Tuesday, September 3, 2013

ukweli ni nini?


      
Historia ndiyo Darubini kali iliyomwibua mmoja wa Wanafalsafa wakubwa Ugiriki, ambaye anaweza kutwambia nini maana ya Ukweli?
Aristotle wa Athens aliyeishi kati ya mwaka 384 hadi 322 BC. Alipata kusema:
“Truth is agreement with FACTS and REALITY” ,Tafsiri yangu ni kwamba,Ukweli ni mwafaka baina ya habari ya kilichotukia na usahihi ama uhalisia wa mambo.
Kulingana na Aristotle, ukweli huweza kuongopa ikiwa UKWELI nusu-nusu unapowaongoza watu kwenye UONGO.
Aristotle  alisema hivi:
“To say what is that is not or of what is not that is-is FALSE, while to say what of what is that it is, and what is not that is not-is TRUE!!
Tafsiri yangu isiyo rasmi ni kwamba Aristotle alisema kusema jambo kwa namna isivyokuwa namna kitu kilivyokuwa hakika,ni UONGO;wakati kusema kitu kilivyo hakika na ukasema kwamba hakiko hivyo wakati hakiko hivyo huo ni Ukweli.
Aristotle, hutwambia kuhusu UONGO WA UKWELI(The lie of Truth) ambao mfano wake ni kama kudondosha tone la ukweli katika pipa la Uongo.Ukweli hauchanganywi na uongo ukabaki ukweli.Sumu kidogo ya panya haichanganywi na unga au mkate,kikabaki kuwa chakula bali sumu!
Chakula jumlisha sumu ni sumu,basi.
Naam, ‘a little truth drop in the bucket’ matokeo yake ni jamii kuamini uongo na kuufanyia kazi, ndivyo ilivyo hata hapa Tanzania.Jamii hufanyia kazi umbeya,uongo na upumbavu tu!
Watu wengi hata hapa Tanzania hudanganywa kwa ukweli kidogo ndani ya uongo mwingi,na tayari wameathiriwa na sumu ya uongo na umbeya,mishipa yao ya fahamu imedhoofishwa na majungu na uvumi.
Nilishaandika kwamba, Daktari akisema ‘Unaumwa Ukimwi’ ni FACTS-ni ukweli dhahiri. Lakini mpigadebe akisema kwakuwa una kikohozi na kichomi na umekonda-ni ‘Opinion’ ni maoni tu-maoni siyo ukweli halisi,ni kukisia na umbeya tu.Angalia sasa nchi hii walivyo hawatofautishi Opinion na Facts!
Ukweli haufahamiki kwa kusemwa na watu wengi ama kwa njia ya sanduku la kura!
Mwandishi,Derek J.Morris aliandika katika Jarida la MINISTRY la Juni mwaka huu 2013, kama ifuatavyo:
“TRUTH is not determined by opinion poll or popular vote!”
Ukweli hauamuliwi kwa wingi wa kura za maoni za watu wengi vijiweni! UKWELI huweza kusemwa na mtu mmoja mwenye taaluma kama daktari kusema ‘una ukimwi’ ndugu zako na jamaa wote wakashikilia umerogwa!
Ukweli hauamuliwi kwa sauti kubwa na maandamano ya vibaka na wanasiasa wakasema ndiyo NGUVU YA UMMA!
Aristotle amesema watu wengi huchelea kusema ukweli wasije wakachukiwa na umma mkubwa, ‘PEOPLES POWER’.
Watu wengi siyo wa kuamini,na mawazo yao siyo ya kufanyia kazi mara zote,wapo wafuata mkumbo tu,mashabiki na mabingwa wa kuigiza kila jambo na kuangamiza jambii kama tunavyoona leo madawa ya kulevya,bangi na ndoa za jinsia moja!
Bendera kufuata upepo tu! Kizazi hiki kimepotoka mno,kwa kuiga ya Magharibi ya watu wengi, sasa wachache hawana cha kusema,wataalam kama madaktari, wahandisi,maprofesa n.k ushauri wao ulishakataliwa na public opinion.
Siku hizi ‘wengi wape’ japo wapumbavu sana!
Watu wengi, aghalabu mbumbumbu mzungu wa reli fuata mkumbo, propaganda za siasa huishia kuipotosha jamii na kizazi hiki kwamba ndiyo haki za Binadamu.Haki za Mashoga,haki za wasagaji,haki za watoto kutochapwa viboko n.k
Watu wachache wenye haki aghalabu hawana ubavu wa kutetea ukweli usiochanganywa na uongo,umbeya,hisia tu na majungu.
Wakristo wameonywa sana kuwa waangalifu katika kuamua kati ya UKWELI(Right) na uongo(Wrong) kwa kufuata kura za maoni za wajinga wengi(Opinion poll) ama kura za watu wengi wanaopenda uhalifu na uovu(popular vote).
Kuna watu hawataki hata sheria ziwepo ili waingie mitaani na kupora mali za wenzao kwa kisingizio, Maisha ni Magumu!
Wachache wenye hekima wanajua matokeo ya kukosekana kwa sheria,lakini wapumbavu wengi watalaani kuwepo sheria,mahakama,polisi,mgambo,mahakimu n.k hawa wote ni vibaka akilini.
Ukweli na uongo,sharti kuamuliwa kwa muktadha wa mafundisho sahihi ya Neno la Mungu(Biblia n.k)Kwa mfano Zaburi 119:105 HUSEMA Neno la Mungu ni Taa iongozayo miguu ya wenye haki.
Watu wanasema Mungu alishakufa,hayupo na neon lake ni batili,sasa hawa wanakwenda njia gani halafu uwafuate gizani?
Watu wanapotaka kwenda upande wa kweli wa Historia,wanapaswa kugeukia hekima ya Mungu tu basi. Hekima ya Mungu ni Ukweli,haki,amani,upendo n.k
Biblia,kwa mfano husema njia ni nyembamba sana iendayo kwenye ukweli nao wanaoona ukweli ni wachache tu.Wengi huenda kwenye uongo,maana njia ya uongo ni pana hata mbumbumbu huiona.
Njia ya haki huonwa na wenye hekima,ni nyembamba hutazamwa kwa hadubini kali.
Ni kwa sababu hii,watu shupavu wanaotetea ukweli(rejea tafsiri ya ukweli) hawapendwi na wengi;huishia kutengwa,kusulubiwa.
Kusema kwamba kitu hiki hakiko hivyo wakati kweli hakiko hivyo ni hatari,unafanywa kama Nabii Yeremia,Martin Luther King Jr,Martin Luther wa Ujerumani,Socrates,Yohana Mbatizaji,orodha ndefu.
Katika kitabu cha Luka Mtakatifu 3:11-14 Yohana Mbatizaji anapokemea rushwa,ufisadi miongoni mwa maofisa wa serikali fisadi, anapokataza masikini kuporwa wake na mali zao, anaishiwa kunyongwa kijinga.
Nani atatetea kichwa ili akatwe kichwa?
Marko Mtakatifu 6: 17 na 18 hutwambia kwamba ni mtu labda mmoja tu anayekubali ukweli usemwe potelea mbali apoteze maisha yake,kuliko kuacha wajinga wengi waseme uongo na kuufurahia.
Public Opinion, mara nyingi hukinzana na ukweli na uhalisia wa mambo-husema minyoo huletwa na wachawi,na wala siyo uchafu na kula bila kunawa ama kunywa maji yasiyo chemshwa!
Ukisema ukweli utaitwa msaliti! Kuna mifano tele katika Biblia,niiache wengine wananiambia hataki kusoma biblia.Biblia ni kitabu,hawapendi kusoma ila kucheza na kucheka-cheka tu.
Nimesema kwamba ukweli huonwa na wachache tu na husimamiwa na watu shupavu wawili ama watatu tu-wengine bendera kufuata upepo unakoelekea, watu wengi wanafiki tu.
Wanaosema ukweli huitwa waongo na waongo huitwa wakweli.Mara nyingi waongo huenda kinyume cha Historia-The wrong side of History.
Historia inamsema Socrates(469-400 BC) ALIVYOULIWA na utawala wa Athens kwa kukataa umbeya kwamba kuna miungu 391 inatawala juu ya Mlima Olympus!
Walimpa sumu ainywe kwa kutetea kwamba kuna Mungu mmoja na huishi mbinguni tu. Yesu aligoma kufuata dini ya ukandamizi ya Kiyahudi, Martin Luther aligomea mafundisho ya Kipapa, Martin Luther King Jr. ambaye juzi Ndoto yake( (I have a Dream)ilisherehekewa miaka 50 na akina Obama, aliuliwa Aprili 1968 kwa kusisitiza ukweli kuhusu ubaguzi wa rangi Marekani, aliuliwa na Pentagon kwa kutetea ukweli.
Wapo akina Mandela wamesota rumande miaka 27, wapo wengine walifukuzwa kazi n.k
Katika mfululizo wa makala haya nitatilia shaka kila kinachoitwa UKWELI ili kutufanya kuchunguza mambo kwa akili tunduizi(critical mind) kuacha mikumbo na umbeya wa siasa za kipumbavu zinzoleta ugomvi katika jamii hii.
Tutajadili ‘fuata mkumbo’ iliyoleta shida hapa Tanzania, katika Nyanja tofauti siyo siasa tumhata dini zinazoshadidiwa na watu.
Nitakuwa nikitumia nukuu za wanafalsafa,wasomi,wataalam lengo ni kukiokoa kizazi hiki na kuiga na kufuata mkumbo wa kila kinachosemwa ili tuepuke propaganda,matangazo ya uongo redioni kwenye tv na maamuzi ya wengi katika kura za maoni(Opinion polls)
Nitatilia shaka hata katiba mpya itakayoamuliwa na wengi,lakini vipofu wakaacha maoni ya wachache ama mmoja mwenye hekima,mtu wa haki mnyoofu n.k
0786 324 074



No comments:

Post a Comment