Monday, January 28, 2013

MAASKOFU,MASHEIKH NA WACHUNGAJI HATARI KWA NGONO




“Mke wake alikuwa amesafiri;sasa nikalazimika kulala na watoto wa Pastor Marco Pollo(siyo jina lake halisi).
Siku ya kwanza nikalala na watoto,ya pili akasem, “Sarah nakupenda!”
“Nikamuuliza, umenipendaje? Akasema,unaona mke wangu hayupo… nilikataa!”
Baada ya siku tatu,akaingia kwa nguvu chumbani,akanishika na kuniziba mdomo,akanibaka! Siku hiyo nilishika mimba!”
Mwandishi wa safu hii alimuuliza Sarah,kwa nini keshoye hakumchukulia hatua za kisheria Mchungaji huyu,Marco,ili sheria ichukue mkondo wake?
“Niliona aibu; lakini nilimwambia dadangu, akanifukuza nyumbani kwake,nikaenda Kitangiri,kwa kaka yake Mchungaji Marco." Sarah akasema.
Nilikutana na Sarah mwaka 2003, wakati huo nikiandika habari za uchunguzi katika gazeti moja la Jijini Mwanza.
Naam, ilikuwa Machi 4,mwaka 2003, mwandishi huyu alipofika Bugarika,jijini Mwanza kumuuliza Mchungaji huyo kwa kanisa moja la Walokole jijini Mwanza:
Kwa nini alimbaka Sarah,  usiku mmoja,wakati alipokuwa akifanya kazi za ndani nyumbani kwake,mke wake alipokuwa safarini?
Sarah(21) alikuwa akiishi Bugarika,Jijini Mwanza, na alifanya kazi za  ndani nyumbani kwa Mchungaji huyo, Bugarika B, wakati yeye alikuwa akiishi huko Maina,Nyakato.
Baada ya kubakwa,Sarah alishika ujauzito mwaka 2001.Alijifungua  watoto mapacha Oktoba Mosi,2002. Mapa wawili wa kiume na kike.
Sarah, alisema Mchungaji Marco Pollo alikataa kuwahudumia mapacha wale, hata yule wa kiume alifariki Julai 9,mwaka 2003.
Sarah, alifungua kesi Mahakama ya Mwanzo iliyoko Barabara ya Makongoro,Jijini Mwanza ili kudai Mchungaji huyo achukuliwe hatua.
Mahakama ikamwamuru Mchungaji huyo kulipa shilingi 20,000 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya pacha aliyenusurika,baada ya mwenzake kufariki dunia.
Huyu pacha aliyenusurika,Lucy aliishi kwa taabu na mamaye,baada ya pacha mwenzake,Robert kufariki.
Basi, Mwandishi wa makala hii akamuuliza Mchungaji; “kwa nini wewe ni Mchungaji halafu unambaka msichana wa kazi,unamsababishia ujauzito,kisha unakataa kumhudumia hadi pacha mmoja anapoteza uhai?”
Akanitazama,kisha akaendelea kupiga kinanda. Nilimuuliza ikiwa Wachungaji wanaruhusiwa kubaka,kuwapa ujauzito wasichana kasha kuwatelekeza?
Akaacha kupiga kinanda na kusema angejinyonga; kwa sababu kazi hii hiyo ya Uchungaji ndiyo iliyomwezesha kula na kuvaa. Kwamba hakuwa na kazi nyingine isipokuwa hiyo.
Alikiri kufanya kitendo hicho, akasema kama ‘stori’ hiyo ingeandikwa gazetini, angetimuliwa kazi; kwa hiyo aliona ilikuwa heri kujinyonga!
Naam, kwa miaka 10 niliazimu kutoandika ‘stori’ hiyo ya Mchungaji Marco kumbaka Sarah(21) ili kunusuru maisha yake.
Hata hivyo,nimeamua kuandika kisa hiki ili kuwaonesha wasomaji wetu namna gani ilivyohatari kuwaamini na kuwategemea wachungaji,maaskofu,mitume,masheikh,maimam na manabii wa siku hizi wanaoota kama uyoga hapa nchini!
Ukisikiliza mahubiri yao yamejaa uchochezi na fitina.
Baadhi yao wameanzisha vituo vya redio,ambazo sasa tunajua kusudi siyo kuhubiri DINI bali uchochezi,fitina na uchafu-bahati mbaya sana wanatumia vitabu vitakatifu,Qur’an na Biblia kuhalalisha uchochezi wao.
Utaona,wanavurugana mno na washiriki wa makanisa na misikiti wanayoongoza.
Wakati mwingine wamebaka hata vichekechea,wamepora wake za waumini wao, wanapowatisha kwa nguvu zao za MIUJIZA na ushetani uliodhahiri,mwisho hujipatia pesa na kununua magari ya fahari.
Rai yangu katika safu hii leo ni kwamba, kama serikali ya Tanzania itaendelea kuwaamini wachungaji,maaskofu na manabii hawa wanaomea kama uyoga, basi Tanzania iko hatarini sasa kuliko jana.
Nadhani, tunakumbuka kilichotokea Kanungu,Uganda,zama za Father Kibwetere na wenzake.Waliteketea raia 530 katika ndimi za moto,kwamba  hiyo ndiyo staili ya kuendea motoni!
Wamebaka watoto,hata wanafunzi.Hawa mafather wamelawiti watoto wa kiume,wamekwapua wake za waumini.
Wanafanya biashara ya maji ya Baraka toka Israeli na kutajirika; wanaendesha magari ya fahari kuliko hata wabunge. Pesa walitoa wapi kama si ufisadi wa kutisha?
Bahati mbaya sana, serikali ya Tanzania imeendela kuwaamini sana matapeli hawa wanaotaharukisha umma kwa kutumia uchawi na nguvu za giza kutoka Nigeria,Jamhuri ya Kongo na Marekani!
Wamewatapeli Watanzania kwa njia anuwai,serikali ikiwa kimya.Sasa wanachochea vita miongoni mwa Wakristo na Waislam.
Wachochezi hawa wamejivika Uislam wenye itikadi kali na Ukristo wenye itikadi kali, “Extremism” wanawachochea waumini wao kwamba kifo ni kifo hata usipokufa kwa risasi za polisi,utakufa kwa Ukimwi!
Migogoro,maandamano na fujo vimeanzia makanisani na misikitini ambako wachungaji,maaskofu,manabii na mitume hawa hupora zaka na sadaka za waumini wao hadi wanapoaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe serikali ikiwa kimya!
Kwa nini wakwapuzi hawa wa fedha za Watanzania hawachukuliwi hatua za kisheria?
Katazame miradi ya ujenzi wa makanisa. Ilishasimama miaka 30 iliyopita,baada ya sadaka kuporwa.Hawana aibu, wana ndimi za Ibilisi, na jeuri na wafedhuli kupindukia.Hufika wakati wakaitisha hata serikali,kwamba wataiombea ipinduliwe!
Kuna baadhi ya viongozi wa siasa wanaoshirikiana na hawa kufanya usihiri na uchawi ili wachaguliwe wakati wa chaguzi za kuwapata viongozi wa kisiasa.
Sasa,Watanzania tunashuhudia misikiti na makanisa yanavyoshindana nani awe rais wa Tanzania mwaka 2015!
Inawezekana Kenya wasipigane katika Uchaguzi wa Machi mwaka huu 2013,lakini mwaka 2015 Tanzania iko hatarini kuliko wakati wowote lilipoanza kuwapo Taifa,Desemba 9,mwaka 1961.
Hayati Mwalimu Nyerere aliwakemea watu hawa,viongozi tulio nao wanawaogopa;wanachelea kuwachukulia hatua kali za kisheria.
Matokeo yake, Tanzania sasa iko mikononi mwa hawa watu wa dini ambao wanachochea waumini wao kupigana,kwa sababu ya tofauti na itikadi za kidini.
Hakuna kuvumiliana tena,makanisa yanachomwa moto na Waislam hao uchwara,na sasa Wakristo nao wanataka kujibu mapigo!
Wanasema ni ujinga kusamehe 7 mara 70 kama alivyosema huyo Yesu wa Nazareti.
Tanzania iko hatarini kuteketea katika miali ya moto wa mapigano ya kidini.
Ibilisi, anapojivika ngozi ya chui na kujilisha ‘kondoo’ walionona;kuwabaka wasichana kama Sarah na kuwapa ujauzito, serikali hii ya Jakaya Kikwete inapumbazwa kwa kupigiwa gitaa,inalala usingizi na kudhani kuna amani na salama misikitini na makanisani!
Amani ya nchi inanajisiwa misikitini na makanisani siku hizi,kuliko wakati wowote.
Shime, serikali iwamulike kwa kurunzi kali hawa masheikh,maimam,mitume na manabii na wachungaji wa siku hizi, ambao ni wachungaji wa mishahara tu wanaojilisha kwa kondoo walionona kama akina Sarah!
Alamsik
 
 
 
 
 

1 comment:

  1. watumishi wengi wa Mungu wametelekeza kazi ya Mungu na kutamani starehe na kuendekeza kujionyesha kwenye mitandao na ndoa na kufanya Happy birthday zao kwa mamilioni ya pesa wakiacha kondoo wakiwa kwenye hali ya sintofahamu na wale ambao hawajafikiwa wakibaki kwenye hali ngumu. hadi sasa kuna vijiji ambavyo havina makanisa lakini watu hawajali kuna kila sababu ya watumishi wa Mungu kudaiwa damu za watanzania wanaokufa kila siku pasipo wokovu huku watu wakipiga kampeni za kupata vyeo na kutafuta heshima huku maelfu wakiwa taabuni ebu wapendwa tuokoe kwanza roho za watu watoke kwenye ufalme wa giza tunawashukuru WAnawake wa Tanzania Assemblies of God kujali UMISHENI NA KUCHANGIA ZAIDI KAZI YA MUNGU NI VIZURI SOTE TUIGE MFANO HUO WA KIMUNGU SANA HONGERA MKURUGENZI KWA MOYO ULIONAO WA KIMUNGU MAMA FARAJA HAMULI.

    ReplyDelete