Wednesday, February 13, 2013

PAPA BENEDICT XVI AMETEMWA NA SYSTEM VATICAN



FEBURUARI 11, mwaka huu wa 2013,Papa Benedict XV1 ametangaza kuachia ngazi ya Upapa(Papacy).
Papa,ni Askofu Mkuu wa Vatican, ambaye huchaguliwa na Makadinari aghalabu Papa mwingine anapofariki dunia,au kuachia madaraka.
Papa Benedict XVI alitishia kuachia ngazi mwaka jana; na tayari katangaza rasmi azma yake ya kuondoka katika kiti cha enzi cha Ukuu wa Kanisa Katoliki na Ukuu wan chi ya Vatican, Feburuali 28 mwaka huu.
Sababu, eti ni afya mbaya, wakati tulishaona PAPA JOHN PAUL II aliugua ugonjwa wa kutetemeka,akashindwa kuongea,lakini wakasubiri hadi alipofariki dunia mwaka 2005.
 Mwaka 753 BC mji uliojengwa Ulaya ni Rome. Na Vatican inazungukwa na Rome, ni mji wenye ukubwa wa ekari 108.7 tu ndani ya Rome.
Hata London haukuwepo, Uingereza ilikuwa kijiji kidogo mwaka 1000 AD. Hata mwaka 500 BC Rome lilikuwa jiji tena “SUPER POWER” Duniani, ulijengwa na Romulus.
 Katika mji huu ndiko yaliko mamlaka ya kidini,Vatican.
Unaposema Vatican unasema kanisa la Mungu. Vatican imekuwa nchi Feburuari 11, mwaka 1929 zama za Benito Mussolini.
Habari zinazovuja(hata BBC walitangaza mwaka jana) kwamba kuna njama za mapinduzi baridi na mchakato wa kumsimika Papa mpya badala ya Benedict XVI.
Rome ni mahali ambapo wameishi ma-Baba Watakatifu(Popes) wa Katoliki wapatao 302.
Mji huu ulikuwa makao makuu ya dola ya Rumi, hata zama za Yesu,mitume na zama za Biblia Takatifu yaani kati ya mwaka BC 1500 na 96 AD.
Profesa  Joseph Ratzinger,Mtaalamu wa theolojia(Profesa wa Theolojia katika Chuo Kikuu cha Munich,Ujerumani) alishiriki katika makongamano ya kutaka mageuzi katika kanisa Katoloki.
Kanisa Katoliki lilipinga Ukomunisti kwa nguvu zama za Vita vya Pili vya Dunia, ambavyo Joseph Ratzinger alishiriki kikamilifu.
Alianza kuaminiwa katika kanisa hili mwaka 1960; amekuwa Askofu Mkuu wa Munich,Kadinari na Mkuu wa Idara  wa Vatican,na Mrakibu wa Jumuiya ya Ulinzi wa Imani; akijua chochote kinachotakiwa kuangaliwa na Kanisa Katoloki.
Kashfa zinazilikumba kanisa: Ulawiti wa watoto wa kiume, yeye alikuwa ‘The Defense of Faith’.
Kuna misimamo ya mapadre kutaka kuoa.kanisa dada la Anglican limeruhusu ndoa za mashoga na wasagaji wakati kukiwa na mbinyo mkali katika kanisa hili. Yeye siku zote amekuwa akipinga,na juzi akaregeza msimamo katika matumizi ya kondomu.
Kuna wimbi la kanisa katika kufuata tamaduni za sikukuu za kipagani.Mfano:Krismasi ni Desemba 25 ambayo ni sikukuu ya kipagani ya SOLLNVICTUS MITHRAS-ni ibada ya jua.
Siku ya mungu jua asiyeshindwa,ilianza karne mbili kabla ya Kristo.Yesu hakuzaliwa tarehe 25 Desemba,isipokuwa ni siku ya kipagani ya kubambkwa.Kanisa linakiri wazi kwamba iliwekwa ili kuwafanya waumini waondoe upagani akilini mwao na kumfikiria mtoto Yesu,badala ya upagani wa mungu jua!
Profesa Ratzinger,naam Joseph Ratzinger,mtafiti wa Theolojia alianza kupingana na ukweli wa Biblia na kusisitiza kuwa Yesu alizaliwa Desemba 25; na akasisitiza siku hii ikumbukwe kama siku ya kuzaliwa Yesu,badala ya sikukuu ya mapagani.
Joseph Ratzinger ametawala Vatican kama Papa Benedict XVI wakati wa mpito ambao siri nyingi za Vatican zikivujishwa katika vyombo vya habari.
Ratzinger (85) alipochaguliwa kuwa Papa, alishadharauliwa,na ilidhaniwa kwamba mkusanyiko wa watu St.Peter’s Square ungepungua na mvuto wa upapa ungetindika.
Hakuheshimika kama mtangulizi wake,Papa Yohane Paulo II, NA Profesa Ratzinger amekuwa akiwachanganya Wakatoliki kwa mambo magumu, ‘difficult things’ wakati fulani Septemba huko Regensburg aliwachefua Waislam kuhusu imani na machafuko yanayoletwa na ugaidi.
Jumamosi usiku, Aprili Pili mwaka 2005,Profesa Ratzinger alichaguliwa kuwa Papa mara baada ya kifo cha Papa Yohanne Paulo II.
Yohanne Paulo II yeye alichaguliwa kuwa Papa Oktoba mwaka 1978,mara baada ya kifo cha Yohane Paulo I.
Alinusurika kuuawa, aliugua ugonjwa wa kutetemeka sana,mbona hakuwahi kujiuzulu?
Kwa miaka 455 kabla ya Papa Paulo II mapapa wote walikuwa Waitaliani,Papa Paulo II alikuwa kutoka Poland,Ulaya.Mwaka 1415 Papa Gregory alijiuzulu,bila shaka kwa sababu ya mbinyo mkali,na papa mwingine alipinduliwa na kufungwa jela alikofia gerezani, wakati wa maasi ya Wafaransa.
 Kuna mapapa takriban 302. Kulingana na Kanisa Katoloki,papa wa kwanza ni Petro(32-67 AD) HADI alipouliwa na Kaisari Nero. Kaisari Nero alichoma moto jiji la Rome akawasingizia Wakristo akina Petro,na ndipo alipofunguliwa kesi ya uhaini na kuhukumiwa kukatwa kichwa.
Mwaka 58 AD Paulo na Batholomayo waliuliwa kwa staili hiyo hiyo na kwa makosa ya kubambikwa,sasa utajiuliza upapa wa Petro ulianza lini?
 Nataka kusema kwamba, Papa Benedict XVI amekumbana na ‘vya kumkuta’kutokana na misimamo yake mikali,na sasa makadinari wasiopungua 118 watamchagua papa mwingine,kura zitakapopigwa na moshi mweupe kupaa angani,kabla ya mwezi Machi kwisha.
Makadinari wanaomchagua Papa huwa umri wao ni chini ya miaka 80;wengine wanasema ni fursa kwa Afrika sasa kupata upapa wanadhani ni uchaguzi wa Marekani,ambako Obama kawa Rais.
Hawajui kuna misimamo ya kanisa na mila na tamaduni anuwai. Na hawajui Papa ni kiongozi wan chi ya Vatican inayozungukwa na Italia.
Ulaya kuna makadinari takriban 50 watakaomchagua Papa,Afrika wapo 12 hivi.Asia wapo takriban 10 na amerika Kusini hususan Brazili wapo makadinari maarufu sana.
Kadinari wa Nigeria,Francio Arinze ndiye anayepigiwa debe kuwa Papa. Papa Gregory(1406-15) ndiye aliyejiuzulu kwa mashinikizo na wala siyo afya mbaya kama anavyosemwa Papa huyu wa siku hizi,Ratzinger.
Kuna ‘Presha’ hadi Vatican,kuna fujo na hata ufisadi na njama za mapinduzi na mauaji ya kinyama.

Rome, ni mahali Kanisa la Mt.Petro lilipojengwa juu ya Kanisa la Petro; linaitwa, St.Peter’s Basilica
 Limejengwa KATIKA ENEO LA EKARI SITA.
Hili kanisa, St. Peter’s Basilica, lina urefu wa futi 700 na upana ni futi 450 na linaweza kuchukua watu 80,000 kwa wakati mmoja.
Rome ni jiji lililopo nyuzi sawa na New York kwa nyuzi za Latitude; ni jiji lenye Coliseum, ambamo yalifugwa masimba yaliyorarua Wakristo maelfu.
Rome,uko futi 40 hadi 270 juu ya usawa wa Bahari
Jiji lenye kelele nyingi kuliko mji wowote duniani,lipo kando ya Bahari ya Mediterranean.
 Zama za Papa Pius XII alibebwa kwenye kiti cha enzi kiitwacho, Sedia Gastatoria ambacho ni kiti cha enzi cha dhahabu chenye rangi nyekundu.Papa huketi hapa mara anapochaguliwa na Moshi  Mweupe, hutoa BARAKA Duniani- Urbi et Orbi.
Rome umejengwa juu ya milima saba: CAPITALINE, PALATINE, AVENTINE, QUIRINAL, VIMINAL, ESQUILINE, na CAELIAN.
Vatican City(The Holy See) mwaka 2004 ulikuwa na watu 870;wengi Waitaliano na wapo Waswisi.
Wanaongea Kiitaliano, Kilatini, na wote ni Wakatoliki-Vatican ni nchi ya dini moja. Fedha wanayotumia ni Lira ya Vatican na ile ya Italia ambazo thamani yake ni sawa.
Lira tatu hivi thamani yake ni sawa na dola moja ya Marekani. Vatican inazungukwa na Italy-eneo lake ni ekari 108.7 na mtawala wake ni Papa.(Papal State).
Katika kitabu kiichwacho THE WORLD ALMANAC toleo la 2002,ukurasa wa 863 kuna maelezo kuhusu Vatican.
Kwamba,Feburuari 11 mwaka 1929 ulitiwa saini mkataba kati ya Kadinari Gasparri na Waziri Mkuu,Benito Mussolini; mkataba wa uhuru wa Vatican na ukatoliki kupewa “Special Status” ndani ya Italia.
Mkataba huu unaitwa, Lateran Agreement (Article 7). Feburuari 10 mwaka 1798 Papa alitiwa mbaroni na akafungwa jela.
Nataka kusema kwamba, ‘donda la mauti’ la Ufunuo 13 lilipona baada ya miaka 131 kamili.
Marekani, hawakuwahi kuitambua mamlaka haya ya VATICAN,SABABU zinafahamika, wakati wa vita kati ya Wakatoliki na wanamatengenezo(Christian Reformation) wa Ulaya walitimkia Marekani ili kukwepa vita vya miaka 1260 yaani kutoka 538 hadi 1798 AD.
Mtu anaweza kusoma vitabu vingi akajua haya, hasa kile kiitwacho, Africa Learns about Europe, The Great Controversy n.k
Marekani ilikuja kutambua mamlaka ya Vatican mwaka 1984,ilikuwa baada ya kuondoa uhusiano wa Kidiplomasia katika mwaka 1867.
Marekani walipata uhuru Julai mwaka 1776,kwa muda wote hawakuitambua Vatican hadi mwaka huo wa 1984.
 Vatican na Israeli walitiliana saini makubaliano ya uhusiano wa kibalozi Desemba 30 mwaka 1993. Msomaji mmoja aliniuliza uhusiano wa Israeli na Vatican, na anapaswa kujua kwamba Israeli maana yake ni dini ya Kiyahudi, ‘Judaism’ na Ukatoliki wa Vatican kuanza kuhusiana, maana yake ni kuondoa kizingiti kati ya Uzayoni na Ukatoliki.Sasa bado Waislam?


.

 Papa ni miongoni mwa viongozi wanaolindwa sana hapa duniani.
Analindwa na askari wa Kiswisi.-SWISS GUARD.
 Baba Mtakatifu ana maadui pia,lazima alindwe. Papa Pius VI alitiwa mbaroni na Jenerali Berthier wa Ufaransa,Feburuari 11 mwaka 1798.
 Papa John Paul II alipigwa risasi. Novemba 27 mwaka 1970 Papa Paulo VI alishambuliwa kwa kisu(hakuumia) katika Uwanja wa Ndege wa Manila, Ufilipino.
 Mwaka 1981 Papa Paulo II na watu wengine wawili waliokuwa jirani naye walipigwa risasi. Ilikuwa Mei 23, mwaka huo wa 1981 Mahmet Ali Agca, akafumua risasi akamjeruhi Papa. Huyu jamaa Mahmet Ali Agca, ni  Mturuki, ambaye alitekeleza tendo hilo la kigaidi wakati Papa akihutubia St. Peter’s Square ,Rome.
Huyu Papa alikufa mwaka 2005 kwa ugonjwa wa kutetemeka.
Mei 12 mwaka 1982  Papa John PauloII ALINYATIWA na muuaji mwenye kisu,walinzi wake wakamnyang’anya kisu huyo jamaa huko Fatima,Ureno.
Papa ni Askofu wa Rome; ni Mwakilishi wa Yesu-THE VICAR OF JESUS CHRIST-NI Mrithi wa Mtume Petro, ni Mkuu wa Mitume wote,ni Mkuu wa Kanisa lote la Kikristo Duniani. Papa ni Mamlaka.
Bila shaka, Profes Ratzinger, amesigana msimamo na maslahi ya Vatican na kuamua kubwaga manyanga,na wala siyo suala la afya mbaya.
Ni kama ‘ametemwa’ na system huko Vatican, Papa siyo kama Lowassa ama Rais Mstaafu Mwinyi waliojiuzulu.
Upapa (Papacy) bi taasisi kubwa hapa duniani,na papa anawasaidizi wajuzi na wengi kiasi kwamba kazi za upapa haziwezi kulala kama wengi wanavyodhani.
Upapa ni taasisi ya mambo mengi ambayo watu wengi hawajui,na papa hawezi kujiuzulu hivi tu.Papa Benedict,katemwa na system ya Vatican,amini usiamini.
www.congesmrambatoday,blogspot.com 














Thursday, February 7, 2013

musoma

Polisi wanapowasaka wauaji wa Musoma kwa bunduki,virungu na pingu,wanaharakati wafungue darasa la uwajibibikaji  na Haki za Binadamu
 
TOLEO nambari 852 la gazeti hili la Rai(Januari 21-27 mwaka huu), niliandika katika Mraba huu kwamba, iko haja ya wanaharakati wa Haki za Binadamu kwenda Musoma, kufundisha Haki za Binadamu.
   Niliandika kwamba, ukitembea Musoma na kusikiliza maoni ya baadhi ya watu, hutakosa kurejesha fikra zako katika zama za mauaji ya kuangamiza(genocide)huko Rwanda , mwaka 1994.
   Katika makala yenye kichwa, “Musoma vijijini uzee ni baraka au laana?” nilifananisha uwezo wa kufikiri wa baadhi ya wakazi wa huko na wauaji wa Jimbo la Darfur( Sudan ) ama huko Chad , Congo Mashariki, Somali n.k
    Nilisema hapa mrabani, kwamba maeneo niliyotaja yamesababisha vikao vingi mjini Geneva , Uswisi, kujadili namna ya kuwaokoa watu katika maangamizi.
  Geneva , ni makao makuu ya Mashirika ya kutetea wakimbizi nay ale yanayoshughulikia Haki za Binadamu. Geneva ni kitovu cha kamati ya kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu(ICRC).
     Msalaba Mwekundu kazi yao ni kulinda na kuokoa maisha ya watu. Kwamba, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoridhia Tangazo la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu, lililotolewa Desemba 10, mwaka 1948.
    Kwamba, mikataba ya Haki za Binadamu na ile ya Geneva (The Geneva Conventions), kama ule wa mwaka 1949; hukataza mauaji.
 Hata mateka wa vita wanalindwa na mikataba hii wasiuliwe kasha wapewe matibabu na huduma za kiafya hata wawapo na majeraha ya risasi, wanapokuwa mikononi mwa adui zao vitani.
  Kinyume cha harakati zza mashirika ya Haki za Binadamu na Msalaba Mwekundu, katika kulinda na kuokoa maisha ya watu, Musoma kuja ‘Janjaweed’ mithili ya wale wanamgambo wa Kiarabu wa huko Sudan , wanaofyeka watu kwa majambia makali sana . Musoma kuna kila dalili za watu kuanza kulipizana visasi.
   Sababu za watu kuwa na majambia au mapanga, ni visasi kufuatia tuhuma za kijinga-jinga, kama uchawi, ulozi, usihiri, wizi wa mifugo na hata chuki za kikabila. Ukitazama kwa maikini, utaona mfumo wa kutoa haki Musoma, mkoani Mara, unaugua kiharusi.
  Katika makala yangu katika mraba huu, Januari 21 mwaka huu, nilitaraji serikali ingechukua hatua haraka kupeleleza na kuyasaka makundi ya wauaji wenye mapanga(Jajaweed) ambao hukodishwa na watu kwenda kutekeleza mauaji ya kinyama; naam mauaji ya kisasi.
  Walemavu wa ngozi(albino) pia huuawa na hawa hawa Janjaweed, wanapotumwa na wenye fedha, kutaka kufanya matambiko yao anuwai.
 Mauaji ya kishenzi kama hayo ya Buhare, nje kidogo ya Manispaa ya Musoma, siku chache zilizopita, bila shaka yamefanywa na Janjaweed.
   Nataka nikwamnie msomaji. Zamani kidogo, walilipwa fedha wauaji wenye pindi na mishale ya sumu. Kwenda kuua mtu yeyote aliyetuhumiwa kuwa mchawi ama mwizi kwa minajiri ya kulipa kisasi, mradi kulikuwa na aliyetangaza ‘zabuni’ hiyo kwa ujira wa pesa.
 Musoma, kuna ‘Janjaweed’ wanaoendesha maisha yao kwa kuua. Musoma kuna vikundi vya siri vya wauaji wa kukodishwa.Wamefuzu medani za kuua na hata kuangamiza kizazi na koo(genocide) kwa mapanga makali na pinde zenye mishale ya sumu kali.
   Akina mama na kina baba vikongwe wanaotuhumiwa kwa uchawi, wameuliwa wengi bila serikali kuchukua hatua. Ulegevu wa serikali-polisi na mahakama- umewapa Janjaweed kupenya mkondo wa sheria.
 Nataka kusema kwamba, polisi mkoani Mara ni wazembe; tena wazembe kuliko. Nachelea kusema ni wala rushwa, wanaoharibu upelelezi wa kesi za namna hii, wanapokuwa wamepewa chochote kitu, ama kama wamelipwa ng’ombe, kondoo, kuku, bata kama siyo fedha taslim.
 Amini usiamini, vyombo vya kutoa haki(polisi na mahakama) mkoani Mara havitendi kazi yake sawa sawa. Kwa sababu, wezi na wahalifu wengine hata wa mauaji, hukamatwa leo, kasha wakaachwa huru kesho asubuhi.
 Kisingizio, ni kukosekana kwa ushahidi ama kushinda rufaa. Rufaa za Musoma husikilizwa wapi usiku wa manane, kama siyo upenuni mwa vilabu vya pombe za kienyeji, ama baa?
 Mahakama gani hukaa usiku, siku za siku kuu na mapumziko?
     Musoma, mhalifu akifungwa jela na mahakama ya Mwanzo Ijumaa jioni, keshoye Jumamosi ama keshokutwa  Jumapili, anarejea nyumbani, kwamba kashinda rufaa!
   Hayo ndiyo ya Musoma, sasa  wana ula wa chuya! Wahalifu wanapoachiwa huru hurejea vijijini kwenda kutishia raia wema waliowasema polisi au kutoa ushahidi mahakamani.
   Musoma, ukatoe ushahidi mahakamani, mhalifu afungwe  jela siku mbili, na kurejea nyumbani baada ya juma moja; hujipendi?! Utakatwa koromeo mchana kweupe.
Raia wema na waadilifu wamekatishwa tamaa na utendaji wa vyombo vya dola.
  Siku hizi watuhumiwa huuawa na wananchi wenye hasira kali. Hufuatwa hata makwao na kuuliwa kinyama, wao, wake na ndugu na jamaa zao, nyumba huchomwa moto hata mchana kweupe.
 Hakuna kuwapeleka watuhumiwa polisi au mahakamani, kwa madai kwamba watarejea kesho! Mahakama zinaugua kiharusi;polisi wana mafua!
    Kuna mahakama 15 tu za Mwanzo mkoani Mara. Mkoa mzima wa Mwanza una mahakama za Mwanzo 20.Mahakimu ni wachache, tunaambiwa kuna upungufu wa mahakimu wa mahakama za Mwanzo 500 nchi nzima!
 Hizi mahakama ambazo ndizo huwahudumia wananchi wengi wa vijijini, zina mahakimu wachache sana . Hawana vitendea kazi, kesi zimefurika.
   Hakimu mmoja husafiri kutoka mahakama moja kwenda nyingine; na huko kuna msongamano wa kesi nyingi tena za miaka mingi.
 Nataka kusema kwamba, ni nadra kupata haki vijijini kupitia mahakama za Mwanzo. Hata mahakama za wilaya ndizo huwaachia wezi na wahalifu kwa rufaa zilizosikilizwa baa au klabuni, siku zisizo za kazi.
  Mfumo wa utoaji haki mkoani Mara, una walakini.
Kama hauugui kifaduro, una kiharusi kikali.Hakimu mmoja husafiri kutoka mahakama moja kwenda nyingine, anaposhindwa, watendaji wa vijiji na kata ndiyo wanaowasomea mashitaka washitakiwa.
   Hawa, hawana hata ‘ABC’ ya sheria. Matokeo yake, dhamana huandamana na kitita cha noti. Bila fedha hakuna dhamana hata kama ni haki ya mshitakiwa kikatiba na kisheria.
   Vituo vya polisi vya vijijini mkoani Mara, vimegeuka kuwa mahakama, kwa sababu polisi hutoa hukumu;hutoza faini vituoni.
Wauza gongo na bangi, wezi wa bata, kuku,ng’ombe n.k huachiliwa vituo vya polisi mradi wawe na pesa za hongo na rushwa!
   Kama hujawahi kuona mtu akikaa mahabusu mwaka mzima, nenda katika mahabusu za Musoma vijijini, ufanye kosa dogo kasha usiwape rushwa polisi, watendaji wa kata na vijiji.
   Hiki ni kichocheo cha watu kuchukua sheria mkononi, ama kukodisha ‘Janjaweed’ ili wakawalipie visasi, kwa kuwa polisi na mahakama walishashindwa kuwafunga jela wauaji, wezi, majambazi, kwa kuwa wana pesa za rushwa.
  Huko Musoma, ile dhana ya Robert Darwin ya “Survival of The Fittest”(ya mwenye nguvu kuua wanyonge bila kufanywa kitu) hutenda kazi. Huna kitu Musoma huna haki polisi, ofisini kwa Mtendaji wa kijiji, wa kata hata mahakamani!
  Musoma vijijini, kama huna fedha za kujaza mafuta katika pikipiki ama gari la polisi, hakuna mtuhumiwa wako kukamatwa. Hata akikamatwa na kufikishwa kituoni, huna fedha za kumlisha chakula au kumlipia nauli kwenda rumande mjini Musoma, hawezi kupelekwa!
  Mkoani Mara, ndipo hakimu mmoja wa mahakama ya mwazo hukabiliwa na kesi nyingi, kwa sababu tarafa nzima huwa na mahakama moja ama mbili. Tarafa inakuwa na takriban watu 600,000.
Kuna kesi ngapi? Kesi nyingi hazitolewi maamuzi kwa wakati; na wanasheria wanamsemo kwamba, “Justice delayed is Justice denied”(haki iliyocheleweshwa ni haki iliyopotea).
 Kwa hiyo, Musoma hakuna haki? Kwa sababu haki hucheleweshwa, haki imepotea. Katika mazingira haya, wananchi wamekata tamaa, wanaamua kuwalipa ujira ‘Janjaweed’ ili wakawalipie kisasi dhidi ya wahalifu,watuhumiwa wao ama wabaya wao hata kama ni tuhuma za kijinga kama za kishirikina.
  Mfumo wa kutoa haki unaugua kiharusi mkoani Mara.Wizi wa mifugo unaendelea kwa sababu ukiwa na fedha utakamatwa leo, kesho utaachwa huru, au utafungwa leo na mahakama ya chini na kushinda rufaa usiku wa manane!
   Wapo watu, wanaposikia Musoma kuna mauaji ya kutisha, wanadhani kuna watu wakatili sana . Hapana! Haya ni mauaji ya visasi kwa sababu mfumo wa sheria umeshindwa.
  Si kila raia mwema huuliwa, ila ukituhumiwa.Mauaji ya kinyama huandamana na visasi kwa sababu mfumo wa sheria unaugua kiharusi kikali.
  Mauaji ya juzi huko Buhare, Musoma, ambako watu 17 wa ukoo mzima walifyekwa mapanga na kuchinjwa mithili ya njiwa, ni matokeo ya kulipizana visasi, kwa sababu vyombo vya dola(polisi, mahakama, mageteza na watendaji) walishashindwa kufanya kazi yao barabara.
 Nazungumzia uwajibikaji wa vyombo vya dola, na umuhimu wa viongozi wa vyama na serikali kuhimiza watu kuishi kwa kufuata sheria za nchi-uadilifu.
   Mauaji ya kulipa visasi; naam kulipa baya kwa baya(tit-for-tat) hudhihirisha kwamba mfumo wa kutoa haki Musoma unaugua kiharusi cha ubongo na kiwili wili.
 Mahali haki inapopatikana mahakamani, watu huridhika, amani hushamiri, maendeleo huja na kuna demokrasia. Tabia ya kuchukua sheria mkononi(Mob justice) iliyoenea Musoma, ni kielelezo kwamba raia hawataki tena kupeleka kesi zao mahakamani ama polisi, kwa sababu wanadhani hakuna haki.
 Siku hizi watuhumiwa huuawa hata mbele ya polisi.Polisi wanapoaachia huru watuhumiwa, waelewe wanasababisha mauaji ya visasi namna hii.
 Niliandika mrabani hapa Januari 21 mwaka huu kwamba, Musoma ndiko wanakofanya mikutano ya hadhara kutafuta namna ya kuwadhibiti wachawi kwa kuwakata mapanga!
 Ujinga umejaa vichwani mwa viongozi wa vijiji, vitongoji, kata n.k hadi sheria na haki za binadamu ni kitenda wili.
 Haki za binadamu ni lugha ya kawaida ya ubinadamu.Haki ingalipo Musoma lakini hutindika.
   Nataka kusema kwamba, Musoma hakuna ubinadamu, kwa sababu watu huongea lugha ya kuua kwa kulipa visasi-ni kuwaondolea watuhumiwa haki ya kuishi, hata kabla ya mahakama(chombo pekee cha kutoa haki nchini)kutoa hukumu.
 Narejea wito wangu kuwataka wanaharakati wa haki za binadamu kwenda Musoma mkoani Mara, kufundisha haki za binadamu, haki za raia, itifaki ya Geneva , uwajibikaji serikalini na vyombo vya dola, ili kukinusuru kizazi hicho na maangamizi!
  Narejea kauli yangu kusema kwamba, unahitajika mkakati mzito wa kuwanusuru watu hawa katika kitisho cha uvuli wa mauti ya kuchunjana kama ng’ombe kwa mapanga utadhani Bosnia , Darfur , Rwanda ya mwaka 1994, Somalia au Congo na Chad !!
   0715-324 074  
 
  
 
  

musoma

Polisi wanapowasaka wauaji wa Musoma kwa bunduki,virungu na pingu,wanaharakati wafungue darasa la uwajibibikaji  na Haki za Binadamu
 
TOLEO nambari 852 la gazeti hili la Rai(Januari 21-27 mwaka huu), niliandika katika Mraba huu kwamba, iko haja ya wanaharakati wa Haki za Binadamu kwenda Musoma, kufundisha Haki za Binadamu.
   Niliandika kwamba, ukitembea Musoma na kusikiliza maoni ya baadhi ya watu, hutakosa kurejesha fikra zako katika zama za mauaji ya kuangamiza(genocide)huko Rwanda , mwaka 1994.
   Katika makala yenye kichwa, “Musoma vijijini uzee ni baraka au laana?” nilifananisha uwezo wa kufikiri wa baadhi ya wakazi wa huko na wauaji wa Jimbo la Darfur( Sudan ) ama huko Chad , Congo Mashariki, Somali n.k
    Nilisema hapa mrabani, kwamba maeneo niliyotaja yamesababisha vikao vingi mjini Geneva , Uswisi, kujadili namna ya kuwaokoa watu katika maangamizi.
  Geneva , ni makao makuu ya Mashirika ya kutetea wakimbizi nay ale yanayoshughulikia Haki za Binadamu. Geneva ni kitovu cha kamati ya kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu(ICRC).
     Msalaba Mwekundu kazi yao ni kulinda na kuokoa maisha ya watu. Kwamba, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoridhia Tangazo la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu, lililotolewa Desemba 10, mwaka 1948.
    Kwamba, mikataba ya Haki za Binadamu na ile ya Geneva (The Geneva Conventions), kama ule wa mwaka 1949; hukataza mauaji.
 Hata mateka wa vita wanalindwa na mikataba hii wasiuliwe kasha wapewe matibabu na huduma za kiafya hata wawapo na majeraha ya risasi, wanapokuwa mikononi mwa adui zao vitani.
  Kinyume cha harakati zza mashirika ya Haki za Binadamu na Msalaba Mwekundu, katika kulinda na kuokoa maisha ya watu, Musoma kuja ‘Janjaweed’ mithili ya wale wanamgambo wa Kiarabu wa huko Sudan , wanaofyeka watu kwa majambia makali sana . Musoma kuna kila dalili za watu kuanza kulipizana visasi.
   Sababu za watu kuwa na majambia au mapanga, ni visasi kufuatia tuhuma za kijinga-jinga, kama uchawi, ulozi, usihiri, wizi wa mifugo na hata chuki za kikabila. Ukitazama kwa maikini, utaona mfumo wa kutoa haki Musoma, mkoani Mara, unaugua kiharusi.
  Katika makala yangu katika mraba huu, Januari 21 mwaka huu, nilitaraji serikali ingechukua hatua haraka kupeleleza na kuyasaka makundi ya wauaji wenye mapanga(Jajaweed) ambao hukodishwa na watu kwenda kutekeleza mauaji ya kinyama; naam mauaji ya kisasi.
  Walemavu wa ngozi(albino) pia huuawa na hawa hawa Janjaweed, wanapotumwa na wenye fedha, kutaka kufanya matambiko yao anuwai.
 Mauaji ya kishenzi kama hayo ya Buhare, nje kidogo ya Manispaa ya Musoma, siku chache zilizopita, bila shaka yamefanywa na Janjaweed.
   Nataka nikwamnie msomaji. Zamani kidogo, walilipwa fedha wauaji wenye pindi na mishale ya sumu. Kwenda kuua mtu yeyote aliyetuhumiwa kuwa mchawi ama mwizi kwa minajiri ya kulipa kisasi, mradi kulikuwa na aliyetangaza ‘zabuni’ hiyo kwa ujira wa pesa.
 Musoma, kuna ‘Janjaweed’ wanaoendesha maisha yao kwa kuua. Musoma kuna vikundi vya siri vya wauaji wa kukodishwa.Wamefuzu medani za kuua na hata kuangamiza kizazi na koo(genocide) kwa mapanga makali na pinde zenye mishale ya sumu kali.
   Akina mama na kina baba vikongwe wanaotuhumiwa kwa uchawi, wameuliwa wengi bila serikali kuchukua hatua. Ulegevu wa serikali-polisi na mahakama- umewapa Janjaweed kupenya mkondo wa sheria.
 Nataka kusema kwamba, polisi mkoani Mara ni wazembe; tena wazembe kuliko. Nachelea kusema ni wala rushwa, wanaoharibu upelelezi wa kesi za namna hii, wanapokuwa wamepewa chochote kitu, ama kama wamelipwa ng’ombe, kondoo, kuku, bata kama siyo fedha taslim.
 Amini usiamini, vyombo vya kutoa haki(polisi na mahakama) mkoani Mara havitendi kazi yake sawa sawa. Kwa sababu, wezi na wahalifu wengine hata wa mauaji, hukamatwa leo, kasha wakaachwa huru kesho asubuhi.
 Kisingizio, ni kukosekana kwa ushahidi ama kushinda rufaa. Rufaa za Musoma husikilizwa wapi usiku wa manane, kama siyo upenuni mwa vilabu vya pombe za kienyeji, ama baa?
 Mahakama gani hukaa usiku, siku za siku kuu na mapumziko?
     Musoma, mhalifu akifungwa jela na mahakama ya Mwanzo Ijumaa jioni, keshoye Jumamosi ama keshokutwa  Jumapili, anarejea nyumbani, kwamba kashinda rufaa!
   Hayo ndiyo ya Musoma, sasa  wana ula wa chuya! Wahalifu wanapoachiwa huru hurejea vijijini kwenda kutishia raia wema waliowasema polisi au kutoa ushahidi mahakamani.
   Musoma, ukatoe ushahidi mahakamani, mhalifu afungwe  jela siku mbili, na kurejea nyumbani baada ya juma moja; hujipendi?! Utakatwa koromeo mchana kweupe.
Raia wema na waadilifu wamekatishwa tamaa na utendaji wa vyombo vya dola.
  Siku hizi watuhumiwa huuawa na wananchi wenye hasira kali. Hufuatwa hata makwao na kuuliwa kinyama, wao, wake na ndugu na jamaa zao, nyumba huchomwa moto hata mchana kweupe.
 Hakuna kuwapeleka watuhumiwa polisi au mahakamani, kwa madai kwamba watarejea kesho! Mahakama zinaugua kiharusi;polisi wana mafua!
    Kuna mahakama 15 tu za Mwanzo mkoani Mara. Mkoa mzima wa Mwanza una mahakama za Mwanzo 20.Mahakimu ni wachache, tunaambiwa kuna upungufu wa mahakimu wa mahakama za Mwanzo 500 nchi nzima!
 Hizi mahakama ambazo ndizo huwahudumia wananchi wengi wa vijijini, zina mahakimu wachache sana . Hawana vitendea kazi, kesi zimefurika.
   Hakimu mmoja husafiri kutoka mahakama moja kwenda nyingine; na huko kuna msongamano wa kesi nyingi tena za miaka mingi.
 Nataka kusema kwamba, ni nadra kupata haki vijijini kupitia mahakama za Mwanzo. Hata mahakama za wilaya ndizo huwaachia wezi na wahalifu kwa rufaa zilizosikilizwa baa au klabuni, siku zisizo za kazi.
  Mfumo wa utoaji haki mkoani Mara, una walakini.
Kama hauugui kifaduro, una kiharusi kikali.Hakimu mmoja husafiri kutoka mahakama moja kwenda nyingine, anaposhindwa, watendaji wa vijiji na kata ndiyo wanaowasomea mashitaka washitakiwa.
   Hawa, hawana hata ‘ABC’ ya sheria. Matokeo yake, dhamana huandamana na kitita cha noti. Bila fedha hakuna dhamana hata kama ni haki ya mshitakiwa kikatiba na kisheria.
   Vituo vya polisi vya vijijini mkoani Mara, vimegeuka kuwa mahakama, kwa sababu polisi hutoa hukumu;hutoza faini vituoni.
Wauza gongo na bangi, wezi wa bata, kuku,ng’ombe n.k huachiliwa vituo vya polisi mradi wawe na pesa za hongo na rushwa!
   Kama hujawahi kuona mtu akikaa mahabusu mwaka mzima, nenda katika mahabusu za Musoma vijijini, ufanye kosa dogo kasha usiwape rushwa polisi, watendaji wa kata na vijiji.
   Hiki ni kichocheo cha watu kuchukua sheria mkononi, ama kukodisha ‘Janjaweed’ ili wakawalipie visasi, kwa kuwa polisi na mahakama walishashindwa kuwafunga jela wauaji, wezi, majambazi, kwa kuwa wana pesa za rushwa.
  Huko Musoma, ile dhana ya Robert Darwin ya “Survival of The Fittest”(ya mwenye nguvu kuua wanyonge bila kufanywa kitu) hutenda kazi. Huna kitu Musoma huna haki polisi, ofisini kwa Mtendaji wa kijiji, wa kata hata mahakamani!
  Musoma vijijini, kama huna fedha za kujaza mafuta katika pikipiki ama gari la polisi, hakuna mtuhumiwa wako kukamatwa. Hata akikamatwa na kufikishwa kituoni, huna fedha za kumlisha chakula au kumlipia nauli kwenda rumande mjini Musoma, hawezi kupelekwa!
  Mkoani Mara, ndipo hakimu mmoja wa mahakama ya mwazo hukabiliwa na kesi nyingi, kwa sababu tarafa nzima huwa na mahakama moja ama mbili. Tarafa inakuwa na takriban watu 600,000.
Kuna kesi ngapi? Kesi nyingi hazitolewi maamuzi kwa wakati; na wanasheria wanamsemo kwamba, “Justice delayed is Justice denied”(haki iliyocheleweshwa ni haki iliyopotea).
 Kwa hiyo, Musoma hakuna haki? Kwa sababu haki hucheleweshwa, haki imepotea. Katika mazingira haya, wananchi wamekata tamaa, wanaamua kuwalipa ujira ‘Janjaweed’ ili wakawalipie kisasi dhidi ya wahalifu,watuhumiwa wao ama wabaya wao hata kama ni tuhuma za kijinga kama za kishirikina.
  Mfumo wa kutoa haki unaugua kiharusi mkoani Mara.Wizi wa mifugo unaendelea kwa sababu ukiwa na fedha utakamatwa leo, kesho utaachwa huru, au utafungwa leo na mahakama ya chini na kushinda rufaa usiku wa manane!
   Wapo watu, wanaposikia Musoma kuna mauaji ya kutisha, wanadhani kuna watu wakatili sana . Hapana! Haya ni mauaji ya visasi kwa sababu mfumo wa sheria umeshindwa.
  Si kila raia mwema huuliwa, ila ukituhumiwa.Mauaji ya kinyama huandamana na visasi kwa sababu mfumo wa sheria unaugua kiharusi kikali.
  Mauaji ya juzi huko Buhare, Musoma, ambako watu 17 wa ukoo mzima walifyekwa mapanga na kuchinjwa mithili ya njiwa, ni matokeo ya kulipizana visasi, kwa sababu vyombo vya dola(polisi, mahakama, mageteza na watendaji) walishashindwa kufanya kazi yao barabara.
 Nazungumzia uwajibikaji wa vyombo vya dola, na umuhimu wa viongozi wa vyama na serikali kuhimiza watu kuishi kwa kufuata sheria za nchi-uadilifu.
   Mauaji ya kulipa visasi; naam kulipa baya kwa baya(tit-for-tat) hudhihirisha kwamba mfumo wa kutoa haki Musoma unaugua kiharusi cha ubongo na kiwili wili.
 Mahali haki inapopatikana mahakamani, watu huridhika, amani hushamiri, maendeleo huja na kuna demokrasia. Tabia ya kuchukua sheria mkononi(Mob justice) iliyoenea Musoma, ni kielelezo kwamba raia hawataki tena kupeleka kesi zao mahakamani ama polisi, kwa sababu wanadhani hakuna haki.
 Siku hizi watuhumiwa huuawa hata mbele ya polisi.Polisi wanapoaachia huru watuhumiwa, waelewe wanasababisha mauaji ya visasi namna hii.
 Niliandika mrabani hapa Januari 21 mwaka huu kwamba, Musoma ndiko wanakofanya mikutano ya hadhara kutafuta namna ya kuwadhibiti wachawi kwa kuwakata mapanga!
 Ujinga umejaa vichwani mwa viongozi wa vijiji, vitongoji, kata n.k hadi sheria na haki za binadamu ni kitenda wili.
 Haki za binadamu ni lugha ya kawaida ya ubinadamu.Haki ingalipo Musoma lakini hutindika.
   Nataka kusema kwamba, Musoma hakuna ubinadamu, kwa sababu watu huongea lugha ya kuua kwa kulipa visasi-ni kuwaondolea watuhumiwa haki ya kuishi, hata kabla ya mahakama(chombo pekee cha kutoa haki nchini)kutoa hukumu.
 Narejea wito wangu kuwataka wanaharakati wa haki za binadamu kwenda Musoma mkoani Mara, kufundisha haki za binadamu, haki za raia, itifaki ya Geneva , uwajibikaji serikalini na vyombo vya dola, ili kukinusuru kizazi hicho na maangamizi!
  Narejea kauli yangu kusema kwamba, unahitajika mkakati mzito wa kuwanusuru watu hawa katika kitisho cha uvuli wa mauti ya kuchunjana kama ng’ombe kwa mapanga utadhani Bosnia , Darfur , Rwanda ya mwaka 1994, Somalia au Congo na Chad !!
   0715-324 074  
 
  
 
  

AFRIKA KIZIMBANI (14)
 
 
 CHARLES GHANKAY Taylor (62), Rais wa zamani wa Liberia aliyekuwa akikabiliwa na mashitaka  11 ya uhalifu wa kivita huko Sierra Leone,  na baadaye kufungwa miaka 50 jela,anatufundisha somo mahsusi.
 Kwamba,katika mahakama ya uhalifu wa kivita(ICC) mjini Hague, Uholanzi, Taylor amesemwa na mashahidi wa upande wa mashitaka kwamba alipokuwa Afrika Kusini wakati fulani, akatumia almasi alizokwiba  bega kwa bega na waasi wa RUF  huko Sierra Leone, kumhonga kidosho,mwanamitindo wa Kiingereza, Naomi Campbell.
 Unaona utajiri wa Afrika unavyotumika?
 Naam, Filamu iitwayo, ‘Blood diamond’ ya Jennifer Connelly, inatueleza kwamba, Charles Taylor, Marehemu Fodday ‘Poppay’ Sankoh na waasi wa Revolutionary United Front(RUF) waliiba almasi,wakabadilishana kwa silaha na Wazungu wa Ulaya na Afrika ya Kusini.
  Kumbuka msomaji, kulikuwa na mikataba ya Umoja wa Mataifa(UN) ya kutofanya biashara ya almasi za damu kutoka Sierra Leone.
 Hata hivyo, almasi hizi zilinunuliwa kwa magendo na kuingizwa Afrika ya Kusini, Zimbambwe kisha Ulaya na Mrekani.
 Kitendo hicho kilichochea sana vita hivi, wakati nia ya Mzungu ilikuwa kunufaika na utajiri wa Mafrika,potelea mbali Mwafrika huyu afe; aaangamie kwa risasi-The Shame of Poverty in Plentiful.
 Je, hujawahi kusikia kwamba hata Congo(DRC) vikosi vya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa(UN),wakati mwingine husahau jukumu la kulinda amani,na badala yake huanza kuiba madini,huku wakiacha kuwaokoa watu wanaouawa na wanawake kubakwa?
 Tangu kifo cha Laurent Desire Kabila katika Ikulu ya mjini Kinshasa, Januari 16,mwaka 2001,ukichungulia ndani ya uasi na uporaji wa rasilimali za ‘Bakongo’ kuna Mzungu.
 Hata ufisadi mithili ya ule wa kampuni ya Kiingereza, British Aerospace(BAE Systems) kutuuzia rada kanyaboya hapa,kwa Dola za Marekani milioni 40, kuna Mzungu anayeshiriki kutuumiza sisi tunapokosa shule, hospitali,maji, barabara na kwa ujumla maisha bora.
  Fedha za wizi: Hufichwa Jersey, Uingereza, Uswisi na katika mabenki ya Ulaya na Marekani, na hawasemi wizi huu.
 Joseph Mobutu aliiba dola za Marelani milioni sita akazificha Ulaya, hawakusema mpaka akatimkia uhamishoni, Morocco, kisha amefariki, wakazirejesha kwa familia yake.
 Mifano iko tele ya wizi. Uingereza iliwahi kutiliana saini mkataba na Misri mwaka 1929 eti sisi tusitumia maji ya Ziwa Nyanza linaoliwa Victoria kwa heshima ya Malkia wa Uingereza.
  Mkataba huu wa 1929 uliorejewa mwaka 1957 lengo lake lilikuwa kutuzuia kutumia maji ya Ziwa hili kwa miradi ya  kilimo cha umwagiliaji ili kujiokoa na kitisho cha njaa , kinachotukabili kila mwaka.
  Sasa tafakari: Kuna Ongezeko la Joto Duniani linalochangia mabadiliko ya  Tabianchi(Global Warming&Climate Change)ambalo chimbuko lake hasa ni Marekani,Ulaya,Uchina, Japan, Mashariki ya Kati n.k-nchi za viwanda.
  Wanamwaga sumu nyingi angani, sisi Afrika tunachangia ongezeko la joto kwa asilimia tatu tu,lakinimadhara makubwa, majanga ya asili tunapata sisi kuliko wao.
 Mifugo imekufa kwa ukame, mazao yamenyauka shambani, kwa kukosa mvua-hata zikinyesha ni mafuriko yanayozoa mazao,kubomoa nyumba na udongo kuporomoka kama huko Same.
  Umasikini wetu unachangiwa na harakati za Mzungu kutafuta utajiri.
 Sasa angalia, Uingereza kutiliana saini na Misri mkataba kwamba tusitumie maji ya Ziwa hilo kumwagilia mashamba yetu mwaka 1929 na 1957.
  Mwaka 1929 na 57 Tanzania,Kenya na Uganda tulikuwa bado kupata uhuru. Uingereza; hili ziwa Nyanza lilikuwa lao lini mpaka wawagawie Misri?
Mzungu anaona mali ya Mwafrika ni ya kugawa kama nyama mezani!
  Wakati mikataba hiyo inatupiga marufuku kumwagilia mashamba maji ya Ziwa Nyanza, ama kuyatumia maji hayo kama chanzo cha umeme(hydroelectric schemes), kama huko Owen Falls,Jinja,Uganda na miradi kama huo wa kupeleka maji Kahama, Shinyanga, hawa Misri wanamwagilia mashamba makubwa ya kama ekari 600,000 jangwani.
  Uhalali huo Uingereza iliutoa wapi?
   Kutoka mwaka 1929 hadi sasa-takriban karne nzima, Uingereza na Misri wametulipa Pauni bilioni ngapi kama gawio katika biashara hii, ili sisi tuache kumwagilia mashamba,tusivue samaki n.k tuwaachie wao maji yote?
 Kwanza,kuliita ziwa hili eti Victoria, ni kesi; ni wizi wa mchana,ni utapeli. Hizi ziwa linaitwa Nyanza, Inyanja, Nyanja, Lweru n.k kulingana na makabila yanayolizunguka.
 Huyo Victoria amekujaje hapa?
 Ziwa Nyanza lilianza lini kuwa mjukuu wa Malkia Victoria, hata alibandike jina la ukoo? Anayo hakimiliki? Waache ujanja.
  Mto Nile(mungu wa Wamisri, “Ra”) unaanzia mto Kagera,hukatisha ziwani humo na kutokea Owen Falls, ambako huanza safari ya kilomita takriban 7,000 hadi huko Bahari ya Mediterranean.
 Nchi za Bonde la Nile ni Uganda, Tanzania, Kenya, Congo,Rwanda,Burundi, Ethiopia,Eritrea na Sudan ,lakini nchi iliyowahi kusema maji ni mali yake!
  Sasa, Uingereza ilikuwa Mungu kumuuzia maji ya Ziwa letu “Faraoh” wa Misri mwaka 1929 na 1957?
  Bila maji haya,hakuna Misri-River Nile is the matter of life and death.
Maji ni yetu,mali yao (basi uwe) ni mto bila maji yatokayo nyumbani kwetu!
Hapo mpo? Bila sisi,hakuna Nile, hakuna Hosni Mubarak waka Wamisri; wajirekebishe!! Ebo! wanatukatazaje kumwagilia mpunga huko Shinyanga na Kahama ili kujinusuru na njaa, na kula mafuvu ya mbwa, wakati wao wanategemea mashamba yaliyomwagiliwa na maji ya mvua inayonyesha huku kwetu Aprili na  Mei na kufika kwao Julai na Agosti?
 Misri ji jangwa,hakina mvua. Sisi tunaambiwa tukome kumwagilia viazi huko Majita, Nassa na Bukoba eti maji yatiririke kwa usalama hadi Bwawa la Aswan, Bonde la Toska n.k
  Eti watu milioni 100 tunaozunguka Ziwa hili kubwa Afrika,tufe njaa,wao watu takriban 75 walime,wavune wapate kuishi.Wao watu,sisi tumbili?
 Misri, imekuwepo tangu mwaka 3,2000 BC ina kila kitu,ina mafuta,madini,samaki, mbona haijatugawia sehemu ya maji ya Suez Canal, tuvue samaki?
 Waache uchokozi kwa mikataba feki ya mwaka 1929 na 57 sisi hatukuwahi kuitwa kusaini mikataba hii ya kitapeli.
  Afrika inajua njama za Mzungu kutaka kupora rasilimali zetu. Ndiyo maana, siku za karibuni, tulimsikia aliyekuwa Mwenyekiti wa AU, Kanali Muammar AL- Qaddafi wa Libya, kabla ya mauti kumkumba, akitaka Waafrika tuungane na kuwa taifa moja, UNITED STATES OF AFRICA.
 Tatizo, naye Gaddafi kaona umuhimu wa Waarabu wa Kaskazini na Weusi wa Kusini mwa Jangwa la Sahara(Pan Afrcanism) baada ya kuwindwa na Wamarekani kwa madege ya kivita huko Benghazi na Tripoli Aprili 14 mwaka 1986.
 Shushushu wa Libya, Abdel Basseti Ali al- Meghri,akahukumiwa kifo Januari 31 mwaka 2001 kwa ugaidi.
 Gaddafi, alikuwa na ugomvi na Wazungu,Wamarekani, kwa sababu wanasema Desemba 21 mwaka 1988 ndege ya Marekani Pan American Airways(Pan Am) aina ya Boeing 747 ililipuliwa na kombora na magaidi wa Gaddafi huko katika anga ya Lockerbie, Scotland.
Huu ulikuwa uongo mkubwa,na waliokamatwa na kuhukumiwa kifo waliachwa huru,ikasemwa walionewa!
  Watu 270 walikufa,wakafa pia 11 waliokuwa ardhini-Gaddafi kakubali yaishe,akalipa fidia.
  Gaddafi  akataka kuwapendeza  na kuacha kuisema Marekani ama Ulaya vibaya. Waburgaria waliwachoma watoto mjini Cairo kwa sindano zenye UKIMWI,wakaachiwa,wakarejea mjini Sofia,Burgaria kama mashujaa. Nani wa kukemea wazungu?
 Mandela? Gaddafi?
Labda, ‘R.G’ Mugabe .Hata Dodoma tuna Uranium,lakini nani wa kuanzisha mradi wa nyuklia ili tupate umeme?
  Najadili sababu za Afrika kuwa bara tajiri lakini watu wake masikini-The shame of plenty in the midst of poverty!
  Waafrika bilioni moja katika ya  wakazi bilioni 6.9 wa dunia ndifo fukara zaidi wakati kuna kila kitu?
 Uchaguzi huru na haki kama huu wa kwetu ndiyo unailetea Afrika matatizo makubwa.
 Transparency International(TI) linasema Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ndiko kitovu cha ufisadi,wizi ndiko kuna nchi masikini zaidi, Highly or Heavily Indebted Poor Countries(HIPC) na sote tunafanya chaguzi za kidemokrasia!
 Huku twafa njaa,lakini akina Charles Taylor wanahonga almasi zetu kwa vimwana wa Uingereza, akina Naomi Campbell!!! Baadaye wanatiwa mbaroni na kufungwa ili kuwaziba midomo.
   0786 324 074
  
 
 
 
 
  
 
 
  
  
 
 

HAKI IKO KWA MUNGU TU



  
BIBLIA, na Wanaharakati wa Haki za Binadamu,hukubaliana kimsingi kwamba, “Haki za Binadamu zilianza wakati Binadamu alipoanza kuishi Duniani”.
Huu ni ukweli kamilifu; pale Mwanzo 2:16 na 17 Mungu anapomwambia Adamu kwamba alipewa ‘Uhuru’ wa kuchagua kumtii Mungu au kukataa(Freedom of Choice) alimpa HAKI ZA BINADAMU-Uhuru.
Hata hivyo, uhuru unawajibu,ukikosea umekwisha,ili haki za binadamu zidumu kuwepo ni sharti kuchagua vizuri kuitii sharia ya unyoofu ,The Moral law.
Dhana kwamba kila mtu anazo haki za binadamu ambazo tunasema ni haki za kimsingi,kwa kuwa kila mtu alizaliwa huru, ni ukweli halisi.
Haki za binadamu haziondolewi;hazipokonywi na  mtu na hakuna wa kuzipora-lakini zimeporwa sana hata na wanaojidai kuzihimiza siku hizi.Mtu anajidai kutangaza Haki za Binadamu,huku ni mwizi,fisadi,mbakaji!
Marekani na washirika wake wa Ulaya wanapojidai kuzitetea sana haki hizi za binadamu,wamezipora sana kwa kuua maelfu ya watu duniani pale wanapopigana vita vingi ili kutafuta maslahi yao.
Angalia vita vya Vietnam miaka ya 68-70;vita vya Irak,Afghanistan,Libya na mahali pengi hapa duniani ambako Shirika lao la Ujasusi, Central Intelligence Agency, wamechochea mno machafuko.
Mikataba na matangazo mengi ya Haki za Binadamu, imewapa watu kwa mkono wa kulia na kuziondoa kwa mkono wa pili wa kushoto.
Magna Carter ya Uingereza(1215),Bill of Rights ya Uingereza(1689),Tamko la Uhuru wa Marekani(1776),Tamko la Ufaransa la Haki za Mtu na Raia(French Declaration of Rights of man and Citizen) la 1789 n.k
Haya mengi,na linguine la Umoja wa Mataifa la Desemba 10,mwaka 1948,hakuna kinachosemwa kwa ukamilifu juu ya Haki zote za Binadamu na ukamilifu wake-ni udanganyifu mkubwa.
Maandamano yangalipo ya kudai haki Uingereza na Marekani,unyanyapaa na ubaguzi wa rangi ndiyo kwanza huendeshwa kila kona ya dunia,Waitalia walimnyanyapaa Zenedine Zidane,na hata sasa wanaongea ubaguzi wa rangi waziwazi.
Eti,misingi ya Haki za binadamu ni USAWA bila ubaguzi! Ubaguzi upo unalelewa Buckingham Palace, No 10 Downing Street na Oval Office, New York!
Vita vya kwanza vya Dunia(1914-18) na vya Pili(1939-45) vililetwa na mataifa makubwa.Waliua watu wengi sana kwa mamilioni,wengine walikosa makazi,wakawa wakimbizi,ili maslahi ya watu hawa yapatikane.
Hiroshima na Nagasaki.
Vita vya Kwanza vya Dunia, vilianza mwaka 1914 na vikaisha 1918.
Sababu hasa za vita hivi ni Mtawala wa Ujerumani, WILHELM  II,alitaka kuleta changamoto kwa maendeleo ya viwanda vya Uingereza,siyo vya Afrika,sawa?
 Katika Vita hivi vya Kwanza vya Dunia, walikufa jumla ya wanajeshi 8,418,000.
Askari wa Marekani waliouliwa vitani ni 126,000 na kiasi cha raia waliokufa katika vita hivyo ni 1,300,000.
Katika Vita vya Pili vya Dunia(1939-1945), walikufa askari 16,933,000; askari wa Kimarekani waliokufa ni 292,000 wakati raia waliouliwa ni 34,305,000.
 Vita hivi vilikoma wakati Marekani ilipolipua mabomu ya Atomiki katika miji ya Hiroshima na Nagasaki, Agosti 6 na 9 mwaka 1945.
Agosti 14, Japan ilitia saini ya kuacha vita na Septemba 2, mwaka huo wa 1945 vita hivi vilikwisha rasmi,vikiacha makovu ambayo hata sasa yangalipo. Hizi ni Haki za Binadamu sampuli gani wewe?
Huku ndiko tuendako,tunarejea katika vita, wakati mikataba ya amani inapovunjika,wakati uharibifu mkubwa wa mazingira unaposababisha karibu sana Mapigo saba ya Mwisho.
Kuharibika kwa utando wa Ozone angani,uharibifu wa vyanzo vya maji na ukataji miti ni janga lingine la hatari.
Tumchambue kidogo Adolf Hitler na chama chake cha NAZI dhidi ya Mayahudi wakati wa vita ya Pili ya Dunia, waliuawa Mayahudi wengi hata Umoja wa Mataifa ukaanzisha, “The Universal Declaration of Human Rights” mwaka 1948.
Mayahudi milioni sita waliuliwa kinyama.Tazama Filamu iitwayo, ESCAPING FROM SOBIBOR-Sobibor ni Poland,ambako Wayahudi waliuliwa na kuteswa kinyama ili kuangamizwa kabisa duniani.
Wauaji, eti walifikishwa mahakama ya Norenberg,iliyoanzishwa ajili ya kuwashitaki wahalifu wa vita,na uhalifu wa binadamu(crimes against humanity and war crimes).
Walipatikana na hatia ya kifungo jela.Kuna mahakama za aina hii nyingi kunapotokea mauaji ya kimbari kama Rwanda,ambako kuna mahakama ya Arusha,UNICTR.
Ipo ya Sierra Leone na ile ya Hague Uholanzi. Je haki hutendeka? Mbona wapo akina Felician Kibuga wamejificha Kenya,hawajawahi kukamatwa ili washitakiwe? Mahakamani kuna haki? Hakuna makengeza,  ‘double standards’?
Hata hivyo, Universal Declaration of Human Rights(UDHR), International Bill of Rights, International Covenant on Economic, Social and Cultural RightsI9CESCR),International Covenant on Civil and Political Rights(ICCPR) na mengine mengi husema kuwe na uhuru na haki,lakini hakuna haki hapa duniani.
Hakuna hata haki ya kuishi kwa masikini na makabwela kwa mfumo huu wa ubepari.
Nani anatengeneza bunduki na madege ya kijeshi? Nani hutengeneza misaili? Mizinga haiuzwi kwa waasi kama M23 huko Kongo? Kwa nini?
Marekani na Ulaya hawatengenezi silaha za maangamamizi hata leo baada ya vita baridi(Cold War) kumalizika?
Usidanganyike!Abu Ghraib,Guantanamo Bay na jela za wakubwa hawa huko Ulaya,huwakamata washukukiwa na kuwatesa,kuwafunga bila kuwafikisha mahakamani wakajitetee, haki gani sasa za binadamu?
Hakuna ‘Fair Trial’ ukikamatwa labda wa tuhuma za ugaidi. Hakuna haki hata katika mahakama za Tanzania,Ulaya na Marekani,tajiri hutazamwa zaidi na wakubwa hutetewa zaidi.
Mahakama ya Hague,Uholanzi ina makengengeza, haijawakamata Bush na Blair kwa kupeleka vita Irak kinyume na MATAKWA ya Umoja wa Mataifa.Wamekamatwa akina Charles Taylor tu, akina Uhuru Kenyatta watatiwa hatiani,lakini siyo wakubwa wa dunia.
Duniani mwenye haki ni mwenye nguvu,mamlaka,mali. Eti ‘retroactive punishment’ imezuiliwa kwa wote? Mbona Gaddafi na Osama waliuliwa kwa risasi bila kufikishwa mahakamani wakajitetee?
Sheria humtambua kila mtu hapa duniani? Huu ndiyo umbumbumbu wetu kushabikia Marekani na Ulaya kwamba kuna Haki za Binadamu!
Nimeeleza kasha cha Conjesta Ulikaye,Wazungu wa Uingereza waliombaka na kumuua na DPP(sasa Jaji)Geofrey Shaidi.Hata uhuru wa dini(Freedom of thoughts, Conscience and Religion)hakuna,subiri National Sunday Law,itatangazwa na Marekani,sasa watu wana uhuru gani wa kuabudu kama kuna New World Order?
Tumuulize Rais wetu Jakaya Kikwete,kama duniani(siyo Tanzania tu)kuna haki za watu wanyonge kabisa, ‘minority rights’? Hii mikataba sijui ya haki za raia na siasa ilishavunjwa na mataifa beberu na makampuni yao yanatumikisha watu kitumwa huko Myanmar!
Saro-Wiwa ameuliwa kwa nguvu za Royal/Dutch Shell,Chevron,Total na mengine huko Nigeria.Mrahaba wa haki za madini,nishati na mali asili zetu huporwa kwa kiburi cha mabwenyenye wa Marekani,viongozi wetu hupewa “Option” ama kuchukua r ushwa,au wakijidai wapotezwe!
Lumumba yuko wapi? Murtala Mohammed yuko wapi? Kabila?
Mnajidai kuandamana nini,waandamanaji huko Niger Delta waliuliwa na nani kama siyo makampuni ya Marekani na Uingereza? Uchochezi tu.
Eti haki za kuandamana! Mtavurugana kama Libya,kama Misri,kama Tunisia n.kWakubwa huongoza kuhalifu usawa na amani duniani,hakuna usawa wala usawia(universality) haki za watu wa mataifa madogo zilishaondolewa(alienable rights),sababu sisi waafrika,masikini?
Tukitaka haki ziwepo duniani,tukatae theories za akina Charles Robert Darwin(1809-1882) kwamba binadamu mwanzo alikuwa nyani,na kwamba dunia imetokea kwa bahati, ‘Big Bang’ ama evolution,uibukaji.
Kwenye uibukaji na maisha ya bahati hakuna usawa na haki,bali mwenye nguvu ndiye atastawi katika vita vya kugombea maisha-struggle for existence!
Katika dhana kwamba dunia imeibuka,na vilivyomo vimetokea kwa maguvu yake(survival of the fittest) hakuna haki na usawa wa binadamu, kuna sangara kuwala dagaa na furu,kuna simba kuwatafuna palahala na nyumbu.magugu kuyasonga mazao tunayolima ili tupate chakula n.k Haki itoke wapi sasa mahali ambapo hakuna sharia ya ulinganifu(universality) ama sharia ya unyoofu, moral conduct?
The Fundamental Code of Ethics ni Amri 10 za Mungu ambazo kila mtu hazitaki.Sasa unyoofu, “Morality’ hutoka wapi ili watu wasiwe wezi na mafisadi,bila Mungu?
Mkubwa atamjalije mdogo mahali ambapo watu hawataki amari ya kuwaheshimu watu,kuwajali na kuwapenda adui?Soma Mathayo 5:43-48. Matokeo yake, ‘Darwinism’ ni dhana ya mwenye nguvu ndiye atakayenusurika katika maisha haya ya kunyang’anyana chakula,maji na rasilimali.
Kwa kuwa hakuna kanuni za kupendana, basi watakaobaki duniani ni wenye nguvu(survival of the fittest) sisi tutakuwa mbolea ya kuneemesha mataifa makubwa,na wakubwa wenye uchumi mzuri-aliye na kidogo atanyang’anywa.
Kila mtu siku hizi hutamani awe na nguvu za utajiri,mamlaka na vyeo,wanaopiga kelele hawana jipya,wamepigwa kipepsi tu,lakini hata wao wakipata nafasi ni mafisadi wakubwa!
Kwa sababu hiyo,pasipo na Mungu akilini mwetu,hapana Haki za Binadamu,usawa,haki katika sharia na mgawo wa rasilimali n.k
Duniani hakuna sharia za unyoofu(morality) sasa haki itakujaje pasipo na sharia za unyoofu?Jambazi atakuwaje na upendo na huruma kazini kwake? Mwizi atakuwaje na huruma? Ingekuwa hivi basi wezi wangeshakoma kuiba.
Hakuna huruma,hakuna upendo kwa sababu pasipo Mungu na pasipo kutii sharia yake ya unyoofu na upendo,hakuna haki,kuna unyang’au.
Haki za Mashoga, Lesbian, Gay, Bisexual and Transgender(LGBT) ndizo haki hizi!Siku zote hakuna haki ila mwenye nguvu ndiye mshindi katika vita vya kupora rasilimali survival of the fittest, vita vya kugombea maisha, struggle foe existence,na vita vya kugombea mamlaka, struggle for supremacy.
Angalia wanasiasa wanavyowapambanisha ili wapate mamlaka! Kuna covenants sijui declarations za haki za binadamu,lakini hakuna haki!
Hakuna standard of rightness, kuna unyama watu wanakwenda upogo sababu hawaikubali sharia ya haki na unyoofu,moral principals, kuna uchoyo tu watu wote ni wanyama.
Sasa mnyama yupi atampa binadamu haki zake?Haki zimeporwa vitani, haki za wanyama kama zile za SHAMBA LA WANYAMA(animal farm) la George Orwell, zilishapokonywa na nguruwe wenye mamlaka!