Thursday, February 7, 2013

HAKI IKO KWA MUNGU TU



  
BIBLIA, na Wanaharakati wa Haki za Binadamu,hukubaliana kimsingi kwamba, “Haki za Binadamu zilianza wakati Binadamu alipoanza kuishi Duniani”.
Huu ni ukweli kamilifu; pale Mwanzo 2:16 na 17 Mungu anapomwambia Adamu kwamba alipewa ‘Uhuru’ wa kuchagua kumtii Mungu au kukataa(Freedom of Choice) alimpa HAKI ZA BINADAMU-Uhuru.
Hata hivyo, uhuru unawajibu,ukikosea umekwisha,ili haki za binadamu zidumu kuwepo ni sharti kuchagua vizuri kuitii sharia ya unyoofu ,The Moral law.
Dhana kwamba kila mtu anazo haki za binadamu ambazo tunasema ni haki za kimsingi,kwa kuwa kila mtu alizaliwa huru, ni ukweli halisi.
Haki za binadamu haziondolewi;hazipokonywi na  mtu na hakuna wa kuzipora-lakini zimeporwa sana hata na wanaojidai kuzihimiza siku hizi.Mtu anajidai kutangaza Haki za Binadamu,huku ni mwizi,fisadi,mbakaji!
Marekani na washirika wake wa Ulaya wanapojidai kuzitetea sana haki hizi za binadamu,wamezipora sana kwa kuua maelfu ya watu duniani pale wanapopigana vita vingi ili kutafuta maslahi yao.
Angalia vita vya Vietnam miaka ya 68-70;vita vya Irak,Afghanistan,Libya na mahali pengi hapa duniani ambako Shirika lao la Ujasusi, Central Intelligence Agency, wamechochea mno machafuko.
Mikataba na matangazo mengi ya Haki za Binadamu, imewapa watu kwa mkono wa kulia na kuziondoa kwa mkono wa pili wa kushoto.
Magna Carter ya Uingereza(1215),Bill of Rights ya Uingereza(1689),Tamko la Uhuru wa Marekani(1776),Tamko la Ufaransa la Haki za Mtu na Raia(French Declaration of Rights of man and Citizen) la 1789 n.k
Haya mengi,na linguine la Umoja wa Mataifa la Desemba 10,mwaka 1948,hakuna kinachosemwa kwa ukamilifu juu ya Haki zote za Binadamu na ukamilifu wake-ni udanganyifu mkubwa.
Maandamano yangalipo ya kudai haki Uingereza na Marekani,unyanyapaa na ubaguzi wa rangi ndiyo kwanza huendeshwa kila kona ya dunia,Waitalia walimnyanyapaa Zenedine Zidane,na hata sasa wanaongea ubaguzi wa rangi waziwazi.
Eti,misingi ya Haki za binadamu ni USAWA bila ubaguzi! Ubaguzi upo unalelewa Buckingham Palace, No 10 Downing Street na Oval Office, New York!
Vita vya kwanza vya Dunia(1914-18) na vya Pili(1939-45) vililetwa na mataifa makubwa.Waliua watu wengi sana kwa mamilioni,wengine walikosa makazi,wakawa wakimbizi,ili maslahi ya watu hawa yapatikane.
Hiroshima na Nagasaki.
Vita vya Kwanza vya Dunia, vilianza mwaka 1914 na vikaisha 1918.
Sababu hasa za vita hivi ni Mtawala wa Ujerumani, WILHELM  II,alitaka kuleta changamoto kwa maendeleo ya viwanda vya Uingereza,siyo vya Afrika,sawa?
 Katika Vita hivi vya Kwanza vya Dunia, walikufa jumla ya wanajeshi 8,418,000.
Askari wa Marekani waliouliwa vitani ni 126,000 na kiasi cha raia waliokufa katika vita hivyo ni 1,300,000.
Katika Vita vya Pili vya Dunia(1939-1945), walikufa askari 16,933,000; askari wa Kimarekani waliokufa ni 292,000 wakati raia waliouliwa ni 34,305,000.
 Vita hivi vilikoma wakati Marekani ilipolipua mabomu ya Atomiki katika miji ya Hiroshima na Nagasaki, Agosti 6 na 9 mwaka 1945.
Agosti 14, Japan ilitia saini ya kuacha vita na Septemba 2, mwaka huo wa 1945 vita hivi vilikwisha rasmi,vikiacha makovu ambayo hata sasa yangalipo. Hizi ni Haki za Binadamu sampuli gani wewe?
Huku ndiko tuendako,tunarejea katika vita, wakati mikataba ya amani inapovunjika,wakati uharibifu mkubwa wa mazingira unaposababisha karibu sana Mapigo saba ya Mwisho.
Kuharibika kwa utando wa Ozone angani,uharibifu wa vyanzo vya maji na ukataji miti ni janga lingine la hatari.
Tumchambue kidogo Adolf Hitler na chama chake cha NAZI dhidi ya Mayahudi wakati wa vita ya Pili ya Dunia, waliuawa Mayahudi wengi hata Umoja wa Mataifa ukaanzisha, “The Universal Declaration of Human Rights” mwaka 1948.
Mayahudi milioni sita waliuliwa kinyama.Tazama Filamu iitwayo, ESCAPING FROM SOBIBOR-Sobibor ni Poland,ambako Wayahudi waliuliwa na kuteswa kinyama ili kuangamizwa kabisa duniani.
Wauaji, eti walifikishwa mahakama ya Norenberg,iliyoanzishwa ajili ya kuwashitaki wahalifu wa vita,na uhalifu wa binadamu(crimes against humanity and war crimes).
Walipatikana na hatia ya kifungo jela.Kuna mahakama za aina hii nyingi kunapotokea mauaji ya kimbari kama Rwanda,ambako kuna mahakama ya Arusha,UNICTR.
Ipo ya Sierra Leone na ile ya Hague Uholanzi. Je haki hutendeka? Mbona wapo akina Felician Kibuga wamejificha Kenya,hawajawahi kukamatwa ili washitakiwe? Mahakamani kuna haki? Hakuna makengeza,  ‘double standards’?
Hata hivyo, Universal Declaration of Human Rights(UDHR), International Bill of Rights, International Covenant on Economic, Social and Cultural RightsI9CESCR),International Covenant on Civil and Political Rights(ICCPR) na mengine mengi husema kuwe na uhuru na haki,lakini hakuna haki hapa duniani.
Hakuna hata haki ya kuishi kwa masikini na makabwela kwa mfumo huu wa ubepari.
Nani anatengeneza bunduki na madege ya kijeshi? Nani hutengeneza misaili? Mizinga haiuzwi kwa waasi kama M23 huko Kongo? Kwa nini?
Marekani na Ulaya hawatengenezi silaha za maangamamizi hata leo baada ya vita baridi(Cold War) kumalizika?
Usidanganyike!Abu Ghraib,Guantanamo Bay na jela za wakubwa hawa huko Ulaya,huwakamata washukukiwa na kuwatesa,kuwafunga bila kuwafikisha mahakamani wakajitetee, haki gani sasa za binadamu?
Hakuna ‘Fair Trial’ ukikamatwa labda wa tuhuma za ugaidi. Hakuna haki hata katika mahakama za Tanzania,Ulaya na Marekani,tajiri hutazamwa zaidi na wakubwa hutetewa zaidi.
Mahakama ya Hague,Uholanzi ina makengengeza, haijawakamata Bush na Blair kwa kupeleka vita Irak kinyume na MATAKWA ya Umoja wa Mataifa.Wamekamatwa akina Charles Taylor tu, akina Uhuru Kenyatta watatiwa hatiani,lakini siyo wakubwa wa dunia.
Duniani mwenye haki ni mwenye nguvu,mamlaka,mali. Eti ‘retroactive punishment’ imezuiliwa kwa wote? Mbona Gaddafi na Osama waliuliwa kwa risasi bila kufikishwa mahakamani wakajitetee?
Sheria humtambua kila mtu hapa duniani? Huu ndiyo umbumbumbu wetu kushabikia Marekani na Ulaya kwamba kuna Haki za Binadamu!
Nimeeleza kasha cha Conjesta Ulikaye,Wazungu wa Uingereza waliombaka na kumuua na DPP(sasa Jaji)Geofrey Shaidi.Hata uhuru wa dini(Freedom of thoughts, Conscience and Religion)hakuna,subiri National Sunday Law,itatangazwa na Marekani,sasa watu wana uhuru gani wa kuabudu kama kuna New World Order?
Tumuulize Rais wetu Jakaya Kikwete,kama duniani(siyo Tanzania tu)kuna haki za watu wanyonge kabisa, ‘minority rights’? Hii mikataba sijui ya haki za raia na siasa ilishavunjwa na mataifa beberu na makampuni yao yanatumikisha watu kitumwa huko Myanmar!
Saro-Wiwa ameuliwa kwa nguvu za Royal/Dutch Shell,Chevron,Total na mengine huko Nigeria.Mrahaba wa haki za madini,nishati na mali asili zetu huporwa kwa kiburi cha mabwenyenye wa Marekani,viongozi wetu hupewa “Option” ama kuchukua r ushwa,au wakijidai wapotezwe!
Lumumba yuko wapi? Murtala Mohammed yuko wapi? Kabila?
Mnajidai kuandamana nini,waandamanaji huko Niger Delta waliuliwa na nani kama siyo makampuni ya Marekani na Uingereza? Uchochezi tu.
Eti haki za kuandamana! Mtavurugana kama Libya,kama Misri,kama Tunisia n.kWakubwa huongoza kuhalifu usawa na amani duniani,hakuna usawa wala usawia(universality) haki za watu wa mataifa madogo zilishaondolewa(alienable rights),sababu sisi waafrika,masikini?
Tukitaka haki ziwepo duniani,tukatae theories za akina Charles Robert Darwin(1809-1882) kwamba binadamu mwanzo alikuwa nyani,na kwamba dunia imetokea kwa bahati, ‘Big Bang’ ama evolution,uibukaji.
Kwenye uibukaji na maisha ya bahati hakuna usawa na haki,bali mwenye nguvu ndiye atastawi katika vita vya kugombea maisha-struggle for existence!
Katika dhana kwamba dunia imeibuka,na vilivyomo vimetokea kwa maguvu yake(survival of the fittest) hakuna haki na usawa wa binadamu, kuna sangara kuwala dagaa na furu,kuna simba kuwatafuna palahala na nyumbu.magugu kuyasonga mazao tunayolima ili tupate chakula n.k Haki itoke wapi sasa mahali ambapo hakuna sharia ya ulinganifu(universality) ama sharia ya unyoofu, moral conduct?
The Fundamental Code of Ethics ni Amri 10 za Mungu ambazo kila mtu hazitaki.Sasa unyoofu, “Morality’ hutoka wapi ili watu wasiwe wezi na mafisadi,bila Mungu?
Mkubwa atamjalije mdogo mahali ambapo watu hawataki amari ya kuwaheshimu watu,kuwajali na kuwapenda adui?Soma Mathayo 5:43-48. Matokeo yake, ‘Darwinism’ ni dhana ya mwenye nguvu ndiye atakayenusurika katika maisha haya ya kunyang’anyana chakula,maji na rasilimali.
Kwa kuwa hakuna kanuni za kupendana, basi watakaobaki duniani ni wenye nguvu(survival of the fittest) sisi tutakuwa mbolea ya kuneemesha mataifa makubwa,na wakubwa wenye uchumi mzuri-aliye na kidogo atanyang’anywa.
Kila mtu siku hizi hutamani awe na nguvu za utajiri,mamlaka na vyeo,wanaopiga kelele hawana jipya,wamepigwa kipepsi tu,lakini hata wao wakipata nafasi ni mafisadi wakubwa!
Kwa sababu hiyo,pasipo na Mungu akilini mwetu,hapana Haki za Binadamu,usawa,haki katika sharia na mgawo wa rasilimali n.k
Duniani hakuna sharia za unyoofu(morality) sasa haki itakujaje pasipo na sharia za unyoofu?Jambazi atakuwaje na upendo na huruma kazini kwake? Mwizi atakuwaje na huruma? Ingekuwa hivi basi wezi wangeshakoma kuiba.
Hakuna huruma,hakuna upendo kwa sababu pasipo Mungu na pasipo kutii sharia yake ya unyoofu na upendo,hakuna haki,kuna unyang’au.
Haki za Mashoga, Lesbian, Gay, Bisexual and Transgender(LGBT) ndizo haki hizi!Siku zote hakuna haki ila mwenye nguvu ndiye mshindi katika vita vya kupora rasilimali survival of the fittest, vita vya kugombea maisha, struggle foe existence,na vita vya kugombea mamlaka, struggle for supremacy.
Angalia wanasiasa wanavyowapambanisha ili wapate mamlaka! Kuna covenants sijui declarations za haki za binadamu,lakini hakuna haki!
Hakuna standard of rightness, kuna unyama watu wanakwenda upogo sababu hawaikubali sharia ya haki na unyoofu,moral principals, kuna uchoyo tu watu wote ni wanyama.
Sasa mnyama yupi atampa binadamu haki zake?Haki zimeporwa vitani, haki za wanyama kama zile za SHAMBA LA WANYAMA(animal farm) la George Orwell, zilishapokonywa na nguruwe wenye mamlaka!






No comments:

Post a Comment