Wednesday, October 23, 2013

uchafuzi wa makampuni ya mafiuta afrika

African Headlines (© ASSOCIATED PRESS)

mwarabu na mwafrika tosha kukataa ukoloni



                                         


NA CONGES MRAMBA

RAIS MSTAAFU wa Afrika Kusini,Nelson Rolihlahla Madiba Mandela, aliwahi kumkemea George Walker Bush wa Marekani kwamba aliivamia Irak mwaka 2003 ili kupora mafuta.

Madiba, alisema Vita vya Ghuba vya miaka ya 1990 na 2003 vilikuwa vya kupora mafuta.Mataifa makubwa ya Ulaya Magharibi, siku hizi hutumia silaha vitani ili kukamata nishati muhimu kama mafuta,gesi,uranium n.k

Hii ni kufuatia mataifa tajiri ya mafuta na gesi,hususan ya Kiarabu kukaribia kuukata koo uchumi wa Mataifa hayo miaka ya 70.

Tangu Vita vya Pili vya Dunia, mafuta yalipatikana tele na kwa bei poa kwa viwanda na ili kusafirishia bidhaa za mataifa makubwa haya.

Mwaka 1973, wakati ule wa vita huko Mashariki ya Kati,Waarabu wanaozalisha mafuta kwa wingi, walipunguza uzalishaji na kuongeza bei ya nishati hiyo maradufu.

Ongezeko la bei ya mafuta huko Mashariki ya Kati, ni kusababisha chumi za nchi za viwanda kuanza kutetereka.

Ukitaka vita mlangoni kwako,basi anzisha sera za kuzuia chumi za ‘Industrialized Nations’ kukua kwa ufanisi. Utasingiziwa ‘Gaidi’ ili upigwe kwa drones!

Nchi za Kiarabu zilitangaza kuinyima nchi yoyote mafuta kwa kuwa inaisaidia Israeli(Adui Mkuu wa Waarabu),kwa hali hiyo,Marekani,Ufaransa,Uingereza na washirika wao wasingeuziwa mafuta na Mwarabu.

Kwa mara ya kwanza mwaka 1973,Mwarabu alitumia nishati ya mafuta kama “SILAHA MUHIMU” katika siasa za kimataifa.

Nchi wazalishaji na wasafirishaji wa mafuta(OPEC) walikubaliana kupunguza uzalishaji wa mafuta,kasha wakaongeza bei ya nishati hiyo muhimu kwauchumi wa dunia.

OPEC walikubaliana kulinda na kutunza akiba yao ya mafuta,ili kuwatoa kamasi Wazungu!

Bei ya mafuta ikapaa;mgogoro mkubwa wa mafuta,maarufu kama, “THE OIL CRISIS” ukatikisa viwanda vya mabwanyenye,uzalishaji ukashuka maradufu.

Mfumuko wa bei(Inflation) ulikita;viwanda vingine vikafungwa na kusababisha ukosefu wa ajira ulioikumba dunia.

Mwaka 1979 Mfumuko wa Bei ulipanda kwa asilimia 334 kuanzia takwimu za mwaka 1969.

Hii ni kusema, bidhaa iliyouzwa kwa Pauni moja ya Kiingereza mwaka huo 1969,sasa ikauzwa kwa Pauni 3.34. Hali hiyo ilifuatia Waarabu kuzuia mafuta yao kuuzwa Ulaya-ARAB OIL EMBARGO-mwaka 1973,kukaleta kiama cha kutisha kwa Marekani,Uingereza, Ufaransa na rafiki zao.

Mfumuko wa bei(Inflation) usiosemeka ulisababisha bei zikapanda kila kulipokucha,fedha zilikosa thamani mfululizo.

Nataka nikwambie msomaji.Ikiwa ili upate nishati ya kupikia chakula chako(kuni,mkaa,mafuta,gesi n.k) ingekugharimu fedha zinazojaa magunia matatu ya noti za elfu kumi-kumi!

Kwa nini usitumie magunia mawili ya noti zenyewe kama kuni ili kupikia chakula chako,kuliko kununua mafuta au kuni kwa magunia matatu ya noti?

Kwenye mfumuko wa bei noti huwa hazina thamani kwa kiwango hiki! Italia,mfumuko wa bei ulifika asilimia 319,Japan(236%),Ufaransa(234%),Marekani(196%) n.k

Nimesema, chanzo kilikuwa ‘reduced supply’ kukaja kuzaliwa shida nyingine ya kitu kinaitwa, “recession”, biashara ikasinyaa,hata bidhaa hazikuzalishwa tena viwandani-sababu ya kiburi cha Mwarabu!!

Hata Urusi haikuwa salama;Afrika nayo iligugumia maumivu ya kupanda kwa gharama kufuatia kupanda bei ya mafuta soko la dunia.Kununua bidhaa soko la dunia kuligharimu bei mbaya wakati huo wa miaka ya 70.

Hali hii ilifanya mataifa ya KIARABU kutajirika maradufu,Waarabu wakawa wanakula maisha sana hata huko Ulaya.Marekani pamoja na kuwa na mafuta yake yenyewe,ikakumbwa na kilio kikuu cha ukosefu wa mafuta.

Marekani hutumia mafuta mengi kuliko nchi yoyote hapa Duniani.

Kufuatia hali hiyo,Marekani ilikaribia kutembelea magoti na kukoma kuwa “economic strong man”.

Nakumbuka, Katuni moja iliyochorwa na Wadachi mwaka 1973,Mwarabu akiwa amewaweka CHINI YA ULINZI viongozi wanne wa Dunia:

Kansela Willy Brandt wa Ujerumani,Rais Georges Pompidou wa Ufaransa,Rais Richard Nixon wa Marekani na Waziri Mkuu,Edward Heath wa Uingereza.

Hawa walionekana kwenye katuni wakiwa wamewekwa chini ya Ulinzi na Mwarabu kwa kutumia ‘Pampu’tu ya mafuta, siyo bunduki wala guruneti!

Walishikiliwa hadi Mzungu alipe kikombozi(ransom) ndipo waachiliwe huru.

Zama hizo, Saudi Arabia,Irak,Iran,KUWAIT,Libya,Abu Dhabi,Algeria n.k zikapata heshima mbele ya mabeberu.Nchi nyingine kama Nigeria,Guinea ya IKWETA,Venezuela,Indonesia,Ecuador,Angola n.k zingeweza kuwa na kiburi cha kuyagomea mataifa haya kwa kutumia mafuta kama silaha.

Norway,Mexico na Uingereza walihaha kusaka vyanzo vipya vya mafuta.Mwaka 1979 kulikuwa na uhaba wa mapipa milioni 2.3 kila siku.

Ni hapa Mwarabu alipotikisa ndevu za Mzungu, hususan Marekani ambayo kwa siku moja hutumia theluthi ya mafuta yoote yanayotumiwa na dunia nzima.

Huu ndiyo wakati Mohammed Reza(Shah) wa Iran alipouza mafuta yote Marekani na kuiacha nchi yake ikiwa kavu kabisa!

Itaendelea

0713 324 074

MWARABU NA MWAFRIKA WAKIUNGANA TOSHA KUKOMESHA UKOLONI




CONGES MRAMBA,MWANZA

 

Mapema mwaka juzi,kulitokea tishio la vita huko HORMUZ STRAIT.

SABABU NI Iran kutishia kuufunga mlango bahari wa Hormuz endapo ingeshambuliwa ama ikiwekewa vikwazo isiuze mafuta yake duniani.

  Mataifa matano wanachama wa   kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Marekani,Uingereza, Ufaransa , China na Urusi ndiyo wanaomiliki makampuni makubwa sana ya mafuta duniani.

Kutoka miaka ya 70 hadi 2011 tayari Mzungu keshanunua hisa katika visima na makampuni ya mafuta, anatawala siasa za mafuta duniani.

 Makampuni haya, ‘SUPERMAJORS’ yanashikilia sasa soko la mafuta kutokana na mitaji yake mikubwa kabisa.

PETROCHINA, BRITISH PETROLEUM (BP), Royal/Dutch Shell,Exxon,Texaco,Gulf,Mobil n.k ni makampuni yenye mitaji mikubwa na maamuzi makubwa katika soko la mafuta duniani. Sibneft,Lukoil na Yukos nayo ni makampuni ya Kirusi yaliyo chini ya Ikulu ya nchi hiyo-Kremlin.

 Kuna Chevron,Total na mengine ambayo huunganisha mitaji ili kulikamata soko la mafuta duniani.

 Ni mataifa haya haya yenye makampuni ya mafuta na viwanda ndiyo huchafua mazingira ya dunia na hugoma kutia saini mikataba ya mazingira kama ule wa Kyoto-Japan,huku visima vya mafuta ni moja ya vyanzo vya uharibifu mkubwa wa mazingira,na hakuna wa kusema.

  Ni hawa ambao leo wanaiona Israeli haina kosa hata kama itaua Wapalestina na kuwakandamiza. Mtu mmoja aliwahi kuniuliza,kwanini Mkristo nawatetea Waislam.

Mimi si msemaji wao,ila hata wao hunilaumu kusema kwamba watalazimishwa hata kuabudu  sanamu ya Mzungu kwa sababu ya maslahi.

  Wazungu wanataka mafuta, na bahati mbaya wameungana na dunia nzima kutaka hata miungu yao iabudiwe na wao waabudiwe kama miungu.Tazama UFUNUO 13:18

Unabii wa Biblia hutuambia hatma ya vita hivi,kwamba mataifa ya Ulaya na Marekani yatakumbatia madhhebu Fulani na wakuu wake(Ufunuo 17:9-11) ili kuwaburuza watu wa dunia nzima.

 Na wenye hekima na akili zenye hekima ndiyo wataelewa jambo hili. Mamlaka haya yatafananishwa na FALME saba zilizowahi kuitawala dunia huko zamani:

 Waashuri,Wamisri,Babeli, Medo-Persia, UGIRIKI,Rumi ya kale na Rumi zama za Upapa .Katika milki hizi Mungu wa kweli alipingwa na waliomwabudu waliuliwa na kuteswa,ukweli ulikataliwa, historia inajirudia.

Ufunuo 17:13 husema wafalme wa dunia watakuwa na AJENDA MOJA YA SIRI,kumrithisha Mfalme mmoja utawala wao wa dunia nzima,na wanaopinga wauawe au wawekewe vikwazo vya uchumi,anayebisha apewe kibano,kama tutakavyoadhibiwa kwa meli za Iran ‘kuvaa’ Utanzania!

Mwanamke anayebebwa mjini Brussels hatimaye atakuwa na sauti duniani, tazameni Goddes Roma.

Huu ni unabii wa Mzungu kutawala nchi zenye rasilimali hususan Afrika na Asia,hata kama Mwafrika na Mwarabu wana rasilimali nyingi kama mafuta,gesi,almasi,dhahabu,ardhi safi n.k

Mzungu anatumia kila njia kuhujumu amani na uchumi wa Mwarabu na Mwafrika!

 

Kampuni ya Shell ya Uingereza,iliwalipa fedha wanamgambo kuwaua wanaharakati wakati walipoandamana huko Niger Delta, kupinga makampuni hayo ya kigeni kuchimba mafuta  eneo hilo wakati wakiharibu mazingira,bila kulipa fidia.

 Niger Delta hakukuwa na mafuta na huduma za kiuchumi hazikuwepo licha ya mapipa mengi kuchimbwa eneo hilo  la Kusini mwa Nigeria.

Kampuni ya Chevron ya Marekani,iliwalipa mishahara polisi na jeshi kuwaua wanaharakati kama Ken Saro-Wiwa, kwa sababu walipinga uhalifu wa makampuni haya kwa maandamano makubwa ya amani.

Watu wajinga wanapoona Afrika polisi wakikabiliana na waandamanaji,akili inawatuma Ulaya hawakabiliwi.

 Kumbe, Ulaya na Marekani walikuwa nyuma ya vikosi vya Sani Abacha kuwaua wanaharakati waliopinga makampuni ya kigeni kuharibu mazingira bila kuleta maendeleo kwa raia hata licha ya kuchimba mafuta katika eneo hilo.

Sasa, kama Gaddafi alishambulia waandamanaji wa Benghazi,akapinduliwa kisha kuuliwa kwa risasi, Kiongozi wa Syria, Bashar al Assad naye anawashambulia raia wanaompinga anashughulikiwa na Ulaya na Marekani,kwanini Shell na Chevron yalishinikiza serikali ya Nigeria kuwaua waandamanaji?

 

Huko Burma,(siku hizi ni Myanmar) kampuni kubwa la Unocal la Marekani, lilitiliana saini mkataba na jeshi kuilinda,ilipokuwa ikitekeleza ujenzi wa Bomba la gesi asilia kama hiyo ya Mtwara, kupelekwa nchi nyingine.

Bomba hilo lilikuwa likijengwa kutoka Yadana,wanakijiji walitumikishwa pasipo ujira,walibakwa,waliuliwa.

Waliteswa na wanajeshi,Marekani wakiwa pembeni,wakatumikishwa kitumwa.

Wapo wajinga,wataanza kusema,ilikuwa kampuni siyo serikali ya Marekani,subiri uone!

Wanakijiji walifungua kesi ya madai dhidi ya kampuni hilo la Unocal,kulitumia jeshi la Yangon kuua vibarua,kubaka na kuwatumikisha kitumwa,pasipo malipo ili gesi iende nchi nyingine.

Shirika la Habari la Agence France Presse(AFP) likasema miaka saba iliyopita kwamba, Unocal walipobanwa wakasema ukweli,wakakubali kuzungumza na wanavijiji wa Burma ili kesi iondolewe mahakamani,walikubali kuwalipa fidia na kuwasaidia kuimarisha maendeleo.

Nimesema Unocal; ni kampuni la Kimarekani la kuchimba gesi.Mahakala ilikuwa inakaribia kuwapa ushindi wanavijiji wa Burma waliofungua kesi Califonia.

Nikusimulie kidogo.Jumanne,Desemba 10, mwaka 2003 kampuni hili katili la Kimarekani lilipandishwa kizimbani huko California ili kujibu mashitaka ya hao wanavijiji wa Burma, na kuhalifu haki za Binadamu.

Nchi ya Burma wakati huo ilikuwa chini ya utawala wa kiimla wa kijeshi ambao Marekani hujidai sana kuupinga hapa Barani Afrika,kumbe sehemu nyingine wanajali maslahi tu.

Hii ‘Brutal Military Junta’ waliwalazimisha raia kujenga bomba la urefu wa kilomita 62,waliokataa waliuliwa,akina mama wakabakwa na kuumizwa bila fidia.

Bomba lenyewe lilikuwa la kilomita 62 sawa na maili 39 ili kupeleka gesi kutoka Myanmar kwenda Thailand.

Basi, Unocal walipobanwa wakakubali kulipa fidia maana kazi waliyofanya wanavijiji hawa wa Myanmar mwaka 1990s ilikuwa ya thamani ya Dola bilioni 1.2.

Sasa jiulize,wewe shabiki wa hawa Marekani na Ulaya, Utumwa kwa wananchi wa      Burma ndiyo Haki za Binadamu?

 Utumwa huu katika karne ya karibuni?

Unocal walishirikiana na kampuni la Ufaransa,Total kupeleka gesi Thai.

Tutazame wanavyoharibu mazingira ya dunia,hasa nchi za dunia ya tatu na kukataa kusaini mikataba ya upunguzaji wa hewa za sumu angani,ili tupatwe majanga ya asili.Laiti nchi hizi zingeungana kupinga ubeberu na ukoloni mambo leo,zingeiamrisha Marekani!

MAREKANI CHIMBUKO LA MAJANGA

haya ni majanga ya kiasili ambayo ukiyachunguza yataletwa na kiburi cha Moabu,Marekani na washirika wake,kwa kuchafua sana anga la dunia,kukataa kusaini mikataba kama ule wa Kyoto(Kyoto Protocol) ili maji yachafuke,viumbe wafe kwa Ongezeko la joto na mabadiliko ya tabianchi, mafuriko kila mahali,

vifo majanga, kansa, ukimwi,vyanzo vya maji kuwa damu,kutoboka kwa utando wa Ozone n.k

 Moabu ya kiroho(Marekani) iligoma kutia saini Mkataba wa Kyoto mwaka 1997,kwa sababu kufanya hivyo kungeleta hasara kwa wafanyabiashara wan chi hiyo-Wakaona heri kuongeza madhara kwa kumwaga hewa chafu angani ili wajipatie UTAJIRI.

 

Miongoni mwa shughuli za kiuchumi za binadamu zinazoharibiwa sana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi ni pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi n.k

    Mkutano wa New York ulioanza Septemba 22 mwak 2009, umefanyika takriban miaka 12 kamili tangu mkutano wa Kyoto, Japan ufanyike Desemba mwaka 1997.

   Katika mkutano wa Kyoto, viongozi wa mataifa zaidi ya 150 duniani walikutana wakaweka  itifaki ambayo ingewezesha kupunguza hewani kiwango kikubwa cha gesi au hewa chafu ya sumu zinazoletwa na hewa ya ukaa(C02) na gesi nyingine kama     CH4,N20, HFC8, PFC8  na SF6.

   Mkataba huo uliojulikana kama  itifaki ya Kyoto(Kyoto Protocol) uliokusudia kupunguza gesi za sumu duniani kwa silimia 5.2 kabla ya kufika mwaka 2012.

  Mataifa yaliyoshurutishwa kusaini mkataba huo wa Kyoto ni nchi zote 38 zenye viwanda duniani..

Mataifa yote 15 ya Umoja wa Ulaya(EU) yakakubali kupunguza asilimia nane ya taka hewa zake duniani. Marekani ilitakiwa kupunguza asilimia saba ya gesi zake inazotupa angani.

 

 Japan, ilitakiwa kupunguza asilimia sita ya taka sumu inazotupa angani, na nchi zinazoendelea zilitakiwa kupunguza kiwango chochote kwa uhuru wake.

 Marekani ilisaini mkataba huo Novemba 12, mwaka 1998, lakini kutokana na kitisho kutoka kwa matajiri wenye viwanda nchini humo, serikali ya Rais Bill Clinton ilichelea kupeleka ajenda hiyo katika Bunge la seneti.

 Kwa sababu, kusaini mkataba wa Kyoto na kuutekeleza, maana yake ni kwamba viwanda vya Marekani vingelazimika kupunguza uzalishaji.

Ni kwa sababu hii serikali ya Clinton iliufyata.

  Mkutano mwingine wa kujadili upunguzaji wa taka za sumu hewani ulifanyika Bonn, Ujerumani Julai 2001.

Utawala wa George .W. Bush ulitangaza kujitoa katika mkataba wa Kyoto kwa madai kwamba uliweka zigo kubwa katika nchi zilizoendelea bila kuzingatia usawa.

 Marekani, waligeuka wapinzani wakubwa katika ajenda za kupunguza hewa za sumu duniani, tangu huko mjini Bonn, Ujerumani na mahali pengine, kwa sababu ya maslahi yake na ya viwanda vyake, bila kujali madhara makubwa yaliyotokana na wingi wa viwanda vyake kutupa angani hewa chafui zenye kusababisha majanga makubwa kwa Ulimwengu mzima..

Hizi ndizo haki za binadamu Ulaya na Marekani?

  Kwa shingo upande, walikubali kupunguza hewa hizo za sumu ili kutekeleza huo mkataba au itifaki ya Kyoto ya 1997.

  Katika makubaliano ya mjini Bonn, mataifa makubwa yenye viwanda yanayomwaga kwa wingi hewa za sumu angani, yalishauriwa kufuata malengo waliyowekewa ya kupunguza hewa ya ukka katika anga.

 Kulingana na Shirika la Kudhibiti Uharibifu wa mazingira, hewa ya ukaa(carbon dioxide) imeongezeka sana angani kutoka mwaka 1990 hadi sasa; na hii ni kutokana na shughuli za binadamu, ikiwa ni  pamoja na viwanda na migodi.

  Wakati hewa za sumu zinapoongezeka sana duniani, misitu ama miti inayopunguza kwa kiwango kikubwa hewa ya ukaa kwa kutengenezea chakula chake(starch) inatoweka kwa kasi na kwa kiwango cha kutisha sana.

  Tazama nchi zinavyoongeza sana kiwango cha hewa za sumu angani.

 Mashariki ya Mbali pamoja na Oceania wanachafua anga kwa kiwango cha asilimia 28.9.

Amerika ya Kaskazini huchafua anga kwa kiwango cha asilimia 28.8.

 Marekani pekee inachafua anga la dunia nzima kwa moshi wa magari na viwanda vyake kwa asilimia 24.7.

   Ulaya Magharibi, kwa pamoja huchafua anga la dunia kwa asilimia 16.5, wakati Amerika Amerika ya Kusini nzima na Kati huchafua anga la dunia kwa kiwango cha asilimia 4.3.

   Ulaya Mashariki, na iliyokuwa Jamhuri ya Kisovieti(USSR) huchafua anga la dunia nzima kwa kiwango cha asilimia 12.8. Mashariki ya Kati huchafua anga kwa kiwango cha asilimia 4.7.

 Afrika, inachangia katika uchafuzi wa anga la dunia kwa asilimia 3.9 tu.

Hii ni kwa mujibu wa Ripoti za Energy Information Administration, kuanzia mwaka 1999.

 Afrika inayochangia kwa kiwango kidogo sana katika uchafuzi wa hewa angani, ndiyo inayoathiriwa sana na madhara makubwa ya uchafuzi wa hewa angani unaoleta mabadiliko ya tabia ya  nchi.

 Mifugo ya Afrika, hususan Kenya  na hapa kwetu hufa kwa ukame unaoletwa na uchafuzi wa mazingira ya anga. Uchafuzi wa anga ndiyo chanzo cha ukame huko kwetu Afrika. Ukamwe huu ndiyo unaochangia jangwa kuongezeka, ukame na njaa na vifo vya watu pia.

 Kulingana na uchafuzi huo wa hewa angani, Benki ya Dunia(WB) ilishasema mwaka 2001 kwamba kila mwaka watoto wachanga wapataao 500,000 wangepoteza maisha duniani pote kwa sababu ya uharibifu huu mkubwa wa anga.

Vifo huletwa na viwanda vya Ulaya na Marekani siyo? Kumnyang’anya mtu uhai siyo haki za binadamu sawa?

  Kunatokea mvua za sumu(acid rains) zitakazosababisha uharibifu mkubwa sana wa misitu hasa ya Afrika, na wala mvua za sumu hizi za viwanda vya mataifa makubwa haziharibu huko kwao peke yake.

 Nataka kusema kwamba, Marekani inaongoza duniani kwa uchafuzi wa anga, lakini athari zake tunapata sisi huku; tunakufa kwa njaa na matokeo ya ukame na hata vimbunga kama Mitch, tsunami na Katrina ambavyo vikitokea, huua maelfu ya watu bila kujali mipaka ya nchi za viwanda na zisizokuwa na viwanda.

  Ni kwa sababu hii, ubeberu wa Marekani wa kukataa kutia saini mikataba ya upunguzaji wa hewa na taka za sumu, kama huo wa Kyoto wa mwaka 1997, ni hatari kwa maisha ya watu, hasa tuishio nchi masikini.

  Ingekuwa heri kama Mkutano wa New York  na Afrika ya Kusini ungeipa kibano kikali Marekani kwa kiburi chake na kuwelka mbele maslahi binafsi ya viwanda vyao, huku ng’ombe wa masikini wanapokufa kwa maelfu huku kwetu, pasipo fidia.

  Marekani, hukimbilia kuliburuza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuzitenga nchi nyingine kaidi kutekeleza mikata kama ya Nyuklia n.k

 Ni  Marekani hiyo hiyo inayotaka Iran na Korea Kaskazini na Iran zitengwe au zishambuliwe kijeshi kwa kukataa kutia saini mkataba wa kupunguza silaha za nyuklia.

 Mbona yenyewe inakataa kwa  ubabe kutekeleza mkataba wa Kyoto, unaotaka hewa za sumu zinazoleta majanga duniani kudhibitiwa. Ongezeko la joto duniani linaloleta hayo majanga kama tsunami, huleta madhara hadi huku Bahari ya Hindi na kusababisha vifo hata Kenya, Tanzania na Somali. Kwa nini Marekani haidhibitiwi ama kupewa kibano au kushambuliwa kijeshi, kama yenyewe ilivyozishambulia Irak na Afghanistan,  na iko mbioni kuzishambulia Iran na Korea Kaskazini kwa kukataa kutekeleza mikataba ya upunguzaji silaha za sumu?

 Sumu inayoua watu si ndiyo iliyo,o pia katika silaha za atomiki na ndiyo ile inayorushwa angani na viwanda vya Marekani na Ulaya, bila kudhibitiwa na mtu, tena kibabe?

 Ni kwa sababu hii, viongozi wa Afrika waliokwenda New York kujadili kitisho cha hewa za sumu angani na mabadiliko ya tabia  ya nchi, wanapaswa kutoa tamko kali la kuikemea Marekani au ikibidi kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kuitenga na Jumuiya za Kimataifa, kwa vitendo vyake vya kibabe vya kuleta maafa Ulimwenguni.

 Dunia haina ubavu wa kuitenga Marekani?

Rasilimali za Waarabu na Waafrika zinatosha kuwa silaha ya kuikomesha Marekani,kama siyo ujinga wetu wenyewe.

Marekani haiwezi kushambuliwa kijeshi na dunia nzima ili kuishikisha adabu iache kuiangamiza dunia kwa kumwaga sumu tani mamilioni kwa siku, huku ikikataa kutia saini kila mkataba unaowataka kupunguza sumu?

  Wakuu wa nchi za Afrika(akiwemo Rais Kikwete) wanaporejea kutoka New York, wanapaswa kuwaambia wananchi wao, ni namna gani wamembana Barack Obama, kwa sababu nchi yake ina kiburi cha ubeberu, kuendeleza uzalishaji wa taka sumu, zinazoleta saratani ya ngozi huku, kuleta jangwa ama ukame na kuua mifugo Afrika, hususan Tanzania na Kenya.

 Shughuli za kilimo na ufugaji, ambazo hufanywa na masikini huku Afrika Mashariki zinatatizwa sasa na mabadiliko ya tabia ya nchi na ukame. Chakula cha binadamu hakuna, kwa sababu Afrika inakuwa jangwa, kwa sababu Jangwa la Sahara lililoko Kaskazini linakaribia kushikana na lile la Kalahari, lililopo Kusini.

 Sasa, mvua itanyesha jangwani?

 Ni kwa sababu hii, tunasema, kiburi cha Marekani kimekwisha kuleta majanga makubwa hapa Kwetu Tanzania tangu wakate kusaini Mkataba wa Kyoto Desemba 1997 hadi mkutano huo ulipofanyika New York, Septemba, 2009.

  Ni kwa sababu hii, Rais Kikwete na ujumbe wake, wanapaswa kuwaambia Watanzania, Rais Obama wa Marekani, ameambiwa kwa kiwango gani kulipa fidia ya mifugo ya Wamasai, Wajitta, Wasukuma, Wakurya na wafugaji wengine ambao mifugo yao inaangamia kwa sababu ya ukame ulioletwa na sumu na taka za hewani kutoka viwanda vya Mabwanyenye wa Marekani?

 Vinginevyo,  ile kasi ya Mwarabu kumnyima Mzungu mafuta ilikwenda wapi ili kukomesha kiburi chao?

 

 

 

Tuesday, October 1, 2013

AL-SHABAAB,AL-QAEDA


    !                                
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki-Moon, ambaye ni raia wa Korea Kusini, hana ubavu wa kusema ukweli kuhusu chimbuko la kitisho cha magaidi hapa Duniani.
Kama hajipendi, anaweza kumfuata kuzimu Katibu Mkuu wa Pili wa Umoja wa Mataifa,Dk.Darg Hjalmar Carl Hammarskjold wa Sweden!
KI-Moon, anatoka nchi kibaraka wa Mataifa Makubwa ya Magharibi, ambayo yameigawa Dunia katika mihimili miwili.
Ugaidi, ni zao la chuki za zama za Vita Baridi,kufuatia Dunia kutengwa mafungu mawili.
Korea mbili ni adui wakubwa,kufuatia kutengwa katika siasa za Kikomunisti na kibwanyenye.
Inakisiwa kwamba,Warusi(Wakomunisti) walikuwa wakidhibiti maisha nchini Somalia tangu mwaka 1968.
Walikusudia kujitanua hadi nchi zote za Upembe wa Afrika(The Horn of Africa) ambazo ni pamoja na Eritrea,Ethiopia, na Djibouti.
Kufuatia hali hiyo,Rais Jimmy Carter wa Marekani alikuwa na wajibu kuzuia Warusi kusambaza ushawishi wao Somalia,Ethiopia na mataifa ya jirani ya Kiarabu.
Urusi,ilikuwa na vituo vya kijeshi(Military Bases) katika nchi hizi za Upembe wa Afrika,hadi katika njia kuelekea Arabuni na Afghanistan na Pakistan.
Kwa hiyo,Marekani ikawa na kazi ya kuondoa ushawishi na utawala wa Kisovieti(Soviet Imperialism) katika Upembe wa Afrika.
Wakati huo, CUBA na raia wake walitoa msaada mkubwa hapa Brani Afrika.Cuba ilikuwa “Mkono Msaidizi” wa Dola kuu la Kisovieti(USSR).
Msomaji, unaweza kutambua sasa kwamba nchi zote za Ulaya Masharikizilionekana kuangukia zaidi siasa za mrengo wa kushoto wa Kambi ya Mashariki,na siasa zao za Ki-Marx na Lenin.
Kwa sababu hiyo,mataifa ya Ulaya Magharibi(ikiwemo Marekani) yalihaha kuhakikisha kuzuia Ukomunisti usisambae mithili ya saratani hadi Upembe wa Afrika, na tuseme Afrika nzima,na maslahi yao(ya kikoloni) yakawa hatarini!
Dola la Kisovieti(USSR)linasemwa kuleta silaha nyingi eneo la Upembe wa Afrika,tena nzito.Vita Baridi vilianza mara baada ya Vita vya Pili vya Dunia kwisha,mwaka1945.
Baada ya vita hivi vya Pili vya Dunia,Mataifa ya Mashariki yakiongozwa na Urusi(USSR) nay a Magharibi yakiongozwa na Mrekani yaliamkakugombea udhibiti wa Mataifa ya Ulimwengu wa Tatu,hususan Afrika,Asia na Amerika Kusini.
Kwa kuwa Warusi hawawezi kushindana na Marekani na washirika wake kwa uchumi, wao walianza kusambaza msaada wa silaha,magari ya deraya na ndege za kivita.
Hata Rais wa Somalia,Muhammad Siad Barre, alipewa msaada wa zana za kivita na USSR. Somalia ya sasa inayolaumiwa kuwafuga magaidi wa al-Shabaab,hutokana na mfuo wa kikoloni wa Kiingereza na Italia,wakijidai kuunganisha taifa mwaka 1960.
Haya ni mataifa mengine duniani yanayouza silaha nje kuliko nchi nyingine nyingi.
Wasomali ni wahamaji(nomadic tribesmen) wasiokuwa na makao maalum zama hizo.
Hawakuwa na rasilimali za kutosha,halafu uchumi wao haukuwa mzuri,kwa sababu ya kutokaa eneo moja na kuzalisha mali.
Wakati mwingine walitaka kuungana na Wasomali wenzao wa Ethiopia,Kenya na Djibouti.
Hivyo,ili kutimiza azma yao walihitaji silaha tena kali.Ikulu ya Marekani(White House) ilipokawia kuwafadhili bunduki,Ikulu ya Urusi(Kremlin) ikawapa bunduki kali hawa Wasomali wanaosemwa kuwa ‘Wakali’ wanapoishi kuzunguka Bandari kuanzia Mogadishu, hadi Ghuba ya Aden na Bahari ya Hindi.
Sasa utaona Pwani BAHARI YA Hindi kuanzia Mogadishu,Pwani ya Djibouti,Aden,Yemen,Kenya na Tanzania ni eneo hatari hata leo kwa maharamia wa Kisomali wenye bunduki za rashasha za Kirusi.
Wamarekani waliwahi kusema, ingawa Siad Barre alijidai kutumikia Warusi na falsafa za  Marx na Lenin, mvuto wake ulielekea kwenye Uislam.
‘Doctrines’ za Kirusi hazikufua dafu Somalia, ila bunduki zao walizipeda sana, nazilipatikana kwa wingi;wakazitumia kwa njia yoyote kupatia chakula na mahitaji mengine.
Inasemwa,Mfalme Haile Selassie wa Ethiopia aliunga mkono siasa za Magharibi; akapinduliwa kwa nguvu za jeshi kutoka Urusi,ili kundi la Wakomunisti washike nchi hii muhimu.
Habari hizi, zikubaliwe au zikataliwe na ubongo wako,lakini tunapata picha halisi kwamba, vita upembe huu wa Afrika(The Horn of Africa) yaani Somalia,Djibouti,Ethiopia na Eritrea ni matokeo ya Ikulu mbili-Kremlin na White House-kunyukana eneo hili tete hata leo,na matokeo yake wamezaliwa al-Shabaab wanaoua watu Kenya,Uganda labda watakuja Tanzania siku si nyingi!
Mungu apishilie mbali!!
Nani adhibiti ushawishi wa eneo hilo,ndiyo shida inayoleta changamoto za visasi vya magaidi hapa kwetu Afrika Mashariki.
Utawala wa Mengistu Haile Mariam(Mkomunisti) baada ya Haile Selassie,ukasemwa na Magharibi kwamba ulileta, “Terror” hofu kuu Ethiopia!
Neno hili, “Terror” hofu.ukiliongezea “ism” unapata  ‘TERRORISM’ maana yake Ugaidi.
Kwa hiyo Kambi ya Magharibi inasema aliyeleta ugaidi eneo hilo ni Urusi. Na tukumbuke Propaganda za Kimagharibi.Bila nguvu nyingine ya Magharibi kutaka kujitanua huko,Urusi wasinge sogea.
Ni kwa sababu hii, twapata picha kwamba chimbuko la ugaidi eneo hilo lote ni Madola makubwa ya Marekani na Urusi kujitanua huko.
Wakati Urusi inatawala mataifa haya kwa ‘remote’ White House hawakuchoka,wakawasaidia wafuasi wao ndani ya nchi hizi fedha na bunduki,ili kukamata Ikulu ambayo ingetawala Bandari za tangu Mogadishu,Djibouti,Aden, na Mlango Bahari wa Shamu,YEMEN,kuelekea Pakistan na Afghanistan.
Sasa unaona umuhimu wa kudhibiti eneo hilo la Bahari ya Hindi na Bandari hizo?
Bahari ya Shamu, ambayo Waisraeli wa zama za Musa waliivuka kwa miguu bila boti,ni muhimu sana kuunganisha Bahari za Hindi na Mediterranean.
MFEREJI WA SUEZ,uliochimbwa na Wafaransa na Uingereza huko Misri ni muhimu eneo hilo ili kuunganisha safari za meli kati ya Bahari za Mediterranean ,Shamu(Red Sea) na Hindi.
Mto Nile,unaoanzia Ziwa Nyanza na kutiririka umbali wa kilomita 6,900 unapita eneo hilo pia.Huu ni mto ambao ni damu itiayo uhai nchini Misri(the life blood to Egyptians), ni muhimu kusafirisha mafuta,bidhaa muhimu kwa uchumi wa Ulaya,Mashariki ya Kati,ya Mbali na Amerika na Afrika.
Hili ni eneo muhimu sana kiuchumi,ndiyo maana madola makubwa hupigana vikumbo kulikamata kwa usalama wa nchi zao, au usalama wa uchumi wao.
Haya madola makubwa-Urusi na Marekani- ndiyo waliochochea vita kati ya Somalia na Ethiopia,kupigania Jimbo la Ogaden, eneo ambalo ni moja ya tano ya Ethiopia.
Ethiopia,Somalia na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Yemen,hukodolewa macho na udenda na madola haya makubwa ili kuweka ‘interests’ zao.
Mpango mkubwa(master plan) wa mataifa makubwa ni kukamata eneo la Kusini mwa Afrika, na Mataifa tajiri ya Mafuta katika Ghuba ya Arabia.
 Chuki za Magharibi dhidi ya Fidel Alejandro Castro Ruz, ni kufika Afrika kusaidiana na washirika wao Urusi,kukomesha ukoloni wa Ulaya Magharibi huku Afrika Kusini.
Walikuja hata kushawishi Somalia kugeukia siasa za Ki-Marx.Utaona hata Shirika la Ujasusi la Marekani(CIA)likahaha kushawishi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar jijini Dar es salaam mwaka 1964,ili Zanzibar sisjekuangukia Ukomunisti!
Rais Jimmy Carter alitoa amri kwa Waziri wa Mambo ya Nje,Cyrus Vance,na Mshauri wake wa Usalama wa Taifa,Zbignew Brzezinski,kuhakikisha(to move to every possible way) yaani hata kwa ugaidi ama mabomu, alisema “to get Somalia to be our friend”.
Hii ni kauli ya Jimmy Carter,ili SOMALIA iwe ‘rafiki’ yao tena kwa gharama yoyote!
 Tazama kilichofanyika! Marekani chini ya Shirika lake la Ujasusi,CIA wakaanza kuipa Somalia msaada wa silaha! Huo ni mwaka 1977.
 Ilisemwa eti ili ‘kujilinda’ ila wasitumie silaha dhidi ya Djibouti na Kenya!
WAPI MAGAIDI WANAPATA SILAHA ZA HATARI?
Sasa silaha za West Gate zimetoka wapi?
‘Msaada’huo wa silaha kutoka MAREKANI kwenda Mogadishu ,ulikuwa na masharti kwamba Marekani isiwasaidie wanamgambo wa KISOMALI(Somali Liberation Front) huko Ogaden.
Msomaji anapofikiri vizuri, aone kwamba Marekani inapotoa msaada hata kwa Waasi,huwa na kwa sababu ya maslahi,vyama vya ukombozi navyo hunyimwa au kupewa msaada kwa sababu ya maslahi.
Hawa Wasomali wameishi Ogaden zaidi ya miaka 500
.Sasa MAREKANI wanaibembeleza Somalia iwakate URUSI ili wao wasaidie Mradi wa kukomboa Ogaden.
Unaanza kuona Somalia inapigana na Ethiopia,Marekani wakiwa nyuma ya Somalia!
Urusi inaleta MiG-21 Jets, vifaru vipya vya kisasa 400,Mi-8 ambazo ni helkopta za kivita 30 na maelfu ya silaha kuizuia Marekani kulitawala eneo hilo.
Huku nyuma,BBC,VoA,SKY NEWS.CNN n.k wanatangaza kwamba,Somalia na Ethiopia wanapigana kwa sababu ya Ogaden!
Mbumbumbu wa Tanzania wanasema,”Afrika Bara la Vita! Bara la Giza ,Magonjwa,na Machafuko!!”
Mabwana wa Vita wa Afrika(war lords) wanabebwa na mataifa haya ya Ulaya,na huwezi kuyaona mpaka uwe na macho matatu.
‘Satellites’ na ‘radar’ za Marekani za upelelezi zinategwa tangu Misri hadi Pakistan,zinaletwa upambe huu wa Afrika ili kukoleza vita,ili Urusi wapigwe waondoke!
Antonov-22 na Ilyushin-76 za Kirusi nazo zinajongea Upembe huo ili kubyesha mabomu makali kupambana na Marekani aliyekificha nyuma ya pazia,mgongoni mwa Msomali,katika vita baina ya Somalia na Ethiopia.
Yemen inatumika kama ‘depots’ za silaha za Mrusi.
Cuba nao wanaleta askari 15,000 toka Angola(Angola ilisaidiwa ikawa huru 1975) sasa CUBA anajitoa mhanga kupambana bega kwa bega na Mrusi ili kumzuia Marekani kutwaa Ogaden, mgongoni mwa Msomali!
General Vasily Petrov wa Urusi anaongoza mapambano huku, akina Vance nao wanachochea upande huu, basi Afrika inanuka riha ya baruti na risasi,kwa maslahi ya madola ya Ulaya!
Somalia inazidiwa,inaomba silaha Magharibi,vita ngumu Ogaden.
Shah wa Iran(alikuwa Kibaraka wa Marekani) anaonywa asije akapeleka silaha yoyote aliyopewa na Marekani katika nchi za Dunia ya Tatu,zisije zikatumika kumsaidia Ethiopia na Warusi,vita ngumu hii bwana!
White House, inatoa amri-hakuna kuuza silaha mEthiopia ili Ogaden itekwe na Msomali!
Ili Urafiki wa Marekani na Msomali upatikane! Naam, maslahi ya mataifa makubwa hupatikana kwa damu mbichi ya Mwafrika,Mwarabu,Mhindi ama Mhindi Mwekundu wa Bara la Kusini mwa Marekani.
Viongozi wa Kiarabu,tangu Sudan hadi Saudi Arabia wanaamrishwa na White House,kuisaidia Somalia, msaada MUHIMU wa silaha(a significant  military aid).
Lengo,ni ili Ukomunisti ushindwe Afrika. Hawa akina Brzezinski walishatengeneza Ukimwi mwaka huo wa 1975 ili kuwaua Waafrika,kuwapunguza ili wao wachukue mali kwa gharama yoyote, sasa wako Somalia.
Wanapoona Warusi na Wacuba wameingia wenyewe vitani,na vita vinamwelemea Msomali,wanaanza kutangaza mikataba ya kusimamisha utengenezaji wa silaha!
Wanaita kwa Kingereza, “Arms-limitation talks” ama Arms Limitation Treaty!
Sasa wanasema Mrusi akiendelea kuwasaidia Wahabeshi, basi mazungumzo hayo ya kupunguza silaha duniani yatakuwa hatarini kuvunjika!
Msomaji,sijui unaona unafiki huu wa Marekani! Kumbuka hii siyo hadithi ya Paukwa Pakawa! Ni ukweli kutokana na Historia.
Urafiki wa Marekani na Somalia unakuja kwa njia ya kuchochea vita Ogaden,Cuba nao wanaleta ‘artillery’ na MiGs zinanyesha mabomu tani nyingi,Wasomali wanapigwa wanakimbia nyuma milimani huko JIJIGA!
Damu ya Wasomali inabubujika kama mto,mvua ya mabomu inaendelea,wanakatwa vipande vipande kwa mabomu-maguruneti kwa uchochezi wa Kimarekani inayotaka kuikamata Somalia kwa gharama yoyote.
Majeruhi walikuwa maelfu.
Nataka ujue ugaidi wa Somalia ulianza lini?
 Kwa nini na kwa sababu gani?
Kumbuka,vita baina ya Somalia na Ethiopia vimechochewa na Rais Jimmy Carter ili ajifanye rafiki wa Somalia,kumzuia Mrusi kujitanua Upembe wa Afrika.
Hii kampeni iliitwa,  ‘THE SOMALIA’S OGADEN CAMPAIGN’ unaweza kufuatilia ujue ninachoandika hapa.Wajinga wanaposema,Wasomali wapenda vita!
 Jiulizeni nani yuko nyuma yao?
 Nani huwapa pesa na silaha? Ni Mwarabu? Mchina? Mzungu!!
Wamarekani wanapoona Msomali kachakazwa vikali,damu inavuja puani, wanaandika barua ya rangi ya njano na nyeusi kusema!
“Serikali ya Somalia itoe tamko, sisi(Marekani) tumeona katika vita hivyo vya Ogaden,kuna mkono wa Mrusi”,Barua ilisema.
Sasa eti ndiyo MAREKANI wanaona kwamba kuna Mrusi ameleta MiG-21 zipatazo 48, na kuna marubani wa Cuba wako mstari wa mbele kuisaidia Ethiopia, vifaru 150 vimetoka Msumbiji nchi nyingine ya siasa za Ki-Marx,sawa na Zimbabwe ya Robert Mugabe ambaye wanamchukia sana.
Hadi Iran kule ambako kuna mafuta ushawishi unaendelea wametoka akina Ahmadnejad,sasa utawala unajipendekeza Marekani. Ni Urusi,Marekani!
Wacuba wanafundisha Wayemen kutumia bunduki za Mrusi,akina Carlos The JACKAL walifunzwa ugaidi na wa Cuba,Warusi ili kupambana na ubeberu wa Kimarekani.Akina Osama walifundishwa ugaidi na Marekani ili kupambana na Ukomunisti walipovamia Afghanistan mwaka 1979!
Muktadha wa makala hii,ni ili msomaji ajue kwamba,Marekani na washirika wake  huwa hawana ‘Clear Policy’ kuhusu BARA LA AFRIKA.
White House na Kremlin huchochea vita hapa Barani;hufunza wanamgambo eneo hili lote kuanzia Somali,Urabuni,Bara Hindi hadi Pakistan na Afghanistan.
Hata Osama Bin Laden, alitokana na makambi ya kigaidi yalifofadhiliwa na Marekani,lengo likiwa kupambana na Urusi waliotaka kusimika Ukomunisti pindi walipovamia Kabul mwaka 1979.
Wanamwaga silaha na mabomu,wanachochea chuki;vita vinapouma wanaitana mkutanoni Ulaya ili kuitisha “ARMS-LIMITATION TALKS”
Waziri kama John Kerry anakwenda Moscow,inadaiwa wanajadili kumaliza vita,ama kuepusha vita Syria,Misri,Libya,IRAK nk.
“Negotiations” zinazofanywa na kutangazwa na vyombo vya habari vya Kimagharibi, si kitu bali uongo na Propaganda.
Wanataka kujitakasa dhidi ya lawama kwa kuwa vitanga vya mikono yao huchuruzika damu mbichi za Waafrika,Waarabu,Wahindi ama raia wa Ulimwengu wa Tatu! Kila mahali penye maslahi ya kisiasa na kiuchumi.
Vita ya Madola Makubwa ni “To conquer The Third World” ama kuutawala Ulimwengu wa Tatu,wa nchi changa,hasa zenye utajiri wa almasi,dhahabu,mafuta,gesi n.k
Wakiona Waafrika mnapukutika kwa vita,damu inamwagika,Putin na Obama wanaitana Moscow ama popote,wanakaa wanaambizana kupeana zabuni.