Friday, June 17, 2011

WELCOME IN MWANZA,THE ROCKY CITY

LANGO Kuu la kuingilia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, iko takriban kilomita 100 tu kutoka hapa jijini Mwanza.

Watalii kutoka mataifa mbalimbali wanaotaka kutembelea Mbuga hizo zilizo miongoni mwa maajabu ya Dunia,yawapasa kutafuta lilipo jiji la Mwanza, ili wapate mahali pa kuanzaia.
Licha ya kuwa kitovu cha nchi nyingi za Maziwa Makuu:Rwanda,Burundi,Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Kenya na Uganda, Mwanza jiji lililopo  kandoni mwa Ziwa Victoria,lina vyanzo tele vinavyoweza kuwaongezea wananchi kipato pamoja na serikali.

Jiji hili liko Kusini mwa fukwe za Ziwa hili kuu kuliko yote Afrika; ziwa ambalo ni miongoni mwa maziwa machache sana Ulimwenguni lenye maji baridi; na linalotoa sangara wanaouzwa katika masoko takriban yote ya Umoja wa Ulaya.

Mwaka 1892 ndipo Mwanza ulipoanzishwa na Mjerumani, EAMIN PASHA ili kuwa Makao Makuu ya kiutawala, ya maeneo yote ya Ukanda wa Ziwa, pia kuwa kituo kikuu cha Biashara kilichotumika kusafirisha nchi za nje zao la pamba.

Mwaka 1978 Mwanza ikawa na hadhi ya Manispaa; kabla ya kuwa Jiji kamili mwaka 2000. Lilikuwa jiji la pili nyuma ya Dar es salaam.

Asilimia 32 ya wakazi takriban milioni moja wa jiji hili wameajiriwa, wakati 27 hawana ajira. Wengi wameajiriwaq sekta binafsi, waliobaki hujishighulisha katika kilimo, biashara ndogo ukiwemo umachinga, na uvuvi mdogo unaowaingizia kipato cha wastani wa Dola za Marekani 21(shilingi takriban 30,000 tu kwa mwezi.

Mwanza kuna viwanda nane vinavyosindika sangara wanaouzwa sana Ulaya na kuliingizia Taifa mabilioni ya fedha. Pia kuna kuna viwanda sita vya kusindika pamba na kuzalisha mafuta ya kupikia. Kuna kiwanda cha Bia(Tanzania Breweris Limited), kiwanda cha vinywaji baridi cha Coca Cola, bekari takriban 100 za mikate, mashine za kusagia nafaka, viwanda vya mbao, kiwanda cha nguo cha Mwatex, magereji, viwanda vya bidhaa za plastiki, magodoro,sabuni vya chakula cha mifugo n.k.

Kuna mahoteli na vitega uchumi vingi. Miongoni mwa vitega uchumi vipya katika jiji hili, ni pamoja na Nyumba 280 za Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma, PPF, zilizokwisha jengwa katika eneo la Kiseke, ambazo zinapangishwa kwa wakazi wa jiji ili kuwapunguzia adha ya makazi.

Nyumba hizo ni sehemu ya mradi wa ujenzi wa nyumba 1,149 katika maeneo anuai ya jiji, ili kuliingizia Shirika hilo mabilioni ya fedha, licha ya kuwaondolea wananchi adha ya upungufu wa makazi.

Pia PPF wamejenga jengo la kitega uchumi, maarufu kama PPF Plaza, katika Barabara ya Kenyatta, kwa gharama ya sh. Bilioni 10.6; .Jengo hilo la ghorofa tisa limekamilika,  li na maofisi,maegesho ya magari, migahawa mikubwa yenye hadhi ya Kimataifa, kumbi za mikutano ya Kimataifa, maduka makubwa; na linakadiriwa kuingiza shilingi Trilioni 1.1 kila  mwaka.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, NSSF, nao wamejenga jengo la kitega Uchumi katika barabara hiyo ya Kenyatta, na tayari wamepewa viwanja 1000 ili kujenga nyumba za makazi, katika eneo la Nyamuhongolo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, anasema lengo ni kulifanya jiji hili kuwa kitovu cha biashara na utalii katika nchi za Maziwa makuu. Rais Jakaya Kikwete, alisema alipokuwa akizindua akifungua nyumba za makazi za Kiseke, kwamba katika kipindi cha utawala wake ataiacha Mwanza ikiwa California ya Tanzania katika sekta ya uwekezaji.

Hadi mwishoni mwa mwaka 2000 pato la mkoa mzima lilikuwa Shilingi Bilioni
643.595.
.Ongezeko la kipato katika eneo zima hili hutokana na ongezeko la vitega uchumi vilivyokwisha tajwa, vinavyotokana na sekta za samaki na madini.

Kilimo kimegawanyika katika mafungu mawili:
Kilimo cha mazao ya Biashara na chakula. Pamba ndilo zao linaloongoza kwa kuingiza kipato. Mwaka 2000 mkoa mzima wa Mwanza, kilimo peke yake kilichangia sh.308.925 Bilioni katika pato la mkoa. Hii ni sawa na asilimia 48 ya pato lote kwa mwaka.

Misitu,samaki, madini na Utalii kwa pamoja viliiuingizia mkoa wa Mwanza sh.199.515 Bilioni mwaka huo wa 2000
.Pato hilo ni sawa na asilimia31 ya pato lote la mkoa. Madini na samaki ndizo sekta zinazokua haraka na kuungizia mkoa kipato kikubwa sana. Mgodi wa Dhahabu wa Geita uko maili chache toka Mwanza mjini.

Sekta ya Biashara na Viwanda, kwa pamoja mwaka 2003 zilichangia sh. Bilioni 115.847 katika pato la mkoa.
Hili pato la sekta za Viwanda na Biashara lilikuwa sawa na asilimia 18 katika pato zima kwa mwaka katika mkoa wa Mwanza.

Sekta zingine zinazojumuisha na Utalii, ziliuingizia mkoa huu sh. Bilioni 19.308 katika mwaka huo, sawa na asilimia 3 ya pato lote la mkoa mwaka 2003.

Tangu mwaka 1995 pato la mkoa mzima wa Mwanza lilikuwa likiongezeka kwa asilimia 215. Yaani kutoka sh. Bilioni 203.939 mwaka huo wa 1995 hadi kufika sh. Bilioni 643.595 mwaka 2000.

Mbali na kipato hicho, bado wakazi wa eneo zima hili wanakabiliwa na changamoto za ukosefu wa miundombinu, hospitali,chakula, shule,ili kuwaongezea wananchi mahitaji ya lazima, huduma za jamii,ajira na maisha bora aliyoahidi Rais Jakaya Kikwete.

Mbali na kipato hiki, Mwanza ingali "Imelala" kufuatia kuwa na fursa tele na vivutio vingi vya utalii.Utalii katika Tanzania ni sekta ya pili kuliingizia Taifa kipato, nyuma ya kilimo. Huchangia asilimia 16.5 ya Pato la Jumla la Taifa(GDP); lakini Mwanza haijavuna vya kutosha kutokana na utalii.
 Ni kwa sababu hii jiji hili lingali linahitaji uwekezaji katika fursa tele katika nyanja tofauti za madini,utalii na kilimo.

Mwanza kuna visiwa vya Rubondo,maarufu kwa sokwe na jamii za jani,kuna Kisiwa cha Saa Nane,, eneo la Kijereshi ambalo ni lango kuu la kuingilia Serengeti.
 Kuna Makumbusho ya Bujora,mahali watumwa walipohifadhiwa kabla ya kusafirishwa hadi Bandari ya Zanzibar, tayari kuuzwa Ulaya na Arabuni.

Kuna miamba yam awe ya Bismark, mapango ya Hendbezyo, katika kisiwa cha Ukerewe, ambayo wenyeji walijificha wakati wa vita vya kikabila. Kuna milima ya Isamilo, ambako John Speke alisimama, alipokuwa akikagua Ziwa Nyanza(kabla ya kuitwa Victoria), kwa heshima ya Malkia wa Uingereza.

Hili ziwa ndilo chanzo cha Mto Nile unaosafiri kilomita zaidi ya 6,000 hadi Misri. Kuna mawe yanayocheza dansi, katika kisiwa cha Ukara, kuna mti wa ajabu uliokatwa, kesho yake ukaota! Upo mti mwingine, ukidondosha majani katika maji ya ziwa Victoria, basi majani hayo hugeuka mamba!

Magu kuna kaburi la Mpelelezi, Henry Stanley, Igoma kuna makaburi ya M.V. Bukoba.
Upo mti uliotumiwa na Wajerumani kunyongea Wazalendo, katika makutano ya Barabara za Makongoro, Kenyatta na Nyerere, jirani na jengo la CCM,Mkoa.
 Mti huu siku hizi umekatwa,lakini kisiki kingalipo.
 Hivi vyote ni vivutio vya utalii vinavyoweza kuingiza kipato kwa watu na kodi serikalini.

Mwanza ikitumia fursa zote kama mahoteli ya kisasa(yatakapojengwa kwa ubia na wawekezaji)uwanja mpya wa ndege wa kimataifa,maduka, kumbi za starehe n.k zitapunguza Umasikini na Kuongeza Kipatp(MKUKUTA).

Kwa kuwa mji huu unafikiwa na reli, kuna barabara nzuri ya rami kati yake na Nairobi,Arusha hadi Dar es salaam. Kuna uwanja wa ndege unaopaswa kupanuliwa hadi kuwa na hadhi ya kimataifa,kwa kuwa unatumiwa hata na ndege za mashirika ya njemkama Kenya Airways.
Miaka michache ijayo barabara iendayo Kampala, Uganda, Rwanda na DR-Congo itajengwa, bandari yake inayotumiwa na meli za abiria na mizigo hadi Kisumu na Jinja, itapanuliwa, na Mwanza utakuwa kituo kikuu cha Biashara katika nchi zote za Kenya,Uganda,Tanzania, Burundi, Rwanda na Congo.

Hadi sasa uwanja wake wa ndege ndio unasafirisha madini kama dhahabu, na pia sangara hadi Ulaya na Marekani.Samaki wa Mwanza husafirishwa kwa barabara hadi Congo, Afrika Kusini, Musumbiji, Kenya na Malawi.

Mpaka mwaka 2003 Uwanja wa ndege wa Mwanza, ulisafirisha wageni wa Kimataifa 5,344; wasafiri wa ndani 125,499 na jumla ya tani za mizigo 13,426.Hiki ni kiwango kidogo kulingana na hali halisi ya uwanja huo ulioko kandoni mwa sangara migodi ya dhahabu na almasi, pamba na kahawa.
mtanzania
Huu ni uwanja wa kwanza nchini ndege ilipotekwa na watu walioitwa wahuni miaka ya 80 hadi ulaya! Ni uwanja unaotarajiwa kubadili maisha ya wakazi wa eneo zima hili katika enzi hizi za utandawazi.

 0786 324 074

No comments:

Post a Comment