Thursday, August 1, 2013

marekani

Turejee nyuma, wakati wa vita vya kumpindua Mtawala wa Nchi ya Mito miwili ya Tigris na Eufrates,Saddam Hussein.
Marekani, aslani haikusubiri ruhusa ya Umoja wa Mataifa(UN);Saddam alipinduliwa,Sanamu lake likang’olewa kuonesha enzi yake ilikwishakoma, baada ya miaka mitatu gerezani, akanyongwa huko Camp Justice,mjini Baghdad.
George Herbert Walker Bush(88),Agosti mwaka 1990 alijaribu kumng’oa Saddam Hussein huko Irak,kipindi alipoivamia Kuwait. Unajua sababu za Saddam kuivamia Kuwait? Waliiba mafuta.Bush huyu (Baba) alipata ushindi mwembamba katika medani ya vita.
Bush baba alisaidiwa sana na vikosi vya Umoja wa Mataifa(UN),vikosi vya Umoja wa Kujihami Ulaya Magharibi(NATO) na Muungano wa Kiarabu, Arab League.
Kuwait ilikombolewa toka mikononi mwa Saddam, Bush baba akapata hadhi katika historia ya nchi hiyo babe sana duniani siku hizi. Uchumi ulikwenda vibaya mno,ukaja kurekebishwa na Bill Clinton baada ya kushinda Uchaguzi mkuu mwaka 1992.
 Bush Baba, aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani(CIA)na alisaidia sana kuparaganyika kwa iliyokuwa Dola ya Kisovieti ya Urusi(USSR) zama za Mikhail Gorbachev.
Kuparaganyika kwa USSR,ilikuwa kupisha njia kwa Mataifa ya Magharibi na Umoja wa Kujihami wa Ulaya Magharibi(NATO) kupanua himaya yake hadi Mashariki, na ilikuwa ishara ya kumalizika kwa VITA BARIDI,kasha UKUTA WA BERLIN ukavunjwa,mwaka 1994.
Kitendo cha George Bush(mtoto)kumnyonga Saddam,ilikuwa kurejesha heshima ya nyumba yao katika Taifa hilo babe sana duniani. Marekani ilivumbuliwa na Christopher Columbus,OKTOBA 12, MWAKA 1492, na ikaja kutangaza uhuru wake Julai 4,mwaka 1776. Juzi walisherehekea miaka 236 ya uhuru.
Sasa, tuchambue Ufunuo 18:11-18. Marekani ilipata uhuru na ikawa nchi kimbilio kwa waliosetwa na tawala katili sana.
Lakini, ilikuja kuwa nchi katili; na ikaanza kufanya mapenzi ya JOKA ambaye ni Ibilisi mwenyewe,pale ilipopindua marais wa mataifa mengine kwa jeuri. Hawa ni pamoja na Jenerali Manuel Noriega wa Panama na Salvador Allende wa Chile, wakamweka kibaraka wao Dikteta, Pinochet.
 Licha ya kupindua serikali za Panama na Chile kama nilivyokwishaandika katika makala zilizotangulia, Shirika lao la CIA lilishirikiana sana na manyang’au kama Dikteta Mobutu  wa Zaire kuua wanamapinduzi wa Afrika, akina Patrice Emely Lumumba.
CIA ilishirikiana na Makaburu wa Afrika ya Kusini kuwawinda wanamapinduzi wa Afrika ya Kusini,ili Botswana, Namibia,,Angola,Msumbiji na hata Afrika ya Kusini waafrika wasijitawale wenyewe.
 Ndani ya Angola,Chama cha MPLA na FNLA vilipambana wakati FNLA wakipewa msaada na CIA hadi uhuru ulipopatikana kutoka Ureno mwaka 1975. Jonas Malheiro Savimbi alikuwa kibaraka wa Marekani,ili kuvuruga maendeleo ya nchi, hadi walipomumwaga juzi juzi  akaachwa kupigwa risasi na majeshi ya serikali. Jambo hili alishalisema Kamara Kusupa.
MMarekani iwe chini ya Barack Obama ama Mgombea wa Republican,Mitt Romney, ina akili ile ile, ya kunena kama Shetani(Ufunuo 13: 11) yaani ubabe wake na kulazimisha watu kile wanachotaka wao.
Angalia, kwamba CIA waliwasaidia Makaburu wa Afrika ya Kusini kuwaua wanafunzi 250 katika kitongoji cha SOWETO(South West Township) mwaka 1976,mjini Pretoria.
Turejee Irak, ambayo baada ya Saddam hamkani si shwari. Nchi imegawanyika sasa ni baina ya dini na dini;msikiti kwa msikiti,ukoo baina ya ukoo wanapambana.
Watu wa Madhehebu ya SUNNI mwaka 2007 walikuwa milioni 3.8 baada ya Saddam ambaye pia alikuwa Sunni kunyongwa. Hawa wako Magharibi.
Wakurdi, ambao Saddam alidaiwa kuua walikuwa milioni 4.4 nao wanaishi Kaskazini  Mashariki mwa Ninawi,ule mji mkubwa aliokwenda kuhubiri Nabii Yona akamezwa na Nyangumi!
 Washia, nao ni milioni 8.4 wanaishi Babeli hadi Kusini Mashariki mwa nchi. Mjini Baghdad na Kati kati mwa nchi kuna watu wa dini mchanganyiko wapatao milioni 9.2.
Najaf na maeneo ya utajiri wa mafuta ni maeneo ya Washia ambao wamewekewa chuki na SUNNI,huku Bush,Obama na hata Mitt Romney(Mgombea wa Republican) wanaweza kuhangaika kurejesha amani,bila mafanikio…ni vita hadi kiama!
Dola lenye nguvu kandoni mwa Mto Frati,lilikuwa limevunjika ili kutoa nafasi kwa madola ya Mashariki kuungana na NATO na European Common Market, ama EU ili kuungana na Marekani kuandaa serikali moja ya Dunia.Huku ndiko kukauka kwa Mto Frati.
 Angalia nchi zilizo Mashariki mwa Mto Frati:Pamoja na nchi zilizokuwa katika Muungano wa Kisovieti(USSR), na Afghanistan,Pakistan,China,India,Korea Kaskazini na Kusini na Japan leo zinalazimishwa ama zinaungana na Marekani kwa hiari katika biashara na katika mambo mengi.
Kabla ya VITA BARIDI kwisha, hali ilikuwa tofauti. Jumatatu, Januari Mosi mwaka 2007, Romania na Burgaria zilijiunga na NATO(Northern Atlantic Treaty Organization); ilikuwa SIKU MOJA tu,baada ya Saddam  kuzikwa. Unabii unatimia bila kukosa.
 Bado Iran na Korea Kaskazini, na Syria itavurugwa kama nitakavyoonesha punde.
Kwa mujibu wa mwqandishi wa Iran anayeishi jijini Paris, Amir Taheri, Yule gaidi wa kale, Carlos The Jackal, alisema Marekani ni “Shaytan” yaani Shetani ama Joka(rejea Ufunuo 13:11) yaani Shetani amejivika mwili wa Marekani ili kuuhadaa Ulimwengu.
 Imesemwa kwamba waumini wa dini ya Kiislam wanapaswa kuichukia Marekani kama Shetani anavyochukiwa pasipo kuulizwa!
 Nirejee kidogo katika Historia ya Carlos ingawa nimeijadili kwa utulivu mwingi katika makala zilizotangulia.
Alizaliwa Oktoba 12,mwaka 1949. Katika kitabu kiitwacho Revolutionary Islam Editions Du Rocher,2003 yeye anadai ni Muislam huko gerezani,Ufaransa.
Babaye alikuwa mwanasheria milionea wa Venezuela,nchi ya Hugo Chavez. Carlos alimkubali sana Osama bin  Laden, na alisoma Patrice Lumumba University,huko Moscow. Hiki ni Chuo Kikuu kilichoanzishwa na Shirika la Ujasusi la Urusi,KGB,ili kuwafundisha wanaharakati wan chi za Dunia ya Tatu,
 Amefanya harakati nyingi mahali pengi kwa miaka 20 hivi, Urusi ilipoparaganyika, akaanza kujificha-ficha, hadi Makachero wa Ufaransa wakaja kumkamata mjini Khartoum, Agosti 14,mwaka 1994.
Alisafirishwa chini ya ulinzi mkali hadi Paris ambako amefungwa maisha. Nataka ujue kwamba 1994 Ukuta wa Berlin uliangushwa na kuondoa Kambi mbili za watu kuashiria kwisha kwa VITA BARIDI,na Marekani kuanza kutawala Dunia,huku Carlos akakamatwa, ambaye pia alipinga mno maslahi ya Magharibi. Umeona?
 Carlos aliwahi kutabiri mambo ambayo yametokea kwa usahihi kabisa. Ametabiri Irak kujengwa upya na Marekani, ametabiri SYRIA kuvunjika vipande vipande, na sasa tunaona vita vikali baina ya majeshi ya kigeni yanayounga mkono waasi na serikali inayoungwa mkono na Urusi na China.
 Ametabiri Lebanon kuanguka na kikundi cha HEZBOLLAH kuharibiwa.Ametabiri Kossovo kuwa huru na kwamba SUDAN(sasa Kusini na Kaskazini) itafanyiwa usanii ili kusukwa upya,hili limetimia,Sudan ni mbili siku hizi.
Ametabiri Ufaransa nayo kusambaratika na kuwa vinchi vidogo-vidogo.Mwisho wa siku Carlos anadhani ni Iran na Korea Kaskazini tu zitakazompinga Marekani.Anasema vita vya kumpinga Marekani vitakuwa virefu sana, na Marekani watashinda sana, anawataka Waislam kufanya JIHAD dhidi ya Marekani kuwa Nguzo Kuu ya Uislam,swala,kufunga,Hija huko Mecca N.K
Alimpenda Sana Rais wa Algeria, Azizi Bouteflika na kumwita,”Kaka yangu mpenzi” na Osama alimwita, “Sheikh” na anaogopa Algeria nayo kumezwa na ubeberu wa Magharibi
Hata hivyo, Carlos hakujua Algeria ilishaungana na Marekani na NATO pamoja na mataifa mengine ya Kiarabu,na Israeli katika urafiki unaoitwa, Partnership for Peace.
Leo, wapo wanaharakati wanaoitwa magaidi walioanzisha JIHAD dhidi ya Marekani na washirika wake.
 Hata hivyo, unabii wa Biblia na hata Carlos tumemwona akitabiri ushindi kwa Marekani,kwani unabii wa Biblia aslani hausemi uongo.
 Tijadili kidogo dhana ya kujitoa mhanga kupambana na Marekani na mabeberu wenzake.
Ni kweli Marekani wanafanya uchafu na unyama duniani. Hata hivyo kwa Wakristo,kupambana na adui kwa kumuua ni dhambi,maana Yesu alikataa chuki na uadui,sembuse kujitoa mhanga?
 Tazama Mathayo 5:43-48 na hata ule ujumbe wa Yesu kwa Petro kurejesha kisu halani mwake.
0786 324 074

No comments:

Post a Comment