Thursday, July 12, 2012

vita hadi Jerusalem Mpya-4



Katika Biblia, Ufunuo wa Yohana 17:13 husema kwamba, Wafalme wa Dunia sasa hufanya majadiliano, ili kumrithisha mamlaka yao Mfalme mmoja tu Duniani.
Ufalme ujao Duniani, huoneshwa kwa mifano ya “Mwanamke” aliyebebwa na Mnyama, ambaye katika makala zilizotangulia,tukaona mwanamke huyu aitwaye, Goddess Roma, akiwa nje za ofisi za Bunge la Umoja wa Ulaya,huko mjini Brussels.
Makao Makuu ya serikali hii mpya, Gideon M. anasema yatakuwa Jerusalem, lakini mimi nasema yatakuwa mahali kilipokuwa kiti cha enzi cha utawala wa Rumi ya kale.
Hata hivyo,tujadili namna Umoja wa Kujihami wa Ulaya Magharibi(NATO) walivyoanza kuuvuka Mto Frati na Tigris ili wajielekeze Mashariki,ilikokuwa iliyokuwa Dola ya Kisovieti,USSR.
Naam, tujadili namna “Mto Frati” ulivyoanza kukauka,ili kutengeneza njia kwa madola ya Magharibi kuzitwaa milki za Mashariki, ili kuzilazimisha kujiunga nao aidha NATO, ama Umoja wa Ulaya(EU),na Soko lao la Pamoja, European Common Market.
Mhariri wa Jarida la Executive Intelligence Review la Marekani, Edward Spannus, amesema vita vinavyochochewa sasa na Marekani na Uingereza huko Syria,hatimaye vitakuwa VITA VYA TATU VYA DUNIA!
 Uingereza,Marekani na washirika wao wanawaunga mkono waasi wa Syria,na Urusi na China wanamuunga mkono kiongozi wa nchi hiyo, Bashir al-Assad.Sasa, inasemwa,mwisho wa siku Marekani na washirika wake wataingia vitani dhidi ya Urusi na Uchina,na hivi ni vita vya tatu vya Dunia?
Biblia, katika Ufunuo 16 inasema vita vya TATU VYA DUNIA ni Har Mageddon, ambamo Mungu atapingwa kwa nguvu za mashetani na mawakala wao,Freemasons,na malaika toka mbinguni watakuja kusimamia mabambano ili kulinda HAKI NA UKWELI Duniani.
 VITA BARIDI vilikwisha mwaka 1991 Desemba, baada ya Russia,Kazakhstan na Belarus kuwa mataifa huru. Baadhi ya nchi kama Georgia na nyingine tayari zimekuwa washirika wa NATO.
Tunaona JAPAN na mataifa mengine ya Mashariki wakiungana na M arekani na washirika wao. Kile kimbembe kilichowapata Marekani zama za vita Baridi,kinapungua sana siku hizi,na mataifa yanayoitishia NATO yanashambuliwa,na mengine yalishapinduliwa na viongozi wake kuuliwa kama tulivyoona katika makala zilizotangulia.
George Herbert Walker Bush ambaye tumuite “Bush Baba(sasa ana umri wa miaka 88) na mwanaye George Walker Bush(65) wamepigana vita vya Ghuba  vya kwanza na vya pili na kufanikiwa kumpindua Saddam Hussein na kumuulia mbali,huko kandoni mwa   Mto Frati.
Jambo hili la vita vya kwanza vya Ghuba na vya pili na mapinduzi kisha kuhukumiwa kifo Mtawala wa Irak yenye Mito Frati na Tigris, ni utimilifu wa Unabii wa “Kukaushwa” kwa Mto Frati, ili njia itengenezwe kwa Wafalme wa Mashariki kuungana na Magharibi,ili kufanya shauri la kumrithisha Kiongozi      Mmoja wa Dunia nzima!
 Tumeona kwamba Muammar al-Qaddafi aliyetaka kuwapinga naye amepinduliwa na kuuawa, kisha Carlos The Jackal na “Magaidi” wengine wamefungwa jela na wengine wameuliwa.
Hao wanaoitwa magaidi,ni wapinzani wa ubeberu wa Magharibi, kwa staili ya kulipua mabomu!
Mataifa ‘bishi na tukutu’ yaliyosalia sasa ni Iran na Korea Kaskazini,iliyoanza kufanya majaribio ya ya silaha za Nyuklia Oktoba 9,mwaka 2007.
 Hata sasa, ingalipo “Homa ya Dunia” mara hii siyo VITA BARIDI vya Ubepari dhidi ya Ukomunisti, bali ubepari dhidi ya NYUKLIA inayomilikiwa na Madola machache ya Mashariki kama Iran na Korea.
Syria inashughulikiwa, sasa na kama lisemavyo Executive Intelligence Review,ni VITA vya aina yake vya kuwatiisha wenye msimamo tofauti na Marekani, Israeli,Ulaya namfumo wa dini moja unaoandaliwa kushita mamlaka ya Dunia nzima.
 Hakika, sasa tunajua,baada ya Saddam kuuawa, alifuata Gaddafi na Osama bin Laden na atafuata huyo Bashir al-Assad wa Syria na wenzake, kama watazidisha upinzani.
Walianza kuambiwa wasaini mikataba ya kupunguza silaha. Mikataba hii ilianza tangu Agosti 5, mwaka 1963,Russia, Marekani na Uingereza walipotiliana saini mkataba wa kuacha majaribio ya Nyuklia baharini,ardhini na angani.Huu ni Mkataba wa mjini Moscow,Urusi.
Urusi na Marekani walitiliana saini tena kuacha Nyuklia Januari 27,mwaka 1967, tena Uingereza na Russia wakatiliana saini Julai Mosi mwaka 1968 na Mei 26 mwaka 1972 Marekani na Urusi wakaingia mkataba mkubwa uitwao, Strategic Arms Limitation Treaty(SALT- 1), NI HUKO Moscow,kwamba baada ya miaka mitano waache kutengeneza Misaili zenye kuweza kulenga shabaha kutoka Bara moja hadi linguine.
 Haya mamisaili yanaitwa, Intercontinental Ballistic Missiles(ICBM)wakaifanyia marekebisho mikataba hii 1974 hadi Septemba 1997.
Mwaka 1978 iliyokuwa kambi ya Northern  Atlantic  Treaty Organization(NATO) ikiongozwa na Marekani ilikuwa na hayo makombora ya masafa marefu ya ICMBs 1,054 wakati ile Kambi ya Mashariki ya Warsaw Pact( Poland) ilikuwa ikiongozwa na Urusi ,ilikuwa na makombora hayo 1527.
Ukitazama Military Balance wakati huo utaona NATO walipokuwa na manowari za kivita(SLBM) 656,Warsaw Pact walikuwa nazo 845. NATO walikuwa na ndege za kivita 387,Warsaw Pact wao walikuwa na ndege 135.
Nataka kusema kwamba,  Kambi ya Urusi ya Mkataba wa Warsaw ilikuwa na nguvu kuzidi NATO ndiyo maana kulifuatwa mikataba mingine kama SALT-2 uliotiwa saini Vienna, Austria  Juni 18,mwaka 1979.
Kila upande ulikubali kusitisha kutengeneza makombora hayo na mabomu zaidi ya 2,400,na makombora ya ICBM 1,320 yasivukwe kwa kila upande.
Mkata huu wa SALT 2 uliingia doa wakati Urusi ilipoivamia Afghanistan Desemba, mwaka 1979 Rais Jimmy Carter akaacha kuamini Mkataba huo. Osama Bin Laden alianza kulelewa na Marekani wakati huu ili awapinge Warusi huko Afghanistan.
Baadaye aliwageuka,kama       Gaddafi naye alivyowageuka.
NATO pia walikuwa na magari ya  kubeba silaha za nyuklia zenye kulenga shabaha tofauti, Multiple Independently Targetable Re-entry Vehicle(MIRV) kama 1,046 wakati Mashariki walikuwa na 140.
Desemba 8,1987 makombora ya masafa ya Kati nayo yakawewa Mkataba wa INF huko Washington baina ya Urusi ya Mikhail Gorbachev na Ronald Reagan wa Marekani.
Ipo mikataba mingine kama START 1 na START 2 ya Januari 3, 1993 iliyosainiwa Moscow,na ipo marufuku ya majaribio ya Nyuklia ya Septemba 24 mwaka 1996(CTBT) pia kati ya Russia na Marekani ili kukataa milipuko ya Nyuklia.
Huu mkataba mwaka 2000 ulitia saini na nchi 160,na baadaye Oktoba 15 mwaka huu 2000 mkataba huu ulipata nguvu.
Kuna madhara mengi ya kuvuja kwa nyuklia kama yale ya  kinu cha Chernobyl, huko Ukraine siku hizi  Aprili 26 mwaka 1986 karibu na Kiev.
Watu 31 walikufa,lakini hata sasa Japan vinu vimelipuka na Ulaya vimelipuka na kuleta madhara makubwa kwa afya za watu sababu ya mionzi ya sumu inayoleta saratani kwa watu.
Septemba 30  1999 ajali nyingine ilitokea Tokoimura,Japan wakati wanarutubisha madini ya Uranium. Hata Tanzania tukianza kurutubisha Uranium na tukaenda kinyume na Marekani na Ulaya,utaona watakavyotuijia.
Marekani iliwahi kupiga mabomu ya Atomik B-26 katika Hiroshima,Japan Agosti 6,mwaka 1945 kisha siku tatu baadaye wakapiga NAGASAKI.Haya ni mabomu yaliyohitimisha vita vya Pili vya Dunia.
Baada ya hivi vita,Kambi ya Mashariki ilikuwa na majeshi 1,303,000 dhidi ya 1,175,000 ya NATO. Nato walikuwa na vifaru 11,000 dhidi ya 26,000 ya vile vya Warsaw Pact. Madege ya vita NATO walizidiwa kwa takriban ndege 2000. Ndiyo maana ililia mikataba.
Sasa, kiama cha SEPTEMBER 11,2001 pale WTC kilicholeta kifusi kilichojaza ekari 16,na kifusi chenyewe cha WTC kilikuwa na uzito wa tani milioni 1.2 hapo walipoita, ‘Ground Zero’ ndicho chimbuko la visingizio vingi vya kuyakomesha mataifa korofi, hasa ya Kiarabu ambayo ni adui wa Israeli.
Marekani inaendesha kinachoitwa VITA DHIDI YA UGAIDI kwa ushirika na Ulaya na Israeli,ili kuwakomesha Waaarabu wenye msimamo mkali ili wasalimu amri. Hivi ni vita vitakavyoendelea hadi Yesu anapokuja mara ya pili duniani.
 Itaendelea
0786 324 074

No comments:

Post a Comment