Monday, April 22, 2013

WALIOWAUA J.F KENNEDY,ABRAHAM LINCOLN NA WENZAO WANAFANYA VURUGU TANZANIA(3)




KATI YA MWAKA 54 na 68 AD, wafuasi wa Yesu Kristo,hususan wale mitume walijipatia wafuasi wengi sana katika ile milki ya Rumi ya kale.
Zama hizo, Makaisari wa Rumi waliabudiwa na raia wao;kwa sababu Kaisari alijidhania yeye ni Mungu!
Ukristo ulipoibuka ukawaambia watu kumwabudu Mungu wa Mbinguni pekee,ukatishia ibada hiyo ya wafalme wa Kirumi(emperors).
Kaisari Nero aliazimu kuwafyeka Wakristo, alifanya njama akauchoma moto mji wa Rome(sasa Italia),akawasingizia Wakristo kwa sababu waliwafundisha watu kuwadharao hao wafalme na kumheshimu Mungu wa mbinguni-ilionekana kama kukosa uzalendo na kutoheshimu maofisa wa serikali na serikali yenyewe.
Mtume Petro, aliuliwa na Kaisari Nero mwaka 67 AD na akazikwa mahali ambapo siku hizi kuna kanisa kubwa la St.Peters Basilica, jijini Rome.
Wengine walitimuliwa jijini humo wakakimbilia mahali pengine Ulaya,        Mitume Paulo,Barnaba,Yohana na wengine walifanyiwa ukatili na kuteswa kwa kesi za kubambikiwa.
Tabia hizi zingalipo hata sasa kwa wale wanaopenda kuabudiwa kusingizia wafuasi  halisi wa Mungu ili waonekane wakosaji wanaostahili kutupwa ama kuuliwa. Hili si jambo la ajabu.
Sababu za Makaisari wa Rumi kudai kuabudiwa ni kwamba kulikuwa na mahekalu na watu wakawa wanawaabudu asubuhi kabla ya kwenda kwenye shughuli zao, waliitwa “Theos” neon la Kigiriki maana yake mungu na ‘Savior’ ni kuonesha heshima.
Hata makaisari hawa walipokufa kukajengwa masanamu yao yaliyoendelea kuabudiwa na raia wa dunia nzima waliyotawala. Julius Caesar sanamu lake liliwekwa kati ya masanamu mengine ya miungu katika mahekalu anuwai.
Kaisari Augusto(27-14 BC)akaitwa ‘Sebastos’ maana yake mungu,Gaius Caligula(37-41AD) alitaka dunia nzima imwabudu,hata sanamu lake likapelekwa ndani ya hekali mjini Jerusalem, ili kuabudiwa,vurugu zikaanza kwa sababu Wayahudi wakati huo walipinga sana kuabudu sanamu.
Nataka msomaji atambue aina ya watu wanaoanzisha migogoro ya kidini,lakini huwasukumia lawama watu wasiohusika.
Vurugu,vita na mauaji ya kinyama siku hizi huchochewa sana na dini hiyo hiyo inayoshurutisha watu wa dunia nzima kuabudu Wafalme wa kale,matajiri ambao hujificha ndani ya imani ya Freemasons,wakijidai watu wa Bwana Mungu,kumbe siyo.
Kupinga aina ya dini hiyo ni kujipatia mauti kwa sababu utaonekana wewe huna uzalendo(Patriotism).Watu wakuu kama Adolf Hitler hujidai kuwa na nguvu za kimungu ndani yao(Divinity) wanachoamuru hutaka dunia nzima kufuata,na wanaopinga kusingiziwa na kubambikwa makosa.
Sasa,unaweza kutambua hata ni kwa nini Saddam Hussein,Osama,Gaddafi na wengine wengi walivyouliwa kwa visingizio kuwa ni watu hatari wanaomiliki Mass Destruction Weapons,Saddam alinyongwa Desemba 30 mwaka 2006 ili wapinzani waone.
Kila kiongozi wa dunia wan chi anapaswa kutii, “To pay divine honors to the emperor and thereby inviting the penalty of ostracism, exile, torture, imprisonment and death”.
Unaweza kuona Charles Taylor wa Liberia akitoroshwa jela gerezani mjini Boston,huko kulipolipuka mabomu juzi, akapelekwa kwa Gaddafi,Libya ili akafunzwe medani ya kijeshi.
Alitumwa baadaye kwenda kupindua serikali ya mjini Monrovia, akaanza kuwasaidia waasi wa Revulutionary United Front(RUF) wakaanza kuiba almasi za Sierra Leone na kuziuza Ulaya na Marekani kwa hawa mabedui.
Muda ulipopita,wakamweka jela wakamsingizia kesi na kumgunga miaka 50 mmjini London ili asije kutoa siri. Njia ni ile ile ya kuziba watu midomo wasije kutoa siri.
Taylor, aliwahi kusema hivi,     When your Master is also your enemy, you are perished” Aliyekutuma kazi anapokugeuka na kuwa adui yako basi unaangamia!
Alitumwa kazi, wakamgeuka na kumwangamiza. Hakuonesha heshima kwa wakubwa wa dunia hii waliorithi heshima ya emperors wa Rumi.
Kuna wakubwa wa dunia hii wanaodai kuabudiwa na kuheshimiwa na ndiyo walioanza kuisumbua Tanzania,kwa sababu hata Rais wan chi anapatakiwa kuonesha heshima kwao,  To pay patriotism and royalty to emperors or Lords of this World”
Unabambikiwa makosa nawe huwezi kujitetea unahukumiwa kama Mitume Paulo, Petro,Baranaba na wenzao, wanasema Kaisari yuko juu kuliko Kristo,Mtume yeyote n/k
Hawa Freemasons ndiyo huleta fujo hapa duniani,mitafaruku kama ile ya Waislam/Wakristo kuchinja au kutochinja n.k
Mgogoro wa kuchinja uliwahi kutokea mwanzoni mwa Ukristo,sababu zilionekana kama za msingi za kupinga ibada ya sanamu.
Baraza la Yerusalem liliketi kukataa Wakristo kula nyama zilizochinjwa na waliohisiwa makuhani wa miungu(Matendo ya Mitume 15:29).
Mtume Paulo, alipuuza maamuzi ya Baraza lile la kuwataka Wakristo kuacha kula nyama hizo zilizouzwa madukani(mabucha),akasema,kula hakuhusiani na ibada ya sanamu wala ibada ya miungu(1Wakorintho 8).
Kula nyama inayohisiwa ilitolewa kafara kwa miungu ama kuchinjwa baada ya kufanyiwa ibada Fulani,Paulo anasema hata sasa kuwa hakumpunguzii mlaji uaminifu kwa Mungu wa kweli(1Wakorintho 8:8-13).
Baraza la Yerusalem lilikaa mwaka 49 AD kupinga Wakristo kula nyama zilizochinjwa na makuhani wa miungu kabla ya kuuzwa sokoni.Paulo akaandika waraka kwa Wakorintho kupuuza ugomvi ule wa kula au kotokula nyama,kuchinja au kutochinja mwaka 55 AD.
“Eating things sacrificed to idols” maana yake ni mtu kula kwa makusudi kuwa nyama zile zilizotolewa sadaka kwa miungu, hiyo miungu ikupe neema wewe mlaji!
Kama huna mpango na mambo yale yanakuhusu nini? Kula au usile.poa tu!Wachinje wasichinje,poa tu!
Freemasons hufundisha  watu kufanya ubaya,kuua na kulipa visasi, wakijiddai kuwa roho  haiwezi kuchafua mwili wa mtu hata akapata hukumu.
Hii ni ‘Modern Gnosticism’ ambayo ni uasi kwa makanisa na misikiti kuhalalisha uasi,fitina,chuki na mapigano wakidhani ni kutetea imani.
Tukumbuke Kaisari Nero aliuchoma mji wa thamani kubwa ili kupata gharama ya kuwashitaki Paulo na wenzake ili waualiwe. Njama/Uongo ndivyo hutumika sasa kama Nero alivyochoma jiji la Rome mwaka 64 AD na kubambika makosa kwa watu waaminifu.
Haya majanga ya sasa ya watu kuchoma makanisa/Misikiti huchochewa na genge hilo ambalo lina pesa nyingi na hupeleka mambo haya kwa nchi wanazotaka kuvuruga.
Hakuna Mkristo safi atakayenufaika na vita dhidi ya Waislam, na hakuna Muislam atakayekuwa mwaminifu kwa Allah akichoma makanisa. Hii ni roho ya wale jamaa wanaotawala dunia.
 Nijadili kidogo upuuzi unaoenezwa kwamba Rais Jakaya Kikwete ndiye muasisi wa udini hapa Tanzania.
Jambo hili la kijinga na kipuuzi sana,huenezwa kwa makusudi kwa watu wajinga wasiotafakari. Mimi nawakumbusha mwaka 2005.
Maaskofu,Wachungaji na makasisi ndiyo waliompigia sana debe Kikwete awe rais kwamba alikuwa ‘Chaguo la Mungu!’
Ilishangaza kuona maaskofu wakiwa wamevaa TSHIRT NA KOFIA ZA CCM huku wakimpigia debe Kikwete madhabahuni kwamba ni ‘Chaguo la Mungu!”
Augustine Lyatonga Mrema,ndiye shahidi wa historia.Aliwapinga sana hawa maaskofu kusema Kikwete ni chaguo la Mungu,akasema  “Hawa maaskofu wanadai Kikwete ni chaguo la Mungu,walikaa kikao na Mungu lini akawaambia  Kikwete ni chaguo lake?”
Mrema, aliwasuta maaskofu hawa katika viwanja vya Furahisha,Mwanza wakati akifanya kampeni za Chama chake, TLP mwaka 2005.
Mrema, alisema hawa maaskofu walikuwa waongo,Mungu hakuwatuma walikuwa manabii wa uongo!
 Sasa,unawezam kuuona hawa ‘Manabii wa Uongo’ wa Mrema,wakigeuka mara moja na kuonesha kwamba huyo Mungu aliyemchagua Kikwete mwaka 2005,sasa ni kigeugeu, ameshamchagua mwingine,na sasa Kikwete hafai ni ‘mdini’ na mkabila!
Siku hizi wanahamasisha watu kugomea kula nyama zilizochinjwa na Waislam,na husema kwa kinywa kipana kwamba Kikwete hafai,siyo chaguo la mungu wao!!
Ilikuwa Januari 20,mwaka 2005,Prof.Ibrahim Lipumba akizungumza na waandishi wa habari,Kirumba Mwanza, alisema, “Kikwete hakuwa na ‘Presidential Material’ akapuuzwa na maaskofu,tena wakamwona yeye Lipumba kwamba anakumbatia udini na chama chake cha CUF, leo Lipumba kawa safi,mwenye ‘Uislam’ ni Kikwete! Tuachane na ujinga huu jamani!
Mbona hawa hawakumsikiliza Lipumba mwaka 2005 walipokuwa wamevaa Tshirt za Kikwete na kofia?
Nadhani, Kikwete alipoingia madarakani,alopoamua kuwa ‘Fair’ kuachana na mpango wa siri wa maaskofu, akawakosea,sasa wanamwandama na mambo ya kijinga!
Sina tabia ya kujikomba kwa mtu! Lipumgba ni shahidi, alisema “Kikwete ni rafiki yangu;ni ndugu yangu,lakini hana Presidential Material”.
Maaskofu walimpuuza Lipumba,wakmbeba Kikwete makanisani mwao,hawakuona Uislam wowote kwake, ati leo wanasema Kikwete anasambaza udini..naam Uislam! Upuuzi mkubwa!
Mrema, alisema hakuna Mungu aliyewatuma hawa kumpigia debe Kikwete mwaka 2005,ni tamaa zao za vyeo na madaraka, walipotupwa wakaanza hila na chokochoko,sasa tumejua udini huanzishwa na maaskofu,wachungaji,makasisi na masheikh,na wala siyo Kikwete na wenzake!
Mungu wa maaskofu angekuwa ‘Omniscient’ kama Mungu ninayemjua, asingemchagua Kikwete mwaka 2005 akajakumkata sasa,ni ujinga mtupu na hila kama za akina Kaisari Nero!
Maaskofu wa mungu ‘kigeugeu’ asiye na macho, ndiye anayetaka kuiangamiza Tanzania kwa vurugu za kidini na siasa uchwara.
Nchi imejaa matusi na ugomvi.Vyombo vya habari vinavyojiita ‘The Fourth     Estate” Mhimili wa  nne wa Dola, leo umeingiliwa na hao hao akina Kaisari Nero, hadi sasa tunashuhudia wahusika wakitoana macho,wasipate kuona ukweli wa mambo!
 Mungu inusuru Tanzania
Itaendelea
0713 324 074





1 comment:

  1. HAUPO KIBAGUZI WALA KIUPENDELEO.....PLZ after arguments, what do you think will be possible mitigations to combat such patriotic situation fot the benefit of all Tanzanians?

    ReplyDelete