Tuesday, July 17, 2012

vita, tangu Jerusalem ya kale hadi Jerusalem Mpya


TUIJADILI ISRAEL, nchi ambayo ina jumla ya watu 757 katika maili moja tu ya mraba.
Jirani za taifa hili babe sana  Mashariki ya Kati na mshirika wa Mataifa ya Magharibi ni Lebanon, Syria ambako vita vya kumwondoa Al Assad vinapamba moto,Ukanda wa Magharibi wa Mto Jordan, Jordan yenyewe, Gaza Strip, na kuna Nchi ya Misri, ambako wanajeshi wamekataa kuheshimu mamlaka ya  Rais mpya, Mohammed Mursi.
Israeli, ina ukubwa wa maili za eneo 7,800. Mwaka 1997 mji mkuu wa zamani wa Israeli, Jerusalem(Yeroo-Shalayim)  yaani mji wa Amani, ulikuwa na wakazi 591,400 sawa lilivyokuwa Jiji la Mwanza,wakati huo.
Tel Aviv, una wakazi 2,181,000. Kuna vikosi vya wanajeshi 172,500. Nchi hii hutumia fedha inayoitwa Shekeli, ambayo miaka michache tu iliyopita, Shekeli Tano zilikuwa na thamani sawa na Dola moja ya Marekani.
 Mji huu wa kihistoria ulijengwa mwanzoni zama za Mfalme Daudi(1004-965 BC), umewahi kutekwa na kutawaliwa na Babeli, Wamedi,Waperizi,Wagiriki,Rumi ambao waliubomoa mji kabisa mwaka 70 AD.
Awali, jiji hilo lilitekwa na Mfalme Nebuchadnezzar mwanzoni kabisa mwaka 605 BC huu ni wakati Nabii Danieli alipotekwa pia na kuchukuliwa hadi Babeli.Danieli aliishi huko uhamishoni hadi mwaka wa BC 530 akafariki dunia.
Nebchadnezzar aliuzingira mji huu na kuutekwa kwa mara ya pili mwaka 598 BC huu ulikuwa wakati wa Nabii Ezekieli, ambaye naye alihamishwa hadi Babeli ambayo sasa iko Irak.
Ezekieli, aliishi Babeli mwaka 593 hadi 570 BC. Mara ya tatu Mfalme huyu aliutekwa Jerusalem mwaka wa BC 586 MJI UKABOMOLEWA kabisa, hadi hapo ulipojengwa wakati wa akina Nehemia.
Waarabu walikuja kuliteka  eneo hilo mwaka wa AD 636; na tangu karne ya 11 Waarabu wamelimiliki eneo hili la Israeli. Hawa ni pamoja na Seljuk, Mamluks na Dola ile ya Ottomans ya Uturuki.
 Uingereza ililichukua eneo hili mwaka 1917, hii ni kudhihirisha kwamba watu wa Israeli wamepata misukosuko ya kutawaliwa na mataifa ya kigeni, na vita vimewaua wengi hadi wakakimbilia uhamishoni katika mataifa mengi sana duniani.
Umepata kuona Filamu iitwayo, ESCAPE FROM SOBIBO?Ukitazama filamu hiyo utaona kwamba Waisraeli hawa wamenja shubiri wakati wa Adolf Hitler, ambaye alikusudia kuwafyeka kabisa katika uso wa dunia.
Awali, baada ya kuchukuliwa mateka mwaka wa BC 586-537 BC Jerusalem ulijengwa upya zama za Ezra, Nehemia hadi kufika BC 404 Mji huu ulishakamilika.
Kwanini Waisraeli wameshambuliwa mara nyingi na wakazoea sana vita? Biblia inatupa jibu kwamba, walimwasi Mungu.
Watu wengi sana hudhani Israeli bado ni Taifa pendwa la watu wa Mungu! Huku ni kuibaka historia kwa kiwango cha kutisha.
Tutazame kwamba, watu hawa(Waisraeli) walimkataa Masihi, wakamchongea hadi akauawa. Yesu, alitabiri maangamizi ya taifa hili, hadi kuwa kwao wakimbizi katika nchi nyingi,kama tutakavyooona.
Wamekuja kurejeshewa taifa  lao Mei 14, mwaka 1948 na Umoja wa Mataifa. Hata hivyo,Waarabu wanapinga vikali jambo hili, kwa kuwa huku kulikuwa kuchukua ardhi ya Waarabu waliyoikalia kwa karne nyingi wakati Waisraeli walipokuwa uhamishoni, mataifa mbalimbali.
 Warejea ,na Umoja wa Mataifa ukawapa eneo hilo ili wakae na Waarabu, wameshambuliwa mara nyingi na Misri, Saudi Arabia,Syria,Lebanon na Irak. Imefanywa mikataba ya amani,bila mafanikio vita vinapamba moto hata leo hii.
Nimejadili Mkataba wa Amani wa Camp     David, wakati ule wa Rais Jimmy Carter,nimejadili mkataba baina yake na Misri,Misri ndiyo nchi yenye ushawishi mkubwa Mashariki ya Kati, nayo sasa Hamkani si Shwari tena.
Unabii unatimia,kwamba nchi za Ulaya na Marekani zinapata nguvu nyingi na zitatawala nchi za Kiarabu.
Vita kati ya Israeli na nchi za Kiarabu vimeanza zamani sana,mikataba ya kulinda amani ilishawekwa mingi sana ikaja kuvunjika. Israeli imeshambuliwa hata wakati wa Siku kuu kama Yom Kippur.
Tumeona katika makala zilizotangulia kwamba Julai 3,mwaka 1976 ndipo waliposhambulia Enttebe,na kuchukua mateka wao.Nimesimulia sana kisa hiki, wengine wananiuliza Entebbe ni mdudu gani?! Poleni sana!
Mwaka 1977 Israeli na Misri walitiliana saini Mkataba wa kuacha vita baina yao kwa miaka 30.
 Hata hivyo, kungali na vita na jiradi zao; kuna “Intifada” naam ni Intifada hadi kiama. Sasa kukosekana kwa siasa tulivi Misri hivi sasa,kunatishia sana amani ya Israeli na Mashariki ya Kati.
Tumemwona Hillary Rodham Clinton akifika Cairo chini ya ulinzi mkali sana kwenda kupoza joto ili vita visizuke, baada ya jaribio la kumpindua Hosni Mubarak(87) na kumtia korokoroni,kuonekana siyo suluhu,baada ya maandamano ya Taharir Square.
 Jerusalem kuna msikiti mkubwa unaoitwa, Al-Aqsa,vita huingia hadi misikitini na katika masinagogi watu hupigwa mabomu na kuuawa.
Israeli, inagombana sana na Chama cha Ukombozi cha Palestina, PLO.Marekani wamejitia kupatanisha mara nyingi sana, bado vita vinapamba moto kila siku, misikitini na mahekaluni watu huuliwa kwa mabomu ya kujitoa mhanga,risasi n.k
Naam, ni vita baina ya Wayahudi na Waislam mjini Jerusalem,kila siku akina Waziri Mkuu, Benyamin Netanyahu na Hayati YasIr Arafat walishakaa vikao, hakuna amani.Hillary Clinton amefika pia Yerusalem lakini hakuna amani na utangamano,ni mtutu wa bunduki tu.
 Sasa inasadikiwa, Kiongozi wa Wapalestina, Yassir Arafat aliuliwa kwa sumu mjini Paris, wanataka maiti yake ifukuliwe na kufanyiwa uchunguzi upya ili kubaini chanzo cha kifo chake-ni vita kila siku.
Mara vita Ukanda wa Magharibi mwa Mto Jordan, Dead Sea ama Gaza Strip huko Peninsula ya Sinai hadi Bahari ya Mediterranean.
Yesu, alitabiri maafa ya Jerusalem ama Yerusalem.Wayahudi walimwasi Mungu karne nyingi wakaungana na mataifa mengine kuabudu miungu na sanamu. Unajua Mungu ni mwenye wivu!
Ibilisi ndiye hasa kiongozi wa hawa taifa la Israeli,kama alivyotabiri Carlos The Jackal, Hugo Chaves, Robert Gabriel Mugabe, na hata Fidel Alejandro Castro Ruz aliwahi kumwita Rais Mstaafu,Bush kwamba ni Shetani!
 Kwa nini? Tazama Luka 21:2-24 na usome pia vitabu vya Isaya,Yeremia na Hosea. Kwa kifupi,unaweza kusoma vitabu hivi Prophets and Kings na Christ’s Object Lessons, katika sura iitwayo, The Vineyard of the Lord, uone Mungu alivyowazira Wayahudi,kwa tabia zao.
Yesu alitabiri Wayahudi kuukimbia mji wao wa Yerusalem, walikimbia uhamishoni wakaangamizwa huko. Tazama Filamu ya ESCAPE FROM SOBIBO uone mateso waliyopata huko, na utaona laana waliyovuna baada ya ukaidi wao; Isaya 27:6
Katika Mathayo 24:15-20 Yesu aliwaonya kutambua kwamba mwaka 70 AD Majeshi ya Warumi yangeubomoa mji, waliambiwa kukimbia wakati huo wakaleta kiburi-waliuliwa wengi hekaluni hadi damu ikavuja kama mto.
Nabii Danieli alishatabiri maafa juu ya Yerusalem,karne sita kabla ya Yesu. Tazama Danieli 9:27 walishupaza shingo zao ngumu wakajidai Mungu angejipendekeza kwao hata wanaposhirikiana na Ibilisi kufanya ukaidi(Yeremia 7:4).
Wayahudi hawa walishakataliwa na Mungu kama taifa lake teule, waliwaua mitume,walimchongea Yesu, waliua wafuasi wengi wa Yesu, Tazama Matendo ya Mitume 6:8-15 na Matendo 7:51-60.
 Ni wakati huu wafuasi waaminifu wa Yesu waliuliwa,wakafukuzwa Yerusalem. Sura ya nane ya kitabu cha Matendo ya Mitume hueleza Wakristo walivoteswa, wakatimkia Ulaya.Wayahudi walimkataa Yesu(Masihi) wakamchagua Jambazi moja aitwaye Baraba(Luka 23:18, Mathayo 27:22).
Kuongozwa na Yesu, walisema afadhali huyo jambazi Baraba kuliko Yesu, na heri wangeendelea kuwa chini ya utawala wa Kaisari wa Rumi kuliko Yesu.
Nataka kusema, Israeli siyo taifa teule la Mungu,na nimetumia Biblia kuonesha ushahidi wa jambo hili.
Tangu mwaka 34 AD walipomuua Stefano na wakawatesa Wakristo(wafuasi wa YESU) Basi wakatawaka Shetani(akina Kaisari Nero)wawatawale(Mathayo 27:24-25) wakajiweka chini ya utawala wa Shetani kama akina Carlos wanavyosema.
 Mungu alishautupa mji huu kitovu cha vita,na Shetani na mawakala wake Freemasonry wanautawala.
Hata hivyo Shetani hawezi kutawala dunia kutokea Jerusalem, atatawala kutokea Babeli ya Kiroho, ambayo ni Jijini Rome,baada ya Washington kukabidhi madaraka yake baadaye siku za usoni.
 Jerusalem ya sasa itaangamizwa kama Babeli,maana hekalu lao na dhabihu zao ni ibada ya sanamu na mizimu,isiyo na maana tena.
Katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana 21:1-8 Nabii Yohana alioneshwa Jerusalem Mpya wenye Amani.Yerusalem wa kale ulishanajisiwa na majeshi na watawala waovu wa dunia.
Katika   Ufunuo 20:7-10 tunaelezwa Jaribio la Shetani na Majemadari wa vita wa kale wakijaribu kuuteka Mji huo wa Jerusalem Mpya.Wamo akina Hitler, Napoleon Bonaparte n.k
Mji huo wa Yerusalem Mpya,huitwa Kambi ya watakatifu Ufunuo 20:9 na Biblia inasema hao majemadari watashindwa,watauliwa kwa nguvu za Mungu.
Tuijadili kidogo, “City Profile”  ya Jiji hili jipya la Jerusalem lililofichwa mahali kusipojulikana. Tusome Ufunuo wa Yohana 21:10 hadi 27. Biblia inasema ni mji halisi, na wala siyo kisasiri ama hadithi za kufikirika(Myth).
Ufunuo 21:16 hutwambia kwamba jiji hili ni mraba,kila upande una urefu wa maili 344.6 hivi. Mji huu unalingana ukubwa na Jimbo la Oregon,huko Marekani,ni kama Colorado hivi.
Katika Afrika Mashariki,ni kama Rwanda na Burundi kwa pamoja. Una ukubwa wa Poland huko Ulaya.
Kimo cha magorofa ya mji ni sawa na urefu wa mji na upana! Hapa ndipo makao ya watakatifu wa Mungu(Yohana 14:2).Kila mkazi wa dunia ana nafasi yake katika majumba yale marefu. Wakazi Bilioni saba,kila mtu anayo sehemu yake katika jiji hilo, isipokuwa mtu akatae mwenyewe,kwa kuhalifu SHERIA ZA MUNGU,Amri 10.
Watu wengine watajenga humo nyumba zao na kuishi(Isaya 65:21-22) wengine watalima mashamba yatakayostawi vizuri.
 Yerusalem Mpya utakuwa na eneo la kilomita za mraba takriban 189,998.7 hivi ni kama Rwanda na Burundi kwa pamoja,kama Cote d’ Ivoire. Mji huu ukubwa wake unazidi Ugiriki, Guinea Bissau, Israeli yote,Italia n.k
Tanzania ina ukubwa wa kilomita za mraba 945,000. Msomaji anaweza kubaini kwamba eneo la Yerusalem Mpya ni kama 1/5 ya Tanzania nzima.
Tujadili kidogo magorofa ya Jerusalem Mpya. Magorofa marefu(SKYCRAPERS) ambayo hakuna hata moja hapa duniani kwa sasa.
Jengo refu kuliko yote hapa Afrika, ni ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Afrika,mjini Addis Ababa, Ethiopia.
 Jengo hilo limejengwa kwa hisani na Wachina,na wamelikabidhi tayari kwa Umoja wa Afrika AU, ambao sasa Mkuu wa Kamisheni yake ni mtaraka wa Jacob Zuma, Bibi Dlamini Zuma. Jengo hilo limejengwa kwa Dola za Marekani milioni 200.
Jengo hilo nalo haliwezi kulingana urefu na magorofa ya Jerusalem utakaoshushwa na Mungu duniani,baada ya Jerusalem wa kale kubomolewa kwa vita kali sana.
Tumeona kwamba magorofa ya jiji hilo yatakuwa na kimo cha maili 344.6 kwenda angani. Kwa mahesabu ya haraka ni kama kilomita 189,998.7 kwenda juu angani.
Kulingana na tovuti za www.worldstallest.com na www.skycraper.com hata jengo pacha la WTC wanalosema lilibomolewa na Osama Septemba 11,mwaka 2001,lilikuwa na kimo cha futi 1,368 tu.
Majengo yote marefu duniani sasa,hakuna lenye urefu wa zaidi ya futi 2000. Kulingana na tovuti hizo,majengo 10 marefu duniani ni pamoja na jengo la Indosat   Telcom huko Jakarta,Indonesia lenye kimo cha futi 1,831. Lilijengwa mwaka 2001.
CN tower la Toronto huko Canada, lina urefu wa futi 1,815 na lilijengwa mwaka 1974. Jerusalem Mpya una majengo yenye urefu wa futi mabilioni.
Majengo mengine marefu yako Moscow,Urusi, Shanghai,China, Iran,Kuala Lumpur huko Malaya,Beijing, Uzbekistan na Kazakhstan haya yalijengwa mashine.
 Huko Giza,Misri yale Mapiramidi anayosema Gideon M.yalijengwa na mikono ya wanadamu,bila mashine wala mitambo. Yalijengwa zamani na yamedumu kwa jumla ya karne 43 sasa, Piramid moja lina urefu wa futi 481.
Kwa kifupi, hakuna jengo hapa duniani litakalolingana na magorofa ya Yerusalem Mpya,yamejengwa na Mungu mwenyewe.
 Ukitaka kujua sura ya Mji huo soma mwenyewe Ufunuo wa Yohana sura nzima ya 21.Biblia inasema hakutakuwa na majambazi, wezi,wachawi,magaidi,majambazi,machangudoa na wasagaji. Hakuna bia wala gongo!
http://t2.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSyID4IligvMKiKtwfcp-1KGTaF1NauOjY6EJROwAK-YCjYTHwL picha ya majengo marefu duniani
 Hii ndiyo sababu watu hawapendi kwenda huko maana hakuna sigara, wala madada poa! Hakuna kiti moto huko. Hakuna majuto Tazama Ufunuo 21:4,8 Mji umejengwa kwa madini safi,barabara ni dhahabu angavu kama kioo(Ufunuo 21:18-21)
Hakuna TANESCO huko, maana ni mchana siku zote(Ufunuo 21:23, 22:5) Hakuna udhaifu,hakuna mbumbumbu na watu dhaifu,hakuna hospitali maana watu hawaugui.
Masharti ya kuingia jiji hili ni kuepuka sifa hizi: Ushoga, uchawi,ibada ya sanamu,utapeli,uongo,ufisadi na uchafu wa tabia(Ufunuo 22:15) Hakuna rushwa na chuki kwa watu na kulipa visasi. Hakuna kuteka nyara na “Kuulimboka” ama ‘kukolimba’ watu huko!!
Hakuna utapeli na uongo,rushwa,kila mtu anatiwa moyo kuchukua uraia wa jiji hilo.Neema ya Yesu iwe nanyi wote,Amina,Ufunuo 22:21.
TAMATI
0786 324 074







3 comments:

  1. Kuwa makini na unachokiandika. Israel kamwe haitaachwa milele, hii ilikuwa ni kwa muda tu. Israel bado ni taifa teule. MUNGU ataliokoa siku za mwisho. Si kwa ajili ya waisrael bali ni kwa ajili ya jina lake mwenyewe...soma Zekaria 10:12,Jeremiah 33:8; Ezekiel 11:17; Romans 11:26.

    ReplyDelete
  2. MUNGU WA ISRAEL KAMWE HAWEZI SEMA UONGO ALISEMA ATAKAE WAPIGA ISRAEL NA YEYE ATAMPIGA KWAHIYO MUNGU WA MBINGUNI NDIYE MUNGU WA ISRAEL .

    ReplyDelete
  3. MUNGU NA AKUBARI KWA KAZI HII YA KUMTUMIKIA

    ReplyDelete