Thursday, May 10, 2012

unataka uatajiri?-8


                           *Kulikuwa na Mkono wa Freemasons katika Ajali ya Titanic
KILA palipo na utajiri:Mafuta(Dhahabu Nyeusi), Almasi, Dhahabu zenyewe, pembe za ndovu na faru,gesi n.k) aghalabu  pana vita kali.
Katibu Mkuu wa Pili wa Umoja wa Mataifa,Dk. Darg Hammarskjold wa Sweden, alifanya kazi tangu Aprili 10 mwaka 1953 hadi Septemba 18 mwaka 1961 akafa.
Alikufa kwa ajali ya ndege nchini Congo(JK Kongo) wakati wa maasi ya Shaba na Katanga. Nani anachochea maasi Kongo? Hadi leo ni nusu karne, vita vinapamba moto Congo.
Shirika la Ujasusi la Marekani(CIA) na washirika wake, walichochea vita na maasi huko Shaba na Katanga(majimbo tajiri ya rasilimali) wakamkamata Mwanamapinduzi, Patrice Emery Lumumba, na kumuulia mbali.
Lumumba, alikuwa na visheni ya kijamaa, kutaka rasilimali za Congo ziwe kwa manufaa ya Wakongo, rasilimali za Waafrika ziwe kwa ajili ya Waafrika wenyewe. Akawakosea hawa majahili.
 Wakawachochea akina Moise Tshombe, Joseph Kasavubu,Joseph Desire Mobutu na vibaraka wengine, Lumumba akauliwa kinyama Januari 17, mwaka 1961.
  Dk. Darg Hammarskjold akasafiri kwa ndege kutoka New York hadi Congo ili kusuluhisha vita, Septemba 18 mwaka 1961 akafa eti kwa ajali ya ndege.
Nataka nikwambie msomaji. Ajali za ndege zimewamaliza wanamapinduzi:Samora Moises Machel, Kanali Dk.John Garang de Mabior, Juvenal Habiarimana na Cyprian Ntarwamira,orodha ni ndefu.
Lumumba alipokufa, akina Moise Tshombe na Mobutu wakatawala Congo ambayo waliita Zaire.
Congo ina makabila zaidi ya 200, ni nchi yenye almasi,dhahabu,mbao za thamani, fedha,uranium n.kWakaiba madini wee. Mobutu alipokufa huko Rabat,Morocco Septemba,  1997, alikuwa kaficha Ulaya Dola za Maremani milioni sita,utajiri sawa na deni la nje la Congo wakati huo.
Mobutu eti alibadili jina na kuitwa Kuku wa Zabanga Mobutu Sese Seko, akaibadili Congo kuwa Zaire,tukadhani mzalendo-kumbe kibaraka wa Wazungu aliyejificha katika ngozi ya chui!
  Penye rasilimali za thamani kama mafuta,dhahabu,almasi, gesi,uranium n.k kuna vita,kuna vurugu. Penye bahari kuu,milango bahari na mifereji kama Panama,Suez n.k kuna mivutano na vurugu za mabeberu, ndiyo Libya,Misri,Nigeria,PANAMA nitaeleza mbele ya safari.
 Bosnia Herzegovina, mwaka 1995 walikufa watu 200,000.Rwanda mwaka 1994 walikufa 800,000.Lakini, kwakuwa hakukuwa na almasi,mafuta na dhahabu na pembe za faru na ndovu,hawakwenda mapema.
Walimsukumia mzigo Boutros Boutros Ghali wa Misri,kwamba alishindwa kuchukua hatua alipokuwa Katibu Mkuu wa UN. Wazungu na mwavuli wao wa NATO hawakwenda huko;kulikuwa na kitu gani cha kurejesha gharama zao? Hata Hague hawakwenda huko.
 Kwenye mafuta: Agosti mwaka 1990 Saddam Hussein alipoivamia Kuwait,kwa sababu zile zile kama za Sudan Kusini na Sudan leo za kuibiana mafuta, tayari UN wakaamrisha NATO na kuigilia kijeshi mzozo huo.
 Novemba 19900 hadi Januari 1991 tayari madege ya vita ya Wazungu yalishanyesha mvua kubwa ya mabomu Irak, Saddam akajisalimisha Aprili 1991.
 Baadaye mwaka 2003, akapinduliwa na Bush mtoto, maana ‘Bush Baba’ aliacha kiporo-Saddam alinyongwa kwa kamba nene shingoni, 2006.
Mfereji wa Panama(Panama Canal) ulisababisha Rais Manuel Noriega kupinduliwa na kutiwa mbaroni na CIA utadhani kibaka,walisema alijihusisha na biashara haramu ya mihadarati! Huwezi kushindana nao,ukapona!!
 Ilikuwa Januari 1980 Noriega alipopinduliwa na kufungwa pingu,kasha kufunguliwa kesi ya mihadarati.Marekani wakitaka kitu Fulani,rais akijidai kujua anatiwa mbaroni, inatangazwa kwamba anauza madawa ya kulevya, sasa utasemaje?
Salvador Allende  wa Chile, zlizingirwa na CIA,akakubali kujipiga risasi na SMG yake aliyokuwa amepewa na rafikiye, Fidel Alejandro Castro Ruz wa Cuba, wakamweka rafiki yao, nitaeleza kisa hiki siku nyingine.
  Kifo cha Laurent Desire Kabila,Januari 16 mwaka 2001 huko Kongo kina mkono wa hawa jamaa, Mafreemasons,Kabila alijidai mjanja, wakatumia Body guard wake kumfyatua, hadi sasa Kongo hakuna amani,kuna akina Bosco Ntaganda, sijui Thomas Lubanga na akina Jen. Nkunda ambao ukitazama wanafungamana na Rwanda na Uganda hivi,kuna mahali mali ya Congo inavushwa.
 Naam, Guns for natural resources! Kongo ni nchi tajiri,maize ya kijani hayataki kuondoka. Mashirika ya Umoja wa Mataifa, eti ya kulinda Amani(UN Peacekeeping Missions) wanapofika nchi yenye vita vya rasilimali,hawalindi amani, wanakalia mahali kwenye dhahabu,almasi au mafuta na gesi-basi wanapora!
Ziwe pembe za ndovu au za faru, wanapora na kusafirisha njia za panya hadi kwao. UNAMSIL huko Sierra Leone(Milima ya Simba) mwaka 99-2002 ndiyo biashara waliyofanya huko,wakipora almasi za damu,mbao n.k
 Congo,kuna MONUC ambao wakati Fulani wanakutwa wakipora madini, wanaacha raia kushambuliwa na waasi nao kukimbilia Rwanda huku, wao wanapora na kujitajirisha…(This is Africa)!
Huko Irak, UNIKOM lazima wawe wanamiliki visima vya mafuta,wanaomba mabomu yaendelee,ili muda wa kukaa huko uendelee,usishangae mabomu mengine wanalipua wao!
 Huko Sahara Magharibi, MINURSO wapo wanataza cha kupora ili watajirike! Unataka Utajiri? Uko Afrika, badala ya sisi wenyewe kutumia rasilimali zetu kwa akili, tunagonganishwa vichwa kama makondoo tu,kisingizio,utawala bora, demokrasia,rushwa,ufisadi…hatuwezi kuondoa haya mpaka bunduki?
  Wakimbizi, nalo ni ‘deal’ kwa mashirika kama UNHCR,UNICEF,FAO,WFP hata ILO n.k. watauza hata mahema hhuko Dar na Mwanza halafu wajenga mahekalu makubwa,ukiuliza unaambiwa, “jamaa yuko na UN Mission” labda Juba hivi au Congo.
 Vita     vina leta utajiri kwa watu wa Ulaya, wananeemeka sana, wanaomba maasi yaendelee.
Nataka kusema kwamba, amani hakuna. Mungu alishaacha kulinda amani. Tazama Ufunuo 7:1-3, Isaya 24:17-20 na Danieli 2: 43-45 uone kwamba kuna kila sababu kusema ni SIKU ZA MWISHO.
Tujadili kidogo kiporo chetu cha meli kubwa ya Titanic ILIYOZAMA huko Bahari ya Atlantic.
 Titanic, iliitwa “The Unsikable” kwa sababu  ilithibitishwa kutozama kwa namna yoyote.
 Basi,ilizama kwa sababu ya Ibilisi na maajenti wake Freemasons.
 Saa nne na dakika 20. Ni usiku wa manane wa Aprili 15, mwaka 1912. Hukuwepo na mimi sikuwepo, wakati huo-imepita miaka 100 kamili. Titanic ilianza kupotelea katika mawimbi makali ya Atlantic.
 Ilikuwa meli ya fahari sana kupita zote wakati huo,iligonga Mlima wa Barafu,ikaanza kupoteza mwelekeo wake.
 Jumla ya watu 1,503 hatimaye walikufa katika ajali ile ya kihistoria, na kulikuwa na majeruhi wengi.
Ajali mbaya zaidi ya meli duniani ni ya Feburuari 26,mwaka 1916 meli ya Provence ya Kifaransa ilizama Mediterranean na kuuaa 3,100. Kwanini haikumbukwi? Hii nayo ‘cha mtoto’.Uchina waliwahi kufa watu 6,000 katika ajali ya meli mwaka 1948,lakini watu hawaambiwi haya,isipokuwa Titanic tu.
 Meli hii Titanic Unsikable,ilikuwa na uzito wa tani 46,500, ilianza kuzama polepole katika muda usiopungua saa tatu hivi. Iliundwa imara sana,lakini ‘Unsikable’ ilizama na kukomesha kiburi cha watu cha utajiri.
Ilikuwa na kimo cha futi 883. Jioni, Aprili 14 mwaka huo 1912 meli hiyo ikiwa safarini baharini Atlantic ilikuwa ikipasua mawimbi shwari kabisa.
Ilikuwa ikienda jijini New York, Marekani na ilitokea Southampton,Uingereza. Meli hii iliambiwa kwamba baharini kulikuwa na mabonge ya barafu, hawakusikia. Ni hapa tunapoambiwa,Nahodha wa meli alipewa maelekezo kuwazamisha watu Fulani waliokuwemo melini,kwa sababu ambazo wao Freemasons walizijua.
 Kama maili 20 hivi nyuma ya Titanic kulikuwa na meli nyingine ikija-CALIFORIAN- ikazima injini zake,ikichelea kugonga milima ya barafu na kuvunjika kasha kuzama.
 Titanic waliziba masikio. Ni kawaida kwa Aprili na Mei baharini kuwa na milima ama mabonge ya barafu makubwa na marefu mno.
Mchanam saa 5:40 tayari Titanic ilikwishapinduka na ijini zake zilikwishaipeleka harijojo.
 Kulikuwa na meli nyingine(The White Star Line) ya kuratibu safari za Titanic ilikuwa ikikatisha bahari ya Atlantic,haikufua dafu ili kuzuia Titanic isizame,maana ilikuwa kwa maelekezo ya Freemasons.
 Angalia, abiria waliambiwa meli ilikuwa inazama,wakakataa kuingia katika boti za uokozi.Waliendelea kucheza muziki mtamu na kukamata ‘Kilaji’ tu, wengine walifunga ndoa humo-walipuuza onyo.
Niliwahi kuona Filamu moja kwamba kulikuwa na maharusi mle,mmoja akafa mwingine akanusurika, Titanic ilikuwa na starehe zote ndani, ndiyo maana watu walioambiwa wajiokoe wakakataa. Hawakuamini “Unsinkable” ingezama hata siku moja.
Wanaume walikataa kupanda boti za uokozi wakasema wanawake na watoto kama waliogopa basi wapande hizo boti, “Haitazama!’ walisisitiza.
Walisalia ndani ya meli hii hadi ilipozama kabisa vilindini,mashua zikajaa watu wengi,wao wakakosa nafasi hatimaye.
 Meli ya Uingereza, Carpathia,ilisikia mlio wa kuomba msaada ikarudi na kupita eneo lile la ajali.Iliokoa watu 712 tu waliokuwa katika zile mashua za TITANIC ILIYOKWISHAZAMA.
 Eneo la ajali hii ni karibu na Pwani ya New Foundland. Hii Titanic-white star-nyota nyeupe ilikuwa ya Uingereza,na ilizama kwa maelekezo ya Freemasons,kulikuwa na MATAJIRI ambao ilikuwa hapana budi wafe kama Freemasons walivyotaka,nahodha alipewa agizo. Sijui unaelewa?
 Meli hii inaacha simulizi, naomba mtafute habari zake, msinisumbue kwa maswali.Titanic inafananishwa na kuzama kwa dunia hii,watu wanaambiwa ajali inakuja,hawasikii ya wahubiri.
  Tazama Lukaa 21:35 utaona zama za Gharika ya Nuhu. Duniani kuna vita siku hizi Luka 21:9,10 na ni vita kuu ya dunia inayoongelewa hapa hadi Luka 21:11
 Isaya 24:19-20 husema dunia inavunjika. Dunia ina uzito wa tani 6,580,000,000,000,000,000,000!!
Hizi ni trilioni bilioni 6.6 hivi kipenyo chake nikama maili 7,926 Ikweta na 7,900 Ncha ya Kusini na Kaskazini. Biblia inasema dunia hii itaanguka imezidiwa uzito,uzito wa dhambi na mauaji ya kinyama na uhalifu na watu kupenda utajiri wa damu kama hao wanaoniomba niwaelekeze ofisi za Ibilisi!
  Hawa nao wataanguka katika hii The worst disaster of the 21st millennia. Tutapataje kupona? Tubuni dhambi, na UN wamtegemee Mungu.
0786 324 074

No comments:

Post a Comment