Monday, December 2, 2013

SHAMBA LA WANYAMA(2)



      
BINADAMU dhaifu hawawezi kufanya chochote cha mafanikio yake bila msaada wa wanyama?
Hatavikosi vya usalama katika tawala zilizofanikiwa sana za wanadamu, haviwzi kubaini hatari za milipuko ya mabomu pasipo kushirikisha mbwa,panya n.k ili kudhibiti hatari za magaidi kama al-Qaeda, al-Shabaab n.k
Novemba 29 mwaka huu huu, pal kwenye Uwanja wa CCM Kirumba,Mwanza wakati wa ujio wa Kombe la Dunia(Fifa World Cup Trophy) na Rais Jakaya Kikwete, nikaona polisi na Usalama wa Taifa,wakiwatumia mbwa kunusa kila kiti,kila meza,kila chumba na hata magari yalinuswa na mbwa zaidi ya mmoja,ili kubaini hatari!
Mbwa mdogo wa Usalama, mwnye madoa meusi na meupe,na mkanda shingoni, akang’ang’ania chupa tupu ya Coca-Cola mdomoni mwake!
Alikuwa ndiyo kwanza katoka kunusa jukwaa na vifaa vilivyokuwa jirani,njiani akakutana na hizo chupa tupu zilizokuwa chini, akachukua moja mdomoni mwake na kuanza kuondoka nayo,utadhani alibaini bomu ndani mwake!
Alipomaizi kuwa mbwa Yule alikuwa akifanya mzaha, askari Yule alimpokonya mbwa huyo mwenye cheo hiyo chupa tupu na kuitupa.Mbwa Yule alitaka kuirudia kisha akaendelea na hamsini zake.
Naam, katika sehemu iliyotangulia ya makala haya,tuliona haja na MAPINDUZI katika kizazi cha wanyama(pamoja na jamii ya wanadamu),kwamba mabadiliko katika maisha ni hitaji la msingi wakati wote ili kuboresha maisha.
Mapinduzi yanapaswa kufanywa kwa makini ili kuleta mabadiliko chanya na aslani siyo mabadiliko hasi yatakayoleta majuto baadaye.
Ustawi wa kundi moja la wanyama,wakati mwingine hugeuka janga la kutisha kwa kundi linguine.Ustawi wa samba na mbwa mwitu huleta mauti kwa jamii ya wanyama walao nyasi. Ustawi wa tembo na hata nyati hulta kilio kwa mashamba ya mwanadamu.
Ustawi wa binadamu husababisha karamu kila siku na hivyo wanyama hujikuta wakichinjwa kila asubuhi na jioni.
Hata hivyo, binadamu ni mnyama mharibifu zaidi kuliko wanyama wote(man is only creature that consumes without producing).Binadamu hazalishi chochote yeye mwenyewe, hawezi hata kukokota jembe la kukokotwa na wanyama kazi(plough),hatagi hata yai moja,wala hawezi kurutubisha ardhi anayoiharibu kila siku.
Hii ni kazi ya wanyama ambao hata kinyesi chao ni mbolea safi. Kitu kinachozalishwa na wanyama huishia katika koromeo la binadamu huyu Dikteta na fisadi!
Naam, huu ndiyo uliokuwa mwito wa wanyama kutaka MAPINDUZI dhidi ya udikteta wa mwanadamu. Bahati mbaya mwito wa mapinduzi uligeuka UASI(rebellion) ulioishia kuleta majuto kwamba, “Heri utumwa wa mwanzo kuliko wa sasa!”
Kwa akili za wanyama, walidhani uasi dhidi ya binadamu,haki(justice) ingekuja yenyewe,na maslahi ya wanyama yangepatikana midhali binadamu fisadi alikwisha timuliwa katika umiliki wa SHAMBA LA WANYAMA.
Dhima ya wanyama ilikuwa, “PERFECT UNITY and PERFECT COMRADESHIP IN THE STRUGGLE”katika harakati za kuondokana na minyororo ya utumwa dhidi ya mwanadamu, wanyama waliona binadamu pekee alikuwa adui yao.
Na kwamba wanyama wote walikuwa ndugu na washirika wa kwale katika harakati za kutafuta ukombozi wa kweli(comrades),kumbe walisahau kwamba hata baadhi ya wanyama walitamani kuishi na kunyonya wqanyama wenzao mithili ya binadamu!
Kulikuwa na akina mbwa,hawakuwa tayari kuishi na sungura pasipo kuwakamata na kuwaua ili kupata kitoweo. Paka hawakuwa tayari kuishi bila kuwafukuza panya,mwewe hakutaka kuacha kuwapora vifaranga n.k
Nataka kusema kwamba,ilikuwa kazi ngumu jamii ya wanyama kujenga upendo wa kweli, uhuru wa kweli,haki na demokrasia halisi kulingana na sheria saba(amri)walizojiwekea zenye maudhui kwamba, “ALL ANIMALS ARE EQUAL”
Njozi yao ilikuwa
, “Golden future time… .Tyrant man to be overthrown and the fruitful fields of Tanzania to be trod by beasts- alone!
Wanyama waliota, siku za usoni utawala katili wa mwanadamu upinduliwe na kutimuliwa daima ili ardhi yenye rutuba inayozalisha maziwa na asali ibaki mikononi mwa jamii ya wanyama pekee!
Wanyama wanapotamani kuvunja minyororo ya utumwa ya jamii ya mwanadamu ili kujipatia uhuru kamili, walisahau kwamba miongoni mwao baadhi yao hawakuwa na nia dhati ya uhuru.
Baadhi yao walijiona bora kuliko wenzao, walikumbatia ubaguzi wa nasaba zao, majimbo yao ama mikoa yao,jamii zao na hata koo na makabila yao-ndiyo akina nyau dhidi ya panya,mbwa dhidi yap aka n.k
Walipigia kelele dhuluma ya mwanadamu dhidi ya wanyama,wakasahau MAPINDUZI sharti yaanzie katika fikra na mitazamo yao kwanza,yaani wote wakubali kuthamini usawa na uhuru wa kila mnyama.
Maslahi binafsi ya baadhi ya wanyama kama akina Nguruwe waliokuwa viongozi, ndiyo kilikuwa chanzo cha majuto makubwa,na ubaguzi wa kinasaba,kijimbo na kikabila hata wanyama wakalia kwamba, ‘Heri utumwa wa zamani kuliko wa sasa!
Miongoni mwa wanaharakati katika SHAMBA LA WANYAMA,kulikuwa na “Spies” na ‘Tale-Bearers” wachuuzi wa wenzao,waongo na wanafiki wakubwa,wasemaji wazuri,waliopigiwa makofi na kupata wafuasi wengi wa makundi ya wanyama,hususan wale wanyama wadogo.
Wapiga debe wengi walioitwa ‘Wapiganaji’ ama ‘wapambanaji’ wakatabiri “The existence of mysterious country called, SUCARCANDY MOUNTAIN”.
Nchi ya maziwa na asali ambayo baada tu ya binadamu kupinduliwa,jamii ya wanyama ingekwenda kuimiliki,nayo ni chi ya utamu mithili ya asali. SUGARCANDY MOUNTAIN eti ni Mlima wa vinono, ambako wanyama wangefanikiwa kuishi tu baada ya kufa!!
Eti hii nchi ilikues angani, ikiwa imejaa meza za vinono(sweets) juu kuvuka mawingu!!
Moses, alikuwa mpigadebe wa siasa za uchochezi kuwafanya wanyama wenzake wavunje sheria ili wafe ili rahisi kuifikia ile nchi ya siri katika Mlima wa sukari-SUGARCANDY MOUNTAIN!!
Yeye, Moses hakufanya kazi yoyote zaidi ya kupiga ‘politiki’(Tazama Animal Farm uk 10)licha ya kuleta uongo kwa wanyama, aliwahimiza kumwaga damu ili kufikia ile  sugar candy mountain.
Wakati akifanya haya,yeye Moses alikuwa akivunja sheria walizojiwekea.Alikula akiguguna kwa wizi mkate uliokuwa umechovywa ndani ya pombe(Kumbuka Amri ya 5 ilisema ilikuwa Marufuku wanyama kunywa pombe)huko katika shamba la wanyama la Uingereza!
Ilipotokea wanyama wakapata uhuru,kufuatia utawala wa binadamu kutimuliwa, viongozi hawa wanafiki wa shamba la wanyama walianza kujifanya nao ni binadamu,wakageuza sheria ambazo zilianza kusomeka hivi:
ALL ANIMALS ARE EQUAL, BUT SOME ANIMALS ARE MORE EQUAL THAN OTHERS!”
Wanyama viongozi-akina nguruwe-walikwenda mbali wakaanza kulewa pombe,kuvuta sigara,mtemba, kusoma magazeti ya binadamu kama Daily Mirror n.k
Wanyama viongozi walianza kuvaa suti,hususan za binadamu kinyume cha sheria(Rejea Amri saba za wanyama katika sehemu iliyotangulia)wakafanya vikao ku-compromise na binadamu katika vikao vilivyoandamana na ulevi na ulaji wa nyama za wanyama wenzao!!
Matokeo, wanyama viongozi-nguruwe- waliafiki wanyama wadogo wafanyishwe kazi nyingi za kuvuja jasho,kazi za harubu,halafu ujira ni chakula kidogo-DHULUMA.
Wanyama walioitana,comrades,rafiki,mwanachama ama ndugu,sasa baadhi yao wakataka waabudiwe utadhani miungu.
Jina SHAMBA LA WANYAMA(ANIMAL FARM) wakataka libadilishwe na kuitwa, ‘Manor Farm’ yaani shamba ndani ya jumba kubwa la zamani lenye shamba lililomilikiwa na kigogo “VIP”.
Wenye masikio na wasikie! Inakuwaje wanyama wenye usawa miongoni mwao wawemo ‘VIP(VERY IMPORTANT PERSONS)?
Mwisho wa siku,jamii hi ya wanyama ikaishia kwenye ugomvi mkubwa sna kufuatia tuhuma dhidi yao,wanadamu na wanyama wakarudi kukubaliana kudhulumu wanyama haki zao na demokrasia.
Kitabu hiki SHAMBA LA WANYAMA kiliandikwa Novemba mwaka 1943 hadi Feburuari 1944,ni somo kwetu kwamba harakati za kutafuta haki,demokrasia na usawa hazifanywi kwa kukurupuka kwa kujumuisha nguruwe,mbwa,mbwa mwitu n.k
Wanyama wadogo wanapaswa kuwa na akili kutambua kuwa wanadanganywa sana na kutumiwa. Ukitaka kujua,ni kwamba ukihoji maslahi(mapato na matumizi ya shamba la wanyama) utaitwa, “Traitor” someone who helps an enemy against his own people.
Wanyama wengine wakubwa wanajiona “Aloof” bora wako juu sana na wanajiona better than others, hakuna kuhoji usawa katika kugawana keki ya shamba hili la wanyama,kufanya hivyo ni kujitakia kifo na kufukuzwa!
Unaweza hata kunyweshwa sumu au kuuliwa kwa namna yoyote. Kupinga vitendo vya akina Nguruwe ilikuwa kuleta eti ‘bewilderment’ machafuko kwenye shamba la wanyama,ninyi ni mashahidi wa haya!
Sasa kumwondoa binadamu ‘tyrant’ na kumwacha nguruwe kukalia kiti na kufanya unyama kuliko binadamu,ndiyo mapinduzi gani haya? Demokrasia gani;usawa upi huu?
Faida yake nini? Kama wapiga debe hawa siyo ‘cunning’ ni nani hawa wanaoongoza kizazi cha shamba la wanyama katika maangamizi kuliko ilivyokuwa kwanza?
SUGARCANDY MOUNTAIN iko wapi watu kukaa vijiweni na kupiga politiki huku wakihamasisha wenzao kufanya machafuko ili eti kufika huko  sugar candy mountain?
Jamhuri ya wanyama,ANIMAL REPUBLIC huru nayenye usawa inakujaje ikiwa akina nguruwe walishaanza ufisadi wa kuvaa suti za akina binadamu? Suti,ni tabia ile ya murder of some animals, wakati nguruwe wanaanza kutembelea miguu miwili(rejea Amri za wanyama) “The Pigs star walking on their two legs” wakajigeuza wakoloni,sheria zinakiukwa makusudi, wanajiona wao wako juu ya sheria,ila binadamu ndiye fisadi tu
Kawimbo, “mafisadi” katamu, lakini waimbaji wake hunuka mithili ya kwapa la ibilisi!
Itaendelea juma lijalo
0713 324 074







No comments:

Post a Comment