Monday, July 4, 2011

UMOJA WA AFRIKA UMEBINAFSISHA WAJIBU WAKE NATO?




   KULINGANA na Agano la kale, katika Bablia Takatifu, Amani ni baraka anazopewa mtu,baada ya kutii maagizo ya Mungu ama sheria zake(Kumukumbu la Torati sura nzima ya 28).
   Kwanza,tufahamu; Amani ni kitu gani?
Amani ni nini na hutoka wapi?
Chimbuko la Amani, ni wapi?
  Kwa Kigiriki, neno hili Amani ni ‘eirene’ maana yake, hali ya kumalizika kwa vita, ama hali ya kutokuwepo vita na uadui.
   Kwa Kiebrania, Amani ni ‘Shalom’ au hata waweza kuita Salem.Mji wa Yerusalem(Yeroo-shalayim) maana yake ni mji wa amani. Hata Dar es salaam, maana yake ni Bandari ya salama; ya amani.
   Amani, huanzia katika nafsi ya mtu mmoja mmoja, na inahusisha na uhusiano wa mtu na watu wanaomzunguka. Uhusiano huu ukiwa mzuri huiambukiza jamii na taifa zima, na hata mataifa mengine yote kwa pamoja hupata amani. Mtu mmoja anapokosa amani, matokeo yake ama athari zake huwapata hata wengine.
   Kukosekana amani Burundi, Congo(DRC),Somali,Libya ama Rwanda,kutayafanya mataifa mengi ya dunia kuathiriwa,ama na wakimbizi,kubanda kwa bei za mafuta,uchumi kuwa mgumu n.k
   Kwa sababu hiyo,kuna tafsiri(definition) nyingi za neno amani:
    Uzima,ukamilifu wa kimwili,kiroho,kiakili na ustawi na utangamano miongoni mwa jamii. Hii ni tafsiri ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa(WHO) ya mwaka 1947.
 Kulingana na Kumbukumbu la Torati,sura nzima ya 28,Amani ni kufanikiwa kimwili,kiroho,kiakili na kutokuwa dhaifu ama mhitaji katika neno lolote. Kwa Kiingereza,ukamilifu huu unaweza kuitwa “Completeness”, ama “Wholeness” au “Wholesomeness”.
    Kwa sababu hii, amani haiwezi kuwa hali ya kutokuwepo vita(absence of war) peke yake; ni pamoja na usalama wa chakula,uchumi mzuri, utangamano na uhusiano mzuri wa raia katika taifa lao na katika mataifa yote ya dunia,uchumi mzuri, mazingira yawe mazuri na rafiki,na kusiwepo na dhiki,shida na taabu kama mgawo wa siku hizi wa umeme.
   Amani ni mlango wa kuingilia katika mambo yote mema-fanaka. Hata watu wanaohitilafiana na matakwa ya Mungu:Usiue,usinyang’anye mke wa mwenzako, usiibe na usiwe fisadi,uwe mtiifu,mwadilifu na mzalendo kwa taifa lako na kwa wenzako n.k,hawana amani,na huwasababisha raia wenzao kukosa amani.
  Mungu, amejitaja kwamba yeye ni Upendo(Agape),Mtu asiye na upendo kwa jirani zake, ndiyo raia wenzake hata wanaomsema vibaya,hana amani moyoni mwake nakatika mazingira yake pia.
 Maishani, huwezi kuwa na furaha na usalama kama una njaa na maradhi-unakosa amani, utaona kwamba, dhana ya kutokuwepo vita(conflict) migawanyiko katika familia na hata mapigano, haiwezi kuwapo amani.
 Kusigana kwa mawazo, magomvi,maandamano,migomo ya wafanyakazi,uchumi mbaya,maisha magumu,njaa,kuvunjika kwa ndoa na watoto wa mitaani,ni dalili za wazi kwamba nchi ama dunia haina amani. Amani ni kinyume cha laana.MAMBO YOTE MABAYA kwa wanadamu.
 Mathayo 10:34 Yesu alisema kwamba, neno tu laweza kuleta vita,migawanyiko katika familia nahata mapigano ya silaha. Kusigana kwa mawazo,migomo na maandamano,kutokuelewana ama kukubaliana,huleta chanzo cha kukosekana amani.
  Mtu mmoja aliwahi kusema, “Amani huanzia kwako”.
   Mtazamo wako chanya(mzuri) kwa jirani zako,kwa taifa lako kwa raia wenzako, huleta amani. Mtazamo hasi(mbaya,masengenyo,chuki,uzushi,majungu,fitina n.k) huleta kinyume cha amani,yaani laana kwa taifa zima. Haya yote huanzisha vita vya silaha.
 Vita vya kugombea madaraka(strife for supremacy),kulipa visasi na ubeberu dhidi ya raia,huipeleka nchi pasipo na amani,yaani vitani. Vita ni chimbuko la maradhi,njaa, wakimbizi,umasikini,vifo,mambo yote mabaya hupingana na amani ya kweli.
 Amani ndiyo chimbuko la maendeleo ya watu,wanyama, wadudu ,ndege na viumbe wengine,na mazingira huwa bora sana.
 Chama cha Mapinduzi(CCM)husema Tanzania kuna utulivu(Tranquility) yaani kuna ukimya, ama kutokuwepo na makelele,fujo,magomvi n.k Utulivu siyo amani kamili. Na kutokuwepo na vita,hakuwezi kuitwa amani,ikiwa myoyo ya watu ina uchungu,majuto,masikitiko,dhiki,taabu na wana maradhi yasiyotibiwa,na hawana matumaini-hii siyo amani, japo kuwa wanagugumia kwa maumivu makali,bila kupigana-utulivu!
  Amani,ni hali ya kutokuwa na fikra hasi,ni uhuru kutoka hali ya vita,ni uhusiano mzuri katika jamii,miongoni mwa mataifa, uhusiano mwema baina ya mataifa ya dunia,na hali ya kutokuwepo kitisho cha vita,njaa,magombano na maradhi ya kufisha.Maendeleo huletwa na amani.
  Amani na afya njema ni hazina nahitaji la msingi kulinganisha na mahitaji yote.Watu huogopa sana vita na kukosekana usalama,lakini hata maradhi mabaya na afya mbaya,ni kukosekana kwa amani.
  Kisiasa, amani eti inaweza kuletwa kwa mtutu wa bunduki! Ndivyo tuonavyo siku hizi,Ufaransa na Marekani chini ya mwavuli wao NATO wanashiriki kuleta amani Libya kwa njia yam tutu wa bunduki, ili kumwondosha Kanali Muammar a- Gaddafi!
  Umoja wa Mataifa,kuna Baraza linaloitwa la Usalama(UN security Council) lenye kuundwa na mataifa 15.
   Mataifa matano:Uingereza, Ufaransa, Uchina, Urusi na Marekani ni wanachama wa kudumu wa Baraza hili lenye jukumu la kuleya amani duniani.
 Hata hivyo, nchi tano pekee hata ziwe na maguvu ya kijeshi kiasi gani aslani,haziwezi kuleta amani duniani. Hizi ndizo nchi zinazoongoza kuvuruga amani ya dunia.
 Ufaransa na Marekani,ndiyo wanaowapa WAASI wa Benghazi, Libya silaha ili kumpindua Kanali Muammar al-Gaddafi,eti kwa sababu utawala wake wa tangu mwaka 1969 umeondoa AMANI katika nchi hiyo, na hakuna demokrasia,haki za binadamu!
  Sijui,kwa Waingereza, Wafaransa na Wamarekani na washirika wao wa NATO, NENO AMANI TAFSIRI YAKE NI VISASI NA VITA DHIDI YA VITA?
 Pasipo shaka, kwa hawa mataifa babe duniani, amani maana yake ni vita, ni kugawa silaha kwa raia wa Libya ili wapigane wa kwa wao eti ili kumwondoa Gaddafi na kutatua matatizo yao!!
 Naam, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, huundwa pia na mataifa 10 yanayochaguliwa kila baada ya muda Fulani, na muda huo ukiisha,mataifa hayo 10 “ya kuja” huondoka kuyapisha mengine,tena na tena.
 Kwa sababu hiyo, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina wanachama wan chi 15;kati yao Urusi,Uingereza, China, Marekani na Ufaransa ni wanachama wa kudumu, wana maamuzi mazito-wanafanya kadiri wapendavyo,wanatumia silaha kuzishambulia nchi nyingine kijeshi,kwa madai kuwa hakuna amani,demokrasia na haki za binadamu huko.
 Je, vita vya silaha vinaweza kuleta amani kusiko na amani,uhuru na demokrasia?Hakuna majadiliano halafu vikwazo vya kiuchumi ama kizuizi cha kufanya biashara na kunyimwa misaada na mengine yanayopunguza vifo na uharibifu huletwao na vita vya silaha?
  Sheria za Umoja wa Mataifa(UN) zinataka,kabla mwanachama mmoja hajashambuliwa kijeshi,lazima kujadiliana naye,halafu asiposikia atengwe kisiasa na kiuchumi.
 Lakini, utaona Marekani na nchi za Ulaya, zilizowahi kutugeuza sisi watumwa wao, wanatoka kuishambulia nchi yoyote adui yao,bila kibali la Umoja wa Mataifa(UN).
  Kuna nchi 192 wanachama wa Umoja wa Mataifa. Kuna harakati za UN Kutuliza vita mahali pengi duniani. Kuna mashirika tele na vikosi tele vya Umoja wa Mataifa vya kulinda amani duniani, UNIKOM, unmibh,minurso,unifil,unmik,monuc,unmogip,unomig,unamsil n.k
 Kuna mahakama Kuu ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia uhalifu wa kivita. Mahakama hii ina mwanachama mmoja tu-Uholanzi, mjini The Hague.
 Kuna majaji 15 huko mjini The Hague wanaoshughulikia kesi za uhalifu na tumeona juzi hapa Mwendesha Mashitaka wa           Mahakama hii,Louis Mareno-Ocampo wa Buenos Aires, Argentina, akiwaita watuhumiwa sita wa mapigano ya Kenya ya Desemba, 2007, “The Ocampo Six” wakiitwa kujibu mashitaka mjini Hague.
 Tumesikia hata akina Charles Taylor,Slobodan Milosevic na wengine wakiwa wamekamatwa na kushikiliwa Hague. Tumesikia   Kanali Gaddafi tayari imetolewa waranti ya kumkamata yeye,mwanaye na mkuu wake wa ujasusi wakamatwe.
 Ilishatolewa waranti Omar Hassan Al Bashir wa Sudan ya Kaskazini naye akamatwe. Fodday,Sankoh, Joseph Kony,Hitler na watu wa kariba hii ni wakushitakiwa,kwa sababu wanakiuka haki za binadamu-wanaua watu,kuua ni kumnyima mtu haki ya kuishi,kila mtu ana haki ya kuishi.
  Sasa,msomaji, jiulize. Huko Libya,NATO inafanya nini? Ufaransa,inapogawa silaha kwa waasi wa Libya wanataka kufanyike nini kama siyo mauaji makubwa?
 Je, kwa kugawa silaha kwa waasi wa Libya, NATO,Marekani na Ufaransa hawaoni kwamba wanashiriki kupora maisha hata ya raia wasio na hatia Libya?
  Wao tayari ni Mahakama? Tayari wamefungua mashitaka Hague dhidi ya Gaddafi,lakini wanatafuta kumuua-wameshamhukumu kifo hata kabla ya kujitetea!
 Wao ni polisi,mahakama,mgambo na wanyongaji kwa wakati mmoja, hii ndiyo amani?
  Marekani, Benge la Congress limeshituka,Rais Obama kupeleka jeshi Libya bila idhini ya bunge,huu ungekuwa ushahidi kwa UN kumtia mbaroni Rais Barack Obama kwa kukiuka sheria za Umoja wa Mataifa na kuiingilia Libya kijeshi.
 Lakini,nani amfunge paka kengele?Waranti zinasainiwa wakamatwe akina Gaddafi, Al Bashir, Paul Kagame, The Ocampo Six, Fodday ‘Poppay’ Sankoh,Tayloy n.k
 Hakuna wa kunyooshea kidole Ufaransa,Uingereza na Marekani wala NATO! Kuivamia Libya ni sawa tu eti ni kulinda amani. Huu ndiyo Umoja wa Mataifa; na huku eti ni kulinda amani!
 Marekani kuwaunga mkono waasi wa Libya kuna tofauti gani na kumpa silaha Joseph Kony au Fodday Sankoh, Jonas Savimbi, Hitler, Idi Amin n.k kuua watu?
  Eti, Fodday Sankoh akakamatwa na kupelekwa mjini Hague kujibu mashitaka yak u ‘abuse human rights’ huko Sierra leone 1999-2000 Marekani na Ufaransa wakabaki.
 Marekani wanapomshitaki Charles Taylor kuwaunga mkono waasi wa RUF huko Sierra LEONE, wao wanawaunga mkono waasi wa Benghazi,Libya wanawapa silaha,wanawalea,Ufaransa inawaletea kila kitu,NATO wanawasaidia kupiga mabomu kwa ndege-mkuki wa nguruwe?
  Hii ni ‘double standadrs’ mwingine akifanya kosa lile anafungwa,wao wakifanya ni kosa takatifu!
  Afrika, haina veto power katika Umoja wa Mataifa wala katika Baraza la Usalama. Afrika kuna watu bilioni moja,lakini ulaya yenye watu wachache tu wana veto, wana ‘gutsy’ uwezo mtukufu wa kuingilia masuala ya Afrika,kupigana vita huku,kuua raia kwa makombora ya madege,na kuingilia masuala ya Afrika,bila Umoja wa Afrika(AU) kusema!
  Itaendelea
   congesdaima@yahoo.com
 0786 324 074
  
  
 

 

No comments:

Post a Comment