NELSON MANDELA MNARA WA KUMBUKUMBU
YA UHURU AFRIKA
Na Conges Mramba
Obama alipokuja Dar es salaam wakati
hakuwahi kusahau hujuma kama hizi na zile za Kanisa la Anglican, za kuwaweka
mhuri wa moto mgongoni Waafrika wenzetu waliofanywa watumwa-The Transafrica
Slave Trade-waliobandika mihuri ya “society”, migongoni!
Napenda kumwambia Barak Hussein
Onyango Obama,kwamba urais wake Marekani umekuja baada ya harakati za ukombozi
za akina Nelson Mandela, Malcolm
X,Martin Luther King Jr, na wenzao ambao walijikuta wakiuliwa na Pentagon ama
kufungwa maisha kwa uhaini.
Mandela sasa atalala kaburini,
lakini jina lake litabaki kama mnara wa
kumbukumbu ya mapambano ya Mtu Mweusi kutafuta Uhuru na Haki.
Wakati Obama anapojitia kushutumu
tawala za kiimla, Authoritarian regimes, asisahau kwamba serikali ya nchi yake
imekiuka haki za msingi za Weusi kwa kuwaunga mkono majambazi kama
Savimbi,majeshi ya Makaburu,Wareno na makampuni ya kifisadi kuihujumu Afrika.
Wakati ule,Marekani iliungana na
Makaburu wa Afrika Kusini kumsaka Tata Mandela kama gaidi,na ilihusika kuua na
kuhujumu harakati za ukombozi kwa kushirikiana na Shirika lake la Ujasusi,CIA.
Nigeria kwa mfano, inasemwa Boko
Haram wameua watu 1000 wakati ukweli ni kwamba hata makampuni ya mafuta ya
Magharibi kama Elf,Agip, Royal/Dutch Shell,Chevron n.k wamehujumu raia wa Niger
Delta,waliodai haki zao zama za utawala wa Dikteta Sani Abacha,ambaye wao
walibeba sana kwenye mbeleko hadi akawaua akina Ken Saro-Wiwa.
Makampuni ya Marekani,Ufaransa na
Uingereza yameua watu wangapi Kusini mwa Nigeria kulinganisha na Boko Haram?
Zaidi ya dola bilioni 400 za mafuta
zimeporwa na makampuni hayo tangu zama za uhuru hata sasa huko kwa
Waogoni,Igbo,(Biafra) na Yoruba.
Obama, anapozungumza utawala bora na
demokrasia ana maana gani kama makampuni ya Magharibi yanashiriki unyonyaji, na
dhuluma hapa Afrika.
Na yumkini Obama akaja Afrika wakati
Mandela akiwa tayari katika kitanda cha mauti. Urais wa Obama,ni matokeo ya
harakati za Mtu Mweusi kudai haki,vinginevyo asingekubaliwa kuwa Rais wa taifa
hili beberu sana duniani
RAIS BARACK Hussein
Onyango Obama, aliwasili katika miji ya Dakar,Johannesburg,Pretoria na Dar es
salaam, mwezi Julai Mandela akiwa anashindana na kifo katika kitanda cha Mauti,
MediClinic
Baadaye, akarejeshwa
nyumbani mjini Johannesburg ambako Desemba 5 mwaka huu 2013, saa 2:57 hivi
usiku akaaga Dunia huku familia yake ikimsindikiza kuzimu.
Afrika ilikuwa chini ya
ulinzi wa makachero wa Marekani,Obama alipotua katika ardhi ya Afrika,Julai
mwaka huu, Mandela alipolala usingizi usiojulikana mustakabali wake huko
Mediclinic.
Hatimaye sasa amefariki
dunia baada ya kuugua muda mrefu.
Ujio wa Obama,Afrika
naam,Afrika Kusini, Senegal na Tanzania kitovu cha harakati za Ukombozi wa Mtu
Mweusi, wakati huu wa mashaka ya kuishi au kufariki kwa Mandela, unatupa
kurejea historia.
HISTORIA YA MAPAMBANO YA
MTU MWEUSI imetamalaki tangu Bahari ya Hindi hadi Pwani ya Atlantiki.
Mzungu wa kwanza kufika
Rasi ya Tumaini Jema(Cape of Good Hope),Afrika ya Kusini, Bartholomew Diaz,mwaka
1485 ilikuwa ni katika safari za kwenda India
Muongo mmoja na ushee
hivi baadaye,(1497-98) alikuja Vasco Da Gama;hawa Wareno wakizunguka dunia ili
kujua ilivyoumbwa-huu ulikuwa mwanzo wa Utandawazi.
Ni wakati huo, Amerigo
Vespucci wa Italia alipofika Pwani ya Amerika Kusini mwaka 1497-99,Zama
hizo(1492-1502) ndipo Christopher Columbus wa Italia alipofika hasa Marekani na
kunakoitwa, West Indies.
Huu ndio wakati wageni
kutoka Ulaya walipoanza safari za kwenda Afrika ya Kusini ambako walisimika
tawala zao za kidhalimu kwa zaidi ya karne nne, hadi Mandela alipozaliwa Julai
18 mwaka 1918.
Nataka kueleza namna
Wazungu walivyofika Afrika na kuanzisha tawala za kidhalimu,kisha wakachukua
ndugu zetu kuwa watumwa Marekani, ambako pia walitawala kabla ya Marekani kupata
uhuru Juni 4,mwaka 1776.
Mandela, ameishi kwa
taabu na wapigania uhuru wenzake wakijificha-ficha wasiuliwe ama kukumbana na
kifungo cha maisha jela.
Rais wa kwanza Mzungu
katika Bara la Afrika, FW De Clerk ,alizaliwa Machi 18,mwaka 1936 mjini Johannesburg,wakati
tayari Mandela akiwa katika madhila ya ukoloni,Afrika ya Kusini.Huyu De Clerk,
ndiye aliyekuja kumwacha huru Mandela Feburuari 11,mwaka 1990.
Mandela ameachwa na
mkewe kufuatia harakati za kujificha-ficha asikamatwe,hakufika nyumbani muda
mrefu, na laifukuzwa Chuo Kikuu cha Port Hare kwa kosa la kujihusisha na migomo
huko Transkei.
Alijisomea nyumbani
akatunukiwa shahada ya kwanza,BA.
Alitiwa mbaroni
1952,1956,1962 na 1964 akafungwa kifungo cha maisha gerezani.
Wakati Mandela anafungwa
huko Afrika Kusini,Mtu Mweusi(Negros) hakuwa na ruhusa kuoa Mzungu katika
majimbo 19 ya Marekani,na Afrika Kusini ilikuwa Mzungu akikukuta ndani ya basi
umeketi,unampisha kiti!
Naam, ni wakati huu
kulikuwa na Mitaa na mahoteli Mweusi huwezi kukanyaga,inaandikwa mlangoni, ‘For
Whites Only’!
Marekani na Afrika ya
Kusini zilifikiwa na wapelelezi(explorers) wakati mmoja,zikajikuta makoloni ya
wageni,wakati Marekani inapata Uhuru mwaka 1776 kutoka Uingereza Afrika Kusini
ilibaki chini ya makucha ya Waingereza, na baadaye Makaburu wabaguzi wa rangi.
Rais Barack Hussein
Onyango Obama, anatua Afrika Kusini wakati Mandela roho yake inapokuwa
ikishindana na malaika wa kifo huko MediClinic; akiwa anapumulia mashine.
Obama, amezaliwa Agosti
4, mwaka 1961 wakati harakati za Uhuru zikiwa zimepamba moto duniani.
Ubaguzi wa rangi ukiwa
umepamba moto hata Marekani kwenyewe, ni wakati huu huu mamaye Obama,Ann
alipokuja kutengana na Hussein Onyango Obama,akaolewa Indonesia akaishi
Jakarta.
Nataka kusema kwamba,
huyu mamaye Obama, alipata msuko-suko kuolewa na ‘Mjaluo’ wa Kenya-Afrika,
akaondolewa chuoni alipopata ujauzito wa Obama, mama huyo akiwa na umri wa
miaka 18!Alionja madhila ya ubaguzi wanaoshuhudia akina Eto'o siku hizi!
Hizi ndizo zama akina
Martin Luther King Jr, walipowindwa mithili ya nguruwe pori, walipinga ubaguzi
wa rangi kabla ya kuuliwa na Pentagon mwaka 1968.
Obama,huyu aliyeko Dar
es salaam sasa, alizaliwa Honolulu huko Hawaii na mama Ann Dunham,mzaliwa wa
Wichita, Kansas.
Kwa mara ya mwisho Obama
alikutana na Mandela mwaka 2005 alipokuwa angali Seneta; na safari hii
alitarajia kukutana na Mandela akiwa Rais wa Taifa baguzi la rangi…
Bahati mbaya,Mandela yu
kimya kitanda cha mauti; kauli haitokei tena kumwambia Obama, “The change has
Come to America! The change must come to Africa!!” Hata kama Obama
atahudhuria mazishi.
Hussein Onyango Obama,
aliachana na Ann, Barack akiwa na miaka miwili,sababu ni mbinyo na ubaguzi wa
rangi,wakati huo akina Martin Luther King Jr,Malcom X na wenzao sheria
ziliwapiga marufuku kumuoa Mzungu.
Naam, Obama na
bintize,Malia na Sasha, ni Weusi wenye damu halisi ya Afrika,wakati huu
wanapokuwa nyumbani Afrika.
Obama, kasoma
Indonesia,kasha Honolulu kabla ya kusoma vyuo vikuu vya Columbia na
Harvard,chini ya usaidizi wa mamaye na nyanyaye, Madelyn Dunham.
Huyu nyanya alikufa
wakati Obama akifanya kampeni mwaka 2008.Ilikuwa Novemba 3,mwaka 2008.
Mkewe Obama, Michelle,
ni binti wa Fraser na Mariam Robinson,mabaki ya watumwa ndugu zetu waliopelekwa
Marekani kulima miwa katika mashamba ya Mzungu.
Hawa ndugu zetu-Obama na
Michele-wametua Dakar,Johannesburg,Pretoria na Dar ili kukumbuka nyumbani
takriban miezi sita iliyopita.
Obama alikusudia kuzulu
kisiwa cha Robben alikofungwa Mandela kwa miaka 18, alizaliwa Julai 18 mwaka
1918, akafungwa Robben kwa miaka 18, na De Clerk aliyemwachia huru alizaliwa
Machi 18,mwaka 1936.
Obama alifika
Robben.Naam mahali ambako patabaki kama kumbukumbu ya utumwa na ukoloni Afrika.
Mandela, amefungwa jumla
ya miaka 27;zamani kisiwa cha Robben kilitengwa kwa sababu ilikuwa ni koloni la
wakoma-Leper colony.
Kwa takriban miaka
30,utawala wa Makaburu uliwafunga maelfu ya Waafrika Weusi waliopinga ubaguzi
wa rangi mahali hapa.
Mwaka 1987(miaka mitano
baada ya Mandela kuhamishwa kutoka kisiwani hapo kwenda Bara) eneo hilo
liligeuzwa Kivutio kikuu cha utalii.
Mandela alifungwa Robben
miaka 18; eneo ambalo Obama huenda amefika,ili kukagua mateso ya Mtu Mweusi-Mandela
na wenzake- ndiyo akina Walter Sisulu, Goven Mbeki, na viongozi wengine wa
African National Congress(ANC) na Robert Sobukwe wa Pan Africanist Congress.
Wafungwa
hawa,Mandela,Mbeki,Sisulu na wenzao waliponda kokoto bila viatu mchana wa
hari-vumbi liliishia kifuani Mandela akaugua kifua.Asskari walinzi wa gereza
waliwakojolea puani,wakati mwingine walilazimishwa kuoga maji ya baridi.
Jela ya Robben ilikuwa
na vitanda 600;mahali ambapo hata baada ya mauti kumkumba ‘TATA’Mandela,itabaki
kumbukumbu ya mateso ya mtu Mweusi wakati wa madhila ya ukoloni na ubaguzi wa
rangi.
Waziri wa Sheria wa
Makaburu, Cobie Coetsee, akahamuru akaina Mandela wahamishwe,wawachie ndege
makazi.Kumbuka lilikuwa eneo la kutupwa wakoma,hakuna aliyeishi maeneo haya.
Siku hizi,kunajengwa
mahoteli ya fahari na ni kituo cha utalii-a world class attraction!
Obama,Michelle,Malian na Sasha, wanafurahi kukanyaga alipofungwa ‘Tata’Mandela.
Lilikuwa eneo la kuzika
wakoma,katika selo nambari 30 B katika chumba kidogo cha mita 2 kwa 2 ndipo
alipolala mtu huyu mwenye urefu wa mita 2.
Alijifunika shuka la
kijivu na blanketila sufu rangi ya kahawia, taulo la samawati.
Gazeti la TIME la Julai
1991,LILIMKARIRI Brigedia Erika Van Zyl, Ofisa Uhusiano wa gereza hilo
akiwakaribisha watalii mahali hapo na kusema mahali hapo ni ‘A world class
attraction!
Zama za utawala wa
Makaburu,hapa palikuwa The Worst Part of Imprisonment!
Hata hivyo, Mwandishi,
Scot Mac Leod, aliandika katika gazeti hilo la TIME,Julai 22 mwaka 1991,mwaka
mmoja baada ya Mandela kuachiwa huru na de Clerk,kwamba Brigedia Erika van
Zyl,aliwakaribisha mahali hapo Robben, alikofungwa Mandela.
Bila shaka,hata kaburi
la Mandela litageuka ‘Tourist Site’ maarufu hapa Afrika na dunia nzima.
Hakika,Mandela ameishi
duniani bila raha na amani,sasa akifariki atazikwa katika kisiwa cha amani ya
milele.
Kwa Obama, kitabu cha
‘Dream from my Father’ kilichoandikwa na wakati babaye anarejea Kenya, ni
kumbukumbu tosha Obama kutomsahau Mandela,Nyerere,Samora Machel,Kwame Nkrumah
na wenzao, zama za harakati za Mtu Mweusi, akina Martin Luther King Jr, naam
akina Malcolm X.
Obama, amekuwa rais wa
taifa beberu lililounga mkono ubaguzi wa rangi akiwa na umri wa miaka 47, na
sasa anapokuwa Dar atambue msingi wa Urais wake ni Mandela,Nyerere,Kwame
Nkrumah,Patrice Emery Lumumba,Martin Luther King Jr, mama Coletha King na
wenzao mashujaa wa kupinga ubeberu na ubaguzi wa rangi.
“The change has come to
America; and it must come to Africa too!
Buriani tata
MANDELA,Mfungwa maarufu kuliko wote duniani aliyegeuka Shujaa kuliko wote
duniani, amelala kitanda cha mauti,lakini atakuwa hai milele kwa ‘legacy’
yake
0786 324 074/0713 324
074
Buriani Mandela!
0713 324 074