Monday, November 7, 2011

BERNARD MEMBE HUNA UBAVU KUZUIA USHOGA TANZANIA!!






KATI ya mambo yanayochekesha sana ni “AMRI” ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron,kuziamrisha nchi za Jumuiya ya Madola(Commonwealth) kufanya Mabadiliko ya Katiba,  ili waweke kipengele cha kuruhusu ushoga!
Watanzania, wameonekana kumpinga sana David Cameron,kuhusu ushoga,  wanasahau kwamba nchi yetu haiko huru kabisa, na wala haijawahi kupata uhuru kutoka Uingereza!
Hili ni jambo linalouma sana; na wengi hawataki kuamini kwamba hatujawahi kupata uhuru,kama inavyodaiwa. Hii ni miaka 50 ya uhuru wa bendera.
Hata hivyo, nitapata fursa kujadili jambo hili kwa kina, siku nyingine.
Mimi najua Tanzania haijawahi kuwa huru,na nchi nyingi za Jumuiya na Madola hazijawahi kuwa huru,ndiyo maana tunaburuzwa na Malkia, wanaye akina Prince Charles, wajukuu akina Prince Harry na William na akina Tony Blair, Gordon Brown,David Cameron na wenzao.
 RAIS Barack Hussein Obama, yeye anawaunga mkono mashoga wazi wazi, na nchi za Afrika zinaona mashoga ni uchuro.
Kwa sababu, siku hizi ndiyo uhuru,usawa na demokrasia na Haki za Binadamu zinavyotaka-mashoga nao ni watu.
 Obama, amewateua mashoga na wasagaji kama 150 hivi,katika nafasi za juu serikalini mwake,kwa sababu Marekani yapo majimbo lukuki yaliyohalalisha mashoga na wasagaji kufunga ndoa.
 Afrika, viongozi wanapinga ushoga na usagaji. Sam Nujoma wa Namibia aliwahi kutoa amri,mashoga na wasagaji watiwe mbaroni na kufungwa jela.
   Rais wa Zimbabwe, Robert Gabriel Mugabe, kawafananisha mashoga kama mbwa koko na nguruwe hivi.
Naam, hizi ndizo kauli zinazolalamikiwa sana na mashoga. Na David Cameron, Malkia Elizabeth II na wenzao,wanawaona hawa viongozi wanawapinga mashoga,kwamba ni Madikteta!
 Uganda, kulikuwa na muswada wa kuwasweka rumande mashoga na wasagaji ama wanaojihusisha na ndoa za jinsia moja.
 Na kwamba,mtu akishindwa kutoa taarifa juu ya haya anafungwa jela miaka mitano au saba!
Hapa kwetu, ndiyo tumeamrishwa kubadili Katiba na kuwaruhusu mashoga waoane kwa uhuru pasipo ngebe!!
Askofu Desmund Tutu wa Afrika ya Kusini, alisema ushoga ni kinyume cha ubinadamu,ni tabia mbaya kabisa kuliko ubaguzi wa rangi. Ni kweli kabisa,lakini Kanisa la Anglikana la Malkia na David Cameron, linaona ushoga, ni bomba tu!!
Shirika la kutetea Haki za wafungwa duniani, Amnesty International, lenyewe hupinga ubaguzi,unyanyapaa dhidi  ya mashoga na wasagaji ama wenzi wa jinsia moja.
   Hata hivyo, wanaharakati wa Haki za Binadamu wameiona Afrika imeshindwa kufuatilia watoto wa mitaani na wagonjwa kulazwa wawili wawili vitandaji hospitalini, waafrika wanafuatilia vyombani na vitandani wanakolala mashoga!
 Desemba 23 mwaka jana,nyumbani kwao Luis Moreno Ocampo,( anayewatoa kamasi akina Uhuru Kenyatta siku hizi),huko kwao Argenjina, Jose Maria Di Bello na Alex Freyre,walikuwa wa kwanza kuoana huko Amerika Kusini.

Mapema  mwaka 2007, umefanyika Dar es salaam mkutano wa Kimataifa wa Kanisa la Anglikana, ili kujadili kama ndoa za jinsia moja na ushoga zihalalishwe. Tanzania ilikuwa ‘Pepo ya Mashoga’ siku nyingi!
    Naam, Tanzania ambako  kwa mujibu wa Katiba ya sasa, inasemwa vitendo hivi vya usagaji na ushoga ni kinyume cha sheria, iliridhia Mkutano huo ufanyike Whitesands,  mwaka 2007  kujadili haki za wasagaji na mashoga, ama usawa wa watu wa jinsia zote katika muungano wa hiari(Civil Partnership)  uitwao ndoa.
    Hapa nchini, sheria  inayoitwa ‘kandamizi’  (na mashoga) inaruhusu tu watu wa jinsia tofauti(heterosexual couples) kuoana.
   Katika Ulimwengu ulioendelea, sheria inaondoa kizingiti; inatoa “haki” kwa kila mtu kuoa ama kuolewa anavyotaka na anayemtaka, mradi tu anao umri wa miaka 18; umri wa mtu mzima kikatiba.
    Watu wakubwa sana wameolewa wanavyotaka katika Dunia hii.
  Naam, watu wenye kuheshimika sana: matajiri, wanaoketi meza moja na wafalme wa Dunia.
    Sir Elton John(60) alifunga pingu za maisha na mchumba wake wa siku nyingi, David Furnish(45) Mei mwaka 2005.
Siku hizi, wame 'adopt' mtoto, eti wameasili mtoto, wanalea!
    Alikuwa miongoni mwa watu 700 waliofunga ndoa  za namna  hiyo, mwaka huo. Hatua hiyo ilifikiwa baada ya England na Wales kupitisha sheria ya Ndoa za Jinsia Moja.
     Basi, baada ya  ndoa ya Sir Elton John, kulikuwa na hafla ‘kali’ katika Jumba la kifahari sana.
   Walitumia ukumbi wa karne ya 17 ambao pia aliutumia Prince Charles, wakati anamuoa mpenzi wake wa siku nyingi, Camilla Parker Bowles.
   Camilla na Prince Charles walifunga ndoa Apirili mwaka huo wa 2005.
    Siku ya harusi, Sir Elton John alivalia suti safi, tai nyeupe na miwani  myeusi, akashangiliwa kwa ushindi.
      Ndoa kama hizo zilishafungwa Ireland na Scotland.
  Waziri Mkuu, Tony Blair (wakati huo) aliwapongeza maharusi kwa kufuata sheria zilizowekwa…sheria za ndoa za mashoga.Haki za Binadamu!! Mimi simshangai David Cameron.
    Huo ulikuwa uhuru wa kikatiba wa mataifa ya Ulaya, Marekani, na Afrika Kusini.
 Sasa uhuru huu-Equal Marriage for All- unainyatia Tanzania, maadam Kanisa la Anglikana limeruhusiwa kujadili kitu hiki katika ardhi yetu.Katika mchakato wa Katiba Mpya,lipo wimbi la mashoga na wasagaji,kutaka haki zao.
   Kwa mara ya kwanza, Dar es salaam inakuwa pepo ya mashoga na wasagaji;wakati ulipofanyika mkutano wa Anglican, jijini Dar.
   naam watu maarufu sana katika jamii. Tazama ndoa ya Sir Elton John na David Furnish.
    David Furnish ni mtengeneza Filamu, raia wa Canada, ambaye amekuwa katika lindi la huba na Sir Elton kwa miaka 12 kabla ya ndoa hiyo. Mwaka huo 2005 ‘walifanyika mwili’ mmoja.Walifunga pingu za maisha.
   Waliiunga mkono sheria hiyo ya Ndoa za Jinsia moja kwa vitendo.
     Miongoni mwa waliohudhuria harusi hii ya kukata na shoka ni mamaye Sir Elton John, Sheila, na Babaye wa kambo Fred.
    Wazazi wa Furnish, Gladys na Jack, pia walikuwepo katika tukio hilo. Ndoa ilifungwa kwa kipindi cha saa moja; iliendeshwa na Msajili maarufu sana, Clair Williams, ambaye pia aliifungisha ndoa kati ya Prince Charles na Camilla.
            Miongoni mwa wageni waalikwa, alikuwepo pia Victoria Posh Adam, mkewe mwanasoka nguri wa Uingereza, David Beckham.
            Wengine walikuwa Jay Jopling. Sir Elton alivalia pete ya ndoa ya almasi; halafu wakaingia katika gari la kifahari, Rolls Royce jeusi; wakashusha vioo vya madirisha na kuendelea kupigana mabusu ya tashtiti!
     Sherehe ya harusi hiyo iligharimu takriban Pauni milioni mbili za Uingereza, yaani zaidi ya shilingi bilioni tano  za hapa.
   Walihudhuria wageni 700, wakastarehe ndani ya mahema. Sir Elton John alikuwa rafiki wa karibu wa Hayati Princess Diana Frances Spencer. Aliimba  Candle in The Wind katika mazishi yake mwaka 1997.
   Walikutana na   Furnish kwenye sherehe mwaka 1993 wakapendana. Miongoni mwa kazi zake ni ‘It’s a Boy Girl thing’.
    Nchi zilizokwisha kubali Ndoa za Mashoga ni pamoja na Afrika Kusini, Novemba mwaka 2006, kupitia Muswada wa Muungano wa Kiraia.
     Mchungaji V. Gene Robinson wa Kanisa la Angikana la New Hampshire, alifunga pingu za maisha na Mark Andrew, akawa Askofu wa kwanza shoga katika Ulimwengu.  Angikana ni ‘pepo ya Mashoga’ ingawa Afrika bado wanajidai shingo ngumu.
 Hiki ni kitendo kilichoigawa dunia katika mihimili miwili. Sasa, amri inatolewa watu wote kusalimu amri.
  Kwa sababu  ‘ubishi’ huu wa uhalali ama uharamu wa ndoa za Jinsia moja umefanyika Dar es salaam, na kualika mashoga wa kimataifa kujadiliana juu ya kuhalalisha ndoa hizi, ni wazi Tanzania tayari imevamiwa!
    Ndoa hizi zilihalalishwa Ulaya Kaskazini tangu mwaka 1990, kisha zikavuka Bahari ya Atlantic. Marekani, majimbo mengi yamebadili sheria kuridhia ndoa hizo. Limo Jimbo la Vermont, Connecticut. Majimbo mengine kama San Francisco na Massachusetts hutoa leseni kwa mashoga na wasagaji kuoana.
      Ndoa hizi zimeruhusiwa pia Canada, New Zealand, Ujerumani, Denmark, Norway, Sweden, Finland, Uhispiania Ubelgiji na Uholanzi.
    Katika Afrika, mwaka 2006 Mahakama Kuu ya Afrika Kusini ilisema Katiba ya nchi hiyo ilikuwa haiwazuii watu wa Jinsia moja kuoana.
   Basi, Waziri wa Mambo ya Ndani, wakati huo, Nosiviwe Mapisa-Nqakula, kufika mwaka 2007 awe amepitia sheria na kuifanyia mabadiliko ili kuruhusu kila mtu kuoa au kuolewa!
 Hata hapa, katiba mya ikikamilika,kutakuwa na huru mtu yeyote kuoa na kuolewa.Tunajidai kukataa,lakini kimsingi tutakubaliana na sera za Sodoma na Gomora,midhali tulishamwasi Bwana Mungu na kukataa amri zake.
  Sheria za Ndoa za kawaida hutoa ruhusa kwa watu wa Jinsia tofauti kuoana.
   Lakini, mashoga na wasagaji wa Afrika Kusini walikuja juu kutaka “usawa” katikama husiano ya kijamii.
  Usawa huu ukiridhiwa basi utatambua muungano wa mashoga na wasagaji; nao watafunga ndoa kisheria makanisani na popote sheria inakoruhusu.
    Kila mtu mwenye umri wa kuanzia miaka 18 na mwenzake wa jinsia yoyote mwenye umri wowote kuanzia miaka hiyo, ataruhusiwa kufunga ndoa, chini ya sheria hiyo.
   Hata wawe wa jinsia moja, mmoja atachagua kuwa mke, mwingine mume; kwa kadiri ya uamuzi wao.
  Mtu mmoaja hataruhusiwa kuwa katika ndoa zaidi ya moja.
            Makanisa yamepewa utaratibu wa kufunga ndoa hizi, na waliooa au kuolewa kabla ya sheria hizi Afrika Kusini, wametakiwa kufuata utaratibu; kukubali ndoa yake au kuomba talaka.
  Ndoa zitafungwa popote, hata kanisani kwa mujibu wa sheria.
    Ndoa itakubaliwa si kwa kubadilishana pete za harusi, bali kwa mtu kumshika mwenzake mkono na kukubali katika kiapo kwamba anakubali kuoana na kuchukuana na mwenzake!
     Hiki ndicho kitu walichokuwa wakijadili wachungaji wa Anglikana, Whitesands, Dar es salaam, mapema mwaka 2007.
Na hivyo ndivyo David Cameron na Ulaya wanavyotaka Afrika ifanye! Mpende,msipende Tanzania itakuwa Sodoma na Gomora! Kwa sababu dunia nzima wanaitawala wao na sasa wanataka iwe Sodoma, sasa mnapinga nini?
Kwa kuwa hata Tanzania tayari wapo wanaume na wanaume waliokwishawekana kinyumba, ni wazi Muswada wa Sheria ya Ndoa ya Jinsia Moja(Civil Union Bill) uko mbioni kufikishwa Bungeni mjini Dodoma,  mwaka na siku itakapofika,siku katiba mpya itakapowapa uhuru mashoga na wasagaji kuoana. Na Uingereza, wanaochangia takriban asilimia 40 ya Bajeti yetu, wanataka  hiyo Civil Union Bill, sasa wanaopinga watachangia kiasi gani kwenye bajeti?
     Na kwa kuwa tunaiga kila jambo kutoka ‘majuu’ au ‘Sauz’ kama tunavyosema, Tanzania iko mbioni kuridhia Ndoa za Wasenge na Wasagaji, maadam hata sasa tayari wameoana kimya-kimya! Hata wanafunzi wa vyuo vikuu hapa…wamewekana kinyumba!
Kenya.viongozi wa madhehebu ya dini wanaipinga katiba mpya kwa kipengele hiki tu cha kila mtu kuwa huru kuoa na kuolewa!
     Ni kwa sababu hii hapa Tanzania, leo kusikia mwanaume akiitwa ‘Anti’ ni kitu cha kawaida sana!
Zamani, hawa walikataliwa na Kanisa la Mitume wa Yesu Kristo, wakaitwa mbwa!
 Kwa Uislam, ushoga ni dhambi ya mauti.Haki za Binadamu zinatambua pia haki za mashoga na wasagaji.
    Leo, Maaskofu(Waangalizi wa Kanisa) ndio wanaoolewa na wanaume wenzao; na mjadala wa Dunia nzima unaletwa Dar es salaam  kutafuta suluhu ama kutowaonea haya mashoga  hawa hata wanapohudumu madhabahuni.
     Kwa kuwa Haki za Binadamu zinawatambua mashoga kuwa ni binadamu wa kawaida wanaostahili haki zao, basi wanastahili watu hata wa Jinsia moja kuoana kama wale wa Jinsia tofauti wanavyooana, bila ubaguzi.
   Ni kwa sababu hii, wanaume wanaofanya vitendo vya kuingiliwa kimwili na wanaume wenzao, wanapata nguvu kubwa za kudai haki hiyo, hata kama baadhi ya watu bado wanawashangaa ama kuwaonea kinyaa!
    Tayari tunao hapa Tanzania wanaume mashoga wanaofanya biashara ya ngono.
Hawa wanaitwa ‘Kaka poa’ na hushindana vilivyo na ‘madada poa’ katika biashara hii haramu.
   Aliyekuwa   Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Simon Sirro, kabla ya kuhamishiwa Dar, alipoulizwa na Safu hii kwamba anawezaje kupambana na wimbi hili akasema,
 “Tunapowakamata, tunawafungulia mashitaka ya uzembe na uzururaji…sheria zetu ni dhaifu sana kuwashitaki hawa  makahaba na mashoga, kuhusiana na makosa yao halisi”, alisema. Naam sheria za sasa ni dhaifu kuwatoa kamasi mashoga!
    Naam, ‘kaka poa’ wapo katika miji mingi hapa nchini,  kasi ya kuwatia mbaroni ili wafunguliwe mashitaka, ama ni ndogo sana, au haipo kabisa. Ukikutana nao hawa, utadhani akinamama…wamebadili tangu mavazi hadi sauti!
    Kidogo kidogo  jamii imeanza kuwazoea hawa na baada ya muda Bunge linaweza kuridhia ushoga na usagaji! Alichosema Cameron ni hakika na kitakuja kutokea, ingawa tunabisha.
Kwa sababu gani serikali iliridhia ushoga kujadiliwa Dar es salaam, kama si kuanza kuukaribisha? Katiba mpya itaacha kuwapa kibali mashoga kufunga ndoa?
     Kwa tabia ya nchi yetu kushabikia kila ‘uchafu’ unaoletwa nchini, wimbi la ushoga na usagaji limeanza kushabikiwa na vijana, wakiwemo wa vyuo vikuu, ambao tayari wamewekana kinyumba ili kuridhisha nafsi zao, ama ili kuwa huru zaidi.
     Kwa sababu tayari watu maarufu sana kama Sir Elton John wamefunga ndoa za fahari sana; tena wamepongezwa na watu ‘wazito’ sana kama Tony Blair, Tanzania ya wapenda kuiga kila kitu  cha ‘majuu’ iko hatarini sasa kumezwa na gharika la ushoga kuliko nchi yoyote ya Afrika Mashariki.
   Na akina dada warembo wataanza kukataa kuolewa ili wapate muda wa kuwaoa wanawake wenzao, ili kusagana.
            Kwa kuwa ushoga na usagaji ‘hupigiwa debe’ na wanaharakati wa Haki za Binadamu wakiwemo wasomi hata wa Vyuo Vikuu; na kwa kuwa Makanisa yameanza kuruhusu mashoga kuhubiri madhabahuni, kumbe dhambi hii ya zamani “Soddomite” imetakaswa kwa damu ya wanaharakati hawa wa Haki za Binadamu!
     Kwa kuwa Tanzania suala la maadili liliachwa kuwa ajenda za kidini; kwa kuwa dini hususan hizi za wageni zimehalalisha usagaji na ushoga, basi vijana wengi wako hatarini kugharikishwa na tamaduni hizi za kishenzi sana kuliko wakati wowote.
    Kwa kuwa ungalipo muda kitambo, kabla ya Muswada wa Ushoga kupelekwa Bungeni, ni wakati mwafaka sasa jamii kutilia mashaka uovu unaokuja kama moja ya haki za Binadamu.

    Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe yeye ametangaza kuwapiga makonde mashoga watakaoleta ‘domo-kaya’ kudai haki zao nchini mwake!
  Mugabe atazamwe kama mpigania haki au Dikteta anayekandamiza uhuru wa watu?
Mimi ni Mwa-Adventista wa Sabato,namwona Mugabe kama shujaa. Lakini wangapi wanamwona Dikteta,kuwaita mashoga nguruwe? Yawezekana hata wewe,sasa wampinga nini Cameron juu ya Tanzania kuwa na mashoga?
    Lakini,  Mugabe anatazamwa kama Mhafidhina na dikteta zaidi kuliko kuwa mtu wa kisasa zaidi anayekwenda na wakati…yaani kwenda na wakati ni kuruhusu ushoga au kuwa shoga, midhali unafurahi na unaridhika kuwa hivyo nafsini mwako!
    Dalili ya mvua ni mawingu.
Kwa kuwa jamii iko katika kipindi cha mpito cha kuwazoea mashoga na wasagaji, basi Tanzania inaanza kuwa ‘pepo’ ya mashoga na wasagaji, siku katiba mpya ikianza kutumika,na mashoga waweza kupata haki na uhuru.
    Mkutano wa Waanglikana uliojadili ushoga, ni dalili kwamba jamii inaanza kushindwa kukememea vitendo hivyo.
 Madhehebu kadhaa ya Kikristo yamegawanyika sana juu ya ushoga na usagaji.
    Leo, viongozi wa kidini waliodhaniwa kuwa watu wa maadili,  ndio wanaoongoza kulawiti. Maadili ya kidini yalidhaniwa yangeiokoa jamii katika maangamizi, kumbe jamii inaanza kutumbukia shimoni.
     Hata Tanzania tunao akina Elton John, David Furnish na   V. Gene Robinson; watu wenye mvuto katika jamii, ambao tayari wameanza kuwavuta vijana wetu katika pepo za ushoga na usagaji.
    Kama hazitachukuliwa hatua za haraka za kukemea hali hii, wakati wowote na siku yoyote, si Dar es salaam tu, bali hata vijijini, tutashuhudia ( hata kwa njia ya televisheni) harusi za fahari sana za mashoga na wasagaji(watu maarufu sana; tena matajiri) zikifanywa kwa mbwembwe ili kuikoga jamii inayopinga  dhambi hii ya miji ya uwanda wa Sodoma na Gomora.
   Kwa kuwa tunao wawekezaji kutoka Ulaya, Marekani na Afrika Kusini, ambako ndoa za Mashoga na wasagaji ni halali, basi tusubiri kuona vijana wetu wakija na wachumba wao kutujulisha kuwa siku ya siku watafunga ndoa na wanaume wenzao!
 Sijui utamaduni wa mahari utaendelea?  
Kama sivyo, tunajiandaaje kupambana na Haki za aina hii za ‘Ndoa za Jinsia zote’ zikiwemo za mashoga na wasagaji?
 Je, Katiba Mpya itaepukaje kuwapa uhuru watu wa jinsia moja kuoana?
Tumewasikia maaskofu nao wakisema wanataka katiba mpya, sasa wasije kesho wakaipinga-wajiandae kufunga ndoa za mashoga makanisani!
Hii ni Sodoma na Gomorah, na kila mmoja anapaswa kujua kwamba hizi ni SIKU ZA MWISHO, huu ni MWANZO WA MWISHO-DUNIA INAKWISHA!!
    0754/0786- 324 074

No comments:

Post a Comment