Monday, January 30, 2012

Dola ipi ya Kiislam itazishinda Ulaya na Marekani?


 
*Saddam, Gaddafi, Osama wameuliwa, sembuse ma-Ayatollah wa Iran?
* Carlos The Jackal alishafungwa jela Ufaransa kwa ‘uzalendo’ wa kuwapinga mabeberu
*Hugo Chavez, Mugabe,Fidel Castro na wenzao waliowapinga Wazungu wamezeeka, falme za Kiarabu za Misri, Yemen,Tunisia, Sysia, nazo  hoi
 
OTTOMAN EMPIRE, ni dola la Kituruki lililokaribia kuitawala Dunia, lilitamalaki Afrika Kaskazini, Asia na Ulaya.
  
Ndiyo dola ya Kiislam iliyoinuka kwa nguvu nyingi na kuzikalia nchi zilizkuwa milki ya Wakristo, zikiwemo zile za Ulaya kwa takriban miaka 150. Tunajua hata Misri ilikuwa nchi ya Wakristo, ila ikatekwa katika karne ya 12 hivi.
 Afrika Kaskazini, ilitekwa na Uislam na falme zake nyingi ziliangushwa kwa ‘Majambia’ ya Waarabu,yaliyong’ata mithili ya mikia ya nge wenye sumu(scorpion stings) zama hizo za vita vya kuwatoa kamasi Wakristo waliokengeuka na kuanza ngula nyama za nguruwe huku wakiabudu sanamu na kutambikia mizimu.
  Dola hii ya Uislam, maarufu sana kama, “Ottoman Empire” ama dola ya Othman, ilikoma Agosti 11 mwaka 1840 AD, kwa hiari yao wenyewe, wakawaachia Wakristo wa Ulaya na Washirika wao(Allied Powers of Europe) wakaukalia mji mkuu wa dola hii wa Constantinople.
Ottoman waliinuka mnamo karne moja na nusu baada ya kifo cha Mtume Mohammed ASW, mwaka 632 AD. Hadi mwaka 1453Waislam hawa(Saracens) walioupinga kwa ‘Jihad’Ukristo(Crusades)ilishapoteza mwelekeo wake wa kuitawala Mashariki mwa iliyokuwa dola ya Rumi-The Roman Empire.
Mapigano baina ya Ukristo uliokengeuka na kumwacha Mungu na Mabedui wa Kiarabu,yalitabiriwa na Mtume Yohana katika Ufunuo wa Yohana 9:1-11.
Ushindi wa vikosi vya wanamgambo wa Kiarabu wenye majambia, waliopanda farasi huko jangwani, ulitabiriwa kuendelea kwa jumla ya miezi mitano ya kiunabii, ambayo ina jumla ya siku 150 ukichukulia ukweli kwamba Kalenda ya kale mwezi mmoja ulikuwa na siku 30 tu.
Miezi mitano ya unabii(Ufunuo 9:5,10) hivyo vikosi vya wapanda farasi vya Waarabu waliotumia majambia makali(mikia ya nge) viliwashambulia Wakristo walioacha imani(kukosa mhuri wa Mungu) na kuanza kuabudu masanamu waliyoyaleta hata makanisani, wakala nyama za nguruwe na kufuata ibada za miungu.(Tazama Ufunuo 9:4)  Walishikishwa adabu kwa ruhusa ya Mungu mwenyewe.
Kulingana na unabii wa Biblia, siku moja ya kiunabii ni sawa na mwaka mmoja(Ezekieli 4:6, na Hesabu 14:34). Kwa sababu hiyo, unabii unashabihiana na Historia kwamba dola ya Ottoman ilikoma baada ya miaka 150.
Leo,Uturuki ilikokuwa hiyo dola ya Ottoman, ilishajifutika yenyewe chini ya mvungu wa miguu ya Umoja wa Kujihami Ulaya Magharibi(NATO) ambao wakigeuza ubavu wanaitwa Soko la Pamoja la Ulaya(European Common Market). Kuna mbio nyingi za mataifa yaliyoupinga ubeberu wa Magharibi sasa kujiunga NATO na Umoja wa Ulaya(EU).
Dola nyingine za kale sana duniani ni Babeli,uliojengwa na Nimrodi(Mwanzo10:8-10). Mnara wa Babeli ulikuwa na kimo cha futi 75 hivi, wakati kulikuwa na hekalu la kuabudia miungu lenye kimo cha futi 600 kwenda angani.
Babeli inayosimuliwa katika kitabu cha Danieli zama za Dikteta Nebuchadnezzar, ilitawala dunia mwaka 606 BC.
Umedi na Uajemi(leo Iran)ilitawala dunia kuanzia mwaka 536 BCbaada ya kuishinda Babeli.
Tutajadili hapa chini, kama Iran ya sasa chini ya ma-Ayatollah na Mujahidina kama Mahmoud Ahmadnejad, wanaweza kuzishinda dola za Magharibi, ambazo zinajiandaa kuishambulia Iran hii kwa kitisho cha Nyuklia!
 Iskanda(Alexander) Mkuu wa Ugiriki, aliwashinda Wamedi na Waperizi ama Waajemi hawa wa Iran ya sasa kati ya mwaka 336 na 323 BC akatawala milki yoote ya hawa. Ugiriki ya sasa imesalia nchi ndogo ya vilima,wakazi wake ni wavuvi masikini tu ambao nao wako European Common Market.
 Ugiriki ingali  inakumbukwa kwa kuasisi michezo kama Olimpiki itakayochezwa mwaka huu mjini London, mwezi Juni.Wanakumbukwa kwa kuanzisha mbio za Marathon, na maarifa ya sayansi,kasha kwa wana falsafa wake mahiri kama Plato, Aristotle na Socrates.
Warumi waliwashinda Wagiriki kuanzia mwaka 168 BC.
  Na eneo lote hili ambalo lilikuwa milki ya Rumi leo ndilo European Union na Soko la Pamoja(Common Market) nchi hizi zimeungana na Marekani; milki hii inatanuka kuelekea Mashariki kulikokuwa na milki za Waarabu wa Ottoman.
 Rumi inakumbukwa kwa watawala wake kama Kaisari Gaius Julius Ceasar aliyechaguliwa kutawala Rumi BC 46, Augustus, Tiberius na Claudius. Hawa wapo katika Biblia.Yesu alizaliwa wakati wa Kaisari Tiberius ama Tiberio aliyetoa amri ya sensa, na alianza kutawala AD 14.
Dola ya Rumi ilishambuliwa na kuvunjwa kabisa ikatawanyika katika vipande vidogo ambavyo ni nchi kubwa za Ulaya siku hizi. Hizi ni nchi 10.
Mamlaka ya Rumi yalirithiwa na Upapa(Papacy Power) huu Upapa ulipigana vita na kuzing’oa falme zifuatazo huko Ulaya.
Vandali(mwaka AD 454), Heruli (AD 493) na Ostrogoths(AD 538), huu ndiyo mwaka Upapa ulianza kuitawala dunia rasmi. Ulikuja kukoma Feburuali 10 mwaka 1798 wakati Jenerali wa Kifaransa, Berthier, alipomtia mbaroni Papa, akamfunga jela ambako alifia.
 Mwaka 1929 Mussolini alitiliana saini mkataba(Literan treaty) ambao ni makubaliano ya kisiasa kwamba sasa mji wa Vatican ingekuwa taifa jipya huru duniani, na mtawala wake angekuwa Baba Mtakatifu-Papa.
Nimeleta kisa hiki hapa, kuwajibu wasomaji wangu Waislam wanaoniuliza kila mara, ‘Kwa nini Papa apigiwe mizinga 21 anapozuru nchi mbalimbali? Kwanini awe na mabalozi? Kwa nini  VATICAN wawe na kiti Umoja wa Mataifa; wakati Waislam hawana?”
 
Mussolini ndiye aliyempa Papa nchi ya Vatican yenye ukubwa wa kama ekari 100.7 hivi; na ni miongoni mwa nchi ndogo sana hapa duniani.
Ni huyu Mussolini aliyeponya ‘donda la mauti’ ama “Jeraha la Mauti” la miaka mingi, Vatican ukawa mamlaka takatifu inayotawaliwa na Papa ambaye pia ni kiongozi wa Katoliki duniani-Papa, ni kiongozi wa dini na siasa.
Ulikuwa mwaka huo wa 1929, Papa Gaspari na Mussolini walipotiliana saini mkataba huo wa kuliponya donda la miaka mingi(Tazama Ufunuo wa Yohana 13:3,12). Kulingana na Biblia,’Mnyama’ siyo mtu,bali ni mamlaka ama falme(Danieli 7:23) Tunajadili falme na mamlaka za dunia. Tangu zama zile hadi leo, tunatafuta kujua yajayo baada ya sasa.
 Nataka kusema kwamba, mapinduzi yaliyoanza mwaka jana huko Tunisia,Misri,Libya na sasa Yemen na vuguvugu limepamba moto Syria na hata Iran ili kuziangusha dola za Uislam wenye itikadi kali duniani, ni kutafuta mabaki ya Ukomunisti, yaani Uislam(nitajadili hili katika makala zitakazofuatia,kwa sababu hata Illich Ramirez Sanchez yaani Carlos The Jackal amegusia hili)
 Uislam, ulianzishwa na Mtume Muhammad AWS, kati ya mwaka 622 AD na ukapinga kwa nguvu Ukristo wa kifisadi(kuacha Amri 10 za Mungu)na ubeberu, baadaye vita hivyo vya Jihad vimetafsiriwa ‘ugaidi’ kwa sababu vinanyang’anya watu maisha.
  Vita vya kigaidi havina tofauti kubwa na mapambano ya kudai uhuru ama haki Fulani,kama nitakavyobainisha baadaye katika makala hii kama alivyosema Carlos The Jackal anayetumikia kifungo cha maisha huko Ufaransa.
                  
 Saddam, Gaddafi na Osama wamekufa ili kutimiza Unabii wa Biblia
 
Kuanguka kwa Saddam Hussein huko Irak(Babeli ya zamani)mwaka 2003 na kasha kunyongwa kwa kamba nene shingoni usiku wa kuamkia Jumamosi, Desemba 30 mwaka 2006 huko Baghdad, na kuangushwa kasha kuuawa kwa Muammar al-Gaddafi huko Sirte,Libya Alhamisi, Oktoba 20 mwaka 2011 ni dalili za wazi kwamba dola za Waislam
  Kuanguka kwa dola za Mashariki dhidi ya Marekani na Washirika wake wa Ulaya ni kutimia kwa unabii kwamba sasa mataifa haya ya Magharibi yanainuka kuitawala dunia kwa pamoja, na yatanena na kutenda kama shetani(Ufunuo 13:11-18).
   Ottoma walisalimisha mamlaka yake NATO, na mataifa haya hususan Uturuki yamejiunga Nato, juma la jana nilimwona Mfalme wa Jordan akiwa katinga suti safi nyeusi jijini Washington,pale ikulu ya White House, alipokutana na Rais Barack Obama. Sijui kwa nini televisheni hazikumwonyesha vizuri, wapo pia wafalme wa Saudia, Falme za Kiarabu na wengi wengine, na hawaipendi Iran ili kujikosha kwa Marekani na washirika wake wa Ulaya.
 Huu Umoja wa Ulaya(EU) na Soko lake la Pamoja, Common Market, na kwa kutumia nguvu za kijeshi NATO, wanajiandaa kutunga sheria kali(kuondoa demokrasia) kwa kutunga sheria kali-NEW WORLD ORDER-ili mtu au nchi itakayojifaragua kuwapinga, wawekewe vikwazo vya kiuchumi(Ufunuo 13:14-18).
 Kwa kutumia ushawishi hata wa Freemasons, watauteka uchumi wa dunia na kuvuruga chumi za mataifa yote mengine na kuwalazimisha kuabudu dini wanayotaka wao, Mungu wanayemtaka wao(zaidi sana teknolojia,sayansi na mizimu) watakaogoma watawekewa vikwazo vya uchumi ili wasiuze wala kununua.
 Iran iko mbioni kuwekewa vikwazo vya uchumi ili wasiuze mafuta yao Ulaya na Marekani,kwa sababu eti wanashupaza shingo kurutubisha Uranium.
 Kumbuka dola ya Afghanistan ya kina Mullah Muhammad Omar ilishapinduliwa kitambo. Katika toleo lijalo nitajadili kuhusu Iran halafu nitazungumzia habari za Carlos The Jackal na Uislam.
   0786 324 074
 
 

Sababu za vifo vya Saddam,Gaddafi na Osama



UNABII WA BIBLIA umetwambia namna dola za Kiislam zinavyojisalimisha zenyewe kwa adui zake, Mabeberu wa Magharibi, ili kuwarahisishia kutangaza ile Amri ya kuunganisha dini zote duniani-New World Order.
Gideon M. amekuwa akijadili jambo hili kila mara, name ninataka kuonesha kwamba mfumo wa kuunganisha Uislam,Ukristo,Umizimu n.k  kwa kuwatumia hao Freemason,leo ni kitu cha wazi sana, na tunaichambua Historia kwa kulinganisha na Unabii wa Biblia Takatifu.
Tuijadili kidogo Iran, kama itanusurika kupinduliwa na Ulaya na Marekani; ama kama itajisalimisha yenyewe, midhani milki zi Kiislam leo zinagongana zenyewe kujisalimisha Washington,London,Paris na Vatican City.
Washirika wa Ulaya na Marekani, Freemasons wanakamilisha taratibu za kuunga Uislam na Umagharibi, na desturi zile za kishenzi mno,kwa kile kinachoitwa,Uhuru,Demokrasia ama Haki za Binadamu.
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Iran anapingwa mno na Marekani na washirika wake. Sababu hasa siyo msimamo wake mkali wa kidini, bali pia itikadi kali ya kikomunisti. Yeye ni ma-Ayatollah, wanaupinga ubeberu,hasa Magharibikutaka kuimeza nchi yao,kama ilivyotaka kutokea zama za Shah.
Ahmadinejad, amerejea madarakani kupitia uchaguzi Mkuu wa Juni mwaka 2009 kwa mbinde; ni utawala ambao Marekani na washirika wake wanauita, ‘Janga la dunia.’
Mataifa ya Magharibi, kama kawaida yao walishapandikiza vibaraka,kama walivyofanya Irak,Misri, Yemen, Uturuki, Afghanistan na popote wanakotaka kwenda. Ahmadinejad anapingwa tena kwa maandamano makubwa, hasa nbaada ya uchaguzi wa mwaka 2009.
Propaganda za Magharibi zinasema polisi na wanamgambo wanaoogopwa sana mjini Tehran, Baseej, waliwaua raia na wengine walipigwa sana na kuswekwa rumande, baada ya ushindi wa Rais Ahmadinejad.
Unajua hawa viongozi wenye msimamo mkali  walimpindua Shah, ambaye alikaribia kuiuza nchi yenye utajiri wa mafuta kwa Wazungu, akapinduliwa na katimkia Bahamas, Panama, Marekani hata baadaye Misri.
Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, na Vikosi vya taifa hili linalojiita Jamhuri ya Kiislam ya Iran, wanajua maandamano katka nchi yao yameletwa na Maadui wa Taifa=Magharibi.
Hawa maadui wa Taifa,NATO na washirika wao, wamesimika vibarama mjini Tehran ili kumng’oa Ayatollah na Rais Ahmadinejad, kwa madai ya kuwatesa wapinzani,kuibaka demokrasia na Haki za Binadamu, ama kwa kuwatoa kolokoloni wapinzani wa serikali.
Vuguvugu la Kijani, “The Green Movement” la Kiongozi wa Upinzani, Mir Hosein Mousavi,lilidhaniwa na washirika wa Nato kwalmba lilishinda uchaguzi wa Juni mwaka 2009. Huyu Mousavi ndiyo wale wale Waarabu wanaolelewa Ulaya kasha wanatumwa kuingia katika nchi zao na kufanya maandamano huku wakitumiwa mishahara kutoka Ulaya na Marekani.
Hii Iran ambayo zamani ilikuwa dola ya Umedi na Uajemi, inatikiswa sasa kwa kutaka Rais ambaye ni Muislam mwenye itikadi kali, na Viongozi wa kidini, ma-Ayatollah waondolewe,ili kupisha mabadiliko, demokrasia na uhuru wa watu kuabudu Mungu,miungu ama nyoka.
Mousavi, ama mpinzani mwenzake Mehdi Karroubi, ambao ingawa ni Waislam hawawezi kuaminiwa na ma-Ayatollah, kama watasimamia maadili ya kidini. Ma ayatollah warichukua uongozi wan chi mwaka 1989 pale Ayatollah Ruhollah Khomeini alipompindua Shah, alipokufa akarithiwa na huyu Ayatollah Ali Khamenei.Zamani walingwa mkono na Urusi kabla ya kuparaganyika mwishoni mwa miaka ya 90.
Iran ni miongoni mwa nchi zinazozalisha sana mafuta duniani. Na wameanza kurutubisha uranium, kitu ambacho sasa kinazidisha joto la vizingizio vya Magharibi kutaka kufanya mapinduzi nchini humo.
Zamani, Russia na China ambao ni wanachama wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wangeweza kupinga uvamizi wowote dhidi ya Iran. Siku hizi hawa ni wafanya biashara na wabia wa Ulaya na Marekani.
Vita ndani ya Misri ama Libya, imeyanufaisha mno makampuni ya mafuta ya Urusi, na wakati vita vya kumpindua Gaddafi vinapamba moto, wao walikuwa wakiuza mafuta kimya kimya. Urusi na China, sasa ni wafanya biashara, siyo tena Dola zenye nguvu kijeshi.
Kufuatia hali hiyo, Iran inaweza kushambuliwa wakati wowote kuanzia sasa,kwa kisingizio cha Nyuklia ama kubaka demokrasia na uhuru wa watu.
Kwa upande mmoja ni kwamba, watu wanaweza kuwa na muda mchache sana wa kuamua kuwa Wakristo,lakini hali hii itadumu kwa kipindi kifupi mno kabla ya Amri ya Marekani kulazimisha watu kuabudu Shetani na Freemasons katika hiyo Amri ya NEW WORLD ORDER!
Tumeshuhudia nchi za KIISLAM kama Misri,Tunisia,Syria,Yemen na Libya zikikumbwa na vuguvugu la Kijani-Green Movement, na anayepinga hukumu yake ni kifo-kwa hiyo Syria na Yemen wataishia kujisalimisha wenyewe Washington, tumeona dalili za upendeleo ama ‘double standards’ siyo kama alivyofanyiwa Muammar Gaddafi,kuuawa.
Iran ndiyo ‘target’ la Wazungu. Iran ni adui mkubwa wa Israeli, wakati Marekani na washirika wake ni ‘wajomba’ wa Israeli na “Uzayoni”.
Na kama Iran itapinduliwa, kama tulivyoeleza katika makala iliyotangulia, basi dola za Kiislam zenye nguvu zitakuwa zimepinduliwa, na kwa sababu hiyo, “Mto Frati” (Euphrates) utakuwa ‘umekaushwa’ ili kuruhusu njia kwa mataifa yaliyo Mashariki-India, Uchina na Japan, kuvuka na kwenda kuungana na Umoja wa Ulaya na Soko lake, European Common Market, ili kuwawekea vikwazo vya uchumi wale vichwa maji wasiotaka kuunganisha dunia nzima!
Ni hapa,unabii wa Biblia unaosema kwamba Dola za Kiislam zilizokuwa zikiwang’ata adui zake kwa  ‘mikia ya nge wenye sumu kali’ wakati wa Jihad, sasa zitakomeshwa.Ukristo uliochanganywa na upagani na umizimu na Freemasons utatamba duniani-dini zote zimeanza kumezwa na ushenzi-dini za wanawake kubatizwa wakiwa uchi huko Uganda, biashara ya maji ya Baraka huko Kenya na Tanzania na ushenzi mwingi katika Ukristo ambao zamani uliruhusiwa kupigwa na mabedui wa KIARABU(Ufunuo sura ya 9).
Mabaki ya dola ya Ottoman eti yameungana na NATO, nchi za Kikomunisti zilikokuwa katika mkataba wa Warsaw,Poland, zilishajisalimisha NATO.
Sasa,Marekanina Soko la Pamoja Common Market ni zamu yao kulazimisha kila mtu,kila nchi kuamini mfumo wanaotaka wa kuabudiwa, na watakaopinga watauliwa kama Gaddafi, Osama na Saddam na wengine watawekewa vikwazo vya kiuchumi kama Iran,Cuba, Zimbabwe,Venezuela n.k
Hakuna tena taifa la Kiarabu ama la Kiislam litakalong’ata kama mikia ya nge(sting in the dragon’s tail),muda huo umepita(Ufunuo 13:15-18) na muda wa Marekani na washirika wake wa Kikristo kutamba.
Marekani sasa wako nyuma ya upinzani wa kijani kila mahali ili kutaka mabadiliko ya sheria,kuwe na uhuru watu kuamua hata wanaume na wanaume kuoana=kama hutaki hakuna msaada!
Marais, kama Mahmoud Ahmadinejad wanapopata fursa kuhutubia Umoja wa Mataifa(UN General Assembly)wanasema unyama huo dhidi ya taifa lao,lakini nani awasikilize? Marekani wanatetea demokrasia na uhuru wa dini,wakati huo huo wataondoa uhuru huo wa kuabudu kwa mkono mwingine.
Novemba, Barack Obama anaweza kurejea White House kwa mhula wa pili wa uongozi mwaka 2012. Na yumkini,Obama atatangaza hii amri ya New World Order.
Wakati wa uchaguzi wa 2008,gazeti la The New Yorker lilichapisha katuni, Michelle Obama na mtindo wake wa nywele wa ‘Afro’ akibadilishana na mumewe ‘Jambia’ lenye ncha kali la magaidi wa Kiarabu kwa bunduki, Machine Gun!!
Tafsiri yake ni kutimia kwa unabii. Osama Bin Laden ameuliwa-na juzi nikitazama televisheni,nikaona Obama akijisifu kwa kumuua Osama,kwamba kwa kipindi chake Marekani imekuwa mahali salama pa kuishi-hii ndiyo silaha yakekubwa ya kampeni za Novemba mwaka huu.
Marekani, zama za Obama huyu, amefanikiwa kuwanyang’anya Waarabu, tena Waislam “uwezo” uliokuwa katika mikia ya nge yaani katika majambia ya wafuasi wa vita vya Jihad. Tusome historia.
  Osama, Saddam,Gaddafi na Carlos The Jackal walikuwa Wakomunisti
Wote hawa walikuwa Waislam waliopata kupinga ubeberu wa Kimagharibi,kila mtu kwa staili yake na kwa mchango tofauti.
Osama Bin Laden alianza kuwapinga Warusi mwaka 1979 walipoivamia Afghanistan=alisaidiwa na Marekani. Osama alikosana na Marekani. Ni vigumu ukiwa na akili timamu kuwatumikia Marekani. Dikteta wa zamani wa Zaire, Mobutu aliyetimkia Togo baada ya kupinduliwa akaishia kuugua kansa na kufa Morocco, aliwahi kusema hivi, “I’m the latest victim of Cold War, because support for US was nothing” nimekuwa mwathirika wa hivi karibuni wa VITA BARIDI,sabababu(nimemaizi) kuwaunga mkono Marekani,hakuna faida!”
 Hii ni kauli ya majuto ya Mobutu alipokuwa katika kitanda cha mauti. Yuko Charles Taylor anasema, “Adui yako anapukuwa ndiye Bwana wako, wewe umekwisha!” huyu yuko The Hague, anashitakiwa kuleta mauti ambako yeye na Wazungu waliiba almasi za damu, Sierra Leone.
Naam, msimamo wa Saddam, Osama,Gaddafi na Carlos The Jackal ni kuupinga ubeberu kwa dhati. Rais wa Venezuela(nchi alikozaliwa Carlos) Hugo Chavez, anasema, Carlos The Jackal, hajawahi  kuwa gaidi,bali ni ‘Mpigania Uhuru’ wa zama za Vita Baridi, aliua watu lakini wengi wao mabeberu!,
Tumjadili kidogo Carlos The Jackal. Wakati huo wa Vita Baridi, Carlos The Jackal aliitwa Illich Ramirez Sanchez, na aliwapenda sana wanamapinduzi wa Amerika Kusini; akina Che Guevara, Camillo Torres na Carlos Merighella.
Babaye Carlos hakutaka kumpeleka Marekani kusoma ‘uchafu’ wa Magharibi.Alimpeleka kusoma Chuo Kikuu cha Patrice Lumumba huko MOSCOW,Urusi . Huko alikutana na wanamapinduzi wa Chama cha Popular Front for Liberation of Palestine (PFLP), ambao miaka hiyo ya 70 walikuwa wakidai uhuru wa Taifa lao.
Urusi inatajwa katika Biblia kama nchi iliyoko Kaskazini mwa Ulaya inayoitwa Gog(Ezekiel 38:)ni nchi kubwa iliyoenea mabara mawili ya Ulaya na ASIA na ina ukubwa ambao ni 1/6 ya dunia.
Carlos,mbali na kushiriki operesheni za ‘kigaidi’ kama kuwateka mawaziri wa OPEC huko Venna,Austria alikuwa Komando aliyefuzu katika Chuo cha Kijeshi cha Mantanzas,Cuba.
Nataka msomaji ajue urafiki uliokuwepo kati ya Wapalestina, Warusi,Venezuela, na hata Cuba ya Field Marshal Fidel Alejandro Castro Ruz, zama hizo.Wakati huo Urusi iliyoongoza nchi za Mashariki(Warsaw Pact) ilikuwa na watu milioni 250 sawa na Marekani.
 
0786 324 074



Friday, January 27, 2012

sangara wetu wamekwenda harijojo

Penye samaki wengi hapana samaki tena. Tunaukumbuka sasa unabii wa Filamu ya ‘Mapanki’ iitwayo, The Darwin’s Nightmare.
Nataka kuwakumbusha wasomaji wa gazeti hili kwamba,kitengo cha samaki cha Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa(FAO) kinachoitwa Globefish,kilishasema kwamba samaki wanakwisha Ziwa Victoria.
Hata Rais Jakaya Kikwete aliyekerwa sana na ‘documentary’ hiyo, akakutana na mtunzi wake, Hubert Sauper huko Ulaya mwaka 2006, Sauper akaingia mitini, alishakiri kwamba Ziwa Victoria samaki wanakwisha.
Samaki hawajaisha Mugango na Suguti, Majita,Musoma mkoani Mara tu.
Hata Mwanza hakuna samaki, Bukoba siku hizi wanakula ndizi pasipo samaki. Visingizio ni vingi,ukiwemo uvuvu haramu, lakini ukweli ni kwamba viwanda vya samaki vya Umoja wa Ulaya(EU) na washirika wao,Wahindi, wamekausha samaki Ziwa Victoria.
Nina takwimu.Sibabaishi ninapoandika jambo!
Globefish, walisema mwaka 2004 kwamba mauzo ya samaki, wa Tanzania,hususan sangara, yalishapungua katika masoko ya Ulaya kutoka tani 56,000 mwaka 2004 hadi tani 52,800 mwaka 2005.
Basi, sangara wakaanza kupanda bei katika masoko hayo ya EU kutoka euro 192 milioni hadi euro milioni 210 kwa sababu sangara walipungua, mahitaji yakaongezeka, wakati huko Mugango, Musoma na Mwanza na Bukoba bei ikisalia ile ile.
Kati ya mwaka 2004/2005 kilo moja ya sangara waliosindikwa viwandani  iliuzwa kwa euro 3.43 hadi euro 5 ambazo zilikuwa kama shilingi za Tanzania kati ya 6,000 na 8,000 tu.
Wakati huo,wavuvi wa Bukima na Bugunda,Majitta, Mugango,Mwanza hadi Bukoba walilipwa shilingi 1,200 hadi 2,000 tu kwa kilo moja ya sangara ghafi. Uporaji wa hali ya juu!
Kulingana na Globefish,kilo moja ya ya fileti ya sangara huko Ulaya iliuzwa kwa wastani wa euro 60. Euro moja wakati huo ilikuwa sawa na shilingi 1,600 za Tanzania.
 Sasa angalia, Mzungu analala usingizi kisha anaamkia supermarket yake na kuuza kilo moja ya sangara kwa euro 60, wakati mvuvi alivua usiku mzima hapa,akapigwa dhoruba, akaishia kulipwa shilingi 1,200!
Maudhui katika Filamu ya Darwin’s Nightmare,iliyotungwa na Hubert Sauper mwaka 2004, akatunukiwa tuzo anuwai duniani,ikiwemo tuzo ya Oscar, ni kwamba Tanzania ilikuwa ikidhulumiwa sana kupitia biashara hii ya sangara Ulaya.
 Tanzania,ilibweteka kwa sifa hewa kwamba inauza sana sangara,kumbe Wahindi na Wazungu walichuma sana migongoni mwa wavuvi(akina Mkono wa huko Bukoba na Musoma) ambao waliishia kulipwa kidogo, wakabaki kunywa gongo na kupukutika na Ukimwi katika makambi ya uvuvi.
Mwandishi wa mwanzo kuwasha moto ,alikuwa Johnson Mbwambo, ambaye aliandika katika Gazeti la RAI Toleo Na 640 la Januari 12-18 mwaka 2006 kwamba documentary ya Darwin’s Nightmare ilituzindua usingizini!
Serikali mkoani Mwanza, wakati huo Daniel Ole Njoolay, akiwa Mkuu wa mkoa, akatoa Tamko kali kulaani documentary hiyo kwamba ilikuwa ya kizandiki; na kwamba Tanzania ilifaidika mno na mauzo ya sangara Ulaya.Akapinga Watanzania kula vichwa na mifupa ya sangara waliotupwa viwandani baada ya kusindika minofu-maarufu sana kama mapanki.
Nimesema wakati huo bei ya sangara ilikuwa shilingi 1,200 na viwanda vya mkoa wa Mwanza pekee vilikuwa vikisafirisha zaidi ya kilo 30,000 za sangara waliosindikwa,wakati Mwanza pekee kukiwa na wavuvi 39,370.Shilingi milioni 200 zilikuwa zikiingia katika mzunguko wa fedha kila siku.
Njoolay,alisema pato lililotokana na sangara mwaka mmoja kabla ya filamu hiyo,lilikuwa shilingi bilioni 5.7 wakati shilingi milioni 200 zinazunguka katika mzunguko kila siku,wavuvi wakitembea na mifuko ya plastiki,’Rambo’ iliyojaa noti!
Kwa ujumla, serikali iliibeza makala ya Johnson Mbwambo, ambaye wakati huo alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wandishi wa Habari za Mazingira(JET).
 Jumatatu,Julai 31 mwaka 2006,Rais Jakaya Kikwete, akafanya mkutano na wazee wa Mwanza kwenye ukumbi wa Chuo cha Benki Kuu(BoT) Capri-Point,Mwanza na kuilaani vikali Filamu ya Mapanki, Darwin’s Nightmare.
Vyombo takriban vyote vya habari vikahanikiza laana hizo za Rais Kikwete kwa Hubert Sauper,kwa sababu huko Ulaya na Marekani, Filamu hiyo “Mapanki’ iliichafua sana Tanzania huko Ughaibuni, hata Rais alipokwenda kujitambulisha huko baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2005, akakutana na habari za filamu hiyo.
Rais Kikwete alikasirika; kwa sababu alidhalilishwa kusikia na kuiona hiyo filamu ikitubeza kwamba tuliuza Ulaya minofu ya sangara,sisi tukabaki kula vichwa na mifupa-mapanki-mithili ya vijibwa! Mapanki yenyewe ni yale yenye funza, tuliyinyang’anyana na mwewe na mbwa huko Kanyama na Nyamuhongolo,nje kidogo ya Jiji la Mwanza, barabara iendayo Sirari na Musoma.
 Naam, mimi na Richard Mugamba(sasa Mhariri wa The Guardian on Sunday)tukajitoa mhanga kuuzindua umma wa Kitanzania juu ya kile alichosema Hubert Sauper,katika filamu ile.
Kwamba,wakati Mzungu anapopelekewa minofu huko, sisi tunakula mifupa na vichwa vya sangara vilivooza,ili kujikimu,kwababu nchi ilikuwa katika janga la njaa,kiasi cha kusaidiwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa,FAO na WFP.
Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC) likafika Mwanza na timu ya Watangazaji wengi, akiwemo Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili, Tido Mhando,nilipewa muda kuzungumza namna biashara hiyo ya sangara ilivyokuwa ikimaliza samaki Ziwa Victoria na kuwaacha wananchi na njaa na umasikini wao.
Kwa sababu zile alizosema Hubert Sauper katika Darwin’s Nightmare, serikali ikabisha,miaka mitano imekwishapita.Sasa ni dhahiri, wakazi wa kando ya Ziwa wanakula maharage na mboga za majani, samaki wamekwenda harijojo.
Nataka niwaambie wasomaji kwamba serikali ilishakubali maoni ya filamu hiyo kimya kimya, na hapa nitaeleza kauli za Rais Kikwete na mawaziri wake.
Jumanne, Mei 13 mwaka 2008, Rais Kikwete alipokuwa akifungua kiwanda cha kusindika samaki cha TFDC,Ilemela,Mwanza, akasema wananchi waanzishe mabwawa ya kufugia samaki,maana Ziwa Victoria ‘linakauka’.
“Ndiyo njia pekee ya kuondokana na kitisho cha kupungua samaki katika Ziwa hili kubwa kuliko yote Afrika”, Rais alisema.
Wavuvi, wakiwemo haramu wengine kutoka nchi jirani za Kenya na Congo DRC walishaongezeka sana kutoka 51,935 mwaka 2002 hadi 98,015 mwaka 2007.
Zana za uvuvi zikiwemo haramu zilishaongezeka mno kutoka 15,434 hadi 29,730 katika kipindi hicho.Bila shaka Rais alishabaini ukweli wa mambo,kwamba kipindi kile wasaidizi wake walimpotosha kwamba hatuli ‘Mapanki’ kwa sababu walizojua wao!
Na uzembe wao ndiyo ulimfanya Sauper kupiga picha za filamu ile(nilishaandika jambo hili katika gazeti hili). Mwaka 2004 samaki waliovuliwa Ziwa Victoria walikuwa wenye uzito wa tani 750,000. Lakini mwaka 2007 samaki waliovuliwa katika Ziwa hili walipungua hadi tani 375,400 tu.
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,wakati huo John Pombe Magufuli akachoma makokoro haramu,wakati maofisa uvuvi wakiwapora wavuvu sehemu moja na kuyauza kwingine-baadhi yao walikuwa na hayo makokoro haramu mengi tu. Samaki wa Musoma wakaendelea kutoroshwa hadi Nairobi na Ulaya kwa magendo.
 Takwimu zikawa zinapikwa tangu viwandani hadi Mamlaka ya Mapato(TRA) bila wasiwasi.
Waziri wa MAALIASILI na Utalii,Prof Jumanne Maghembe, Juni 11 mwaka 2007 wakati akifungua semina kuhusu uvuvi endelevu  hapo BoT,Mwanza akasema samaki wamekwisha,wakati bei imebeki ile ile tu.
 Prof. Maghembe akaagiza hadi Juni 11,mwaka 2008 samaki waliosalia angalau waachwe wazae uzazi mmoja tu!
“Pasipo kufanya mkakati wa kuepusha samaki kutoweka Ziwa Victoria,Tanzania haitaepuka ‘HUKUMU YA ULIMWENGU’ kwa kuruhusu rasilimali zake wakiwemo sangara kutoweka,na hivyo maisha ya watu kuathiriwa vibaya”, alisema Prof. Maghembe hiyo Juni 11 mwaka 2007.
 Hiyo hukumu ya ulimwengu aliyosema Prof. Maghembe ni  ipi kama siyo kilichosemwa na documentary hiyo ya Mapanki serikali ikabisha?
 Kwamba, sangara wa Ziwa Victoria waliliwa Ulaya, sisi tukabaki na njaa yetu na kuomba misaada, wakati wavuvi wakifa kwa ukimwi makambini,wakibugia gongo na dada zetu wakijiuza kwa marubani wa madege ya Kirusi-Ilyusin-kwa ujira wa dola 10
Niliitazama Filamu hiyo, DARWIN’S NIGHTMARE ofisini kwa Mkuu wa mkoa, Daniel Njoolay wakati huo kabla ya kuhamishiwa Rukwa.
 Niliitazama kwa mara ya pili ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mwanza(MPC)nikaandika habari kadhaa na makala za kutosha. Habari iliyokaribia kunitia matatani,ni ile ya Alhamisi, Agosti 3,mwaka 2006 iliyotolewa katika Gazeti la Tanzania Daima,ikiwa na kichwa, “Mapanki yamgeuka J.K”
Katibu wa CCM, mkoa wa Mwanza,wakati huo,Mujuni Kataraia,akaitisha maandamano ya kuipinga habari hiyo, halafu akaniambia, “Kwanini kila mara wewe uko against na(unaipinga) serikali?”
Nadhani Rais Kikwete aliyapuuza maandamano yale. Ingawa alikuwa jijini Mwanza kwa mapumziko,hakujali maandamano yale ya kunipinga.
Darwin’s Nightmare,imejengwa katika Falsafa za mwanabaiolojia wa Kiingereza, Charles Robert Darwin(1809-1882) ya viumbe vyenye nguvu kuvitafuna dhaifu, “Survival of The Fittest” katika Ulimwengu wa utandawazi.
Wazungu wanapoacha akiba samaki wa maziwa yao na bahari, wanachuma hawa wa kwetu kwa bei chee,halafu wakiisha wanang’oa viwanda vyao na kutoweka huku wakituacha na njaa yetu-hii ndiyo Theory na ‘Darwinism’ na Survival of the Fittest. Wenye nguvu wanawala dhaifu ama masikini!
Tanzania ilivikwa kilemba cha ukoka kwamba ilikuwa msafirishaji namba wani wa sangara duniani,kumbe samaki sasa hawapo baada ya madege ya Kirusi, Illyushin kusomba takriban tani 50 kila dege kwa siku.
“Falsafa” hii ya Darwin haikutuzindua usingizini, waandishi kama Johnson Mbwambo wakaishia kubezwa na serikali,mwisho wa siku sasa kilio cha kutoweka kwa samaki kinasikika kila upande!
Samaki ni fursa muhimu katika nchi.Lakini, wameporwa na wawekezaji kwa bei poa, na hata Wacongo wanavua huko visiwani,maofisa wa maliasili wapo tu,wanapewa rushwa ndogo ndogo na samaki wanazdi kutoweka!
 Kitengo cha Globefish cha FAO kilishasema mwaka 2006 kwamba samaki wanatoweka kwa kasi Ziwa Victoria na kuwaacha Watanzania na njaa,na umasikini na dhiki nyingi huku watoto wa mitaaani wakigombea ubwabwa katika sufuria la mpita njia,mama ntilie!
 Madege ya Kirusi yalisomba sangara hadi yakaanguka Ziwani kwa kuzidisha uzito ili kukwepa Mamlaka ya Mapato(TRA).
Sauper, katika filamu hiyo ya mapanki alitukumbusha namna Yesu wa Nazareti alivyotumia visamaki viwili tu(Tanzania tulikuwa na masangara makubwa mengi tu)na mikate mitano kuwalisha zaidi ya watu 5,000 katika kijiji cha Bethsaida,wakasaza mabaki yaliyojaa vikapu 12!
Katika filamu hii,Darwin’s Nightmare, muujiza wa Yesu wa kuwalisha watu hao( Injili ya Marko 6:34-44 na Luka 9:10,11) ili Tanzania tujifunze kutumia rasilimali zetu vizuri kuwalisha watu wenye njaa siku hizi tunapolia na ukame.
Sauper, alimtangaza Yesu katika filamu hiyo kama kiongozi bora, anayejua kutumia rasilimali chache kwa maslahi ya wengi hadi kusaza vikapu 12!
 Laiti Yesu angekuwepo leo Tanzania,penye masangara makubwa haya, na jodari mithili ya wale wa Magufuli, dagaa, almasi, tanzanite,dhahabu,wanyamapori,misitu,matunda, mifugo,mito,bahari,milima mirefu na mabonde,bila kusahau madini mengi haya, watu milioni 43 wa Tanzania wasinge kula na kusaza vikapu bilioni nyingi?
Tatizo, Watanzania siyo wazalendo, na siyo viongozi tu wasio wazalendo, hata wavuvi siyo wazalendo kama wale wanafunzi wa Yesu walioleta visamaki viwili na mikate yao mitano Yesu akaibariki na kuwalisha watu zaidi ya 5,000!
 Tanzania, tuna njaa katika utajiri wa rasilimali?
Sababu,hakuna viongozi wazalendo kama Yesu wa Nazarethi, na kila mtu ni mchoyo, mzalendo wa tumbo lake mwenyewe, asiyewajibika.
 Tuna rasilimali tele,fursa tele.
Tuna ‘Jodari’ kama wale wa Magufuli na masangara makubwa, lakini yamekwisha na kutuacha masikini na wenye njaa-hatuna akili.
Itaendelea
www.congesmrambatoday.blogspot.com
0786/0754-324 074
 
 
 
 

sangara wameuaka ziwa victoria


 
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, alisema mwaka 2007 kwamba, sangara walioliingizia Taifa mabilioni ya fedha za kigeni, sasa wametoweka.
 
  " Wanapungua kwa kasi sana . Kama hatua za dharura hazitachukuliwa, watakwisha; wananchi watateseka kwa kukosa kipato. Viwanda wa samaki vitafungwa na kuathiri mapato ya nchi na ajira muhimu." Alisema Prof Maghembe, mwaka huo 2007
 
    Prof. Magembe, ambaye alikuwa akifungua kikao-kazi kwa viongozi wa mikoa na wilaya kuhusu uvuvi endelevu Ziwa Victoria , Juni 11 mwaka  2007 katika Ukumbi wa Chuo cha Benki Kuu Mwanza, ameonya kuwa maisha bora kwa Watanzania hawa yanaweza kuwa pwaji, ama porojo tupu.
   Lishe kwa wakazi milioni 30 wanaozunguka ziwa hili, wa Tanzania , Kenya na Uganda , itaporomoka; wakati fedha nyingi zikiwemo za kigeni, zitakosekana. Prof. Maghembe aliagiza, angalau ifikapo Juni mwaka 2007 ufanywe mkakati kuhakikisha sangara waliobaki wanazaa japo uzazi mmoja tu!
    Akasema, kitu kimoja muhimu sana , ambacho ni muktadha wa makala hii leo: Kwamba, bila kufanya mkakati wa kuepusha sangara ama samaki kutoweka Ziwa Victoria , Tanzania haitaepuka ‘Hukumu ya Ulimwengu’ kwa kuruhusu rasilimali zake wakiwemo sangara, kutoweka, na hivyo maisha ya watu wake kuathiriwa vibaya.
    “Hili, inabidi litimie. Vinginevyo, hatutaepuka hukumu ya Ulimwengu kwa kuruhusu rasilimali hii kutoweka, na hivyo watu wetu kuathirika vibaya”, alisema Profesa Maghembe.
   Aliweka kipindi cha nusu mwaka, kuhakikisha taarifa ya kazi inatolewa. Kwamba jambo hili si muhali; hivyo kushindwa kulitekeleza ili kuondoa kitisho hiki si chaguo la serikali yetu.
    Kwa upande mwingine, ‘Hukumu hii ya Ulimwengu’ aliyosema Prof. Maghembe, ilikwisha tolewa na Hubert Sauper, yule Mtunzi wa Filamu ya tashtiti, ya Mapanki(The Darwin’s Nightmare), serikali ikabisha!
   Kwamba, sangara wa Ziwa Victoria walikuwa wakiliwa Ulaya, wakati wazalendo wa nchi hii wakiambulia vijisenti kidogo vya kikunjajamvi, wakati wengine wakiambulia vichwa na mifupa-mapanki!
  Jinamizi la Darwin;Charles Robert Darwin (1809-1882) lililosimuliwa na Hubert Sauper, kwa njia ya kejeli, miaka michache iliyopita, kupitia filamu iliyomfedhehesha hata rais wetu, lilikuwa onyo tosha.
   Onyo kwa serikali yetu kuwamaizi Pwagu,(wezi na wadanganyifu), Pwaji(wapiga porojo) na Pwaguzi(wajanja zaidi kuliko Pwagu), waliokuwa wakikomba sangara wetu na kutuacha  masikini.
     Filamu hii iliwataka Watanzania kuondoka usingizini mara moja na kuepuka kugombea ubwabwa kidogo katika sufuria chafu, kula mapanki yenye funza, na kunywa pombe haramu ili kupata tafaraji, baada ya kuvua sana na kuuza samaki wengi sana kwa  Pwagu, yaani wakala wa   Pwaguzi, bila faida!
   Watanzania tulionywa na filamu hiyo kuwa na akili; yaani kuvua kwa tija, badala ya kuvua sana tukiishi katika makambi mithili ya manamba, ambako wavuvi huishia kufa kwa Ukimwi, na  dada zetu huishia kuwa machangudoa wanaopigwa ‘kipopo’  mithili ya wezi, na Wazungu kwa ujira wa dola dola 10 tu.
   Athari hasi za utandawazi, muktadha wake ni pamoja na kugombea maisha(struggle for existance); ni harakati zinazowafanya viumbe dhaifu kushindwa mapambano; na hivyo kuishia kuliwa mithili ya mchwa, panzi na kumbikumbi.
   Falsafa ya ya Charles Robert Darwin, mwanasayansi maarufu sana wa Kiingereza(alizaliwa Feburuali 12 mwaka 1802 na kufa Aprili 19, mwaka 1882) iitwayo Darwinism, huonya kwamba, katika maisha viumbe dhaifu ikiwemo mimea, abadan havishindani na vyenye nguvu.
    Katika zama hizi za utandawazi, mataifa dhaifu kama Tanzania ,  hujikuta yakinyang’anwa chakula, maji, hewa na mwanga wa jua, ili kuyapisha yenye nguvu kustawi.
    Tanzania kama mmea, itanyauka baada ya kuzongwa na magugu(Super powers), au baada ya kutafunwa kama sangara anavyowatafuna samaki wadogo, ama kama simba anavyowatafuna swala,pofu, nyumbu na palahala porini.
   Kitu hiki, ndicho Darwinism; yaani kwamba wenye kupona ni wenye nguvu tu(survival of the fittest).
     Kitendo cha sangara wetu kuuzwa Ughaibuni kwa vijisenti kidogo na kuwalisha Wazungu na Wahindi huku Watanzania wakihangaika kwa njaa kali, ni athari yakinifu za utandawazi unaoruhusu wakubwa kuwatafuna wadogo.
     Yesu wa Nazareti aliwalisha watu zaidi ya 5,000 katika kijiji cha Bethsaida kama miaka 2010 iliyopita, kwa visamaki viwali vidogo, ukilinganisha na sangara wa Ziwa Victoria, na mikate mitano.
   Katika Darwin’s Nightmare, muujiza huu unaosimuliwa katika Injili ya Mtakatifu Luka 9:10-11 na Marko 6:34-44 umeonyeshwa.
     Bila shaka, muujiza uliwekwa ili kuwakumbusha Watanzania kwamba, kama Yesu aliwalisha watu hao(walihesabiwa wanaume pekee, bila wanawake na watoto) kwa visamaki viwili; wakala hadi wakasaza vikapu12, Watanzania hushindwaje kujilisha kwa mabilioni ya sangara, dhahabu, almasi, tanzanite, ruby,  wanyamapori, misitu,shaba, pamba, kahawa, katani, korosho na rasilimali zingine anuwai?
 Kwa upande mwingine, hofu ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Maghembe, kwamba samaki wetu(si visamaki) watatoweka na kuwafanya wananchi kuathiriwa vibaya, ni sawa na kilio cha uchungu kuashiria maombolezo ya taifa.
    Sauper, alitaka kuwasagua Watanzania, tena kuwagutua kwamba umasikini na njaa yetu wakati sangara mabilioni wakitoroshwa Ulaya na akina Pwagu, bazazi, dumizi na pwaguzi kwa mrabaha kidogo, ulikuwa umbumbumbu.
    Hata rasilimazi nyingine kama madini, wanyamapori na mazao ya kilimo hutoroshwa hivihivi na ma-Pwagu, Pwajizi na mapwaguzi, pasipo sisi kunufaika na chochote. Sisi ni ng’ombe wa maziwa-watu wa kukamuliwa hadi tone la mwisho la damu.
    Pwagu, Bazazi na Pwaguzi wanavyowanyonya wavuvi. Wanasomba sangara kwa ujira kidogo.
    Hushirikiana na Maofisa uvuvi,polisi, maofisa wa Forodha, TRA, na hata baadhi ya Mawaziri husafirisha sangara kwa magendo!
Kama Profesa Maghembe na  aliyekuwa Mkurugenzi wa Uvuvi,Geoffrey Nanyaro walikuwa hawajui, shime wamaizi kuwa sangara wetu hukombwa na'pwaguzi’ kwa ujira kidogo wanaolipwa akina Pwagu!
    Katika biashara hii, wamo bazazi na dumizi wanaojipendekeza kwa Pwagu, ili kujipatia makombo!
    Naam. Hapa, Tanzania inaliwa na kubakizwa mifupa mitupu-mapanki. Mapanki nayo huuzwa nje yakaliwe na kuku, wakati Watanzania wakibaki  kugombea fadhila na chakula cha wahisani.
    Masikini wavuvi wanapofikisha sangara kiwandani, huambiwa na Mapwaguzi kwamba ni ‘reject’ kisha huambulia kipeto na kuondoka na njaa yao.
   Kitengo cha samaki (Globefish)cha Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa(FAO), Agosti mwaka jana kilisema kwamba sangara walikuwa wakitoweka kwa kasi Ziwa Victoria.
   Ni taathira kwa Watanzania watakaobaki hawana chakula, wakiomba msaada Ulaya na Marekani, ili kujiepusha kupotea katika uso wa dunia. Tunaambiwa Watanzania huambulia milioni 500 kwa siku kutokana na biashara ya samaki kila siku
     Kwamba kila mwaka wavuvi na wachuuzi wa samaki hupata sh. Trilioni176.
Kwa mwaka Wazungu hutafuna minofu maelfu ya tani kutoka Tanzania , wakati samaki wao wakiachwa akiba.
Vya walevi huliwa na mgema.
    Wavuvi wadogo leo husukumiwa laana ya kusababisha sangara kutoweka; kwamba wanavua kwa kutumia nyavu haramu. Hizi nyavu haramu hukamatwa hapa na maofisa uvuvi, kisha huuzwa pale, baada ya kuchoma  moto chache tu, mbele ya polisi na waandishi wa habari!
    Nyavu au makokoro hayo ya polisi na maofisa uvuvi ndiyo yanayoharibu mazingira ya ziwa na mazalia ya samaki.
 Leo,Maofisa wanadanganywa kwamba wavuvi haramu ni wananchi vijijini! Wakale wapi sasa?
Samaki wawili wa kitoweo wanapunguza samaki?
    Sangara wadogo wanaosafirishwa nje ya nchi, wanavuliwa na nani kama si na hao maofisa uvuvi na ndugu zao?
     Kwanini wasikamatwe? Watanzania masikini wanaovua bila leseni, huvua tani ngapi kama si kitoweo? Wanayuga-yuga kuepuka mhali, ama njaa inayowakabili. Kwanini akina Pwagu na Pwaguzi wanaachwa kuvua na kusafirisha  mamilioni ya sangara kwa magendo?
     Tatizo si wavuvi wadogo, ni mapwagu, mabazazi,dumizi na pwaguzi wanaokomba samaki Ziwa Victoria na kuwauza nje kwa magendo, lakini hawakamatwi. Vigogo, wakiwemo hata baadhi ya Mawaziri wana vikampuni hewa, wanapewa mgawo wao na akina Pwagu na Pwaguzi.
   Waziri Maghembe anawataka wabadilike! Waache kuimumucha Tanzania ? Hizi ni porojo, pwaji na soga! Waondolewe katika madaraka, tena wafilisiwe. Je, viongozi watazinduka? Wataweza? Shime wawafunge mikatale ili kuinusuru Tanzania.
    Wanao ubavu wa kuwakomesha akina Bazazi, pwajizi, pwagu na pwaguzi wasilikaushe ziwa Viktoria? Labda.
   0754 324 074
   0715 324 074.