Monday, December 24, 2012

HAKI ZA BINADAMU MAREKANI



MWAKA 1970.mfuasi wa siasa za Ki-Marxi, Salvador Allende,alikuwa Mkomunisti wa Mwanzo huko Latin Amerika kuwa kiongozi wa nchi.
Iliwatisha mabeberu, Mkomunisti kuwa Rais nchini Chile.Allende alianza kutaifisha mabenki na viwanda vilivyomilikiwa na mabepari;viwanda vya makaa tam awe na chuma.
Akawapora makabaila ardhi na kuwagawia wakulima wadogo. Nadhani,msomaji unajua kilichotokea Zimbabwe, “R.G”Mugabe kuwapora ardhi walowezi na kuwapa wakulima wadogo wa Zimbabwe.
Kama rais anataka kuchukiwa na Marekani na Ulaya,ni kuwapora ardhi mabwenyenye na kuwapa wazawa ardhi hiyo ili walime na kujikimu. Hujuma zikaanza,mfumuko wa bei ukapanda.
Mabeberu wakaanzisha vurugu kwa kuwatumia vijana wadogo,Chile ikajaa maasi kila mahali.Jeshi lililazimishwa kumpindua,Allende akajikuta anazingirwa na wafuasi wake wakajikuta katikaji ya adui.
Miji yote mikubwa ya Chile ikajaa uasi, kama ilivyotokea Libya,Misri,Tunisia na Syria.
Mwaka 1973,jeshi likampindua Allende.Jeshi hilo kama kawaida lilisaidiwa na Shirika la Ujasusi la Marekani(CIA),ALIPOONA KAZINGIRWA kila upande,akaazimu kujimaliza yeye mwenyewe kuliko kukamatwa na waasi.Alijipiga risasi kwa Bunduki,SMG aliyopewa na rafikiye, Fidel Alejandro Castro Ruz wa Cuba.
Ndipo alipoanza kutawala Jenerali Pinochet ambaye tumeona habari zake juma lililopita.Pinochet, aliwekwa mamlakani Chile kwa msaada wa CIA,yaani rais aliyechaguliwa na wananchi Kidemokrasia akapinduliwa na vibaraka wa Marekani,wanajeshi.
Marekani inapoimba kuleta demokrasia duniani,mbona tena raia wa Chile wamchague rais wao halafu aje kupinduliwa na jeshi,tena kwa msaada wa CIA?
Nataka msomaji amaizi kuwa,Marekani na washirika wao wanapojidai kuimba demokrasia,basi huwa na AJENDA YA SIRI.
Hakuna rais anayeingia mamlakani katika nchi yeyote yenye rasilimali nyingi,hasa hapa Afrika,akabinafsisha makampuni ya Wamarekani na mabepari wengine akaachwa,wao hutaka viongozi kama hawa wa sasa ambao wametkeleza masharti yote ya Benki ya Dunia na IMF ya kubinafsisha mashirika ya umma na mabenki,hata kama yalikuwa na faida kubwa.
Ubinafsishaji ni sera ya kibeberu,na viongozi wa kijamaa walitaifisha makampuni hayo ya kinyonyaji,na kufanya rasilimali za nchi kama migodi,wanyamapori,ardhi kuwa mikononi mwa umma husika wan chi hiyo.
Tunajadili,kilichofanya viongozi wa Uhuru,akina Nyerere,Gamal Abdel Nasser,Ahmed Sekou Toure,Lumumba,Kwame Nkrumah na wenzao,kuanza kuvutana na mabeberu. Baadhi yao waliuliwa ama kuondolewa mamlakani kwa njia ya jeshi kuasi na kupindua serikali za kiraia.
Leo watu hupiga kelele wakidhani viongozi tulio nao wa vyama vyote wana weza kujiondoa mikononi mwa ubepari uliorejea duniani kwa njia ya Ubinafsishaji!
Hivyo, Amerika Kusini Mabeberu walimwondoa Allende wakamweka Pinochet,Dikteta ambaye alitokea kutesa raia wa Chile,akaua zaidi ya watu 2000.Wengine walipotea katika mazingira ya kutatanisha, hata waandishi wa habari takriban 7,000 walijikuta wakizuiliwa katika viwanja vya michezo.
Watu walifungwa pasipo kufikisha mahakamani Sasa shangaa kama madiketa wanaolindwa na Marekani kama hawa akina Pinochet,ndiyo demokrasia ya Marekani?
Nimeleta kisa hiki,kumjibu mzungu wa reli mmoja aliyenipigia simu kusema madikteta hawajawahi kutengenezwa na Marekani na Ulaya,bali hustawishwa na rasilimali za nchi zetu.
 Huu ni ujinga uliopindukia. Hakuna dikteta atakayedumu bila kulindwa na Ulaya na Marekani.Akina Jean Bedel-Bokassa, Nguema Mbasongo Teodoro wa Equatorial Guinea, wanalindwa.
Wanalindwa,ili waibe fedha na kuficha Uswisi ama wapore rasilimali na kupeleka ng’ambo,wanapewa hisa katika makampuni yaliyobinafsishwa kwa bei chee.Wananchi wanapolia kwa maisha magumu, makampuni haya hulifadhili jeshi na kulipa hata mishahara ya polisi kama walivyofanya Nigeria zama za Dikteta Sani Abacha, ambaye alikuwa mshirika wa makampuni kama Royal / Shell, Chevron,Total n.k
Kuna wajinga wengi leo,hawajui historian a kwa sababu hiyo hawatajua kesho na leo.Kama hujui ya jana aslani huweza kujua ya leo na kesho.
Dikteta Pinochet aliyeingizwa mamlakani na CIA kwa njia ya mapinduzi ya kijeshi, akapiga marufuku uchaguzi katika nchi hiyo kutoka 1974-1985. Naam, hii ndiyo demokrasia na Haki za Binadamu za Marekani?
Duniani kuna mafisadi na madikteta wengi wanaoumbwa na nchi hizi za Magharibi. Juan Peron wa Argentina,alitawa tangu 1946-55.Akarudi kupindua tena nchi akatawala mwaka 1973,mkewe Isabel,akafanywa kuwa Makamu wa Rais.
Dikteta Peron alipokufa mwaka 1974 Isabel akawa Rais! Nchi ikamshinda,mfumuko wa bei ukapanda hadi asilimia 500! Hapa,mfumuko wa bei umefika takriban 20 tunakaribia kuzimia kwa njaa na kiu.
Hapa Afrika,utawaona akina Museveni wanaoigeuza Uganda kama kampuni binafsi. Baba,Mama na Watoto(BMW) ni viongozi wa serikali,lakini kwa kuwa bado wanauhusiano na wakubwa wa Magharibi,umesikia amri kutoka White House?
Juzi,tumesikia Rais Barack Hussein Obama akimpigia simu Kagame wa Rwanda kuacha maramoja kuwasaidia Waasi wa M23 HUKO CONGO.Sasa,kwanini asipige simu kumzuia Museveni kumchagua Janet na Muhozi kuwa vigogo katika serikali anayoiongoza? Tuwe na akili jamani,mbona sisi mbumbumbu kiasi hiki?
Noriega wa Panama.                                            
 Desemba 1989 George Herbert Walker Bush(Bush Baba) alituma jeshi Panama City,likampindua Jen. Manuel Noriega na kumfunga pingu kama alivyofungwa Saddam zama za mwanaye, George W.Bush.
 Makampuni ya Marekani,Uholanzi,Uingereza n.k ya mafuta,yamechochea vita na mauaji mahali pengi,yametumikisha watu huko Burma ama Myanmar sasa, ukiwapinga Marekani unakamatwa na kufungwa jela,labda uwe kibaraka wao.
 Na viongozi wetu wengi ni vibaraka wa Marekani, wanaogopa kukamatwa au kupinduliwa!
 Si unasikia kwamba hata maandamano ya kupinga serikali wanachochea wao katika nchi nyingi,kwa kisingizio cha demokrasia?
 Nigeria, Ken Saro-Wiwa, aliuliwa na Jen. Sani Abacha Novemba 10 mwaka 1995 kwa sababu alilipinga sana kampuni la mafuta la Royal/Dutch Shell la Uingereza na Uholanzi.
 Marekani wanajidai kuimba demokrasia na haki za binadamu,lakini ukiwapinga wanakuua wakiwa nyuma ya pazia!
 Nataka nikwambie msomaji. Orodha ya watu waliouliwa na Marekani na washirika wao na Mashirika ya Ujasusi kama CIA,MI6 na MI5,Mossad , BOSS la Makaburu,na mengine ni kubwa sana.
 Sasa, kaangalie huko Mahakama ya Uhalifu wa Kivita(ICC)The Hague,Uholanzi, wanashitakiwa akina nani?
  Orodha ya washitakiwa,kama wale wa Luis Moreno Ocampo maarufu kama “Ocampo Six” wamo Wakenya tu na Waafrika,na Wazungu adui zao kama wafuasi wa Adolf Hitler na Dikteta Slobodan Milosevic wa Serbia!
 Bush na Tony Blair hawamo,kuna Fodday Sankoh, Charles Taylor na ‘Ocampo Six’ kwa sababu hawana maslahi ya Marekani na washirika wao.
 Kanali Muammar al-Qaddafi wa Libya, siku hizi anasakwa kama nguruwe-pori,huko Benghazi na Tripoli,kisa…Marekani na washirika wake wanasema anahatarisha ubinadamu!
  Aprili 14 mwaka 1986 mvua ya masika ya mabomu ya madege ya Kimarekani,ilinyesha Tripoli na Benghazi, wakashambulia kasri la Qaddafi, hakuwemo wakaua wanaye wa kambo.
 Qaddafi, alikuwa adui yao tangu mwaka 1988,magaidi wake wakiwemo maofisa usalama wake walipoilipua ndege ya Pan American Airways, Flight 103 huko Lockerbie, Scotland. Pia alisaidiwa kupindua serikali mwaka 1969 akaja kugeuka.
 Akina Abdel Basset Ali Al-Meghri wakahukumiwa kifo,baadaye wakaachwa huru lakini Qaddafi bado anatafutwa ili afuate nyazo za ‘waasi’ wenzake kama Noriega,Saddam,Hosni Mubarak, Ben Ali, Samora Moises Machel,Murtala Mohamed, Patrice Emery Lumumba-ya watu wa kufa, ni ndefu.
Akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika(AU),Qaddafi alitaka Afrika iwe nchi moja(Pan Africanism)  ili kupinga ubeberu wa Magharibi.
 Visingizio vya kutaka kumumaliza ni vingi tu. Anataka kumrithisha mwanaye urais wa Libya.
Makampuni mengi makubwa ya Marekani yanayochimba na kusafisha mafuta duniani:Exxon, Mobil,Chevron,Texaco,Conoco,Phillips n.k yanaongoza kwa mikataba ya wizi na utapeli na mikataba yenye dhuluma duniani.
 Nchi nyingine zenye makampuni makubwa ya kuchimba na kuchakata mafuta ni pamoja na Uingereza,( British Petroleum au BP), Uholanzi na United Kingdom wanamiliki kampuni kubwa la Royal/Dutch Shell, Ufaransa na Ubelgiji wanamiliki kampuni la Total,na Urusi ina makampuni kama Lukoil,Yukos na Sibneft.
 Misri, alikopinduliwa punde Rais Hosni Mubarak,ina rasilimali tele ya mafuta,gesi,phosphate, matunda n.k
Mwaka 2000, Misri ilikuwa na akiba ya mafuta kama mapipa bilioni 2.9 hivi, nchi hii ina ushawishi mkubwa kwa nchi za Kiarabu zenye hazina kubwa ya mafuta  kama ulivyokwishaona hapo juu.
 Ni nchi yenye mfereji wa Suez wenye urefu wa maili 103 unaoziunganisha Bahari za Shamu(Red Sea)na Mediterranean.
Ulijengwa(ulichimbwa) kwa ushirika na Ufaransa na Uingereza mwaka 1859-69 kukatokea vita vya kuumiliki mfereji huo,kwa sababu yanapita mameli makubwa.Julai 28 mwaka 1956 serikali ya Misri ikautaifisha.Lazima Marekani iukodolee mimacho mfereji wa Suez. Kutaifisha mali za nchi kutoka kwa Mkoloni ndiyo uadui mkubwa kwa mataifa haya beberu.
 Tunakusudia kuona jinsi nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani zinavyochochea maasi katika nchi zenye rasilimali nyingi na muhimu sana kama mafuta, gesi,madini muhimu kama Uranium,almasi,dhahabu, bahari,maziwa makubwa n.k
Je, msomaji, unaona uhusiano gani kati ya Marekani na washirika wake dhidi ya nchi zenye mafuta mengi kama Algeria, Iran,Irak, Kuwait.Libya,Venezuela na Misri?
 Hapa Afrika,umeona uhusiano hasi kati ya Marekani na Misri, Algeria,Libya, Guinea ya Ikweta,Angola  n.k hapa Barani Afrika?
 Nitashuhudia,ubabe uchochezi, maandamano, migomo,migogoro ya kutengenezwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe na uasi.
Tumeona ugomvi mkubwa kati ya Marekani na nchi zinazomgomea kuwa kibaraka wake,kama Iran ya Mahmoud Ahmadnejad(Iran ya Shah ilikuwa kibaraka wa Marekani,wakaiba mafuta kwa wingi hadi watu walipomkataa miaka ya mwisho ya 70,akatimkia Marekani), kuna Irak ya Marehemu Saddam Hussein, Venezuela ya Hugo Chavez na Libya na Kanali Muammar al-Qaddafi.
Ukiyanyima mataifa haya babe duniani wanachotaka, utaanza kusikia kwamba Hosni Mubarak anamiliki utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 70(Zaidi kumshinda Carlos Slim, Bill Gates Na Warren Buffet),utasikia baadaye kwamba Rais Yoweri Kaguta Museveni anamiliki utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 10,siku wakikosana.
  Ukiwanyanyima maslahi yao unakuwa adui yao;tena wakimaliza kukutumia kama “kondomu”,kama Charles Taylor,Fodday Sankoh na Jonas Savimbi,wanakutupa jela au wanakuua!
 Osama bin Laden, alikuwa mtu wao akawaasi, wanamsaka!Siku hizi hawamsemi sana,labda walishakutana, wakayamaliza!
 Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela,aliwahi kusema kwamba Vita vya Ghuba vilikuwa vita vya mafuta.
 Yaani vita na migogoro ya Kuwait na Irak ya Saddam Hussein katika miaka ya 90-vita ya kwanza ya Ghuba na ile ya Pili ya 2003 iliyomsababishia Saddam Hussein kukamatwa,kufungwa jela na kunyongwa Alfajiri ya Jumamosi, Desemba 30 mwaka 2006,huko jengoni Camp Justice, mjini Baghdad,vilikuwa vita vya mafuta
Itaendelea
0786 324 074


No comments:

Post a Comment