Monday, July 22, 2013

MISRI NA DEMOKRASIA YA AFRIKA

KUNA masuala machache tunayofanana na Misri.
Msri na mataifa ya Waafrika Weusi,tunasafiri katika barabara moja kurejea katika utumwa wa kidini,kiuchumi,kitamaduni na kisiasa.
Bahati mbaya sana!
Wakati mataifa ya rasilimali nyingi yanarejea katika utumwa,wananchi wake wana kiu ya mabadiliko ya serikali zao,mabadiliko ya siasa na kijamii pasipo kujua mabadiko haya yana athari gani kwao?
Watu wengi katika Afrika wana kiu ya maisha bora pasipo kujua atayaleta shetani ama mfadhili wa aina gani! Ufadhili. Kila kitu ufadhili,hakuna ujamaa na kujitegemea tena.
Matokeo yake Afrika inakwenda kasi kurejea utumwani,inarejea katika mapinduzi baada ya mapinduzi,yawe ya raia dhidi ya serikali, ya wanajeshi dhidi ya serikali za kiraia, ama jeshi na raia kwa upande mmoja dhidi serikali za kiraia kama ilivyotokea Misri.
Naam, hii huitwa struggle for freedom, harakati ambazo sasa ni za uhuru ndani ya nchi huru,uhuru dhidi ya uhuru bandia ili kurejea katika ukoloni.
Uhuru wa kwanza(1950-1970) ulidhaniwa ungeboresha uchumi,siasa na jamii ikashindikana,leo tunasema ilikuwa uhuru wa kuondoa Wakolobi Wazungu ili waingie wakoloni Weusi!
Serikali za vyama vya uhuru zilipambana na ukoloni mamboleo ukashindwa kufikia malengo.Rasilimali za nchi hazikugawanywa vizuri.Kada ya watawala walijipa kipaumbele,wakasaua tabaka la watwana,walalahoi.
Tutaondokaje katika shida hii,vijana sasa wakipata ufadhili toka nje,wanataka kununua bunduki ili kupambana kwa lengo la kujikomboa!
Bunduki na fedha kutoka Magharibi,ili kujikomboa dhidi ya Mkoloni Mweusi! Hakuna anayejali matokeo ya Wazungu kufadhili vita na fujo Afrika,atakuja nani kutawala?
Swali,tukipigana vita kali kuondosha serikali za vyama vya uhuru kwa msaada wa Mzungu,tutamlipa nini kama siyo rasilimali hizo anazochukua sasa kupitia uwekezaji?
Ni kweli mafisadi na wakoloni weusi hutorosha mali kwenda Ulaya na Marekani,sawa. Tukiwaondoa kwa vita kama Tunisia,Misri,Libya n.k tunawalipa nini wafadhili wetu? Au tunadhani wanatupenda sana?
Tufikiri vizuri,njia bora ya uhuru wa kweli.Ndiyo tunaona vyama vya siasa vinatamani kuanzisha majeshi eti kujilinda. Ukweli ni kuanzisha majeshi ili kupambana kukamata dola na rasilimali.
Ukichunguza kwa makini unaona sote tunakumbatia utegemezi wa Metropolitan Power kufanikisha malengo ya kwenda au kusalia Ikulu,kwa lengo la kufaidi rasilimali na madaraka!
Vyama halisi vya kumkomboa Mwafrika sasa havipo.tuambizane ukweli,kuna vyama vya malengo tofauti ya kushika dola na wala siyo kuleta ukombozi wa kweli wa Bara hili na watu wake kutoka kwa wakoloni mamboleo.
Mataifa haya yanayojidai sasa wafadhili na wawekezaji hayajasahau nia yao ya kuitawala Afrika na kujichotea rasilimali na rasilimali watu.
Ubinafsishaji ni sera za IMF na Benki ya Dunia(WB) zilizoanzishwa baada ya Vita kuu ya Pili ya Dunia.
Sasa,ni vita ya sisi kwa sisi,kila mtu na staili yake ya kumpelekea Mzungu rasilimali na madini,mafuta,gesi,wanyamapori,mazao ya kilimo n.k
Umwagaji wa damu unatumiwa sasa ili kuuza bunduki na kubadilishana kwa madini ama nishati na nguvu kazi ya chee.
Watu wanaomba vita viendelee Afrika ili hata hao wanaotaka kuanzisha majeshi katika vyama wagawane maeneo ya rasilimali na kuuza Ulaya na Marekani,kama wanavyofanya Waasi wa Uganda na Rwanda huko Congo(DRC).
Ni vita kama vya RUF dhidi ya serikali ya Sierra Leone miaka ya 1990-2000 ili kuchota almasi kwa damu ya raia.
Nataka kuseka kwamba ‘social revolution’ siyo kuunda jeshi ama kuchukua silaha na kuuana! Njia sahihi ni kulinda maslahi ya taifa nay a kila mwananchi kwa njia za haki bila kunyang’anya maisha ya watu ama umwagaji damu.
Hili la kwanza,Pili National Interests siyo kupambana jino kwa jino kama Chad,Misri,Libya.Mali n.k
Hizi dola kubwa,Urusi,Uchina,Marekani,Uingereza,Ufaransa n.k wakati Fulani hukubaliana kutugombanisha ili waendelee kuchota rasilimali na kufanya biashara ya bunduki kwa kubadilishana na mafuta,pembe za ndovu,dhahabu, almasi n.k
Kama hujui hili,jiulize silaha kwa waasi wa Congo hutoka wapi? Nani hulipa mishahara ya Waasi misituni? Nani huwapelekea maji na mafuta?
Kama hujui,ni kwamba Waasi hukamata eneo lenye manufaa ya biashara haramu ya magendo.Mataifa makubwa lao moja-kutuchonganisha.
Ni hapa ninapoona haja ya Waafrika kuwa na vyama vya siasa kwa lengo la kushindana kwa sera nzuri na kamwe siyo kugombania madaraka ya kushika dola ili kugawana rasilimali.
Hiki ndicho chanzo cha mapinduzi mapya katika Afrika.
Misaada ya Ulaya, “The Myth of Aid” katika vyama hivi vya siasa ndiyo nguvu yao ya kuleta vita na kuanzisha majeshi mapya ili kuwafunza vijana vita,ili kufikia malengo ya kushika dola,na kamwe si kumkomboa Mwafrika!
Hakuna ajenda ya kuondoa rasilimali zetu mikononi mwa wageni ili kujikomboa, ni kupambana kwa namna yoyote-hata kwa gharama za damu za wananchi-ili kushika ama kusalia madarakani ili kujineemesha!
Hakuna jipya katika vyama vyenu hivi vya siasa.Ajenda za ukombozi za kweli za akina Nyerere,Mandela na wenzake hakuna siku hizi.
Adui yetu Mkoloni,pande zote zimemgeuza Mfadhili na mshauri katika medani ya vita vya umwagaji damu.Akitoka Mwingereza kumfadhili Amin kuua watu anakuja Mrusi na kambi yake!
Hakuna jipya.Mursi na Adly Mansour wote wana wafadhili wao,kama si Warusi ni Waingereza na Wamarekani na wote lengo lao ni rasilimali na cheap labour kwa wananchi wetu.
Ni kufuatia hali hii Afrika bado haiko huru na inakwenda njia isiyo sahihi,watu wanaposhangilia,vyama siyo masihi.
Bungeni,vyama vya siasa na NGOs kumejaa mafisadi wanapaza sauti kusema serikali ni mafisadi.
Utashangaa kuona vyama vya waandishi wa habari mikoa na NGO za wajanja wanaojidai vyama vya wanahabari,wajidai kukemea ufisadi, huku wenye viti wanapowaita nyumba ndogo zao na ndugu zao kugawana posho za Pres conference!
Watu wanapandia katika ulaji kwa migongo ya wanahabari,wanunua magari na kuwanunulia nyumbandogo magari ya fahari huku wakiimba, “Mafisadi!”
Kawimbo ‘Mafisadi’ huibwa na watu wanaonuka mithili ya kwapa la shetani!
Hii ndiyo tabu! Hatujui adui yetu ni nani? Shetani naye anamtukana Shetani! Mwisho tutamalizana tusipojisahihisha ili kujua adui yetu ni nani? Ni rushwa,ni ufisadi na kila fisadi katika jamii,na siyo waliomo serikalini tu,wengine tunao hata humu kweye habari.
Akitoka fisadi anaandaa mkewe naye kurithi NGO na serikali ziko hivyo.Museveni-Janet-Muhoozi Trinity Power.
Hawa madikteta wako kila mahali siyo serikalini tu, bahati mbaya sana hawajui kuwa hawajui kwamba ni mafisadi na waporaji wa haki za wenzao.Wanadhani mafisadi na madikteta ni wa serikalini tu,hata vyama vya siasa ni mali za watu Fulani,mkikosana wanakutimua!
Wanachama hawana nguvu wala sauti.Hakuna full democratic liberties.Mtoto,mjukuu,shangazi, ndiyo huruhusiwa kukamata mamlaka.Kuongoza vyama.
Akina Nasser,Obote,Nyerere,Nkrumah walijaribu kujenga usawa wakashindwa,waliondoka wakaingia akina Amin Dada katika kila Nyanja ya maisha. Kinachoendelea ni uongo wa propaganda,na hakuna hatua kuelekea uhuru wa Mwafrika! Upendeleo na unyama. Hakuna jipya.
Ni kumalizana,kukanyagana,kuandamana kila asubuhi. Utumwa ni utumwa,hauna rangi!
Itaendelea
0786 324 074
 

amin

Dk.Milton Apollo Obote, alikuwa akihudhuria Mkutano wa kilele wa Commonwealth,huko Singapore alipopinduliwa na Amin.
Vikosi vilivyomtii Amin Dada,vilikamata uwanja wa ndege wa Entebbe,na jiji la Kampala likawekwa chini ya Ulinzi mkali,Makazi ya Obote yakazingirwa na jeshi,kasha mabarabara makubwa yaliwekewa vizuizi.
Radio Uganda,ikamlaumu Obote na serikali yake kwamba ilijaa upendeleo hususan kwa kabila lake la Acholi na Lango.
Raia nao hawakai mbali kwa viherehere,walishangilia majeshi kuipindua serikali ya mjini Kampala,wakidhani Amin angekuja na jipya,labda kuwapikia chai ya asubuhi!
Amin akatangaza kwamba yeye si mwanasiasa,nia skari;hivyo jeshi likashika hatamu hadi hapo siku ya uchaguzi mkuu ingetangazwa,baada ya hali kuwa shwari.
Haikutangazwa.Ila,wafungwa wa kisiasa waliachwa huru,ni wale ambao serikali ya Obote iliwasweka jela ama kizuizini.
Wakati huo msafara wa Obote uliokuwa Singapore ulilazimika kutua Dar es salaam,Obote akawa mkimbizi wa kisiasa kwa rafikiye, Hayati Mwalimu Nyerere. Obote aliungana na Waganda wenzake hapa Tanzania.
Mwaka 1972 hawa wakimbizi walijaribu kuipindua serikali ya Nduli Iddi Amin.Hawakujipanga vizuri;walishindwa vibaya.Amin akitaka kujikosha, akawaachia huru wafungwa wa kisiasa na akampa mazishi ya kitaifa Sir Edward Mutesa,aliyefia uhamishoni.Mazishi hayo yalifanywa Aprili, mwaka 1971.
Feburuali Pili, mwaka 1971 Amin alijitangaza mwenyewe kuwa Rais,Mkuu wa Majeshi,Mnadhimu Mkuu na Mkuu wa Vikosai vya Anga na akawa kila kitu.
Baadhi ya vipengele katika katiba ya Uganda vilibadilishwa vikaondolewa kabisa,Baraza la Kijeshi likaongoza nchi,wanajeshi wakaongoza Mahakama,serikali, Ikulu ya Kampala ikawa ‘Command Post’.
Amin aligeuza kikosi cha General Service Unit(GSU) kuwa kikosi cha kupeleleza wanaomsema vibaya The State Research Bureau,na ole wako ukutwe unaisema vibaya serikali ama Amin mwenyewe!
Unapelekwa Nakasero,unateswa kinyama hadi unakufa kasha maiti yako wanapewa mamba wa Mto Nile.
Tafuta filamu ya Whittaker,  THE LAST KING OF SCOTLAND, utajua Amin alikuwa nani?
Polisi nao walipewa ruhusa kukamata wenye midomo mirefu vijiweni asubuhi-subuhi,na kulikuwa na ma ‘MP’ wa jeshi na kikosi cha usalama wa Raia(PSU) kikitanda kila sehemu kubaini wapinzani wa serikali.
Ndugu zake Obote,Acholi na Lango waliteswa sana maana walihusishwa na jaribio la mapinduzi la 1972.
Kambi za Mbarara na Jinja zilifanya mauaji ya wapinzani wa serikali hii ya kiimla.Askari 5000 Waacholi na Lango waliuliwa kinyama sana,inakisiwa raia 10,000 walipotezwa!
Hawa walikuwa wa makabila hayo ya Obote na wale viongozi wa dini waliojitia kugeuza madhabahu kuwa kijiwe cha siasa za kumpinga Amin.Wanahabari pia walichinjwa ‘wakapotezwa’,wasanii waliokosoa serikali,majaji,wasomi,wanasheria na wanazuoni na raia wa kigeni,miili yao ilikuja kugunduliwa ikiliwa na mamba Mto Nile.
Utawala wa Amin(1971-1979) uliua watu wengi wasiofahamika idadi.Inakisiwa labda watu 80,000 walikufa ama labda 300,000.Amnesty International walisema Amin aliua watu 500,000.
Miongoni mwa watu maarufu waliouawa ni Benedicto Kiwanuka,Waziri Mkuu wa zamani na Jaji Mkuu,mwingine Askofu Mkuu wa Anglikan,Janani Luwum,Joseph Mubiru,Frank Kalimuzo,BYRON Kawadwa,na mawaziri,Erinayo Wilson Oryema na Charles Oboth Otumbi-unakutwa asubuhi nyumbani kwako na maofisa wa SRB unachukuliwa ndani ya buti ya gari,kisha mke wako hakuoni tena-umeliwa na mamba wa Mto Nile.
Amin aliwalisha mamba wa Nile kwa maiti za wapinzani wa serikali yake,mwaka 1972 ilikuwa Agosti,Amin akatangaza vita vya kiuchumi. Aliwatimua Waasia 80,000 walioishi Kampala huku wakiwa na passport za Uingereza,maduka yake walipewa nduguze Amin.
Hawa Wahindi wengine walizaliwa Uganda zama za ukoloni,wakajidai kutojipambanua kama raia,wakafanya biashara na passport za kigeni mkononi,walitimuliwa wakaacha maduka yao nyuma,magari na mali nyingine.
Walijifanya si wazalendo wa nchi, wakijidai kuthamini uraia wa Uingereza,Canada,Marekani na mahali pengine.Amin alivunja uhusiano na Uingereza, akataifisha biashara 85 za Waingereza.
Uhusiano wa Uganda na Israeli nao ulikufa,ingawa Waisraeli walishajenga miradi kadhaa pamoja na uwanja wa Entebbe.Israeli iliwauzia Waganda silaha. Walikuwa washauri wa kijeshi lakini Amin akawatimua akajenga uhusiano na Kanali Muammar al Qaddafi na Warusi.
Mwaka 1976 Juni,likatokea tukio la Wapalestina(PFLP-EO) na Wajarumani wa Revolutionare Zellen kuteka Waisraeli hadi Entebbe,watu 156 ambao hawakuwa na passport za Israeli waliachwa huru ndege hiyo ilipotua Entebbe.
Watu 83 na wengine 20 wakiwemo wafanyakazi wa ndege walishikiliwa na wateka nyara hao hapo uwanja wa Entebbe.
Umewahi kusikia Operation Thunderbolt? Ama umewahi kusoma 90 Minutes at Entebbe? Umewahi kutazama filamu ya Raid on Entebbe? Nitakupa full stori katika matoleo yajayo juu ya Waisraeli kukomboa mateka wao hapo Entebbe, usikose toleo lijalo
0713 324 074
 

AMIN

Dk.Milton Apollo Obote, alikuwa akihudhuria Mkutano wa kilele wa Commonwealth,huko Singapore alipopinduliwa na Amin.
Vikosi vilivyomtii Amin Dada,vilikamata uwanja wa ndege wa Entebbe,na jiji la Kampala likawekwa chini ya Ulinzi mkali,Makazi ya Obote yakazingirwa na jeshi,kasha mabarabara makubwa yaliwekewa vizuizi.
Radio Uganda,ikamlaumu Obote na serikali yake kwamba ilijaa upendeleo hususan kwa kabila lake la Acholi na Lango.
Raia nao hawakai mbali kwa viherehere,walishangilia majeshi kuipindua serikali ya mjini Kampala,wakidhani Amin angekuja na jipya,labda kuwapikia chai ya asubuhi!
Amin akatangaza kwamba yeye si mwanasiasa,nia skari;hivyo jeshi likashika hatamu hadi hapo siku ya uchaguzi mkuu ingetangazwa,baada ya hali kuwa shwari.
Haikutangazwa.Ila,wafungwa wa kisiasa waliachwa huru,ni wale ambao serikali ya Obote iliwasweka jela ama kizuizini.
Wakati huo msafara wa Obote uliokuwa Singapore ulilazimika kutua Dar es salaam,Obote akawa mkimbizi wa kisiasa kwa rafikiye, Hayati Mwalimu Nyerere. Obote aliungana na Waganda wenzake hapa Tanzania.
Mwaka 1972 hawa wakimbizi walijaribu kuipindua serikali ya Nduli Iddi Amin.Hawakujipanga vizuri;walishindwa vibaya.Amin akitaka kujikosha, akawaachia huru wafungwa wa kisiasa na akampa mazishi ya kitaifa Sir Edward Mutesa,aliyefia uhamishoni.Mazishi hayo yalifanywa Aprili, mwaka 1971.
Feburuali Pili, mwaka 1971 Amin alijitangaza mwenyewe kuwa Rais,Mkuu wa Majeshi,Mnadhimu Mkuu na Mkuu wa Vikosai vya Anga na akawa kila kitu.
Baadhi ya vipengele katika katiba ya Uganda vilibadilishwa vikaondolewa kabisa,Baraza la Kijeshi likaongoza nchi,wanajeshi wakaongoza Mahakama,serikali, Ikulu ya Kampala ikawa ‘Command Post’.
Amin aligeuza kikosi cha General Service Unit(GSU) kuwa kikosi cha kupeleleza wanaomsema vibaya The State Research Bureau,na ole wako ukutwe unaisema vibaya serikali ama Amin mwenyewe!
Unapelekwa Nakasero,unateswa kinyama hadi unakufa kasha maiti yako wanapewa mamba wa Mto Nile.
Tafuta filamu ya Whittaker,  THE LAST KING OF SCOTLAND, utajua Amin alikuwa nani?
Polisi nao walipewa ruhusa kukamata wenye midomo mirefu vijiweni asubuhi-subuhi,na kulikuwa na ma ‘MP’ wa jeshi na kikosi cha usalama wa Raia(PSU) kikitanda kila sehemu kubaini wapinzani wa serikali.
Ndugu zake Obote,Acholi na Lango waliteswa sana maana walihusishwa na jaribio la mapinduzi la 1972.
Kambi za Mbarara na Jinja zilifanya mauaji ya wapinzani wa serikali hii ya kiimla.Askari 5000 Waacholi na Lango waliuliwa kinyama sana,inakisiwa raia 10,000 walipotezwa!
Hawa walikuwa wa makabila hayo ya Obote na wale viongozi wa dini waliojitia kugeuza madhabahu kuwa kijiwe cha siasa za kumpinga Amin.Wanahabari pia walichinjwa ‘wakapotezwa’,wasanii waliokosoa serikali,majaji,wasomi,wanasheria na wanazuoni na raia wa kigeni,miili yao ilikuja kugunduliwa ikiliwa na mamba Mto Nile.
Utawala wa Amin(1971-1979) uliua watu wengi wasiofahamika idadi.Inakisiwa labda watu 80,000 walikufa ama labda 300,000.Amnesty International walisema Amin aliua watu 500,000.
Miongoni mwa watu maarufu waliouawa ni Benedicto Kiwanuka,Waziri Mkuu wa zamani na Jaji Mkuu,mwingine Askofu Mkuu wa Anglikan,Janani Luwum,Joseph Mubiru,Frank Kalimuzo,BYRON Kawadwa,na mawaziri,Erinayo Wilson Oryema na Charles Oboth Otumbi-unakutwa asubuhi nyumbani kwako na maofisa wa SRB unachukuliwa ndani ya buti ya gari,kisha mke wako hakuoni tena-umeliwa na mamba wa Mto Nile.
Amin aliwalisha mamba wa Nile kwa maiti za wapinzani wa serikali yake,mwaka 1972 ilikuwa Agosti,Amin akatangaza vita vya kiuchumi. Aliwatimua Waasia 80,000 walioishi Kampala huku wakiwa na passport za Uingereza,maduka yake walipewa nduguze Amin.
Hawa Wahindi wengine walizaliwa Uganda zama za ukoloni,wakajidai kutojipambanua kama raia,wakafanya biashara na passport za kigeni mkononi,walitimuliwa wakaacha maduka yao nyuma,magari na mali nyingine.
Walijifanya si wazalendo wa nchi, wakijidai kuthamini uraia wa Uingereza,Canada,Marekani na mahali pengine.Amin alivunja uhusiano na Uingereza, akataifisha biashara 85 za Waingereza.
Uhusiano wa Uganda na Israeli nao ulikufa,ingawa Waisraeli walishajenga miradi kadhaa pamoja na uwanja wa Entebbe.Israeli iliwauzia Waganda silaha. Walikuwa washauri wa kijeshi lakini Amin akawatimua akajenga uhusiano na Kanali Muammar al Qaddafi na Warusi.
Mwaka 1976 Juni,likatokea tukio la Wapalestina(PFLP-EO) na Wajarumani wa Revolutionare Zellen kuteka Waisraeli hadi Entebbe,watu 156 ambao hawakuwa na passport za Israeli waliachwa huru ndege hiyo ilipotua Entebbe.
Watu 83 na wengine 20 wakiwemo wafanyakazi wa ndege walishikiliwa na wateka nyara hao hapo uwanja wa Entebbe.
Umewahi kusikia Operation Thunderbolt? Ama umewahi kusoma 90 Minutes at Entebbe? Umewahi kutazama filamu ya Raid on Entebbe? Nitakupa full stori katika matoleo yajayo juu ya Waisraeli kukomboa mateka wao hapo Entebbe, usikose toleo lijalo
0713 324 074
 

amin

Dikteta idi Amin Dada(1)

Na conges mramba
ALIPOTIMULIWA na majeshi ya Tanzania Uganda, Aprili 11 mwaka 1979,Amin alitimkia Saudi Arabia.
Aliishi katika gorofa za juu katika Hoteli ya Novotel,iliyoko Palestine Street ,mjini Jeddah,Saudi Arabia.
Julai 20 mwaka 2003 mmoja wa wake zake,Madina, alitoa taarifa kwamba Amin alikuwa mahututi hospitalini King Faisal,mjini Jeddah.
Mafigo yalikuwa yakimsumbua;yalishashindwa kufanya kazi.Kwa sababu hiyo,Madina alimtaka Rais Yoweri Kaguta Museveni kuruhusu Amin arejee nyumbani na akifa azikwe Uganda.
Serikali ya Museveni iliweka masharti makali kwa Amin,kwamba kabla hajarejea nyumbani atubu dhambi zake.Agosti 16 mwaka 2003 Amin aliaga dunia hapo hospitalini mjini Jeddah. Ilibidi azikwe kwenye makaburi ya Ruwais mjini humo,kwani Museveni alimwekea nguMU Amin hata maiti yake kuzikwa Uganda.
Amin alizaliwa labda mwaka 1925 hivi huko kijiji cha Koboko.Baba yake alikuwa Andreas Nyabire(1880-1976)na alikuwa wa kabila la Kakwa.Mwanzoni walikuwa Wakatoliki,wakabadili dini na kuwa Waislam mwaka 1910.
Akaitwa Amin Dada, alipomzaa mtoto naye akamwita jina hilo hilo la Amin DADA.Kama Adolf Hitler,Amin naye alitelekezwa na babaye,Amin akakulia ujombani,Kaskazini Magharibi mwa Uganda.
Mama yeke,Assa Aatte(1904-1970) wa kabila la Lugbara,alikuwa mganga wa miti shamba au tuseme ‘Sangoma’ hivi.Amin akasoma Madrassa, akasoma Kiingereza kidogo katika shule ya msingi hakumaliza huko Bombo,kilomita 30 Magharibi mwa Kampala .Huo ulikuwa mwaka 1941.
Alipoacha shule akafanya vibarua kama Hitler alivyokuwa,baadaye akajiunga na jeshi la Kikoloni la Mwingereza, King’s African Rifles(KAR).
Amin alikuwa mwanajeshi wa KAR tangu mwaka 1946,akianza kama mpishi msaidizi na baadaye alipanda vyeo kila mwaka hadi kuwa Mkuu wa majeshi zama za Apollo Milton Obote(PhD).
Aliingia Batalioni ya 21 ya KAR kikosi cha ardhini huko Gilgil,Kenya ambako walipelekwa KASKAZINI ya Kenya ili kudhibiti majambazi(magaidi)wa Kisomali.
Mwaka 1952 Amin akapata u corporal na mwaka uliofuata akapandishwa cheo na kuwa sergeant.Mwaka 1959 Amin alikuwa warrant officer,cheo ambacho hakuna Mwafrika aliyekuwa nacho katika jeshi la kikoloni.
Amin alirejea  Uganda na mwaka 1961 alipewa cheo cha Luteni,kazi yake ilikuwa kuwafagia wezi wa mifugo baina ya Karamajong wa Uganda na Turkana ambao ni wafugaji wahamaji wa Kenya.
Wakati wa Uhuru 1962 Amin alipandishwa cheo na kuwa Captain na 1963 akawa Major.Mwaka ulipopita akawa Naibu Commander wa jeshi.Watu walisema huenda alisaidiwa na uchawi wa mamaye ili kupanda vyeo!
Alikuwa mwanariadha.Alikuwa na urefu wa sentimita 193 yaani futi 6 na inchi 4.Jitu lenye miraba minne na alikuwa Bingwa wa ndondi wa uzito wa juu mwepesi-light heavy weight.
Mwaka 1951 alikuwa pia mwogeleaji nguli na alicheza rugby katika nafasi ya ushambuliaji, akichezea timu ya Nile RFC mwaka 1951.
Alishiriki magendo ya pembe za ndovu na shahabu huko Congo(DRC) inawezekana walidhulumiana na OBOTE chuki zikaanza ingawa alishampandisha cheo sasa na kuwa Mkuu wa majeshi(CDF) ya Uganda.
Ni Amin aliyemshambulia Kabaka Mutesa akatimkia Uingereza ambako alifia 1969.Amin alikula fedha za jeshi, alipooNA Rais anakwenda kuhudhuria Mkutano wa kilele wa Commonwealth huko Singapore,Amin akapindua serikali Januari 25,mwaka 1971.
Obote akiwa njiani akaambiwa Amin kapindua serikali,wanajeshi wakatanda tangu uwanja wa ndege wa Entebbe hadi Kampala, Obote akaenda kutua Tanzania-Dar.Wakati huo kulikuwa na wakimbizi 20,000 wa Uganda,akina MUseveni.
Itaendelea

MAGUFULI JEMBE BWANA

  Kweli Yahya Bilal, Dk.Magufuli 'Jembe'Bwana!
       Na conges mramba,Mwanza
NI JANUARI mwaka huu wa 2013, huko Uwanja wa ndege wa Mwanza.
Magufuli anafika huko kukagua miradi ya ujenzi na kuanza kuwachambua wazembe kama ilivyo kawaida yake!


WAZIRI WA UJENZI,John Pombe Magufuli,  ‘alimgonga’kiaina Waziri wa Uchukuzi,Dk.Harrison Mwakyembe,kuhusu mkandarasi kuchelewesha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza.
Dk.Magufuli, alifika Mwanza Januari 10 mwaka huu, na kukagua barabara ya kutoka Nyakato National kwenda Buswelu,itakayotumika baada ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza kuanza.
Ijumaa,Januari 11, mwaka huu 2013,Dk.Magufuli akafika uwanja wa ndege wa Mwanza,ili kukagua barabara iendayo Igombe,inayopita mita chache kutoka unapoanzia uwanja huo na kukuta mkandarasi hajaanza ujenzi; na wala hakukuwa na vifaa vilivyoletwa kuanza ujenzi huo.
Awali,kulikuwa na malalamiko kutoka kwa mkandarasi kwamba,Wizara ya Ujenzi ilikuwa ikikwamisha kuanza kwa ujenzi wa uwanja wa ndege,kwa kushindwa kuifunga barabara hiyo ya Igombe inayopita eneo ambalo  limo ndani ya ramani mpya ya uwanja huo.
Magufuli, alipoona hakuna dalili za kuanza kwa ujenzi wa uwanja huo,wakati tayari wizara yake ikilalamikiwa kwa kushindwa kuifunga barabara ipitayo ndani ya eneo la mradi wa ujenzi, akaja juu:
“Kwani barabara hii ya kwenda Igombe inamzuia nini Mkandarasi huyu kuanza ujenzi wa uwanja?
 Mkandarasi huyu tayari amelipwa malipo ya awali shilingi bilioni 8; angekwisha ‘clear site’ lakini hakuna alichofanya, wala hajaanza kupanua zile mita 500 za runway inayopanuliwa; na anasingizia kufungwa barabara!” Magufuli alisema.
Akasisitiza kuwa hawezi kuifunga barabara ya Igombe hadi mkandarasi huyo aanze kujenga uwanja huo.
Barabara itokayo katikati ya Jiji hili kwenda Igombe,hupita kandoni mwa uwanja wa ndege unaopanuliwa ili kufikia viwango wa kimataifa.Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema,Mkandarasi anayejenga uwanja huo, Beijing Construction Engineering Group(BCEG) alikuwa amesaini mkataba tangu mwezi Juni mwaka jana,na muda wa kusafirisha vifaa(mobilizing period) wa miezi mitatu ulipita bila kuleta vifaa eneo la mradi, kwa sababu vifaa vilikuwa vingali kisiwani Zanzibar.
Kufuatia hali hiyo,Dk.Magufuli akataka maelezo kutoka BRELA,ikiwa BCEG walikuwa wamesajiliwa,na kama walikuwa na uzoefu.
Mwakilishi kutoka BRELA,akamwambia Dk.Magufuli kuwa kampuni hiyo kutoka Uchina ilisajiliwa miaka mine iliyopita,na ilikuwa imejenga uwanja wa Taifa,Dar es salaam.
“Okay,sitaifunga barabara hii,kwani inawahudumia hata akina mama wanaotaka kujifungua hospitalini.Nitafungaje barabara halafu akina mama wajifungulie barabarani hapa eti kwa sababu barabara imefungwa,wakati hata vifaa,hata toroli halijaletwa hapa ili kuanza ujenzi?”,Magufuli alisaili.
Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza uko chini ya Wizara ya Uchukuzi ya Dk.Harrison Mwakyembe,lakini Magufuli akamwambia Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi,Eng.Omar Chambo, “Miezi mitatu ya ‘mobilization’ imepita,mkataba ulisainiwa Juni mwaka jana,leo ni miezi saba hakuna kinachoendelea hapa, halafu anasema kinachomkwamisha kuanza ujenzi ni barabara hii! Sasa niifunge basi,tuone kama ataanza ujenzi wakati hana vifaa,hakuna hata  tingatinga, hata toroli!” alisema Magufuli,huku akiuliza, “Injinia Mshauri(consultant) yupo wapi?”
Akatokea mbele zake.
Magufuli akampiga maswali kama alikuwa na uzoefu wa kazi. Consultant huyo toka Zambia, akajaribu kujitetea. Magufuli akamwambia kwa kimombo: “Make sure not to compromise with that bogus Contractor… message has sent and delivered!”,
Kwamba huyo injinia toka Zambia aangalie asikubaliane na uzembe huo, akasema tena kwa umombo, “You may have a bogus contractor, but you must be very tough, otherwise this may be the last job in           East Africa”, kwamba awe makini la sivyo hii ndiyo itakuwa mara ya mwisho kufanya kazi hapa Afrika ya Mashariki!
Wakati Magufuli akimcharukia Mkandarasi huyo na mshauri wake toka Zambia, akatangaza kufungwa barabara hiyo pindi ujenzi wa uwanja ukianza.
Akasema,serikali tangu mwaka 2008 imewatimua makandarasi wazembe wanaoshindwa kuzingatia masharti ya mikataba.
Uwanja wa ndege wa Mwanza unapanuliwa kufika viwango vya kimabara kwa gharama ya shilingi bilioni 105 zinazotolewa na serikali pamoja na Benki ya Waarabu ya Maendeleo(The Arab Bank for Economic Development of Africa, BADEA).
Hatua hiyo ya Magufuli kumcharukia mkandarasi huyo imetafsiriwa kuwa ilikuwaa ‘kugongana’ na waziri Mwakyembe hadharani.
Utakapopanuliwa,uwanja huo utakuwa na njia ya kurukia yenye urefu wa mita 3,700 badala ya ilivyo sasa mita 3,300.
Utakuwa na jingo jipya la kuongozea ndege jirani na kilima(Traffic control tower),jingo jipya la abiria,maegesho na maeneo mengine muhimu pamoja na sehemu ya mafuta ya ndege,ili ndege zinazotoka Mwanza kwenda Ulaya au Asia,zisilazimike kupitia Dar es salaam kunywa mafuta.
 
 
NILIMPIGIA kura Mgombea wa chama fulani, ili awe rais  wa Jamhuri  ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano,katika uchaguzi uliopita, 2010.
Lakini, nimepata mashaka moyoni mwangu!
Sioni mgombea wa kupigia kura mwaka 2015.
Wagombea wengi,hawana ‘a certain unique qualities’ ni kelele tu.
Rais wa NCHI YANGU ubongoni mwangu mimi, anatakiwa asiwe na mke au mume, awe hivi muda wote awapo Ikulu, na asiwe na watoto wala jamaa,rafiki,mashemeji.
Rais Dikteta,mwenye akili nyingi kama Magufuli; na hana jamaa,lakini jamaa zake na watoto wake ni sisi raia wake.
Watoto wa rais ni nywele za kila raia wake!
Mwandishi,Mike Royko, wa Chicago Sun-Times, aliwahi kuandika jambo hili zamani sana, President’s family in everyone’s hair.
Nilikuwa nikimheshimu Rais Kikwete na hata Dk. Wilbrod Slaa,lakini...
  Siyo kwamba, Kikwete ni Rais mbaya; la hasha. Si kwamba amefanya kazi mbaya.
Nafurahishwa na  baadhi ya mambo na vitu vingi anavyofanya Rais wetu; lakini ningependa Tanzania iongozwe na Rais mwenye sifa mbadala, ambazo hazijawahi kuwepo.
Nawaheshimu viongozi wa Kambi ya Upinzani, na kazi njema waliyofanya,ya kuikosoa serikali hii ya Chama cha Mapinduzi, ambayo ilishaanza kuota mapembe.
Hata hivyo, sijaona mgombea mwenye sifa za kutosha kuwa Rais wa TANZANIA NINAYOITAKA. Naam, Tanzania ya kesho niitakayo mimi lazima iongozwe na Rais asiye na watoto, asiye na mke,asiye na ndugu wala jamaa!
 Isipokuwa,ndugu,mke na jamaa zake tuwe sisi Watanzania kwa ujumla wetu,na Rais atulee mithili ya nywele zake kichwani!
   Ningependa sasa Tanzania iongozwe na Rais mwenye sifa za pekee, ili kuondokana na majanga kama haya ya viongozi kuendesha Biashara zao(japo halali) wakiwa Ikulu.
Naam, namtaka Rais ambaye ana sifa ambazo Kikwete hana!
 Hata Slaa na wanasiasa wengine kama Prof Lipumba hawana sifa ninazotaka!
   Nimeorodhesha hapa baadhi ya sifa ninazotaka Rais mpya baada ya Kikwete awe nazo:
Rais asiwe na mke, yaani awe mseja; na awe hivyo kipindi chote cha kuwa  kwake Ikulu yetu ya Magogoni, Dar es salaam !
 
   Pili, Rais atakayekuja baada ya Mhula wa Kikwete kumalizika mwaka 2015, awe yatima. Hatutaki marais wenye wake,watakaojaza mashemeji Ikulu!
Rais asiyekuwa na ndugu na jamaa wenye madhambi yanayoigubika nchi kwa kashfa; tena kashfa zenyewe kubwa zinazopamba kurasa za mbele za magazeti. Tumeshochwa na kashfa za wake na watoto wa vigogo, ambao pengine huua raia kwa risasi,lakini polisi hugwaya kuwatia mbaroni.
  Naam. Rais asiye na mke anayepenyeza pua yake katika masuala ya uongozi wan chi, wakati hakuna aliyempigia kura kufanya hivyo!

Rais mwenye mke ambaye anafungua makampuni yanayoendesha biashara pengine bila kulipa kodi.
 Mke wa Rais(First Lady) ambaye atapewa leseni na kukopeshwa fedha na mabenki kwa kasi, ili kufanya biashara kubwa kubwa, akijidai mjasiliamali.Kumbe,hata kodi halipi?
Rais asiwe na watoto ambao wanatajirika haraka haraka,baba yao anapokuwa Ikulu,wakati sisi raia tunahangaika!
    Lazima Tanzania yenye watu kama Milioni 44.9  iwe na Rais mwenye sifa za pekee, kuliko Benjamin William Mkapa, au Jakaya Kikwete.
Kuliko Dk.Slaa,Mbowe, Prof.Lipumba, ama wanaotajwa siku hizi,akina Magufuli,Membe,Mwakyembe,Lowassa n.k
 
Nataka Rais awe Mwenye hekima, mtu wa haki, mwenye akili.
Lakini, hana familia, hana jamaa wa kumharibu akili awapo Ikulu pale.Hana mashemeji.
Rais ambaye familia yake ni sisi Watanzania, na awe anatutunza mithili ya mboni ya jicho lake.
   Nimewahi kusikia tetesi za wake za Marais wastaafu, jamaa zao na watoto wao kuitumia vibaya ikulu kufanya biashara.
Nakiri, sijawahi kusikia tetesi za Mjane wa Hayati Mwalimu, Mama Maria Nyerere kutumia Ikulu kufanya biashara. Hata hivyo, simpendi Rais kama Nyerere,najua familia yake haiwezi kuwa waadilifu na wajamaa tena.
    Tetesi kwamba Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa waliendesha kampuni yao , ANBEN wakiwa Ikulu, zinanivuruga akili.
Biashara hiyo ya Mkapa na Mama Anna, iwe halali au haramu, si hoja kwangu.
Lakini, napendekeza Tanzania isiwe na Marais wenye familia zinazowasukuma kufanya biashara mapema wakiwa Ikulu, ili kukimbia umasikini!
Nimesikia tetesi za utajiri wa watoto wa  mararais kama Kikwete, na Mkapa! umepatikana haraka!
    Wapo marais waaminifu na ndugu zao na watoto wao ni waaminifu; hawaitumii vibaya Ikulu.
Lakini, hatuhitaji sasa Rais mwenye mke,watoto,ndugu na jamaa na familia.
   Kadhalika, wapo wake wabaya wa marais  wenye wapambe, ndugu na jamaa wanaowashauri vibaya ili kujinufaisha na Ikulu. Wake, jamaa, wapambe na ndugu hawa nao hujigeuza maofisa wa serikali.
   Nani aliyewachagua kufanya chochote?
Nani aliwateua kuwa na sauti hadi kuwafokea mawaziri?
Unakumbuka Kenya, Lucy Kibaki aliwahi kuwachapa makonde maofisa wa serikali na kubomoa makompyuta na magazeti?
Kama ni hivyo, basi tungepewa nafasi ya kuwapigia kura hawa jamaa za marais, na wake zao  kabla hawajaingia Ikulu.
   Au, kwa sababu ndugu yao anapoingia Ikulu, wao hujigeuza ‘Mabalozi’ ama ‘Wabunge’ Fulani, basi wangepelekwa kula kiapo mahakamani, kwamba hawataitumia Ikulu kwa maslahi binafsi kipindi chote cha Bwana, Bibi, Mjomba au Shemeji yao, anapokuwa Ikulu.
   Leo, tunashuhudia mbio kali za watoto wa vigogo kutaka kuwania madaraka. Sisemi kwamba watoto wa wakubwa hawana haki ya kuwania madaraka, la hasha!
Wawe watoto wa wakubwa wenye Visheni; waachane na hadithi za kurithi damu za uchifu wenye falsafa ya kurithishana madaraka.
    Siasa si maneno matupu majukwaani.
 Ni kuzifanya sera zizae maendeleo ya watu. Je, watoto wa vigogo wanaosaka madaraka kwa udi na uvumba, kupitia vyama Tawala, wanayo Visheni hii?
    Au,wanawania madaraka  ‘kutetea’ madhambi ya baba zao pindi wanapomaliza mhula wao, baada ya kushindwa kubadili Katiba ili kurefusha muda wa kusalia madarakani?
   Licha ya wake za marais kudaiwa kufanya biashara ama kufungua vikampuni visivyotozwa kodi wakiwa Ikulu, watoto wao wamekuwa wakiwasaidia baba  au mama zao kutawala kwa mabavu. Wamekuwa wakishiriki kuwatesa raia na kukiuka Haki za Binadamu.
    Rais wa zamani wa Liberia, Charles Ghankay Taylor ambaye juzi amefungwa London miaka 50 kufuatia mashtaka ya Uhalifu wa kivita  huko The Hague, Uholanzi, mtoto wake, Charles Mc Arthur Emmanuel, au Charles Taylor Jr; ambaye Liberia alifahamika sana kama, Roy Belfast Jr, alitiwa mbaroni Desemba 15 mwaka 2005, akafunguliwa kesi mbili.
   Alitiwa mbaroni huko Miami , Marekani kwa kosa la kuwatesa kinyama waliompinga baba yake, na pia alikuwa na kesi ya kughushi Hati ya kusafiria.
   Ghankay Taylor, ambaye sasa amefungwa jela, na mahakama ya  The Hague, alishirikiana na rafikiye, Foday Sankoh, wa kikundi cha RUF kufanya unyama Sierra Leone na kuwauzia waasi hao silaha kwa kubadilishana na almasi.
    Licha ya kuwepo kwa tetesi za wake za marais kuingilia mambo ya serikali, kuwafokea mawaziri na hata kuwatwanga makofi waandishi wa habari hapa Afrika, watoto wa Marais pia wanatuhumiwa kuhusika na kashfa nzito.
Wanakuwa matajiri upesi bila kujua mitaji ya biashara walipata wapi?
    Gideon Moi, mtoto wa Rais wa zamani wa Kenya , Mzee Moi, alikuwa na tuhuma za kuhusika katika kashfa anuai za ufisadi nchini humo. Wengine, wakiwemo watoto wa wakubwa wa Dunia hii, wanatuhumiwa kubwia unga, kuuza ama kuvuta bangi na kuendesha biashara haramu hata katika Vyuo vikuu, lakini kwa sababu ya upendeleo, woga au kujikomba, vyombo vya Usalama hujikuta vikishindwa kuwachukulia hatua.
Mtoto wa Makamu wa Rais wa Marekani, AlGore, aliwahi kutiwa mbaroni kwa tuhuma za madawa ya kulevya.
   Hata kama  watoto hawa wa wakubwa waliua, au hata kama walijeruhi ama kutaharukisha umma, huachiwa mara moja, wasiyaone magereza!
   Mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Bi Margaret Thatcher(86), Mark Thatcher(60) lituhumiwa kuendesha biashara haramu na kufanya uhaini.
   Sir Mark Thatcher, mwenye vituko vya “Front Page” katika magazeti, aliwahi kupotea katika Jangwa la Sahara . Alipotea kwa siku kadhaa, wakati akishiriki Mashindano ya Paris-Dakar( Senegal ) Rally, akasababisha Bi Thatcher kuangua kilio hadharani, wakati akiwa Waziri Mkuu!
    Margaret Thatcher, alikuwa Waziri Mkuu wa Uingereza tangu mwaka 1979 hadi 1990. Lakini mtoto wake huyo aliwahi kutiwa mbaroni na polisi wa Afrika Kusini kwa tuhuma za kuongoza njama za kupindua serikali ya Guinea ya Ikweta.
    Ametiwa mbaroni na vikosi vya usalama mahali pengi Afrika; hata Zimbabwe . Polisi wa Afrika Kusini walisema, walikuwa na ushahidi wa kutumainiwa, kwamba Mark Thatcher aliwapa fedha waasi wa Guinea ya Ikweta, ili wampindue Brigedia Jenerali Mstaafu, Teodoro Nguema Mbosongo, Rais wa Baraza la Kijeshi la nchi hiyo, aliyedaiwa kuvunja Haki za Binadamu.
   Guinea ya Ikweta ni ya tatu Afrika kwa kuzalisha mafuta kwa wingi. Pengine, Mark anayetuhumiwa hata kuhusika katika biashara haramu ya silaha, alitaka mafuta ya nchi hiyo. Naam, hao ndiyo watoto wa wakubwa.
   Hata hivyo, wapo watoto wa viongozi waliopata kuwa viongozi wazuri. Waziri Mkuu wa zamani wa India , Indira Ghandhi, alikuwa Binti wa Waziri Mkuu wa Kwanza wa India , Jawaharlal Nehru. Baadaye, Sanjay na Marehemu Rajiv Ghandi nao wakafuata nyayo.
    John Quincy Adams aliyekuwa Rais wa Marekani 1825-1829, alikuwa mtoto wa Rais John Adams aliyetawala Marekani mwaka 1791 hadi 1801. Adams alikuwa Rais wa pili baada ya George Washington.
    Yupo George W.Bush ambaye baba yake George  Herbert Walker Bush, alikuwa rais miaka ya 90.
Nduguze, kama Jeb Bush ni viongozi; ni wanasiasa maarufu. Hata hivyo, katika orodha, wapo wengi viongozi watoto wa viongozi kama akina Sir Mark Thatcher  wenye tuhuma kama wahaini, wezi, wauza unga na wahujumu uchumi, wao na wapambe wao, lakini hawakamatwi wala kuhojiwa!
    Wako akina Roy Belfast Jr. wanaoghushi hati mbalimbali na  kufanya biashara haramu na halali, wanaotesa wapinzani wa serikali za baba zao, ambao pia hugeuza Ikulu kuwa ‘mapango’ ya wanyang’anyi ama ‘Mungiki’ wanao ifanyia jamii ugaidi mkubwa.
   Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kuwaonya watu kuiogopa Ikulu. Ikulu ni mahali Patakatifu. Si mahali pa kufanyia biashara hata ziwe halali na nyeupe kama sufi.
Rais anapoboronga, ama mkewe, jamaa au shemeji zake wanapoendesha magendo ikulu(Doing Business from Ikulu), ndipo harakati za kutafuta warithi huanza!
    Akina Umaru Yar’ Adua wa Nigeria wametafutwa na akina Obasanjo mara nyingi sana kupitia kitu ambacho si Uchaguzi, bali unyafuzi na Uchafuzi Mkuu wa Haki, Demokrasia na Uhuru Afrika!
    Ni kwa sababu hii, ningependekeza wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu, angetazamwa Mgombea ambaye jamaa, wapambe, rafiki, mke na watoto wake hawataiabisha ikulu kwa magendo, vituko, skandali na biashara zisizolipiwa kodi.
     Kama watoto, wake na wapambe wa Rais wangepelekwa Bungeni kwanza kuthibitishwa na kula viapo mahakamani, basi hofu kama ya Rais Jakaya Kikwete ya kumchunguza mtangulizi wake, isingekuwepo. Hofu ya kutafuta kubadili katiba isingekuwepo, kama wake, watoto na jamaa wa Rais wangedhibitiwa na Bunge au Mahakama.
    Lakini, pamoja na haya yote, ili kuepuka Marais kufanya Biashara Ikulu, napendekeza Tanzania ingekuwa na Rais Mseja, lakini asiye mzinzi wa kukwapua wake za raia wake; asiyekaribisha machangudoa Ikulu na kuitia unajisi nchi, rais mjane asiye na familia ya kumtia majaribuni; na yatima ambaye baba, mama na watoto wake ni sisi raia wake.
Nikijadili, agenda 2015 katika televisheni ya Star, nikamfananisha mtu Dikteta ninayemtaka kama Magufuli,kidogo!!
Kosa lake aliwahi kujitia doa katika nyumba za serikali wakati wa Awamu ya tatu,lakini Magufuli 'Jembe' kali Bwana!!
   0713 324 074
www.congesmrambatoday.blogspot,com