Wednesday, August 29, 2012

LEO NI JANA YA KESHO(3)

  MIAKA SABA KAMILI iliyopita,Kimbunga Katrina(unaweza kuita Catherine au Katarina),kiliyakumba maeneo ya Pwani ya Ghuba yenye utajiri wa nishati,nchini Marekani.
Ilikuwa Jumapili,Alasiri majira ya saa 10. Ilikuwa siku ya Agosti 28. Mamlaka ya Hali ya Hewa(National Weather Services) ikaonya raia wan chi hiyo juu ya janga la Kimbunga Katrina kuvuruga eneo hilo,hususan New Orleans.
Agosti 30; saa 7:30 usiku, tayari maji ya Ziwa yakisombwa na kimbunga kikali,yalishavuka kingo na kuingia mitaani, ambako yaligharikisha watu.
Barabara Kuu ya London(London Avenue) hapo New Orleans, zilipokuwa kingo zenye kimo cha futi 300 zikagharikishwa na mawimbi yenye kubeba maji,yaliacha makazi yake ya kawaida na kuhamia mjini.
Miundombinu kama umeme ikaharibiwa vibaya,kukawa kiza totolo. Mawimbi ya maji yenye kina cha futi hadi 10 yakagharikisha mji, wakazi wengi wakakwea katika mapaa ya nyumba zao ili kujiokoa,wakisubiri msaada.
Msomaji, piga picha ya Gharika ya Nuhu mwaka wa BC 4000,kasha tazama kilichotokea miaka saba kamili iliyopita huko New Orleans.
Ilikuwa Agosti 28 hadi 30, mwaka 2005.
Katrina, iliwafanya raia 25,000 wa New Orleans kuwa wakimbizi katika mji wao wenyewe,wakalazimika kukwea katika mapaa ya nyumba zao,kusubiri uokozi.Maji yenye kimo cha futi hadi 10 yalikuwa yakiotea maisha yao.
Hiki ni kiama cha Katrina ama ‘Katarina’. Jumanne, Agosti 28 mwaka huu, Historia ikajirudia wakati na mahali pale pale, safari hii wanakabiliwa na kimbunga Isaac.
Nataka kukwambia msomaji,zamani vimbunga vikibatizwa majina ya akina mama, Hellen, Katrina,Katarina,Mitch n.k. Akina mama wa Haki za Wanawake wakaja juu sana,kusema kwanini majanga yanabatizwa majina ya wanawake?
Ndiposa, utasikia kuna Hurricane Isaac, Robert, Andrew ,Charles n.k
Sasa huko Louisiana na New Orleans, tunasikia kuna Kimbunga Isaka. Hili ni eneo la njia ya tufani na vimbunga,eneo la Kusini na Mashariki mwa Marekani.
Ni eneo lenye mito mikubwa duniani,kama Mississippi, ambao ni wa kwanza kwa ukubwa hapa Duniani. Unafuatiwa na Nile,unaoanzia Owen Falls, Jinja nchini Uganda, unasafiri kilomita 6,900 hivi hadi Misri.
Naam,kufuatia Katrina,visiwa jirani na New Orleans vilizama penye kinamansi.Maeneo oevu ya ya Ghuba hii ya Pwani ya Marekani,yakazamishwa na kina cha maji cha futi 30 hivi.
Mto Mississippi, ukatapika maji, na Ziwa Pontchartrain,Kaskazini mwa mji likamwaga gharika mjini. New Orleans uko chini ya usawa wa Bahari.
Tufani ama kimbunga chenye kasi ya maili hadi 165 kwa saa,hadi kufika Agosti 31 mwaka huo 2005 kilishabeba mawimbi ya maji yenye futi hadi 29,mji ukazamishwa,uchumi na biashara vikatiwa kiharusi.
Bidhaa zikapanda bei kupindukia. Paketi ya sigara iliuzwa sasa kwa Dola 10(sawa na shilingi 16,000 za Tanzania),magereza yakasombwa na maji,malango yakafunguka,wafungwa na mahabusu wakajiendea zao.
Wahalifu walianza kutamba mitaani. Sasa,kama maofisi ya serikali,polisi na mahakama yaligharikishwa maji,mafaili yakasombwa na mafuriko,hata kama ukikutana na kibaka au jambazi aliyetoroka jela,ungemkamata tena ili ukamshitaki kwa ushahidi upi,midhali vielelezo vilishasombwa na mafuriko?
Wahalifu walipotoroka gerezani, wakasomba silaha zilizoachwa nyuma na skari, wakaanza kufanya vitu vyao! Askari na raia wote walitoroka.
Nataka nikwambie msomaji.
Serikali ya Rais George W.Bush ililaumiwa sana kwa kushindwa kuokoa maisha ya Watu Weusi wengi. Helkopta za uokozi zilipofika eneo lile zikawatupia kamba Wazungu kwanza,Weusi masikini wakaachwa!
Mji wenye wakazi 500,000 zoezi la uokozi likafanywa kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, ambao hata sasa ungalipo.Waliuanza akina Adolf Hitler, wakaja makaburu wa Afrika ya Kusini,hata sasa akina Samuel Eto’o Fils wanaushuhudia huko Ulaya,na Olimpiki huko London kulikuwepo hali hiyo.
Uhalifu ulikuwa mkubwa,magenge ya wakora yakanyatia polisi na kuwapokonya silaha,bunduki na vilipuzi.Polisi nao waliasi kazi yao wakaanza kupora kilichoachwa na Katrina-wengine walikwenda kuangalia majumba yao na familia zao. Kumbe, wewe siku ya kiama utakumbuka kazi?
Nimesema,wafungwa magerezani walitoroka wakaingia mjini,mafaili na vielelezo vya ushahidi vilishasombwa na maji.
Makao Makuu ya Jeshi la Marekani(The Pentagon) yalikuwa chini ya Ronald Rumsfeld wakati huo.
Yakalaumiwa kwa uzembe wa kushindwa kuokoa watu na mali zao.
Huko Marekani, unapotaja,” Hollywood” unazungumsa burudani; ukisema Wall Street unasema Pesa, sasa ukisema eneo lililokumbwa na Katrina, maana yake ni mahali inapopatikana nishati.
Katrina,ilileta kiharusi kwa uchumi wa Marekani.Takriban asilimia 60 ya mafuta yanayoingizwa Marekani,huingilia maeneo haya ya Ghuba ya Marekani.
Viwanda vya kusafisha mafuta viko huko,uchumi wa taifa hilo ukatikiswa Agosti 28-31 mwaka 2005.
Niandikapo hapa,leo ni Agosti 29,miaka saba kamili baada ya Katrina. Leo katika eneo hilo,tarehe kama ya mwaka huo, kimbunga kingine sasa kilichobatizwa jina la mwanaume, Isaka, kinalikumba eneo hilo!
Agosti 28-31 kimbunga Katrina kikalikumba eneo hilo, leo tarehe hizo hizo,kimbunga Isaac kinarejea nyuma kupitia njia yake.
Nataka kusema kwamba, Historia inakawaida ya kujirudia-rudia.Yaliyotokea zamani, siku huenda na kupita,hujirudia tena, nataka tujifunze Historia.
Nimerejea jambo hili,ili msomaji wangu abaini kwamba mambo ya usoni yalishatokea huko nyuma.Hata wanasiasa ghiliba tupu walishakuwepo huko nyuma, yaliyowapata,yalitokea kutufundisha sisi wa sasa.
Ndiyo maana kichwa cha makala haya hiutwa, “LEO NI JANA YA KESHO!”.Hakuna jambo jipya hapa duniani. Suruwali za kubana zilikuwepo zamani, vijana wakora walikuwepo,tabia mbaya ya kutoheshimu serikali na mamlaka ilikuwepo tangu zama za Kaini!
Kaini, ndiye mwanzilishi wa wakora na magangwe.Biblia,katika kitabu cha Kohelethi au Mhubiri husema kwamba:
Pepo huyarudia mazunguko yake na mito hurejea inakotoka; wala hakuna jambo jipya chini yajua”, Mhubiri 1:6-10.
Huyu Mhubiri, ambaye ni Mfalme Suleiman mwana wa Mfalme Daudi wa Yese,(Tazama Mhubiri 1:12),aliishi kati ya mwaka 965-926 BC.
Msomaji mmoja ananiandikia kwamba nirahisishe lugha ili wasome watu wa kawaida pia.
Hata hivyo, hiyo miaka ya Kabla ya Kristo(Before Chris) inapungua na AD inaongezeka. Tujifunze historia.
Kiwango cha elimu cha huyu mtu aitwaye Suleiman, au nimwite Prof. Solomon, kilikuwa cha juu sana, Falsafa yake ni kwamba mambo mengi hapa duniani hujirudia rudia sana,yalikuwepo na yatakuwepo,ndiyo maana Leo ni jana ya kesho!
Tawala katili sana leo duniani,zilishakuwepo hapo zamani sana,zikatoweka zitakuja nyingine na kutoweka kama upepo.
Walikuwepo akina Julius Caesar,Augustus(27BC-14 AD),Caligula(AD 37-41), hata watu wakawaabudu kama miungu, akina Tiberius, wakati ule wa sensa, wakati Yesu anazaliwa.
Sensa ipo hata sasa, na watu wanasusa kwamba ni kinyume cha dini! Hata Yesu alihesabiwa, maana Mariam mamaye alihesabiwa akiwa mjamzito wa kujifungua.
Tiberius alikusanya kodi kubwa Rome hadi kufikia kama dola za Marekani1,700,000 katika mji mmoja.
Walikuwepo akina Kaisari Nero waliowakata vichwa mitume wa Yesu, watakuwepo wengine wakatili kama hao. Gidion M. anatwambia jambo hili kwa kina.
Mathayo alichunwa ngozi akiwa hai, Thomas alichomwa mkuki huko India, Marko alifia Ethiopia, Mathayo alifia Alexandria,Misri,Luka akafia Ugiriki, Yohana alichemshwa katika pipa la mafuta,Petro alisulubiwa kichwa chini-miguu juu! Hapa ni mjini Rome.Yakobo alifia mjini Yerusalem n.k
Wamekuwepo hapa duniani akina Farao,Nebchadnezzar, akina Malkia Cleopatra wa Misri.Hata sasa kuna hadithi za kuhusu huyu mwanamama mrembo sana labda kuliko wote duniani.
Historia inasema Malkia Cleopatra aliwachanganya wanaume wawili wakuu sana-Julius Caesar na Marc Anthony.Alitumia udhaifu wa ngono wa wanaume kuwamaliza,halafu yeye akajiimarisha madarakani.
Kuhusu ngono, akina baba wenye misuli na maarifa katika medani ya vita kama Julius Caesar, ni dhaifu kwa wanawake- Strongest But Weak!
Cleopatra alikufa mwaka wa BC 30,hakuacha hata maandishi yake. Cleopatra, “The Last Queen of Egypt” ilidhaniwa kifo chake kingekuwa mwisho wa Misri?
Hata leo, wametoka akina Gamal, akina Hosni Mubarak wako kolokoloni wakiwa mahututi,lakini akina Mohamed Mursi, wapo!
Watu hutoweka na wengine huja-hakuna mtu wa kudhaniwa mungu hapa duniani.
Cleopatra, alitumia mwili wake kwa ghiliba ya ngono,kama silaha mithili ya misaili.
Hata leo wapo akina Joyce Banda,leo ni kama jana.Wamekuja akina Joyce BANDA wanatumiwa na madola makubwa kwa kisingizio cha demokrasia. Wameruhusu ushoga, sasa wanataka kuchukua ziwa Nyasa lote ili makampuni ya Marekani,Uingereza na Ufaransa wachote mafuta na gesi humo. Watu kama yeye wamekuwepo zamani!
Namwonya Rais Jakaya Kikwete, asiwasikilize sana hawa wakoloni,ni laghai na wasaliti, wanajifanya rafiki,kumbe wafitini na wana hila.Tumkumbuke Julis Caesar eti aliuliwa sababu ya udhaifu wa hila za mwanamke.
Nawaonya wanasiasa wa Afrika. Wakiloni leo wanajidai kupromoti Demokrasia,kumbe leongo lao ni kuchochea vurugu na vita Afrika, nchi inaposalia katika miali mikali ya moto na mtutu wa bunduki,wao wachote rasilimali na kuondoka!
Shime, wanasiasa hata wa upinsani wasidhani wanatafuta haki na demokrasia,kumbe wanasababisha nchi zetu zisitawalike.Wakoloni wametoka Libya, walikowachanganya vichwa vijana wasio na ajira, wametoka Irak, sasa wako Syria baadaye watakwenda Iran.
Wanaharakati wanalipwa hela eti kuhamasisha demokrasia na haki za mashoga, wajiulize Yule wanayemtumikia kwa yakini. Harakati siyo mbaya,ujira wa kufanya hivyo wanatoa wapi?
Baadaye, watalipa nini? Haya ya njama za akina Cleopatra kwa akina Julius Caesar na Marc Athony yalishakuwepo mahali pengi duniani. Tuitazame historia.
Leo ni kama jana tu-Leo ni jana ya kesho,leo na jana havina tofauti.
TAMATI
0786 324 074






1 comment:

  1. Naomba coments zenu na nitaziheshimu kwa ajili ya wasomaji wengine

    ReplyDelete