Tuesday, June 28, 2011

Mheshimiwa Spika, naomba kuondoa shilingi kwenye bajeti ya Waziri Ngeleja!

TANESCO wanataka serikali iwape takriban shilingi za TANZANIA trilioni moja ili mgawo huu wa umeme umalizike!
 Hili ni janga kubwa kwa wananchi wa Tanzania. Siku hizi tunalala gizani, wizi,vibaka, siyo jambo la kuepuka,kwa sababu ya giza.
 Tunavaa nguo zenye kukunjamana, sababu pasi bila umeme?
 Usafi... sasa ni jambo la kutazama kwa mbali.
 Ndiyo maana tunakuuliza, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, bora ungejiuzulu hata kabla ya Bajeti yako kusomwa bungeni
 Kwanini Ngeleja hujajiuzulu uwaziri wa Nishati na Madini, wakati hatuna umeme? Maji nayo hayapandi katika vilima vya Mwanza pasipo umeme, televisheni hatuangalii, kazi hazifanyiki sasa maana kompyuta bila umeme,ni kama ugali bila mboga bwana!
 Ni kwa sababu hiyo, niombe muongozo wa spika,ili nimwondolee shilingi, Ngeleja kwenye bajeti yake hata kabla ya kusomwa bungeni!
 Kwa nini tulale njaa..kisa umeme umekosekana hata kusaga unga? Magazeti nayo hayachapwi sasa,kazi hakuna,barafu hazitengenezwi, kazi zifungwe tukale wapi Ngekeja?
 Wewe ni mtu mmoja,jiuzulu ili kunusuru maslahi ya Watanzania?
 Kwanini useme mgawo utakwisha,kumbe umegeuka mkali zaidi?
 Siku tatu bila umeme?
 Ngeleja ondoka bwana kazi imekushinda!

No comments:

Post a Comment