Wednesday, October 23, 2013

mwarabu na mwafrika tosha kukataa ukoloni



                                         


NA CONGES MRAMBA

RAIS MSTAAFU wa Afrika Kusini,Nelson Rolihlahla Madiba Mandela, aliwahi kumkemea George Walker Bush wa Marekani kwamba aliivamia Irak mwaka 2003 ili kupora mafuta.

Madiba, alisema Vita vya Ghuba vya miaka ya 1990 na 2003 vilikuwa vya kupora mafuta.Mataifa makubwa ya Ulaya Magharibi, siku hizi hutumia silaha vitani ili kukamata nishati muhimu kama mafuta,gesi,uranium n.k

Hii ni kufuatia mataifa tajiri ya mafuta na gesi,hususan ya Kiarabu kukaribia kuukata koo uchumi wa Mataifa hayo miaka ya 70.

Tangu Vita vya Pili vya Dunia, mafuta yalipatikana tele na kwa bei poa kwa viwanda na ili kusafirishia bidhaa za mataifa makubwa haya.

Mwaka 1973, wakati ule wa vita huko Mashariki ya Kati,Waarabu wanaozalisha mafuta kwa wingi, walipunguza uzalishaji na kuongeza bei ya nishati hiyo maradufu.

Ongezeko la bei ya mafuta huko Mashariki ya Kati, ni kusababisha chumi za nchi za viwanda kuanza kutetereka.

Ukitaka vita mlangoni kwako,basi anzisha sera za kuzuia chumi za ‘Industrialized Nations’ kukua kwa ufanisi. Utasingiziwa ‘Gaidi’ ili upigwe kwa drones!

Nchi za Kiarabu zilitangaza kuinyima nchi yoyote mafuta kwa kuwa inaisaidia Israeli(Adui Mkuu wa Waarabu),kwa hali hiyo,Marekani,Ufaransa,Uingereza na washirika wao wasingeuziwa mafuta na Mwarabu.

Kwa mara ya kwanza mwaka 1973,Mwarabu alitumia nishati ya mafuta kama “SILAHA MUHIMU” katika siasa za kimataifa.

Nchi wazalishaji na wasafirishaji wa mafuta(OPEC) walikubaliana kupunguza uzalishaji wa mafuta,kasha wakaongeza bei ya nishati hiyo muhimu kwauchumi wa dunia.

OPEC walikubaliana kulinda na kutunza akiba yao ya mafuta,ili kuwatoa kamasi Wazungu!

Bei ya mafuta ikapaa;mgogoro mkubwa wa mafuta,maarufu kama, “THE OIL CRISIS” ukatikisa viwanda vya mabwanyenye,uzalishaji ukashuka maradufu.

Mfumuko wa bei(Inflation) ulikita;viwanda vingine vikafungwa na kusababisha ukosefu wa ajira ulioikumba dunia.

Mwaka 1979 Mfumuko wa Bei ulipanda kwa asilimia 334 kuanzia takwimu za mwaka 1969.

Hii ni kusema, bidhaa iliyouzwa kwa Pauni moja ya Kiingereza mwaka huo 1969,sasa ikauzwa kwa Pauni 3.34. Hali hiyo ilifuatia Waarabu kuzuia mafuta yao kuuzwa Ulaya-ARAB OIL EMBARGO-mwaka 1973,kukaleta kiama cha kutisha kwa Marekani,Uingereza, Ufaransa na rafiki zao.

Mfumuko wa bei(Inflation) usiosemeka ulisababisha bei zikapanda kila kulipokucha,fedha zilikosa thamani mfululizo.

Nataka nikwambie msomaji.Ikiwa ili upate nishati ya kupikia chakula chako(kuni,mkaa,mafuta,gesi n.k) ingekugharimu fedha zinazojaa magunia matatu ya noti za elfu kumi-kumi!

Kwa nini usitumie magunia mawili ya noti zenyewe kama kuni ili kupikia chakula chako,kuliko kununua mafuta au kuni kwa magunia matatu ya noti?

Kwenye mfumuko wa bei noti huwa hazina thamani kwa kiwango hiki! Italia,mfumuko wa bei ulifika asilimia 319,Japan(236%),Ufaransa(234%),Marekani(196%) n.k

Nimesema, chanzo kilikuwa ‘reduced supply’ kukaja kuzaliwa shida nyingine ya kitu kinaitwa, “recession”, biashara ikasinyaa,hata bidhaa hazikuzalishwa tena viwandani-sababu ya kiburi cha Mwarabu!!

Hata Urusi haikuwa salama;Afrika nayo iligugumia maumivu ya kupanda kwa gharama kufuatia kupanda bei ya mafuta soko la dunia.Kununua bidhaa soko la dunia kuligharimu bei mbaya wakati huo wa miaka ya 70.

Hali hii ilifanya mataifa ya KIARABU kutajirika maradufu,Waarabu wakawa wanakula maisha sana hata huko Ulaya.Marekani pamoja na kuwa na mafuta yake yenyewe,ikakumbwa na kilio kikuu cha ukosefu wa mafuta.

Marekani hutumia mafuta mengi kuliko nchi yoyote hapa Duniani.

Kufuatia hali hiyo,Marekani ilikaribia kutembelea magoti na kukoma kuwa “economic strong man”.

Nakumbuka, Katuni moja iliyochorwa na Wadachi mwaka 1973,Mwarabu akiwa amewaweka CHINI YA ULINZI viongozi wanne wa Dunia:

Kansela Willy Brandt wa Ujerumani,Rais Georges Pompidou wa Ufaransa,Rais Richard Nixon wa Marekani na Waziri Mkuu,Edward Heath wa Uingereza.

Hawa walionekana kwenye katuni wakiwa wamewekwa chini ya Ulinzi na Mwarabu kwa kutumia ‘Pampu’tu ya mafuta, siyo bunduki wala guruneti!

Walishikiliwa hadi Mzungu alipe kikombozi(ransom) ndipo waachiliwe huru.

Zama hizo, Saudi Arabia,Irak,Iran,KUWAIT,Libya,Abu Dhabi,Algeria n.k zikapata heshima mbele ya mabeberu.Nchi nyingine kama Nigeria,Guinea ya IKWETA,Venezuela,Indonesia,Ecuador,Angola n.k zingeweza kuwa na kiburi cha kuyagomea mataifa haya kwa kutumia mafuta kama silaha.

Norway,Mexico na Uingereza walihaha kusaka vyanzo vipya vya mafuta.Mwaka 1979 kulikuwa na uhaba wa mapipa milioni 2.3 kila siku.

Ni hapa Mwarabu alipotikisa ndevu za Mzungu, hususan Marekani ambayo kwa siku moja hutumia theluthi ya mafuta yoote yanayotumiwa na dunia nzima.

Huu ndiyo wakati Mohammed Reza(Shah) wa Iran alipouza mafuta yote Marekani na kuiacha nchi yake ikiwa kavu kabisa!

Itaendelea

0713 324 074

No comments:

Post a Comment