Wednesday, June 27, 2012

VITA JERUSALEM YA KALE HADI MPYA


      
KABLA ya kuendelea na tukio la Makomando 100 wa Israeli kuwakomboa mateka wao, Entebbe, Julai 4mwaka 1976, tuangalie tukio la juzi la ugaidi,Mombasa.
Mombasa,juma lililopita, magaidi waliua watu wasiopungua watatu katika Hoteli moja, walipokuwa wakitazama mechi ya Soka,kati ya Italia na England.
Aghalabu, matukio ya kigaidi yamekuwa yakitokea katika Jiji la kitalii la Mombasa,katika Pwani ya Kenya.
 Novemba 28, mwaka 2002,magaidi wa Kipalestina walishambulia Hoteli ya kitalii ya Paradise iliyoko Kikambala,takriban kilomita 25 kutoka mjini Mombasa, wakaua watu.
 Magaidi hao hao walijaribu kuirushia kombora ndege ya Israeli ya Arkia Airlinesiliyokuwa ikiruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Moi, hapo Mombasa. Jaribio hilo la kigaidi halikufanikiwa.
Naam, nataka msomaji amaizi kuwa vita baina ya Israeli na Wapalestina, vilishapiganwa maradufu katika ardhi ya Afrika Mashariki.Msukosuko wa Mashariki ya Kati ulishaleta dhama kubwa katika Dunia nzima.
Agosti 7,mwaka 1998,Balozi za Marekani Tanzania na Kenya zilishambuliwa na magaidi wanaohisiwa al-Qaeda, na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 200.Hawakuwemo Wazungu wala Mayahudi, bali Waafrika tu.
 Kampala, haikulipuliwa wakati huo,kwa sababu ndiyo kwanza vikosi vya Marekani vilikuwa na program kamambe ya mafunzo ya kijeshi mjini Kampala,kumbe Kampala ilikuwa, “More alert” kuliko Nairobi na Dar.
Naam,vita kati ya al-Qaeda Israeli kwa upande mmoja, na kati ya Waarabu na Marekani na Ulaya  na wajomba zao Israeli,kwa upande wa pili,havina mipaka ya Kijiografia.Vita hivi vitadumu muda mrefu,kama tutakavyoona mbele ya safari.
Uganda, wakati wa Dikteta,Field Marshal Idi Amin Dada,iliwasaidia wateka nyara wa Kipalestina kufuatia urafiki wake na Waarabu, na ni uadui mkali  kwa Israeli na Magharibi.
Turejee kidogo Entebbe,usiku wa kuamkia Julai 4,mwaka 1976.Muda kitambo baada ya makomandoo 100 washirika wa Mossad,kumtia adabu Amin,Marekani walituma ndege Uganda,naam Entebbe, ili kuwasaidia majeruhi wa Operesheni ile kamambe.
 Unajua, maofisa 53 wa Ubalozi wa Marekani walishikiliwa na wanamgambo wa Kiislam mjini Tehran,huko Iran.
Wateka nyara wa Kipalestina waliuliwa katika tukio hilo la Entebbe, na kabla ya kukumbwa na mauti walisikika wakitaka Israeli iwaachie huru Wapalestina 40 walioshikiliwa nchini Israeli.
Hadi sasa akina Mahmoud Abbas na Benyamin Netanyahu, wanazungumza hay ohayo hata baada ya kifo cha Yasser Arafat.
 Naam vita vya kisasi vya miongo mingi.Hadi sasa Israeli napambana na wanamgambo wa Kipalestina, na wakati mwingine ndege zimetekwa ama zimejaribiwa kulipuliwa angani-VITA VYA KISASI.
 Waama, nipende kusema basi kwamba,Mossad ni majasusi hodari duniani kupambana na uadui wa Waarabu wengi duniani. Unajua kuna Waisraeli milioni nane tu huko Israeli?
Kamanda wa Operesheni ya Entebbe, Muki Besta, alikiri kwamba Operesheni ya Entebbe ilifanikiwa kufuatia ukusanyaji wa data nyingi na muhimu wa Mossad.
Msomaji wangu, Nyalapa, aliniuliza Mossad walipataje ramani ya Entebbe hadi kuweza kushambulia ngafla na kuokoa mateka?
 Hata kama Israeli waliujenga uwanja huo wa ndege wa Entebbe,bado wangeweza kuingia Uganda na kupiga picha muhimu na kujiondokea,pasi na kushtukiwa.
Katika nchi za watu wazembe,wasio na uzalendo,wapenda rushwa na wazalendo wa matumbo yao wenyewe,  Mossad, CIA,MI5,MI6,BOSS la Makaburu ama majasusi wengine wangeweza kufanya lolote na kuondoka,kwa nguvu ya pesa,ama kwa kutumia ulegefu wa fikra.
 Ungedhani, hawa ‘NJAA TUPU’ wanaohujumu fedha za umma katika Halmashauri zetu, wangeweza kulinda maslahi ya watu?Na wengine hupiga kelele nyingi  za hasira,kwa kuwa matumbo yao yangali na njaa! Hasira hutuka tumboni mwa wenye njaa!!
 Ulimwengu wa Kiarabu unasalitiana mno siku hizi. Miaka ya 70 Waarabu walishikilia uchumi wa Dunia kwa silaha moja tu-Mafuta.
Mchora katuni wa Kidachi aliwahi kuchora Mwarabu akiwa kawaweka ‘Chini ya Ulinzi’Wakuu wa Mataifa babe sana Ulaya na Marekani kwa kutumia “Pampu” ya mafuta.
Mafuta ni silaha ambayo siku hizi imesalimishwa Magharibi na Mwarabu mwenyewe,wanaobisha wanakiona cha mtemakuni,nao ni Saddam Hussein,Gaddafi na wenzao.
Mwaka 1976, Ujerumani iliongozwa na Kansela Willy Brandt,Ufaransa iliongozwa na Rais Georges Pompidou,Uingereza ilikuwa chini ya Waziri Mkuu,Edward Heath na Marekani ilikuwa chini ya Richard Milhous Nixon,kabla ya kashfa ya ‘Watergate’. Unaifahamu?
 Unatazama nini kuona viongozi hawa kuwekwa chini ya ulinzi kwa pampu ya mafuta ya Mwarabu,mwaka 1973? Bila shaka,utaona baada ya hapa hawa mabepari wakifanya juu chini kumpora Mwarabu mafuta,kwa kutumia kila njama, hapo upo?
 Nilikwishaandika katika safu hii,kwamba makampuni makubwa sana ya mafuta,”SUPERMAJORS” kutoka mataifa haya na mengine rafiki, yalishafanya Mapinduzi hadi kushikilia siasa za mafuta(Oil Politics) za Mashariki ya Kati.
  Lengo ni kuishikilia ‘silaha’ hii iitwayo, Dhahabu Nyeusi. Viongozi wa Saudi Arabia,Irak, Abu Dhabi,Kuwait,Libya na Algeria, ama wamepinduliwa na kufumbwa midomo, ama wamewekwa mfukoni,waachane na misimamo mikali ya Waarabu.
 Unajua sasa,ni kwanini Iran, Syria,Yemen,Misri na wenzao wamefanyiwa ‘ukarabati’kwa kisingizio cha Demokrasia na Haki za Binadamu,wengine watauawa tu.
 Angalia uhusiano wa Paka na Panya kati ya Urusi ya kale(USSR)na Marekani,Venezuela ya kichwa maji Hugo Chavez,Nigeria,Uingereza, Indonesia,China, Mexico ya madawa ya kulevya na Ecuador. Hizi ni nchi za mafuta.
Maskini, Yoweri Kaguta Museveni, nchi yake itakapofika katika kilele cha uzalishaji wa mafuta, na akawagomea wakubwa hawa,utawala wake utakuwa hatarini maradufu,kuliko sasa polisi wanapowatomasa wanawake matiti,wakubwa wamemnyamazia tu.
  Wee washikie wakubwa bango la mafuta,utakiona cha mtema kuni.Marekani na washirika wake wa NATO ni ‘rafiki maslahi’ na aslani, hawana udugu na mtu masikini; hawafiki Somalia wala Syria,kama hakuna almasi,dhahabu,gesi ya kutosha na mafuta.
  Unapokuja mzozo wa Waarabu na Israeli, Marekani na wenzake hujidai hawaoni uvunjaji wa sheria Israeli maana kuna kanchi kadogo ka mchanga mtupu-wanakodolea jicho nchi za Waarabu,kuna mafuta chini ya ardhi.
  Mwezi Feburuari, tarehe 21 mwaka huu,niliandika katika safu hii kwamba hata Vatican City,Makao Makuu ya Kanisa Katoliki walishakubaliana na Israeli uhusiano wa Kibalozi. Ilikuwa Desemba 30 mwaka 1993.
 Gidion M. alikuja na jina la makubaliano hayo kuwa ni ‘FUNDAMENTAL AGREEMENT’lengo ni kufungua mazungumzo zaidi kati ya Mayahudi hawa na Kanisa Katoliki,lengo ni kukomesha ‘kiherehere’ cha Mwarabu.
 Vatican wanapoungana Marekani,Israeli na Ulaya iliyokuwa dola ya Rumi wakiungana pamoja na Israeli,maana yake ni kwamba Ulimwengu wa Kiarabu utasimama peke yao?
Wengine wanasema Urusi na China. Hawa nao ni wafanyabiashara wa mafuta tu-wanapopewa zabuni ya faida kubwa Mwarabu akipigwa kinyama,watakataa? Usiseme Syria,hakuna unono kama Iran bwana!
 Mwarabu yuko hatarini,kutekwa na kubinywa katika dini yake,utamaduni wake na uchumo wake uliomo katika mapipa ya mafuta ghafi.
 Mzungu anapata ushindi mnono katika medani za kijeshi na siasa, ‘bao la kisigino’ linafungwa,wakati Waarabu hawako tena pamoja,wamefungwa OPEC.
 Unabii wa Ufunuo 9 ulishatimia zamani. Kwamba,nguvu za wanamgambo wa Kiarabu zilizoitesa Ulaya miezi mitano ya kiunabii(miaka 150) hazipo tena Tazama Ufunuo 9:1-11.
 Ottoman Empire haipo, Istanbul siyo tena mji wa Waarabu,ni mali ya Mzungu, adui wa Mwarabu,ndiyo maana Uturuki na Syria  ni mahasimu tu.
 Kulingana na Unabii wa kitabu cha Ufunuo 13,Ulaya na Marekani zitapata ushindi dhidi ya dola za Mashariki,na wataunda Umoja na serikali yenye kuwabagua watu wasiowapigia magoti, watawafanya kama Sadaam, Osama ama Gaddafi, watu watafungwa maisha kama Carlos The Jackal, wengine watawekewa vikwazo vya uchumi(Tazama Ufunuo 13:15).
Umoja wa Mataifa(UN) ullishashindwa kutoa maamuzi ya haki uwanjani-Marekani,Israeli na Ulaya wanacheza ‘rafu’ sana lakini hakuna hata mwamuzi wa pembeni kunyanyua kibendera! Hujipendi?!
Hii ni AJENDA YA SIRI.Al-qaeda,al-Shabaab,Black SEPTEMBER na magaidi wa Kiarabu mwisho wa siku watatokomezwa na vikosi hivi vya CIA,FBI,MI5,MI6,MOSSAD na hata KFB la Urusi likijai kuwasaidia Iran,litauza siri Tel Aviv ama Pentagon.
Asilimia 80 ya Waisraeli wanaabudu dini ya Kiyahudi na  asilimia 15 ndiyo Waislam wa madhehebu ya SUNNI.
Israeli ina watu milioni nane na ardhi ni finyu. Ilijitangazia uhuru Mei 14 mwaka 1948 katika uadui mkali dhidi ya jirani zake Misri,Jodan,Syria,Irak na Saudia.
Jerusalem ilishagawanywa Mashariki na Magharibi, na hapa ndiyo kitovu cha uadui na vita. Vita vilivyokuja kupiganwa hadi Rntebbe Julai 3,mwaka 1976 ili kuwakomboa mateka 103 wa Israeli,tumewaona makomandoo 100 walioandaliwa vema na Mossad wakimkomesha Mwarabu na rafiki yao Amin Dada.
Naam, vita vya dakika 90 tu, The 90 minutes at             Entebbe. Kwa Israeli, Waziri Mkuu anayekuliana na Waarabu ili kuleta amani anauliwa kama Yizak Rabin aliyepigwa risasi Novemba 4 mwaka 1995.
Itaendelea
0786 324 074
 

No comments:

Post a Comment