Tuesday, December 11, 2012

"Sitaki-nataka" Raila Odinga awe Rais Kenya!!

KAMA kuna Mwanasiasa ambaye harakati na mienendo yake ya kisiasa ni utata mtupu, mafumbo na kiini macho hapa Afrika Mashariki, si mwingine bali Waziri wa zamani wa Barabara, Ujenzi na Nyumba, wa Kenya, Raila Odinga.Raila Odinga, siku hizi ni Waziri Mkuu wa Kenya
      Msomi wa Nigeria, Dk. Babafeni A.Badejo ameandika kitabu, “An Enigma in Kenyan Politics” (Utata katika siasa za Kenya) akiufumbua macho umma wa jamii ya Afrika Mashariki, harakati za mwanasiasa huyo machachari sana, kuwa alishiriki Mapinduzi ya kijeshi, kutaka kumwondoa madarakani Rais Mstaafu, Daniel arap Moi, Agosti Mosi 1982.
       Katika kitabu hicho kilichozinduliwa Nairobi zaidi ya wiki mbili zilizopita,Dk. Badejo amwemweleza Raila kuwa mtu asiyeeleweka katika siasa za nchi hiyo.Maoni ya watu katika kitabu hicho humweleza Raila kama mwenye tabia ya kinyonga; ambaye si rahisi kumtambua au kumwamini katika harakati za kisiasa.
        Raila ameelezwa kama bingwa wa “michezo michafu” dhidi ya wapinzani wake wa kisiasa.Baadhi ya wabunge wa Kenya katika kitabu hicho wamemfananisha na Dikteta wa zamani wa Ujerumani, Adolf Hitler! Kwamba wakati mwingine huonekana mzalendo,mwenye msimamo mkali ambaye kama babaye, Marehemu Jaramogi Odinga Oginga, aliwahi kuswekwa kizuizini kwa kile anachoita yeye kutafuta dira ya Wakenya!
       Raila Odinga, anadhihirishwa katika kitabu hicho kama kinyonga, popo, na ‘sungura mjanja’ awezaye kuchochea mabalaa, halafu akajiweka kando bila umma kumaizi.
   Asubuhi, kwa mara nyingine, miaka michache iliyopita, Raila alishindwa kukubali au kukanusha madai kwamba alihusika katika jaribio la mapinduzi ya mwaka 1982. Alikuwa akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazi la Uingereza (BBC), kupitia kipindi cha Wiki Hii.
         “Nitaweka mambo yote wazi katika kitabu changu kitakachotolewa, ili uuma ujue ukweli”, alisema Raila kajika mahojiano hayo na Tido Mhando wakati akiongoza idhaa hiyo.
Kwa kauli hiyo, bila shaka Raila anajibanza katika pazia la mlango wa madai hayo.Anakiri kuliunga mkono jaribio hilo la mapinduzi kwa madai kuwa, kwa kuwa Kenya ilikwisha piga marufuku vyama vingi nchini, hapakuwa na namna nyingine ya kuuondoa utawala wa Kidikteta wa Moi,isipokuwa njia hiyo pekee ya mapinduzi.
      Kwa kuwa katika jaribio hilo watu walimwaga damu yao, na wengine wakatiwa mbaroni na kufunguliwa mashitaka ya uhaini, wapo waoishinikiza serikali Raila akamatwe sasa na kufunguliwa mashitaka hayo, hata baada ya miaka 24.
     Hata hivyo, katika mahojiano na BBC, Raila aliwafananisha waliohusika katika jaribio hilo la mapinduzi, lililoshindwa, na mashujaa waliokufa wakipigania haki tangu enzi za uawala wa rais wa kwanza, Mzee Jomo Kenyatta: J.M. Kariuki, Pio Gama Pinto, Tom Mboya,  Dk. Robert Ouko, na wengineo wengi.
           Raila alijitetea katika mahojiano hayo kuwa, anaonekana ‘mpinzani’ mara nyingi kwa sababu ya kutafuta haki, uhuru, haki na usawa kwa Wakenya.
        Kauli hii inalenga kumsafisha na hisia za watu kuwa ni mbinafsi, anayeendekeza mno ukabila kwa lengo la kuwapendelea watu wa kabila lake la Waluo. Raila anatazamwa na wengi kuwa chanzo cha migawanyiko na migogoro tangu KANU, NARC na hata umoja wao wa Orange Democtatic Movement(ODM)!
    Anadaiwa kuivuruga KANU, kabla ya uchaguzi mkuu wa Desemba 2002,ulioiweka madarakani serikali legelege ya Narc.Akaivuruga Narc yenyewe. Alianza kuivuruga Narc mara tu baada ya Baraza jipya la Mawaziri kutangazwa. Alikuwa amejibanza nyuma ya ndugu zake. Ilikuwa siku mbili tu, kabla ya baraza jipya kuapishwa.
     Januari 4, mwaka huo wa 2002, kakaye Raila, Oburu Odinga,(Mbunge wa Bondo)akiwa na wenzake wa chama chao cha Liberal Democratic (LDP), walitangaza kumpinga rais Emillio Mwai Kibaki!
      Katibu mkuu wa LDP,Joseph Kamotho, aliitisha kikao cha wabunge wa LDP mjini Nairobi.Ilikuwa baada ya Oburu kukutana na waandishi wa habari kutangaza kutokubaliana na rais Kibaki kuhusu kushindwa kuipa LDP mawaziri wengi zaidi.
    Oburu alimlaumu rais Kibaki kwamba uteuzi wake wa mawaziri haukuwa wa haki. Kwamba LDP kilichangia viti 54 vya Bunge kati ya vyote 125 walivyopata NARC Katika uchaguzi mkuu; hivyo kilistahili kupewa mawaziri wengi zaidi ya wanane kati ya mawaziri wote 23!
      Kama kawaida yake, Raila ‘alijibanza’ kando ya mgogoro huo ulioanza kufukuta hata kabla ya serikali mpya ya Narc kuapishwa, baada ya kumtoa madarakani Moi kwa njia za kidemokrasia, kitu walichokuwa wakililia kwa miaka mingi!
       Akasema, akiwa mjini Kisumu kwamba yeye alifurahia uteuzi huo;kwa kuwa serikali ilikuwa makini kuteua watu wenye karama ya kusaidia kupanga mipango ya kukuza uchumi, kwa lengo la kutimiza ahadi zake.
      Odinga, na aliyekuwa Wazuri wa Nchi, Christopher Murungaru, wakasisitiza kuwa Narc kilishiriki uchaguzi kama chama kimoja cha siasa, na siyo vyama mbalimbali. Kwamba, katika makubaliano yao (Memorandum of Understanding) waliyotiliana saini kati ya  NAK(National Allience Party) na LDP, walizungumza kupeana stahili katika mgawanyo wa nafasi; na siyo mgao sawa.
    Tangu hapo LDP kikaanza kumpinga rais Emilio Mwai Kibaki, hadi majuzi walipotaka kumwondoa madarakani kwa kura ya kutokuwa na imani naye.Kampeni kali dhidi ya katiba ikazaa umoja wa Orange Democratic Movement(ODM).
    Aidha, yaliyotokea Kenya yanafahamika kuwa yameleta seriakali legelege, vigogo wengi wamefukuzwa serikalini, akiwemo Raila mwenyewe,hivi sasa kinacosubiriwa kuokoa hali hiyo ni uchaguzi wa mwaka kesho, ambao kampeni zinaonekana kuanza japo si rasmi.
      Wakati Raila Odinga angali ‘akiuponda’ utawala wa Moi, anasema ulitaka kumbeba Uhuru Kenyatta. Anasema ni kheri Kibaki dhaifu na legelege anayejali demokrasia, kuliko utawala wa kiimla wa Moi.
      Raila ndiye aliyeanzisha uasi katika KANU katikati ya mwaka 2001, ukaanzishwa muungano wa Upinde wa Mvua(NARC), Kibaki akaruhusiwa awe rais, kisha abadili katiba na kumpa Raila Odinga wizara yenye nguvu.
    Bila shaka ilitegemewa kuwa kama katiba ingerekebishwa, ili kupunguza madaraka ya rais(Kibaki) ili kumpa madaraka makubwa Waziri mkuu ambaye angekuwa Raila!Baada ya Rais kukataa kutekeleza ahadi hiyo,uasi dhidi yake uliowatupa akina Raila nje ya serikali ukatokea.Hapa kilinachodhaniwa ni kwamba Waluo walitaka kunufaika zaidi, ingawa Raila amekanusha katika mahojiano na BBC, kuwa siyo mbinafsi kiasi hicho.
   Kama Ofisi ya Waziri mkuu ingeundwa, yaani kama mapendekezo ya katiba mpya iliyoahidiwa wakati wa kampeni ingekubaliwa, basi wizara nyeti kama Usalama,Utawala wa mikoa au majimbo na Utumishi wa umma zingekuwa chini yake.
      Hata hivyo, katika mahojiano na BBC, Raila Odinga amesema siyo mtu hatari.Si mbinafsi wala mkabila. Anasema ni mwanaharakati na mpambanaji. Kwa kuwa mapambano ya kudai haki hayana kikomo, ndiyo maana Raila anaonekana mvurugaji wa mambo kila wakati. Harakati zake za kudai haki, uhuru na usawa, huzifanya wakati wowote, mahali popote dhidi ya adui au rafiki anayetaka kuweka vizuizi barabarani mwa demokrasia, haki na uhuru! Hakika hii ni njozi njema aliyonayo Raila…nakubaliana na kiongozi kama huyu!
    Hata hivyo, sikubaliani kabisa na tabia ya Raila kutaka kuitawala Kenya kwa sababu za kikabila. Kwamba kwa kuwa Wakikuyu na Wakalenjin wamekwishatawala, sasa ni zamu ya Waluo.Hili ni doa baya linaloweza kuifanya Kenya kama Somalia, Congo na penginepo penye machafuko.
   Baadhi ya vigogo kutoka Magharibi ya Kenya waliokuwa maarufu mni pamoja na Tom Mboya, James Gichuru, Jaramogi Oginga Odinga, Chiedo Moa Gem Arwings-Kodhek, J.D. Otiende, Achieng Oneko,na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje “Mr. Clean”,Dk. Robert Ouko.
    Ouko alidaiwa kuondoka nyumbani kwake Asubuhi ya  Feburuari 13 mwaka 1990, hakurudi; mwili wake ulikuja kugunduliwa kichakani akiwa Marehemu, huko Got Alila, takriban kilometa sita toka kwake, Koru, Nyanza, Magharibi mwa Kenya.
        
    Baba yake Raila, pia aligombana na wenzake akaanzisha Kenya Peoples Union, baada ya kuhitilafiana na Kenyatta. Hali hii huleta maoni ya kuwepo katika ubinafsi miomgoni mwa Waluo, lakini Raila anasema wengi wao ni wanaharakati wasiochoka kudai haki siku zote, ndiyo maana wamekuwa watoa dhabihu maisha yao, kama Marehemu, Dk. Ouko.
    Kufuatia hali hiyo, sitaki Raila awatumie akina Ouko kama mtaji wa kuendea madarakani Kenya…sitaki wanasiasa wa Nyanza wamnufaishe Raila katika harakati zake za Urais Kenya, kwa kuwa ataigawanya nchi hiyo zaidi ya kuleta umoja na kuondoa ukabila.
    Kwa upande mwingine, navutiwa mno na harakati za Raila, kuwa tayari hata kumpinga rafiki yake anapokwenda kinyume na matakwa ya Wakenya…ni kwa sababu hii nami nakuwa na utata dhidi ya mwanasiasa huyu kama anastahili kuongoza au la! Utata huo ndio chanzo cha kisebusebu na kiroho… “Sitaki-nataka”(half reluctance) dhidi ya Raila, sawa na utata aliosema Dk. Babafemi A.Badeja!
itaendelea
 

Want to be your own boss? Learn how on Yahoo! Small Business.

No comments:

Post a Comment