaye alikuwa Mmisonari wa Katoliki, alifunguliwa mashitaka jijini Mwanza kwa makosa ya kufanya ngono na wanafunzi wa kike wenye umri wa miaka 17.
 Pia, alikutwa na picha za uchi na viungo bandia vya shemu za    siri za kiume(toy boy). Badala ya kutiwa hatiani na kufungwa jela miaka 30 kwa kubaka wanafunzi hao huku wakichukuliwa mkanda wa video wa kitendo hicho kichafu, Yunus Santy aliamuriwa kuondoka nchini mara moja.Hiki ni nini kama siyo woga?
Ni wazi,serikali yetu iliogopa kuwatia mbaroni hawa na kuwafunga kwa sababu Afrika haijawa huru; na iko kizimbani.
   Idara ya Uhamiaji ikaamuriwa na mahakama kuhakikisha jamaa huyo anaondoka nchini mara moja, badala ya kufunguliwa mashitaka ya ubakaji na kufungwa miaka 30 jela akaenda kwao Italia, asikanyage jela za Tanzania, ambazo utadhani walijengewa masiki Weusi, wanaotenda wizi mdogo, uzururaji na umachinga tu.
  Miaka michache iliyopita, kulitokea ugomvi kati ya mwekezaji Muingereza, Stewart Middleton na mbia wake wa biashara, raia wa Tanzania , Benjamin Mengi.
   Vyombo vya dola vya Tanzania vilipomtia mbaroni Middleton, kufuatia ugomvi wa makampuni ya kilimo ya Silverdale Tanzania Limited na Mbono Farms ya huko Hai, Kilimanjaro, Bunge la Uingereza likachachamaa.
  Mbunge toka chama cha Mahafidhina(CONSERVATIVES),Bwana Roger Gale, akasema Bungeni Uingereza kwamba Tanzania ilistahili kunyimwa misaada kwa sababu huyo Middleton katiwa mbaroni na polisi huko Kilimanjaro.
  Ilidaiwa kwamba, kitendo cha Middleton kutiwa mbaroni na kushitakiwa kwa ugomvi wao na Benjamin Mengi, basi kulikuwa kuondoa mazingira bora ya uwekezaji yanayowanyanyasa wawekezaji, hususan mabwana wakubwa wa Uingereza!
 Uingereza, kupitia Shirika lake la misaada(DFID) ilikuwa ikiongoza kutupatia msaada kuliko nchi yoyote duniani.
 Mwaka 2003\2004 misaada toka Uingereza iliongezeka kutoka pauni milioni 80(sh. Bilioni 208) hadi pauni milioni 110(sh. Bilioni 286) mwaka wa 2005 na 2006. Asilimia 70 ya fedha zote hizo zilikuwa zikiingia moja kwa moja katika bajeti ya serikali.
  Nataka kusema kwamba, katika mazingira kama hayo, vyombo vya dola vya Tanzania na mfumo wa kutoa haki wan chi hii, ulikuwa na ubavu gain kuthubutu kuwatia mbaroni Waingereza hata kama walifanya uhaini hapa?
  Tunadhani, kwa sababu ya misaada tupewayo na mataifa ya Ulaya na Marekani, basi raia wao wameanza kuabudiwa kama miungu na mabunge yao na serikali zao huogopwa kama radi ama ngurumo na mafuriko.
  Ni kwa sababu hii tu, tunadhani wale Wazunagu wawili waliokuwa mapumzikoni, Silver sands, Dar es salaam (wakitokea vitani, Irak) waliogopwa kutiwa hatiani kwa kumbaka Conjesta Ulikaye kwa zamu hadi alipokata roho.
 Naam, Serikali ya mjini Dar es salaam, wakati huo ilichelea kuwatia hatiani na kuwahukumu Wazungu wale kutoka Uingereza kifo cha kitanzi hapa hapa jijini Dar, habari zisije kufika London, halafu misaada yote ikakatwa, na vigogo woote wa hapa wakazuiliwa kukanyaga London!!
 Ilikuwa siyo rahisi Nigel David na Brett Richards kutiwa hatiani na kunyongwa hata kufa kwa kamba jijini Dar, lisije Bunge la Uingereza likajua, likafoka, misaada huku ikakatwa na mashirika mengine kama Oxfam yakafunga virago hapa.
 Ni kwa sababu hii, tunadhani hakuna haki na usawa katika mfumo wa sheria wan chi hii iliyowahi kutawaliwa na wakoloni Waingereza.
 Bado mawaziri wakuu wa Uingereza:Harold McMillan,(waziri mkuu wa Uingereza 1957-63 wakati Tanzania inapata uhuru), Alec Douglas Home, Harold Wilson, Edward Heath, James Callaghan, Margaret Thatcher, John Major,, Tony Blair na Gordon Brown wanaogopewa bungeni na katika ikulu ya Dar es salaam kama mizuka.
Utadhani sisi siyo watu huru tuliopata uhuru toka Uingereza Desemba 9 mwaka 1961. Bado tunamwogopa sana Malkia wa Uingereza, Elizabeth II(alitawazwa Feburuari 6, mwaka 1952) kiasi kwamba tunaondoa haki na uhuru wa watu wetu ili kumpigia goti          Mzungu?
  Naam, tunawapigia goti Wazungu, makaburu na wenye pesa hadi raia masikini wan chi hii wananyimwa haki au kucheleweshewa haki zao, tangu polisi hadi mahakamani.
  Mzungu tapeli akionyesha pua yake polisi, hapo hapo anadhaminiwa asije kufikishwa nyuma ya nondo. Lakini, Mweusi fukara, mpaka utoe rushwa.
 Ikitokea masikini Mweusi umedhulumiwa na Mzungu au mwenye pesa, basi mfumo wetu wa sheria unawa ‘gwaya’ hawa, sheria zinapindishwa ‘fasta’ hadi wanaachiwa huru.
 Hapa jamii yetu inaona imetengwa katika madaraja kama zilivyokuwa zama za Ukaburu, Afrika ya Kusini.
Ziko wapi sheria zinazojali haki na usawa. Iko wapi Katiba ya haki na usawa wa binadamu sasa?
  Kwa majuma mawili tumejadili ushoga,shuruti za mataifa haya na usawa katika sheria za Tanzania unavyodhulumiwa na mahayawani wachache, kwa tama zao au kwa ubaguzi.
 Ni furaha kwamba wanasheria wameanza kujadili jambo hili kupitia kituo cha televisheni cha Star cha jijini Mwanza.
  Tunakusudia haki za waliowengi zinarejeshwa, na usawa uliowekwa na katiba kisha ukaporwa na baadhi ya watu, unarejeshwa haraka.
  Kwanini tutengwe katika madaraja ya walionacho na wasio nacho, Weusi, Wazungu, machotara, mabwana
na watwana n.k utadhani zama za       Ukaburu na ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini?
 Nakupongeza Rais Kikwete,kwa ushindi,lakini nimekukumbusha haya ili awamu hii Watanzania waheshimiwe na serikali yao inayopigia goti wageni na magabacholi, na kuwapuuza raia wazalendo.
Tunapaswa tangu sasa kukemea tabia hii ya ukaburu na ukoloni wa Wazungu kama  David Cameron na wenzao
Ni kwa sababu hii, mashirika ya misaada ya Uingereza na Bunge huwa na sauti kubwa sana hapa kwetu hadi kuingilia ‘mambo ya jikoni’ kwa maslahi ya Uingereza. Haya ndiyo Amin aliyokataa enzi zake.
 Nahitimisha Msumeno wangu leo, kwa kuwakumbuka Waingereza vijana wawili: Nigel David(23) na Brett Richard(20) waliotiwa mbaroni kwa tuhuma za kumbaka kisha kumuua msichana kigori wa Kitanzania, Conjesta Ulikaye, mnamo Novemba 10, mwaka 2004.
   Tukio hilo lilitokea katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, katika hoteli ya Silver Sands, Dar es salaam .
   Shauri la kesi ya mauaji likashughulikiwa kwa siku 36 tu, Nigel na Brett wakafikishwa mahakamani ‘Fasta’ Novemba 16 yaani siku sita tu baada ya tukio. Vibaka wa hapa wanasota rumande hata miezi sita bila upelelezi kukamilika!
   Kesi hiyo ilifutwa Desemba 22 mwaka huohuo kwa mujibu wa kifungu 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 1985.
   Mraba   wangu, uliwahi kumuuliza Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Geofrey Shaidi(sasa Jaji), Machi Mosi mwaka 2005 alipokuwa jijini Mwanza:
    “Hao Waingereza wawili(walikuwa wanajeshi wan chi hiyo waliokuwa mapumzikoni Dar, wakitokea vitani Irak) waliachwa huru kwa maslahi ya umma wa Tanzania au maslahi ya Uingereza?”
    “Hawakuachwa huru kwa maslahi ya Uingereza au ya Tanzania …ushahidi uliokuwepo haukutosha!Wasingeendelea kung’ang’aniwa bila ushahidi” DPP Shaidi alisema.
   “Hata hivyo, kesi(dhidi ya raia) hazicheleweshwi na ofisi ya DPP, zinacheleweshwa mahakamani, zinaposubiri kupangiwa tarehe ya kusikilizwa. Hivyo, faili la Wazungu lilipofika kwetu, tukalishughulikia(fasta?) kama kawaida”,
  alifafanua DPP Shaidi wakati huo, huku akikanusha madai kwamba Waingereza hao hawakuachwa huru kwa sababu ya kuchelea kunyimwa misaada na Uingereza endapo wangehukumiwa kutiwa kitanzi.
    Laiti Nigel David na Brett Richard wangefanya unyama wao huo wa kumbaka msichana kwa zamu na kumsababishia kifo huko Uganda , enzi za Amin, bila shaka wasingeepuka kitanzi!
   Hata kama Mawaziri Wakuu kama Margaret Thatcher, James Callaghan, Edward Health, John Major, Tony Blair na Gordon Brown kwa pamoja wangemkoromea Amin, bila shaka Nigel na Brett wangenyongwa tu!
Afrika inazidiwa na Amin? Afrika iko kizimbani kwa kukosa sauti hadi sasa majeshi ya kigeni ya Kifaransa yanapoingilia mizozo Mali,Afrika ya Kati n.k Umoja wa Afrika(AU) ukiwa kimya!
      0786/0754-324 074
  
 
 
 0786-324 074
 
 
 

KAMBONA NA NYERERE NANI ALIKWAPUA MABILIONI YA WATANZANIA?

AZIMIO LA ARUSHA ,lilipoanzishwa mwaka 1967, liliwafanya baadhi ya mafisadi waliojichotea mali za mabilioni kutimkia uhamishoni?
Kwa sababu hiyo, miongoni mwa ‘mabilonea’ hao, labda ni Oscar Salathiel Kambona?
Tujadili msuala ya zamani kidogo,ili kutazama kwa kina ujanja wa siasa. Kambona alishika nafasi nyingi,nyeti sana serikalini na katika Chama cha Tanganyika National Union(TANU) zama hizo.
Alikuwa waziri katika wizara nyeti, tena akawa Katibu Mkuu wa TANU,kabla ya kutimkia Uingereza mwaka 1967 baada ya kukosana na Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Ilikuwa kuhusu Azimio la Arusha.
Kambona, ati alikuwa na mali nyingi za mabilioni ya fedha,majumba mengi ya kupangisha jijini Dar es salaam na kwingineko nchini.
Wakati wa Azimio la Arusha kumiliki mali nyingi ilikuwa kuhalifu sera za nchi,na ulikuwa Ubepari.Kambona alipingana na Nyerere.
Aliteuliwa kuwa waziri kwa mara ya kwnza katika serikali ya MADARAKA.Septemba 9 mwaka 1960 wakati Tanganyika ikijiandaa kupokea uhuru kutoka kwa ukoloni wa Kiingreza.
Aliteuliwa waziri wa Elimu,wakati huo Julius Kambarage Nyerere alikuwa waziri Kiongozi,wadhifa sawa na Waziri Mkuu.Aliendelea kuwa waziri wa Elimu chini ya Waziri Mkuu,Kambarage Nyerere,na baadaye Rashid Mfaume Kawawa.
Madaraka hayo yalimpa kuheshimiwa sana na kupendwa na wananchi.Baada ya nchi kuwa Jamhuri,Desemba 9,mwaka 1962,Kambona aliteuliwa kuwa waziri wa Mambo ya Nchi za Nje,baadaye tena akaongezewa  madaraka na kuwa waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ulinzi.
Alikuwa na kawaida ya kuchana nyewele zake akazipinda pembeni kidogo mwa uso wake.Mtindo huo ulijulikana sana miongoni mwa vijana wa wakati huo kama, “Kambona Style”,wakati huo kabla hujachana nywele kwa mtindo huo wa Kambona,basi ulionekana wa kuja.
Kambona,ndiye aliyezima uasi wa jeshi lililotaka kumpindua Mwalimu,Januari 20 mwaka 1964.Siku hiyo wakati Jeshi likiasi,Rais NYERERE,Makamu wa Rais Kawawa na mawaziri wengine walitimkia mafichoni kusikojulikana.
Baadaye,jeshi likavunjwa likaanzishwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ), lakini baadaye baada ya kuanzishwa Azimio la Arushwa,mwaka 1967 Kambona akapinga,kwa kile wanachosema, alikuwa na mali nyingi ambazo zilikuwa mbioni kutaifishwa na umma.
Alijifanya kuugua, akaenda Nairobi nchini Kenya kutafuta tiba. Akiwa Nairobi,yeye Kambona na mkewe,Flora na binti yao wakakwea ‘pipa’ kwenda London,Uingereza.
Alipofika London,akaomba ukimbizi wa kisiasa.Wakati huo,Mwalimu alikuwa amevunja uhusiano wa kibalozi na Uingereza,wakati huo ikiwa serikali ya Waziri Mkuu,Harold Wilson,kufuatia mgogoro wa Rhodesia, siku hizi ni Zimbabwe.
Uhusiano wa kibalozi wa Tanzania na Uingereza ulivunjwa kuanzia mwaka 1966 hadi 1969.
Kufuatia hali hiyo,Kambona alikubaliwa ukimbizi wa kisiasa Uingereza, huku byuma aliacha wafuasi ambao wengine walitiwa mbaroni na wengine kutimkia ng’ambo.
                            Dk.Masha mshirika wa Kambona?
Kambona akatimuliwa uanachama wa TANU,akaondolewa ubunge pamoja na wenzake  wanne.
Miongoni mwa wabunge waliotimuliwa mwaka 1968 ni Dk.Fortunatus Lwantyantika Masha(Mbunge wa Jimbo la Geita Mashariki zama hizo),Joseph Kaselabantu(Nzega Mashariki),Wilfred Mwakitwange(Taifa),Stephen Kibuga(Mufindi) na Modestus Chogga(Iringa Kusini.
Wengine ni Eli Anangisye(Rungwe Kaskazini),Gervas Kaneno(Karagwe) na Jeremiah Bakampeja(Ihangiro,Bukoba).
Januari 22,mwaka 1968,kikao cha kwanza cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kikatajiwa mali nyingi za Oscar Kambona,aliyetimkia Uingereza.
Kwamba,kabla hajatimkia London,aliingiziwa katika akaunti zake katika benki moja ya Uingereza shllingi 500,000 ambazo leo ni kama milioni 600 hivi.Ilikuwa Desemba 6,mwaka 1966 miezi miwili kabla ya Azimio la Arusha.
Kauli hiyo ilitolewa na Kawawa,wakati huo Waziri Mkuu, alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Rombo,Alphonce Maskini,bungeni.
                                             KAMBONA FISADI?
Baada ya Azimio la Arusha,ikatangazwa kwamba Kambona alimiliki majumba mengi ya kupangisha Dar es salaam,Morogoro,Songea ambayo thamani yake ilikuwa shilingi 485,612 sasa ni kama shilingi milioni 500 hivi.
Kawawa alisema pia kwamba,KATI YA Juni 1965 na Desemba 1966 Kambona aliweka katika akaunti yake ya Jijini Dar es salaam kiasi cha shilingi 896,800 ambazo leo zingekuwa na thamani  kama shilingi bilioni moja hivi.
Matokeo ya uchunguzi wa Benki Kuu(BoT)ULIBAINI PIA KWAMBA,Juni 1965 Kambona aliingiza Pauni za Uingereza 65,800 ambazo leo ni kama shilingi milioni 165.Julai 1967 eti aliweka Pauni 60,000 ni shilingi milioni 150 za sasa.
Na kwamba,alikuwa akiingiza pesa nyingi kwenye akaunti zake,na alimiliki majumba mengi yaliyojengwa Dar kwa mabilioni ya shilingi.
                        Ati, Mwizi Mkubwa?
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alimtaja Kambona kama ‘mwizi mkubwa’ leo tungesema Fisadi Kubwa lililojilimbikizia mali nyingi.Benki kuu ya Tanzania(BoT) Ikamwandikia barua aeleze alikopata fedha za kigeni kumwezesha kukwea ‘pipa’ kutoka Nairobi hadi London.Kumbuka wakati huo kupata fedha za kigeni ilikuwa ‘mbinde’ siyo kama siku hizi kuna Bureau De Change, tena kuna dola nyingi na Euro kwenye Black Market.
Haya yalielezwa Bungeni na Waziri Mdogo wa Fedha,Bwana S.Rashid alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Bagamoyo,Bwanga Mgaza.
Kambona akiwa Uingereza alishinda Bahati Nasibu, ‘Bingo’ ya kimataifa na kulipwa mamilioni ya pesa.
Wakati vyama vingi vikianzishwa hapa nchini mwaka 1992,Kambona alirejea nchini na mkewe,Flora na binti yao.
                               Bilionea,Masikini gani huyu?
Aliishi Sinza, katika nyumba ya kawaida sana.Alidai arejeshewe nyumba yake ya Msasani,ambayo ilidaiwa ilikaliwa na Rashida Kawawa.
Huyu anadaiwa kuongoza majaribio ya kutaka kumpindua Mwalimu Nyerere,mapinduzi ambayo aghalabu yalishindikana.Kambona alikanusha kuteka ndege ya abiria kutoka Mwanza hadi London,mwaka 1982,nilishasimulia kituko hicho.
Mwaka 1992, aliporejea Tanzania Kambona akachaguliwa kuwa Rais wa Chama cha TADEA.Alipokonywa uraia akaambiwa ni Mnyasa wa Malawi,akaamuliwa aondoke nchini.
Alikaidi, akabaki Dar lakini mwaka 1993 serikali ikamrejeshea uraia wake kwa sababu za kiutu.Alifariki akiwa London,Uingereza mwaka 1997,mwili wake ukarejeshwa Dar es salaam kwa mazishi.
TADEA Kimeongozwa muda mrefu na RIFA Chipaka,Mshirika wa Kambona aliyewahi kufungwa kwa makosa ya uhaini,mwaka 1971 baadaye alisamehewa.
Azimio la Arusha likatokomezwa miaka ya  karibuni,kwa sababu hiyo Kambona angekuwa hai na mali zake angekuwa ‘tycoon’ la Afrika kama siyo duniani.
Sasa jiulize,pesa zake zilikwenda wapi? Majumba yake yalikwenda wapi? Angekuwa mwekezaji!
Oscar Salathiel Kambona, alizaliwa Agosti 13, mwaka 1928 kandoni mwa ufukwe wa ziwa Nyasa ambalo linaleta kasheshe baina yetu na Joyce Banda,mjukuu wa Kana-Ka Mzizi,Banda.
Alizaliwa katika kijiji cha Kwambe,Mbamba Bay eneo la wilaya ya Mbinga.
                                       Rafiki Mkia wa Fisi?
Walikutana na Mwalimu,Julius(Butiama walimwita Kambarage tu)Nyerere katika sekondari ya Tabora Boys.Wakati huo,Mwalimu alikuwa akifundisha katika shule ya  St. Mary’s  ya Wakatoliki pale Tabora. Baadaye sasa ndipo Kambona aliteuliwa Katibu Mkuu wa TANU.
Wakati wa maasi ya jeshi la kikoloni,Januari 1964,Kambona alijitoa mhanga akawafuata wanajeshi Calito(Lugalo) jeshini;badala ya kurushwa kichura akaongea nao na wakakubaliana.Akina Nyerere na Kawawa na mawaziri walishajificha kabisa.
Askari walitaka nyongeza ya mishahara,na walitaka wale askari wa Uingereza wapishe vyeo askari Weusi wazalendo,ilikuwa ngoma nzito,Nyerere  na Kawawa walishatoroka-Mapinduzi!
Kambona katuliza fujo,mambo yakawa shwari,ukawa urafiki mkubwa na Mwalimu.Wakati Kambona anamwoa aliyekuwa Miss Tanzania,Flora,Nyerere alikuwa Best Man!
Kumbe,rafiki mkia wa fisi? Kambona na Nyerere wakakorofishana,Kambona katimkia London, Julai mwaka 1967akawa anafanya kazi ya mshahara mdogo,na nyumba ya kuishi alilipiwa na Uingereza kwa ruzuku ya serikali. Utajiri alipeleka wapi?
Kufuatia kuondoka kwake,nduguze,Mattiya na Otini Kambona walitiwa mbaroni na serikali. Unacheza wee!
Jaribio la mapinduzi la Oktoba 1969 alisemwa kuhusika,alihukumiwa akiwa uhamishoni,aliporejea nchini mwaka 1992 akaahidi ‘kutoboa siri’ mahali Nyerere na Kawawa walipoficha mabilioni ya fedha walizouibia umma wa Watanzania!!
Kumbe, ‘geresha’ tu, wanasiasa bwana! Kambona hakuwahi kuwatajia Watanzania fedha walizoiba Nyerere na Kawawa tangu Uhuru.
“Credibility” ya Kambona ilishuka,watu wakamwona aliyechanyikiwa tu,akazidiwa kete na akina Mtikila na Mrema, alisema uongo. Hadi anakufa London Julai mwaka 1997 hakuwa na mvuto tena katika siasa za Tanzania.
Atakumbukwa kama mkimbizi wa kwanza wa Tanzania London, alipigia debe mfumo wa vyama vya upinzani,na alijaribu kumpindua Mwalimu.
              Propaganda,chenga ya mwili ama Danadana?
Hayati Mwalimu Nyerere na Kawawa,walisema Kambona aliiba mabilioni ya shilingi na kutokomea nayo Uingereza.
Wakati Oscar Salathiel Kambona, alipofika uwanja wa ndege wa Dar wakati anarejea toka uhamishoni,akasema angemwaga mtama mahali Nyerere na Kawawa walipoficha pesa walizoiba nchini!
Hata hivyo, hawa wote watatu wamefariki.Nasi tungali tunajiuliza, “Hizo fedha zilizodaiwa kuibwa(na pande mbili za shilingi) na Nyerere,Kawawa na Kambona, zilifichwa wapi? Ama,ndiyo mabilioni ya Uswisi?
Bila shaka, hapakuwa na mwizi mahsusi kati yao wote watatu,bali propaganda tu kati yao na kuchafuliana majina!
0713 324 074
 
 
 
 
 
 

siyo vurugu,ni ukosefu wa kazi!!

      VURUGU  MWANZA
      Wananchi wadai mabomu ya machozi,risasi za moto ,magereza makubwa,  siyo suluhisho
Na conges mramba,mwanza
NI UKWELI USIOPINGIKA, kwamba Jiji la Mwanza linakabiliwa na ‘milipuko ya Volkano’ya machafuko mara kwa mara.yaletwayo na makundi ya vijana wasio na ajira rasmi,kila kunapokucha.
Kwa miaka mitatu sasa Mwanza inashuhudia,mirindimo ya risasi za moto,mabomu ya machozi na virungu, ambavyo hutumika kuwatawanya na kuwadhibiti vijana wenye mawe,magongo,matofali na magogo ya miti waofunga barabara,kuchoma moto magari na majumba,wakati mwingine huvunja maduka hususan ya wafanya biashara wa Kiasia na kupora mali nyingi za thamani.
Siku moja baada tu ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010,(Jumatatu,Novemba Mosi) makundi ya vijana,waliodaiwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)walifunga barabara ya Makongoro iendayo Uwanja wa ndege,mahali paitwapo,Nera na kuichoma moto ofisi ya CCM ya kata ya Isamilo,ambayo iliteketea pamoja na mali nyingi za thamani.
Jumanne, wiki iliyopita(Januari 22,mwaka huu) katika barabara hiyo ya Makongoro,jirani na eneo hilo la Misheni na Nera, kundi kubwa la waendesha pikipiki maarufu kama ‘Bodaboda’ walikivamika kikosi cha polisi(TASK FORCE) kilichokuwa kikiendesha kampeni kamambe ya kudhibiti makosa ya Usalama Barabarani.
Ilikuwa saa 3.30 hivi,asubuhi, polisi waliwatia mbaroni waendesha Bodaboda wasiozingatia sheria na kuwatoza faini.
Wakavamiwa na makundi ya waendesha bodaboda na kupigwa mawe hadi walipolazimika kufyatua mabomu ya machozi na risasi za moto hewani,ili kuwatawanya.
Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza,Ernest Mangu, amesema waendesha bodaboda wasiozingatia sheria waligoma kukamatwa na waliazimu kuwatorosha wenzao waliokuwa chini ya ulinzi.
“Hawakuwa na leseni,na wengine walipakia abiria zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja,maarufu kama mishikaki,hawakuwa na kofia ngumu,helmet,wakati mwingine hukatisha barabara na kuwagonga waenda kwa miguu na kutokomea pasipo kujali…tumeamua tu ‘deal’nao,tuliwatoza faini ndipo wakatokea wahuni kutaka kupora pikipiki zilizokamatwa kwa nguvu”,alisema Kamishna Msaidizi wa Polisi,Ernest Mangu,Jumanne iliyopita.
Kamanda Mangu akaongeza kuwa hao Bodaboda walikuja juu wakafunga barabara hiyo iendayo uwanja wa ndege kwa mawe makubwa na matofali,polisi wakawadhibiti na kuwatia mbaroni baadhi yao wengine wakatokomea.
Alisema kwamba, waendesha bodaboda 26 walitiwa mbaroni,10 kati yao wakalipa faini wakati wengine waligoma kufanya hivyo wakaanzisha vurugu.
“Tumewadeaka wanne wanaisaidia polisi na pikipiki 13 zilikamatwa za wale wengine waliotimka wakaacha pikipiki zao nyuma,wakichelea kutiwa mbaroni na kufikishwa mbele ya sheria”,amesema Kamanda Mangu akipa kuwa ni lazima jeshi la polisi lisimamie sheria za usalama barabarani.
“Hatutakubali Bodaboda wavunje amani ya nchi.Wanasababisha ajali nyingi;vifo vingi vya wasio na hatia,na hata wakimgonga mtu hukimbia,hawataki kusimama..tulifikiri tuwavumilie tuwafundishe kuihshimu sheria,kumbe hawataki…wamejipalia makaa ya moto vichwani!”amesisitiza.
Katika makabiliano hayo ya wiki iliyopita,hakuna aliyefariki dunia. Lakiki,katika matukio yaliyotangulia, watu walikufa ama kujirehiwa kwa risasi za moto.Mwaka 2004, wakati wamachinga wakichoma moto matairi barabarani,mtu mmoja alifariki kwa kupigwa risasi alipojaribu kuvamia duka la SH Amon,Barabara ya Nyerere.
Kamanda Mangu,alipoulizwa kuhusu hali za polisi waliodaiwa kujeruhiwa vibaya katika vurugu hizo, alisema alipatwa michubuko midogo tu,kitu ambacho hutegemewa kila mara na Jeshi hilo wakati wa makabiliano na wahalifu.
Mwaka 2011 makundi ya vijana waliojiita Wamachinga, walifanya vurugu na kuvamia maduka na nyumba za ibada za Wahindi katika mitaa ya Rwagasore,Lumumba,Makoroboi na Barabara ya Nyerere nakuvunja na kupora mali nyingi za thamani,huku wakisema ‘Wahindi waondoke’.
Vurugu hizo zilifuatia kampeni ya Halmashauri ya Jiji ya Usafi wa mazingira, hali iliyosababisha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani,Shamsi Vuai Nahodha kufika Mwanza ili kujionea uharibifu.
Kulingana na wasifu, wa Jiji la Mwanza(Mwanza City Profile) Jiji hili lina watu wasio na ajira rasmi wanaovuka asilimia 30, ambao hukaa vijiweni kutwa wakisubiri machafuko yatokee ili wakapore ngawira madukani na majumbani mwa watu.
Kufuatia hali hiyo,Mwanza kuna makundi ya vijana na watoto wa mitaani, ambao huota vurugu iwepo ili wapore mali za watu.
Changamoto lilimuuliza RPC,Mangu kwamba sasa sura ya Jiji la Mwanza ni ipi,ikiwa RPC Liberatus Barlow kauliwa Oktoba 13 mwaka jana huko Minazi Mitatu,Kitangiri, maduka ya Wahindi na nyumba za ibada zimeporwa,majumba yamechomwa moto na vijana hawa?
Je,wawekezaji toka nje wanaweza kuwa na moyo mgumu kuja kuwekeza Mwanza yenye vurugu za wamachinga na waendesha bodaboda za kila siku?
“Mwanza ni shwari ka ukuaji wa uchumi na vitegauchumi,isipokuwa wakorofi wachache ambao tutawadhibiti”,alisema.
Wataalam wa Soshoolojia waliofanya mazungumzo na gazti hili wiki iliyopita,wamesema changamoto kubwa inayolikabili Jiji la Mwanza na makundi ya watu kutoka vijijini katika mikoa yote ya Kanda ya Ziwa,na hata Sindiga,Rukwa na Kigoma ili kuja Mwanza kutafuta ajira.
Wanapokuta ajira hakuna na maisha ni magumu,chakula hakuna,hujiingiza katika vitendo vya uvunjaji wa sheria.
“What the hell do you do about a whole generation of unemployed people? What they do is turn to crime”, wamesema wataalam hao kwa masharti ya kutotajwa majina,wakimaanisha kwamba kizazi cha wasio na ajira,wasio na kazi hugeuka kuwa wahalifu,endapo serikali haitafanya mkakati wa kuboresha uchumi na miundombinu ya uchumi huko vijijini ambako vijana hukimbia ili kuingia mjini kutafuta maisha.
Wananchi waliofanya mahojiano na Changamoto wamesema,kama serikali haitaanzisha  sheria ya Nguvu Kazi iliyokuwepo zama za Mwalimu Nyerere na kuboresha miundombinu vijijini,vijana watazidi kuingia mjini,kufanya vurugu na kupora mali za watu,wengine watakuwa bodaboda wasiozingatia sheria.
“Sheria kali,kuimarisha na kujenga magereza makubwa,magari ya upupu,mabomu ya machozi na risasi za moto hazitakomesha machafuko,fujo na maandamano na uhalifu wa kila siku Jijini Mwanza,ikiwa serikali na jamii hawatatafuta njia mwafaka ya kupunguza tatizo la ajira na wimbi la vijana kukimbia vijijini na ku

TUMKUMBUKE KABILA WA CONGO HII JANUARI

Tumkumbuke Hayati Laurent Desire Kabila na Patrice Lumumba, na tujiulize nani aliwaua?
 
 Januari 16 mwezi huu, Rais wa zamani wa J.K. Kongo, Laurent Desire Kabila, alitimiza miaka 12 kamili tangu auliwe na mlinzi wake, Meja Rashid Kasereka katika Ikulu ya Kinshasa .
  ‘Papa’ Kabila, alikufa Jumanne, Januari 16 mwaka 2001, kwa kupigwa risasi ndani ya Ikulu hiyo, kufuatia mgogoro baina yake na washirika wake waliomwezesha kuwa kiongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Waliomwezesha Kabila kuingia Ikulu walimuua na sasa wanautafuta uhai waaaaa Kabila mtoto!
  Kabla ya mauaji hayo, nchi hiyo maarufu sana Barani Afrika, ilikwisha geuka uwanja wa vita vilivyosababisha  Mataifa ya kigeni: Rwanda , na Uganda kujipenyeza ndani yake kwa kisingizio cha usalama wan chi zao.
 Sambamba na kuyasaidia majeshi ya waasi wa serikali katika harakati zao za kutaka kuipindua serikali kwa madai kuwa ilikithiri kwa rushwa, ukabila,upendeleo na utawala mbovu.
   Naam. Miaka 12 kamili baada ya kifo cha ‘Papa’ Kabila, roho mchafu wa rushwa, ukabila, upendeleo na utawala wa hovyo, angali akitafuna mataifa haya yote ya Maziwa Makuu; hata kama mengine yana amani ya kuegesha.
    Rwanda , Burundi , Kongo yenyewe na sasa Kenya hutafunwa na ukabila; wakati majirani zetu kama Somalia na Sudan , hususan Darfur, tatizo hilo linafanya nchi kuvunjika vipande, na maelfu ya watu kufa, wengine makazi kutafuta hifadhi ya ukimbizi katika mataifa  mengine,
   Angola , Zimbabwe na Namibia zilijitosa kumsaidia Hayati Kabila asipinduliwe mapema na vikosi vya waasi wakiongozwa na Watutsi wa ‘Banyamulenge’.
 Licha ya kukubaliana kuacha mapigano katika majadiliano ya siku 13 mjini Lusaka , Zambia yaliyofanyika tangu Julai 10 mwaka 1999; vita vikaendelea katika nchi hiyo ya tatu kwa ukubwa Afrika; na yenye utajiri wa madini ya thamani kubwa.
   Mahali penye utajiri wa nishati na madini kama almasi na dhahabu ndipo mafisadi huchochea ukabila na vita vya kila mara ili wananchi wa kawaida, wasije wakapata fursa kusaka maendeleo huru nay a dhati. Naam,makampuni ya Magharibi.
   Kati ya Feburuari 24 na Juni 16 mwaka 2000, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliingilia kati mgogoro wa Kabila na Banyamulenge, na kuamuru majeshi ya kigeni kuondoka.
    Tumeona Rwanda na Uganda wakiwasaidia Banyamulenge kumwondoa ‘Papa’ Kabila madarakani, na tumeona Namibia , Zimbabwe na Angola yakisaidia majeshi ya serikali kuvitimua vikosi vya waasi
Hapakuwa na mafanikio.
   Basi, Baraza hilo likaamuru kupelekwa askari wa Umoja wa Mataifa wapatao 5,537 ili kusaidia kutekeleza makubaliano na kusitisha vita.
Katika jitihada za kumwokoa Kabila, alikutanishwa na Rais wa Rwanda , Meja Paul Kagame nchini Kenya ambako nako siku hizi baadhi ya watu, wakiwemo watoto na akina mama wanateketea katika miali mikali ya moto na maiti zao kuwa majivu. Unakumbuka vita vya baada ya uchaguzi,mwaka 2007?
   Kagame alikutana na Kabila nchini Kenya Juni 13 mwaka 2000.
Mapigano yakaendelea; yakasambaa hadi katika roho ya nchi penye utajiri wa madini na shughuli za kiuchumi.Siku hizi wanakutana Kampala.
   Naam. Utawala wa Kabila ulikoma Januari 16, mwaka huo 2001; yeye mwenyewe akauliwa kwa risasi kutoka kwa mlinzi wake ndani ya ikulu. Mlinzi huyo, Rashid Kasereka, aliuawa punde.
Kabila akarithiwa na mwanaye, Meja Joseph Kabila Kabange(42), anayejaribu kurejesha amani na kuleta maelewano miongoni mwa makabila yote ya ‘Bacongo’.
   Bado kuna vita na mauaji; na majeshi ya kigeni yangali yakichochea migogoro Kongo.
Naam, migogoro ya Kongo huchochewa na baadhi ya waafrika wenzetu, vibaraka wa Wakoloni wa zamani, kwa tamaa ya rasilimali za nchi.
  Kabila alifanya kazi moja…kukomesha utawala wa kibaraka mkongwe wa wazungu Afrika, Marehemu Dikteta Kuku Mbendu wa Zabanga wa Zaire ,maana yake Buldoza,linakopita hakibaki kitu!
, koplo wa zamani Seseseko Joseph Desire Mobutu!
Ilikuwa Mei 17, mwaka 1997.
   Kabila, akaibadili Zaire kuwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, baada ya kushika hatamu zote, kufuatia ushindi katika vita ‘laini’ dhidi ya serikali taabani ya Mobotu.
Baadaye, Banyamulenge waanzisha uasi dhidi ya ‘Papaa’ katika miji ya Bukavu na Goma mnamo Agosti Pili, 1998. Vikosi vya waasi vilipata nguvu kutoka nadharia ya Kitutsi ya majeshi ya Rwanda na Uganda .
   Inadaiwa, utawala wa Kabila uligubikwa chuki, mafarakano na uchoyo uliozaa mauti yake mwenyewe.
   Alirithi utawala wa choyo na rushwa toka kwa Mobutu, aliyesimikwa madarakani kwa masaada wa Mabeberu wa Magharibi, baada ya mauaji ya Waziri Mkuu, Patrice Emery Lumumba, mwaka 1961.
Tumekwishaona jambo hili,usikose safu hii.
   Kabila alipiga marufuku vyama vya siasa Mei 20 mwaka 1997. Akamweka kizuizini mwanasiasa aliyempinga, Etiene Tshisekedi. Tshisekedi alizuiliwa kijijini kwao Kasai, Feburuali 12, mwaka 1998 kwa sababu zili walizonazo watawala wetu hadi sasa- za hofu ya kuondoshwa mamlakani.
   Hayati Kabila alikuwa na uhusiano na Rwanda na Uganda tangu zamani. Biashara ya magendo ya almasi na dhahabu pengine ilifanyika wakiwa pamoja, ili kuimarisha vikosi vyao.
Kabila aliipinga serikali ya Kongo, Museveni alimpinga Obote na baadaye Tito Okello, na Kagame aliwahi kwenda msituni na waasi wa RPF dhidi ya serikali ya Rwanda .
    Walihitilafiana.
Museveni na Kagame wakaanza kumpinga Kabila, wakasaidia waasi ili kumwondoa huku kukiwa na madai ya kuiba madini.
 Baadaye majeshi ya Rwanda na Uganda yalichapana ndani ya Kongo kwa sababu zinazofahamika. Kumbukumbu ya hayati Kabila itufundishe kujua aina ya viongozi tulionao Afrika. Ni vibaraka wa adui wa Afrika.
   Uganda iliingiza jeshi lake Kongo mwaka 1998 kwa kisingizio cha kuharibu makambi ya waasi wa serikali wa Allied Democratic Front.
Ilidaiwa, walipata msaada toka Sudan .
Serikali ya Kampala ikihofia kwamba kulikuwa na makambi ya mafunzo ya waasi katika Kabaya, Kanyabayonga, Kibumba na maeneo ya jirani  na Goma.
    Majeshi ya UPDF na RPA yaliingia Kongo kupigana bega kwa bega  na waasi dhidi ya serikali ya Kabila.
Umoja wa Mataifa uliweka sharti majeshi hayo kuiacha Kongo chini ya Jeshi lake, UN Military Observer Mission for Congo (Monusco).
   Uganda na Rwanda zilionyesha kudharau amri hiyo wakaendelea kuwalea waasi wengi, akina Mbusa Nyamwisi(baadaye alijiunga na serikali), Profesa Ernest Wamba dia Wamba, na wale wa RCD Kisangani.
Mbusa Nyamwisi alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje  baadaye. Ni vita,ili kugawana madini ya Afrika.
   Hata baada ya Kongo kufanya uchaguzi wa Kidemokrasia, na  Rais Kabila kushinda, Kongo kungali na vita ya kikabila.
Yamefanyika mapatano kati ya Marais Kabila na Yoweri Museveni yaliyosimamiwa na Rais Kikwete katika hoteli ya Ngurdoto, Arusha. Hakuna kitu,vita vinaendelea kwa miaka 51.
   Inadaiwa, licha ya mapatano ya kuacha chokochoko, Rais Kabila hajamwamini sana Museveni.
   Kongo, kungali na Waasi wa Kitutsi kama, Laurent Nkundabatwale, wanaojaribu kukalia milima ya  Rumuhe na Mumba, Kaskazini mwa mji wa Ngundu. Kuna akina Bosco Ntaganda na wenzao wa M 23.
   Joseph Kabila, ambaye aliwahi kusoma Tanzania na kupata mafunzo ya kijeshi, JKT Makutupora, na baadaye Uchina, alimrithi babaye Januari 24, akaapishwa siku mbili baadaye, mwaka huo wa 2001.
    Baada ya kushinda uchaguzi na kuunda serikali, anaongoza nchi kubwa yenye watu zaidi ya milioni 60.
Hii ndiyo nchi mabeberu walimuua Patrice Lumumba Januari 17 mwaka 1961.
    Ndiyo, mwezi huu unaokwisha tunamkumbuka pia mwanamapinduzi Patrice Emery Lumumba, katika mapambano ya kudai uhuru wa kweli,  na njama za vibaraka.
 Ni kipindi cha kukumbuka urais wa akina Moise Tshombe, Juni 30 mwaka 1964.
    Jenerali Mobutu alitawala 1965, Congo ikawa Zaire mwaka 1977 kutoka Jamhuri ya Kongo toka 1966.
 Kabila, aliwatumia Watutsi kupindua serikali ya Mobutu ambaye alikuwa akitibiwa saratani, Ughaibuni, Mei 17, mwaka 1997.
   Mobutu alikwenda uhamishoni, na baadaye akafariki mjini Rabat Morocco , Septemba 7 mwaka huohuo.
 Mobutu ametawala Congo miaka 33; lakini ameondoka bila heshima sawasawa na Idi Amin, Jean Bedel Bokassa, na wengine wa kariba hiyo. Mafisadi wanaojifanya vibaraka wa Mzungu hapa nyumbani.
 Historia haiwaheshimu watawala mafisadi wa dunia, japokuwa wataiba sana na kuwa matajiri.
  Hawa hawana heshima kama akina Nyerere, Nkrumah, Samora, Gamal Abdel Nasser, Mandela na wengine.
   Tunapomkumbuka Kabila na Lumumba, tuitazame Afrika inavyoteketea katika moto baada ya madai ya mbinyo wa demokrasia na wizi wa kura.
Tuwatazame raia fukara dhidi ya watawala matajiri walioshiriki kuiuza Afrika vipande thelathini vya fedha.
    0786 324 074’0754 324 074

 

KUTOKA ANOLOJIA HADI DIGITALI YA USHOGA

MWANZA:Kutoka ‘Anolojia’ kwenda ‘Digitali’ kiaina!!
JANUARI MOSI,mwaka huu mpya,2013 nilikuwa Buswelu,katika Halmashauri mpya ya wilaya ya Ilemela, kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka na mwanzo mwaka mpya.
Nimebaini kuwa wenyeji wa eneo hilo wameuza mashamba yao na kujiondokea.Wanapisha jiji linalokua kwa kasi ya ajabu. Mwanza ni Jiji la wakazi milioni moja, ambalo majumba ya fahari yanamea kama uyoga,na vitega uchumi vipya huanzishwa,zikiwemo taasisi za kigeni.
Inawapasa wenyeji kuuza viwanja na mashamba yao na kuuhama mji;wanatafuta pa kwenda kuishi.
Umasikini unapoongezeka vijijini, kuna watu hulazimika kuuza ardhi:Mashamba,viwanja na mifugo na kuingia mijini,wakijaribu kufanya biashara ndogo kwa mitaji midogo,ili kujinusuru.
Kufuatia hali hiyo ya baadhi ya wanakijiji kuhamia mijini, “Urbanization” hata Wazungu hununua mashamba ya wenyeji pembezoni mwa mji kama Buswelu,Buhongwa,Bugogwa n.k
Wakati wamasikini wa mjini huuza viwanja na mashamba na kujiondokea, wale wa vijijini huuza masahamba ma viwanja vibanda vyao na kuingia mijini,kujitafutia ajira,maana maisha ni magumu vijijini,na hakuna miundo mbinu.
Kwa sababu hiyo,ukosefu wa ajira, “Unemployment” unakimbia kutoka asilimia 30 hivi,kwenda asilimia 50.Ombaomba ni wengi,wengine huvalia suti na tai, na watoto wa mazingira magumu hashikiki.
Ukisikia ‘bomu’la watoto wa mitaani,basi Mwanza linakaribia kulipuka,litawalipukia watawala usoni.Mtu akiwapa chakula akawaambia waandamane na kufanya vurugu ama kupora maduka ya watu,hawatasita aslani.
Vurugu,maandamano na fujo za Mwanza,hufanywa na watu wa kariba hii,baadhi yao sasa ni watu wazima wasio na makazi.Huishi mitaloni na vibarazani mwa maduka ya Wahindi.Mvua yao,jua lao,na baridi za usiku wanazijua wao.
Vitendo vya ukahaba,ushoga,ujambazi,uporaji na unyang’anyi sasa hufanywa na kundi hili.
Jiji  kama New York, asilimia 80 ya wafungwa na wanaoswekwa rumande ni watu wa kundi hili,hususan Wahamiaji Weusi kutoka Latin Amerika au Caribbean.
Wakati watoto wa matajiri na wenye fursa bora za ajira na ukwasi, wakisoma shule na vyuo bora,wanajiandaa kushika nafasi za uongozi serikalini na katika jamii.Masikini hawana uchaguzi mwingine zaidi ya kuwa watumishi ama watumwa na watwana wa hawa ‘supervisors, principals and rulers’.
Licha ya serikali kuajiri polisi vijana na wengine askari wa Jiji,Mwanza hushuhudia uvunjaji wa sheria wa makusudi na mapambano ya kila mara ya wanamgambo wa Jiji,polisi na makundi ya vijana wanaojiita,Wamachinga.
Maisha magumu,husababisha uvunjaji wa sheria na vifo kila siku. Uhalifu,uvutaji bangi,ubwia unga,kutafuna mirungi. Hawa, “Drug addicted burglars” hutamani vita vitokee,wenye maduka makubwa, ‘shopping malls’ watimue mbio,wao wajimilikishe kile kinachosalia!
Nataka nikwambie,kwamba Mwanza hapa,vijana wanawachukia polisi na wenye mamlaka,kuliko kawaida. Mwanza kunanuka machafuko ‘violence’ kila kunapokucha,sababu kubwa ni umasikini kuongezeka-money shortage!
Watu wanakosa kulipa kodi ya pango(inaongezeka kila mchana na usiku),mtu huachia chumba na kwenda kujibwaga mtaloni.Fedha hazipatikani,ni balaa za pesa-financial doom.
Kila siku, polisi hufukuzana na machangudoa wanaouza miili yao katika mahoteli makubwa ya wageni,katika vilabu vya usiku na maeneo mengine ya starehe.
Unaweza kukutana na msichana wa mwaka wa pili au wa tatu katika Chuo Kikuu hapa, anajiuza ili apate mahitaji.Wengine ni wasichana warembo, na hawapendi kuitwa changudoa,wanataka waitwe ‘Wafanyabishara’ au watoa huduma ya ngono, “Commercial Sex Workers” kwa kifupi,waite “CSW”.
Maisha magumu eti yameleta uwekezaji wa ajabu na miradi ya kushangaza,biashara ya ngono,picha za uchi “Pornography”na zingine hupigwa na Wazungu mchana kweupe,wakati mamlaka ikiangalia,na kukosa meno.
YUNUS Santy, maarufu kama Angelo(67) alihukumiwa kifungo cha miaka  mitano jela, au kulipa faini ya shilingi 300,00 baada ya kupatikana na hatia ya kupiga picha za uchi na visichana viwili vyenye umri wa miaka 16 na 17.
   Angelo, ambaye ni raia wa Italia, alikutwa na visichana hivyo vyenye umri wa miaka 17(bila shaka wanafunzi) katika chumba cha Hoteli ya Paradise,iliyopo Unguja, jijini Mwanza.
    Alikuwa akifanya ngono na kasichana kamoja wakati kengine kakipiga picha ya tukio hilo. Pia, alikutwa na viungo bandia vya sehemu za siri za kiume.-toy boy.
Bila shaka, alikuwa akivitumia viungo hivyo bandia kuzima kiu ya ngono kwa visichana kama hivi.
    Ilikuwa Septemba 20 mwaka 2007, Mtaliano huyu aliyejitambulisha kama Mmisionari wa Kikatoliki, alipovichukua visichana hivyo katika mitaa ya jiji la Mwanza, akavipeleka hoteli ya Paradise(Paradiso) ili kula maraha!
      Wasichana hao wakaacha masomo ili kwenda kusaka pesa zinazosakwa leo kwa udi na uvumba, kuliko utu.
    Naam, Angelo aliposhindwa kutimiza ahadi kwa wasichana hao, walitoa taarifa polisi, ambao walimtia mbaroni kisha kumfikisha Mahakamani.
    Mwendesha Mashitaka, Inspekta Msaidizi wa Polisi, Inogu Kimasa, akaiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mwanza kwamba, Angelo ambaye ni Mmisionari wa Kanisa Katoliki, alifanya kosa la Jinai kinyume cha Sheria ya Kujamiana ya mwaka 1998.
   Siku chache kabla ya Siku Kuu ya Idi, Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Auqinea Lujwahuka, akamhukumu Angelo kifungo cha miaka mitano jela(alikiri kosa), au kulipa faini ya shilingi 300,000.
   Mmisionari huyo alilipa faini hiyo kwa kosa hilo alilotenda wakati wa mfungo wa Ramadhan. Hata hivyo, aliamuriwa kuondoka nchini, kwa sababu makosa yake yanakiuka sheria na Katiba ya nchi.
Akakabidhiwa kwa Idara ya Uhamiaji, mkoa wa Mwanza ili hatua za kumwondoa nchini zitekelezwe.Angekuwa Mswahili,bila shaka angefungwa kifungo cha maishajela au miaka 30.
     Hili ni tukio moja kati ya mengi yaliyoibuka wakati wa ujio wa Wazungu, wakiwemo watalii, wawekezaji wa migodi na wamisionari uchwara.. Hawa, wanatambua uzumbukuku, ulafi, ushamba na ulimbukeni wa wasichana wan chi hii kupenda sana kuzuzukia  kila kitu, mradi kililetwa na Wazungu.
      Naam, Filamu za uchi, “Nudie Film” hususan zile za ngono(sex film) hutengeneza pesa nyingi. Kwa sababu ya jamii tuliyomo kuwa na kiu ya ngono, anasa na pesa, filamu hizi hupendwa.
    Filamu hizi zina wateja wengi, watu wa kila rika, kila tabaka; hivyo wauzaji wa filamu hizi wananafasi ya pekee sana ya kutengeneza pesa nyingi na kujipatia maisha mazuri kwa kipindi kifupi.
   Watu wengi, hususan wanafunzi wa shule zetu za sekondari wenye umri huo wa kuanzia miaka 17 hupenda sana ngono na picha za aina hiyo.     Wasichana wa umri huu wamekubuhu sana kwa ngono kupitia filamu hizo.
   Hivyo, akitokea mtu mwenye fedha-awe Mmisionari au tapeli-akaahidi kuwalipa pesa wasichana hawa, atafanya atakavyo kwa hawa wengi sana. Watatoroka masomo, watafanya ngono hata na mbwa, midoli na chochote kile, mradi tu walipwe ujira kidogo, juisi na hata chakula cha mchana katika mahoteli haya ya Nyota Tano.
    Kisha, watarejea shuleni au nyumbani kwa na vizawadi vya kitoto, bila walimu, walezi na wazazi kubaini, ufirauni wa Wamisionari kama Angelo.
     Kwa kutumia fedha walizolipwa na akina Angelo, watanunua vivazi vya aibu, suruali za kubana sana makalioni na vijishati vinavyoacha vitovu nje. Watanunua vipodozi hata vya kugeuza midomo kuwa myekundu mithili ya radi.
   Angalia vitabu wanavyosoma watu hawa. Angalia magazeti wanayopenda kusoma. Ni yale yenye picha, maandishi ama filamu za ngono(Pornography).
       Vitabu vya ngono, magazeti ya watu wanaotembea uchi, au waliopigwa picha wakifanya ngono; na wengine waliofumaniwa! Magazeti ya aina hii hupendwa sana na watu wakizazi cha zinaa.
   Siku hizi kuna mitandao ya Intaneti; humo kunapatikana picha nyingi za ngono na za wasichana warembo walioacha utupu maungo yao ya tashtiti. Katika vibanda vyenye kompyuta za intaneti, tunaambiwa wanazuia watu kuangalia picha za ngono.
 Lakini, siku hizi hata katika simu za mkononi kuna intaneti; na mtu aweza kupokea picha ama kuzituma kwa yeyote. Siku hizi, visichana hujipiga picha vikiwa maliwatoni vikioga, picha hizo za utupu husambazwa kwa njia za kisasa sana kama ‘broadband’ wakati mwingine vitendo vya ngono na fumanizi hurushwa moja kwa moja.
Wiki chache zilizopita, zaidi ya wanafunzi 20 wa Seminari ya Nyegezi inayomolikiwa na Kanisa Katoliki,walitimuliwa masomo kwa kosa la kujihusisha na ushoga!Wavulana hao wa sekondari,walibainika ni mashoga,wakafukuzwa shule,kwa sababu Kanisa Katoliki limesema,halitavumilia matendo hayo ambayo ni kinyume na maadili ya dini.
Sasa,unaweza kuna namba Mwanza,vijana wa kiume na kike wanavyohama kwa kasi ya ajabu ‘KUTOKA ANOLOJIA KWENDA DIGITALI’.
Mwanza,kiunga cha Sodoma na Gomorrah,kwa sababu mamlaka inakaribia kurasilimisha biashara ya ukahaba na ngono-sexual entertainment businesses.
Biblia,inapinga ushoga:Mambo ya Walawi 18:22.Lakini katika zama hizi za maisha magumu na uchumi mbaya,nani amfuate Bwana Mungu ili akafe njaa?
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mwanza,Zelothe Stephen(sasa kastaafu) aliwahi kusema, “Haijatungwa sharia ya kuwatia hatiani watu wenye mwelekeo wa ushoga ama makahaba.Tunapowatia mbaroni,tunawashitaki kwa makosa ya Uzembe na uzururaji”, alikuwa akitoa maelezo kwa wanahabari juu ya mvulana aliyekutwa asubuhi akiwa kavaa heleni,vivazi vya kike, ana akiwa kapaka wanja wa midomo huko Mabatini!
Mwenyekiti wa Wenye Viwanda,Biahsra na Kilimo(TCCIA)Joseph Kahungwa, hawezi kusema biashara ya ngono nayo itambuliwe na Chamber of Commerce!
Labda,wanafanya hivi kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete aliwahi kusema,Mwanza utajengwa ili kuwa mithili ya Los Angeles.Uwekezaji mkubwa!
Jiji lenye uhaba mkubwa wa ajira,lenye wahamiaji wapya,wageni wanywa mchuzi wa mbwa(hot dogs) fukweni mwa maji ya ziwa kubwa Victoria. Jiji hili ni vigumu ku ‘accommodate the latest influx or poor marching guys!
Jiji la vijana wanaoishi ghetto,ndani ya majengo ya magorofa marefu, skyscrapers, wakati wengi wanapoishi vilimani.Naam, mapangoni na mtaroni. Ndani ya makazi ya mbavu za mbwa-slums!
          Umasikini,panya,magofu ndani ya Jiji la fahari
Nihitimishe kwa kusema, Rais Jakaya Kikwete akifanya ziara katika makazi ya polisi,hususan Kigoto, atakutana na mabango makubwa ya watoto wa polisi na wake zao yameandikwa hivi:
“Rais tuokoe mapanya buku yanatumaliza huku!” Lingine litaandika, “Tumechoka kukaa katika maghala ya Wahindi kama pumba!” na linguine litasema,  “Walinda usalama wa raia wakati hatuna usalama katika magofu yaliyoachwa na Wahindi!”
Naam,Rais akifika Kigoto na kukumbana na mabango haya ya jamaa za polisi(nasikia polisi wenyewe wamekula kiapo cha kutoandamana au kubeba mabango kama raia wa Mtwara)basi Kikwete atashuka kwenye Limousine yake na kuahidi kuwasaidia hao akina mama wenye kuhema kwa kubeba mabango yenye ujumbe mzito! Ataahidi polisi kupewa makazi bora.
Vinginevyo,mapanya buku yaliyojazana katika magofu ya Kigoto wanakoishi polisi wa Mwanza,yatawamaliza vidole,yanakomba hata mboga chunguni! Usalama wa Raia pasipo usalama wa Polisi?
0786 324 074