BINADAMU
dhaifu hawawezi kufanya chochote cha mafanikio yake bila msaada wa wanyama?
Hatavikosi
vya usalama katika tawala zilizofanikiwa sana za wanadamu, haviwzi kubaini
hatari za milipuko ya mabomu pasipo kushirikisha mbwa,panya n.k ili kudhibiti
hatari za magaidi kama al-Qaeda, al-Shabaab n.k
Novemba 29
mwaka huu huu, pal kwenye Uwanja wa CCM Kirumba,Mwanza wakati wa ujio wa Kombe
la Dunia(Fifa World Cup Trophy) na Rais Jakaya Kikwete, nikaona polisi na
Usalama wa Taifa,wakiwatumia mbwa kunusa kila kiti,kila meza,kila chumba na
hata magari yalinuswa na mbwa zaidi ya mmoja,ili kubaini hatari!
Mbwa mdogo
wa Usalama, mwnye madoa meusi na meupe,na mkanda shingoni, akang’ang’ania chupa
tupu ya Coca-Cola mdomoni mwake!
Alikuwa
ndiyo kwanza katoka kunusa jukwaa na vifaa vilivyokuwa jirani,njiani akakutana
na hizo chupa tupu zilizokuwa chini, akachukua moja mdomoni mwake na kuanza
kuondoka nayo,utadhani alibaini bomu ndani mwake!
Alipomaizi
kuwa mbwa Yule alikuwa akifanya mzaha, askari Yule alimpokonya mbwa huyo mwenye
cheo hiyo chupa tupu na kuitupa.Mbwa Yule alitaka kuirudia kisha akaendelea na
hamsini zake.
Naam, katika
sehemu iliyotangulia ya makala haya,tuliona haja na MAPINDUZI katika kizazi cha
wanyama(pamoja na jamii ya wanadamu),kwamba mabadiliko katika maisha ni hitaji
la msingi wakati wote ili kuboresha maisha.
Mapinduzi
yanapaswa kufanywa kwa makini ili kuleta mabadiliko chanya na aslani siyo
mabadiliko hasi yatakayoleta majuto baadaye.
Ustawi wa
kundi moja la wanyama,wakati mwingine hugeuka janga la kutisha kwa kundi linguine.Ustawi
wa samba na mbwa mwitu huleta mauti kwa jamii ya wanyama walao nyasi. Ustawi wa
tembo na hata nyati hulta kilio kwa mashamba ya mwanadamu.
Ustawi wa
binadamu husababisha karamu kila siku na hivyo wanyama hujikuta wakichinjwa
kila asubuhi na jioni.
Hata hivyo,
binadamu ni mnyama mharibifu zaidi kuliko wanyama wote(man is only creature
that consumes without producing).Binadamu hazalishi chochote yeye mwenyewe,
hawezi hata kukokota jembe la kukokotwa na wanyama kazi(plough),hatagi hata yai
moja,wala hawezi kurutubisha ardhi anayoiharibu kila siku.
Hii ni kazi
ya wanyama ambao hata kinyesi chao ni mbolea safi. Kitu kinachozalishwa na
wanyama huishia katika koromeo la binadamu huyu Dikteta na fisadi!
Naam, huu
ndiyo uliokuwa mwito wa wanyama kutaka MAPINDUZI dhidi ya udikteta wa
mwanadamu. Bahati mbaya mwito wa mapinduzi uligeuka UASI(rebellion) ulioishia
kuleta majuto kwamba, “Heri utumwa wa mwanzo kuliko wa sasa!”
Kwa akili za
wanyama, walidhani uasi dhidi ya binadamu,haki(justice) ingekuja yenyewe,na
maslahi ya wanyama yangepatikana midhali binadamu fisadi alikwisha timuliwa
katika umiliki wa SHAMBA LA WANYAMA.
Dhima ya
wanyama ilikuwa, “PERFECT UNITY and PERFECT COMRADESHIP IN THE STRUGGLE”katika
harakati za kuondokana na minyororo ya utumwa dhidi ya mwanadamu, wanyama
waliona binadamu pekee alikuwa adui yao.
Na kwamba
wanyama wote walikuwa ndugu na washirika wa kwale katika harakati za kutafuta
ukombozi wa kweli(comrades),kumbe walisahau kwamba hata baadhi ya wanyama
walitamani kuishi na kunyonya wqanyama wenzao mithili ya binadamu!
Kulikuwa na
akina mbwa,hawakuwa tayari kuishi na sungura pasipo kuwakamata na kuwaua ili
kupata kitoweo. Paka hawakuwa tayari kuishi bila kuwafukuza panya,mwewe
hakutaka kuacha kuwapora vifaranga n.k
Nataka
kusema kwamba,ilikuwa kazi ngumu jamii ya wanyama kujenga upendo wa kweli,
uhuru wa kweli,haki na demokrasia halisi kulingana na sheria
saba(amri)walizojiwekea zenye maudhui kwamba, “ALL ANIMALS ARE EQUAL”
Njozi yao
ilikuwa
, “Golden future time… .Tyrant man to be overthrown
and the fruitful fields of Tanzania to be trod by beasts- alone!
Wanyama
waliota, siku za usoni utawala katili wa mwanadamu upinduliwe na kutimuliwa
daima ili ardhi yenye rutuba inayozalisha maziwa na asali ibaki mikononi mwa
jamii ya wanyama pekee!
Wanyama
wanapotamani kuvunja minyororo ya utumwa ya jamii ya mwanadamu ili kujipatia
uhuru kamili, walisahau kwamba miongoni mwao baadhi yao hawakuwa na nia dhati
ya uhuru.
Baadhi yao
walijiona bora kuliko wenzao, walikumbatia ubaguzi wa nasaba zao, majimbo yao
ama mikoa yao,jamii zao na hata koo na makabila yao-ndiyo akina nyau dhidi ya
panya,mbwa dhidi yap aka n.k
Walipigia
kelele dhuluma ya mwanadamu dhidi ya wanyama,wakasahau MAPINDUZI sharti yaanzie
katika fikra na mitazamo yao kwanza,yaani wote wakubali kuthamini usawa na
uhuru wa kila mnyama.
Maslahi
binafsi ya baadhi ya wanyama kama akina Nguruwe waliokuwa viongozi, ndiyo
kilikuwa chanzo cha majuto makubwa,na ubaguzi wa kinasaba,kijimbo na kikabila
hata wanyama wakalia kwamba, ‘Heri utumwa wa zamani kuliko wa sasa!
Miongoni mwa
wanaharakati katika SHAMBA LA WANYAMA,kulikuwa na “Spies” na ‘Tale-Bearers” wachuuzi
wa wenzao,waongo na wanafiki wakubwa,wasemaji wazuri,waliopigiwa makofi na
kupata wafuasi wengi wa makundi ya wanyama,hususan wale wanyama wadogo.
Wapiga debe
wengi walioitwa ‘Wapiganaji’ ama ‘wapambanaji’ wakatabiri “The existence of
mysterious country called, SUCARCANDY MOUNTAIN”.
Nchi ya
maziwa na asali ambayo baada tu ya binadamu kupinduliwa,jamii ya wanyama
ingekwenda kuimiliki,nayo ni chi ya utamu mithili ya asali. SUGARCANDY MOUNTAIN
eti ni Mlima wa vinono, ambako wanyama wangefanikiwa kuishi tu baada ya kufa!!
Eti hii nchi
ilikues angani, ikiwa imejaa meza za vinono(sweets) juu kuvuka mawingu!!
Moses,
alikuwa mpigadebe wa siasa za uchochezi kuwafanya wanyama wenzake wavunje
sheria ili wafe ili rahisi kuifikia ile nchi ya siri katika Mlima wa
sukari-SUGARCANDY MOUNTAIN!!
Yeye, Moses
hakufanya kazi yoyote zaidi ya kupiga ‘politiki’(Tazama Animal Farm uk 10)licha
ya kuleta uongo kwa wanyama, aliwahimiza kumwaga damu ili kufikia ile sugar candy mountain.
Wakati
akifanya haya,yeye Moses alikuwa akivunja sheria walizojiwekea.Alikula
akiguguna kwa wizi mkate uliokuwa umechovywa ndani ya pombe(Kumbuka Amri ya 5
ilisema ilikuwa Marufuku wanyama kunywa pombe)huko katika shamba la wanyama la
Uingereza!
Ilipotokea
wanyama wakapata uhuru,kufuatia utawala wa binadamu kutimuliwa, viongozi hawa
wanafiki wa shamba la wanyama walianza kujifanya nao ni binadamu,wakageuza
sheria ambazo zilianza kusomeka hivi:
“ALL ANIMALS ARE EQUAL, BUT SOME ANIMALS ARE
MORE EQUAL THAN OTHERS!”
Wanyama viongozi-akina
nguruwe-walikwenda mbali wakaanza kulewa pombe,kuvuta sigara,mtemba, kusoma
magazeti ya binadamu kama Daily Mirror n.k
Wanyama
viongozi walianza kuvaa suti,hususan za binadamu kinyume cha sheria(Rejea Amri
saba za wanyama katika sehemu iliyotangulia)wakafanya vikao ku-compromise na
binadamu katika vikao vilivyoandamana na ulevi na ulaji wa nyama za wanyama
wenzao!!
Matokeo,
wanyama viongozi-nguruwe- waliafiki wanyama wadogo wafanyishwe kazi nyingi za
kuvuja jasho,kazi za harubu,halafu ujira ni chakula kidogo-DHULUMA.
Wanyama walioitana,comrades,rafiki,mwanachama
ama ndugu,sasa baadhi yao wakataka waabudiwe utadhani miungu.
Jina SHAMBA
LA WANYAMA(ANIMAL FARM) wakataka libadilishwe na kuitwa, ‘Manor Farm’ yaani
shamba ndani ya jumba kubwa la zamani lenye shamba lililomilikiwa na kigogo “VIP”.
Wenye masikio
na wasikie! Inakuwaje wanyama wenye usawa miongoni mwao wawemo ‘VIP(VERY
IMPORTANT PERSONS)?
Mwisho wa
siku,jamii hi ya wanyama ikaishia kwenye ugomvi mkubwa sna kufuatia tuhuma
dhidi yao,wanadamu na wanyama wakarudi kukubaliana kudhulumu wanyama haki zao
na demokrasia.
Kitabu hiki
SHAMBA LA WANYAMA kiliandikwa Novemba mwaka 1943 hadi Feburuari 1944,ni somo
kwetu kwamba harakati za kutafuta haki,demokrasia na usawa hazifanywi kwa
kukurupuka kwa kujumuisha nguruwe,mbwa,mbwa mwitu n.k
Wanyama
wadogo wanapaswa kuwa na akili kutambua kuwa wanadanganywa sana na kutumiwa.
Ukitaka kujua,ni kwamba ukihoji maslahi(mapato na matumizi ya shamba la
wanyama) utaitwa, “Traitor” someone who
helps an enemy against his own people.
Wanyama
wengine wakubwa wanajiona “Aloof” bora wako juu sana na wanajiona better than
others, hakuna kuhoji usawa katika kugawana keki ya shamba hili la
wanyama,kufanya hivyo ni kujitakia kifo na kufukuzwa!
Unaweza hata
kunyweshwa sumu au kuuliwa kwa namna yoyote. Kupinga vitendo vya akina Nguruwe
ilikuwa kuleta eti ‘bewilderment’ machafuko kwenye shamba la wanyama,ninyi ni
mashahidi wa haya!
Sasa
kumwondoa binadamu ‘tyrant’ na kumwacha nguruwe kukalia kiti na kufanya unyama
kuliko binadamu,ndiyo mapinduzi gani haya? Demokrasia gani;usawa upi huu?
Faida yake
nini? Kama wapiga debe hawa siyo ‘cunning’ ni nani hawa wanaoongoza kizazi cha
shamba la wanyama katika maangamizi kuliko ilivyokuwa kwanza?
SUGARCANDY
MOUNTAIN iko wapi watu kukaa vijiweni na kupiga politiki huku wakihamasisha
wenzao kufanya machafuko ili eti kufika huko sugar candy mountain?
Jamhuri ya
wanyama,ANIMAL REPUBLIC huru nayenye usawa inakujaje ikiwa akina nguruwe
walishaanza ufisadi wa kuvaa suti za akina binadamu? Suti,ni tabia ile ya
murder of some animals, wakati nguruwe wanaanza kutembelea miguu miwili(rejea
Amri za wanyama) “The Pigs star walking on their two legs” wakajigeuza
wakoloni,sheria zinakiukwa makusudi, wanajiona wao wako juu ya sheria,ila
binadamu ndiye fisadi tu
Kawimbo, “mafisadi”
katamu, lakini waimbaji wake hunuka mithili ya kwapa la ibilisi!
Itaendelea
juma lijalo
0713 324 074
No comments:
Post a Comment